Umesema kweli.
Mimi nilibahatika kuoa mwaka 2008 tulidumu kwenye ndoa miaka mi 4 tu, na mimi sikuwa na mpango wa kuoa wala nini MAZA alinishikia bango akawa ananisumbua nioe, nikaoa Mwarabu ambae MAZA alinichagulia, kwa kweli mimi na yule Mama watoto hatukuwa na matatizo, tatizo Mama yake(Mama watoto) alikuwa anataka aolewe na Mwarabu mmoja anaishi umangani na yule wa Umangani akasikia kaolewa ilimuuma sana. Baba wa Mama watoto wangu alikuwa hana tatizo, tatizo yule Mkewe(Mama mkwe) alikuwa anasumbua sana ikafikia mtoto wake anakuja niambia maneno yote anayopewa na Mama yake ikawa inaleta tafrani hadi mimi inafikia napoteza na kuanza kumchapa Mama watoto, ni story ndefu sana, ngoja niikatishe.
Unajua mila za waarabu wa kibongo msichana akifikia umri fulani wanamuweka ndani hatoki hadi siku ya kuolewa na lazima aolewe bikira.
Basi tena mimi kwa sasa sijui kama nitaoa, kwa kweli nimedumu kwenye ndoa yetu 2008 mpaka 2012 nikachemka. Nilichobahatika watoto wawili wa kwanza Dume(miaka 5) na wa pili Binti (miaka 3 ambayo Mungu akipenda mwezi wa 12 atatimiza mitatu kamili) na watoto wangu wote wawili wapo nyumbani kwetu wanadeka kwa Mama yangu(bibi yao)