Simulizi ya kusisimua

Simulizi ya kusisimua

Jaman story mbona imesitishwa? Inasisimua sana kwakweli
 
SIMULIZI : YALIYONIKUTA TANGA
MSIMULIAJI : MARTIN MEKU
MAHALI : TANGA
SEHEMU: Live another day.
ILIPOISHIA
Msimuliaji akiwa na mama yake kwa mganga wanaanza safari ya kurudi nyumbani kwa ahadi ya kwenda tena kwa mganga kupeleka kile kisanduku chenye dhahabu.
SASA ENDELEA...
Msimuliaji akiwa nyumbani kwao anatafakari aendelee kuturushia story au atangaze kitabu kinapatikana duka gani tukanunue, ghafla mlango wa chumba chake unagogwa kwa fujo sana. Anatoka huku amechukia mno, kufungua mlango asione mtu. Akatoka mpaka nje ya nyumba na asione mtu pia. Akaamua kurudi ndani.
Alipotaka kuingia chumbani, akashtuka kuona mlango umefungwa kwa ndani. Akaamua kuchungulia kupitia kwenye kitasa, hakuamini macho yake alipomuona maimuna amekaa kitandani anaipitia hadithi ambayo bado haijatumwa mtandaoni kwa umakini mkubwa huku akibubujikwa na machozi, pembeni yake kulikuwa na upanga uliojaa damu sambamba na kile kichwa cha Erick.
Je, maimuna ataifuta hadithi tunayoisubiri kwa hamu? Unafikiri msimuliaji atafanikiwa kuingia ndani kwake?
Usikose sehemu ya pili ya LIVE ANOTHER DAY
 
[<br />endelea tu na kiranga chako
Ukithutha wenzio twalaaaa
 
SIMULIZI : YALIYONIKUTA TANGA
MSIMULIAJI : MARTIN MEKU
MAHALI : TANGA
SEHEMU YA 21

ILIPOISHIA

Yule jini alipoondoka, yule
mwanamke alituuliza
tulichozungumza , tukamueleza.
“Sasa kesho mtakuja?” akatuuliza.
“Tutakuja kesho asubuhi”
nikamjibu.
“Ngoja nikupe dawa yangu”
akatuambia na kuinuka.
Aikwenda pembeni mwa chumba
hicho. Alikuwa ameweka
makorokoro yake ya kiganga.
Akachukua pembe moja ya
mnyama aliyokuwa ameifunga
kitambaa cheusi. Ule upande
uliokuwa na shina la ile pembe
aliukung’uta kwenye kiganja
chake, ukatoka unga mweusi.
Alinifungia unga huo kwenye
kikaratasi.
“Usiku utatia dawa hii kwenye
maji yako ya kuoga halafu utaoga”
akaniambia.
Nikakichuku kile kikaratasi na
kukitia mfukoni.
“Niitie yote au niibakishe?”
nikamuuliza.
“Tia yote”
“Sawa”
SASA ENDELEA
Mganga huyo nilimpa shilingi elfu
kumi tukaondoka. Tuliporudi
nyumbani nilifanya kama
nilivyoagizwa na mganga huyo.
Usiku kabla ya kulala nilitia ile
dawa kwenye ndoo ya maji ya
kuoga kisha nikaenda kuoga.
Nilipotoka kuoga nilikaa barazani
mwa nyumba yetu nikazungumza
na ndugu na jamaa waliokuwa
pale nyumbani hadi muda wa
kulala ulipowadia.
Asubuhi kulipokucha baada ya
kunywa chai nilichukua kile
kisanduku nikakitia ndani ya saflet
na kukibeba kama mzigo.
Tukatoka na mama kuelekea kwa
yule mganga.
Tulipofika, nilikitoa kile kisanduku
na kumuonesha.
“Kisanduku chenyewe ndio hiki?”
Mgnga akaniuliza.
“Ndio hicho” nikamjibu.
“Hebu kifungue” akaniambia.
Nikakifungua. Mganga alishangaa
alipoona mapambo ya dhahabu
yaliyokuwemo ndani.
“Hivi vyote vinaweza kufika
shilingi ngapi?” akaniuliza.
Mara moja nikagundua kuwa
mganga huyo alikuwa ameshapata
tamaa ya zile dhahabu.
“Bei ya dhahabu kwa sasa
imeshuka. Hizo zote zinaweza
kufika shilingi laki mbili”
nikamdanganya.
“Laki mbili tu zikutoe roho yako!”
“Kwanini?”
“Naona ni pesa ndogo sana”
“Hata mimi nimeona ni ujinga
kutolewa roho yangu kwa pesa
hizo ndio maana tumekuja kwako
uwazuie hao majini wasinifuate”
Mganga huyo akanifanyia uganga
wake kisha akatuma mtu aende
akachukue mchanga wa kaburini.
Alitaka aletewe kiasi kidogo cha
mchanga huo. Mtu aliyemtuma
alimletea mchanga huo alioufunga
kwenye kitambaa. Akamuagiza
tena akamletee kinyesi cha
nguruwe.
Kinyesi hicho kilipatikana katika
nyumba ya jirani ambako
walikuwa wanafuga nguruwe.
“Sasa nenda kaninunulie bangi
moja” Mganga akamuagiza tena
yule mtu.
Kutokana na kazi yangu ya upolisi,
“neno” bangi ninapolisikia huwa
nasisimkwa na mwili na akili
yangu inakwenda kwenye sheria.
Lakini muda ule nilitulia kimya
kama maji ya mtungi kama vile
bangi ilikuwa kitu cha kawaida
kwangu.
Hata hivyo nilikuwa nikijiuliza
bangi ilikuwa inatumikaje katika
uganga wakati kilikuwa kilevi
kisichokubalika ? Sikupata jibu la
swali hilo.
Yule mtu aliyetumwa bangi
hakuchelewa sana akarudi akiwa
na bangi yake mkononi. Nikahisi
kwamba bangi ilikuwa ikiuzwa
sana pale kijijini.
Nikakumbuka zamani nilishuhudia
kesi ya mvuta bangi mmoja
aliyedai kuwa akivuta bangi huwa
anapata nguvu ya kulima.
Nikajiambia huenda zilitumika
pale kijijini kwa sababu hiyo.
Ile bangi ilipoletwa ilichanganywa
na vile vitu vingine vilivyoletwa
kwanza, yaani ule mchanga wa
kaburini na kile kinyesi cha
nguruwe.
Baada ya vitu hivyo
kuchanganywa vilitiwa kwenye
chungu na kuwekwa kwenye jiko.
Baada ya sekunde chache vilianza
kuungua na kutoa moshi. Yule
mganga alikuwa ameshika mwiko
akivigeuza huku na huku.
Vilikuwa vikitoa harufu mbaya
iliyokuwa inaumiza kichwa. Mama
yangu alipiga chafya mara mbili.
“Kama unasikia vibaya toka nje”
Mganga huyo akamwambia mama.
Mama akatoka nje. Mganga
aliendelea kuvichoma vile vitu
mpaka vikaungua na kuwa vyeusi.
Aliepua kile chungu na kukiweka
kando ya jiko.
ITAENDELEA
 
SIMULIZI : YALIYONIKUTA TANGA
MSIMULIAJI : MARTIN MEKU
MAHALI : TANGA
SEHEMU YA 22

ILIPOISHIA

Hata hivyo nilikuwa nikijiuliza
bangi ilikuwa inatumikaje katika
uganga wakati kilikuwa kilevi
kisichokubalika ? Sikupata jibu la swali hilo.
Yule mtu aliyetumwa bangi
hakuchelewa sana akarudi akiwa
na bangi yake mkononi. Nikahisi
kwamba bangi ilikuwa ikiuzwa
sana pale kijijini. Nikakumbuka zamani
nilishuhudia
kesi ya mvuta bangi mmoja
aliyedai kuwa akivuta bangi huwa
anapata nguvu ya kulima.
Nikajiambia huenda zilitumika
pale kijijini kwa sababu hiyo. Ile bangi
ilipoletwa ilichanganywa
na vile vitu vingine vilivyoletwa
kwanza, yaani ule mchanga wa
kaburini na kile kinyesi cha
nguruwe.
Baada ya vitu hivyo kuchanganywa vilitiwa
kwenye chungu na
kuwekwa kwenye jiko. Baada ya
sekunde chache vilianza kuungua
na kutoa moshi. Yule mganga
alikuwa ameshika mwiko
akivigeuza huku na huku. Vilikuwa vikitoa
harufu mbaya
iliyokuwa inaumiza kichwa. Mama
yangu alipiga chafya mara mbili.
“Kama unasikia vibaya toka nje”
Mganga huyo akamwambia mama.
Mama akatoka nje. Mganga aliendelea
kuvichoma vile vitu
mpaka vikaungua na kuwa vyeusi.
Aliepua kile chungu na kukiweka
kando ya jiko.
SASA ENDELEA
Alisubiri chungu hicho kilipopoa akaanza
kuvisaga vile vitu
alivyokuwa amevichoma kwa
kutumia aina fulani ya jiwe
lililokuwa na rangi ya kahawia.
Vitu hivyo vilisagwa na kuwa unga
unga mweusi ambao aliutoa kwenye
chungu hicho na kuutia
kwenye karatasi nyeupe. Akaanza
kuutabania maneno ya kiganga
huku akiugeuza geuza kwa kidole
chake.
Alipomaliza kuutabania aliuchota kidogo
akautia kwenye kile
kisanduku akauchnganya
changanya na yale mapambo ya
dhahabu. Ule unga uliobaki
aliufunga kwenye ile karatasi
akanipa. “Utakuwa unachota kisdogo na
kutia kwenye maji ya kuoga kama
ulivyofanya jana. Utaoga asubuhi
na jioni kwa siku saba” akaniambia.
Ili nipate uhakika wa alichoniagiza
nikamuuliza. “Umeniambia niioge hii dawa
kidogo dogo kwa siku saba asubuhi
na jioni?”
“Ndio. Usipitishe hata siku moja”
Nikabaki kumtazama yule mganga
wakati akiniambia hivyo. Sikumtazama kwa
sababu nilikuwa
namsikiliza. Nilimtazama kutokana
na mawazo yaliyokuwa yakipita
akilini mwangu.
Nilikuwa nikijiambia, yaani niende
nikaoge bangi na mavi ya nguruwe kwa
siku saba!
Uganga wa kienyeji unahusisha
mambo mengi machafu!
Licha ya kuona kinyaa, niliona
sikuwa na budi kutekeleza vile
nilivyoambiwa ili kusalimisha maisha yangu
na pia nipate zile
dhahabu ambazo nazo zilitiwa ile
dawa.
“Ukioga dawa hiyo shetani
hatakufuata hata siku moja.
Atakupitia mbali sana na hizo dhahabu
hatazitaka tena kwa
sababu zimeshanajisika na wewe
mwenyewe pia unapata najisi
ukioga dawa hiyo” Mganga
aliniambia.
“Hata zikipita hizo siku saba hao majini
hawatanifuata?”
nikamuuliza ili nipate ufafanuzi.
“Ukishaioga kwa siku saba,
inakuwa ni basi. Hawatakufuata
tena”
“Sawa, nimekuelewa” Kule kwetu ni mwiko
kwa mganga
kukwambia nataka kiasi fulani cha
pesa isipokuwa mteja mwenyewe
ndio unamkadiria kutokana na kazi
aliyokufanyia.
Nilitoa shilingi elfu ishirini nikampa.
Akatuambia kwamba tunaweza
kwenda zetu.
Tukaondoka.
Tuliporudi nyumbani nilikitia kile
kisanduku kwenye begi langu kisha
nikampa mama begi hilo ili alihifadhi
chumbani kwake.
Nikaanza kutumia ile dawa. Kila
siku nikawa ninaioga mara mbili
asubuhi na jioni. Mpaka siku saba
zikaisha. Nikakaa kwa mwezi
mzima, sikuona tatizo lolote. Nikaamini
kwamba ile dawa
ilikuwa inafanya kazi.
Udadisi ukanifanya nipige simu
kwa mpelelezi mwenzangu
aliyekuwa Tanga ili anieleze hali
ilivyo. “Tuko shwari tu” akaniambia.
“Vipi kuhusu wale majini wa
barabara nane, polisi bado
wanawafuatilia? ’
“Ule upelelezi ulishaachwa waka
hakuna afisa yeyote anayehoji kuhusu kesi
ile”
“Huenda wameingia uoga”
“Sio huenda, wameingia uoga
kweli”
Baada ya kuelezwa hivyo na
kupata picha kamili ya hali iliyokuwa huko
Tanga nikapata
matumaini kuwa yale matatizo
yalikuwa yamekwisha na kwamba
ningefaidi zile dhahabu.
Siku moja mama yangu alinifuata
chumbani na kuniambia kuwa kuna
msichana ambaye alitaka nimuoe
ili niende naye Tanga. Nikataka
kumjua huyo msichana.
“Nitatuma mtu jioni amuite,
utakuja kumuona” Mama
aliniambia. “Sawa”
ILipofika jioni mama akaja
chumbani mwangu akiwa na
msichana mmoja mzuri wa kihaya.
Akaniambia kwa kinyumbani.
“Nimekuletea mchumba mwanangu”
“Ndiye huyu?” nikamuuliza nikiwa
nimemtumbulia macho.
“Ndiye yeye niliyekwambia
asubuhi, ni msichana mpole sana
na ana tabia nzuri anafaa kuwa mke wako”
Msichana akanipigia goti kisha
akanisalimia. Nikafurahi kupewa
heshima za kinyumbani. Baada ya
kusalimiana naye nilimwambia
aketi kwenye kiti, akakaa. “Unaitwa nani?”
nikamuuliza.
“Naitwa Mage”
“Haya zungumzeni, mimi niko hapa
ukumbini” Mama akaniambia na
kutoka mle chumbani.
“Unaishi na wazazi wako?” nikamuuliza.
“Ndiyo naishi na wazazi wangu”
“Umesoma hadi darasa la ngapi”
“Nimekomea kidato cha nne”
“Mwaka gani?”
“Mwaka juzi” “Mama yangu amekupenda,
kwa
hiyo uko tayari tufunge uchumba?”
“Kama na wewe umenipenda”
“Kusema ukweli alichokipenda
mama yangu na mimi nitakipenda
tu” “Wewe unafanya kazi gani?”
“Mimi ni polisi upande wa
upelelezi”
“Unafanya kazi mkoa gani”
“Kwa sasa nimehamishiwa Tanga”
“Kwa hiyo ukishanioa tutakwenda kuishi
Tanga?”
“Ndiyo”
“Sawa. Sasa uje ujitokeze kwa
wazazi wangu”
“Nitafanya hivyo katika siku chache
zijazo” Baada ya kuzungumza na Mage,
msichana niliyechaguliwa na mama
yangu na ambaye mimi
mwenyewe pia nilimpenda
nilimuita mama nikamwambia
kuwa nimeshazungumza naye.
“Mmeshakubalian a”
“Ndiyo, tumekubaliana”
“Basi ngoja nimsindikize arudi
kwao”
Mama akatoka na yule msichana.
Je nini kitaendelea? Usikose kuendelea na
hadithi hii
 
SIMULIZI : YALIYONIKUTA TANGA
MSIMULIAJI : MARTIN MEKU
MAHALI : TANGA
SEHEMU YA 23

ILIPOISHIA

“Mimi ni polisi upande wa
upelelezi”
“Unafanya kazi mkoa gani”
“Kwa sasa nimehamishiwa Tanga”
“Kwa hiyo ukishanioa tutakwenda
kuishi Tanga?”
“Ndiyo”
“Sawa. Sasa uje ujitokeze kwa
wazazi wangu”
“Nitafanya hivyo katika siku chache
zijazo”
Baada ya kuzungumza na Mage,
msichana niliyechaguliwa na mama
yangu na ambaye mimi
mwenyewe pia nilimpenda
nilimuita mama nikamwambia
kuwa nimeshazungumza naye.
“Mmeshakubalian a”
“Ndiyo, tumekubaliana”
“Basi ngoja nimsindikize arudi
kwao”
Mama akatoka na yule msichana.
SASA ENDELEA
Aliporudi aliniuliza kama
nimempenda yule msichana.
“Nimempenda” nikamjibu.
“Sasa una mawazo gani ya
kumuoa?”
“Nilikuwa sijapanga kuoa kwa
sasa…”
“Nimekuonesha yule msichana ili
kukutia mawazo ya kuoa.
Umeshafikia umri wa kuwa na
mke”
“Ni kweli, kwa hiyo mama
unanishauri nimuoe yule msichana”
“Tena tuwaozeshe haraka
iwezekanavyo, ukimaliza likizo
yako uondoke na mke wako”
“Itawezekana mama?”
“Kwanini isiwezekane. Harusi za
vijijini usizifananishe na harusi za
mijini”
“Sasa la muhimu ni kupeleke barua
ya uchumba kwa wazazi wake
tusikie watatujibu nini”
“Kama msichana mwenyewe
amekubali na wazazi wake
watakubali tu. Hilo halina tatizo.
Niliandika barua ya uchumba siku
ile ile baada ya mama kunitia
mawazo ya kuoa. Barua ilipelekwa
na siku ya pili yake majibu
yakarudishwa.
Nilifurahi kwa kukubaliwa
uchumba wangu na Mage.
Nilitajiwa mahari iliyokuwa
inatakiwa pamoja na ada
nyinginezo kwa mujibu wa mila
zetu.
Siku ile tulikaa kikao cha ndugu
tukaijadili ile barua na kukubaliana
na kila kilichoandikwa. Baada ya
siku tatu nilipeleka mahari pamoja
na ada zote.Tukatakiwa tutoe siku
ya kwenda kuoa.
Tulikaa tena kikao cha ndugu
tukapanga siku ya kwenda kuoa.
Tulipokubaliana juu ya siku hiyo
tukatoa taarifa upande wa pili.
Mipango ya harusi ikafanyika kwa
pande zote mbili na siku ilipowadia
nikaoana na Mage.
Nilikaa na Mage nyumbani kwetu
kwa wiki mbili tu kabla ya
kuondoka kurudi Tanga, kwani
likizo yangu ilikuwa ikikaribia
kwisha.
Nilipoondoka nilikichukua kile
kisanduku changu cha dhahabu na
kuondoka nacho. Nilipofika Tanga
nilimtambulisha mke wangu kwa
polisi wenzangu tuliokuwa tunakaa
kambini.
Polisi wenzangu walitupongeza
kwa uamuzi wetu wa kufunga
ndoa lakini pia walinilaumu kwa
kutowaarifu kuwa ninaoa.
Siku mbili baada ya kufika, Tanga
nilitoa mkufu wa dhahabu, bangili
mbili na vipuli na kumpa mke
wangu avae.
Usiku wa siku ile nilikwenda
kutembea mjini na mke wangu ili
kumuonesha mji. Tulirudi
nyumbani karibu saa sita usiku.
Tukafikia kulala.
Usiku ule ulikuwa balaa!
Hatukulala. Mke wangu alikuwa
akipiga kelele usiku kucha akidai
kuwa kila alipofumba macho
alikuwa akiona msichana anampiga
bakora akimwambia avue zile
dhahabu alizovaa.
Mwisho wake ilibidi mke wangu
atii na kavua zile dhahabu
nilizokuwa nimempa na hapo
ndipo alipopata usingizi.
Kulipokucha asubuhi nilikichukua
kile kisanduku nikakitia kwenye
begi na kumpa polisi aliyekuwa
jirani yangu.
“Tafadhali nihifadhie hili begi langu
nitalichukua kesho” nikamwambia.
Kwa vile yule polisi alikuwa rafiki
yangu akalichukua begi hilo na
kunihifadhia chumbani kwake.
Nikaenda zangu kazini.
Niliporudi kutoka kazini mke
wangu akaniuliza maswali mengi
kuhusu zile dhahabu nilizokuwa
nimempa ambazo zilikuwa
zimemtia wasiwasi mkubwa.
Nikamdanganya kwamba dhahabu
hizo nilizinunua kwa sonara na
kwamba nilishazirudish a.
“Sasa kwanini nilikuwa naota ile
ndoto ya kuchapwa?” akaniuliza.
“Sijajua lakini nimemueleza sonara
huyo ameniambia alikosea
akaniuzia dhahabu za majini lakini
kwa vile nimezirudisha
hakutakuwa na tatizo.”
Nikaendelea kumdanganya ili
kumtoa wasiwasi.
ITAENDELEA
 
SIMULIZI : YALIYONIKUTA TANGA
MSIMULIAJI : MARTIN MEKU
MAHALI : TANGA
SEHEMU YA 24

ILIPOISHIA

Usiku ule ulikuwa balaa!
Hatukulala. Mke wangu alikuwa
akipiga kelele usiku kucha akidai kuwa kila
alipofumba macho
alikuwa akiona msichana anampiga
bakora akimwambia avue zile
dhahabu alizovaa.
Mwisho wake ilibidi mke wangu
atii na kavua zile dhahabu nilizokuwa
nimempa na hapo
ndipo alipopata usingizi.
Kulipokucha asubuhi nilikichukua
kile kisanduku nikakitia kwenye
begi na kumpa polisi aliyekuwa
jirani yangu. “Tafadhali nihifadhie hili begi
langu
nitalichukua kesho” nikamwambia.
Kwa vile yule polisi alikuwa rafiki
yangu akalichukua begi hilo na
kunihifadhia chumbani kwake.
Nikaenda zangu kazini. Niliporudi kutoka
kazini mke
wangu akaniuliza maswali mengi
kuhusu zile dhahabu nilizokuwa
nimempa ambazo zilikuwa
zimemtia wasiwasi mkubwa.
Nikamdanganya kwamba dhahabu hizo
nilizinunua kwa sonara na
kwamba nilishazirudish a.
“Sasa kwanini nilikuwa naota ile
ndoto ya kuchapwa?” akaniuliza.
“Sijajua lakini nimemueleza sonara
huyo ameniambia alikosea akaniuzia
dhahabu za majini lakini
kwa vile nimezirudisha
hakutakuwa na tatizo.”
Nikaendelea kumdanganya ili
kumtoa wasiwasi.
SASA ENDELEA Nilidhani kwa kuhamisha kile
kisanduku kwa mwenzangu ndio
ningemaliza yale matatizo ya
majini lakini nilikuwa
nimejidanganya.
Yapata saa nane usiku wakati nimelala, yule
polisi niliyempa lile
begi lenye kisanduku anihifadhie
alinibishia mlango.
Nilipofungua mlango nilimuona
amesimama mbele ya mlango
akiwa na lile begi mkononi. “Chukua hili
begi lako, linaniletea
miujiza chumbani kwangu”
akaniambia huku uso wake ukiwa
umetaharuki.
“Miujiza gani tena?”
“Kuna joka linatoka ndani ya hili begi halafu
linazunguka chumbani
kwangu”
Nikajifanya nashangaa.
“Joka?”
“Ndio joka. Tena joka kubwa sana.
Linazunguka chummbani kisha linarudi
kwenye hili begi linapotea”
“Mh! Unanieleza habari ya ajabu
sana”
“Kwani umeweka nini humu ndani”
“Sijui kilichomo humo ndani. Hilo
begi alilisahau mtu mmoja aliyekuja hapa
nyumba kuomba
maji ya kunywa” nikamdanganya.
“Mh! Basi lichukue. Siwezi kuliweka
kwangu”
Nikalichukua lile begi. Yule polisi
akarudi nyumbani kwake. Na mimi
nikapatwa na kizungumkuti.
Nilikuwa sijui nikaliweke wapi. Yale
maelezo ya polisi mwenzangu
yalinitisha.
Nilipoona nimekosa pa kuliweka
nililiweka chini ya meza pale sebuleni.
Nikafunga mlango wa
chumbani ili kama kuna joka
linalotoka lisiingie chumbani
mwetu.
Wakati ule mke wangu alikuwa
amelala. Hakuwa akijua kilichokuwa
kinaendelea.
Nilishukuru kwa hilo. Laiti
angekuwa macho akasikia yale
niliyokuwa nikiyazungumza na
yule polisi, ingekuwa taabu.
Wakati nimejilaza kitandani nikiwaza,
nilijiambia kuwa ule
uganga niliofanyiwa na yule
mganga wa kijijini kwetu haukufaa
kitu, sasa vituko vilikuwa vinanijia
nyumbani kiasi kwamba mimi
mwenyewe nilikuwa nimeshapata uoga na
nilikuwa sijui la kufanya.
Nikajiambia tamaa yangu ya
kumiliki zile dhahabu sasa
inaniponza.
Wakati niko kwenye lindi la
mawazo nikapitiwa na usingizi ghafla,
nikaota nimeamka saa kumi
na mbili asubuhi, nikatoka na lile
begi na kwenda kule magomeni
kwenye yale mkaburi. Nilipofika
nikakitoa kile kisanduku na
kukiweka juu ya kaburi mojawapo. Hapo
hapo nikaona kinatitia chini
na kupotea kabisa.
Baada ya hapo nilizinduka
usingizini nikatazama saa na kuona
ilikuwa saa kumi na mbili
kasorobo, nikavaa nguo na kutoka
chumbani. Nilikwenda kuosha uso
na kusukutua maji. Nikalichukua
lile begi na kutoka nalo bila hata
kumuaga mke wangu.
Nilikwenda kupanda daladala
nikaenda Magomeni. Nilifika kule
makaburini nikakitoa kile
kisanduku na kukiweka juu ya
kaburi kama vile nilivyoota usiku.
Hapo hapo nikaona kile kisanduku
kinazama chini.
Kilizama hadi kikapotea kabisa. Nilitishika
sana lakini kwa vile tukio
lenyewe nilishaliota nilijikaza.
Kile kisanduku kilipopotea, nikajua
kimerudi kwa wenyewe.
Nikaondoka na kurudi nyumbani.
Nilipofika nilimkuta mke wangu bado
amelala. Nikaenda kuoga.
Wakati narudi kutoka kuoga
nikamkuta ameshaamka.
Sikumwambia chochote.
Baada ya siku ile sikuona tena vile
vituko vya majini. Tukio hilo licha ya kunitesa
lilinipa fundisho
ambalo sitalisahau. Nikawa polisi
muadilifu sana niliyefanya kazi
yangu kwa misingi ya haki na
sheria na sio kama nilivyokuwa
hapo mwanzo. Hayo ndiyo yaliyonikuta
tanga’
usiache kunitumia maoni yako
 
Hehehe sasa maoni tunakutumia wewe kizeze au?


Ila kwa vyovyote vile huyu mwandishi nitakuwa namfahamu/ananifahamu sana. Umeitoa wapi hii hadithi?
 
SIMULIZI : YALIYONIKUTA TANGA
MSIMULIAJI : MARTIN MEKU
MAHALI : TANGA
SEHEMU YA 24

ILIPOISHIA

Usiku ule ulikuwa balaa!
Hatukulala. Mke wangu alikuwa
akipiga kelele usiku kucha akidai kuwa kila
alipofumba macho
alikuwa akiona msichana anampiga
bakora akimwambia avue zile
dhahabu alizovaa.
Mwisho wake ilibidi mke wangu
atii na kavua zile dhahabu nilizokuwa
nimempa na hapo
ndipo alipopata usingizi.
Kulipokucha asubuhi nilikichukua
kile kisanduku nikakitia kwenye
begi na kumpa polisi aliyekuwa
jirani yangu. “Tafadhali nihifadhie hili begi
langu
nitalichukua kesho” nikamwambia.
Kwa vile yule polisi alikuwa rafiki
yangu akalichukua begi hilo na
kunihifadhia chumbani kwake.
Nikaenda zangu kazini. Niliporudi kutoka
kazini mke
wangu akaniuliza maswali mengi
kuhusu zile dhahabu nilizokuwa
nimempa ambazo zilikuwa
zimemtia wasiwasi mkubwa.
Nikamdanganya kwamba dhahabu hizo
nilizinunua kwa sonara na
kwamba nilishazirudish a.
“Sasa kwanini nilikuwa naota ile
ndoto ya kuchapwa?” akaniuliza.
“Sijajua lakini nimemueleza sonara
huyo ameniambia alikosea akaniuzia
dhahabu za majini lakini
kwa vile nimezirudisha
hakutakuwa na tatizo.”
Nikaendelea kumdanganya ili
kumtoa wasiwasi.
SASA ENDELEA Nilidhani kwa kuhamisha kile
kisanduku kwa mwenzangu ndio
ningemaliza yale matatizo ya
majini lakini nilikuwa
nimejidanganya.
Yapata saa nane usiku wakati nimelala, yule
polisi niliyempa lile
begi lenye kisanduku anihifadhie
alinibishia mlango.
Nilipofungua mlango nilimuona
amesimama mbele ya mlango
akiwa na lile begi mkononi. “Chukua hili
begi lako, linaniletea
miujiza chumbani kwangu”
akaniambia huku uso wake ukiwa
umetaharuki.
“Miujiza gani tena?”
“Kuna joka linatoka ndani ya hili begi halafu
linazunguka chumbani
kwangu”
Nikajifanya nashangaa.
“Joka?”
“Ndio joka. Tena joka kubwa sana.
Linazunguka chummbani kisha linarudi
kwenye hili begi linapotea”
“Mh! Unanieleza habari ya ajabu
sana”
“Kwani umeweka nini humu ndani”
“Sijui kilichomo humo ndani. Hilo
begi alilisahau mtu mmoja aliyekuja hapa
nyumba kuomba
maji ya kunywa” nikamdanganya.
“Mh! Basi lichukue. Siwezi kuliweka
kwangu”
Nikalichukua lile begi. Yule polisi
akarudi nyumbani kwake. Na mimi
nikapatwa na kizungumkuti.
Nilikuwa sijui nikaliweke wapi. Yale
maelezo ya polisi mwenzangu
yalinitisha.
Nilipoona nimekosa pa kuliweka
nililiweka chini ya meza pale sebuleni.
Nikafunga mlango wa
chumbani ili kama kuna joka
linalotoka lisiingie chumbani
mwetu.
Wakati ule mke wangu alikuwa
amelala. Hakuwa akijua kilichokuwa
kinaendelea.
Nilishukuru kwa hilo. Laiti
angekuwa macho akasikia yale
niliyokuwa nikiyazungumza na
yule polisi, ingekuwa taabu.
Wakati nimejilaza kitandani nikiwaza,
nilijiambia kuwa ule
uganga niliofanyiwa na yule
mganga wa kijijini kwetu haukufaa
kitu, sasa vituko vilikuwa vinanijia
nyumbani kiasi kwamba mimi
mwenyewe nilikuwa nimeshapata uoga na
nilikuwa sijui la kufanya.
Nikajiambia tamaa yangu ya
kumiliki zile dhahabu sasa
inaniponza.
Wakati niko kwenye lindi la
mawazo nikapitiwa na usingizi ghafla,
nikaota nimeamka saa kumi
na mbili asubuhi, nikatoka na lile
begi na kwenda kule magomeni
kwenye yale mkaburi. Nilipofika
nikakitoa kile kisanduku na
kukiweka juu ya kaburi mojawapo. Hapo
hapo nikaona kinatitia chini
na kupotea kabisa.
Baada ya hapo nilizinduka
usingizini nikatazama saa na kuona
ilikuwa saa kumi na mbili
kasorobo, nikavaa nguo na kutoka
chumbani. Nilikwenda kuosha uso
na kusukutua maji. Nikalichukua
lile begi na kutoka nalo bila hata
kumuaga mke wangu.
Nilikwenda kupanda daladala
nikaenda Magomeni. Nilifika kule
makaburini nikakitoa kile
kisanduku na kukiweka juu ya
kaburi kama vile nilivyoota usiku.
Hapo hapo nikaona kile kisanduku
kinazama chini.
Kilizama hadi kikapotea kabisa. Nilitishika
sana lakini kwa vile tukio
lenyewe nilishaliota nilijikaza.
Kile kisanduku kilipopotea, nikajua
kimerudi kwa wenyewe.
Nikaondoka na kurudi nyumbani.
Nilipofika nilimkuta mke wangu bado
amelala. Nikaenda kuoga.
Wakati narudi kutoka kuoga
nikamkuta ameshaamka.
Sikumwambia chochote.
Baada ya siku ile sikuona tena vile
vituko vya majini. Tukio hilo licha ya kunitesa
lilinipa fundisho
ambalo sitalisahau. Nikawa polisi
muadilifu sana niliyefanya kazi
yangu kwa misingi ya haki na
sheria na sio kama nilivyokuwa
hapo mwanzo. Hayo ndiyo yaliyonikuta
tanga’
usiache kunitumia maoni yako


hongera sana.
 
Back
Top Bottom