SMS za Account Namba zimekuwa Blocked na Mtandao wa Tigo?

ACCOUNT FULL

JF-Expert Member
Sep 24, 2012
1,984
360
Wakuu habari,

Jana nilikuwa nahitaji kumtumia Mtu Account namba yangu ili anitumie pesa nikatoe, hii yote ni katika kupunguza gharama ya Makato.

Nikamuandikia SMS, mimi natumia mtandao wa Tigo, niliandika Majina kamili, jina la bank husika na namba ya Account cha ajabu kila nikituma ile SMS, SMS inakataa kwenda, nikituma sms ya kawaida inaenda, nikajaribu kuandika sms ndefu zaidi bado ikaenda, nikirudia kuituma ile sms ya Account namba ikawa bado inakataa!

Cha kushangaza nilipoamua kuzituma zile namba za Account kwa mafungu, SMS ilikubali kwenda nikajaribu pia kuituma ile Account namba tupu (bila majina yangu wala jina la bank, yani ikaonekana kama Vocha tu) SMS ilikubali kwenda!

Leo pia nimejaribu, matokeo ni yale yale.

Je, kuna uwezekano Tigo wamezuia watu kutumiana Account namba ili tutumie tigo pesa yao kwa sisi wateja wa Tigo?
 
Kuna jambo apa sio bure maana ata meseji za kutoa pesa kwa atm(Cardless banking) zinasambua kufika huenda kuna mpango unasukwa kuhimiza tigopesa.
 
Ngoja nijaribu
---------
APDATES
Msg imeenda ila bado haijapokelewa.

Hatimaye imepokelewa. Ilikuwa na taarifa za NMB.
 
Mkuu ACCOUNT FULL pole kwa usumbufu. Hili tatizo nilikutana nalo kama wiki moja iliyopita ambapo ukitaja tu jina la Bank fulani hiyo sms haiendi ILA ukituma account number tu hiyo sms inaenda. Yamkini hiyo ni minyukano ya kibiashara inayoendelea baina ya mitandao ya simu na Bank.
 
Labda wameshtuka Watu mnakwepa makato, hivyo wanajitahidi kuwaweka mstarini kama Ng'ombe wanavyoingizwaga kwenye josho.

josho 90.png
 
Ukituma jina la CRDB ndio wanazuia, NMB, NBC, Equity etc zinafanya kazi, ni CRDB tu ndio wamepigwa pini
 
Mkuu Cannabis habari. Nami nilituma jina la CRDB, sasa hapo tusemeje kwamba hii Bank ndio ime-Engineer mpango mzima wa makato ya Simu?
Tusubiri tuone.
Ahsante
Hapo sifahamu ,lakini inawezekana CRDB ndio mnufaika mkubwa wa hali ya makato kwenye simu. Inawezekana Tigo wameona kuna volume kubwa ya transactions za sim-Banking ya CRDB au sms nyingi zenye jina la CRDB Bank...ni uhuni uliofanyika kama wameamua kuziblock hizo SMS kwa sababu za kibiashara.
 
Mkuu ACCOUNT FULL pole kwa usumbufu. Hili tatizo nilikutana nalo kama wiki moja iliyopita ambapo ukitaja tu jina la Bank fulani hiyo sms haiendi ILA ukituma account number tu hiyo sms inaenda. Yamkini hiyo ni minyukano ya kibiashara inayoendelea baina ya mitandao ya simu na Bank.
Asante, pole na wewe pia kwa usumbufu huo mkuu
 
Wakati wa uchaguzi walikuwa wanafilter neno Tundu Lissu, ngoja nijaribu sasa hivi nione.
 
Haya mamitandao ya simu yanayoshirikiana na hii Serikali dhalimu na ambayo haina kibali cha wananchi katika kudhulumu watu yapeni adhabu kwa kukataa kuyatumia.
 
Back
Top Bottom