Sinema tosha mauaji ya bilionea Msuya

Sinema tosha mauaji ya bilionea Msuya

imenikumbusha enzi zile nasoma vitabu vya Elvis Musiba R.I.P. kama kikomo, kikosi cha kisasi, uchu najua wengi hawajakisoma hiki ni baada ya mauaji ya kimbari ya Rwanda na vinginevyo vingi jinsi Willy Gamba alivyokuwa anafanya upelelezi na hatimae kuhakikisha watuhumiwa wanakamatwa. Big up Jeshi la polisi kwani machalii wa AR chuga walikuwa wakorofi sana.
Kikomo na Kufa na kupona vyote nimevisoma na hadi leo siwezi kulala bila kujua siraha nimeiweka wapi, ni sehemu gani takimbilia wakigoga au kuvunja mlango na ni nini takifanya endapo watamkteka mtoto na kuingia nae chumbani kwangu kama kinga yao
 
Duh ila nahisi wataendelea kuchomoka mmoja mmoja.
 
Ilikuwaje mpaka wakaanza kukamatwa...wapi walikosea?
Kubwa unalopaswa kujua siku zote ni kuwa huwa hakuna siri ya watu wawili. Inaweza kudumu kwa muda mfupi au muda fulani lakini lazima itatoka. Sasa idadi yote hiyo ingewezekanaje kutunza siri hiyo. Hata mke mnayekula naye kiapo kanisani siku mkichokana atatoa yote ndio watu watajua kuwa una mikopo na watoto siyo wako ila ni wa rafiki yako kama tulivyoshuhudia juzi ya Muna na Peter kuhusu yule mtoto. Siri huwa ni mtu mmoja basi na wa pili atakuwa ni Mungu. Ndiyo maana huwa nashangaa wanaposema eti siri za serikali. Serikali ni kikundi cha utawala kilichopo kwa muda fulani hivyo hakiwezekani kukawa na siri hasa watunza siri ikiwa ni kwa watu wanaolipwa. Ndiyo maana naamini katika mtiririko huo huo waliomdhuru Lissu ni suala la muda tu tutawajua wote hata kama walirudi kwa msafara wa king'ora. Azori itajulikana tu. Kama makaburi ya halaiki ya miaka ya 40 iliyopita yanajulikana leo itakuwa hao waliompoteza Ben? It's just the matter of time. Time is a very good teacher - Time'll tell
 
Hivi ile kesi ya Baro iliishia wapi?
Ninachokumbuka atuhumiwa wote walikamatwa hadi ile simu ya marehemu ilikutwa kwenye karo la maji taka!!sasa sijui kama kesi ilifikia wapi ila hadi mwaka juzi hukumu ilikuwa bado!!
 
Kubwa unalopaswa kujua siku zote ni kuwa huwa hakuna siri ya watu wawili. Inaweza kudumu kwa muda mfupi au muda fulani lakini lazima itatoka. Sasa idadi yote hiyo ingewezekanaje kutunza siri hiyo. Hata mke mnayekula naye kiapo kanisani siku mkichokana atatoa yote ndio watu watajua kuwa una mikopo na watoto siyo wako ila ni wa rafiki yako kama tulivyoshuhudia juzi ya Muna na Peter kuhusu yule mtoto. Siri huwa ni mtu mmoja basi na wa pili atakuwa ni Mungu. Ndiyo maana huwa nashangaa wanaposema eti siri za serikali. Serikali ni kikundi cha utawala kilichopo kwa muda fulani hivyo hakiwezekani kukawa na siri hasa watunza siri ikiwa ni kwa watu wanaolipwa. Ndiyo maana naamini katika mtiririko huo huo waliomdhuru Lissu ni suala la muda tu tutawajua wote hata kama walirudi kwa msafara wa king'ora. Azori itajulikana tu. Kama makaburi ya halaiki ya miaka ya 40 iliyopita yanajulikana leo itakuwa hao waliompoteza Ben? It's just the matter of time. Time is a very good teacher - Time'll tell
Kweli kabisa, ndo maana kikundi cha MAFIA kilikuwa hatari sana kwasababu walikuwa na viapo vya damu, ukitoa siri unakufa wewe na ukoo wako wote, wakihisi kuwa mwenzao amekuwa soft na anaweza toa siri walikuwa wanamuua haraka, kama mwanachama anateswa ili atoe siri akiona anaanza kuwa soft alikuwa anajiua mwenyewe.
 
Chusa yuko wapi mkuu. Very good narration.
Kwenye maelezo Chusa bado anatumikia kifungo cha mauaji mengine ambayo yeye anahisi aliyechoma utambi ama kukoleza moto ni Msuya; ndiyo maana akaona pia na yeye aondoke duniani ndiyo akaamua kufanya mipango ya remote assimilation.

Kuua kwa kuagiza hii sijui kama sheria inakutia hatiani.
 
Back
Top Bottom