Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 5,180
- 17,646
Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa, Deogratius Mahinyila, amesema ni muhimu taarifa zote kuhusu mazingira ya kifo cha marehemu Maradufu kuwekwa wazi ili kuondoa sintofahamu. Mahinyila ameeleza kuwa marehemu alikutwa na fedha taslimu kiasi cha Tsh. 428,000 ambazo alikabidhiwa, huku pia akibainisha kuwa mwili wa marehemu ulikuwa umetokwa na damu mdomoni.
Amesema wataalamu wa uchunguzi wa maiti (pathologists) waliowasili usiku wa kuamkia leo kutoka mikoa ya Mwanza na Geita walikuwa bado hawajaanza kufanya uchunguzi hadi majira ya saa nane mchana. Aidha, Mahinyila amesema walipata taarifa kuwa mtaalamu mwingine wa uchunguzi kutoka Dodoma anatarajiwa kuungana na timu iliyopo kwa ajili ya kuendelea na uchunguzi huo.
Soma: Dereva wa John Heche akutwa amefariki chumbani Kigoma
Mahinyila pia amehoji hatua ya wataalamu hao kupelekwa katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Simon Sirro, mara baada ya kuwasili asubuhi ya leo. Amesema haijulikani kikao hicho kilihusu nini na kama ni sehemu ya utaratibu wa kawaida wa kazi zao, huku akieleza wasiwasi kuhusu kauli ya Sirro aliyenukuliwa na Clouds TV akisema kuwa kwa uzoefu wa kipolisi, kifo cha Maradufu kinaonekana kuwa cha kawaida.
Amesisitiza kuwa muda ni mwalimu mzuri na ukweli utajidhihirisha kwa wakati wake, akibainisha kuwa wao wataendelea kuwepo Mochwari ya Maweni, Kigoma hadi uchunguzi utakapokamilika. Mahinyila amesema matokeo ya uchunguzi yatasaidia kuweka kumbukumbu sahihi ya tukio hilo na kutoa majibu ya maswali yanayoendelea kuibuliwa.
Amesema wataalamu wa uchunguzi wa maiti (pathologists) waliowasili usiku wa kuamkia leo kutoka mikoa ya Mwanza na Geita walikuwa bado hawajaanza kufanya uchunguzi hadi majira ya saa nane mchana. Aidha, Mahinyila amesema walipata taarifa kuwa mtaalamu mwingine wa uchunguzi kutoka Dodoma anatarajiwa kuungana na timu iliyopo kwa ajili ya kuendelea na uchunguzi huo.
Soma: Dereva wa John Heche akutwa amefariki chumbani Kigoma
Mahinyila pia amehoji hatua ya wataalamu hao kupelekwa katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Simon Sirro, mara baada ya kuwasili asubuhi ya leo. Amesema haijulikani kikao hicho kilihusu nini na kama ni sehemu ya utaratibu wa kawaida wa kazi zao, huku akieleza wasiwasi kuhusu kauli ya Sirro aliyenukuliwa na Clouds TV akisema kuwa kwa uzoefu wa kipolisi, kifo cha Maradufu kinaonekana kuwa cha kawaida.
Amesisitiza kuwa muda ni mwalimu mzuri na ukweli utajidhihirisha kwa wakati wake, akibainisha kuwa wao wataendelea kuwepo Mochwari ya Maweni, Kigoma hadi uchunguzi utakapokamilika. Mahinyila amesema matokeo ya uchunguzi yatasaidia kuweka kumbukumbu sahihi ya tukio hilo na kutoa majibu ya maswali yanayoendelea kuibuliwa.