Siri ya Mwenge wa Uhuru

Siri ya Mwenge wa Uhuru

Jaribu kuweka thread ya maana kama huna wacha,ila upuuzi huu hakuna atakayeuamini,Rombo wana matamiko gani ya kuweza kuleta laana kwa nchi,siamini kuwa mtu mzima jiamini.

hata mimi rombians siwaamini
 
Kichwa cha kufugia nywele akili za masaburi!!Rombo ndio kuna nini cha maana?potezea kama huna hoja!
 
Mwenge wa UHURU hukimbizwa kila mwaka nchi nzima ukiwa na kauli mbiu mbalimbali, katika mbio hizo mwenge huzindua majengo mbalimbali ya umma kama vile Ofisi, Zahanati na Shule ambapo zaidi ya 95% ya majengo hayo yanakuwa yamejengwa chini ya kiwango. Utasikia ndugu mgeni rasmi ofisi hii imegharimu shilingi milioni 10 wakati ujenzi wake halisi umeghlimu shilingi milioni 2. Hamisi Kagasheki mkoani Kagera aliwahi kuamuru shule iliyofunguliwa na Mwenge ipigwe nyundo yote kabla haijatumika kisa ilikuwa na nyufa za kuweza kupitisha simu ya mkononi.Mwenge wa uhuru una gharama zifuatazo:a) Mafuta ya magari kuzunguka nchi nzima.b) Malipo kwa wanaoukimbiza nchi nzima.c) Magari ya kuzunguka nchi nzima na matengenezo yake ya mara kwa mara.d) Gharama za maandalizi ya kila mahali utakapolala nchi nzima.e) Gharama za walinzi mahali unapolala kila usiku nchi nzima.f) Muda wananchi wanaopoteza kuusubiri na kukesha nao n.kMaswali ninayohitaji wenzangu mnisaidie majibu yaje:a) Mbona kila mwaka mwenge unapozimwa hatujawahi kusomewa mapato ya mbio hizo?b) Tunapata faida gani kutokana na kuukimbiza mwenge kila mwaka?c) Hivi kweli viongozi wa mbio za mwenge wanapozindua majengo yanayotaka kubomoka hawaoni kuwa yako chini ya kiwango?WABUNGE WETU MWENGE HATUUTAKI,,,,,,,,,,,,,. HAUNA TIJA KWETU ……..
 
Tija kubwa ya mbio hizi ni "KUWALAZA" wadanganyika waendelee kusema ndio mzee kwenye kila kitu........
 
Mwenge ni janga linalounguza kipato cha walala hoi. Mbaya zaidi baadhi ya watu hulazimishwa kuchingia bila kupenda.
 
Mwenge hauna tija, mwenge ni umasikini , mwenge ufutweee
 
Mimi nashauri mwenge uwekwe jumba la makumbusho sasa. Wakati mwingine ni kuendekeza ujinga. Msafara wa mwenge unaweza kutumia shilingi milioni 200 kwenda kuzindua au kuweka jiwe la msingi la chumba cha darasa ambalo thamani yake ni sh milioni 6 au 7!
 
mimi nashauri mwenge uwekwe jumba la makumbusho sasa. Wakati mwingine ni kuendekeza ujinga. Msafara wa mwenge unaweza kutumia shilingi milioni 200 kwenda kuzindua au kuweka jiwe la msingi la chumba cha darasa ambalo thamani yake ni sh milioni 6 au 7!

ndio maana watz tunadharaulika sana kwa upuuzi kama huu
 
Hii ndiyo serikali ya Bongo, cha kwanza ndiyo cha mwisho na ujinga ndiyo ujanja, angalia hii: hospitali za mikoa mfano ya Tabora (kitete) imefanyiwa matengenezo ya mamilioni lakini hakuna dawa, wagonjwa wanataka dawa au majengo? Wamejenga shule nyingi za kata pasipo kuwa na walimu, kilimo kwanza bila kuwa na soko na njia za kusafirishia mazao, msikate miti kuchoma mkaa bila kuwa na njia mbadala ya kupikia. Ni bora mjinga kuliko mwenye elimu asiyeweza kutumia elimu yake.
 
Ngojeni 'mchonga' awasikie.


.......................................
Historia haiishiwi wino.
 
Wadau,

Naamin kuna watu ambao kwa namna moja au nyingine wamewahi kuona faida za mwenge! Vilevile, kuna wengi kati yetu ambao hawajui kwa nini mwenge bado upo mpaka leo.
Binafsi, naona kwa sasa Mwenge wa Uhuru hauna maana tena kwa jamii ya Watanzania! Mara nyingi mwenge umekua ukipita kuzindua miradi, na kueneza virusi vya ukimwi pale unapolala!
Wanaohudhuria sherehe za mwenge kwa siku hizi ni viongozi wa mikoa au wilaya, vikundi vya sanaa, wanafunzi na wananchi wachache, hasa vijijini!
Kama mwenge umepoteza mvuto, kwanini ukimbizwe kila mwaka?
Zaidi unatuingiza hasara tu kwa kuchoma mafuta nchi nzima, kulipa posho za viongozi wake na kusambaza ukimwi.
Tuuweke makumbusho tu!

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Inawezekana kuna mambo ya kishirikina ndani yaki, lastime kuna waliokuwa wanasema yule kiongozi wa Mwenge at last lazima anakufa sijui kama lina ukweli hili.
Kuna wazee fulani pale Kilimanjaro maeneo ya Kiboriloni(kwa sasa hawapo tena) walikuwa wakisikia mwenge unakuja Moshi walikuwa wanaondoka maeneo ya hapo wanaenda huko milimani suala ni kwamba wasiuone tu huo mwenge mpaka utakapoondoka na wanasema walikuwa wakiamini kwamba ukiuona Mwenge unaweza kupata nuksi, balaa, mikosi na vilevile kuna mambo makubwa ya kishirikina yanafanyika.
Sisi vijana wa leo tujiulize Mwenge una faida gani kwa mwananchi na nchi wa/ya Tanzania?
 
wakuu mi nilisikia mwenge ni ushirikina, na kazi yake kubwa ni kuwapumbaza watanzania ili watawala waendelee kututawala. Maoni yangu ni kuwa kizazi hiki hatupumbazwi tena na washinde kabisa.
 
Laiti kama ningepewa mamlaka kufuta vitu visivvyo na manufaa kwa kwa watz ni mwenge maana huwasaidia makaburu weusi kuongeza magorofa na makampuni huku watz wakibaki hoi bin taabani
 
Hauna jipya zaidi ya kuabudu mashetani. Kuna taarifa rasmi kuwa Mwenge huo unapofika Rombo-Kilimanjaro hufanyiwa tambiko mablimbali ili kulinda viongozi wa nchi.

Taarifa zinaonesha kuwa kuna Wazee maalum wameandaliwa kule Rombo kwa ajili ya matambiko haya kila mwaka.Mmoja wa wazee hao aitwaye Mzee Malamsha amenithibitishia hicho.

Kwenye matambiko hayo,kafara hutolewa.Na kadhalika na kadhalika.Ndio maana,kila mwaka Mwenge wa Uhuru lazima ukimbizwe Mkoa wa Kilimanjaro na kufika Wilaya ya Rombo.

Mwenge huu ni wa kuupiga vita. Unaleta laana zaidi ya baraka. Unatubakisha kama nchi kwenye kuabudu mizimu badala ya kusonga mbele kimaendeleo.

Laana za Mwenge huu ndizo zinazotufanya tusieendelee. Ni muda sasa wa kuachana na imani hizi za kishirikina kwa kuachana na Mwenge huu.

Hii post ni ukweli mtupu, kula tano Vuta-Nikuvute. Kuna mistari kwenye biblia takatifu kwenye agano la kale (sikikumbuki vizuri) inazungumza kila kitu kuhusu Ibada za Mashetani, kwa uchache nakumbuka hivi........' Mmeweka miale ya moto kwenye milima na kuibudu, hii ni chukizo mbele za Mungu'. Kwa tafsiri ambayo haitaji mtu uwe na elimu ya chuo kikuu kuelewa Mwenge unahusika moja kwa moja. Ndio maana nchi hii inavitu vingi vya kishirikina kwa sababu nchi hii ina misingi ya Kishetani. Kwa ushahidi tu tizama utajiri tulionao na level ya maendeleo tuliyopo, inversely proportional.
 
Back
Top Bottom