Wana JF natamani Sitta
angegombea urais kupitia Chadema 2015 awe Rais halafu Dr Slaa akagombee
ubunge ateuliwe kuwa PM. Mawaziri akina mwakyembe, Ole Sndeka, Kilango,
Mnyika, Mdee, Lissu nk. Nadhani hiyo timu ingefanikiwa sana.
Sitta na Dr ni watu wakali, wanaichukia rushwa, wana busara na ni
waadilifu.
Ukimwangalia Sitta na ukirudi ukimwangalia Dr Slaa, unauona unyerere
ndani yao. Pamoja na hawa mabwana kuwa na maadui wengi, ulishawahi
kusikia wanatuhumiwa au kuzushiwa rushwa? Hawa maadui wangekuwa hata na
chembe ya ushahidi wa rushwa wangeutumia.
Waulizeni watu wanaotokea Hanang au Urambo na pia chunguza mwenyewe
utagundua hawa mabwana ni kati ya rare breeds zilizobaki Tz.