Sio kila Mhaya ana dharau

Sio kila Mhaya ana dharau

Wahaya hawana dharau, ni kwamba majority wanapenda sifa. Wahaya ni watu poa sana. Yan ombea Mungu dada ako aolewe na Mhaya, ata enjoy balaa. Badala ya kutembelea sijui ki Porte au Ki Paso, atasukuma Prado, Rav 4 au Range.
Wahaya wako so caring nakwambia...
 
Ndio maana naendelea kusema kuwa ukiona unambagua binadamu mwenzako kwa kigezo cha ukabila au udini ujue hauna tofauti na wale wanaowabagua wenye ngozi tofauti wakati binadamu wote ni sawa! Kila binadamu ana mapungufu yake na unapochukua mapungufu ya mtu mmoja ukayajumlisha kuwa ya jamiii anakotoka huo ni ubaguzi wa hali ya juu! Naandika hivi nikijua kuwa kuna taasisi nyingi sana na nyeti hapa Nchini na nje ya nchi zinashikiliwa na wahaya na zinafanya vizuri...mbona hayo hamyaoni?

Yaani mhaya na kujisifia ni uji na mgonjwa!:smile-big::smile-big:
 
Naandika hivi nikiwa na masikitiko makubwa sana juu ya ukabila unaoota mizizi hasa katika kipindi cha hvi karibuni ndani ya nchi yetu! Hivi karibuni aliyekuwa Waziri wa nyumba na makazi mama Tibaijuika alikaririwa akisema MILIONI KUMI NI KWA AJILI YA MBOGA!

Kwa kweli hii ni dharau kubwa sana; lakini hoja yangu ni kuhusu maneno yanayoendelea kwenye mitandao mbalimbali ikiwahusisha wahaya wote na huyu MTU! Kimsingi hili jambo linanikera sana maana ni kuendekeza ukabila na ubaguzi kwani mtu mmoja hawezi kuwa KIGEZO cha kuwaamulika watu wote wa jamii husika!

Bila shaka ninyi ni mashahidi juu ya kauli nyingi zilizowahi kutolewa na watu wa aina mbalimbali hasa viongozi lakini hazikuhusishwa na ukabila! Tafadhali epukeni ukabila kwani ulileta madhara makubwa Rwanda & Burundi pamoja na Kenya! Ni hayo tu kwa Leo..

WAHAYA wananyodo mtu asikwambie! Si mtoto, si mkubwa. Si msomi, si nani. Wote shiiiiiiida! Wanatutesa sana mtaani huku.

Hata kama hajasoma au hana hata mia, utasikia "Mimi ni MUHAAYA!", Babu yangu ni KANALIII, bibi yangu ni Lecture, Mujomba wangu ni DC!


Shida sana watu nyie.

Lakini; usiogope. Hatuwezi kufika huko yalikofikia Rwanda e.t.c kwani huo ndio udhaifu wenu na tushawazoea.

Kikubwa tu nikwamba, hatupendi of course. Tunawakanya na kuwapa reactions kidogokidogo hukuhuku kitaa.
 
Makabila makubwa ni lazima yazungumziwe kwa maana yana vitu vingi pia na yanatumia influence yao kudominate vidogo ambavyo kimsingi haiwezekani vikapenda hari hiyo,vitajaribu kuwasema ilimradi tu vinasema lakini huo ndo ukweli.Wahaya wengi wako vizuri tena wanatisha na hata mkoa wao Kule hakunaga jua wala joto,wana vyakula wanakula wanashiba kila siku Victoria na maroli yanabeba matani ya ndizi kwenda masokoni ,sasa kwanini mnataka wajione wanyonge? msifuni bwana kama Amekupa na unavyo na wala usione aibu watu kuona in vitu gani Mungu alikupa,kwani so hata yeye anajua unavyo na ndo vipawa vyake kwako? vitumie!
 
Kifupi ni kwamba wahaya wana roho mbaya, wajivuni, wajuaji na wanadharau sana.

Yupo mmoja ana dharau sijapata kuona, anafanya kazi maeneo ya mbuga za wanyama huku Arusha ikatokea akabahatika kununua ka forster na kupanga self contained house maeneo ya Moshi huku wenzake wakiwa bado wanajipanga panga. Jamaa ana maneno hata nusu saa hukai nae...anadai toka anunue gari anajisikia furaha maana anatembea huku amekaa.Anasema hawezi kuishi nyumba ya chumba kimoja maana atakuwa anaishi stoo na pia hawezi kuoga kwa kutumia karai maana atachoka kuinama na kuinuka. yaan full maringo na misifa hawa watu.
 
Nachukia sana malumbano ya dini na ukabila na vingine ambavyo ni GOD CREATED.hatuna ujuzi/utaalam wa kumkosoa MUNGU.
 
  • Thanks
Reactions: R.B
Mimi huwez aisee hata uweke ngoma hapa nakulia buyu

Huna ujasiri wa kuwakataa wahaya make wana sifa zote za kuwa-care wanawake. Na kwa posts zako nyingi hapa jf unaonekana(ga) we ni mala.ya tu mtafta fedha huna jeuri ya kuwakataa wahaya wazee wa kutumia... hahahahaha... iwe bojo nitumie sms ushinde mihela.
 
Huna ujasiri wa kuwakataa wahaya make wana sifa zote za kuwa-care wanawake. Na kwa posts zako nyingi hapa jf unaonekana(ga) we ni mala.ya tu mtafta fedha huna jeuri ya kuwakataa wahaya wazee wa kutumia... hahahahaha... iwe bojo nitumie sms ushinde mihela.

Mkuu punguza jazba, tufanye midala ya kistarabu.
 
Huna ujasiri wa kuwakataa wahaya make wana sifa zote za kuwa-care wanawake. Na kwa posts zako nyingi hapa jf unaonekana(ga) we ni mala.ya tu mtafta fedha huna jeuri ya kuwakataa wahaya wazee wa kutumia... hahahahaha... iwe bojo nitumie sms ushinde mihela.

Jukwa la watu uhaya wako peleka fb penda kuheshimu wenzako.
 
Mkuu punguza jazba, tufanye midala ya kistarabu.

Iwe bojo,nawakubali sana nawaza hata kuifanya lugha yenu iwe ya taifa ..tuombe lile gazeti letu LA Rumuri lianze kusambazwa nchi nzima ili watani waelewe kwamba nyie ni soo
 
Iwe bojo,nawakubali sana nawaza hata kuifanya lugha yenu iwe ya taifa ..tuombe lile gazeti letu LA Rumuri lianze kusambazwa nchi nzima ili watani waelewe kwamba nyie ni soo

Unawakubali wakina nani? Na kwa nini usijikubali wewe?
 
Back
Top Bottom