Siyo lazima kila alama ya mvuka kwa miguu (zebra) dereva wa gari asimame, Sheria ifumuliwe imepitwa na wakati

dmkali

JF-Expert Member
Nov 17, 2014
11,284
21,403
Habari

Tunaongozwa na sheria zilizo expire muda wake!

Iko haja sheria ya usalama barabarani ifanyiwe marekebisho kwani ilitungwa zamani enzi hizo Tanzania hatukuwa na barabara za lami na magari ya kutosha!

1. Siyo kila zebra lazima mwenye gari asimame hata kama hakuna mtu,
lakini baadhi ya Trafiki waliowrngi huitumia sheria hii vibaya kujinufaisha na kubambikia watu!

Hii yote inawezekana kwasababu sheria inawalinda trafiki kumkandamiza dereva! Hivyo hiyo sheria imepitwa na wakati kuwepo sasa!

Kama nchi sasa tunatakiwa tuwe na zebra za aina tofauti kuliko sasa vibao vyote ni black and White!

Nashauri Kuwekwe sheria mpya kwa vibao vya alama za wavuka kwa miguu iwe kama ifuatavyo!

1. Zebra za mistari nyekundu na nyeupe hiyo viwekwe kwenye vivuko vya watembea mguu kuonesha ni lazima kwa dereva kusimama (Lazima); na mara nyingi vibao hivyo vitawekwa kwenye maeneo mhimu tu ya msongamano! (Hii itamuamrisha dereva lazima kusimama kupisha watembea kwa miguu)

2. Zebra za mistari nyeupe na kijani itumie kuonesha utahadhari lakini hii iwe rasmi kwa wote kwa mtembea kwa miguu kuonesha atavuka endapo tu kukiwa salama!
(Hii itamuelekeza mtembea kwa miguu kuvuka kwa tahadhari kwa usalama wake)

Je, Endapo kuna kosa na dereva hakubaliani na kosa hilo sheria inasemaje kuhusu adhabu?

Kwa sheria ya sasa kwakweli ni mbovu mno, Endapo traffic akiamua kumbambikia kosa dereva ambalo hakubaliani nalo, huwa kuna fomu maalum ya kujaza na dereva kusaini ili kwenda mahakamani!
Na kama itakuwa hivyo lazima chombo cha moto anachoendesha dereva kishikiliwe police hadi pale mahakama itakapoamua!
Sasa chukulia mfano: dereva anakwenda mbeya, halafu kakamatwa chalinze kwa kosa ambalo hakubaliani nalo, inabidi Apache gari hapo chalinze hadi pale mahakama itakapoamua ( Hii sheria ya muundo huu haitekelezeki na sijui waliotunga walikuwa na akili gani)

Nashauri, endapo kuna mazingira ya dereva kutokubaliana na kosa, uwekwe utaratibu wa kuchukua maelezo ambayo yanakuwa kwenye karatasi kaboneted, polisi aandike maelezo yake, pia dereva naye aandike palepale maelezo yake pasipo kushurutishwa, halafu nakala ya juu achaniwe dereva apewe ili akaripoti kwenye kituo cha polisi kilichokaribu naye ndani ya siku 7 baada ya tukio, then ipangwe Sikh ya kusikiliza hiyo kesi online kupitia ofisi za police traffic na iamuriwe baada ya kusikiliza pande zote (dereva na traffic )

Kwa dereva ambaye hatakwenda kuripo kwa ajili ya kesi hiyo aandikiwe faini kwa maana kesi itakuwa imesikilizwa kwa upande mmoja!

Hii italeta nidhamu kwa trafiki wanaobambikia watu makosa kwasababu, endapo kutakuwa na malalamiko mengi ya dereva kutokubaliana na kosa kwenye database ya polisi na ikionesha trafiki yule yule kufanya kosa kwa wengi basi ASKARI huyo aondolewe barabarani!

Zipo sheria nyingi sana za kufumua lakini kiufupi sheria ya usalama barabarani ifumuliwe!

Usipokuwa mvumilivu barabarani kwa sasa unaweza piga trafiki kwa jaziba barabarani kumbe yeye hana hatia Bali anasimamia sheria mbovu ipasavyo kwa maslahi yake!
 
Habari

Tunaongozwa na sheria zilizo expire muda wake!

Iko haja sheria ya usalama barabarani ifanyiwe marekebisho kwani ilitungwa zamani enzi hizo Tanzania hatukuwa na barabara za lami na magari ya kutosha!

1. Siyo kila zebra lazima mwenye gari asimame hata kama hakuna mtu,
lakini baadhi ya Trafiki waliowrngi huitumia sheria hii vibaya kujinufaisha na kubambikia watu!

Hii yote inawezekana kwasababu sheria inawalinda trafiki kumkandamiza dereva! Hivyo hiyo sheria imepitwa na wakati kuwepo sasa!

Kama nchi sasa tunatakiwa tuwe na zebra za aina tofauti kuliko sasa vibao vyote ni black and White!

Nashauri Kuwekwe sheria mpya kwa vibao vya alama za wavuka kwa miguu iwe kama ifuatavyo!

1. Zebra za mistari nyekundu na nyeupe hiyo viwekwe kwenye vifuko vinavyomlazimisha dereva kusimama (Lazima); na mara nyingi vibao hivyo vitawekwa kwenye maeneo mhimu tu ya msongamano! (Hii itamuamrisha dereva lazima kusimama kupisha watembea kwa miguu)

2. Zebra za mistari nyeupe na kijani itumie kuonesha utahadhari lakini hii iwe rasmi kwa wote kwa mtembea kwa miguu kuonesha atavuka endapo tu kukiwa salama!
(Hii itamuelekeza mtembea kwa miguu kuvuka kwa tahadhari kwa usalama wake)

Je, Endapo kuna kosa na dereva hakubaliani na kosa hilo sheria inasemaje kuhusu adhabu?

Kwa sheria ya sasa kwakweli ni mbovu mno, Endapo traffic akiamua kumbambikia kosa dereva ambalo hakubaliani nalo, huwa kuna fomu maalum ya kujaza na dereva kusaini ili kwenda mahakamani!
Na kama itakuwa hivyo lazima chombo cha moto anachoendesha dereva kishikiliwe police hadi pale mahakama itakapoamua!
Sasa chukulia mfano: dereva anakwenda mbeya, halafu kakamatwa chalinze kwa kosa ambalo hakubaliani nalo, inabidi Apache gari hapo chalinze hadi pale mahakama itakapoamua ( Hii sheria ya muundo huu haitekelezeki na sijui waliotunga walikuwa na akili gani)

Nashauri, endapo kuna mazingira ya dereva kutokubaliana na kosa, uwekwe utaratibu wa kuchukua maelezo ambayo yanakuwa kwenye karatasi kaboneted, polisi aandike maelezo yake, pia dereva naye aandike palepale maelezo yake pasipo kushurutishwa, halafu nakala ya juu achaniwe dereva apewe ili akaripoti kwenye kituo cha polisi kilichokaribu naye ndani ya siku 7 baada ya tukio, then ipangwe Sikh ya kusikiliza hiyo kesi online kupitia ofisi za police traffic na iamuriwe baada ya kusikiliza pande zote (dereva na traffic )

Kwa dereva ambaye hatakwenda kuripo kwa ajili ya kesi hiyo aandikiwe faini kwa maana kesi itakuwa imesikilizwa kwa upande mmoja!

Hii italeta nidhamu kwa trafiki wanaobambikia watu makosa kwasababu, endapo kutakuwa na malalamiko mengi ya dereva kutokubaliana na kosa kwenye database ya polisi na ikionesha trafiki yule yule kufanya kosa kwa wengi basi ASKARI huyo aondolewe barabarani!

Zipo sheria nyingi sana za kufumua lakini kiufupi sheria ya usalama barabarani ifumuliwe!

Usipokuwa mvumilivu barabarani kwa sasa unaweza piga trafiki kwa jaziba barabarani kumbe yeye hana hatia Bali anasimamia sheria mbovu ipasavyo kwa maslahi yake!
Hizi ndiyo hoja za kizalendo na inabidi wote tuiunge mkono, katika kumuunga mkono nashauri sjitokeze kituo chochote cha polisi wa usalama barabarani na awatake wakague magurudumu ya gari lake ni ya mwaka gani, na gari lake pia lilitengenezwa mwaka gani.
Usalama barabarani huanzia kwenye chombo, nawasilisha.
 
Hizi ndiyo hoja za kizalendo na inabidi wite tuiunge mkono, katika kumuunga mkono nashauri sjitokeze kituo chochote cha polisi wa usalama barabarani na awatake wakague magurudumu ya gari lake ni ya mwaka gani, na gari lake pia lilitengenezwa mwaka gani.
Usalama barabarani huanzia kwenye chombo, nawasilisha.
Asante kwa kujazia nyama
 
Shule nyingi zimejengwa nje kdg ua vijiji. Unakuta wameweka zebra kwa ajiri ya wanafunzi. Lkn unakuta traffic police kaganda hapo siku ya jumapili jioni na anakupiga faini kisa eti unepita bila kusimama. Huo ni ushenzi tu
 
Shule nyingi zimejengwa nje kdg ua vijiji. Unakuta wameweka zebra kwa ajiri ya wanafunzi. Lkn unakuta traffic police kaganda hapo siku ya jumapili jioni na anakupiga faini kisa eti unepita bila kusimama. Huo ni ushenzi tu
Huo ni unaa! Hata kama hakuna MTU wanataka usimame ndo sheria zetu za hovyo kabisa
 
Hata wakibadili sheria mimi ntaendelea kusimama na kuwapisha Wenda kwa miguu hasa hiki kipindi cha Mvua na kuwapa kipaumbele wanafunzi na watoto na wazee maisha yaendelee unakuta mtu yupo na gari harafu pana mtu anatumia nguvu kusukuma mkokoteni anampigia honi huwa siwaelewi madereva wa hivi aisee wanakosa utu kabisaa..
 
Habari

Tunaongozwa na sheria zilizo expire muda wake!

Iko haja sheria ya usalama barabarani ifanyiwe marekebisho kwani ilitungwa zamani enzi hizo Tanzania hatukuwa na barabara za lami na magari ya kutosha!

1. Siyo kila zebra lazima mwenye gari asimame hata kama hakuna mtu,
lakini baadhi ya Trafiki waliowrngi huitumia sheria hii vibaya kujinufaisha na kubambikia watu!

Hii yote inawezekana kwasababu sheria inawalinda trafiki kumkandamiza dereva! Hivyo hiyo sheria imepitwa na wakati kuwepo sasa!

Kama nchi sasa tunatakiwa tuwe na zebra za aina tofauti kuliko sasa vibao vyote ni black and White!

Nashauri Kuwekwe sheria mpya kwa vibao vya alama za wavuka kwa miguu iwe kama ifuatavyo!

1. Zebra za mistari nyekundu na nyeupe hiyo viwekwe kwenye vifuko vinavyomlazimisha dereva kusimama (Lazima); na mara nyingi vibao hivyo vitawekwa kwenye maeneo mhimu tu ya msongamano! (Hii itamuamrisha dereva lazima kusimama kupisha watembea kwa miguu)

2. Zebra za mistari nyeupe na kijani itumie kuonesha utahadhari lakini hii iwe rasmi kwa wote kwa mtembea kwa miguu kuonesha atavuka endapo tu kukiwa salama!
(Hii itamuelekeza mtembea kwa miguu kuvuka kwa tahadhari kwa usalama wake)
Hizi sheria nyingine kama za zebra crossing nadhani ni za kimataifa kama sikosei, kwani dunia nzima ukiona hizo ziko hivyo na dereva anajua kwamba anatakiwa kusimama na kupisha mtembea kwa miguu.

Sasa wewe unataka sheria zako za nyeupe na kijani au nyekundu duh!
 
Hata wakibadili sheria mimi ntaendelea kusimama na kuwapisha Wenda kwa miguu hasa hiki kipindi cha Mvua na kuwapa kipaumbele wanafunzi na watoto na wazee maisha yaendelee unakuta mtu yupo na garo pana mtu anatumia nguvu kusukuma mkokoteni anampigia honi huwa siwaelewi madereva wa hivi aisee wanakosa utu kabisaa..
Kuna zebra zingine miyeyusho tu kila hatua 100 zebra ...hata kama hakuna mtu usimame hiyo safari au kero
 
Ukijua mbele Kuna zebra wewe dereva unapaswa kupunguza mwendo, angalau ishirini hapo hujaona mtu, kisheria pale unaomba wewe kuvuka
Zebra zingine hakuna vibao zinakuja hivi hamadi bin vuu ...hata kama hakuna watu ukivuka mbele trafiki anakuandikia
 
Hiyo sheria inatumika nchi zote ni sheria ya kimataifa ya usalama barabarani,kuiondoa ni kuiambia dunia Tanzania si sehemu salama kwa waenda kwa miguu hivyo kutembelea Tanzania litakalokukuta barabarani ni juu yako
 
Hata wakibadili sheria mimi ntaendelea kusimama na kuwapisha Wenda kwa miguu hasa hiki kipindi cha Mvua na kuwapa kipaumbele wanafunzi na watoto na wazee maisha yaendelee unakuta mtu yupo na garo pana mtu anatumia nguvu kusukuma mkokoteni anampigia honi huwa siwaelewi madereva wa hivi aisee wanakosa utu kabisaa..
Usilete hisia kwenye mambo yanayohitaji sheria, hakuna dereva asiyepisha LA sivyo kila siku tungesikia vifo vya watembea mguu,

Tunachosema hapa, hizo zebra hata kama hakuna MTU wa kuvuka, ukipita trafiki anakukamata ,
 
Back
Top Bottom