schlumberger
JF-Expert Member
- Jun 15, 2012
- 890
- 350
Hakuna mwana chadema anayependa zitto afe ila wanataka mikono ya ccm inayomuelekea zitto ikatiliwe mbali ..
zitto ni kipenzi cha wana chadema hilo halina ubishi..wanachadema huwa wanasikitika sana wasiojua mienendo ya zitto....
wanataka kumuona zitto wao majukwaani,kwenye kila matukio ya chadema wanataka kumuona yupo ...hivyo ndo ilivyo mkuu...
zitto ni chadema na chadema ni zitto...
zitto + mbowe +dr.slaa == ushindi wa chadema 2015...
zitto + mbowe +dr.slaa== maumivu,kuchanganyikiwa kwa ccm
mbowe +dr.slaa - zitto == furaha na ahueni kwa ccm na mafisadi wote...
Hatimaye amewakana. Aibu yenu.
Umeambiwa utumie muda kuimarisha chama chako
Mateka wa fikra.Jadilini yote, Toeni pongezi zote lakin hii tamko la Zitto halitakuwa na maana endapo tu hataitisha press conference ili jamii ya nje ambayo idadi kubwa iweze kujua ukweli huu, Pia Zitto uache lugha tata katika maelezo yako kwan unazidi kuchanganya watu na kuwapa binamu zako wa damu CCM cha kupigia propaganda mfano unaposema sijui "malengo ya mtu mmoja yasifanywe kuwa ni ya taasisi"
Pia cha mwisho uache vita yako kwa Ben Saanane kwan unajishushia hadhi mwenyewe kwan Ben si mjinga kama unavyofikiri ww, kwani unapotumia masalia kumchafua usifikiri taarifa hazimfikii,
All in all Bravo Zitto kwa kuonesha uthubutu.
wewe sio muumini wa CDM ni mfuasi wa DR pamoja na kijakazi wake Benn.Acha ujinga kijana, Mimi si muumin wa CHADEMA tu bali ni muumini watu wanaosimamia ukweli ambao wapo CHADEMA mfano Rais wangu Dr.W.Slaa, Sasa yanapotokea mazingira yenye utata kutoka kwa wanafiki kama ww kwa lengo la kuwachafua viongozi ambao wanatupigania, Mimi hapo huwa sileti unafiki bali ni kutoa ukweli tu, Ndio maana huwa nasema mtu yeyote anayepinga na kudharau kazi aliyoifanya Ben Saanane mpaka tukagundua uozo wa masalia basi mtu huyo atakuwa ni mwendawazimu zaidi ya pepo mchafu.
Kaka nimekupata: Lakini huoni mikono ya CCM ikikatiliwa mbali hata hivyo vyeo vinavyompatia sifa hatavipata??. Umeona ya Mchhungaji Msigwa?? We need sometimes to be considerate and rational on important issues!!
...Sidhani kama CCM wamewahi mhofia Zitto. Bali hilo husemwa sana na CCM wenyewe (ZeMacopolo, Ritz nk) ili kumpa kichwa Zitto aikoroge CDMHakuna mwana chadema anayependa zitto afe ila wanataka mikono ya ccm inayomuelekea zitto ikatiliwe mbali ..
zitto ni kipenzi cha wana chadema hilo halina ubishi..wanachadema huwa wanasikitika sana wasiojua mienendo ya zitto....
wanataka kumuona zitto wao majukwaani,kwenye kila matukio ya chadema wanataka kumuona yupo ...hivyo ndo ilivyo mkuu...
zitto ni chadema na chadema ni zitto...
zitto + mbowe +dr.slaa == ushindi wa chadema 2015...
zitto + mbowe +dr.slaa== maumivu,kuchanganyikiwa kwa ccm
mbowe +dr.slaa - zitto == furaha na ahueni kwa ccm na mafisadi wote...
Ben: 'Nimeshawahi kuonana na Zitto'
Zitto: 'Sijawahi kuonana na Ben'
Integrity: Sifa kuu ya kiongozi
Ukweli ndio msingi wa uaminifu kwa kiongozi. Kiongozi ni Yule anayesema ukweli siku zote na sehemu yoyote.
Nimegundua kitu kimoja ndani ya CHADEMA: Baadhi ya viongozi si wa kweli.
Ni nani mkweli kati ya Zitto na Ben Saanane?
Kwa vile wote hawawezi kuwa wakweli, what is the future of politics in our country and CHADEMA in particular?
Ikiwa mmeanza kuwa waongo ndani ya chama chenu, mtakuwa wakweli kwa taifa?
Kwa vile wote hawawezi kuwa wakweli, what is the future of politics in our country and CHADEMA in particular?
Ikiwa mmeanza kuwa waongo ndani ya chama chenu, mtakuwa wakweli kwa taifa?
Mmeona mafunzo ya JKT yalivyo na manufaa?
Kijana fresh from JKT huyo...
Katika gazeti la Mtanzania toleo na. 7269 la Jumatano Machi 27, 2013 kuna habari yenye kichwa chenye maneno ‘SIRI YA KUUWAWA ZITTO YAFICHUKA' na vichwa vidogo ‘yadaiwa ilipangwa anyweshwe sumu hotelini' dk. Slaa atajwa kumtuma Saanane kummaliza'. Habari hii imeniletea usumbufu mkubwa kwani ndugu, jamaa, marafiki na wapiga kura wangu, wamejazwa na wasiwasi mkubwa sana kwamba ninaweza kuuwawa.
Napenda kusema yafuatayo:
Moja, sijawahi katika maisha yangu yote kukutana na mtu anayeitwa Ben Saanane na hivyo hicho kikao ambacho inasemekana nilikuwa naye na akajaribu kunipa sumu hakijawahi kutokea. Imetajwa Hoteli ya Lunch Time ambayo sio tu sijawahi kufika, pia hata siijui ipo wapi. Haijawahi kutokea mimi kufanya kikao cha pamoja na Ben Saanane, Juliana Shonza na Mtela Mwampamba. Hivyo habari iliyoandikwa ni ya kufikirika na hivyo naomba mwandishi ahakikishe kuwa vyanzo vyake vya habari vimempa habari sahihi.
Pili, Siamini kamwe kuwa Katibu Mkuu wa chama changu anaweza kupanga kuniua maana hana sababu ya kufanya hivyo. Napenda kurudia kusema kwamba mimi ninaamini kuwa kila nafsi itaonja mauti. Kila mtu atakufa. Kama nitakufa kwa kuuwawa na mtu mwingine ndio itakuwa nimeandikiwa hivyo na Mungu. Ndio maana hata siku moja silalamiki kuhusu vitisho vya kuuwawa nk. Kama kuna mtu anafikiria kuwa kumuua Zitto ndio furaha ya maisha yake atakuwa anajidanganya tu maana Zitto anaweza kufa kimwili lakini mawazo, fikra na maono ya Zitto yataishi tu. Siogopi kufa maana maisha niliyoyachagua ndio haya ambayo yamejaa vitisho. Muhimu kwangu ni kufanya kazi zangu kwa bidii, uhodari na uaminifu. Siku zote nitasimamia ukweli bila kujali uchungu wa ukweli huo.
Tatu, nawashauri watu ambao wamehama CHADEMA na kuhamia vyama vingine watumie muda wao kujenga vyama vyao badala ya kila siku kuzungumzia masuala ya chama ambacho wao sio wanachama tena. Kama mtu kaamua kuhama CHADEMA anapoteza haki ya kujadili masuala ya CHADEMA maana kama angekuwa anapenda kuyajadili asingehama. Naonya mtu yeyote ambaye anatumia jina langu ili kufanikisha malengo yake ya kisiasa. CHADEMA sio pango la watesaji wala wauaji. Kama kuna mwanachama wa chama kingine cha siasa anayedhani kuna mtu ndani ya CHADEMA anapanga mipango ovu aende kwenye vyombo vya sheria kumshtaki. Matendo ya mtu mmoja yasifanyiwe propaganda kama ni malengo ya taasisi.
Nne, Nawashauri viongozi wenzangu wa CHADEMA na hasa wanachama tutumie muda wetu kujenga mshikamano ndani ya chama. Fitna, majungu, uongo, uzandiki nk kamwe havijengi chama. Chama chetu lazima kiwe mfano bora wa kuheshimu demokrasia na haki za binaadamu. Wananchi hawawezi kutoa dola kwa chama chenye mifarakano. Tusiruhusu kugawanywa kwa matakwa ya watu wachache. Tusimamie misingi ya kuanzishwa chama chetu.
Hakumaanisha mtu huyo lazima awe kiongozi bali mwanachama yeyote mfano ni Ludovick aliyeamua kuwa msaliti na inawewzekana na Lwakatare kama naye alisaliti
logic
wapo wale wawazao mema kuanzia nafsini mwao hadi kwenye jamii yao, hawa huitwa wenye hekima
kuna wale wawazao njama, visa,chuki, machafuko na hata vita,hawa tunawaita washenzi''
conclusion: Zitto : Mwenye hekima
dr.slaa: Mshenzi
logically proved.
Ww unasemaje????????????????????????????