Sinema tosha mauaji ya bilionea Msuya

Sinema tosha mauaji ya bilionea Msuya

Duuuh nimeamini Jeshi la Polisi wanafanya kazi, wanao beza hili jeshi hawajapata matatizo
Ni kweli wanafanya kazi ila kuna baadhi ya ishu wanazengua sana huwez amini , aidha kesi kama hizi ni za vigogo na ni mgumu sana, ila kesi za kina kajampa nani hutawatamani hawa askari wetu.
 
Duuuh nimeamini Jeshi la Polisi wanafanya kazi, wanao beza hili jeshi hawajapata matatizo
Kuna task force ndani ya jeshi la polisi. Ni polisi walipitia mafunzo maaluma kabisa ya kiaskari. Na wanachapa kazi vizuri sana.

Tatizo ni pale siasa zinapo penyezwa kati yao ndipo hapo wanaonekana wabaya
 
imenikumbusha enzi zile nasoma vitabu vya Elvis Musiba R.I.P. kama kikomo, kikosi cha kisasi, uchu najua wengi hawajakisoma hiki ni baada ya mauaji ya kimbari ya Rwanda na vinginevyo vingi jinsi Willy Gamba alivyokuwa anafanya upelelezi na hatimae kuhakikisha watuhumiwa wanakamatwa. Big up Jeshi la polisi kwani machalii wa AR chuga walikuwa wakorofi sana.
Waliotajwa hapo wengi si wa ara chuga ni wakuja tu.
 
Kubwa unalopaswa kujua siku zote ni kuwa huwa hakuna siri ya watu wawili. Inaweza kudumu kwa muda mfupi au muda fulani lakini lazima itatoka. Sasa idadi yote hiyo ingewezekanaje kutunza siri hiyo. Hata mke mnayekula naye kiapo kanisani siku mkichokana atatoa yote ndio watu watajua kuwa una mikopo na watoto siyo wako ila ni wa rafiki yako kama tulivyoshuhudia juzi ya Muna na Peter kuhusu yule mtoto. Siri huwa ni mtu mmoja basi na wa pili atakuwa ni Mungu. Ndiyo maana huwa nashangaa wanaposema eti siri za serikali. Serikali ni kikundi cha utawala kilichopo kwa muda fulani hivyo hakiwezekani kukawa na siri hasa watunza siri ikiwa ni kwa watu wanaolipwa. Ndiyo maana naamini katika mtiririko huo huo waliomdhuru Lissu ni suala la muda tu tutawajua wote hata kama walirudi kwa msafara wa king'ora. Azori itajulikana tu. Kama makaburi ya halaiki ya miaka ya 40 iliyopita yanajulikana leo itakuwa hao waliompoteza Ben? It's just the matter of time. Time is a very good teacher - Time'll tell
Hongera maneno mazuri na ya kutafakarisha
 
Kazi wanafanya lakini kwa upendeleo au wanakula Rushwa, iweje leo waliomjeruhi Tundu Lissu hawajakamatwa wakati Cctv camera waling'oa wao? Kunanini apo? Nitakuwa wa mwisho kuwaelewa Polis.
 
Hamna plan yao ilikuwa Mbovu,ishu kama hiyo haitakiwa kuwa ya watu wengi wala kitumia simuu,the point to note,sishabikii mauaji
Nope. Chusa ndio head of the game. Alijua jinsi ya kupanga , na akapanga kabisa hata kama plan itaharibika basi madhara hayatamfikia yeye yatawaharib waliotekeleza.
 
Mpiga dili hakuwa na mtu au watu wawili tofauti chen inaonekana ni ndefu sana kiasi ambacho .. nahisi wengine walikamatwa kwa kutumia simu ambayo aliweka line wakati wanafanya mipango na baada ya kumaliza akatupa line akaweka nyingine kwenye simu ileile lazima umezwe
 
Ukisoma mtiririko wa ushahidi utagundua kuwa upelelezi ulianzia kwenye mtandao wa simu.

Makosa yalikuwa wapi..... 1. Ni Sharif Mwenyewe kujihusisha na uratibu wa mauaji ilihali yeye Mwenyewe ndiyo alikuwa mwenye takwa la kutimiza mauaji.

2. Mtiririko ilikuwa sharif kumtumia Mussa ambaye ni mfanyakazi wake kusajili line za simu, ambaye Mussa alimtumia Adam na huyu alimtumia mwanamke na huyu mwanamke alimtumia mwanamke mwingine ambaye naye kwa kutokujua alitumbukiza hiyo line kwenye simu yake hivyo IMEI yake ikasoma huko airtel.

Pili uzito wa ushahidi uliotumika mahakamani ni kitu kinachodaiwa hati ya tamko la washitakiwa wanne kukiri kosa (sasa inawezekana walikiri kwa hiyari au kwa kifinyo cha polisi).... Kinyume na hapo wangekuwa smart kidogo na ngangari sidhani km ingekuwa rahisi
Hapa nimepata picha Kamili.Walipoenda kampuni husika.Wasikia sauti zao.vizuuuuuuri.
Kazi kwisha.
 
Back
Top Bottom