Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,606
- 29,754
Umuofia kwenu,
Nguvu ya Taifa lolote ni vijana. Nchi inaweza kuwa na advancement kubwa kwenye teknolojia na sekta zingine lakini kukiwa na ombwe la vijana kwenye jamii ama nchi hiyo ni kujiweka rehani. Vijana wa jamii yeyote huandaliwa kushika hatamu pale wazee ama wazazi wao wanapoishia.
Nimeanza na dibaji hiyo kwa kuangazia kwa umuhimu dhima ya vijana ndilo Taifa la kesho, mimi ninadhani Vijana na Taifa iwe ndiyo slogan yetu kwa sababu neno Kesho kutumika ni kuwabagua ama.kuwaengua vijana kwenye michakato muhimu inayohusu Taifa letu kujikwamua kutoka nyanja mbalimbali.
msomaji wangu, hebu jaribu kuvuta hisia na kumbukumbu ya safari yako ya maisha. Tuangalie kwenye stream ya elimu. Tangu umeanza shule mlikuwa wangapi, na endapo ilifanikiwa kusonga mbele, ni wanafunzi wangapi mlipata alama za kusonga mbele kielimu? Ni wangapi waliachwa kwa kukosa vigezo vya kuchaguliwa elimu ya mbele?
Ukiangalia kwa jicho tunduizi utagundua kuwa vijana wengi wanaachwa mitaani bila tentative plans kuwasaidia juzi mbalimbali ili kuwaandaa kuwa wanafamilia ama viongozi wa baadaye.
VIjana wanapopishana na maarifa yanayoweza kuwasaidia kuyakabili na kuyabadili mazingira ni dalili na maandalizi mabaya kwa Taifa zima. Nasema Taifa kwa sababu tunapokuwa na wataalam wachache na kundi kubwa la illetrate ni ngumu sana kufikia malengo chanya ya kisekta.
Tunaona polisi wakikabiliana na mamundi ya kihalifu ambapo wengi ni vijana. Tunapaswa kuweka mikakati ya kuondoa uhalifu kwenye jamii hususan vijana ili kuwaepusha kujiingiza kwenye mambo yasiyofaa
USHAURI
CC: Pascal Mayalla Retired LIKUD FaizaFoxy Maxence Melo Depal Deborah9007 raraa reree Extrovert Erythrocyte G70 mangi jr mrangi ChoiceVariable MP0NJ0LI
Nguvu ya Taifa lolote ni vijana. Nchi inaweza kuwa na advancement kubwa kwenye teknolojia na sekta zingine lakini kukiwa na ombwe la vijana kwenye jamii ama nchi hiyo ni kujiweka rehani. Vijana wa jamii yeyote huandaliwa kushika hatamu pale wazee ama wazazi wao wanapoishia.
Nimeanza na dibaji hiyo kwa kuangazia kwa umuhimu dhima ya vijana ndilo Taifa la kesho, mimi ninadhani Vijana na Taifa iwe ndiyo slogan yetu kwa sababu neno Kesho kutumika ni kuwabagua ama.kuwaengua vijana kwenye michakato muhimu inayohusu Taifa letu kujikwamua kutoka nyanja mbalimbali.
msomaji wangu, hebu jaribu kuvuta hisia na kumbukumbu ya safari yako ya maisha. Tuangalie kwenye stream ya elimu. Tangu umeanza shule mlikuwa wangapi, na endapo ilifanikiwa kusonga mbele, ni wanafunzi wangapi mlipata alama za kusonga mbele kielimu? Ni wangapi waliachwa kwa kukosa vigezo vya kuchaguliwa elimu ya mbele?
Ukiangalia kwa jicho tunduizi utagundua kuwa vijana wengi wanaachwa mitaani bila tentative plans kuwasaidia juzi mbalimbali ili kuwaandaa kuwa wanafamilia ama viongozi wa baadaye.
VIjana wanapopishana na maarifa yanayoweza kuwasaidia kuyakabili na kuyabadili mazingira ni dalili na maandalizi mabaya kwa Taifa zima. Nasema Taifa kwa sababu tunapokuwa na wataalam wachache na kundi kubwa la illetrate ni ngumu sana kufikia malengo chanya ya kisekta.
Tunaona polisi wakikabiliana na mamundi ya kihalifu ambapo wengi ni vijana. Tunapaswa kuweka mikakati ya kuondoa uhalifu kwenye jamii hususan vijana ili kuwaepusha kujiingiza kwenye mambo yasiyofaa
USHAURI
- Sera ya elimu iboreshe hitaji la kila Mtanzania kuanzia umri wa miaka 18 awe anakiwango cha elimu ya cheti au juu ya hapo. Cheti ninachozungumzia hapa ni cha ujuzi na siyo certificate of attendance.
- Shirika la Viwango TBS wabuni mkakati wa kutoa elimu ya viwango kwa uzalishaji unaofanyika ngazi za awali kabisa. Hivi sasa TBS imegeuka mradi wa maafisa wachache ambao wamejifungia maofisini wakiwasubiri wazalishaji kwenda kujisajili huku ikiweka urasimu mkubwa kwa wateja. Sana sana outreach ya TBS yaani kazi za nje ya ofisi ni kwenda kukagua, kukamata na kuharibu bidhaa zilizochini ya viwango. Vijana wakianza kuelimishwa mashuleni kuhusu umuhimu wa ubora wa bidhaa itassidia kuondokana na uzalishaji wa kienyeji ambao umeshamiri nchini
- Serikali ngazi ya wilaya kuanzisha makambi ya vijana ili kuwakutanisha na wataalam, wajuzi na wakufunzi mbalimbali wajifunze ujasiriamali wa uzalishaji, ufundi na huduma mbalimbali. Wahitimu wa makambi hayo wapewe vyeti ama.leseni za ujuzi husika.
- Jeshi la Magereza lianzishe program ya uzalishaji kwa kuwahusisha vijana ambao watajitolea. Programu hizo zijikite kwenye kutoa ujuzi kwa vijana ili kuongeza soko la ajira kwa wahitimu
- Vijana waliopo ngazi ya familia na hawana ajira, elimu wala ujuzi wowote waanze kuandaliwa program za kuwafikia na kuwapatia ujuzi na nyenzo za kujikimu.
- Mikopo ya vijana, wanawake na wenye ulemavu iboreshwe ili kusaidia wimbi kubwa la vijana ambao kwa namna mbalimbali wamekosa nafasi za kuendelea kimasomo.
CC: Pascal Mayalla Retired LIKUD FaizaFoxy Maxence Melo Depal Deborah9007 raraa reree Extrovert Erythrocyte G70 mangi jr mrangi ChoiceVariable MP0NJ0LI