Soko la Kariakoo Kuanzia Upya Wake 1900s

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,920
30,263
SOKO LA KARIAKOO KUANZIA UPYA WAKE MWANZONI MWA MIAKA YA 1900
Sisi tuliozaliwa miaka ya 1950 tumelikuta Soko la Kariakoo kama linavyoonekana katika picha ya tatu na ya nne.
Nikiangalia picha ya mwanzo ya Kariakoo akili yangu inanipeleka katika nyumba ambazo nyingine mimi zinanihusu na nyingine nawafahamu wenyewe najiuliza kama kipindi hicho zilikuwa zipo zimekwishajengwa?

Jibu ni kuwa nyumba hizo zilikuwapo kabla ya soko na sababu ni kuwa baadhi ya baba na shangazi zangu mathalan wamezaliwa katika nyumba yetu ya Swahili miaka ya 1920.

Hawa wameliona soko katika upya wake na wakalishuhudia soko likivunjwa na kujengwa soko jipya la Kariakoo hili lililopo hivi sasa kabla halijaungua.

Nyumba za jirani sana na Kariakoo ambazo mimi nazikumbuka ingawa zilikuwapo nyingi ya kwanza kabisa ni nyumba ya bibi yangu Bi. Deborah Mgone (1890 - 1995) ambayo iko Mtaa wa Swahili.

Bi. Deborah ni mtoto wa bibi yetu mkuu Bi. Catherine Hamadi ambae sisi tumezaliwa tumemkuta hapo kwenye nyumba ya Mtaa wa Swahili.

Yeye kafariki 1969 akiwa na umri kwa kukisia labda miaka 90.
Nina kumbukumbu nyingi na Soko la Kariakoo lile ambalo mimi nililikuta wakati nazaliwa.

Ilikuwa mwaka wa 1956 au 1957 nikipelekwa kushinda kwa mama yangu mkubwa Bi. Mwanaisha Bint Mohamed Mtaa wa Nyamwezi na Narung'ombe.

Nyumba hii ilikuwa ya Mzee Kasembe ikatazamana na nyumba ya akina Hariz ambako kulikuwa na mnada maarufu katika mji wa Dar es Salaam - Hariz Auction.

Mnada huu bado upo hadi hivi sasa.
Nyumba ya Mzee Kasembe haipo.

Leo hapo ndipo lilipo lango kuu la kuingilia Shimoni Kariakoo.
Kulikuwa na mwendawazimu jina lake Boimanda na watoto tukimuogopa sana.

Matembezi ya Boimanda siku zote yalikuwa pale sokoni na watu wakimtisha Boimanda kwa kumwambia kuwa askari wa kodi wanakuja na yeye atatoka mbio kukimbia ovyo.

Ilikuwa katika kutishwa kama hivi ndipo alipovamia meza ya biashara ya mtu mmoja anaitwa Manyanga na yeye kwa hasira ya kumwagiwa vitu vyake akampiga kichwa Boimanda akafa palepale.

Kisa hiki kikawa maarufu hadi zikatoka khanga na jina la Boimanda.
Kumbukumbu yangu nuyingine ni ya Ayubu Kiguru shabiki mkubwa sana wa Sunderland (sasa Simba).

Ayubu mguu wake mmoja ulikuwa na athari na hii ndiyo sababu ya yeye kuitwa jina hilo "Ayubu Kiguru."
Nikimjua Ayubu kwa karibu sana na sababu ni kuwa alikuwa na ubao wa biashara pale sokoni jirani na ubao wa mjomba wangu Bwana Khamis Salum.

Soko la Kariakoo enzi hizo lilikuwa moja ya vituo vya ushabiki mkubwa wa mpira Dar es Salaam kati ya Sunderland na Yanga.

Sijui kama hali hii iliendelea hadi miaka hii.

Yanga na Sunderland walitawala soko na Yanga washabiki wao wengi walikuwa na biashara ya kuuza samaki kiasi ikawa watani wao wakiwaita Yanga, ''Wauza Samaki.''

Siku ya mechi ya Sunderland na Yanga moto ulikuwa unawaka sokoni pale toka mapema asubuhi.
Ushabiki huo utaendelea kwa juma zima takriban baada ya mechi.

Sasa ikitokea kuwa Yanga imefungwa na Sunderland washabiki wa Yanga walikuwa tabuni kwa juma zima pale sokoni wakipigwa makombora na Ayubu Kiguru.

Namfananisha Ayubu na Haji Manara na kwa kweli siwezi kuamua nani amemshinda mwenzie kwa kipaji cha kupanga maneno.

Ayubu alikuwa na uwezo wa yeye peke yake kuwanyamazisha Yanga wote pale sokoni.

Ayubu alikuwa bingwa wa maneno ya kejeli na kebehi lakini katika namna ambayo mtu hawezi kughadhibika bali atakuwa yeye anacheka tu.

Ilikuwa Sunderland ikiwafunga Yanga na kuchukua kikombe Ayubu atakuja sokoni na kikombe kile na kukiweka mbele yake anauza nyanya zake huku amevaa jezi no 6 ya Hamisi Kilomoni.

Hapo siku hiyo kutwa nzima washabiki wa Sunderland watapita kwa Ayubu kuja kutunza.

Lakini kubwa kabisa linalostahili kuhifadhiwa katika historia ya Soko la Kariakoo ni historia yake katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Wakati huo Market Master alikuwa Abdul Sykes na Nyerere alikuwa hapungui hapa khasa baada ya kuacha kazi ya ualimu na kuja kuishi na Abdul Sykes nyumbani kwake Mtaa wa Stanley na Sikukuu.

Huu ulikuwa mwaka wa 1955.

Hapo sokoni ndipo Nyerere alipofahamiana na Shariff Abdallah Omar Attas na Mshume Kiyate pamoja na wazalendo wengine waliokuwa mstari wa mbele katika TANU.

1665065007071.png

1665065036876.png

1665065060742.png
1665065086337.png
1665065111785.png
 
SOKO LA KARIAKOO KUANZIA UPYA WAKE MWANZONI MWA MIAKA YA 1900
Sisi tuliozaliwa miaka ya 1950 tumelikuta Soko la Kariakoo kama linavyoonekana katika picha ya tatu na ya nne.
Nikiangalia picha ya mwanzo ya Kariakoo akili yangu inanipeleka katika nyumba ambazo nyingine mimi zinanihusu na nyingine nawafahamu wenyewe najiuliza kama kipindi hicho zilikuwa zipo zimekwishajengwa?

Jibu ni kuwa nyumba hizo zilikuwapo kabla ya soko na sababu ni kuwa baadhi ya baba na shangazi zangu mathalan wamezaliwa katika nyumba yetu ya Swahili miaka ya 1920.

Hawa wameliona soko katika upya wake na wakalishuhudia soko likivunjwa na kujengwa soko jipya la Kariakoo hili lililopo hivi sasa kabla halijaungua.

Nyumba za jirani sana na Kariakoo ambazo mimi nazikumbuka ingawa zilikuwapo nyingi ya kwanza kabisa ni nyumba ya bibi yangu Bi. Deborah Mgone (1890 - 1995) ambayo iko Mtaa wa Swahili.

Bi. Deborah ni mtoto wa bibi yetu mkuu Bi. Catherine Hamadi ambae sisi tumezaliwa tumemkuta hapo kwenye nyumba ya Mtaa wa Swahili.

Yeye kafariki 1969 akiwa na umri kwa kukisia labda miaka 90.
Nina kumbukumbu nyingi na Soko la Kariakoo lile ambalo mimi nililikuta wakati nazaliwa.

Ilikuwa mwaka wa 1956 au 1957 nikipelekwa kushinda kwa mama yangu mkubwa Bi. Mwanaisha Bint Mohamed Mtaa wa Nyamwezi na Narung'ombe.

Nyumba hii ilikuwa ya Mzee Kasembe ikatazamana na nyumba ya akina Hariz ambako kulikuwa na mnada maarufu katika mji wa Dar es Salaam - Hariz Auction.

Mnada huu bado upo hadi hivi sasa.
Nyumba ya Mzee Kasembe haipo.

Leo hapo ndipo lilipo lango kuu la kuingilia Shimoni Kariakoo.
Kulikuwa na mwendawazimu jina lake Boimanda na watoto tukimuogopa sana.

Matembezi ya Boimanda siku zote yalikuwa pale sokoni na watu wakimtisha Boimanda kwa kumwambia kuwa askari wa kodi wanakuja na yeye atatoka mbio kukimbia ovyo.

Ilikuwa katika kutishwa kama hivi ndipo alipovamia meza ya biashara ya mtu mmoja anaitwa Manyanga na yeye kwa hasira ya kumwagiwa vitu vyake akampiga kichwa Boimanda akafa palepale.

Kisa hiki kikawa maarufu hadi zikatoka khanga na jina la Boimanda.
Kumbukumbu yangu nuyingine ni ya Ayubu Kiguru shabiki mkubwa sana wa Sunderland (sasa Simba).

Ayubu mguu wake mmoja ulikuwa na athari na hii ndiyo sababu ya yeye kuitwa jina hilo "Ayubu Kiguru."
Nikimjua Ayubu kwa karibu sana na sababu ni kuwa alikuwa na ubao wa biashara pale sokoni jirani na ubao wa mjomba wangu Bwana Khamis Salum.

Soko la Kariakoo enzi hizo lilikuwa moja ya vituo vya ushabiki mkubwa wa mpira Dar es Salaam kati ya Sunderland na Yanga.

Sijui kama hali hii iliendelea hadi miaka hii.

Yanga na Sunderland walitawala soko na Yanga washabiki wao wengi walikuwa na biashara ya kuuza samaki kiasi ikawa watani wao wakiwaita Yanga, ''Wauza Samaki.''

Siku ya mechi ya Sunderland na Yanga moto ulikuwa unawaka sokoni pale toka mapema asubuhi.
Ushabiki huo utaendelea kwa juma zima takriban baada ya mechi.

Sasa ikitokea kuwa Yanga imefungwa na Sunderland washabiki wa Yanga walikuwa tabuni kwa juma zima pale sokoni wakipigwa makombora na Ayubu Kiguru.

Namfananisha Ayubu na Haji Manara na kwa kweli siwezi kuamua nani amemshinda mwenzie kwa kipaji cha kupanga maneno.

Ayubu alikuwa na uwezo wa yeye peke yake kuwanyamazisha Yanga wote pale sokoni.

Ayubu alikuwa bingwa wa maneno ya kejeli na kebehi lakini katika namna ambayo mtu hawezi kughadhibika bali atakuwa yeye anacheka tu.

Ilikuwa Sunderland ikiwafunga Yanga na kuchukua kikombe Ayubu atakuja sokoni na kikombe kile na kukiweka mbele yake anauza nyanya zake huku amevaa jezi no 6 ya Hamisi Kilomoni.

Hapo siku hiyo kutwa nzima washabiki wa Sunderland watapita kwa Ayubu kuja kutunza.

Lakini kubwa kabisa linalostahili kuhifadhiwa katika historia ya Soko la Kariakoo ni historia yake katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Wakati huo Market Master alikuwa Abdul Sykes na Nyerere alikuwa hapungui hapa khasa baada ya kuacha kazi ya ualimu na kuja kuishi na Abdul Sykes nyumbani kwake Mtaa wa Stanley na Sikukuu.

Huu ulikuwa mwaka wa 1955.

Hapo sokoni ndipo Nyerere alipofahamiana na Shariff Abdallah Omar Attas na Mshume Kiyate pamoja na wazalendo wengine waliokuwa mstari wa mbele katika TANU.

View attachment 2378922
View attachment 2378923
View attachment 2378924View attachment 2378926View attachment 2378927
Shukrani.....makala nzuri
 
Mkuu Asante Sana hata sisi wazee wa Kesho tunajifunza kitu

Pia ukipata nafasi tuje utuambie kuhusu historia ya kuzaliwa kwa Ccm ,
 
Kaka yangu Mohamed; kiswahili fasaha ni kutunza, au kutuza! Naona kama tunachanganya haya maneno yenye maana tofauti.
Gagnija,
Sina ujuzi wa lugha ya Kiswahili kuweza kusema lipi neno sawa.

Mimi nakisema Kiswahili kama nilivyofundishwa kukizungumza na wazazi wangu toka udogoni.
 
Gagnija,
Sina ujuzi wa lugha ya Kiswahili kuweza kusema lipi neno sawa.

Mimi nakisema Kiswahili kama nilivyofundishwa kukizungumza na wazazi wangu toka udogoni.
Hapana, kubali kuwa umeteleza. Wazee wa Kariakoo nawafahamu vyema. Hawakukufunza hivyo.

Ingekuwa enzi zetu mzee kifimbocheza angekuhusu 😆😆. Naghadhabika napokuta mtu anasema nyimbo hii badala ya wimbo huu, nazani badala ya nadhani...

Kiswahili miaka 20 ijayo kitakuwa kimeharibiwa sana.
 
Sipendi kuwa mnafiki kuwa nisubir mtu afe ndio niseme kuwa mwandishi Fulani nilikuwa nampenda.

Mzee wangu Mohamed Said wewe ndio sababu ya Mimi kupenda kupitia pitia hilI jukwaa la historia, napenda Sana uandishi wako na makala zako.

Endelea kutupa  elimu kupitia jukwaa hili.
 
Hapana, kubali kuwa umeteleza. Wazee wa Kariakoo nawafahamu vyema. Hawakukufunza hivyo.

Ingekuwa enzi zetu mzee kifimbocheza angekuhusu 😆😆. Naghadhabika napokuta mtu anasema nyimbo hii badala ya wimbo huu, nazani badala ya nadhani...

Kiswahili miaka 20 ijayo kitakuwa kimeharibiwa sana.
[/QUOTE
Gagnija,
Umeniuliza swali nami nimekujibu.
La hukuridhika sawa hakuna tatizo.
 
Kuna watu huja kuleta ubishan uso na maana
Kutunza ndio sahihi.
Kutuza sio.
Ndio haya mambo ya kusema dhamani badala ya thamani.yan haingii akilini hata kidogo
Mzee mohamed achana na huyu mfalme juha.
Any way.kuna haja kukawekwa vibao bya maelezo ya kihistoria katika maeneo haya kusudi watoto na kizaz cha sasa kujifunza.
Watu wa mambo ya kale ndio kaz zao
 
Kuna watu huja kuleta ubishan uso na maana
Kutunza ndio sahihi.
Kutuza sio.
Ndio haya mambo ya kusema dhamani badala ya thamani.yan haingii akilini hata kidogo
Mzee mohamed achana na huyu mfalme juha.
Any way.kuna haja kukawekwa vibao bya maelezo ya kihistoria katika maeneo haya kusudi watoto na kizaz cha sasa kujifunza.
Watu wa mambo ya kale ndio kaz zao
Julai...
Kila mtafiti akija kunihoji huwa na hamu kubwa sana ya kuona nyumba ya Abdul Sykes ambayo aliishi na Julius Nyerere Stanley Street wakati wa mapambano.

Huwaeleza kuwa nyumba yenyewe haipo lakini huwapeleka pale na wakapiga picha kisha nawapeleka nyumba ya Ally Sykes Kipata Street na nyumba ya mama yao Bi. Mruguru bint Mussa baada ya hapo tunakwenda Kariakoo Market na kuwaonyesha mahali ilipokuwa ofisi ya Market Master Abdul Sykes.

Hii ofisi ya Abdul Sykes Nyerere ndipo a;ipofahamiana na watu wengi waliokuja kuiunga mkono TANU na ndiyo moja ya vituo vya mwanzo kusambaza kadi za TANU kwa wananchi.

Hawa watafiti hamu yao kubwa ni kutaka kuona wapi Nyerere alianzia harakati zake dhidi ya Waingereza harakati ambazo zikaja kuenea kusini yote ya Afrika katika ukombozi.

Nawapiitisha Mnazi Mmoja mbele ya Elimu ya Watu Wazima ilipokuwa inafanyika mikutano ya kwanza ya TANU.

Wote huniuliza iweje hakuna ''plaque,'' yaani vibao kuonyesha historia muhimu ya sehemu hizi?

Mamlaka haziwezi kufanya haya endapo kuna watu wenye mamlaka hawaitaki historia hii.

Hii ndiyo sababu hadi leo tunahangaika na historia ya African Association haifahamiki ingawa historia ipo na iliandikwa mna Kleist Sykes kabla hajafa mwaka wa 1949.

Angalia Mnazi Mmoja mkutano wa TANU mwaka wa 1954:

1665247371013.jpeg
 
Hiyo nyomi kwa 1954 itakuwa 3/4 ya wakazi wote Dar walihudhuria hapo.

TANU walikuwa vizuri sana kwenye uhamasishaji.
Gag...
Ilikuwa kama kesho TANU wana mkutano jioni ile kamati ya ndani itakutana nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Stanley na Sikukuu.

Kwenye kikao hiki watakuwapo akina mama kama Titi Mohamed, Tatu bint Mzee, Hawa bint Maftaha, Bi. Chiku bint Said Kisusa kwa kuwataja wachache na hapo watapeana majukumu nini kifanyike kesho katika uhamasishaji.

1665250647035.png

Kulia: Mama Sakina (Bi. Chiku bint Said Kisusa mke wa Shariff Abdallah Omar Attas), Bi. Titi Mohamed, kushoto wa kwanza Bi. Tatu Bint Mzee na Nyerere huyo katkati wanamsindikiza uwanja wa ndege safari ya kwanza UNO mwezi February 1955.
 
Back
Top Bottom