Another Sunday, another boredom, another weekend. Nimeamka Salama namshukuru Mungu. It got me thinking, when was the last time going to church? Je namshukuru Mungu kweli, au naongea tu Kwa vile ni msemo wa Kila siku(jumapili especially!) je huyo Mungu WA kanisani nisiyemuamini Kwa nini bado naona anafaa?
Wengi walio kulia katika strong religious families one of the things never miss church. Lazima uende hata kama unaumwa, Mzee alikua anatucharaza, sikupenda kwenda, wala sikutaka kusikia mambo ya kanisani. I hated it, I hated false claims of God, who I knew never believed existed. Toka nikiwa mdogo sikupenda na sikutaka kukubali kuamini Kuna Mungu, mungu aliyefanya mtu wangu wa karibu kuugua na kufa mbele yangu bila hatia.
Ilikua ni scam ya kuwafanya watu wa hope kwenye kitu kisicho kuwepo, na kujifariji life will get better, while ukweli nothing changes when nothing happens.
Ila, Kuna kitu najifunza, despite all that Kuna maana iliyopo behind.. sometimes tuna Fanya vitu based on our experiences. Tunamkataa mungu, (najua hayupo) because tunajichukia wenyewe. Tunaepuka maandhari Fulani kwasababu yana tu trigger past hurts.
Tunaaacha kukaa karibu na watu Fulani kwa sababu tunahisi wana element za wale walotuumiza.
Moja ya vitu vikuu vinavyo ifanya society I thrive, ni social connection.
Lakini kadri unavyokua, unaanza kuona kwamba si kila kitu kinabebwa na “belief.” Kuna vitu vina survive hata pale ambapo imani imekufa.
Na mojawapo ni connection ya watu kwa watu.
Kanisa, msikiti, temples, vikundi vya jamii mara nyingi havikudumu tu kwa sababu watu waliamini kila kitu walichoambiwa. Vimedumu kwa sababu vilitengeneza sehemu ya watu kuonana, kusikilizana, kusaidiana, kuombolezana, kucheka pamoja.
Human beings are social beings before they are ideological beings.
Ndiyo maana hata mtu asiyeamini Mungu bado anahitaji belonging.
Anahitaji kuitwa na mtu akiwa kimya sana.
Anahitaji kukumbukwa siku mbaya.
Anahitaji sehemu ambayo presence yake ina matter.
Ila with rise of technology na false idealisms, watu wengi tunafanya vitu based on hypertension na kutaka ku satisfy ego zetu. Nimeacha kwenda kanisani since chuo, na hata kama nilienda nilienda out of special events kama ndoa. Hii kitu imwnifanya nifikirie sana, of course God is what we go church for, but there's more to that.
Watu wazima wenye emotional integrity wanajua kabisa, it's people we lve for, it's love and connection we long for. Ukiangalia depression levels zinakuwa Kwa sababu hiyo, watu wanapata mental illnesses because of isolation. Tunazidi kuwehuka, tunazidi kuwa watu wasio na clear thought process Kwa sababu tunajilimbikizia vitu ambavyo in a grand scheme of life havina mashiko. Maisha yalikua simple zamani, sawa wazee walikuwa ignorant to some extent ila at least walikuwa na direction. Walikuwa na kitu cha kufia, kitu cha kuwa sukuma, when things felt impossible. Though it was delusional it still worked. Kuna nguvu katika belief.
Mwisho wa siku, labda maana halisi haipo kwenye doctrine zote tulizolazimishwa kuamini.
Labda ipo kwenye uwezo wa binadamu kuwa sehemu salama kwa binadamu mwingine.
Nawasilisha.
Happy Sunday y'all