Simulizi ya kusisimua

Simulizi ya kusisimua

Ivyo ndivyo sisi wazee tunahadithiana adithi njoo kizee chenzangu nakungoja apa barabaran
Kizee chenzangu nimeahirisha mama. Ntakuja kesho. Kwa sasa ishia tu hapo ulipokewishasoma. Palipobaki ntakumalizia kesho. Si unajua sisi wazee kutembea usiku siyo wa eeegh? Mwambie mjukuu akurudishe nyjmbani tu!
 
Dah hii stori hii, inanikumbusha kitu, ila kama hii ni simulizi tuu, sawa ila haya mambo yapo na wengine yashatukuta japo c kwa dhulma, ila huyu polisi safar hii aliingia cha kike, am waiting
Nawe tupe kisa chako
 
Nawe tupe kisa chako
Mimi niliwahi kupotea ndugu, wakati nipo darasa la tano, kisa ka mbwa, kuna ka mbwa kalipita mitaa ya home, enzi hizo tulikuwa tunafuga mbwa kama watano, wale mbwa wetu walikuwa na wakali sana, brother alikuwa anawachanganyia bangi na gongo ktk msosi wao, sasa hiyo cku cjui kalikotokea nilipomuona nikaanza mkimbia alikuwa kakonda sana, nikapanda juu ya mpera, sasa wale mbwa wetu c wakamuona wakawa wanabweka sana, kiasi walivunja mlango wa banda wakaanza mkimbizayule mbwa, sasa mimi kuona huu msala ikanibidi nianze kuwafuatilia wale mbwa wetu kila nilipokuwa nawaita ndivyo walivyokuwa wakitokomea porini, nakumbuka ilikuwa saa tatu asubui niliwafuatilia huku na mimi nawakimbiza maana wale mbwa wetu walikuwa wakorofi sana, nikajua nikiwaacha watauma watu, hivyo nia yangu ilikuwa niwarudishe home, haikuwa hivyo, nilipotelea msituni na nilikuja pata ufumbuzi wa kutoka huko baada ya siku tatu, niliona mengi ya kuogofya ila Naamini mungu tu aliamua kunilinda, sitokuja niisahau hii...hakuwa mbwa yule, nikuja kujua huko porini baada ya kumuona akichange....aaagh ndo hivyo....
 
Mimi niliwahi kupotea ndugu, wakati nipo darasa la tano, kisa ka mbwa, kuna ka mbwa kalipita mitaa ya home, enzi hizo tulikuwa tunafuga mbwa kama watano, wale mbwa wetu walikuwa na wakali sana, brother alikuwa anawachanganyia bangi na gongo ktk msosi wao, sasa hiyo cku cjui kalikotokea nilipomuona nikaanza mkimbia alikuwa kakonda sana, nikapanda juu ya mpera, sasa wale mbwa wetu c wakamuona wakawa wanabweka sana, kiasi walivunja mlango wa banda wakaanza mkimbizayule mbwa, sasa mimi kuona huu msala ikanibidi nianze kuwafuatilia wale mbwa wetu kila nilipokuwa nawaita ndivyo walivyokuwa wakitokomea porini, nakumbuka ilikuwa saa tatu asubui niliwafuatilia huku na mimi nawakimbiza maana wale mbwa wetu walikuwa wakorofi sana, nikajua nikiwaacha watauma watu, hivyo nia yangu ilikuwa niwarudishe home, haikuwa hivyo, nilipotelea msituni na nilikuja pata ufumbuzi wa kutoka huko baada ya siku tatu, niliona mengi ya kuogofya ila Naamini mungu tu aliamua kunilinda, sitokuja niisahau hii...hakuwa mbwa yule, nikuja kujua huko porini baada ya kumuona akichange....aaagh ndo hivyo....
Mbona umekatisha alivo change akawaje? Na uliishi vipi siku tatu na pia ulitokaje huko polini
 
Mimi niliwahi kupotea ndugu, wakati nipo darasa la tano, kisa ka mbwa, kuna ka mbwa kalipita mitaa ya home, enzi hizo tulikuwa tunafuga mbwa kama watano, wale mbwa wetu walikuwa na wakali sana, brother alikuwa anawachanganyia bangi na gongo ktk msosi wao, sasa hiyo cku cjui kalikotokea nilipomuona nikaanza mkimbia alikuwa kakonda sana, nikapanda juu ya mpera, sasa wale mbwa wetu c wakamuona wakawa wanabweka sana, kiasi walivunja mlango wa banda wakaanza mkimbizayule mbwa, sasa mimi kuona huu msala ikanibidi nianze kuwafuatilia wale mbwa wetu kila nilipokuwa nawaita ndivyo walivyokuwa wakitokomea porini, nakumbuka ilikuwa saa tatu asubui niliwafuatilia huku na mimi nawakimbiza maana wale mbwa wetu walikuwa wakorofi sana, nikajua nikiwaacha watauma watu, hivyo nia yangu ilikuwa niwarudishe home, haikuwa hivyo, nilipotelea msituni na nilikuja pata ufumbuzi wa kutoka huko baada ya siku tatu, niliona mengi ya kuogofya ila Naamini mungu tu aliamua kunilinda, sitokuja niisahau hii...hakuwa mbwa yule, nikuja kujua huko porini baada ya kumuona akichange....aaagh ndo hivyo....
Mbona juu juu mkuu, embu tiririka tory kamili tujue.ujue duniani kuna vitu vya ajabu sana.wakati mwingine anasimulia kama story tu ya kuburudisha, kuna mwingine kayapitia kabisaa.
 
Mbona juu juu mkuu, embu tiririka tory kamili tujue.ujue duniani kuna vitu vya ajabu sana.wakati mwingine anasimulia kama story tu ya kuburudisha, kuna mwingine kayapitia kabisaa.
YinshaAllah kesho, ntahadithia ilikuwaje kwa saa hizi siwezi kidogo nna kazi za watu nnazimalizia, ila ni kweli haya mambo yanawakuta wengi tuu, na kuna wakati unapohadithia unahisi kuna mzigo flani umeutua moyoni..naamininwapo watu wengi tuu wanapotea katika mazingira kama haya..ni wengi na yapo yanatokea..kesho inshaAllah nitaweka kisa kilichinikuta huko na vipi nilisalimika kurudi kwa uwezo wa Mungu maana sikuwa na ujanja wala mbinu yoyote ya kunifanya nirudi salama nyumbani zaidi ya miujiza tu ya mungu,,,ila nakumbuka kila kitu mpaka hii leo.
 
SIMULIZI : YALIYONIKUTA TANGA
MSIMULIAJI : MARTIN MEKU
MAHALI : TANGA
SEHEMU YA 16

ILIPOISHIA

Wakati naamka nilisikia sauti ya
mwanamke ikiniambia.
“Bado wewe sasa!”
Nikazinduka na kutazama huku na
huku. Sikuona kitu. Moyo ulikuwa
ukinienda mbio na mwili ulikuwa
umenitota jasho.
Sikutaka kulala tena, nikatazama
saa na kuona ilikuwa saa kumi na
moja jioni. Nikaenda tena kuoga.
Nilipotoka bafuni nilivaa nikatoka
kwenda kutafuta chakula. Siku zote
huwa nakula kwenye mikahawa
kwa sababu sikuwa na mke.
Wakati nakula kwenye mkahawa
mmoja jirani na stendi ya mabasi
niliwaza ile ndoto niliyokuwa
nimeota. Mwili wangu ulinisisimka
nilipoona ile picha ya upanga
ukikereza kwenye shingo ya Erick
kama msumeno.
Nikajiuliza ni kwanini nimeota
ndoto ile? Au wale majini
waliniotesha kunionesha jinsi
mwenzangu alivyochinjwa?
Hapo hapo ile sauti iliyosikika
ikiniambia “Bado wewe!” ilinijia
akilini mwangu.
Nikahisi kama lilikuwa onyo la
kunijulisha kwamba na mimi siko
salama.
SASA ENDELEA
Kwa sababu ya hofu nilitamani
niende nikairipiti ile ndoto kwa
maafande wangu ili lolote
litakalonitokea wajue limetokana
na majini hao, lakini niliona
ningeonekana mzembe
ninayehofishwa na ndoto niliyoota
mwenyewe.
kulikuwa na kitu kingine
kilichonifanya nisite kusema
ukweli. Ni kile kitendo cha
kidhalimu ambachoo mimi na
marehemu Erick tuliwafanyia yule
mwanamke na binti yake, cha
kuwabambikia kesi na kumkamata
yule mwanamke bila kujua kuwa
alikuwa ni jini.
Kitendo kile ndicho
kilichosababisha balaa lote na kwa
muda ule kuyaweka rehani maisha
yangu. Lakini mbali na kitendo
hicho, pia ule wizi nilioufanya wa
kukichukua kile kisanduku cha
dhahabu na kukihamishia
nyumbani kwangu, uliwaudhi wale
majini.
Nisingeweza kuusema uovu huo
tulioufanya kwa sababu pia
ungeniweka mahali pabaya kikazi
kwani ningeweza kufukuzwa kazi
ambayo ilikuwa ndio tegemeo la
maisha yangu.
Nilikuwa nimepanga
nitakapokwenda likizo nikichukue
kile kisanduku kwani ile dhahabu
iliyokuwemo ilikuwa na thamani
kubwa na ingetosha kunipa utajiri.
Baada ya kumaliza kula sikuwa na
mahali pengine pa kwenda. Lakini
kama si lile tukio ambalo lilikuwa
limefadhaisha akili yangu
ningekuwa na sehemu nyingi za
starehe ambazo ningeweza
kwenda kupoteza wakati.
Nikaona nirudi kituoni ingawa
niliambiwa nipumzike hadi saa sita
usiku. Nilipofika kituoni nilikaa hadi
saa sita usiku ambapo baadhi ya
maafisa wetu walifika na kuandaa
kikosi cha kwenda nyumbani kwa
yule mwanamke itakapofika saa
nane usiku.
Muda huo ulipofika, polisi sita
tulipanda kwenye gari. Polisi
wawili walipewa bunduki.
Tulilisimamisha gari nyumba ya
tatu kutoka nyumba ile ya
watuhumiwa wetu.
Afande wangu Meja Elias aliniambia
nishuke peke yangu niende
nikajaribu kubisha mlango wa ile
nyumba nione kama kuna watu au
sauti zozote zinazosikika.
Nikashuka na kwenda kwenye
mlango wa nyumba hiyo.
Ingawa nilibisha mlango, nyumba
ilikuwa kimya na hakukuwa na
sauti yoyote iliyosikika kwa ndani.
Nikarudi kuwambia wenzangu
kuwa nyumba ilikuwa kimya.
“Nadhani hawajakuja” nikawambia.
“Basi tukae tusubiri hapa hapa”
Meja Elias akasema.
Tulitarajia kuwa muda si mrefu
tutawaona watu hao wakiwasili.
Tulisubiri kwa muda mrefu.
Tulikuwa tunazungumza, mwisho
maneno yalituishia tukawa kimya.
Muda si mrefu Meja Elias
akatuambia.
“Mimi nasinzia, wakitokea
mtaniamsha”
Baada ya dakika tano hivi
nikamuona askari mwingine
akisinzia na kugemea siti ya gari.
Haukupita muda na mimi nikaanza
kusikia usingizi. Baada ya hapo
sikujijua tena. Mpaka nafumbua
macho kulikuwa asubuhi
kumekucha! Tulilala hapo hapo.
Wakati naamka wenzangu wote
walikuwa wamelala. Nikaanza
kuwaamsha.
“Vipi jamani, mbona tumejisahau?”
nikawauliza.
Wengine walikuwa wakitoka ute.
Kila aliyezinduka macho yalikuwa
mekundu kuonesha alikuwa katika
usingizi mzito.
“Vipi?” Meja Elias aliuliza kwa
kubabaika.
“Mbona tumelala hadi asubuhi?”
nikauliza.
“Kwani kuna nini?” Askari mmoja
akauliza.
“Si tulikuja hapa kuwatega watu
wa nyumba ile…” nikawambia.
Hapo ndipo walipozinduka.
“Kweli tumejisahau, kumbe sote
tulilala?” Meja Elias akauliza.
“Naona tumelala sote” nikasema.
“Si bure iko namna”
“Mimi pia nimefikiria hivyo hivyo”
nikakubaliana naye.
“Itabidi turudi kituoni, kama
walikuja wameshaondoka” Meja
Elias akasema.
“Lakini afande si vibaya kama
tutakwenda kuwauliza wale
majirani” nikamwambia.
“Tuwaulize nini?”
“Tuwaulize kama hizo sauti
wanazozisikia usiku zilisikika usiku
wa jana”
“Sawa. Ngoja twende tukawaulize”
Mimi na Meja Elias tukashuka
kwenye gari na kuelekea kwenye
ile nyumba. Meja alibisha mlango.
Mwanamke yuleyule wa jana yake
akatokea tena.
“Habari ya asubuhi?” Meja
akamsalimia.
“Nzuri, za kazi?” Mwanamke huyo
naye akatuuliza.
“Tunashukuru, si mbaya”
“Ndiyo”
“Nadhani umetukumbuka?’
“Ndiyo, nawakumbuka”
“Tumekuja kuuliza tena kama zile
sauti zilisikika tena jana usiku”
“Tena jana ndio kulikuwa kama
kuna sherehe, watu walikuwa
wakiimba, wakicheka na wengine
wakila vyakula. Harufu ya pilau
tuliisikia hadi alfajiri”
“Hizo sauti mlianza kuzisikia kama
saa ngapi?”
“Muda ule ule wa saa nane, kama si
saa nane ni nane na nusu”
Meja akanitazama na kutikisa
kichwa kwa fadhaa. Nilikijua
alichokuwa anawaza. Muda ule
ndio tulioanza kulala.
“Kwani wana matatizo gani?”
Mwanamke huyo akamuuliza Meja.
“Tulikuwa tunataka kumjua
mwenye nyumba”
Je nini kitatokea? Usikose
 
SIMULIZI : YALIYONIKUTA TANGA
MSIMULIAJI : MARTIN MEKU
MAHALI : TANGA
SEHEMU YA 17

ILIPOISHIA

“Mwenye nyumba alikwishakufa”
Mwanamke huyo alituambia.
“Sawa. Nani anayemiliki kwa sasa?”
“Ndiyo haijulikani”
“Sasa hicho ndicho tunachotaka
kujua. Na hatuwezi kujua bila
kuwapata wahusika’
“Kama mngeweza kuja usiku
mwingi mnaweza kuwapata.
Mchana hawapo”
“Tutajaribu kufanya hivyo, Asante”
Meja akamuaga yule mwanamke,
tukaondoka na kurudi kwenye
gari.
Tulipofika kituoni tulianza kufanya
uchambuzi. Katika uchambuzi wetu
tulipata mashaka kuwa jinsi
tulivyolala fofofo usiku ule na
kuamka asubuhi ilitokana na hao
majini. Meja mwenyewe aliamini
kuwa majini hao ndio waliotutia
usingizi.
“Sasa leo tutakwenda kukaa
barazani kabisa. Gari la doria liwe
linatupitia mara kwa mara ili
tusilale” Meja akatuambia.
Tukapanga tena kukutana saa sita
usiku. Kwa upande wangu mawazo
yangu yalikuwa kwenye likizo
yangu. Siku zilikuwa zimeshawadia.
Nilibakisha siku moja tu nianze
likizo, nikaona niende kwa bosi
wangu, afisa upelelezi wa wilaya
nikamueleze suala hilo.
Nilipokwenda kwa afisa upelelezi
akaniambia nimuone afisa
upelelezi wa mkoa. Nikaenda
kwake. Baada ya kumueleza
kuhusu likizo yangu nilimuona
akiuma midomo yake.
SASA ENDELEA
”Itawezekanaje kwa sasa?”
akaniuliza lakini kama aliyekuwa
akijiuliza mwenyewe kisha
akaongeza.
“Subiri kidogo”
“Hadi lini?” nikamuuliza.
“Kwani ulitakiwa uanze lini likizo
yako?”
“Nilitakiwa kuanza kesho”
“Subiri hadi utakapoambiwa”
Afisa upelelezi wa mkoa aliponiona
nimenywea aliniambia.
“Si unajua kuna huu upelelezi wa
mauaji ya Sajenti Erick ambao
unakuhusu sana wewe”
“Sasa sijui upelelezi huu utaisha
lini. Nadhani utachukua muda
mrefu”
“Hauwezi kuchukua muda mrefu,
kuna mambo tu tunataka
tuyaelewe vizuri”
Afisa upelelezi akainua mkono wa
simu iliyokuwa juu ya meza yake
akampigia afisa upelelezi wa
wilaya.
“Hivi huu upelelezi wa mauaji ya
Sajenti Erick umefikia wapi?”
akamuuliza.
“Kuna timu ya polisi inaendelea na
uchunguzi, niliambiwa jana usiku
walikwenda kwenye nyumba ya
yule mwanamke aliyekufa
mahabusi pale barabara ya nane,
kuwavizia watu wanaofika hapo
wakati wa usiku lakini polisi wote
walipitiwa na usingizi hadi
asubuhi…” nikaisikia sauti ya afisa
upelelezi wa wilaya akimueleza ule
mkasa uliotutokea usiku uliopita.
Alimuelezea mwanzo hadi mwisho.
“Sasa leo wamepanga kwenda tena
lakini watakuwa barazani mwa ile
nyumba. Na gari letu la doria
litakuwa linawapitia mara kwa
mara” Afisa upelelezi aliendlea
kumueleza.
“Lakini wana uhakika kwamba hao
watu wanafika usiku?”
“Majirani waliwaeleza kuwa
wanafika kuanzia saa nane usiku.
Hata jana walipoamka asubuhi
waliuliza, wakaambiwa walifika”
“Martin anataka kwenda likizo
unadhani kuondoka kwake
kutaathiri uchunguzi huo?”
“Nafikiri hadi kesho ninaweza
kuwa na jibu”
“Sawa”
Afisa upelelezi wa mkoa akakata
simu.
“Basi wewe nenda, njoo uniulize
keshokutwa” akaniambia.
Nikatoka hapo ofisini na kurudi
kituoni.
Wakati wote nilionekana kuwa na
fadhaa na kwa kweli sikuweza
kufanya kazi kama ilivyo kawaida
yangu. Nilikuwa nawaza mengi.
Japokuwa kwa upande wa ile kesi
sikuwa na wasiwasi sana, nilikuwa
na wasiwasi na wale majini.
Niliamini kuendelea kuwa na kile
kisanduku cha dhahabu
kungewafanya majini hao
waendelee kuniandama na mwisho
wake waitoe roho yangu. Sikuwa
na pa kukipeleka. Ningeweza
kukitupa lakini nilijiambia,
nikikitupa kinaweza kuokotwa na
mtu mwingine na hivyo
kunisababushia matatizo zaidi.
Na akama ni kukirudisha kwa
wenyewe, sikujua ningekirudisha
wapi. Sikuwa na haja nacho tena
kwa kujua kingeniangamiza. Pia
ningeweza kukisalimisha polisi
lakini ndio ningeumbuka kwa
kuonekana nilimdhulumu yule
mwanamke.
Yale mawazo ya kupata utajiri
baada ya kuuza ile dhahabu
yalikwishafutika akilini mwangu.
Kama ningefanikiwa kupata ile
likizo yangu, niliendelea kuwaza,
ningekwenda na hicho kisanduku
hadi kwetu Kagera. Huko ningepata
ushauri kutoka kwa wazazi na
ndugu zangu na ningejua nini cha
kufanya.
Pia kule kwetu kuna waganga wa
kienyeji wanaojua mambo ya
majini ambao nilitarajia kuwa
wangenisaidia baada ya kuwaeleza
ukweli wote. Lakini kwa jinsi
mambo yalivyokuwa yanakwenda
nilipata wasiwasi sana.
Nilikuwa sijui nifanye nini. Akili
yangu ilikuwa ikiwaza kila kitu. Ile
juhudi yetu ya kumtafuta mwenye
ile nyumba haikuwa na maana
yoyote kwangu kwani hata
akifahamika bado tatizo
lingeendelea kuniamdma,
nilijiambia.
Lakini kwa vile lilikuwa zoezi
lililopangwa na viongozi wangu wa
kazi ilibidi nilitekeleze ili niweze
kujinasua na tuhuma za mauaji ya
Erick. Kwa kanuni za kipolisi
ninaweza kuwa mshukiwa namba
moja kutokana na uhusika wangu
katika mauaji ya polisi huyo.
Usiku haukuchelewa. Saa sita usiku
polisi watano nikiwemo mimi na
meja wetu, tukaenda barabara ya
nane kwenye ile nyumba.
Kwanza tulimgongea na
kumfahamisha yule mwenyeji
wetu wa nyumba ya jirani kuwa
tumekuja kuwasubiri hao watu
ambao kelele zao wanazisikia
kuanzia saa nane usiku.
“Kama mtazisikia, tunaomba
mtufahamishe. Sisi tutaendelea
kuwepo hadi watakapokuja hao
watu” Meja Elias alimwambia yule
mwanamke.
“Sawa. Kma tutawasikia
tutawafahamisha”
Mwanamke akarudi ndani na
kufunga mlango. Tukapata wazo
kuwa tukae katika nyumba ile ile ili
tusiwagutushe hao watu.
Wakati tumekaa mazungumzo
yakaanza. Meja Elias ndiye
aliyeanza kusimulia visa vya majini
ambavyo alidai kuwa alikutana
navyo akiwa katika kazi yake ya
upolisi.
Alituambia kwamba kulikuwa na
siku alitongoza mwanamke
alipokuwa mkoa wa Pwani. Kumbe
mwanamke yule alikuwa ni jini.
Yule mwanamke alimwambia
kuwa alikuwa na chumba chake
akamtaka Meja waende katika
chumba hicho.
Meja akakubali na wakaenda katika
chumba cha mwanamke huyo
ambacho kilikuwa kimepambwa
vizuri. Walipofika Meja
hakukumbuka nini kilitokea.
Alishitukia kumeshakucha.
“Nilijikuta nimelala juu ya mti wa
mbuyu nikiwa peke yangu na
nikiwa na nguo zangu vile vile. Kwa
kweli nilishituka sana” Meja
akatuambia na kuongeza.
“Nilishuka kwenye ule mti na
kurudi zangu nyumbani na tangu
siku hiyo nilipata adabu”
Je nini kitaendelea? Endelea
 
SIMULIZI : YALIYONIKUTA TANGA
MSIMULIAJI : MARTIN MEKU
MAHALI : TANGA
SEHEMU YA 18

ILIPOISHIA
Baada ya kumaliza kisa chake
polisi mwingine naye akatueleza
kuwa dada yake alichunukwa na
mwanaume ambaye alikuwa jini
na akataka amuoe.
“Alikuwa akimuona wazi wazi?”
nikamuuliza.
“Ndiyo alikuwa akimtokea na
kumuona kama hivi tulivyokaa
hapa” Polisi huyo akasema na
kuongeza.
“Basi dada yangu alihangaika
sana kwenda kwa waganga
kumuondoa yule jini. Waganga
wengi walishindwa”
“Alikuwa akifanya naye
mapenzi?” Meja Elias akamuuliza.
“Ndiyo alikuwa akifanya naye
mapenzi”
“Sasa walikuwa wanakwenda
wapi?”
“Kwenye mahoteli”
“Nani anapangisha chumba hapo
hoteli?”
“Ni yule jini. Yaani amekaa kama
mwanaadamu tu. Anavaa nguo
kama hizi tunazovaaa, sema
alikuwa muarabu. Mwenyewe
alimwambia ni mwenyeji wa
Misri’
Na mimi nikamuuliza.
“Alikuwa akija naye nyumbani?”
“Nyumbani hakuwahi kufika naye.
Yaani yule jini anapofika kutoka
huko kwao anampigia simu dada
yangu, hapo hapo dada yangu
akili zinapotea anakwenda
mwenyewe mahali alipoambiwa
wakutane”
“Na alikuwa akimpa pesa?”
nikamuuliza.
“Alikuwa akimnunulia vitu
alivyokuwa anahitaji”
SASA ENDELEA
“Sasa mwisho wao uliishaje?”
nikamuuliza.
“Yule dada yangu alivyojaribu
kwenda sana kwa waganga yule
jini alimtia kichaa”
“Ha! Baadaye alipata kichaa?”
“Alipata kichaa. Aliaguliwa sana.
Mpaka hivi karibuni akapata
mganga mmoja aliyetoka Pemba
ndiye aliyemponesha”
“Na huyo jini ameishia wapi?”
Meja akamuuliza.
“Hajamuona hadi leo”
“Mimi nimesikia Wapemba
wanawakamata majini” Meja
akasema.
“Hata mimi niliwahi kusikia hivyo
hivyo. Nilisikia wanawatia
kwenye chupa au kuwafungia
kwenye sanduku” Yule polisi
aliyekuwa akitusimulia alisema.
Pakapita ukimya kidogo. Mimi
nilikuwa nikiwaza juu ya simulizi
hizo zilizokuwa zikitolewa hapo.
Nilishangaa kusikia kuwa majini
wanafungiwa kwenye chupa.
Nikajiuliza wanapata wapi pumzi?
Sikutosheka kujiuliza peke yngu,
nikauliza.
“Sasa jini unapomfungia kwenye
chupa atapata wapi pumzi?”
“Wanajua wenyewe waganga”
alinijibu yule polisi.
“Kwani hawa majini ni nini, ni
upepo tu na miujiza miujiza.
Popote tu anaweza kukaa. Wewe
unaambiwa majini wanaishi chini
ya bahari, wewe unaweza kuishi
chini ya bahari? Kuna hewa
huko?” Meja akatoa hoja yake.
Hakuna aliyejibu. Mazungumzo
yalikuwa ya kutisha lakini
yalisaidia kupitisha muda na
kukimbiza usingizi. Ghafla gari la
polisi la doria likatupitia.
Polisi mmoja alishuka kwenye
gari hilo akatuuliza kama
tulikuwa na tatizo lolote.
Tulipomjibu kuwa hatukuwa na
tatizo alirudi kwenye gari.
“Tutawapitia baadaye”
akatuambia kabla ya gari hilo
kuondoka.
Baada ya gari hilo kuondoka, sote
tukapitiwa na usingizi kwa mpigo
lakini haukupita muda mrefu
tukazinduka mmoja mmoja.
Kilichotuzindusha zilikuwa ni
kelele za vicheko zilizokuwa
zikitokea ndani ya ile nyumba.
Tuliona pia mwanga wa taa
ukitokea mle ndani. Tukajua kuwa
wale watu tuliokuwa tukiwasubiri
walikuwa wameshafika.
Hatukujua waliingia kwa mlango
gani. Kama ni kwa mlango ule wa
mbele watakuwa wametuona
tukiwa tumelala.
Vicheko vilikuwa vikiendelea mle
ndani. Tukatazamana kisha sote
tukainuka. Meja Elias ndiye
aliyekwenda kubisha mlango.
Hatukupata jibu.
Meja akaujaribu ule mlango
akaona ulikuwa wazi, akaufungua
na kuchungulia ndani. Kitendo
hicho cha kufungua ule mlango
kikazinyamazisha zile kelele
zilizokuwa zikisikika. Kukawa
kimya.
Ghafla na zile taa zilizokuwa
zikiwaka zikazimika. Kukawa kiza.
“Kachukue tochi kwenye gari,
wametuzimia taa” Meja
akaniambia.
Nikakimbilia kwenye gari letu na
kuchukua tochi. Nikenda nayo na
kumulika kwenye ule ukumbi.
Ukumbi ulikua mtupu.
Meja akapiga hodi lakini
hakukuwa na jibu.
“Tuingie ndani” Meja akatuambia.
Alitangulia yeye kuingia
nikafuatia mimi niliyekuwa na
tochi. Wenzetu wakafuatia
nyuma. Hatukuwa na wasiwasi
kwa sababu tulikuwa na bunduki
lakini nilijiambia kama ni majini
wasingeweza kutishika na
bunduki zetu.
Wakati tunaingia tulisikia vicheko
kwa uani mwa nyumba hiyo.
Tukaenda hadi uani huku
nikiendelea kumulika tochi.
Tulipofika uani hatukuona mtu.
Na vile vicheko havikusikika tena.
Tukashangaa sana. Tukaanza
kutafuta kwenye vyumba vya
uani. Kila chumba tulichoingia
kilikuwa kitupu. Ghafla tukasikia
tena sauti ya vicheko ikitokea
ukumbini kule tulikotoka.
Tukasita na kutazamana.
Tukaamua kiurudi ukumbini.
Hatukukuta watu. Tukafungua
milango ya vyumba na
kuchungulia ndani. Tukasikia sauti
ya vicheko ikianza kusikika tena
kwa uani.
“Hii nyumba ni ya majini kweli!”
Meja akatuambia.
“Tunasikia watu wanacheka lakini
hatuwaoni” Polisi mwingine
akasema.
“Sasa tufanyeje?” nikauliza. Hofu
yangu kubwa ilikuwa ni
kukutana na yule mwanamke
chinjachinja.
“Tutafute swichi zilipo tuwashe
taa” Meja akasema.
Nikamulika mulika tochi pale
ukumbini, tukaziona swichi. Meja
akawasha taa za nyumba nzima.
Tuliendelea kupekua kwenye vile
vumba vya ukumbini. Hatukukuta
mtu. Vile vicheko vya uani
vilikuwa vikiendelea.
Tukaamua kutoka uani ambako
sasa kulikuwa na mwanga wa taa.
Vile vicheko vikakoma.
Tukafungua tena milango ya
vyumba vya uani tukidhani labda
kulikuwa na watu waliokuwa
wamejificha lakini hatukuona
mtu. Vicheko vikaanza tena
kusikika ukumbini.
“Hapa tutazunguka hadi asubuhi,
hawa watu wanaocheka
hatutawaona” nikawambia
wenzangu. Lengo langu ni kutaka
tuondoke.
Hapo hapo tukasikia gari
likisimama nje, tukajua lilikuwa
gari la polisi la doria. Tukatoka
sote. Mimi nilikuwa wa kwanza
kutoka.
Tulipofika nje tukaona kweli
lilikuwa gari la polisi la doria.
Polisi wanne walishuka na
kutufuata.
“Vipi jamani, mmewaona hawa
watu?” Polisi mmoja akatuuliza.
Meja akawaeleza vituko
vilivyokuwa vikitokea mle ndani.
Hapo hapo tukasikia sauti ya
vicheko imeanza tena. Vicheko
hivyo vilisikika nyumb nzima.
“Si watu hao wanacheka?” Polisi
mmoja akatuuliza.
“Ndiyo, lakini ukiingia hukuti
mtu” Meja alimjibu.
“Hebu twendeni, tuone”
Tukarudi tena humo ndani
pamoja na polisi hao. Sauti
zilizokuwa zikisikika ukumbini
zikaacha, zikabaki sauti
zilizokuwa zikisikika uani.
Tulikwenda uani. Sauti hizo nazo
zikaacha.
Wale polisi tulioingia nao
wakashangaa.
“Mbona hivi!” mmoja akauliza.
“Hii ni miujiza ya mwaka” Meja
akamjibu.
Wale polisi waliotoka kwenye
gari la doria wakataka kuingia
kwenye vile vyumba vya uani ili
kuhakikisha kama kweli
hamkuwa na watu.
Tukawaacha waingie, waliingia
kila chumba na kuchunguza
ndani. Hawakuona mtu. Wakarudi
ukumbini na kuendelea kufungua
vyumba vya ukumbini ambavyo
pia havikuwa na watu. Wakati wa
zoezi hilo zile sauti za vicheko
zilikuwa zimenyamaza.
Baada ya hapo tulitoka nje tukiwa
tumekubalina kwamba ile
nyumba ilikuwa na miujiza.
Uamuzi huo ulinifurahisha kwa
sababu ungekomesha ule
upelelezi wetu na mimi ningepata
nafasi ya kwenda likizo ambako
ningefanya mashauri mengine.
Je nini kitafuatia?
 
SIMULIZI : YALIYONIKUTA TANGA
MSIMULIAJI : MARTIN MEKU
MAHALI : TANGA
SEHEMU YA 19

ILIPOISHIA

Meja akanichagua mimi na polisi
mmoja mwenye bunduki tulinde
ile nyumba hadi asubuhi ili mwizi
asije akaingia na kuiba vitu kwani
mlango wake wa mbele ulikuwa
umesindikwa tu kama ambavyo
tumeukuta.
Meja na polisi wengine
wakaondoka na kutuacha sisi. Saa
yangu iliniambia ilikuwa saa tisa
na nusu usiku. Kulikuwa na baridi
kali ambayo ilitupiga. Mimi
ambaye nilivaa nguo nyepesi ndio
niliisikia vizuri sana.
Tukakaa pale barazani kulinda ile
nyumba kama tulivyoagizwa. Taa
za ndani ya ile nyumba tulikuwa
tumezizima. Mara tukaona zile taa
zinawashwa. Tukasikia kama sauti
za mapanga yakigongana pamoja
na hatua za watu wanaopishana.
Wakati tumetega masikio
tukisikiliza, tulisikia sauti ambayo
mimi niitambua kuwa ni ya yule
mwanamke ikisema.
“Chinja chinja tu sasa…kila mtu
chinja….hapana kuacha…!”
Ghafla tulisikia kishindo kikubwa
kwenye ule mlango wa mbele
kama vile ulipogwa na kitu kizoto.
Mlango huo ukafunguka na kuwa
wazi huku sauti ya yule
mwanamke ikiendelea kusikika.
“Chinja chinja tu sasa…kila mtu
chinja….!”
SASA ENDELEA
Tulisikia kishindo cha watu
waliokuwa wakikumbana kuwania
kutoka katika mlango huo hku
mlio wa mapanga
yanyoyogongana ukisikika.
Askari mwenzangu niliyekuwa
naye alikuwa wa kwanza kuinuka
pale tulipokuwa tumeketi
akatimua mbio. Laiti kama ule
mkanda wa buduki yake
usingekuwa begani angeiacha
bunduki yake pale pale. Kwa vile
alikuwa ameuvaa mkanda wa
bunduki hiyo kwenye bega
aliweza kukimbia nayo.
Nilipoona mwenzangu anatimua,
na mimi nikainuka na kumuata
mbio!
Tulichokikimbia hapo ilikuwa ni
kuchinjwa na majini. Tulishatia
imani kuwa wale walikuwa majini
na ndio waliokuwa wamemchinja
Sajenti Erick hivyo tilona kwamba
na sisi tungechinjwa kutokana na
ile sauti iliyokuwa ikiashiria
kuchinja.
Tuliendelea kwenda mbio bila
kutazama nyuma mpaka
tukaikafika kituo cha polisi. Polisi
wenzetu walitushangaa.
“Vipi?” Polisi mmoja akatuuliza.
Tukaeleza kilichokuwa kimetutoa
mbio. Hapo hapo ikapigwa radio
Call, gari lililokuwa kwenye doria
likawasili. Mimi na mwenzangu
tukapanda katika gari hilo
kuelekea katika ile nyumba.
Tulipofika tulishuka na kwenda
kwenye mlango. Tuliujaribu
mlango na kukuta ulikuwa
umeffungwa. Zile taa zilizokuwa
zimewashwa tulikuta zimezimwa.
Hakukuwa na dalili yoyote
iliyoonesha kuwa ndani ya
nyumba hiyo mlikuwa na watu.
Polisi mmoja kampigia mkuu wa
zamu wa kituo kutaka apewe
ruhusa ili tuvunje mlango tuingie
ndani. Ile timu tuliyokwenda nayo
ilikuwa haiamini mashetani.
Ruhusa ikatolewa kuwa tunaweza
kuvunja mlango na kuwakamata
waliokuwa ndani. Polisi mmoja
aliupiga vikumbo vitatu mlango
huo ukafunguka. Moyo wangu
ulikuwa ukinienda mbio. Polisi
wakaingia ndani, mimi nilikuwa
wa mwisho kuingia.
Niliwasha taa ya ukumbini na na
uani. Tukaanza kutafuta.
Hatukukutamtu yeyote humo
ndani. Nyumba ilikuwa tupu.
“Wako wapi?” Polisi mmoja
aliyekuwa na kimbelembele
akauliza kwa umori.
“Nadhani wameshaondoka”
nikamjibu.
“Wameondoka wamekwenda
wapi?”
“Hatuwezi kujua”
Nikapiga simu tena kituoni
kuwajulisha kuwa tumevunja
mlango na tumeikuta nyumba iko
tupu.
Amri tuliyopewa ni kuwa
tubakishe askari wawili walinde
nyumba na wengine warudi
kituoni. Polisi wawili
wakabakishwa kulinda nyumba na
waliagizwa kumkamata mtu
yeyote atakayeingia mle ndani.
Tuliporudi kituoni, mimi
niliruhusiwa kurudi nyumbani. Ile
gari ya doria ikanipeleka
nyumbani. Asubuhi kulipokucha
nikaenda tena kituoni.
Nikaambiwa ninaitwa kwa aisa
upelelezi wa mkoa.
Nilipofika akaniambia ameshapata
taarifa zote za matukio
yaliyotokea usiku uliopita.
“Miujiza imekuwa mingi. Utaanza
likizo yako kesho isipokuwa
tufahamishe utakuwa wapi ili
tutakapokuhitaji tuweze
kukupata”
“Nitakuwa nyumbani Kagera”
“Sawa. Leo kamilisha taratibu za
kuanza likizo, kesho utaondoka”
“Nashukuru aande”
Nikamuaga na kutoka.
Siku ya pili yake nikaanza likizo
yangu. Na siku ya tatu nikaondoka
kwenda Dar nikiwa nimekichukua
kile kisanduku cha dhahabu.
Nilikitia kwenye begi langu.
Nilipofika Dar siku iliyofuata
nikatafuta usafiri wa kuelekea
Kagera. Mpaka ninafika kijijini
kwetu ilinichukua siku mbili. Japo
nilikuwa nimekutwa na madhila
huko Tanga, nilipata furaha
kukutana tena na wazazi wangu
pamoja na ndugu zangu ambao
tuliachana kwa karibu miaka
mitatu iliyopita.
ITAENDELEA
 
SIMULIZI : YALIYONIKUTA TANGA
MSIMULIAJI : MARTIN MEKU
MAHALI : TANGA
SEHEMU YA 20

ILIPOISHIA

“Sawa. Leo kamilisha taratibu za
kuanza likizo, kesho utaondoka”
afande wangu aliniambia.
“Nashukuru afande”
Nikamuaga na kutoka.
Siku ya pili yake nikaanza likizo
yangu. Na siku ya tatu nikaondoka
kwenda Dar nikiwa nimekichukua
kile kisanduku cha dhahabu.
Nilikitia kwenye begi langu.
Nilipofika Dar siku iliyofuata
nikatafuta usafiri wa kuelekea
Kagera. Mpaka ninafika kijijini
kwetu ilinichukua siku mbili. Japo
nilikuwa nimekutwa na madhila
huko Tanga, nilipata furaha
kukutana tena na wazazi wangu
pamoja na ndugu zangu ambao
tuliachana kwa karibu miaka
mitatu iliyopita.
Iliuwa ni siku iliyofuata
nilipowakusanya ndugu zangu
wawili ambao walikuwa wakubwa
zangu pamoja na wazazi wangu
na kuwaeleza mkasa uliokuwa
umenitokea huko Tanga.
Niliwaeleza wazi makosa ambayo
tuliyafanya mimi na Sajenti Erick
ya kumbambikia kesi mwanamke
ambaye alikuwa ni jini baada ya
kukataa kutupa rushwa. Lakini
nilijitetea kuwa aliyepanga
mpango huo alikuwa mkuu wangu
wa kazi ambaye alichinjwa kama
kuku.
Pia nilificha kuwaeleza habari ya
kile kisanduku cha dhahabu
ambacho nilikuwa nimekiiba
nyumbani kwa yule mwanamke na
ambacho nilikwenda nacho Kagera.
Baada ya kuwaeleza mkasa huo
ambao uliwashangaza na kuwatia
hofu, wazazi wangu waliniambia
ni lazima tutafute mganga
tumueleze suala hilo halafu
tumsikilize atatuambia nini.
SASA ENDELEA
Baada ya mazungumzo yetu
mama alinichukua tukaenda kwa
mganga. Mganga mwenyewe
alikuwa kijiji cha pili na tulikwenda
kwa miguu.
Wakati tunatembea pole pole,
mama aliniambia nilifanya vyema
kuwahi kurudi kijijini hapo na
kuwaeleza mkasa huo kwani kama
ningechelewa majini hao
wangenichinja kama aivyochinjwa
Sajenti Erick.
“Tangu zamani tulikuwa tunasikia
sifa za mji wa Tanga, ni mji wenye
majini wa hatari. Kumbe wengine
wanaishi na binaadamu na
wanafanya biashara za dhahabu!”
Mama aliniambia.
“IIitokea bahati kwamba likizo
yangu ilikuwa ipo tayari,
nilicheleweshwa na hayo matatizo
tu”
“Bahati yako mwanangu”
Tulipofika kwa mganga
nilishangaa kukuta mganga
mwenyewe niiyesifiwa kuwa
hodari kwa matatizo ya majini
alikuwa mwanamke tena akiwa
bado msichana.
Hatukukuta watu, tulikuwa ni sisi
tu. Baada ya kusalimiana naye
alitukaribisha ndani kwani
tulimkuta nje ya nyumba yake.
“Tumekuja tuna shida” Mama
alianza kumwambia mganga huyo
mara tu tulipoingia kweye chumba
chake cha uganga kilichokuwa
uani mwa nyumba yake.
“Shida gani?” mwanamke huyo
akatuuliza.
“Wewe ndiye mtaalamu, tunataka
utuambie shida yetu” Mama
akamwambia.
“Mimi si mtaalamu, mimi ni
mtumishi tu wa wenyewe. Ngojeni
niwaite mzungumze nao”
Mwanamke huyo baada ya
kutuambia hivyo alichukua upande
wa kaniki akajifunika kisha
akanusa ugoro. Baada ya kuunusa
mara tatu alipiga chafya kisha
akatikisa kichwa chake kwa
mfululizo.
Wakati anatikisa kichwa alitupa
mkono na kutusalimia kwa lugha
ya kikwetu ambayo ndiyo
iliyokuwa ikitumika zaidi pale
kijijini. Lakini wakati ule sauti yake
ilikuwa imebadilika na kuwa ya
kiume.
Akatuambia kwamba yeye ndiye
mganga mwenyewe na amekuja
kusikiliza shida yetu.
“Mimi ni jini wa kiti, mwenye
uganga huu. Nataka kusikiliza
shida zenu” akatuambia.
“Tunataka ramli” mama
akamwambia.
“Oh mnataka ramli…mtapata”
akatuambia na kutazama juu ya
dari ya miti ya chumba
tulichokuwemo.
Aliangalia boriti za ile dari kwa
sekunde kadhaa kama aliyekuwa
akiangalia kitu kisha akakishusha
kichwa chake na kututazama.
“Ramli inakwenda kwa kijana”
akatuambia.
“Taire” Mama alitumia neno la
kinyumbani lenye maana ya neno
hilo taire.
Mwanamke huyo aliinua tena
kichwa chake, safari hii
hakuchelewa sana akakishusha
taratibu.
“Nimeona” akatuambia na
kuongeza.
“Nimeona matatizo makubwa
sana, yametokea mbali na amekuja
nayo hapa”
Mimi na mama tukatazamana.
“Matatizo gani?” Mama akauliza
haraka.
Mganga akatazama tena juu.
“Wewe na mwenzako mlifanya
makosa, naona damu nyingi…”
akatuambia baada ya kukishusha
kichwa chake kisha akatazama
tena juu.
Iikuwa kama vile pale juu ndipo
alipokuwa anasoma habari zetu.
“Mtu mmoja ameuliwa na mmoja
amechukua mali, ile mali ni ya
majini” mwanamke huyo
aliendelea kutuambia.
Tukanyamaza kimya huku
tukiendeea kumsikiliza.
Niishayatafsiri maneno yake
kwamba mtu aliyeuliwa ni Sajenti
Erick na aliyechukua mali ni mimi.
Mali ilikuwa ile dhahabu
iliyokuwemo kwenye kisanduku.
Mwanamke huyo baada ya
kutazama juu alishusha kichwa
chake na kunitazama mimi.
“Hebu nieleze, nini kimetokea”
akaniambia.
Kwa vie aishaigusia habari
yenyewe nikaona nimueleze.
Nikamueleza.
Mwanamke huyo akapiga mluzi
wa mshituko.
“Hatari!” akasema na kuongeza.
“Wewe pia ungekufa. Umri wako
bado mrefu”
Akaendelea kutuambia.
“IIe nyumba inakaa majini.
Mwenyewe amekwishakufa. Majini
wa pwani wanafanya biashara.
Wewe unapenda sana kutongoza
wasichana. Sasa umetongoza jini.
Alikuwa anakutafuta akukomeshe”
Nilimuelewa alichomaanisha.
Alikuwa na maana kwamba mimi
napenda kutongoza kwa sababu
nilimtongoza yule msichana wa
kijini kwenye simu, kumbe
msichana mwenyewe naye
alikuwa ananitafuta baada ya
kumkamata mama yake na
kumbambikia kesi ya uongo.
“Sasa nifanye nini ili niweze
kusalimika” nikamuuiza
mwanamke huyo.
Niipomuuliza hivyo alitazama juu.
Baadaye aliurudisha chini uso
wake akatuambia.
“Wenyewe wanataka dhahabu
yao”
“Hakuna namna ya kufanya
nikabaki nayo mimi?” nikamuuliza.
“Mimi utanipa nini?”
“Nitakupa pesa utakayoitaka”
“Sawa. Kesho lete kile kisanduku,
nitakufanyia uganga wake. Hao
majini hawatakufuata tena na
wewe utabaki na dhahabu yako”
“Hivyo ndivyo ninavyotaka. Basi
tutakuja kesho. Nitakileta na kile
kisanduku” nikamwambia.
Yule jini alipoondoka, yule
mwanamke alituuliza
tulichozungumza, tukamueleza.
“Sasa kesho mtakuja?” akatuuliza.
“Tutakuja kesho asubuhi”
nikamjibu.
“Ngoja nikupe dawa yangu”
akatuambia na kuinuka.
Aikwenda pembeni mwa chumba
hicho. Alikuwa ameweka
makorokoro yake ya kiganga.
Akachukua pembe moja ya
mnyama aliyokuwa ameifunga
kitambaa cheusi. Ule upande
uliokuwa na shina la ile pembe
aliukung’uta kwenye kiganja
chake, ukatoka unga mweusi.
Alinifungia unga huo kwenye
kikaratasi.
“Usiku utatia dawa hii kwenye
maji yako ya kuoga halafu utaoga”
akaniambia.
Nikakichuku kile kikaratasi na
kukitia mfukoni.
“Niitie yote au niibakishe?”
nikamuuliza.
“Tia yote”
“Sawa”
Je nini kitaendelea?
 
Back
Top Bottom