Sitta atoboa siri ya CCJ

Bandugu mnajadili nini?maana sielewi kati ya 6 na matumizi ya lugha na pia ukabila.tuwe makini kidogo basi.
 
kunauwezekano anatoka mwakaleli msimshangae maana watu wa mbeya ndio walivyo
Mwanaweja huo ni utambulisho wa mtz kwa kukulupuka hatujambo anza mwanzo utaona walio jiita watalamu wamekosolewa jenga hoja utasomeka kama hauna potezea
 
ha! ha! ha! ha! ha! duh! hii sridi nimecheka mpaka nikahisi nipo jukwaa la funs and gossip! mkuu asante kwa habari, umeeleweka sana ndo maana watu wamejibu wanakukosoa ili kupunguza stress za maisha tu.
 
WakUu wa CCJ wakiongozwa na katibu mpya wa CCJ Nape wafana sana kwenye uzinduzi wa CCJ.

Wale vigogo wa CCJ waja na njia mpya kabisa ya kujinasubua ndani ya ccm sasa waamua wafanye mikutano kwa mlango wa CCM lakini cha ajabu ambacho waelevu tumegundua ni ile safu kuu ya CCJ akina Sitta, Mwakyembe, Kilango na wengine wengi kasoro Mpendazoe.

Hawa jamaa wameapa kuwa CCJ ni kama Parasite ndani ya CCM ambaye anataka apewe nafasi 2015 la sivyo watajuta.
Uwezo wa kifedha hasa Sitta na wenzake ndio jeuri yao kwa sasa ikionekana wakuu wa kaya haswa JK akibaki anashangaa tuu.
Hawa ni vigogo mafisadi wema ambao kwa sasa wanaishi ndani ya CCM lakini huku wakiamua kuitangaza CCJ
Kwa dhana ileile CHAMA NI WATU SIO JINA KAMA WENGINE WADHANIAVYO.


Nawasilisha
 
wana jf mnasoma wapi? mbona mi nimemuelewa sana tu, na hayo matamshi hiyo ni result tu ya mazingira na mother tongue. lakini si kwamba akiwa na matamshi hayo ndo hamake sense,
 
Waungwana, hakuna ubishi tena kwamba mapacha watatu wa CCJ. Nnape Nauye, Samwel Sitta na Harrison Mwakyembe wameamua kutinga magogoni Street 2015. Hawa waanzilishi wameamua kumpiku mzee wa monduli Edward Lowassa kushika uongozi wa 2015. Huu mpasuko ndani ya CCM kwa hakika unakuja kuimaliza chama cha magamba. Ila kwa kasi ninayoiona ndani ya mapacha watatu wa CCJ.....wagombea wengine inabidi wawe macho. EL na kundi lake, JK na chaguo lake pia inabidi wajipange kisawasawa.....
 
Huyu bwana sitta naona anazeeka vibaya.
Kama ana jamaa zake hapa JF wamshauri akapumzike na heshima yake kabla hajageuka kioja.
 
Mwanangu, Sita siyo stable tena kwa sababu nyingi tu. Lakini kubwa ni dhamira yake (nadhani iliyo nzuri) na matendo yake ambayo ni kinyume, na dhamira yake. Na anafanya hivyo kwa sababu ya chama chake. Wote tunajua ukiwa ndani ya sisiem inabidi uwe mnafiki kubwa uweze kulinda maovu ya kifisadi ambayo ni itikadi ya chama hicho. Hili linamsumbua sana Sitta, ndio maana alitaka kuanza ccj. Sasa hili la kutaka kuanza ccj kuwekwa hadharani kuwa alihusika linamtesa sana, anashindwa kupima ni kwa namna gani hasa wanafiki wenzake ndani ya chama wanamfikiria. Angekuwa na pa kukimbilia angeondoka lakini kwa sasa hana, inambidi anganganie ndani ya ccm kwa unafiki unaomdhalilisha sana akiomba kuwa muda utapita na yote yatakwisha (time is a great healer). Uspika walimnyima kwa kuwaumbua mafisadi, sasa anataka kuwabambeleza mafisadi walewale wasimtoe roho, kwa uhakika anajua urais hawezi kuupata akiwa ndani ya hiki chama kinachoelekea ambako siko.
Mungu msaidie Sitta aweze kufikiria tena kama msomi. Amen.
 
Magamba hawana effect tena, juzi Mbeya hao mapacha wa CCJ waliulizwa na wananchi kuwa kuna msiba? Hawana jipya, hawana ajenda ya msingi. Huyo Sita kawambia wanambeya wachache waliohudhuria kuwa wana mpango wa kuzalisha umeme ambao watauzia na S. Africa, muda huo huo wanadaiwa kutoa rushwa ili bajeti yao ipite. CDM iko juu sana wajipange miaka miwili hii kwani magamba wako karibuni kulipuana wenyewe, hawana mvuto, hawana sera.
 
Hivi nyie vizabinazabina mnashida gani jamani toeni hoja zene akili na siyo huu upupu utawawasha wenyewe!!
 
Chama cha magamba wanajaribu kumtumia Mnafiki Sitta ili aje awasaidie kwenye kampeni Igunga wakidhani kuwa kupitia kwa Mnafiki Sitta ambaye ni mwenyeji wa Tabora wataweza kushinda ubunge Igunga baada ya Rostam Mizizi kujiuzulu!
 
mwanakijiji ni kama mtoto wa mkulima!, nawashauri wabadilishe hayo majina yasiyoendana na ukweli!
@foxy fanya mawasiliano na msajili wa vyama atakupa majibu sahihi zaidi!, umuulize pia kuhusu CCK!
 
Back
Top Bottom