EL ELYON
JF-Expert Member
- Jan 2, 2013
- 1,563
- 1,886
Wakuu habari..
Mmebarikiwà sana na Mungu wa Mbinguni hakuna laana.
Aisee Mimi Nina wadogo zangu wawili Mimi nikiwa mtoto wa Kwanza tena wa kiume mdogo wangu wa pili ni wa kike na wa mwisho ni wa kiume.
Cha ajabu toka nikiwa mdogo hata sijaanza chekechea nilikuwa naishi na shangazi yangu ndiye kanilea mpaka najitambua nilikuwa namuita mama mpaka namaliza darasa la Saba nilijua ndiye mama yangu.
Wakati huo mdogo wangu wa kike anayenifuata yeye alikuwa anaishi na Baba mkoa mwingine huko Naye sikuwa namjua wala yeye hakuwa ananijua zaidi ya kujua Tu Nina mdogo wangu yupo mkoa Fulani
Yule dogo wa mwisho yeye ndo alikuwa na mama mzazi sasa maana kumbe Mzee aliachana na mama mara Tu baada ya kumzaa dogo wa mwisho na tetesi zilizopo inasemekana alienda kwao huku nyuma akamuacha beki tatu ambaye shangazi zangu walifanya mapinduzi ili beki tatu awe mama wa familia sa mama aliporudi kwake akakutana na mapinduzi hayo akaamua kusepa Hz ni tetesi Tu huwa naskia na huyo beki tatu ndiye mama wa familia hata sasa akiwa na watoto kadhaa.
Shida imekuja kwamba malezi yangu yote sikuwahi muona mama pale kwa shangazi nakumbuka nilipohitimu darasa la Saba nilisafiri na shangazi kwenda huko alipokuwa mama tulipofka shangazi akawa anaongea na watu fulan akanionyesha njia nipite nitangulie anakuja njiani nikapishana na mama mmoja nikamsalimia tukapishana kumbe aunt aliona si ndo akamstua mama kwamba huyo ndo mtoto wako unayepishana Naye hapo.
Ndo tukafahamiana sasa.
Sasa shida inayonikabili si Mimi Tu hata mdogo wangu wa pili hatuna mapenzi kabisa na mama yetu yaani hamna kabisa mama Naye Kila siku tunasikia anasema Sisi tuna mama zetu wengine mbaya zaidi anarusha mpaka na maneno mazito hata akifa tusiende kwenye msiba yaani hata sielewi kabisa.
Kingine mama anaamini uganga sana anaendaga kwa waganga sjui wampe dawa ya kurudsha uhusiano wake na Sisi lakini wapi imeshindikana.
Wakuu mnanishauri nn aisee maana sielewi siguswi kabisa na uwepo wa mama yangu.
NB: Wazazi hakikisheni mnakaa na watoto wenu hata kama wako mbali mjitahidi watambue uwepo wenu vinginevyo mtalaumu watoto bure Tu na kutupa laana.
Mmebarikiwà sana na Mungu wa Mbinguni hakuna laana.
Aisee Mimi Nina wadogo zangu wawili Mimi nikiwa mtoto wa Kwanza tena wa kiume mdogo wangu wa pili ni wa kike na wa mwisho ni wa kiume.
Cha ajabu toka nikiwa mdogo hata sijaanza chekechea nilikuwa naishi na shangazi yangu ndiye kanilea mpaka najitambua nilikuwa namuita mama mpaka namaliza darasa la Saba nilijua ndiye mama yangu.
Wakati huo mdogo wangu wa kike anayenifuata yeye alikuwa anaishi na Baba mkoa mwingine huko Naye sikuwa namjua wala yeye hakuwa ananijua zaidi ya kujua Tu Nina mdogo wangu yupo mkoa Fulani
Yule dogo wa mwisho yeye ndo alikuwa na mama mzazi sasa maana kumbe Mzee aliachana na mama mara Tu baada ya kumzaa dogo wa mwisho na tetesi zilizopo inasemekana alienda kwao huku nyuma akamuacha beki tatu ambaye shangazi zangu walifanya mapinduzi ili beki tatu awe mama wa familia sa mama aliporudi kwake akakutana na mapinduzi hayo akaamua kusepa Hz ni tetesi Tu huwa naskia na huyo beki tatu ndiye mama wa familia hata sasa akiwa na watoto kadhaa.
Shida imekuja kwamba malezi yangu yote sikuwahi muona mama pale kwa shangazi nakumbuka nilipohitimu darasa la Saba nilisafiri na shangazi kwenda huko alipokuwa mama tulipofka shangazi akawa anaongea na watu fulan akanionyesha njia nipite nitangulie anakuja njiani nikapishana na mama mmoja nikamsalimia tukapishana kumbe aunt aliona si ndo akamstua mama kwamba huyo ndo mtoto wako unayepishana Naye hapo.
Ndo tukafahamiana sasa.
Sasa shida inayonikabili si Mimi Tu hata mdogo wangu wa pili hatuna mapenzi kabisa na mama yetu yaani hamna kabisa mama Naye Kila siku tunasikia anasema Sisi tuna mama zetu wengine mbaya zaidi anarusha mpaka na maneno mazito hata akifa tusiende kwenye msiba yaani hata sielewi kabisa.
Kingine mama anaamini uganga sana anaendaga kwa waganga sjui wampe dawa ya kurudsha uhusiano wake na Sisi lakini wapi imeshindikana.
Wakuu mnanishauri nn aisee maana sielewi siguswi kabisa na uwepo wa mama yangu.
NB: Wazazi hakikisheni mnakaa na watoto wenu hata kama wako mbali mjitahidi watambue uwepo wenu vinginevyo mtalaumu watoto bure Tu na kutupa laana.