Sirro: Marufuku bodaboda baada ya saa 6 usiku

Sirro: Marufuku bodaboda baada ya saa 6 usiku

Hapa mzee sirro hakufikiri kwa kina, mtaongeza umasikini kwa watanzania
Bodaboda za usiku ndio usafiri mkuu wa ma Bar maid wote wa mijini, unakuta mtu anatoka Waungwana Bar na anaishi Kimara, saa saba usafiri ni Bodaboda tu,
Kuna wauza Nyama ambao wanakwenda machinjioni saa sita usiku kuwahi foleni ma pia kuna dharura za hapa na pale za usiku

Kweli kazi tunayo awamu hii
 
Sasa umekodishwa saa tano na nusu kwenda mahali, saa sita imekukuta njiani unarudi kwako - ukikutana na hao polisi ukiwaeleza watakuelewa kweli?
 
Anadhani kila mtu analala saa 2 usiku kama yeye?
 
Majambazi yanayotumia pikipiki huwa wanafanya matukio mchana kweupe wala hawasubiri giza liingie
 
em twende mbele na kurudi nyuma RPC anaweza kuzuia chombo cha moto?
je ajavunja KATIBA kwamba kila mtanzania ana haki ya kwenda popote pale na kuishi/kufanya mambo yake) mradi havunji sheria?

Au anataka tupunguze kumuongelea makonda na utumbo Wao walioufanya
 
Kwanini wao wasihakikishe usalama unakuepo masaa 24...kazi yao nin..mbona hawaendani na technologia...nilitegemea aje aseme sasa ni ruksa kufanya kazi muda wowote....hii polisi ni analog ndo mana ata JF imewatoa jasho...
 
Kamanda wa polisi mkoa wa Dar Simon Sirro amepiga marufuku boda boda kufanya kazi baada ya saa 6 usiku kutokana na sababu za kiusalama


Mkuu hapo kabugi .
Kwa hiyo ukitoka ukachelewa uwe na bajeti ya Guest.
Alafu pia hakuna dharura mkuu.
Hii habari ni fupi sana.
Funguka zaidi.
 
Siyo marufuku anawashauri maana kwa kuongeza chumvi ndo wenyewe
 
Wenzetu huko dunia ya kwanza pamoja na maendeleo yoote.., Wanafanya kazi mchana na usiku.

Hapa TANZANIA Bw.Sirro anakataza watu kufanya kazi kwa sababu za kiusalama.

[HASHTAG]#TANZANIA[/HASHTAG]yaVi-wonder
Mda huo wanaopaswa kuhakikisha kuna usalama(polisi wake) wanaota ndoto za kipuuzi na wengine wamelala na machangu
 
kwa hiyo watu watembee kwa mguu! maana hapa Dar saa saba usiku wapo wanaorudi makazini na wale wanaoenda mfano machinjioni kuchukua nyama za supu na kuuza kesho yake, Hamuoni mtakuwa mmewapa wakati mgumu watu kama hawa. We kujibu ndio bila kubalance, hii haitazuia uharifu, sana sana itaongeza rushwa mana sasa polisi watazunguka mitaani kuwabugudhi bodaboda wawape chochote au kuwakamata.
Serikali iwekezekwa polisi kukabiliana na changamoto hii na wala sio kuwazuia bodaboda usiku, wanatusaidia sana sie wa mtaani tusikabwe ovyo. Hapa kipaumbele unachosema hakizingatiwa
Unayeongea naye anakula kwa shemeji yake. Hajui kuwa kuna watu saa kumi alfajiri kwenda feri kuchukua samaki
 
Afadhali ili wale wamama wa ccm nao waisome namba vilivyo. Shenz.
 
Back
Top Bottom