Simulizi ya kweli: Mpaka kieleweke

Simulizi ya kweli: Mpaka kieleweke

Story: Mpaka Kieleweke
Mtunzi: Nira Saire
SEHEMU YA 15

Ilipoishia...

Sauda akanitambulisha kwa watu wale ambao walionekana kujua kila kitu juu ya mpango wangu kisha akamtaka bwana yule kuandaa mpango mzuri "sasa Mkude nataka uhakikishe kuwa huyu bwana anafanikiwa kuingia nyumbani kwa Magugi kisha mambo mengine yatafuata" aliongea Sauda maneno ambayo yalinishtua sana, kuingia kwa Magugi tena? mtu ambaye ameapa kuwa atanipata kabla siku haijaisha, tena nijipeleke mpaka kwake? Niliwaza..
"Hakuna shida, ingawa ili kumuingiza kwa Magugi itagharimu maisha ya mtu asiye na hatia" aliongea bwana yule ambaye kwa harakaharaka alionekana mpole sana.
"Unazungumzia mtu mmoja? Jambo hili ni lazima litimie hata kwa kuua mamilioni ya watu" alijibu Sauda kwa maneno yale ambayo hayakufanana hata kidogo na muonekano wake..

Endelea..

baada ya Sauda kuondoka nilibaki na bwana yule kila mmoja wetu akiwa kimya!. Ndani ya kichwa changu kulikuwa kukiendelea mawazo ya hapa na pale, huku nikiwa najaribu kupanga na kupangua mipango ya kujitoa Muifufu nikiwa na wote ambao natakiwa kuwarudisha duniani!.
"nawezaje kuingia kwa Magugi na nikawa salama?" nilivunja ukimya na kumuuliza bwana yule ambaye naye alionekana kama alikuwa na mambo mengi yakiendelea kichwani kwake..
"hiyo sio kazi rahisi hata kidogo, kuna mambo mengi ya kufanywa kabla ya kulifikia hilo, umeshajiuliza tayari Magugi amejuaje kama umeingia Muifufu?" alihojo bwana yule..
Nilitulia nikijaribu kufikiri kwa sekunde chache kisha nikajibu "ni jambo la kustaajabisha, sijui namna gani aliweza kugundua ikiwa hakuna mtu yeyote ambaye alishuhudia kuingia kwangu" bwana yule akakaa sawa akijisogeza karibu zaidi na ambapo nilikuwa nimekaa mimi kisha akaanza kunielezea.. "Magugi anafuga majini!.. majini ambayo anayategemea sana kwenye kupata taarifa za kila ambacho kinaendelea!, majini hao wapo kila sehemu na humuotesha kila ambacho wamekiona na kudhani kinaweza kuwa cha madhara kwake!, bila shaka majini hao ndio ambao walikuona na kumfikishia habari ndotoni kama ilivyo kawaida yao"
"duuh! sasa kuingia kwake si nisawa na kujinasisha mtegoni?" niliuliza nikionesha wasiwasi wa wazi juu ya habari ile mpya ambayo nilikuwa nimeipata!..
"ndo maana nikakwambia kuwa kuna mambo ya kufanywa kabla ya kufikia kwenda, kwanini haujiulizi tunawezaje kuongea hapa habari za kumletea madhara na hazipati pamoja na kwamba majini wake wako doria?" aliuliza tena bwana yule nami nikaelewa kuwa alikuwa akijaribu kunionesha kuwa kuna njia za kudhibiti uwezo wa wale majini kusafirisha taarifa kwenda kwa Magugi..
"kwani hakuna njia ya kufanya bila ya kwenda nyumbani kwa Magugi" nilizidi kuuliza masawali kama k awaida yangu, huwa sikai na swali lisilo na jibu ikiwa namuona ambaye anaweya kunipa majibu!..
"unaogopa?" aliuliza bwana yule lakini akawahi kuendelea kabla hata sijamjibu "hii ni vita, tena vita kubwa kwelikweli!.. kushinda kwenye vita hii ni ukombozi kwa watu wengi sana, lakini kushindwa kwake ni maangamizo kwa watu wote hao ambao wanautegemea mno ushindi huo! wewe ndiye kiongozi wa vita hii! nataka ulitambue hilo kuanzia sasa na mambo ya uoga uyaache kuanzia leo kwani kuna wengi nyuma yako wako tayari kufanya chochote kwa kukutegemea wewe!.. ikiwa utaonesha uoga basi wao watakata tamaa kabisaa!"
alisema kwa msisitizo bwana yule!..
"kama ni kuogopa nimeshaogopa sana juu ya jambo hili!.. mpaka nimefikia uamuzi wa kuja huku ni kutokana na kuamua kwa dhati kuwa niko tayari kukabiliana na changamoto zozote zilizopo! usichukulie kuuliza kwangu kama uoga, ila ni kutaka kujua nini cha kufanywa na kuhakikisha kinafanyika kwa usahihi" nilijieleza kwa msisitizo wa hali ya juu kujaribu kumuonesha bwana yule kuwa sikuwa mtu wa kutoaminiwa hata kidogo!.. bwana yule alionesha sura ya kutabasamu baada ya maelezo yangu yale kisha akaongea "sasa umeongea, nafurahi pia kuona kuwa unajiamini sana! jambo hili litafa nikiwa kwa hakika" bwana yule akanitaka kupumzika ili baadae anielezee juu ya mipango ambayo inatakiwa kufuatwa kukamilisha zoezi la mimi kuingia nyumbani kwa Magugi, lakini nikamtaka kuendelea tu na maelekezo kwani sikuwa nimechoka na pia jambo la kuelezewa tu halinihitaji kuwa na nguvu, bwana yule hakuwa mtu mbishi! akaanza kunielezea! "Muifufu kulikuwa na wachawi wa kila aina na wenye mbinu mbalimbali!..
baada ya kushindwa kurudi duniani na kubaki huku, Magugi ambaye alikuwa mwanafunzi mzuri wa uchawi huko duniani aliteuliwa kuwa kiongozi na wazee ambao baada ya muda mfupi wote walikufa na kuiacha jamii hii chini ya utawala wa Magugi ambaye aliaza akiwa kiongozi mzuri tu mwenye kuonesha kuijali hatma ya Wanamuifufu! akawaweka wachawi katika makundi kulingana na ujuzi waliokuwanao kisha akawatumia vizuri kujifunza mbinu ambazo walikuwanazo na baada ya hapo aliwafuta kumbukumbu na kuwafunza machache ambayo alijua angehitaji wamsaidie na akahakikisha anakuwa na uwezo wa kuwatawala!..
miongoni mwa makundi ya wachawi ambao walikuwepo walikuwa ni wafugaji wa majini ambao aliwatumia wakamtengenezea majini ya kutosha ambayo angeweza kuyatumia kwa ulinzi na shughuli nyingine! baada ya kazi hiyo alitaka kuwafuta kumbukumbu kama ambavyo alifanya kwa makundi mengine lakini kwa kundi hili ilishindikana kwakuwa majini wale walikuwa tayari kupambana kuhakikisha hilo halitokei hivyo kundi lile kupitia kwa kiongozi wao wakaomba waachwe kama walivyo nao wakatoa ahadi ya kutoingilia mipango ya Magugi, ikabidi busara itumike na Magugi akakubaliana nao kwa sharti ya kuwaweka mbali na jamii, jambo ambalo walikubaliananalo hivyo wakapelekwa nyuma ya kilima kileee!..." aliendelea kuelezea kuku akinionesha kilima kilichokuwa kikionekana kwa mbali, kilima kile kilikuwa kikionekana kama ambacho kimegawanyiki mbele kikiwa kifupi huku nyuma kukizidi urefu kidogo! "kundi lile la wafugaji wa majini waliwekwa huko huku wakiahidiwa kupewa huduma zote nao wakaapa kutorudi kwenye jamii hii, lakini Magugi aliwageuka na kuwatelekeza huko huku akitumia uchawi kuzuia watu wa huku pia wasiende kule! kwa kutumia uwezo wa majini watu wale wangeweza kurudi ila kinachowakwamisha ni mila zao! watu wale huwa hawavunji kiapo ambacho wamekiweka hata iweje, kuna tetesi kuwa iwapo mtu wa jamii ile akivunja kiapo hufa! njia pekee ya kiapo chao kuvunjika huwa ni kifo cha ambaye walimuapia! hivyo kurudi kwao huku ni mpaka afe Magugi" Aliweka kituo bwana yule, akaniacha nikiwaza kuwa alikuwa ananitaka kumuua Magugi kwaajili ya watu hao! "maisha ambayo wanaishi watu wale ni magumu mno!, hata chakula na maji safi ya kunywa ni ngumu sana kupatikana kwao, hivyo wanatamani sana kurudi, tatizo ni kutoweza kwao kuvunja kiapo! iwapo utaenda kuwaona na kuwaahidi kumuua Magugi ili wao wame huru basi bila shaka watakusaidia namna ya kuwanyamazisha majini ambayo ni wao waliyatengeneza na ndio tegemezi pekee la Magugi" alimaliza kueleza bwana yule. Nilimuelewa vizuri bwana yule na kuamua kuwa ni lazima kufanya kama ambavyo amenielezea ili kujihakikishia uwezo wa kupam bana na Magugi, kwakuwa kwa msaada wa majini wale isingekuwa rahisi.
"nawezaje kufika huko walipo wafugaji wale wa majini?" niliuliza nikiwa tayari kwa safari hiyo, sikutaka kabisa jambo lile lichelewe! "itakupasa kungoja usiku uingie ili tuweze kukupatia dawa ambayo unatakiwa kuiogea katikati mwa saa nne na saa tano usiku ili kujikinga na majini wa Magugi kisha ndipo safari itakapoanza! kupanda mlima ule mpaka kushuka upande wa pili itakuchukua usiku wote mpaka kunakucha" alielezea bwana yule!!..
"huku hakuna wanyama ambao wanaweza kutumika kama usafiri na wakaenda kwa kasi za kunipikisha huko mapema?.. niliuliza naye akajibu "wanyama wapo ila hutumika kwa ruhusa ya Magugi, mtunzaji wa wanyama wale ni bwana mmoja katili sana ambaye ni mtiifu kwa Magugi kama walivyo watu wote wa Muifufu" alielezea bwana yule!..
nikachukua ule mkoba wangu niliopewa na Mnaro na kuchukua ule mkate ambao alinielezea kuwa endapo ningemlisha mtu yeyote basi angefanya chochote ambacho ningemwambia! nikakata kidogo na kumkabidhi yule bwana.. "hakikisha mtu huyo anakula mkate huu, kisha tunaweza kumtuma na hakuna mtu ambaye atamuelezea juu ya hilo" bwana yule akapokea kipande kile bila ubishi wala maswali, kisha akatoka akinitaka kupumzika, kwaajili ya safari ya usiku!..
nilibaki nikiwa na wasiwasi mwingi kwakuwa sikuwa nimejaribu kutumia mbinu ile ambayo alinifundisha Mnaro ambaye yeye mwenyewe hakuwa na uhakika kama bado huku Muifufu kuko kama ambavyo alipaacha.. vipi kama huyo bwana anayepelekewa mkate ule atakuwa ana nguvu ya kuzidi uchawi ule na hivyo kugundua dhamira yetu?! niliwaza na kubaki kuomba tu mambo yaende kama ambavyo tulihitaji....

usikose sehemu ya kumi na sita.

mawasiliano:
0653686008
0718274130
nirasaire@gmail.com
facebook.com/nira.saire
@nira_saire (instagram)
 
kaka yangu mleta story, ningekushauri ukae kimya tu! tutakaoweza tutakutafuta, kubali tu kwamba umetukatisha maana tulizoea hapa lakin sio mbaya, ni maamuzi yako dear!
 
Story: Mpaka Kieleweke
Mtunzi: Nira Saire
SEHEMU YA 15

Ilipoishia...

Sauda akanitambulisha kwa watu wale ambao walionekana kujua kila kitu juu ya mpango wangu kisha akamtaka bwana yule kuandaa mpango mzuri "sasa Mkude nataka uhakikishe kuwa huyu bwana anafanikiwa kuingia nyumbani kwa Magugi kisha mambo mengine yatafuata" aliongea Sauda maneno ambayo yalinishtua sana, kuingia kwa Magugi tena? mtu ambaye ameapa kuwa atanipata kabla siku haijaisha, tena nijipeleke mpaka kwake? Niliwaza..
"Hakuna shida, ingawa ili kumuingiza kwa Magugi itagharimu maisha ya mtu asiye na hatia" aliongea bwana yule ambaye kwa harakaharaka alionekana mpole sana.
"Unazungumzia mtu mmoja? Jambo hili ni lazima litimie hata kwa kuua mamilioni ya watu" alijibu Sauda kwa maneno yale ambayo hayakufanana hata kidogo na muonekano wake..

Endelea..

baada ya Sauda kuondoka nilibaki na bwana yule kila mmoja wetu akiwa kimya!. Ndani ya kichwa changu kulikuwa kukiendelea mawazo ya hapa na pale, huku nikiwa najaribu kupanga na kupangua mipango ya kujitoa Muifufu nikiwa na wote ambao natakiwa kuwarudisha duniani!.
"nawezaje kuingia kwa Magugi na nikawa salama?" nilivunja ukimya na kumuuliza bwana yule ambaye naye alionekana kama alikuwa na mambo mengi yakiendelea kichwani kwake..
"hiyo sio kazi rahisi hata kidogo, kuna mambo mengi ya kufanywa kabla ya kulifikia hilo, umeshajiuliza tayari Magugi amejuaje kama umeingia Muifufu?" alihojo bwana yule..
Nilitulia nikijaribu kufikiri kwa sekunde chache kisha nikajibu "ni jambo la kustaajabisha, sijui namna gani aliweza kugundua ikiwa hakuna mtu yeyote ambaye alishuhudia kuingia kwangu" bwana yule akakaa sawa akijisogeza karibu zaidi na ambapo nilikuwa nimekaa mimi kisha akaanza kunielezea.. "Magugi anafuga majini!.. majini ambayo anayategemea sana kwenye kupata taarifa za kila ambacho kinaendelea!, majini hao wapo kila sehemu na humuotesha kila ambacho wamekiona na kudhani kinaweza kuwa cha madhara kwake!, bila shaka majini hao ndio ambao walikuona na kumfikishia habari ndotoni kama ilivyo kawaida yao"
"duuh! sasa kuingia kwake si nisawa na kujinasisha mtegoni?" niliuliza nikionesha wasiwasi wa wazi juu ya habari ile mpya ambayo nilikuwa nimeipata!..
"ndo maana nikakwambia kuwa kuna mambo ya kufanywa kabla ya kufikia kwenda, kwanini haujiulizi tunawezaje kuongea hapa habari za kumletea madhara na hazipati pamoja na kwamba majini wake wako doria?" aliuliza tena bwana yule nami nikaelewa kuwa alikuwa akijaribu kunionesha kuwa kuna njia za kudhibiti uwezo wa wale majini kusafirisha taarifa kwenda kwa Magugi..
"kwani hakuna njia ya kufanya bila ya kwenda nyumbani kwa Magugi" nilizidi kuuliza masawali kama k awaida yangu, huwa sikai na swali lisilo na jibu ikiwa namuona ambaye anaweya kunipa majibu!..
"unaogopa?" aliuliza bwana yule lakini akawahi kuendelea kabla hata sijamjibu "hii ni vita, tena vita kubwa kwelikweli!.. kushinda kwenye vita hii ni ukombozi kwa watu wengi sana, lakini kushindwa kwake ni maangamizo kwa watu wote hao ambao wanautegemea mno ushindi huo! wewe ndiye kiongozi wa vita hii! nataka ulitambue hilo kuanzia sasa na mambo ya uoga uyaache kuanzia leo kwani kuna wengi nyuma yako wako tayari kufanya chochote kwa kukutegemea wewe!.. ikiwa utaonesha uoga basi wao watakata tamaa kabisaa!"
alisema kwa msisitizo bwana yule!..
"kama ni kuogopa nimeshaogopa sana juu ya jambo hili!.. mpaka nimefikia uamuzi wa kuja huku ni kutokana na kuamua kwa dhati kuwa niko tayari kukabiliana na changamoto zozote zilizopo! usichukulie kuuliza kwangu kama uoga, ila ni kutaka kujua nini cha kufanywa na kuhakikisha kinafanyika kwa usahihi" nilijieleza kwa msisitizo wa hali ya juu kujaribu kumuonesha bwana yule kuwa sikuwa mtu wa kutoaminiwa hata kidogo!.. bwana yule alionesha sura ya kutabasamu baada ya maelezo yangu yale kisha akaongea "sasa umeongea, nafurahi pia kuona kuwa unajiamini sana! jambo hili litafa nikiwa kwa hakika" bwana yule akanitaka kupumzika ili baadae anielezee juu ya mipango ambayo inatakiwa kufuatwa kukamilisha zoezi la mimi kuingia nyumbani kwa Magugi, lakini nikamtaka kuendelea tu na maelekezo kwani sikuwa nimechoka na pia jambo la kuelezewa tu halinihitaji kuwa na nguvu, bwana yule hakuwa mtu mbishi! akaanza kunielezea! "Muifufu kulikuwa na wachawi wa kila aina na wenye mbinu mbalimbali!..
baada ya kushindwa kurudi duniani na kubaki huku, Magugi ambaye alikuwa mwanafunzi mzuri wa uchawi huko duniani aliteuliwa kuwa kiongozi na wazee ambao baada ya muda mfupi wote walikufa na kuiacha jamii hii chini ya utawala wa Magugi ambaye aliaza akiwa kiongozi mzuri tu mwenye kuonesha kuijali hatma ya Wanamuifufu! akawaweka wachawi katika makundi kulingana na ujuzi waliokuwanao kisha akawatumia vizuri kujifunza mbinu ambazo walikuwanazo na baada ya hapo aliwafuta kumbukumbu na kuwafunza machache ambayo alijua angehitaji wamsaidie na akahakikisha anakuwa na uwezo wa kuwatawala!..
miongoni mwa makundi ya wachawi ambao walikuwepo walikuwa ni wafugaji wa majini ambao aliwatumia wakamtengenezea majini ya kutosha ambayo angeweza kuyatumia kwa ulinzi na shughuli nyingine! baada ya kazi hiyo alitaka kuwafuta kumbukumbu kama ambavyo alifanya kwa makundi mengine lakini kwa kundi hili ilishindikana kwakuwa majini wale walikuwa tayari kupambana kuhakikisha hilo halitokei hivyo kundi lile kupitia kwa kiongozi wao wakaomba waachwe kama walivyo nao wakatoa ahadi ya kutoingilia mipango ya Magugi, ikabidi busara itumike na Magugi akakubaliana nao kwa sharti ya kuwaweka mbali na jamii, jambo ambalo walikubaliananalo hivyo wakapelekwa nyuma ya kilima kileee!..." aliendelea kuelezea kuku akinionesha kilima kilichokuwa kikionekana kwa mbali, kilima kile kilikuwa kikionekana kama ambacho kimegawanyiki mbele kikiwa kifupi huku nyuma kukizidi urefu kidogo! "kundi lile la wafugaji wa majini waliwekwa huko huku wakiahidiwa kupewa huduma zote nao wakaapa kutorudi kwenye jamii hii, lakini Magugi aliwageuka na kuwatelekeza huko huku akitumia uchawi kuzuia watu wa huku pia wasiende kule! kwa kutumia uwezo wa majini watu wale wangeweza kurudi ila kinachowakwamisha ni mila zao! watu wale huwa hawavunji kiapo ambacho wamekiweka hata iweje, kuna tetesi kuwa iwapo mtu wa jamii ile akivunja kiapo hufa! njia pekee ya kiapo chao kuvunjika huwa ni kifo cha ambaye walimuapia! hivyo kurudi kwao huku ni mpaka afe Magugi" Aliweka kituo bwana yule, akaniacha nikiwaza kuwa alikuwa ananitaka kumuua Magugi kwaajili ya watu hao! "maisha ambayo wanaishi watu wale ni magumu mno!, hata chakula na maji safi ya kunywa ni ngumu sana kupatikana kwao, hivyo wanatamani sana kurudi, tatizo ni kutoweza kwao kuvunja kiapo! iwapo utaenda kuwaona na kuwaahidi kumuua Magugi ili wao wame huru basi bila shaka watakusaidia namna ya kuwanyamazisha majini ambayo ni wao waliyatengeneza na ndio tegemezi pekee la Magugi" alimaliza kueleza bwana yule. Nilimuelewa vizuri bwana yule na kuamua kuwa ni lazima kufanya kama ambavyo amenielezea ili kujihakikishia uwezo wa kupam bana na Magugi, kwakuwa kwa msaada wa majini wale isingekuwa rahisi.
"nawezaje kufika huko walipo wafugaji wale wa majini?" niliuliza nikiwa tayari kwa safari hiyo, sikutaka kabisa jambo lile lichelewe! "itakupasa kungoja usiku uingie ili tuweze kukupatia dawa ambayo unatakiwa kuiogea katikati mwa saa nne na saa tano usiku ili kujikinga na majini wa Magugi kisha ndipo safari itakapoanza! kupanda mlima ule mpaka kushuka upande wa pili itakuchukua usiku wote mpaka kunakucha" alielezea bwana yule!!..
"huku hakuna wanyama ambao wanaweza kutumika kama usafiri na wakaenda kwa kasi za kunipikisha huko mapema?.. niliuliza naye akajibu "wanyama wapo ila hutumika kwa ruhusa ya Magugi, mtunzaji wa wanyama wale ni bwana mmoja katili sana ambaye ni mtiifu kwa Magugi kama walivyo watu wote wa Muifufu" alielezea bwana yule!..
nikachukua ule mkoba wangu niliopewa na Mnaro na kuchukua ule mkate ambao alinielezea kuwa endapo ningemlisha mtu yeyote basi angefanya chochote ambacho ningemwambia! nikakata kidogo na kumkabidhi yule bwana.. "hakikisha mtu huyo anakula mkate huu, kisha tunaweza kumtuma na hakuna mtu ambaye atamuelezea juu ya hilo" bwana yule akapokea kipande kile bila ubishi wala maswali, kisha akatoka akinitaka kupumzika, kwaajili ya safari ya usiku!..
nilibaki nikiwa na wasiwasi mwingi kwakuwa sikuwa nimejaribu kutumia mbinu ile ambayo alinifundisha Mnaro ambaye yeye mwenyewe hakuwa na uhakika kama bado huku Muifufu kuko kama ambavyo alipaacha.. vipi kama huyo bwana anayepelekewa mkate ule atakuwa ana nguvu ya kuzidi uchawi ule na hivyo kugundua dhamira yetu?! niliwaza na kubaki kuomba tu mambo yaende kama ambavyo tulihitaji....

usikose sehemu ya kumi na sita.

mawasiliano:
0653686008
0718274130
nirasaire@gmail.com
facebook.com/nira.saire
@nira_saire (instagram)
waoooh nilikuwa sijaona jamani, umeamua kutuonea huruma, ubarikiwee
 
Nzi chuma asante kwa kuamua kuiendeleza

Kwenye comments zako hukutumia busara ungekaa kimya ingekua poa zaidi
 
yeyote anayetaka kupata muendelezo wa hii kitu ani-PM au anicheck kupitia 0653686008. Wako Nira Saire (Mtunzi)
 
Back
Top Bottom