Sina mapenzi na mama yangu

EL ELYON

JF-Expert Member
Jan 2, 2013
1,563
1,886
Wakuu habari..

Mmebarikiwà sana na Mungu wa Mbinguni hakuna laana.

Aisee Mimi Nina wadogo zangu wawili Mimi nikiwa mtoto wa Kwanza tena wa kiume mdogo wangu wa pili ni wa kike na wa mwisho ni wa kiume.

Cha ajabu toka nikiwa mdogo hata sijaanza chekechea nilikuwa naishi na shangazi yangu ndiye kanilea mpaka najitambua nilikuwa namuita mama mpaka namaliza darasa la Saba nilijua ndiye mama yangu.

Wakati huo mdogo wangu wa kike anayenifuata yeye alikuwa anaishi na Baba mkoa mwingine huko Naye sikuwa namjua wala yeye hakuwa ananijua zaidi ya kujua Tu Nina mdogo wangu yupo mkoa Fulani

Yule dogo wa mwisho yeye ndo alikuwa na mama mzazi sasa maana kumbe Mzee aliachana na mama mara Tu baada ya kumzaa dogo wa mwisho na tetesi zilizopo inasemekana alienda kwao huku nyuma akamuacha beki tatu ambaye shangazi zangu walifanya mapinduzi ili beki tatu awe mama wa familia sa mama aliporudi kwake akakutana na mapinduzi hayo akaamua kusepa Hz ni tetesi Tu huwa naskia na huyo beki tatu ndiye mama wa familia hata sasa akiwa na watoto kadhaa.

Shida imekuja kwamba malezi yangu yote sikuwahi muona mama pale kwa shangazi nakumbuka nilipohitimu darasa la Saba nilisafiri na shangazi kwenda huko alipokuwa mama tulipofka shangazi akawa anaongea na watu fulan akanionyesha njia nipite nitangulie anakuja njiani nikapishana na mama mmoja nikamsalimia tukapishana kumbe aunt aliona si ndo akamstua mama kwamba huyo ndo mtoto wako unayepishana Naye hapo.

Ndo tukafahamiana sasa.
Sasa shida inayonikabili si Mimi Tu hata mdogo wangu wa pili hatuna mapenzi kabisa na mama yetu yaani hamna kabisa mama Naye Kila siku tunasikia anasema Sisi tuna mama zetu wengine mbaya zaidi anarusha mpaka na maneno mazito hata akifa tusiende kwenye msiba yaani hata sielewi kabisa.

Kingine mama anaamini uganga sana anaendaga kwa waganga sjui wampe dawa ya kurudsha uhusiano wake na Sisi lakini wapi imeshindikana.

Wakuu mnanishauri nn aisee maana sielewi siguswi kabisa na uwepo wa mama yangu.

NB: Wazazi hakikisheni mnakaa na watoto wenu hata kama wako mbali mjitahidi watambue uwepo wenu vinginevyo mtalaumu watoto bure Tu na kutupa laana.
 
Duh pole sana, ila wewe ni mimi kabisaaaaaaa yaaani, copy and paste kwenye maisha yangu hatujatofautiana kitu, ila tulicho tofautiana ni kuwa mimi shangazi yangu nae sasaivi naona kama ni ananivuruga tu sina ukaribu nae kutokana na matukio aliyo nifanyia hapo nyuma
 
Poleni wote wewe na mama yako.Una umri gani? Unaonekana hufahamu hata historia ya ukweli kwanini mama aliwaacha na haujataka hata kukaa nae mzungumze.
Umeshaweka kinyongo hutaki hata kusikia upande wake.Nakushauri tafuta muda mfuate mama upate kukaa nae mzungumze yote unayohisi yamefifisha mapenzi yako kwake.
Huenda mkapata muafaka na mkaboresha mahusiano yenu japo hayawezi kua sawa na waliolelewa na mama zao.
 
Ndugu pole sana kwa hilo nikuombe tu kwa unyeyekevu jaribu kwa njia yoyote ile kwa kadiri itakavyo wezekana uongee na Mama yako ana kwa ana ili mliweke sawa hili maana akitangulia mbele za haki mtihani wake ni mkubwa sana na hauwezi kuukabili kirahisi.
Imeandikwa waheshimu MAMA NA BABA UPATE MIAKA MINGI NA HERI DUNIANI.
 
Roho mbaya imepandikizwa na baba yako na hao shangazi zako.

Mama yako kufikia kupinduliwa na beki tatu kwa vile tu katoka kwenda kusalimia kurudi tayari kitanda chake analala mdada wa kazi uliyemtafuta mwenyewe.

Mbaya zaidi hao hao shangazi wakachukua watoto wake ili baba yako apeleke bajeti ya matunzo yako kwao.

Viatu vya mama yako havivaliki japo pia wengine tumepita humo ila mama yako kateswa zaidi.

okay well, Mungu amewakuza, leo wewe unajitambua lakini yale maroho mabaya uliyopandikiziwa yameshaugeuza moyo wako.

Anyways mpe mama yako haki yake ya upendo, ukiweza mpe matunzo.

Remember, haya mambo huwa hayaishii yaweza kuja kwako in other side ukabaki unalala kwenye ngozi kwa waganga kumbe umejiroga mwenyewe.
 
Wewe ni mtu mzima sasa. Kumbuka maisha mama aliyoyapitia, stress alizonazo, wewe ndie mtu wa kumfariji, kumwondolea concepts alizonazo. So unataka yeye ndie akutafte???? Be mature make your mother happy with you. Take trouble to settle any ill concepts alizonazo. Think maturely.
Umesema kw uchungu sana na amtengenezee uzee mwema mzazi wake huyu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom