Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

SEHEMU YA 215

“Roma wewe ni mjukuu wangu Denisi, unaweza usiamini maneno yangu lakini huo ndio ukweli na uthibitisho wote ninao na utanisamehe sana kwa kile ambacho ninakwenda kukuambia..”Aliongea na kisha akampa ishara Zenzei ampe mkoba wake aliokuja nao , uliokuwa upo pembeni na baada ya kuufungua alitoa karatasi na kumpatia Edna aliekaribu na Edna alimparia Roma.

Karatasi alioshika Roma mkononi ilikuwa ni cheti cha hospitalini cha Denisi Senga , ni cheti ambacho hakikuwa na picha bali jina pekee na kwa jinsi Roma alivyosoma cheti hiko kilikuwa kikionyesha Denisi kuwa mgonjwa wa Saratani ya ubongo ilikokuwa kwenye steji namba tatu.

Chini kabisa ya cheti hiko kuna maoni kutoka kwa daktari yaliokuwa yakionyesha Denisi ana muda wa miezi minne tu ya kuweza kuishi kutokana na ugonjwa wake.

“Hiki cheti ni cha nani?”Aliuliza Roma huku akimpatia na mke wake kusoma.

Mzee Senga alitoa picha nyingine mbili na kumpatia Roma na baada ya picha zile kuziangalia kwa umakini hakuzitambua , lakini mtu aliekuwa kwenye picha hizo alikuwa akifanana kwa kiasi kikubwa na yeye

“Hizo ni picha za utoto wako , hiko cheti ni cha kwako,, sina maelezo ya ziada ya kuthibitisha maneno yangu kwasababu siju nini kilichotokea baada ya kufanya maamuzi mwaka 1998”Aliongea Mzee Kweka na kisha akatoa karatasi nyingine na kumpatia Roma na karatasi ile juu kabisa ilikuwa na nembo ya Zeros Organisation hakukuwa na maelezo mengi kutoka kwenye karatasi hio , lakini kilichoandikwa ni namna taasisi hio ilivyokuwa ikijihusisha na maswala ya kisayansi.

“Nadhani unaijua hilo shirika?”

“Nalifahamu lakini mpaka sasa sijaelewa pointi yako ni ipi?”

“Pointi yangu ni hii”Aliongea na kutoa karatasi nyingine”

“Hio ni karatasi ambayo inaonyesha makubaliano nilioyafanya miaka ishirini nyuma ya kukubali kukutoa kwa shirika la Zeros Organisation kwa ajili ya majaribio ya kisayansi”Aliongea Mzee Kweka pasipo wasiwasi , alionekana kujiamini kutokana na uwezo wa Zenzhei.

Edna mwenyewe hakuwa akijua kinachoendelea mpaka hapo , majaribio ya kisayansi , ina maana Roma huyu mzee alimtoa mjukuu wake kwa ajili ya majaribio ya kisayasi? Hayo ndio maswali aliokuwa akijiuliza Edna wakati huo.

“Ni uamuzi ambao mtu anaweza akadhania ni kichaa , lakini sijutii kwa uamuzi ambao nilifanya , ulikuwa na miezi mitatu tu ya kuishi duniani na kwasababu nilikuwa nakupenda kama mjukuu wangu wa kwanza sikufikiria hata mara moja baada ya kuona kuna nafasi ya kuendelea kukufanya uwe hai ndio maana nilikubali kucheza mchezo wa kubahatisha juu ya uhai wako , lakini yote hayo sijuitii kwani naamini maamuzi yangu yalikuwa sahihi kwasababu umerudi nyumbani ukiwa mzima”Aliongea Camillius na kumfanya Roma kichwa chake kianze kuuma , ukweli Roma hakuwa akikumbuka chochote na hii ni kutokana na kwamba hakuwa na kumbukumbu za utoto wake wote , yaani kumbukumbu alizokuwa nazo ni baadhi tu alizokuwa nazo walipokuwa kwenye kisiwa na kumbukumbu nyingine ni alipokuwa ndani ya maabara kwenye visiwa vya Madagascar.

Wakati Roma akiendelea kusharabu maneno ambayo kwake yalikuwa magumu kuyameza mara muda huo huo Mzee kweka alitoka kwenye sofa na kupiga magoti mbele ya Roma na kumfanya Edna kushangaa na sio kwa Edna tu hata kwa Zenzhei, ila kwa Roma hakushangaa kwakua muda huo ni kama alikuwa amechanganyikiwa na hata muda ambao Mzee kweka alipiga magoti hakuona.

“Roma jina lako halisi uliozaliwa nalo ni Denisi Senga , Raisi Senga ndio baba yako mzazi , Blandina ndio mama yako mzazi na mimi ndio Babu yako nimepiga magoti haya sio kwa ajili ya kukuomba msamaha kwani sijutii kwa kile nilichokifanya ila nimepiga magoti haya kwa ajili ya kukuomba usahau Maisha yote yaliopita na sasa unapaswa kuanza upya, nimekusubiria kwa miaka mingi huku siri iliokuwa kwenye moyo wangu nikiishi nayo kwa miaka mingi licha ya kwamba ilikuwa kama kaa la moto , lakini kwasababu mimi ni mwanajeshi maumivu yalikuwa seehemu ya Maisha yangu”Aliongea Camillius na kisha akasimama.

“Blandina mama yako yupo hai… yupo nchini Kenya kama mke wa Raisi na kwasasa kafungiwa na mume wake , wewe ndio mtoto wa pekee kwa mama yako nakupa baraka kwa chochote utakachoamua kufanya juu ya mama yako kwani ameteseka vya kutosha kwa ajili ya kukuweka hai”Aliongea Mzee Camillius na kumwangalia Edna ambaye machozi yalikuwa yameloanisha mashavu yake , haikuelweka kwanini alikuwa akitoa machozi.

Mzee Kweka alionekana kutokuwa na maneno mengi bali aliacha karatasi nyingine juu ya sofa na kisha yeye Pamoja na Zenzhei walitoka nje ya chumba hiko kuondoka zao.

Lakini huku nyuma Roma alikuwa akitetemeka mwili na ni kama baadhi ya matukio yalikuwa yakijirudia kwenye kichwa chake kwa kasi mno , ni kama picha za utoto wake zilianza kupita moja moja kwenye akili yake na alishindwa hata kujielewa na Edna aliiona hali aliokuwa nayo Roma na alimsogelea kwa ajili ya kumgusa lakini ile anapeleka mkono npalepale Roma aliyeyuka kama hewa na kupotea kwenye macho yake.

“Romaa…!!!!”Aliita Edna kwa nguvu lakini hakuweza kumuona Roma tena mbele yake na aliishia kukaa chini na kuanza kulia kwa kwikwi kama mtoto na muda ule ule Bi Wema , Sophia , Na Yezi waliingia ndani ya chumba cha Edna na hali waliomuana nayo Edna ilimshangaza na Bi Wema ndio aliekuwa wa kwanza kumkimbilia Edna na kumkumbatia kumtuliza.

********

THE HAGUE -UHOLANZI 1996

Ni ndani ya ukumbi mkubwa mdogo unaomilikiwa na shirika la siri duniani , Zeros organization , kulikuwa na kikao kilichokuwa kikiendelea , kikao hiki kilikuwa kikihusisha serikali zenye nguvu kubwa duniani huku kiongozi mkuu akiwa ni The First Black , Director wa shirika la kijasusi la CIA.

Kikao hiki licha ya wahudhuriaji wengi kuwa viongozi wakubwa duniani , lakini pia walikuwepo wanasayansi wakubwa duniani katika Nyanja zote ambao pia wamehudhuria kwenye kikao hiko.

Ajenda kuu ya kikao hiki ilikuwa ni juu ya tukio ambalo lilitokea miaka ya tisini huko Sweeden.

“Mr First Black walisema nini kabla ya kupoteza Maisha?”Aliuliza mmoja ya wahudhuriaji ambaye jina lake halikufahamika ila alikuwa ni kiongozi wa taifa kubwa duniani.

“Walisema licha ya wao kuhimili mazingira ya hapa Duniani lakini watakuja wengine kuwatafuta dada zao na kaka zao waliopotea hapa duniani ambao wanaamini bado wanaishi kutokana na Signal wanzopokea kila siku”

“Una uhakika na hayo maneno Director?”

“Ndio nina uhakika na maneno yangu na pia mashahidi wapo , We Can Prove it”

“Director tuseme maneno yao ni ya kweli kwa asilimia mia moja je hao dada zao na kaka zao wapo wapi hapa duniani kwasababu kwa wanavyosema ni tukio ambalo limetokea miaka mingi nyuma , wanatushawishi vipi kuamini kama maneno yao ni ya kweli?”

“Kwasababu naamini wanachozungumza ni kweli?”

“Unatuthibitishia vipi kama maneno yao ni ya kweli?”

Aliuliza kiongozi mwingine kwa hasira kweli , ni kama hawakua wakimuelewa Director wa CIA kwa maneno yake , lakini First Black wala hakujihangaisha bali alimpa ishara moja ya mwanasayansi aliekuwa mita kadhaa upande wa kushoto na muda ule ule waliingia watu wanne waliokuwa wamebeba boksi la kioo la pembe mraba huku ndani yake kukionekana kijimti mfano wa vimbao vinavyotumika kanisai kuwekea mishumaa(Candlestick) , baada ya sanduku lile kuweka juu ya meza mbele ya Fist Black, wale walirudi nyuma na Director alifungua lile boksi na kisha akavuta kitabaa kilichokua kimefunika kijimti kilichokuwa kimekaa ndani yake na paleple lilionekana jiwe mfano wa kitenesi na kitendo kile cha First Black kutoa kile kitambaa jiwe lile lilitoa mwanga mkali ambao ulisababisha miale yake kujaa chumba kizima na kushangaza umati mzima wa watu waliokuwa kwenye mkutano huo.

“This is our Proof”

“Director …..Elezea hiko ni nini?”

“We call it Godstone”

“Godstone!!!!”

“Ndio..”Aliiitikia na kufanya zogo lianze kusikika pande zote za ukumbi huu.

“Hili ni aina ya jiwe ambalo mpaka sasa wanasayansi wetu wanaendelea kulifanyia utafiti ili kulifahamu Zaidi , na jina la jiwe hili limetokana na pendekezo kutoka kwa Profesa Banosi na aliamua kulipa jina hili kutokana na uwezo mkubwa, lakini pia kutokana na madini yanayopatikana ndani yake”Aliongea First Black.

“Tueleze mmelitoa wapi hili jiwe”

“The So called sister`s and Brother`s who are claimed to be in this world , this was their possession and it’s only proof “

“Watu wanaoitwa dada na kaka ambao wanaaminika kuwa katika huu ulimwengu , hili jiwe lilikuwa umiliki wao”Aliongea First Black.

“Meaning…”

“Meaning that this is Alien`s mineral we do not know about”

“Nikimaanisha kwamba ni jiwe lenye madini kutoka sayari nyingine ambayo hatuyajui”Aliongea na kufanya watu kuchanganyikiwa Zaidi , likuwa ni jambo jipya kwao , hivyo kuchanganyikiwa ilikuwa n sehemu ya ubinadamu na kwa upande wa First Black alichukuliwa swala hilo kama hatua ya kwanza ya ushawishi wa mpango wake.

Unafikiti ni mpango gani?”
 
SEHEMU YA 216.

1980-USA. CALIFORNIA , KABLA YA KIKAO CHA 1996

Ni ndani ya maabara ya kisasa ambayo ipo ndani ya jiji la Calfornia , maabara hii licha ya uwepo wake ndani ya jiji hili , lakini haikueleweka uelekeo wake, wala sehemu mahususi ilipojengewa na hii yote ni kuhakikisha siri iliokuwepo ndani ya mabaara hii inabakia kuwa siri.

Katika maabara hii walionekana watu kumi wakiwa katika kazi zao kama kawaida na wote wakiwa wamevalia PPE , mavazi ya kujikinga na mionzi , lakini pia na maambukizi yanayosambaa kwa njia ya hewa.

Watu hawa kumi waliendelea na utaalamu wao ndani ya maabara hii ya kisasa kabisa , huku mbele yao kukiwa na makabati mengi yaliokuwa yamepangwa kwa ustadi mkubwa , yaliokuwa yamezungukwa na mwanga wa LED.

“Profesa Banos”Ilisikika sauti ikigonga ndani ya chumba hiki kikubwa cha maabara na kufanya mwanaume mmoja kwenye mwili mkubwa aliekuwa ameketi kwenye tarakishi ya chogo akisoma baadhi ya data ambazo hazikueleweka.

“Yes Director ….”

“Nahitaji kuongea na wewe ofisini kwangu” ilisikika sauti hii ndani ya chumba hiki huku wanasayansi wengine tisa wakiendelea na kazi yao kama vile hawakuwa wakisikia sauti iliokuwa ikisikika kwa kutumia spika zilizofungwa ndani ya maabara hio ya level 4.

Profesa Banos baada ya kusikia ujumbe huo alifuata Protocol za kufungua maabara hio kwa muda wa nusu saa nzima mpaka alipotoka nje kabisa ya chumba hiko na moja kwa moja alitembea mpaka kwenye chumba kilichokuwa upande wa kulia kwenye korido ndefu iliokuwa na vyumba vingi ambavyo mwanga wake wote ulikuwa hafifu huku kila kona kukiwa kumefungwa CCTV kamera.

‘Director Office’ Ndio mlango ulivyosomeka juu ya kibao na Profesa Banosi aliekuwa kwenye muonekano wa kizee kama miaka sabini hivi , aliingia ndani ya ofisi ya Director na hapa ndani alionekana mwanaume mmoja aliekaa nyuma ya tarakishi ya chogo akiwa bize , alikuwa ni mwanaume rangi mchanganyiko yaani ya kizungu Pamoja na ya kiafrika, makadirio ya umri wa miaka arobaini hivi.

“Profesa nataka kuandaa ripoti ambayo nitaiwakilisha White House siku ya Ijumaa juu ya maendeleo ya Project , hivyo kwakua wewe ndio mwanasayansi unaeongoza hapa ndani , nitahitaji uniambie ni hatua gani tuliofikia”Aliongea Yule kijana huku Profesa Banosi akikaa kwenye kiti.

“Jiwe la kimungu naweza kusema kwamba madini yake sio ya kawaida kabisa na linatoa mionzi ambayo sijapata kuona kwenye Maisha yangu , haimizi , haionekani lakini ina athari kubwa sana kwa mwili wa binadamu”Aliongea Profesa Banosi.

“Endelea Profesa…”

“Hakuna binadamu ambaye anaweza kuhimili mionzi inayotokana na madini yanayotoka kwenye jiwe hili”

“What is your Suggestion Professor , I mean as Scientist what is your perception?”

“I have hypothesis ….”

“Endelea …”

“Kwa jinsi nilivyotumia muda wangu mwingi kusoma athari zinazotokana na Godstone ,nimegundua kwamba hakuna binadamu ambaye anaweza kuhimili athari zake mpaka afanyiwe matayarisho”

“Unamaanisha nini kuhusu matayarisho?”

“Our DNA is so much weak to withstand radiation`s from Godstone and every modification lead to death and that is point where my thesis begin”

“Mfumo wa vinasaba vya damu vya sisi binadamu ni dhaifu mno kiasi kwamba hatuwezi kuhimili mionzi na kila uchakachuzi unasababisha kifo na hapo ndio sehemu ambapo wazo langu la kisayansi huanzia”Aliongea Profesa na akaendelea.

“Tunatakiwa kufanya tafiti kujua ni kwa namna gani tunaweza kukomaza DNA za mwili kabla ya kuzimulika na Divine Light”

“Divine Light..What is that ..”

“It`s moral name I came up with , The Word Radiation is Cruel in human right stance”

“Haha…nimekuelewa Profesa , lakini hilo wazo lako ambalo bado halipo kwenye majaribio unafikiri linawezekana vipi?”

“I am thinking about kind of Virus which can rewrite human DNA after infection’s”

“Virus!!”

“Ndio kama nitaweza kutengeneza kirusi ambacho kitakuwa na uwezo wa kuandika upya DNA za binadamu nahisi litakuwa jambo jepesi sana kufanikiwa kutumia Godstone kwa binadamu”

“Kwahio unamaanisha unataka kutengeza kirusi na kuwaambukiza watu na watakao nusurika na maambukizi hayo ndio watakuwa na uwezo wa kuhimili miale ya Godstone?”

“Ndio Director , unakichwa chepesi kuelewa sana,,, ijapokuwa kwa sasa hilo ni wazo , lakini nitayatoa maisha yangu kwa ajili ya kufanya utafiti wa kugundua kirusi ambacho kitakuwa na uwezo wa kukomaza DNA za binadamu na hilo likifanikiwa basi na mpango wa kutumia Godstone utafanikiwa kwa asilimia mia moja , na utaweza kutengeneza miungu watu hahaha..”Director alijikuta akikuna kichwa licha ya kwamba ameelewa wazo hilo ila aliona kama linawezekana basi itakuwa vyema kujaribu.

Kwani mpaka wakati huo ni vifo vingi vimepotea kwa ajili ya majaribio na hakukuwa na mafanikio ya aina yoyote ile.

“Nitaongea na wakuu wangu then nitakupatia jibu”

“Sawa director , lakini kama jambo hilo litawezekana sitoweza kufanyia kazi zangu ndani ya hii maabara nitaomba kufanyia msituni”Aliongea Profesa na director alifikiria kidogo na kisha akatingisha kichwa na kumuahidi profesa kwamba na swala hilo atalifikisha sehemu husika.

*******

NAIROBI -KENYA

Mheshimiwa Kamau Kamau alikuwa kwenye wasiwasi mwingi sana na hii ni mara baada ya kupokea ripoti kutoka kwa shushu wake nchini Tanzania, taarifa ambayo iilikuwa ikimuelezea Mzee Kweka Kwenda kuonana na Roma Ramoni.

Licha ya kwamba hakujua kile ambacho Mzee Kweka ameongea na Roma Ramoni lakini aliamini ni jambo ambalo lilikuwa likihusiana na mke wake Blandina kwa asilimiia kubwa , jambo ambalo hakutaka kabisa litokee hivi karibuni , kabla ya kumaliza miaka yake ya uongozi.

Wakati akiwa ofisini kwake alikuwa ashatoa oda ya kuitwa kwa mkuu wa majeshi kwa ajili ya kuonana nae ofisini na muda huu alikuwa akimsubiria kwa hamu kubwa na ni takribani dakika therathi tokea afike ofisni kwake akimsubiria na ziliongezeka dakika kumi nyingine ndio mkuu wa Majeshi alievalia gwanda za jeshi la Kenya aliingia ofisini hapo na kupiga salute kwa mheshimiwa.

“Afande Wambai Rai karibu sana”

“Asante sana mheshimiwa nimeitikia wito”Aliongea Afande Rai Wambai huku akiketi kwenye kiti.

“Afande nitaenda moja kwa moja katika jambo ambalo nimekuitia , wewe ni rafiki yangu lakini pia ni mkuu wa majeshi , hivyo nitaomba ushauri kwa jambo ambalo napitia kwa wakati huu”

“Mheshimiwa ni juu ya Blandina?”

“Ndio, ni juu ya mke wangu Maina au Blandina”

“Kuna nini mheshimiwa?”Aliuliza Afande Wambai na mheshimiwa alimkabidhi faili Afande Wambai na akaanza kusoma.

“Hades!!!”

“Unalifahamu hilo jina?”

“Ndio nishawahi kulikiskia mara kibao , lakini sikuwahi kuhakikisha taarifa hizo”

“Basi kama hukuwahi kuhakikisha taarifa hizo , leo nakuhakikishia kwamba taarifa hizo ni za kweli na mtu unaemuona kwenye picha ni Hades mwenyewe”Aliongea Mheshimiwa na kumfanya Afande Wambai achukue picha iliokuwa kwenye bahasha na kuiangalia.

“Impossible ..!!!”

“Inawezekana Afande na mbaya Zaidi mtu unaemuona kwenye picha ni mtoto wa mke wangu Blandina”Aliongea na kumfanya Jenerali huyu wa majeshi yote kushangaa mno.

“Inawezekana vipi hili mheshimiwa?”

“Kwa mawazo yetu linaweza lisiwezekane , lakini mtu unae muona ni halisi na mtu ambaye umemsikia na sina muda wa kukueleza mengi , lakini kwa sasa nashindwa kujua maamuzi ambayo napaswa kuchukua kwa sasa”

“Unamaanisha nini huwezi kuchukua maamuzi kwa sasa , Kamau wewe ni rafiki yangu na siku zote umekuwa ni mtu wa maamuzi , kwani kuna nini kinaendelea?”

“Blandina anajua uwepo wa mtoto wake , kumbuka alikuwa akijua alikufa na ajali ya ndege?”

“Ndio nafahamu hili , lakini bado ndio maana naona kuna maelezo mengi ambayo labda nikiyasikia ndio nitaelewa unachomaanisha”

“Maelezo ni ya siku nyingine Mwambai .. ninachokueleza kwa sasa Maina hataki tena kuendelea na mimi na anataka kuwa na mtoto wake pekee na ashachoka Maisha ya kuigiza swala ambalo linaweka taifa katika hatari , jambo lingine naamini pia na Roma Ramoni ashafahamu uwepo wa mama yake hapa Kenya”Aliongea.

“Kama kweli hizi taarifa ni sahihi na huyu ndio Hades ninaemsikia basi tupo kwenye tatizo kubwa”

“Unamaanisha nini?”

“Kama atamuhitaji mama yake basi hakuna haja ya kuzuia hili , lazima tumruhusu amchukue taifa letu halina uwezo wa kuwa upande mbaya na Hades”

“Lakini hili ni swala gumu kufanyika , Blandina hawezti Kwenda Tanzania”

“Hahaha..Kamau sio kwamba Blandina hawezi Kwenda Tanzania ila moyo wako haupo tayari kumruhusu Blandina Kwenda Tanzania”

“Ni kweli , lakini hata moyo wangu umuachilie unafikiri linawezekana vipi?”

“You faked her at front of whole Citizen and we as your Subordinates we kept your Secret , it`s simple we can repeat the process”

“Umemfanya kuwa feki mbele ya raia wote na sisi washirika wako tulitunza siri yako ,… ni rahisi tunaweza kurudia mchakato”

“Unamaanisha nini?”

“Maina is Dead that is my point”

“Maina kafa hio ndio point yangu”

NB:miliki ya kijini ambayo Athena anapanga kuiangamiza ni Hongmeng na miliki nyingine iliopo Tanzania don’t be confused.
 
SEHEMU YA 217

Mambo ya Edna yalikuwa ya kushangaza muda mwingine , siku mbili zote alikuwa amemchunia Roma na hakuongea neno lolote na yeye na alikuwa akijifanyisha kuwa bize , lakini sasa hivi baada ya Roma kupotea mbele yake alikuwa akilia kama mtoto.

Sophia , Bi Wema na Yezi walimuona Edna muda mwingine kama mtoto kutokana na mambo yake , kwani alikuwa mlaini mno likija swala la mahusiano.

“Miss nini kimetokea?”

“Alikuwa na hasira na nilipotaka kumfariji kapotea..”Aliongea Edna na Bi Wema ni kama hakumuelewa Edna vizuri.

Yaani Edna aliona ile alivyomsogelea Roma na akapotea akiwa kwenye hali kama ile ni kwamba hakutaka yeye amfariji na ndio maana aliona kaondoka kimazingara hapo ndani ukijumlisha pia na kitendo chake cha kumnunia Roma tokea walivyokuwa Ufaransa aliona kabisa Roma anamakasiriko na yeye.

Bi Wema walisikiliza kila kitu kutoka kwa Edna juu ya mambo walioongea na Afande Camillius Kweka na wote kwa Pamoja walishangaa na kufurahi kwa wakati mmoja , hawakuamini kama Roma familia yake imepatikana , jambo hili kwao halikuwa la huzuni bali furaha , kwani hata hivyo Roma alikuwa akiitafuta familia yake.

Sophia ndio aliekuwa wa kwanza kushika karatasi zilizoachwa na Afande Kweka na karatasi moja ya mwisho ilikuwa ni ya majibu ya DNA ya Roma na Afande Kweka.

“Kwahio Miss! , Roma na raisi Senga ni baba na Mwana?”

“Ndio..”Aliitikia Edna na wote wa wakangaliana kwa mshangao .

“Anko Roma atarudi nyumbani , hii taarifa ni kubwa kwake hivyo anahitaji muda wa kuwa peke yake”Aliongea Yezi na kasauti kake na wote walikubaliana na maneno yake , lakini kwa Edna licha ya kukubali alijihisi kuwa na hatia katika moyo wake.

*******

CHINA-BEIJING

Yan Buwen baada ya kuachwa na Athena kwenye chumba cha hoteli ya Hiltoni, alitoa simu yake na kupiga na ndani ya dakika kadhaa tu mlango wake uligongwa.

Alikuwa ni mwanamke mrembo sana wa Kichina aliekuwa amesimama mlangoni baadaya Yan Buwen kufungua mlango.

“Zhin Xhilin ulikuwa ndani ya hii hoteli nini?”Aliuliza Yan Buwen kwa lugha ya kichina.

“Mbona una maswali mengi Yan Buwen , haujafurahia kuja kwangu kwa haraka ,nipishe niingie”Aliongea Zhin Xhilin kwa kulalamika na ilibidi Yan Buwen kumruhusu mwanamke huyo kuingia ndani, alikuwa mrembo kweli ila kasoro yake akija hapa Tanzania wanaume wengi watakuwa na jibu linalofanana , kwani mwanamke huyo alikua Flat.

Zhin Xhillin ni mtoto wa raisi wa China na ni mpenzi wa Yan Buwen wa muda mrefu sana na Media nyingi wanatangaza hilo kila siku , lakini licha ya wawili hao kuwa katika mahusiano ya muda mrefu lakini hakuna siku hata moja ambayo walitangaza kufunga ndoa.

“Yan Buwen leo hatufanyi mpaka nijue msimamao wako kwangu”Aliongea.

“Msimamo gani tena , kumbuka wewe mwenyewe ndio ulinitongoza na ukaniambia unapenda watu wenye akili nyingi kama mimi na mimi nikakuambia kabisa siwezi kukupa moyo ambayo unamilikiwa na mtu mwingine”

“Ni kweli Yan Buwen nilifanya hivyo , lakini najua unanidanganya tu , unanipenda ndio maana , kama kweli moyo wako unamilikiwa na mtu mwingine huyo mtu ni nani mbona sijawahi kumuona kwenye Maisha yako”Aliongea kwa Kichina.

“Hutonielewa hata nikikuelezea wewe mwanamke , kifupi mwanamke ninaempenda ndio mzuri dunia yote hii na siku moja lazima nimmiliki , hivyo kama unanipa nipe, wewe si umesema unapenda watu Majiniasi, mimi ndio Jiniasi Yan Buwen nitaibadilisha hii dunia na yote itakuwa kiganjani kwangu”Aliongea Yan Buwen kwa kujigamba mbele ya Zhin Xhillin.

Na mrembo huyo alionekana kweli anampenda Yan Buwen licha ya kuambiwa maneno hayo ila aliishia kulala na Yan Buwen mpaka kukakucha.

“Damn it , Zhin xhillin unajua mama… unajua ila kasoro moja tu”

“Ipi hio Yan Buwen ukiniambia nibadilike nitabadilika kwa ajili yak..”

“Huwezi kunipa utamu tukiwa angani”Aliongea Yan Buwen huku akigugumia utamu kwani Zhin xhillin alikuwa akiendesha gari kwa spidi huku akinguruma na ni kama alikuwa akimkomoa Yan Buwen kwa maneno yake kwani alikuwa akiangusha huku ameshika masikio ya Yan Buwen.

“Nuinaweza kufanya hivyo Yan Buwen , nitakodi ndege kubwa ya kifahari kwa ajili yako usiwaze kuhusu pesa”

“Unaona sasa… unajua kwanini sikupendi na siwezi kuwa na wewe.. because you are damb Ass, nimesema angani, hewani sio kwenye ndege, mpuuzi wewe”Aliongea Yan Buwen kwa hasira na kumsukumia mrembo huyu mtoto wa raisi pembeni na Kwenda bafuni.

Maongezi hayo yalikuwa yakifanyika asubuhi hivyo Yan Buwen baada ya kumaliza kuoga alijiandaa na kutoka ndani ya hoteli hio akimuacha Zhin Xhillin kwenye mawazo.

“Yan Buwen unajifanya mjanja sana , lakini siku moja tu utanasa kwenye mtego wangu , I will Destroy you”Aliongea Zhin Xhillin kwa hasira huku akikunja ngumi.

Ni kama nusu saa hivi baada ya Yan Buwen kutoka ndani ya hoteli ya Hilton , alionekana upande wa mashariki mwa jiji hili la Beijing , sehemu iliokuwa ikifahamika kama Dragon Villa Garden , mtaa ambao matajiri wengi wanaishi.

Baada ya Yan Buwen kufikishwa na dereva wake ndani ya jumba moja la kifahari , moja kwa moja aliingia ndani na kuvua koti lake na kulitupia kwenye sofa na akalegeza na tai na kisha akasogelea Friji na kutoa maji na baada ya hapo alitembea upande mwingine wa jumba hili ambalo lilionekana yeye pekee ndio aliekuwa akiishi hapo na baada ya kufika kwenye mlango uliokuwa upande wa kushoto wa korido uliokuwa ukiangaliana na Swimming Pool , aliingiza nywira sehemu maalumu mlangoni na kisha akaweka jicho lake na mlango ule ulifunguka.

Ndani ya chumba alichoingia kilikuwa ni kama sehemu ya kujisomea kwani kulikuwa na makabati yaliojaa vitabu huku mbele yake kukiwa na meza ambayo ilikuwa na tarakishi ya Apple.

Yan Buween alisogelea Tarakishi ile na kisha akaiwasha na baada ya kumaliza kuiwasha na akasukuma mouse mpaka kwenye program ilikuwa na Icon ya jicho na kisha akabonyeza mara mbili na kioo chote kikabadilika rangi na kuwa nyeusi , program ile ilifunguka kama ‘Command Prompt’ .

Alianza kuandika maneno ya kichina anayoyajua yeye kwa dakika kadhaa mpaka tarakishi ile ilivyomletewa ‘Pattern’ na palepale alibonyeza kitufe cha Enter na palepale masanduku mawili ya vitabu yaliachiana , ni kama vile Lift na Yan Buwen aliingia ndani ya mlango uliojifungua na masanduku yakajifunga vilevile.

Dakika chache mbele alikuwa chini ya ‘Basement’ iliojengwa kwa usanifu wa hali ya juu sana , baada ya kufungua mlango upande wake wa kushoto , aliingia ndani na chumba alichoingia kilikuwa kama ofisi ya Secretary kwani kulikuwa na meza Pamoja na tarakishi kubwa ya Apple , alitumia utaratibu uleule wa mwanzo na mlio wa ‘Chwii.. Chwii”Na ukuta ulislide Kwenda pande mbili kwa namna ya Triangle.

Kwa nama ambavyo Yan Buwen anafanya ni kama vile kwenye muvi za Science Fiction.

Baada ya kuingia ndani hapo ndipo tunaweza sana kukuona bonge la maabara ya kisasa mno , ilikuwa na taa za Ultraviolet, mbele kabisa pande wa kushoto kuna meza kubwa ya mviringo yenye ramani ya dunia nzima , meza ya kio na juu yake kuna maboksi mawili ya mbao yaliosanifiwa vizuri

Yan Buwen aliyasogelea yale maboksi na juu yake yalikuwa na maandishi makubwa GODSTONE boksi la kwanza na ‘THANATOS , Boksi la pili.

Sasa hapa haikueleweka Athena alimaanisha nini kusema kwamba vitu hivyo vipo kwenye Safe Room ndani ya hoteli , nadhani alitumia maneno ya kimafumbo kufikisha ujumbe.

Yan Buwen alifungua lile boksi la kwanza na kisha alitoa Godstone na kuweka kwenye mikono yake na palepale jiwe lile kama kitenesi lilitoa mwanga mkali , ni kama lilimtambua Yan Buwen kama mmiliki kwani mwanga wake ulikuwa mkali kuliko ilivyokuwa kwa Roma na kwa Director, The First Black , hapa lilitoa mwanga mwingi kiasi kwamba hazikuhitajika hata taa kwani mng`ao wake ulikuwa wa ajabu mno na wenye nguvu.

“Ha,, ha,.. ha hahahahaha….. hahahahaha ….. hahaha…. Hahahah… God,, I am God hahaha.”Kama ni mzungu angesemema ‘He is Freaking out’ yaani Yan Buwen alicheka kama chizi.

Yan Buwen alipeleka jiwe lile na kuanza kulinusa nusa kama vile anatafuta harufu huku akiendelea kucheka na kuanza kuruka ruka juu.

“Denisiii… amka tufurahie … We are God… hahaha.. haha…”Aliongea Yan Buwen kwa furaha kubwa huku akisogea upande wa kulia uliokuwa kama korido kutokana na kuwa na makabati kama yale ya kuhifadhia maiti mochwari na aliponyeza bonyeza mbele ya kabati la kwanza na palepale kama mlango wa CD kabati lilitoka nje lote na kufunguka mlango kwa juu na palepale mwanaume ambaye kwa jinsi alivyokuwa akionekana kama vile amefunikwa na barafu alitoka kwenye lile kabati na kusimama chini huku bila ya Yan Buwen kutokuwa na Habari nae.

Kilikuwa ni kitendo cha dakika chache tu mwili wake wote ulibadilika na kurudi katika hali ya kawaida huku nywele zake fupi zote zikirudi katika Weusi wake , kasoro macho pekee yake yalikuwa kama ya Mbwa Mwitu(Wolf).

“Denisii..hahaha..”Aliongea Yan Buwen na kumkumbatia Denisi aliekuwa uchi wa mnyama.

“Ndio alikuwa ni Denisi Senga mtoto wa Raisi Senga na haikueleweka Yan Buwen alikuwa akimfanyia nini , ila alionekana kubadilika mno.
 
SEHEMU YA 218.

Haikueleweka Roma alikuwa wapi muda wote wa mchana ila muda wa usiku alikuwa ndani ya Upepo Beach Garden akijipatia Sea Food kutoka kwa mgahawa wa Mzee Chino , kwa jinsi alivyokuwa akifurahia msosi ni kama hakuna kilichotokea mchana.

Wakati akiendelea kufurahia na msosi wake , alijikuta akifumbwa macho na mikono milaini ya mtoto wa kike na kujikuta akiweka kijiko chini.

“Bebi Neema usiniambie Mzee Chino kakuambia nipo hapa”Aliongea Roma na mrembo yule akamuachia na ni kweli alikuwa ni Neema Luwazo , Naibu Waziri wa Sanaa na utamaduni.

“Sikutarajia kama nitakukuta hapa?”Aliongea Neema huku akiweka mkoba wake pembeni na kukaa kwenye kiti cha mbele yake Roma.

“Nikajua yule mzee ndio kakuambia nipo hapa”

“Hapana .. ila kwa nilivyokumisi nilitamani kukukipigia simu muda wowote, sikuwa sawa kimawazo tokea nimetoka bungeni”Aliongea Neema kwa sauti chini na kumfanya amwangalie mrembo huyu , licha ya kuonekana mtu mzima , ila alikuwa anaita na kuvutia balaa.

“Nadhani leo tunahitajiana kufarijiana , nimefika hapa kwasababu sikuwa kwenye mudi nzuri”

“Mh!, nilitegemea utakuwa kwenye mudi nzuri kutokana na Kwenda na mkeo Ufaransa”Aliongea Neema na kumkumbusha Roma kuhusu Edna , alikumbuka tokea siku wanarudi hawakuongea Zaidi ya Edna kujifanyisha kuwa bize na kumkwepa muda wote.

“Bebi Neema unakumbuka mara ya mwisho hatukumaliza , leo nadhani ni siku iliopangwa maana wote hatupo kwenye mudi”Aliongea Roma huku akimkonyeza Waziri na mwanamke huyu alijikuta akicheka kicheko cha kwikwi na haikueleweka alifurahishwa na nini.

Ila ndani ya nusu saa mbele walikuwa ndani ya hoteli ya Mapple huku Neema akiwa amekodolea bahari ya Hindi huku Roma akiwa nyuma yake akicheza Boringo na kwa upande wa Neema network zilikuwa zikija na kukata.

“Hehe… hii staili ya kuiangalia bahari inafurahisha,unaonaje”

“Roma… Arggh .. miguu”

“Imefanyaje tena”.

“Inakosa..aa nguvu” Aliongea Neema Luwazo kwa kulalamika na Roma alimbeba juu juu na Kwenda kumtupia kitandani na kilichoendelea ni Neema kuyaita maji MMA”

Muda wa asubuhi saa mbili ndio Roma alifika Kigamboni kwa kutumia V8 mpyaa , yenye namba za serikali, na Roma alikuwa akiendeshwa na Dereva wa Neema Luwazo na Roma hakutaka kuingia nayo ndani na ndio maana baada ya kufika getini ilisimama na yeye akashuka.

Edna alionekana bado hakwenda kazini kwani gari yake anayoipenda kuitumia ilikuwepo , ila Roma hakujali sana alipiga hatua na Kwenda ndani na Sebule ilionekana kupoa sana, kwani hata Bi Wema hakuonekana kabisa sebuleni kama Alivyozoea , lakini Roma aliamini atakuwa amepumzika.

Roma aliingia kwenye chumba chake na kisha alivua nguo na kubadilisha zingine, alikuwa na mpango wa Kwenda kazini muda huo na ndio maana aliwahi kurudi.

Lakini baada tu ya kumaliza kuvaa koti, mlango wake ulifunguliwa bila hodi na ile anainua macho yake Edna alionekana kwenye mavazi ya kawaida kama mtu asiekuwa na mpango wa Kwenda kazini alionekana akimsogelea Roma kwa kasi na kumkumbatia Roma.

Jana yake usiku tokea Roma aondoke Edna hakulala kabisa , alikesha mpaka saa saba usiku akimsubiria Rona mpaka pale alipopotelea usingizini akiwa kwenye sofa na Bi Wema ndio aliekuja kumuamsha na kumwambia akalale chumbani.

Roma alishangazwa na kupokewa na kumbatio lililoambatana na kilio, Roma alijiambia siku zote Edna atakuwa mbabe tu mbele za watu akiwa kwenye biashara zake lakini alikuwa mdhaifu sana likija swala la mahusiano , alipewa mchunio wa siku mbili zote lakini leo hii anakumbatiwa na kilio juu.

“Wife una machozi ya karibu mno.. ndio mana unazidi kuwa M’cute”Aliongea Roma akiwangalie Edna akiwa ameshika mabegani kwa mikono miwili na Edna aliona aibu na kuangalia chini.

“Ulikuwa wapi nilikuwa na wasiwasi , na umeamua nini?”Aliuliza Edna maswali mawili kwa mpigo na Roma ilibidi amkalishe Edna kwenye kitanda kwanza.

“Nianze kukujibu swali lipi?”

“Ni jibu swali la pili?”

“Unamaanisha kuhusu yule Kikongwe asie na akili aliekuja kubwabwaja jana, nimeamua kumpotezea”Aliongea Roma kwa sauti ya kawaida , lakini kwa Edna lilionekana jibu la kuumiza , aliamini Roma anaficha kile anachojisikia moyoni kwa kuamua kupotezea.

“Roma najua unajisikia vibaya kwa muda huu na hujui cha kufanya na ndio maana unaamua kupotezea , sijui nini kilichotokea lakini katika mazungumzo yote nimezingatia sana maneno ya mwisho ya Afande Kweka”Aliongea Edna..

“Yapi hayo?”

“Kuhusu mama yako , amesema anateseka na aliteseka sana kwa ajili yako , Roma unajua nilichojisikia siku nilivyosikika baba yangu ambaye nilijua ni mzazi wangu wa damu siku nilivyopokea kifo chake..”

“Ile siku nilijutia sana kutokwenda kumtembelea na kumuona hata mara moja , licha ya kwamba hakuwahi kunipenda kwenye Maisha yangu yote , lakini iliniuma baada ya kuambiwa kafariki kabla sijamuoa kwa mara ya mwisho”

“Ninachomaanisha ni kwamba wanandoa wanaweza kupeana talaka , marafiki wanaweza wakageukana na kuwa maadui lakini upendo wa mama kwa mtoto siku zote ni wa kudumu na hakuna kitu ambacho kinaweza kumtenganisha mtoto na familia yake .. nakushauri umfikirie mama yako kwa muda huu , najua unaumia na mimi pia najisikia vibaya kwa ajili yako, Usilipotezee hili swala kama vile haujaufahamu ukweli”Aliongea Edna na maneno yalionekana kumwingina Roma vizuri na hata hivyo moja ya misheni yake ilikuwa ni kurudi Tanzania kutafuta familia yake na kuwauliza kwanini walimtelekeza na akajikuta kwenye mikono ya watu waliomtesa.

Roma aliona maneno ya Edna yana ukweli ndani yake , licha mpaka muda huo hakujua ni nini kilichotokea , lakini kama mama yake anateseka kama alivyosema Mzee Kweka aliona anasababu ya kuchukua hatua.

“Una akili sana mke wangu.. kesho nitaenda kumleta Mama Mkwe wako”Aliongea Roma na kumfanya Edna kutabasamu.

Upande mwingine ndani ya familia ya Mzee Atanasi , Jestina alikuwa na furaha isiokuwa ya kawaida mara baada ya kusikia taarifa ya Mzee Kweka kumtembelea Roma.

Kile kilio chake alichokuwa nacho cha kumsaidia dada yake aliamini kinakwenda kujibiwa , hakuweza kujua ni kwa namna gani Blandina dada yake atakuwa na mshangao baada ya kumuona Roma.

*******

Blandina tokea siku aweke msimamo wake juu ya kutotaka kuvaa sura ya bandia tena , swala hili lilifanya kuwe na ugomvi mkubwa sana na mume wake Kamau Kamau.

Mwanamke huyu licha ya kwamba ni siku kadhaa tu tokea atoke Tanzania , lakini pia kujua kuwa mwanae Denis yupo hai , alionekana kukokanda ghafla , haikueleweka kinachomkondesha ni kitendo cha kamau kutomruhusu Kwenda kuonana na mwanae au kuna sababu nyingine.

Wakati Maina akiwa amejilaza chumbani kwake , chini ya ulinzi mkali wa walinzi wa ikulu , mlango wa chumbani kwake ulifunguliwa na akaingia Kamau Kamai raisi wa Kenya.

Kamau alimwangalie mke wake aliekuwa akikodolea picha zilizokuwa kwenye mikono yake na Kamau jambo lile lilimkasirisha sana na aliingia kwa pupa na kumpokonya zile picha na kisha akazichana chana na kumfanya Blandina kuanza kulia.

“Kamau kwanini lakini … nakuliza kwanini umechana picha za Denis , unajua ni kiasi gani nimemkumbika mwana…”

“Paaah!”

Kamau alikasirika maradufu kila mara alipokuwa akisikia jina la Denisi , yaani kwa jinsi alivyomuona Maina haikuwa na tofauti na miaka ishirini na tano iliopita , Blandina amerudi kuwa Blandina yule yule anaempenda mtoto wake kuliko kitu kingine na hakujali tena nafasi yake kama mke wa raisi.

Blandina licha ya kupigwa kibao , wala hakujali alimwangalia Kamau huku machozi yakimtiririka na kuchuchumaa chini na kuanza kukusanya vipande vipande vya picha za utotoni alizokuwa amepatiwa na Linda , msaidizi wa karibu wa Raisi Jeremy.

“Maina utakuwa hivi mpaka lini mke wangu?”

“Mimi sio Maina , niache Kamau…”Aliongea Blandina na kusimama na kusogela kitandani na kuanza kupanga upya picha za Denisi , kwa jinsi alivyokuwa akionekana ni kama akili zimruka kidogo , hakuonekana kama yule mama ambaye anasaidia Watoto Yatima tena.

Kamau kwa jinsi alivyomuona Mke wake aliona kabisa hawezi kumrudisha kwenye hali yake ya kawaida na alipaswa kukubali ukweli kwamba muda huo Blandina alichokuwa akikiwaza kwenye kichwa chake ni Denisi tu.

Alikaa takribani dakika kumi na tano akiangalia kile ambacho Maina anakifanya na ilimchukua dakika kama tano tu hivi kwa Maina kuweza kuunganisha vipande vyote vya picha vilivyokuwa vimechanwa na Mheshimiwa Kamau na Maina alitabasamu baada ya zoezi lake kufanikiwa.

Noo.. Siwezi kukubaliana na mpango wa Mwambai , Hades kitu gani bwana akija Kenya namuua”Aliwaza Raisi Kamau na kisha alisogea mpaka kitandani na kisha akampokonya Blandina picha zile na kutoka nazo na kumuacha mwanamke huyo akitoa ukulele wa kilio ndani ya chumba, ila hakujali , na walinzi waliokuwa nje ya chumba cha Blandina First Lady waliishia kushikwa na huzuni.

“Ni mimi…”Alionekana Kamau akiongea na simu.

“Ndio mheshimiwa”

“Nataka ufanye mpango, kuna mwanamke analetwa hapo kambini , nataka ulinzi juu yake uimarishwe kwa masaa ishirini na nne na yoyote ataketaka kuongea nae , lazima ruhusa itoke kwangu”

“Sawa mheshimiwa , lakini tunaweza kumfahamu huyo mwanamke?”

“Hilo sio juu yako , ninachotaka ni ulinzi kwake , maswali mengi sitaki”Aliongea Mheshimiwa na kukata simu na kurudi alikotoka.

“Njiro nifuate”Aliongea Kamau na Njiro mlinzi wa First Lady alimfuatisha Kamau mpaka kwenye ofisi yake.

“Ndio mheshimiwa”

“Nataka mfanye utaratibu na mke wangu atapelekwa Kambi ya Moi Airbase kwa ajili ya usalama wake”Aliongea Mheshimiwa Kamau na kumfanya Njiro kushangaa.

“Kwanini mhesh..”

“Fanya utaratibu wa mke wangu kuepelekwa huko , na jambo hilo liwe siri , hakuna mtu anaeruhusiwa kumjua Blandina ndio Maina , nafikiri unajua ninchomaanisha, unaweza Kwenda”

“Sawa mheshimiwa”Aliongea Njiro

“Nishaongea na mkuu wa Kambi hivyo kazi yenu ni kumfikisha tu , hakikisha unampa maelezo ya kupewa huduma nzuri”

“Sawa mheshimiwa”Aliongea Njiro na kutoka kwa ajili ya Blandina kupelekwa kambi ya Moi.

ITAEND3LEA

HAYA NIMEWAPUNGUZIA LIPENI 2000 MKUKE WATSAPP TUENDELEE TUPO 278 NICHEKI 0687151346.WATSAPP ONLY
 
SEHEMU YA 218.

Haikueleweka Roma alikuwa wapi muda wote wa mchana ila muda wa usiku alikuwa ndani ya Upepo Beach Garden akijipatia Sea Food kutoka kwa mgahawa wa Mzee Chino , kwa jinsi alivyokuwa akifurahia msosi ni kama hakuna kilichotokea mchana.

Wakati akiendelea kufurahia na msosi wake , alijikuta akifumbwa macho na mikono milaini ya mtoto wa kike na kujikuta akiweka kijiko chini.

“Bebi Neema usiniambie Mzee Chino kakuambia nipo hapa”Aliongea Roma na mrembo yule akamuachia na ni kweli alikuwa ni Neema Luwazo , Naibu Waziri wa Sanaa na utamaduni.

“Sikutarajia kama nitakukuta hapa?”Aliongea Neema huku akiweka mkoba wake pembeni na kukaa kwenye kiti cha mbele yake Roma.

“Nikajua yule mzee ndio kakuambia nipo hapa”

“Hapana .. ila kwa nilivyokumisi nilitamani kukukipigia simu muda wowote, sikuwa sawa kimawazo tokea nimetoka bungeni”Aliongea Neema kwa sauti chini na kumfanya amwangalie mrembo huyu , licha ya kuonekana mtu mzima , ila alikuwa anaita na kuvutia balaa.

“Nadhani leo tunahitajiana kufarijiana , nimefika hapa kwasababu sikuwa kwenye mudi nzuri”

“Mh!, nilitegemea utakuwa kwenye mudi nzuri kutokana na Kwenda na mkeo Ufaransa”Aliongea Neema na kumkumbusha Roma kuhusu Edna , alikumbuka tokea siku wanarudi hawakuongea Zaidi ya Edna kujifanyisha kuwa bize na kumkwepa muda wote.

“Bebi Neema unakumbuka mara ya mwisho hatukumaliza , leo nadhani ni siku iliopangwa maana wote hatupo kwenye mudi”Aliongea Roma huku akimkonyeza Waziri na mwanamke huyu alijikuta akicheka kicheko cha kwikwi na haikueleweka alifurahishwa na nini.

Ila ndani ya nusu saa mbele walikuwa ndani ya hoteli ya Mapple huku Neema akiwa amekodolea bahari ya Hindi huku Roma akiwa nyuma yake akicheza Boringo na kwa upande wa Neema network zilikuwa zikija na kukata.

“Hehe… hii staili ya kuiangalia bahari inafurahisha,unaonaje”

“Roma… Arggh .. miguu”

“Imefanyaje tena”.

“Inakosa..aa nguvu” Aliongea Neema Luwazo kwa kulalamika na Roma alimbeba juu juu na Kwenda kumtupia kitandani na kilichoendelea ni Neema kuyaita maji MMA”

Muda wa asubuhi saa mbili ndio Roma alifika Kigamboni kwa kutumia V8 mpyaa , yenye namba za serikali, na Roma alikuwa akiendeshwa na Dereva wa Neema Luwazo na Roma hakutaka kuingia nayo ndani na ndio maana baada ya kufika getini ilisimama na yeye akashuka.

Edna alionekana bado hakwenda kazini kwani gari yake anayoipenda kuitumia ilikuwepo , ila Roma hakujali sana alipiga hatua na Kwenda ndani na Sebule ilionekana kupoa sana, kwani hata Bi Wema hakuonekana kabisa sebuleni kama Alivyozoea , lakini Roma aliamini atakuwa amepumzika.

Roma aliingia kwenye chumba chake na kisha alivua nguo na kubadilisha zingine, alikuwa na mpango wa Kwenda kazini muda huo na ndio maana aliwahi kurudi.

Lakini baada tu ya kumaliza kuvaa koti, mlango wake ulifunguliwa bila hodi na ile anainua macho yake Edna alionekana kwenye mavazi ya kawaida kama mtu asiekuwa na mpango wa Kwenda kazini alionekana akimsogelea Roma kwa kasi na kumkumbatia Roma.

Jana yake usiku tokea Roma aondoke Edna hakulala kabisa , alikesha mpaka saa saba usiku akimsubiria Rona mpaka pale alipopotelea usingizini akiwa kwenye sofa na Bi Wema ndio aliekuja kumuamsha na kumwambia akalale chumbani.

Roma alishangazwa na kupokewa na kumbatio lililoambatana na kilio, Roma alijiambia siku zote Edna atakuwa mbabe tu mbele za watu akiwa kwenye biashara zake lakini alikuwa mdhaifu sana likija swala la mahusiano , alipewa mchunio wa siku mbili zote lakini leo hii anakumbatiwa na kilio juu.

“Wife una machozi ya karibu mno.. ndio mana unazidi kuwa M’cute”Aliongea Roma akiwangalie Edna akiwa ameshika mabegani kwa mikono miwili na Edna aliona aibu na kuangalia chini.

“Ulikuwa wapi nilikuwa na wasiwasi , na umeamua nini?”Aliuliza Edna maswali mawili kwa mpigo na Roma ilibidi amkalishe Edna kwenye kitanda kwanza.

“Nianze kukujibu swali lipi?”

“Ni jibu swali la pili?”

“Unamaanisha kuhusu yule Kikongwe asie na akili aliekuja kubwabwaja jana, nimeamua kumpotezea”Aliongea Roma kwa sauti ya kawaida , lakini kwa Edna lilionekana jibu la kuumiza , aliamini Roma anaficha kile anachojisikia moyoni kwa kuamua kupotezea.

“Roma najua unajisikia vibaya kwa muda huu na hujui cha kufanya na ndio maana unaamua kupotezea , sijui nini kilichotokea lakini katika mazungumzo yote nimezingatia sana maneno ya mwisho ya Afande Kweka”Aliongea Edna..

“Yapi hayo?”

“Kuhusu mama yako , amesema anateseka na aliteseka sana kwa ajili yako , Roma unajua nilichojisikia siku nilivyosikika baba yangu ambaye nilijua ni mzazi wangu wa damu siku nilivyopokea kifo chake..”

“Ile siku nilijutia sana kutokwenda kumtembelea na kumuona hata mara moja , licha ya kwamba hakuwahi kunipenda kwenye Maisha yangu yote , lakini iliniuma baada ya kuambiwa kafariki kabla sijamuoa kwa mara ya mwisho”

“Ninachomaanisha ni kwamba wanandoa wanaweza kupeana talaka , marafiki wanaweza wakageukana na kuwa maadui lakini upendo wa mama kwa mtoto siku zote ni wa kudumu na hakuna kitu ambacho kinaweza kumtenganisha mtoto na familia yake .. nakushauri umfikirie mama yako kwa muda huu , najua unaumia na mimi pia najisikia vibaya kwa ajili yako, Usilipotezee hili swala kama vile haujaufahamu ukweli”Aliongea Edna na maneno yalionekana kumwingina Roma vizuri na hata hivyo moja ya misheni yake ilikuwa ni kurudi Tanzania kutafuta familia yake na kuwauliza kwanini walimtelekeza na akajikuta kwenye mikono ya watu waliomtesa.

Roma aliona maneno ya Edna yana ukweli ndani yake , licha mpaka muda huo hakujua ni nini kilichotokea , lakini kama mama yake anateseka kama alivyosema Mzee Kweka aliona anasababu ya kuchukua hatua.

“Una akili sana mke wangu.. kesho nitaenda kumleta Mama Mkwe wako”Aliongea Roma na kumfanya Edna kutabasamu.

Upande mwingine ndani ya familia ya Mzee Atanasi , Jestina alikuwa na furaha isiokuwa ya kawaida mara baada ya kusikia taarifa ya Mzee Kweka kumtembelea Roma.

Kile kilio chake alichokuwa nacho cha kumsaidia dada yake aliamini kinakwenda kujibiwa , hakuweza kujua ni kwa namna gani Blandina dada yake atakuwa na mshangao baada ya kumuona Roma.

*******

Blandina tokea siku aweke msimamo wake juu ya kutotaka kuvaa sura ya bandia tena , swala hili lilifanya kuwe na ugomvi mkubwa sana na mume wake Kamau Kamau.

Mwanamke huyu licha ya kwamba ni siku kadhaa tu tokea atoke Tanzania , lakini pia kujua kuwa mwanae Denis yupo hai , alionekana kukokanda ghafla , haikueleweka kinachomkondesha ni kitendo cha kamau kutomruhusu Kwenda kuonana na mwanae au kuna sababu nyingine.

Wakati Maina akiwa amejilaza chumbani kwake , chini ya ulinzi mkali wa walinzi wa ikulu , mlango wa chumbani kwake ulifunguliwa na akaingia Kamau Kamai raisi wa Kenya.

Kamau alimwangalie mke wake aliekuwa akikodolea picha zilizokuwa kwenye mikono yake na Kamau jambo lile lilimkasirisha sana na aliingia kwa pupa na kumpokonya zile picha na kisha akazichana chana na kumfanya Blandina kuanza kulia.

“Kamau kwanini lakini … nakuliza kwanini umechana picha za Denis , unajua ni kiasi gani nimemkumbika mwana…”

“Paaah!”

Kamau alikasirika maradufu kila mara alipokuwa akisikia jina la Denisi , yaani kwa jinsi alivyomuona Maina haikuwa na tofauti na miaka ishirini na tano iliopita , Blandina amerudi kuwa Blandina yule yule anaempenda mtoto wake kuliko kitu kingine na hakujali tena nafasi yake kama mke wa raisi.

Blandina licha ya kupigwa kibao , wala hakujali alimwangalia Kamau huku machozi yakimtiririka na kuchuchumaa chini na kuanza kukusanya vipande vipande vya picha za utotoni alizokuwa amepatiwa na Linda , msaidizi wa karibu wa Raisi Jeremy.

“Maina utakuwa hivi mpaka lini mke wangu?”

“Mimi sio Maina , niache Kamau…”Aliongea Blandina na kusimama na kusogela kitandani na kuanza kupanga upya picha za Denisi , kwa jinsi alivyokuwa akionekana ni kama akili zimruka kidogo , hakuonekana kama yule mama ambaye anasaidia Watoto Yatima tena.

Kamau kwa jinsi alivyomuona Mke wake aliona kabisa hawezi kumrudisha kwenye hali yake ya kawaida na alipaswa kukubali ukweli kwamba muda huo Blandina alichokuwa akikiwaza kwenye kichwa chake ni Denisi tu.

Alikaa takribani dakika kumi na tano akiangalia kile ambacho Maina anakifanya na ilimchukua dakika kama tano tu hivi kwa Maina kuweza kuunganisha vipande vyote vya picha vilivyokuwa vimechanwa na Mheshimiwa Kamau na Maina alitabasamu baada ya zoezi lake kufanikiwa.

Noo.. Siwezi kukubaliana na mpango wa Mwambai , Hades kitu gani bwana akija Kenya namuua”Aliwaza Raisi Kamau na kisha alisogea mpaka kitandani na kisha akampokonya Blandina picha zile na kutoka nazo na kumuacha mwanamke huyo akitoa ukulele wa kilio ndani ya chumba, ila hakujali , na walinzi waliokuwa nje ya chumba cha Blandina First Lady waliishia kushikwa na huzuni.

“Ni mimi…”Alionekana Kamau akiongea na simu.

“Ndio mheshimiwa”

“Nataka ufanye mpango, kuna mwanamke analetwa hapo kambini , nataka ulinzi juu yake uimarishwe kwa masaa ishirini na nne na yoyote ataketaka kuongea nae , lazima ruhusa itoke kwangu”

“Sawa mheshimiwa , lakini tunaweza kumfahamu huyo mwanamke?”

“Hilo sio juu yako , ninachotaka ni ulinzi kwake , maswali mengi sitaki”Aliongea Mheshimiwa na kukata simu na kurudi alikotoka.

“Njiro nifuate”Aliongea Kamau na Njiro mlinzi wa First Lady alimfuatisha Kamau mpaka kwenye ofisi yake.

“Ndio mheshimiwa”

“Nataka mfanye utaratibu na mke wangu atapelekwa Kambi ya Moi Airbase kwa ajili ya usalama wake”Aliongea Mheshimiwa Kamau na kumfanya Njiro kushangaa.

“Kwanini mhesh..”

“Fanya utaratibu wa mke wangu kuepelekwa huko , na jambo hilo liwe siri , hakuna mtu anaeruhusiwa kumjua Blandina ndio Maina , nafikiri unajua ninchomaanisha, unaweza Kwenda”

“Sawa mheshimiwa”Aliongea Njiro

“Nishaongea na mkuu wa Kambi hivyo kazi yenu ni kumfikisha tu , hakikisha unampa maelezo ya kupewa huduma nzuri”

“Sawa mheshimiwa”Aliongea Njiro na kutoka kwa ajili ya Blandina kupelekwa kambi ya Moi.

ITAEND3LEA

HAYA NIMEWAPUNGUZIA LIPENI 2000 MKUKE WATSAPP TUENDELEE TUPO 278 NICHEKI 0687151346.WATSAPP ONLY
Kule watisap Iko mbali
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom