Siri gani mwanamke hawezi kusema mpaka kaburini?

Siri gani mwanamke hawezi kusema mpaka kaburini?

Jeanclaude

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2013
Posts
259
Reaction score
238
Wana MMU, wanawake kwa wanaume naombeni msaada. Ni siri gani mwanamke hawezi kusema hadi kaburini? Rafiki yangu wa kike anayeishi Moshi ambaye tumedumu kwenye uhusiano kwa miaka 2, katika maongezi nilimuuliza ni jambo gani hawezi kulisahau akasema kuna mtu hawezi kumsamehe kwa kuwa alimfanyia kitendo kibaya. Nimembembeleza aniambie ni kitu gani na nani alimtendea lakini amegoma katu. Nahisi huenda alibakwa. Je, ni jambo gani mwanamke hawezi kulisema?

Nimekosa amani kufikia kumchukia jamaa ambaye simfahamu wala sijui alimtendea nini.
 
Sioni ni kitu gani mwanamke anaweza asikwambie, ni suala la muda tu ila usilazimishe saana mpk ukajikuta unaonesha hasira kwa jambo ambalo hulijui. Nakumbuka mi x wangu alikuwa rafiki yangu sana kiasi kwamba akawa ananiambia mambo mengi sana mazito na mojawapo ni la kubakwa akiwa mdogo na houseboy wao....na hili jambo ni siri ndani ya family yao
Labda akiwa ameenda kwa mganga kukuroga, na hata hili pia siku ukimzunguka zunguka basi atakwambia ukweli wote na kukuomba msamaha.
 
Asanteni Mamndenyi@Mtimti@Malafyale. Kama ni kubakwa Mungu anijalie moyo wa kusamehe. Duniani nahisi nawachukia wabakaji kuliko baba yao shetani.
 
Last edited by a moderator:
Sioni ni kitu gani mwanamke anaweza asikwambie, ni suala la muda tu ila usilazimishe saana mpk ukajikuta unaonesha hasira kwa jambo ambalo hulijui. Nakumbuka mi x wangu alikuwa rafiki yangu sana kiasi kwamba akawa ananiambia mambo mengi sana mazito na mojawapo ni la kubakwa akiwa mdogo na houseboy wao....na hili jambo ni siri ndani ya family yao
Labda akiwa ameenda kwa mganga kukuroga, na hata hili pia siku ukimzunguka zunguka basi atakwambia ukweli wote na kukuomba msamaha.

Kutembea nje ya ndoa, kuzaa nje ya ndoa, kutembea na rafiki wa bwana, kupigwa mande na kukutajia idadi ya wanaume aliolala nao mara nyingi atapunguza idadi
 
Ukiendelea kulazimisha ndo atakudanganya
Siri yake tulia hivyo hivyo
 
....ahhh, unajitoa amani bure tu. Kama alivyosema King'asti, anaweza kutajia jambo ukabaki mdomo wazi kwa mshangao lilivyo #NonIssue ....

Wana MMU,

Wanawake kwa wanaume naombeni msaada, ni siri gani mwanamke hawezi kusema hadi kaburini. Rafiki yangu wa kike, anayeishi Moshi, ambaye tumedumu kwenye uhusiano kwa miaka 2, katika maongezi nilimuuliza ni jambo gani hawezi kulisahau akasema kuna mtu hawezi kumsamehe kwa kuwa alimfanyia kitendo kibaya. Nimembembeleza aniambie ni kitu gani na nani alimtendea lakini amegoma katu. Nahisi huenda alibakwa. Je, ni jambo gani mwanamke hawezi kulisema?

Nimekosa amani kufikia kumchukia jamaa ambaye simfahamu wala sijui alimtendea nini.




#MosKwito !
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom