Sitta Rais, Dr Slaa Waziri Mkuu, 2015

ibange

JF-Expert Member
Dec 31, 2010
1,543
550
Wana JF natamani Sitta angegombea urais kupitia Chadema 2015 awe Rais halafu Dr Slaa akagombee ubunge ateuliwe kuwa PM. Mawaziri akina mwakyembe, Ole Sndeka, Kilango, Mnyika, Mdee, Lissu nk. Nadhani hiyo timu ingefanikiwa sana.

Sitta na Dr ni watu wakali, wanaichukia rushwa, wana busara na ni waadilifu.

Ukimwangalia Sitta na ukirudi ukimwangalia Dr Slaa, unauona unyerere ndani yao. Pamoja na hawa mabwana kuwa na maadui wengi, ulishawahi kusikia wanatuhumiwa au kuzushiwa rushwa? Hawa maadui wangekuwa hata na chembe ya ushahidi wa rushwa wangeutumia.

Waulizeni watu wanaotokea Hanang au Urambo na pia chunguza mwenyewe utagundua hawa mabwana ni kati ya rare breeds zilizobaki Tz.
 
muda bado ngoja kwanza makundi yaendelee kugawanyika kwanza ndani ya CCM wakiishiwa nguvu then ndio kina sitta wahame acha tu aendelee kuwavuruga!!pia nina wasiwasi kuna uwezekano mkubwa sana kura za 2015 CCM wakagawana na CUF na CHADEMA wakachukua sababu nimeona udini unanukia baada ya shekhe mkuu kutoa tamko juzi!
 
Duh,gahfla tu imekuwa hivi?kwanini Sitta na si Dr.Slaa au candidate mwingine atakayekuwa nominated through democratic process? To me,Dr.Slaa is still the best

He is an outstanding leader; he's very tough, knowledgeable, focused and has a clear vision.
 
muda bado ngoja kwanza makundi yaendelee kugawanyika kwanza ndani ya CCM wakiishiwa nguvu then ndio kina sitta wahame acha tu aendelee kuwavuruga!!pia nina wasiwasi kuna uwezekano mkubwa sana kura za 2015 CCM wakagawana na CUF na CHADEMA wakachukua sababu nimeona udini unanukia baada ya shekhe mkuu kutoa tamko juzi!

Tatizo lako hadi akili zako zimesha chakachuka mkuu, mufti kuongea ndio umeona ni udini? hebu niambie Maaskofu siku hizi nao ni madiwani? kama siyo niambie nini kiliwafanya waseme hawamtambui meya wao kama maaskofu?

Kwanza walivunja katiba walipasa kushitakiwa.kwasababu kauli ile ni sahihi tu ikitolewa na madiwani, kwani ndio wanaomchagua meya. lakini kwa jinsi akili zako zilivyochakachuka hayo huyaoni, ila unamshangaa mufti kuwaambia waumini wake wasiende kwenye maandamano ya kisiasa!!! Kama kweli wewe siyo mnafiki unajua kabisa wakati wa kampeni jinsi kanisa lilivyo-play.

Katika taratibu za kisheria chama cha siasa ndicho chenye mamlaka ya kutoa ILANI YA UCHAGUZI sasa niambie Maaskofu walipokaa na kutoa ILANI YA UCHAGUZI chama chao cha siasa kilikuwa kipi? Unajua ududzi wote mnaoufanya waliotafuta uhuru wa nchi hii wanawaangalia kwa macho na kuwatungia sheria.
 
na ninyi si mlisema hamtaingilia siasa sasa mbona mnakula matapishi yenu tena kwa mkuu wenu kuongea pumba kama zile eti waislamu wote msiende kwenye mikutano ya CHADEMA kweli vikao vya ghahawa vinawaharibu sana
 
hii picha naona ingependeza kuiangalia
Dr Slaa ni mtendaji makini (Katibu Mkuu) so uwaziri mkuu angeuweza sanaa
Sita hapendi wala hana aibu na wala rushwa so parallel with Slaa akina Rostam and Lowassa wangepanda ndege mara mmoja kuikimbia nchi.
 
na ninyi si mlisema hamtaingilia siasa sasa mbona mnakula matapishi yenu tena kwa mkuu wenu kuongea pumba kama zile eti waislamu wote msiende kwenye mikutano ya CHADEMA kweli vikao vya ghahawa vinawaharibu sana
....Kaka upo vizuri kichwani??? Au dawa zako zimekwisha?? Jaribisha kwa BABU.......
 
Mimi binafsi nawakubali wote wawili -- Sitta na Slaa. Yeyote kati yao akiwa Rais nina uhakika Tanzania itakuwa tofauti kabisa. Hawa watalinda raslimali za nchi yetu kwa manufaa ya Watanzania wote. Watakata mirija yote ya unyonyaji.
 
Sita ana kashfa ya kujenga ukumbi wa spika urambo kwa zaidi ya milion mia tano.Huwezi kumweka na Dr Slaa
 
hii picha naona ingependeza kuiangalia
Dr Slaa ni mtendaji makini (Katibu Mkuu) so uwaziri mkuu angeuweza sanaa
Sita hapendi wala hana aibu na wala rushwa so parallel with Slaa akina Rostam and Lowassa wangepanda ndege mara mmoja kuikimbia nchi.
Big up. hadi napata msisimko wa mwili. Nadhani matumaini ya Tz yaliyopotea yangerudi. Nchii hii inaweza kwenda kwa kasi ya ajabu ndani ya miaka mitano.
 
Hahahahhaha! Hii ina maana kwamba Sitta ana akili kuliko Rais wenu wa Moyoni Dr wa Ukweli Padre Slaa! Kweili akili ni nywele! Yani unataka tuamini Chadema haina mkakati wa kuandaa mgombea hadi Sitta atoke Chadema!

Mbowe aliwahi sema kuwa wote waliopo CCM wameoza! Sasa Sitta hajaoza!? Hamad Rashid aliwahi kusema Chaema ni Kichaka cha watu kukimbilia kutoka CCM! Basi Chadema ni CCM-C! Kazi ipo!
 
yes, afu tundu lisu awe spika wa bunge na mwakyembe naibu spika, blv me hii inji itasonga mbele!
 
Sitta na wenzake wote walioko ccm ambao unawapgia debe hapa hawafai hata kidogo. Wote wana tamaa ya madaraka, wana nidhamu za uoga 2. Kama kwel ni majasiri bas watoke huko waliko il tujue kama kwel wana uchungu na wa Tz.
 
Mtoto wa nyoka ni nyoka tu....Huyu SITTA amefanya kazi na MAFISADI wa CCM so anajuwa njia zote na michezo yote ya kuiba hela bado hafai kuwa Rais lazima DR SLAA ndio awe RAIS huyu hata akiwa waziri mkuu ni powa maana akileta upuuzi kazini anapigwa chini...ila hicho kiti cha Rais hatutaki tena kumuona CCM
 
DR Slaa bado ana nafasi ya kuiongoza Tanzania. pia chadema bado haijamtangaza mgombea wa 2015. Demokrasia itatuletea mgombea mwenyesifa na anaekubalika kwa wakati huo. kama DR anakubalika au mwingine the time will tell as a minutes in politics ha great impact
 
Wachangiaji na jazba masuala hayo ya Dini yaacheni kama yalivyo waTZ hatujalelewa hivyo jamani.Mawazo yako ni mazuri kwani Product zote za Upinzani orijin yake unaijua hivyo ni uamuzi wa Mtu
 
Habari wana JF,
Mimi naona CHADEMA bado ina safu inayojitosheleza kuongoza nchi ikiongozwa na Dr Slaa, ofcoz japokuwa chama hakijachagua mgombea kwa mwaka 2015. Sioni kwa nini mtoa hoja umeona kuna pengo linalomwitaji Mzee Sita. Sijafikiria kama kuna mtu Tanzania mwenye uwezo wa kuongoza hii nchi zaidi ya Dr Slaa kwa sasa. Sita, Magufuli, sumaye, Ahmed salimu, Mwakyembe, Sinde, Mwandosya, na wengine kama wakitaka kuhamia CHADEMa wahamie lakini si kwa lengo la kugombea nafasi ya Uraisi 2015. Watahitaji kufanya kazi ya ziada kwa kuwa tayari CHADEMA kuna candidate wa nguvu na wala hatuchanganywi na propaganda za kuanza kuonyesha kwamba et CHADEMA hakina competent candidate wa kuongoza nchi hadi kianze kumezea mate makada wa CCM.

Nimeona hoja za udini zinatumiwa na watu waliokata tamaa ili kuwagawa wa Tz. Ni jambo la ajabu sana kuona mtu anapokosa hoja anakimbilia katika uchochoro wa udini. Acheni mambo hayo. Tanzania hakuna udini. Hatutachagua kiongozi kwa misingi ya kidini bali tutachagua viongozi kwa misingi ya uwezo wao kutuongoza. Dini ndiyo zichague viongozi wake kwa misingi ya dini huko huko katika mambo yahusuyo dini na wala msituletee habari hizo za dini zenu katika masuala ya uendeshaji wa Serikali.

Itakuwa ni jambo la kujidhalilisha ikiwa eti na sisi wengine tutahamishwa kwenye hoja za misingi na watu wasio na uelewa wa kina wanaoshindwa kuchanganua hoja na kuamua kuchochora kwenda usawa wa udini. NAOMBA WANA JF AMBAO WENGI WANAELEWA, TUWE TUNADHARAU NA KUTOKUYUMBISHWA TUNAACHA MAMBO YA MSINGI, TUNAANZA KWENDA UCHOCHORONI KUJADILI udini, hoja ambazo zinachomekewa kutoka kusikojulikana kwa lengo la kuhamisha mijadala.

HAKUNA UDINI TANZANIA. ANAYEKOSEA ATADHIBITIWA NA ANAYEFANYA VEMA ATAPEPELEWA BILAKUJALI DINI ZAO.
 
Wadau,
Sitta ni nguli wa siasa na yuko vizuri sana. Dr. Slaa analijua hili.
Alitamani sana kumpa Sitta nafasi yake 2010...
 
Back
Top Bottom