Sina mapenzi na mama yangu

Wakuu habari..

Mmebarikiwà sana na Mungu wa Mbinguni hakuna laana.

Aisee Mimi Nina wadogo zangu wawili Mimi nikiwa mtoto wa Kwanza tena wa kiume mdogo wangu wa pili ni wa kike na wa mwisho ni wa kiume.

Cha ajabu toka nikiwa mdogo hata sijaanza chekechea nilikuwa naishi na shangazi yangu ndiye kanilea mpaka najitambua nilikuwa namuita mama mpaka namaliza darasa la Saba nilijua ndiye mama yangu.

Wakati huo mdogo wangu wa kike anayenifuata yeye alikuwa anaishi na Baba mkoa mwingine huko Naye sikuwa namjua wala yeye hakuwa ananijua zaidi ya kujua Tu Nina mdogo wangu yupo mkoa Fulani

Yule dogo wa mwisho yeye ndo alikuwa na mama mzazi sasa maana kumbe Mzee aliachana na mama mara Tu baada ya kumzaa dogo wa mwisho na tetesi zilizopo inasemekana alienda kwao huku nyuma akamuacha beki tatu ambaye shangazi zangu walifanya mapinduzi ili beki tatu awe mama wa familia sa mama aliporudi kwake akakutana na mapinduzi hayo akaamua kusepa Hz ni tetesi Tu huwa naskia na huyo beki tatu ndiye mama wa familia hata sasa akiwa na watoto kadhaa.

Shida imekuja kwamba malezi yangu yote sikuwahi muona mama pale kwa shangazi nakumbuka nilipohitimu darasa la Saba nilisafiri na shangazi kwenda huko alipokuwa mama tulipofka shangazi akawa anaongea na watu fulan akanionyesha njia nipite nitangulie anakuja njiani nikapishana na mama mmoja nikamsalimia tukapishana kumbe aunt aliona si ndo akamstua mama kwamba huyo ndo mtoto wako unayepishana Naye hapo.

Ndo tukafahamiana sasa.
Sasa shida inayonikabili si Mimi Tu hata mdogo wangu wa pili hatuna mapenzi kabisa na mama yetu yaani hamna kabisa mama Naye Kila siku tunasikia anasema Sisi tuna mama zetu wengine mbaya zaidi anarusha mpaka na maneno mazito hata akifa tusiende kwenye msiba yaani hata sielewi kabisa.

Kingine mama anaamini uganga sana anaendaga kwa waganga sjui wampe dawa ya kurudsha uhusiano wake na Sisi lakini wapi imeshindikana.

Wakuu mnanishauri nn aisee maana sielewi siguswi kabisa na uwepo wa mama yangu.

NB: Wazazi hakikisheni mnakaa na watoto wenu hata kama wako mbali mjitahidi watambue uwepo wenu vinginevyo mtalaumu watoto bure Tu na kutupa laana.
Kosa halikuwa la mama ako
Unadhani mama ako alikuwa na uwezo wa kuwalea?
Jitahidi kumpenda mama ako,unamuumiza nafsi yake
 
Wakuu habari..

Mmebarikiwà sana na Mungu wa Mbinguni hakuna laana.

Aisee Mimi Nina wadogo zangu wawili Mimi nikiwa mtoto wa Kwanza tena wa kiume mdogo wangu wa pili ni wa kike na wa mwisho ni wa kiume.

Cha ajabu toka nikiwa mdogo hata sijaanza chekechea nilikuwa naishi na shangazi yangu ndiye kanilea mpaka najitambua nilikuwa namuita mama mpaka namaliza darasa la Saba nilijua ndiye mama yangu.

Wakati huo mdogo wangu wa kike anayenifuata yeye alikuwa anaishi na Baba mkoa mwingine huko Naye sikuwa namjua wala yeye hakuwa ananijua zaidi ya kujua Tu Nina mdogo wangu yupo mkoa Fulani

Yule dogo wa mwisho yeye ndo alikuwa na mama mzazi sasa maana kumbe Mzee aliachana na mama mara Tu baada ya kumzaa dogo wa mwisho na tetesi zilizopo inasemekana alienda kwao huku nyuma akamuacha beki tatu ambaye shangazi zangu walifanya mapinduzi ili beki tatu awe mama wa familia sa mama aliporudi kwake akakutana na mapinduzi hayo akaamua kusepa Hz ni tetesi Tu huwa naskia na huyo beki tatu ndiye mama wa familia hata sasa akiwa na watoto kadhaa.

Shida imekuja kwamba malezi yangu yote sikuwahi muona mama pale kwa shangazi nakumbuka nilipohitimu darasa la Saba nilisafiri na shangazi kwenda huko alipokuwa mama tulipofka shangazi akawa anaongea na watu fulan akanionyesha njia nipite nitangulie anakuja njiani nikapishana na mama mmoja nikamsalimia tukapishana kumbe aunt aliona si ndo akamstua mama kwamba huyo ndo mtoto wako unayepishana Naye hapo.

Ndo tukafahamiana sasa.
Sasa shida inayonikabili si Mimi Tu hata mdogo wangu wa pili hatuna mapenzi kabisa na mama yetu yaani hamna kabisa mama Naye Kila siku tunasikia anasema Sisi tuna mama zetu wengine mbaya zaidi anarusha mpaka na maneno mazito hata akifa tusiende kwenye msiba yaani hata sielewi kabisa.

Kingine mama anaamini uganga sana anaendaga kwa waganga sjui wampe dawa ya kurudsha uhusiano wake na Sisi lakini wapi imeshindikana.

Wakuu mnanishauri nn aisee maana sielewi siguswi kabisa na uwepo wa mama yangu.

NB: Wazazi hakikisheni mnakaa na watoto wenu hata kama wako mbali mjitahidi watambue uwepo wenu vinginevyo mtalaumu watoto bure Tu na kutupa laana.
Pole sana sana sana. Waliopitia haya ndio wanaweza kuelewa. Mimi haya nayapitia lakn nimejifunza kitu kimoja kupitia mawaidha na nasaha za viongozi wa dini. Fanya kila jambo kwa ajili ya mwenyezi Mungu, kwa hiyo pamoja na nafsi kuwa nzito, kutokua na mapenzi naye jitahidi kumtafta kwa kadri uwezavyo, na kwa upande wako afadhali hata huyo mama yako nae anatamani wengine hata hatuelewi historia ilikuaje, hajakulea na bado unajitahidi kumtfta na hayupo tauari kuupokea ukaribu wako.
Mimi namtafta tu sababu Mungu ndio kaamrisha, lkn mapenzi kiukweli hakuna lkn ni kwa ajili Allah kampa daraja kubwa mzazi
 
Roho mbaya imepandikizwa na baba yako na hao shangazi zako.

Mama yako kufikia kupinduliwa na beki tatu kwa vile tu katoka kwenda kusalimia kurudi tayari kitanda chake analala mdada wa kazi uliyemtafuta mwenyewe.

Mbaya zaidi hao hao shangazi wakachukua watoto wake ili baba yako apeleke bajeti ya matunzo yako kwao.

Viatu vya mama yako havivaliki japo pia wengine tumepita humo ila mama yako kateswa zaidi.

okay well, Mungu amewakuza, leo wewe unajitambua lakini yale maroho mabaya uliyopandikiziwa yameshaugeuza moyo wako.

Anyways mpe mama yako haki yake ya upendo, ukiweza mpe matunzo.

Remember, haya mambo huwa hayaishii yaweza kuja kwako in other side ukabaki unalala kwenye ngozi kwa waganga kumbe umejiroga mwenyewe.
Mtoa mada nimemshangaa sana
Natamani nijue umri wake,hlf eti ndio mtoto wa kiume wa kwanza,anashindwa hata kujiongeza nini shida
 
Nakukumbusha tu shangazi ako na mama ako ni mtu na wifi yake....
Fatilia zaidi mahusiano ya mawifi utagundua kitu, pole kwa yote.
Mpnz usiombe ukakua kweny mazingira ya hivi, imagine bibi ambae ni mama wa mama yangu anamwambia mwanae tengeneza uhusiano mzuri na mtoto wako lkn bado.
Ni mtihan hasa
 
Mkuu skuelewi kbs aisee ngoja nikunyamazie Tu maanA maana kelele za vuvuzela hazizuii nyavu kutingishika na kama ni mwanamke bs kama umeolewa mumeo ana wakati mgumu sana aisee inaonekana we ni mjuaji Fulani halafu Una mdomo sana na kiherehere
Mtoa mada nimemshangaa sana
Natamani nijue umri wake,hlf eti ndio mtoto wa kiume wa kwanza,anashindwa hata kujiongeza nini shida
Mtoa mada nimemshangaa sana
Natamani nijue umri
 
Sasa kilichotokea tena ni kwamba haohao mashangazi wametupindua Sisi watoto WA WiFi Yao WA Kwanza kwani mpk wamemlisha sumu Mzee kwamba dogo WA mwisho si mtoto WA Mzee Mimi pia na Mzee hakuna maelewano kbs na ndo nilikuwa kipenz chake na nilionyesha wazi sina masihara kabisa na watu wapuuzi kwny familia aisee kumbe Mzee kuwa sn upande wangu hiyo iliwauma inasemekana wakaanza uganga na uchawi kunigombanisha na Mzee na wamefanikiwa kbs sister Alishaolewa ingawa Naye kutwa nzima hao mashangaz wanaombea na kutamka ndoa haitadumu Yani vurumai Tu bt nashukuru Mungu naendelea na family yangu nilichoamua ni kuishi kama Osama hakuna kujua mawasiliano yangu wala kujua nafanya kaz wapi. Yule ma mdogo pia wivu ulimjaa kuona Mzee Yuko sn upande wangu naona ilipgwa kolabo tena kunimalza aisee. Maana Mzee alikuwa Mambo Safi na wake mashangaz njaa Kali wakaona nitakata mirija Yao ndo hivyo kwahiyo hata home Nina miaka sjakanyaga wala sina mawasiliano na Mzee tena Ila simlaumu yeye tatzo ni Dada zake Tu na na mdogo. So pale ni kama watoto WA mke wakwanza tulishaondolewa kinamna Yani pale ni kama si kwetu tena kabaki ma mdogo na watoto wake na ndugu zake Tu. Ndo maisha yalivyo Ila Niko imara kuliko Jana siyumbushwi kbs uzuri nao wananijua misimamo yangu si ya kuyumba hata Mzee ananijua. Kuna SKU shangazi mdogo wake na shangazi aliyenilea alipeleka umbea Fulani Kwa Mzee sa Mzee akapotezea ma mdogo akaja nigusia aisee nilimuwashia Moto mkali sn ni zaidi ya mara moja namuwashia Moto nadhan haya nayo yalichangia kuanza mapambano ya kunitengenisha na Mzee.
Mbona kama mchawi wa haya mambo anajulikana, hapa shida ni shangazi utakuta mama hata hakuna baya alilofanya.
 
Roho mbaya imepandikizwa na baba yako na hao shangazi zako.

Mama yako kufikia kupinduliwa na beki tatu kwa vile tu katoka kwenda kusalimia kurudi tayari kitanda chake analala mdada wa kazi uliyemtafuta mwenyewe.

Mbaya zaidi hao hao shangazi wakachukua watoto wake ili baba yako apeleke bajeti ya matunzo yako kwao.

Viatu vya mama yako havivaliki japo pia wengine tumepita humo ila mama yako kateswa zaidi.

okay well, Mungu amewakuza, leo wewe unajitambua lakini yale maroho mabaya uliyopandikiziwa yameshaugeuza moyo wako.

Anyways mpe mama yako haki yake ya upendo, ukiweza mpe matunzo.

Remember, haya mambo huwa hayaishii yaweza kuja kwako in other side ukabaki unalala kwenye ngozi kwa waganga kumbe umejiroga mwenyewe.

Hahahaahahaah


Unadhani wanaume wana tabia za kupandikiza machuki kama nyie wanwake.


Mtoto katengwa namama yake ipo wazi kabisa wewe unaleta mambo ya chuki zenu ukidhani wanaume nao wana tabia zenu
 
Mi bnafsi sina tatzo na mama kbs na najua watu wabaya ni mawifi zake na mbaya zaidi Mzee katekwa na Dada zake. Shida mi sina mapenzi na mama Tu Ila si kwamba nini shida Naye maana sjawahi gombana Naye maana sjawahi ishi Naye kbs kbs hatujuani Kwa undani bifu zake na Mzee mpk kuachana Sisi watoto hatujui Kwa undani zaidi Ila mi hicho kisa cha beki tatu nilikiskia Tu kikisemwa na ndugu tena mama alipinduliwa wakati kajifungua Yule mdogo wangu WA mwisho akaenda kwao kupumzka kurudi akakuta mji si wake tena.
Mbona kama mchawi wa haya mambo anajulikana, hapa shida ni shangazi utakuta mama hata hakuna baya alilof
 
Tatizo limeanzia kwa Baba yako,mtu mzima utashawishiwaje umuache mkeo na kuoa beki 3?

Si ajabu huyo Mama yako alipigwa marufuku hata kukanyaga kuja kuwaona nyie watoto wake,
Uchungu wa mwana aujuaye mzazi,Mama yako hana kosa lolote,sema anajua nyie watoto wake mmesha pandikizwa maneno ili mumchukie,

Usifuate akili za Baba yako za kupangiwa maisha na wengine,unamchukia Mama yako kwa maneno ya kusikia au kwa kujiaminisha kua hakua anakuja kuwaona coz hakuwajali?

Tafuta sababu ambayo ilimfanya Mama yako asije kuwaona,huenda hata alisha ongopewa kua nyie mlisha kufa toka kitambo,

Kaongee na Mama yako,anayo mengi sana ya kukusimulia,ana maumivu makubwa sana ndani ya nafsi yake.
 
Wakuu habari..

Mmebarikiwà sana na Mungu wa Mbinguni hakuna laana.

Aisee Mimi Nina wadogo zangu wawili Mimi nikiwa mtoto wa Kwanza tena wa kiume mdogo wangu wa pili ni wa kike na wa mwisho ni wa kiume.

Cha ajabu toka nikiwa mdogo hata sijaanza chekechea nilikuwa naishi na shangazi yangu ndiye kanilea mpaka najitambua nilikuwa namuita mama mpaka namaliza darasa la Saba nilijua ndiye mama yangu.

Wakati huo mdogo wangu wa kike anayenifuata yeye alikuwa anaishi na Baba mkoa mwingine huko Naye sikuwa namjua wala yeye hakuwa ananijua zaidi ya kujua Tu Nina mdogo wangu yupo mkoa Fulani

Yule dogo wa mwisho yeye ndo alikuwa na mama mzazi sasa maana kumbe Mzee aliachana na mama mara Tu baada ya kumzaa dogo wa mwisho na tetesi zilizopo inasemekana alienda kwao huku nyuma akamuacha beki tatu ambaye shangazi zangu walifanya mapinduzi ili beki tatu awe mama wa familia sa mama aliporudi kwake akakutana na mapinduzi hayo akaamua kusepa Hz ni tetesi Tu huwa naskia na huyo beki tatu ndiye mama wa familia hata sasa akiwa na watoto kadhaa.

Shida imekuja kwamba malezi yangu yote sikuwahi muona mama pale kwa shangazi nakumbuka nilipohitimu darasa la Saba nilisafiri na shangazi kwenda huko alipokuwa mama tulipofka shangazi akawa anaongea na watu fulan akanionyesha njia nipite nitangulie anakuja njiani nikapishana na mama mmoja nikamsalimia tukapishana kumbe aunt aliona si ndo akamstua mama kwamba huyo ndo mtoto wako unayepishana Naye hapo.

Ndo tukafahamiana sasa.
Sasa shida inayonikabili si Mimi Tu hata mdogo wangu wa pili hatuna mapenzi kabisa na mama yetu yaani hamna kabisa mama Naye Kila siku tunasikia anasema Sisi tuna mama zetu wengine mbaya zaidi anarusha mpaka na maneno mazito hata akifa tusiende kwenye msiba yaani hata sielewi kabisa.

Kingine mama anaamini uganga sana anaendaga kwa waganga sjui wampe dawa ya kurudsha uhusiano wake na Sisi lakini wapi imeshindikana.

Wakuu mnanishauri nn aisee maana sielewi siguswi kabisa na uwepo wa mama yangu.

NB: Wazazi hakikisheni mnakaa na watoto wenu hata kama wako mbali mjitahidi watambue uwepo wenu vinginevyo mtalaumu watoto bure Tu na kutupa laana.

Pole sana. Una umri gani sasa?

Maumivu huathiri sana fikra, jitahidi wewe umpende sana mama yako. Unaweza kuwa tiba kwake na kubadili mambo yote mabaya anayofanya

Najaribu ku imagine maumivu ya kurudi kwangu halafu nakuta housegal ndio mwenye nyumba na mume, halafu wifi zangu ndio washikadau na wamegawana watoto niliowazaa. Halafu ukute hapo sina hata pa kuanzia...... Wababa muwe na huruma jamani
 
Mkuu skuelewi kbs aisee ngoja nikunyamazie Tu maanA maana kelele za vuvuzela hazizuii nyavu kutingishika na kama ni mwanamke bs kama umeolewa mumeo ana wakati mgumu sana aisee inaonekana we ni mjuaji Fulani halafu Una mdomo sana na kiherehere
Mkuu kwa hii comment ni wazi wewe ni binadamu wa ajabu sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwann mnapenda kuweka personal/family issue public??
Unamchoresha tu mama yako
Anamchoresha kwani ametaja jina? Au ww unamjua mleta maada au mama yake? Mtu amekuja kuomba kusaidiwa mawazo jnc ya kutatua tatizo lake ww umekalia unamchoresha mama yako.

Nyie ndo hamkawiagi kujitia kitanzi kisa tu hamuwezi kushirikisha wngn matatizo yenu.
 
Pole Sana mtoa mada naelewa unachokipitiaTuna share tatizo Ila Tofauti ni kuwa wewe huna mapenzi na Mama Mimi Sina Mapenzi Na BABA MZAZI,

Nina umri wa miaka zaidi ya 30 now. Jitihada zimeshafanywa na ndugu na marafiki ili kurudisha uhusiano wangu na Baba but ni kama Imeshindikana. Binafsi hiki kitu kinanitesa sana, na kinachonitesa zaidi ni kuona watoto wangu hawamfahamu Babu yao hata kwa sura hata sauti wakati yupo hai hata miaka 60 hajafikisha.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom