Sirro: Marufuku bodaboda baada ya saa 6 usiku

Sirro: Marufuku bodaboda baada ya saa 6 usiku

Alafu kuna mtu atasema hawa watu wanafikiri kwa makini.
Bado tunataka uchumi ukue.....teh teh
Badala ya kufanya kazi yako ya kulinda usalama wa raia na mali zao, unawalazimisha kulala ili na wewe ulale.
Hapa kazi tu!!!
 
Kamanda wa polisi mkoa wa Dar Simon Sirro amepiga marufuku boda boda kufanya kazi baada ya saa 6 usiku kutokana na sababu za kiusalama


Lakini ukisikiliza hajasema ni marufuku, alichosema anawashauri kutokufanya biashara hiyo baada ya saa sita kwa usalama wao
 
Kawapa ulaji taksi haya wale wazee wa UBER fursa hyo ya kutoboa mpaka mornieeee
 
Kamanda wa polisi mkoa wa Dar Simon Sirro amepiga marufuku boda boda kufanya kazi baada ya saa 6 usiku kutokana na sababu za kiusalama


Mbona mnapenda kuwawekea watu maneno mdomoni?, Na kwa namna wadau wanavyo comment inaonekana hawajajisumbua kupoteza mb zao kumsikiliza Siro!. Kamanda hajapiga marufuku, ameshauri, ndio maana amehusisha Na muda wa kufunga bar, kwa maana baada ya hapo hakuna wateja salama Sana. Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.
 
Saa 6 ni mapema sana kwa mishemishe za dar ndo kwnz unakuta watu wanaamka, ikumbukwe pia ndio muda huduma za daladala maeneo mengi hukata hivyo kukataza daladala baada ya saa 6 usiku ni mateso kwa wale raia wema wanaofanya kazi zao usiku.
 
Hiki ni kituko kingine.
Shughuli nyingi za Kiuchumi huwa zinafanyika usiku pia kwa Dar, watu hutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine, na usafiri rahisi wa binafsi kwa mtanzania wa kawaida ni pikipiki, iwe ya mtu binafsi anaimiliki au Kukodi bodaboda. Sasa unapozuia zisifanye kazi, unataka watu watembee kwa miguu au wasitoke usiku?
 
Mbona huyo bwana katoa ushauri alafu wewe unasema kapiga marufuku?

Ushauri sio lazima upokelewe.. Ni wewe mwenyewe kuangalia usalama wako, ila mwanausalama ndio kashauri hivyo!
 
Wenzetu huko dunia ya kwanza pamoja na maendeleo yoote.., Wanafanya kazi mchana na usiku.

Hapa TANZANIA Bw.Sirro anakataza watu kufanya kazi kwa sababu za kiusalama.

[HASHTAG]#TANZANIA[/HASHTAG]yaVi-wonder
Anakwepa majukumu yake, maana kazi lake ni kulinda raia na Mali zao...sasa anajipunguzia kazi!!!
 
mbona matukio mengi ya uhalifu kwa kutumia bodaboda yanafanyika mapema tu kabla ya huo mda....aje na mbinu nyingine ya kukomesha uhalifu sio hii!
 
Moja ya sababu ya ajali nyingi za boda boda ni usingizi, wengi wanakesha labda kulala kuanzia sasa tatu asubuhi . Nina jirani yangu alikesha sasa mida ya alfajiri akapata abiria alikuwa anawahi kazini kwenye kona, alilaza pikipiki utafikiri yupo ktk mashindano pikipiki likamshindwa akapalamia mtaro, akapoteza faham bahati nzuri alivaa kofia la sivyo tungemzika.
 
Kabla ya kutoa,matamko lazima muwe mnajua kuna mgawanyo wa kazi,kama wewe unafanya kaz mchana,jua wapo wengine wanafanya usiku,Kama umeshindwa kulinda Usalama unajiudhuru wanakaa wanaoweza,msikwepe majukumu yenu ya ulinz na Usalama kwa kuzuia kaz za watu wengine.
 
Nashauri;

Jukumu lao la msingi ni kulinda Wananchi na Mali zao. Hata kama natoka Dar na kuelekea Mwanza, mwanausalama hapaswi kuniambia niahirishe safari yangu kwakuwa pori fulani lina wahalifu, badala yake wanapaswa ama kuwaondoa wale waharifu pale ili nipite salama au wanipitishe pale salama.

Kuzuia raia kufanya shughuli zao kisa wanataarifa za kiintelijensia za kuwaambia mipango ya uhalifu bila kuzuia uharifu ni ku-surrender kwa wahalifu na ni kukiri kushindwa na wahalifu.

Nimeshauri tu.
 
Back
Top Bottom