Siwachongei TFDA lakini ni kweli Mchele wa Plastic upo na unauzwa

Hii hatari sana,lakini Mamlaka ya chakula na Dawa (TFDA)wanasema hawana taarifa yoyote rasmi ya kuwepo kwa mchele aina hiyo wa plastiki hapa nchini.

Lakini pia taasisi hiyo ya TFDA inawaasa wananchi watoe ushirikiano wa taarifa za mchele huo ili hatua za haraka zichukuliwe.

Kila siku TFDA wanasema huo mchele haupo. Mimi nmeshindwa kuelewa. Kama sio wa Plastic, ni mchele gani huu? Kama vipi tuwatumbue tuwaweke watakaoweza kutuambia ni mchele gani.

Kwanini video inapoanza anaanza kwa kufinyanga tonge la huo mchele anaosema ni fake? Kwanini asinze shooting kwa kuchota mchele kutoka sahani ya mama lishe ili tuamini ya kwamba hilo tonge la ubwabwa limetoka katika hiyo sahani?

Inaweza kuwa ni video ya propaganda ya kutia hofu watanzania.

Kwenye age ya technological advancements kama hii never trust virtual materials kabla ya ku prove wewe binafsi.
 
Upo dunia gani mkuu?
Mkuu nipo dunia hii hii ila mimi nimejaribu kuchunguza sana lakini hii inakuw kama ile hadithi ya chinja chinja tu. Halafu tusidhani huu uvumi umeanza leo... la hasha. Ni wa siku nyingi na mara nyingi na umeshatokea katika nchi nyingi duniani (hasa za dunia ya tatu) lakini hakuna mamlaka ya nchi yoyote iliyokwisha thibitisha hili jambo (kwa kadiri ya uchunguzi wangu). Mimi kitu nitakachokubali ni kuwa unakuwa na mchele ulioharibika na usiofaa kwa matumizi. Kitu chochote kikikaa muda mrefu kinabadilika. Hivi mkuu kweli mtu ale vipande vya plastic vilikatwa katwa kama mchele sahani moja na digestion ifanyike kama kawaida?
 
Asante Sana mkuu. Wale waliochukua masomo ya science angalau wanaweza kukuelewa. Wale 'wengine' acha waendelee kuamini kile walichoambiwa au kusikia.
Mkuu tatizo wengi wetu hatuna muda wa kujifikirisha... kwa akili ya kawaida plastic ina tabia ya kuelea kwenye maji!! Nimefafanua mchele feki unavyotengenezwa na wengi hawasomi wanapita mabandiko na kuendeleza mjadala bila kutafakari kwa sababu nani kasema!!! Yaleyale ya Ambilikile Mwasapile wa Samunge Loliondo!!

Yale Yale ya kumwona popobawa.....Watanzania bana ili mradi Mange kasema tunaibeba kama ilivyo
 
We leta science zako za kata hapa kwenye mambo muhimu..ndo ivo mchele wa plastic hata nigeria ushawai kamatwa...

Wwbongo kwa story za vijiweni

Ona kilichokamatwa Nigeria
Screenshot_2017-06-19-18-59-30.png
 
We unayetukana jiangalie na hiyo ajira yako TFDA!Watu wanawasi wasi kwa vile inawezekana kuwepo kwa mchele usiokidhi viwango ukachanganywa na mchele safi na kuuzwa tu sokoni.
Hivi ninyi TFDA mna watalamu gani huku mikoani zaidi ya hawa jamaa mabwana afya wasio na vifaa,na wafamasia walevi na wazinzi wasiojua chochote zaidi ya dili za kuweka vyeti kwenye maduka ya dawa?

Umewahi ona wapi mfamasia mwajiriwa wa TFDA katundika cheti dukani?

Ama una chuki zako kwa hawa watu au hujajielimisha
 
Huwezi kuizungumzia sayansi kwa akili timamu na issue za kuamini tu!Sayansi ni kanuni zinazohitaji akili ya ziada kuzizungumzia na siyo akili timamu pekee!
well ...umesema vema..

sayansi ni utimamu plus, lazima huwe na ABC zake ndipo huweze ku judge vema
 
Tfda Mara nyingi ni pharmacy, quality assurance, chemists na physician,na public health ata food science... Ila TBS ata walimu wapo,..
Haulitendei haki Shirika la viwango Tanzania TBS kwa kulifananisha na TFDA! TBS ni lina majukumu mengi ya kuhakikisha ubora na usalama wa bidhaa zote zinazozalishwa au kuingizwa nchini kutoka mataifa mengine ikiwa ni pamoja na kuaandaa viwango vya kitaifa katika nyanja zote za kiuchumi, biashara na huduma.
 
Hakuna digestion ya plastic kwenye tumbo la binadamu ebu tuache uzushi na sayansi ichukue mkondo wake,kama binadamu angeweza kula plastic na akaishi bila tatizo Basi pia angeweza kula cellulose (majani) kama ngombe na akaishi katika hali ya kawaida ili plastic ichemke inahitaji joto linalozidi boiling point ya maji na hata ikichemka ikapoa kwa joto ambalo binadamu anaweza sasa kula au kutia mdomoni plastic inakuwa tayari imeshaganda,kwa hiyo ukiona huo mchele unaodai wa plastic umeweza kuufinyanga mkononi bila kuungua na kisha ukaula na next day ukapata Choo that isn't Plastic ni something else!
unajua wabongo tunaenda na matukio.sijui kama kweli wanaifahamu plastic vizuri .
 
Hakuna digestion ya plastic kwenye tumbo la binadamu ebu tuache uzushi na sayansi ichukue mkondo wake,kama binadamu angeweza kula plastic na akaishi bila tatizo Basi pia angeweza kula cellulose (majani) kama ngombe na akaishi katika hali ya kawaida ili plastic ichemke inahitaji joto linalozidi boiling point ya maji na hata ikichemka ikapoa kwa joto ambalo binadamu anaweza sasa kula au kutia mdomoni plastic inakuwa tayari imeshaganda,kwa hiyo ukiona huo mchele unaodai wa plastic umeweza kuufinyanga mkononi bila kuungua na kisha ukaula na next day ukapata Choo that isn't Plastic ni something else!
SAWASAWA
 
Hii hatari sana,lakini Mamlaka ya chakula na Dawa (TFDA)wanasema hawana taarifa yoyote rasmi ya kuwepo kwa mchele aina hiyo wa plastiki hapa nchini.

Lakini pia taasisi hiyo ya TFDA inawaasa wananchi watoe ushirikiano wa taarifa za mchele huo ili hatua za haraka zichukuliwe.

Kila siku TFDA wanasema huo mchele haupo. Mimi nmeshindwa kuelewa. Kama sio wa Plastic, ni mchele gani huu? Kama vipi tuwatumbue tuwaweke watakaoweza kutuambia ni mchele gani.


UPDATES:

TFDA imeunda kikosi maalum ili kupata ukweli juu ya mchele unaodaiwa kutengenezwa kwa kutumia plastiki baada ya picha kusambaa mitandaoni.

Watu wanakosa Maarifa, Wana ufahamu zero wa kisayansi na wanakurupuka kuongea mambo ya kusadikika na kufikirika @ kukicha. Plastic is polymer, hence this is hoax thus "Fools die"
 
Hii hatari sana,lakini Mamlaka ya chakula na Dawa (TFDA)wanasema hawana taarifa yoyote rasmi ya kuwepo kwa mchele aina hiyo wa plastiki hapa nchini.

Lakini pia taasisi hiyo ya TFDA inawaasa wananchi watoe ushirikiano wa taarifa za mchele huo ili hatua za haraka zichukuliwe.

Kila siku TFDA wanasema huo mchele haupo. Mimi nmeshindwa kuelewa. Kama sio wa Plastic, ni mchele gani huu? Kama vipi tuwatumbue tuwaweke watakaoweza kutuambia ni mchele gani.


UPDATES:

TFDA imeunda kikosi maalum ili kupata ukweli juu ya mchele unaodaiwa kutengenezwa kwa kutumia plastiki baada ya picha kusambaa mitandaoni.

Kwa manufaa ya Taifa si uwaambie unapatikana ghala gani au duka gani
Mbona watanzania ni kulalamika tuuu,
Mi nilitarajia baada TFDA kusema huo mzigo haupo nchini, ungekuja na kusema, uliwapa taarifa au kuwapelekea sampuli ya huo mchele na wao hawakulifanyia kazi
NB: au umeogopa mambo ya Dr. Fupi (RIP) Mzee wetu
 
Mchele wa Plastiki unaingia kupitia Zanzibar ukitokea India. Kwenda Bara hutumika hasa bandari ya Mkokotoni Kaskazini Unguja inayopitisha vitu vyote haramu, au Majahazi kwa bandari bubu.
 
hivi, kutengeneza mchele debe zima kwa kutumia plastic ni garama ndogo kuliko kuulima? najaribu tu kujifunza uchumi. alafu, hivi hao wanaotengeneza uo mchele china, lengo lao ni nini? na hadi mtu anaweka plant ya kutengeneza, serikali iko wapi?
 
hivi, kutengeneza mchele debe zima kwa kutumia plastic ni garama ndogo kuliko kuulima? najaribu tu kujifunza uchumi. alafu, hivi hao wanaotengeneza uo mchele china, lengo lao ni nini? na hadi mtu anaweka plant ya kutengeneza, serikali iko wapi?
Hizo ni western propaganda kujaribu kuwaharibia wachina baada ya kuona Kila kitu kinatengenezwa na nguvu kazi za china
 
Back
Top Bottom