Siri ya Mwenge wa Uhuru

Hauna jipya zaidi ya kuabudu mashetani. Kuna taarifa rasmi kuwa Mwenge huo unapofika Rombo-Kilimanjaro hufanyiwa tambiko mbalimbali ili kulinda viongozi wa nchi.

Taarifa zinaonesha kuwa kuna Wazee maalum wameandaliwa kule Rombo kwa ajili ya matambiko haya kila mwaka.Mmoja wa wazee hao aitwaye Mzee Malamsha amenithibitishia hicho.

Kwenye matambiko hayo,kafara hutolewa.Na kadhalika na kadhalika.Ndio maana,kila mwaka Mwenge wa Uhuru lazima ukimbizwe Mkoa wa Kilimanjaro na kufika Wilaya ya Rombo.

Mwenge huu ni wa kuupiga vita. Unaleta laana zaidi ya baraka. Unatubakisha kama nchi kwenye kuabudu mizimu badala ya kusonga mbele kimaendeleo.

Laana za Mwenge huu ndizo zinazotufanya tusieendelee. Ni muda sasa wa kuachana na imani hizi za kishirikina kwa kuachana na Mwenge huu.
Nilifundishwa kazi za mwenge ni kulika maadui wetu wakubwa kama ujinga, maradhi na rushwa sasa nashanga vyote vinazidi kukua inamaana mwenge umeshindwa kuvimulika mika yote 51? kama umeshindwa ni bora ukawekwe makumbusho tutauenzi kwa kushindwa kwake kufanya kazi iliyo kusudiwa.
 
mimi niliwahi kumuuliza baba nikiwa mdgo ya maana ya mwenge na faida zake,, nikaambulia kofi kali la mdomo na kuniambia unataka tufungwe!! nikashangaa tufungwe??!!!
 
Hongera kk kwa hoja yako nzur kiukweli hata mm nimekuwa na maswali mengi niliyokuwa nikijiuliza juu ya umuhimu wa huhu mwenge lakini sijapata jibu sahihi.Kama umuhimu wake nikuzindua miradi ya maendeleo bado haitoshi kuonekana kuwa unaumuhimu.kihistoria nchi nyingine duniani iliyowahi kuwa na kitu mwenge ni german but wenzetu walishaa chana na huu utumwa wa kuambudu kitu kisicho na manufaa achia mbali kwa wananchi wake hata taifa kwa ujumla. Hiv jama kwanini hiki kitu kisiwekwe makumbusho kiwe kama kumbukumbu ili kisiendelee kutafuna bure fedha za walipa kodi.
 
Nilifundishwa kazi za mwenge ni kulika maadui wetu wakubwa kama ujinga, maradhi na rushwa sasa nashanga vyote vinazidi kukua inamaana mwenge umeshindwa kuvimulika mika yote 51? kama umeshindwa ni bora ukawekwe makumbusho tutauenzi kwa kushindwa kwake kufanya kazi iliyo kusudiwa.

Kitu hakiwezi kushindwa ukakienzi mkuu, zaidi zaidi utakidistroy ili usikione klkukumbushe machungu
 
mimi niliwahi kumuuliza baba nikiwa mdgo ya maana ya mwenge na faida zake,, nikaambulia kofi kali la mdomo na kuniambia unataka tufungwe!! nikashangaa tufungwe??!!!

Kama kweli huyo babako hafai
 
Chenye mwanzo hakikosi kuwa na mwisho, mwisho wake ndo waja sasa kwani waTz wengi tunazidi kujitambua na kukataa vitu visivyokuwa na faida kama hivi
 
Kifupi serikali zote ni chawi serikali ya marekani unaabudu vichwa vya mbuzi pale jengo yai kuna matambiko nakila rahisi lazima ayafanye itakuwa serikali ombaomba!
 
Mwenge wa UHURU hukimbizwa kila mwaka nchi nzima ukiwa na kauli mbiu mbalimbali, katika mbio hizo mwenge huzindua majengo mbalimbali ya umma kama vile Ofisi, Zahanati na Shule ambapo zaidi ya 95% ya majengo hayo yanakuwa yamejengwa chini ya kiwango. Utasikia ndugu mgeni rasmi ofisi hii imegharimu shilingi milioni 10 wakati ujenzi wake halisi umeghlimu shilingi milioni 2. Hamisi Kagasheki mkoani Kagera aliwahi kuamuru shule iliyofunguliwa na Mwenge ipigwe nyundo yote kabla haijatumika kisa ilikuwa na nyufa za kuweza kupitisha simu ya mkononi.Mwenge wa uhuru una gharama zifuatazo:a)Mafuta ya magari kuzunguka nchi nzima.b)Malipo kwa wanaoukimbiza nchi nzima.c)Magari ya kuzunguka nchi nzima na matengenezo yake ya mara kwa mara.d)Gharama za maandalizi ya kila mahali utakapolala nchi nzima.e)Gharama za walinzi mahali unapolala kila usiku nchi nzima.f) Muda wananchi wanaopoteza kuusubiri na kukesha nao n.kMaswali ninayohitaji wenzangu mnisaidie majibu yaje:a)Mbona kila mwaka mwenge unapozimwa hatujawahi kusomewa mapato ya mbio hizo?b)Tunapata faida gani kutokana na kuukimbiza mwenge kila mwaka?c)Hivi kweli viongozi wa mbio za mwenge wanapozindua majengo yanayotaka kubomoka hawaoni kuwa yako chini ya kiwango?WABUNGE WETU MWENGE HATUUTAKI,,,,,,,,,,,,,. HAUNA TIJA KWETU ……..

Umenena mkuu, ni Gharama sana na bajet yake hivi huwa inapita chini ya wizara gani utamaduni? Au ni zile wanazochangishwaga wafanyakazi wa Gvt na wanafunzi
 
wachangiaje acheni ushabiki wa vyama ongeeni fact mkiwa kama GT. kama huji kitu ni afadhali kuuliza ufahamishwe. mwenge kila mwaka azima uzunguk mikoa yote na wilaya zotebia kubagua. sasa iweje useme lazima upite rombo utambikiwe? wewe umeshaenda wilaya zingine ukaona wanafanyaje. Fanya uchunguzi sio kuleta ushabiki wa vyama vya siasa. Kama hujui kaa kimya.
 
Wale jamaa zetu siku hizi wanatumia magari aina ya Nissan private No.Huwa wanaichukua hiyo tochi wanaenda nayo chemba kuibadirisha tambi na kuongeza wese,infact mmoja wao ni shemeji yangu alishawahi kuniambaiaga kuwa katika ile tochi kuna siri kubwa sana ya kiuchawi na mizimu iliyoachwa na........ aliniambia kuwa siku tukiupuuza ndiyo itakuwa mwisho wa SISIEMU,
Mimi ndiye bwana mungu wako usiabudu miuungu wengine. Je tochi ile ni sanamu,muzimu,nyoka wa shaba,au Msukule?????????????????????????????????????????????????

Mkuu shaka ondoa!
Sie hatuna lazima ya kuushika bt yupo mwenye nguvu,jemedari wa vita asiyeshidwa!tunamlilia kila siku/tunamuomba ndo anafanya kazi yake ndo maana mambo yanazidi kuharibika kila kukicha!
...ile ni miungu/mizimu watu wanaiabudu bila kujua!
Mungu wetu na ikajulikane km ww ndie Mungu
 
Kitu hakiwezi kushindwa ukakienzi mkuu, zaidi zaidi utakidistroy ili usikione klkukumbushe machungu

Nakubaliana na wewe mkuu lakini pia tunapo sema historia haimaanishi mazuri tu hata mabaya ni sehemu ya historia mkuu na jua nawewe katika maisha yako kwa ujmla kuna mambo mazuri mengi unayyakumbuka na mambaya pia yanaweza kuwepo mkuu, lakini kwa ujumla naunga mkono kkuuwa mwenge ikiwezekana uteketezwe mazima kwani ukiacha kushindwa kufikia malengo yake pia unatumia gharama kubwa sana katika kuukimbiza. Wewe fikiria mwenge unaenda wilaya 1 kwa milioni zaidi ya 600 halafu unazindua mradi wa milioni80 na unakuta miradi mingine tayari imeanza kuharibika si ukichaa hou mkuu?
 
mimi nawashangaa watanzani mnatamani kuua kila kilicho chenu sijui mtabaki na nini kinachotuunganisha kama TAIFA

MWENGE mnataka hata kesho itangazwe mbio za mwenge zimepigwa stooop for good

MCHAKAMCHAKA SHULENI mmesha futa na kutokomeza kabisaa!

MUUNGANO ndio huo mnapiga kelele usiku kucha mnatamani uvunjike hata leo jioni!

JKT mnataka waende vijana wakujitolea na wasomi wasiguswe.
Mtaua kila kitu chenu mwisho mbaki kama TAIFA lisilo na identity yake.mwisho mtataka na shule mzifute sijui mtabaki na nini. CHANZO CHA UMASIKINI WETU NI KUTOJITUMA KAZINI NA MATUMIZI MABAYA YA MALI.Watanzania kila mtu anataka ku win maisha hata bila kufanyakazi! Akipata kazi atakunywa pombe 24 hours seven days a week.sasa mtu akikuuliza huo mwenge wewe umewahi kuchangia hata cent tano? jitume, fanyakazi,acha kulalamikia vitu ambavyo siyo sababu ya umasikini wa kipato.
 
unachosema mkuu acheche kina ukweli, nakumbuka 2007 nilikuwa najitolea kufundisha shule flani kijijini kwetu, mwenge ukaja kuzindua jengo la bweni la wasichana, nilipewa assignment ya kuandaa ndoo ya mchanga na kuupeleka staff room, baada ya mwenge kufika ulioelekwa ofisini kisha ukazungukwa na wanajeshi, then ulizimwa halafu wakamwaga majivu na(mchanga?) kwenye mfuko, kisha wakaweka tena mchanga kidogo kutoka kwenye ile ndoo kwenye ule mwenge, ukawashwa shuguli za uzinduzi zikaendelea. nilipouliza hakuna aliyenipa jibu zaidi ya kusema kuwa baada ya kuhitimisha mbio za mwenge mchanga ule na majivu yale yaliyokusanywa nchi nzima huwekwa kwenye chombo kimoja na kusemewa vineno hv, then hutupwa baharini, ati ili kudumisha muungano...

Kama hujui kitu ni bora kunyamaza kuliko kutuletea imaginative story. Msingi wa story ni intuitive nature ya wachaga ambao wamebobea katika mambo ya imani yaani intuition. Let it be true kuwa mwenge una uhusiano na ushirikina, mbona hata hizo dini zote mnazoziamini ni full ushirikina? Acheni kudanganya watu.
 
Back
Top Bottom