Sinema tosha mauaji ya bilionea Msuya

Sinema tosha mauaji ya bilionea Msuya

Kwenye maelezo Chusa bado anatumikia kifungo cha mauaji mengine ambayo yeye anahisi aliyechoma utambi ama kukoleza moto ni Msuya; ndiyo maana akaona pia na yeye aondoke duniani ndiyo akaamua kufanya mipango ya remote assimilation.

Kuua kwa kuagiza hii sijui kama sheria inakutia hatiani.
Jamaa we ni Mtaalamu wa hii Kesi..
Hongera sana..
Na vipi huna tetesi Why Mdogo wa Marehemu (Aneth naye aliuawa?)
Alikosa nini
 
Siku zote wauaji lazma wafanye kosa pahala....
Ukiona hawajadakwa basi wapelelezi hawajakua makini killers always makes mistake somewhere...

Hawa naona kuna mtu aliwachoma au hizo simu ndio zili wa cost na pia ishu walifanya kienyeji sana open kabisa
Nasikia Na Kijana wa Kimasai aliwaona Live.Ni Rahisi walimtumia..
Hapa police tuwafungulie thread ya Kuwapongeza.
 
Hawa watu hawakuwa wataalamu ni amateurs wa uhalifu ndio maana wamekamatwa kirahisi.
 
Hapa nimepata picha Kamili.Walipoenda kampuni husika.Wasikia sauti zao.vizuuuuuuri.
Kazi kwisha.

Hapana siyo hivyo....

Soma haya maelezo ya ushahidi yaliyotolewa mahakamani na shahidi wa Jamhuri.....


Chilumba ambaye alikuwa kiongozi wa timu ya mawasiliano ya kimtandao (Cyber), alidai mahakamani jana kuwa timu yake ndiyo iliyobaini uwapo wa namba ya mwisho iliyowasiliana na marehemu.

Akiongozwa na wakili mwandamizi wa Serikali, Abdallah Chavulla kutoa ushahidi wake, shahidi huyo alidai baada ya kufanikiwa kuondoa neno la siri katika simu za marehemu, walikuta SMS mbili.

Kwa mujibu wa shahidi huyo, baada ya kufungua simu mojawapo ya marehemu, walikuta SMS hizo zikiwa zimetumwa kupitia namba ya mtandao wa Airtel siku moja kabla ya mauaji na siku ya mauaji.

“Ujumbe wa kwanza ulitumwa tarehe 6/8/2013 ukimjulisha (marehemu) kuwa ‘nina riziki’ na ujumbe wa tarehe 7/8/2013 saa nne au saa tano hivi ulisema niko Kia nakusubiri hapa,” alidai shahidi huyo na kuongeza:

“Tulianza kufuatilia ujumbe huo (wa tarehe 7/8.2013) ambao ndiyo ulikuwa wa mwisho kwenye simu ya marehemu na saa chache baadaye akauawa. Tuliandika barua Airtel kupata taarifa zake.”

Katika barua hiyo, shahidi huyo alidai waliiomba kampuni ya Airtel kuwapa taarifa mmiliki wa laini hiyo ya simu, ilikosajiliwa na kwa wakati huo ilikuwa ikisomeka eneo gani.

Alidai kuwa majibu ya Airtel yalionyesha kuwa laini hiyo ilikuwa imesajiliwa Arusha Agosti 3, 2013 kwa jina la Motii Mongululu lakini wakati huo haikuwa tena hewani.

“Walituambia baada ya kusajiliwa, laini hiyo ilifanya mawasiliano na namba nne tu na wakatuambia iliwahi kuchomekwa kwenye handset (simu) ambayo inatumia namba nyingine,” alidai na kuongeza:

“Tulifanikiwa kumkamata dada mmoja pale Arusha kituo kikuu cha mabasi anaitwa Hamisa (Kassim), ambaye ndiye mwenye hiyo namba, ambaye alikumbuka kusajili line kwa jina la Motii Mongululu.”

Hata hivyo, shahidi huyo alidai katika mahojiano, Hamisa aliwaeleza kuwa alisajili laini hiyo kwa maelekezo ya wakala mwenzake aliyemtaja kuwa ni Aneth Shija ambaye naye alikamatwa.

“Aneth alikiri ndiye aliyempa maelekezo Hamisa kusajili hiyo laini na nyingine mbili na kwamba, alizisajili kwa maelekezo ya mtu aliyemtaja kuwa ni Adam ambaye ni kijana wa kimasai,” alieleza.

Shahidi huyo alidai kupitia kwa Aneth walifanikiwa kupata namba ya Adam ambaye alikamatwa Mirerani, lakini naye akadai aliagizwa na mshtakiwa wa tatu, Mussa Mangu kusajili laini hizo.

Mkaguzi huyo wa polisi aliieleza mahakama kuwa baada ya Mangu kukamatwa na kuhojiwa, alikiri kusajili laini hizo za simu lakini naye akadai kuwa alitumwa na mshtakiwa wa kwanza, Sharifu.

“Alituambia maelekezo ya kusajili laini na kununua simu alipewa na bosi wake aliyemtaja kuwa ni Sharifu Mohamed. Alitueleza kuwa kwa ufahamu wake, yote yalikuwa ni maandalizi ya mauaji.

“Siku hiyo hiyo tulimkamata Sharifu nyumbani kwake na katika mahojiano ya awali alimtambua Mussa kama mfanyakazi wake na kukiri vitu vyote vilivyonunuliwa naye vilikuwa maelekezo yake,” alieleza.
 
Hapana siyo hivyo....

Soma haya maelezo ya ushahidi yaliyotolewa mahakamani na shahidi wa Jamhuri.....


Chilumba ambaye alikuwa kiongozi wa timu ya mawasiliano ya kimtandao (Cyber), alidai mahakamani jana kuwa timu yake ndiyo iliyobaini uwapo wa namba ya mwisho iliyowasiliana na marehemu.

Akiongozwa na wakili mwandamizi wa Serikali, Abdallah Chavulla kutoa ushahidi wake, shahidi huyo alidai baada ya kufanikiwa kuondoa neno la siri katika simu za marehemu, walikuta SMS mbili.

Kwa mujibu wa shahidi huyo, baada ya kufungua simu mojawapo ya marehemu, walikuta SMS hizo zikiwa zimetumwa kupitia namba ya mtandao wa Airtel siku moja kabla ya mauaji na siku ya mauaji.

“Ujumbe wa kwanza ulitumwa tarehe 6/8/2013 ukimjulisha (marehemu) kuwa ‘nina riziki’ na ujumbe wa tarehe 7/8/2013 saa nne au saa tano hivi ulisema niko Kia nakusubiri hapa,” alidai shahidi huyo na kuongeza:

“Tulianza kufuatilia ujumbe huo (wa tarehe 7/8.2013) ambao ndiyo ulikuwa wa mwisho kwenye simu ya marehemu na saa chache baadaye akauawa. Tuliandika barua Airtel kupata taarifa zake.”

Katika barua hiyo, shahidi huyo alidai waliiomba kampuni ya Airtel kuwapa taarifa mmiliki wa laini hiyo ya simu, ilikosajiliwa na kwa wakati huo ilikuwa ikisomeka eneo gani.

Alidai kuwa majibu ya Airtel yalionyesha kuwa laini hiyo ilikuwa imesajiliwa Arusha Agosti 3, 2013 kwa jina la Motii Mongululu lakini wakati huo haikuwa tena hewani.

“Walituambia baada ya kusajiliwa, laini hiyo ilifanya mawasiliano na namba nne tu na wakatuambia iliwahi kuchomekwa kwenye handset (simu) ambayo inatumia namba nyingine,” alidai na kuongeza:

“Tulifanikiwa kumkamata dada mmoja pale Arusha kituo kikuu cha mabasi anaitwa Hamisa (Kassim), ambaye ndiye mwenye hiyo namba, ambaye alikumbuka kusajili line kwa jina la Motii Mongululu.”

Hata hivyo, shahidi huyo alidai katika mahojiano, Hamisa aliwaeleza kuwa alisajili laini hiyo kwa maelekezo ya wakala mwenzake aliyemtaja kuwa ni Aneth Shija ambaye naye alikamatwa.

“Aneth alikiri ndiye aliyempa maelekezo Hamisa kusajili hiyo laini na nyingine mbili na kwamba, alizisajili kwa maelekezo ya mtu aliyemtaja kuwa ni Adam ambaye ni kijana wa kimasai,” alieleza.

Shahidi huyo alidai kupitia kwa Aneth walifanikiwa kupata namba ya Adam ambaye alikamatwa Mirerani, lakini naye akadai aliagizwa na mshtakiwa wa tatu, Mussa Mangu kusajili laini hizo.

Mkaguzi huyo wa polisi aliieleza mahakama kuwa baada ya Mangu kukamatwa na kuhojiwa, alikiri kusajili laini hizo za simu lakini naye akadai kuwa alitumwa na mshtakiwa wa kwanza, Sharifu.

“Alituambia maelekezo ya kusajili laini na kununua simu alipewa na bosi wake aliyemtaja kuwa ni Sharifu Mohamed. Alitueleza kuwa kwa ufahamu wake, yote yalikuwa ni maandalizi ya mauaji.

“Siku hiyo hiyo tulimkamata Sharifu nyumbani kwake na katika mahojiano ya awali alimtambua Mussa kama mfanyakazi wake na kukiri vitu vyote vilivyonunuliwa naye vilikuwa maelekezo yake,” alieleza.
Hapa ndio penyewe hasa
 
Washtakiwa ni wajinga sana.hao waliokamatwa kwa MINARA ya SIMU.
Zama hizi unafanya tukio hilo na unabakia hewani???[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Wajinga bado wapo
 
Na nadhani amepona kwa kuwa alipokuwa anawatuma hakuacha Alama yoyote nyuma
Mfano.Walikuwa wawili tu Hakuna picha wala recording
Swali kama Chusa alikuwa gerezani Pesa za kuwalipa hao wauaji Nani alikuwa anatoa?
Kama ni Yeye mwenyewe Sharifu basi alitaka tu kumtengenezea mwenyewe Kesi
Hiyo ya kusema angetoka Jela angeuwawa Yeye is not True at all.
Na kama ni Chusa alipanga bila kuacha alama yoyote bus.Ni Bonge La MAFIA.
Hii case kuna mengi mnaongea ila mahakama imetenda haki yke,hivi sharif kwa pesa zke atumwe kuua mtu na atende,dili yote imefanywa na watu wake wote hata mredii ni mtu wke sana sharif
 
Ukitaka fanya uharifu, nunua line mpya fanya uharifu tupa simu na line. Hama hata nchi
Mkuu umesahau kitu. Simu mpya na line mpya sawa.
Lakini hiyo simu ama line usithubutu kumpigia mtu hata m1. Pia usivitupe bali viharibu kwa kuviteketeza hadi kuwa jivu ndipo uvichimbie chini ukiwa mwenyewe.
Nimesema hivyo kwa sababu watu wasioijua kiundani teknolojia ya mawasiliano ya kisasa, wanadhani kutumia line ama simu na kuvitupa ni kupoteza ushahidi, hao bado wapo kwenye giza totoro.
 
Back
Top Bottom