Simulizi ya Dorcas 01 Mtunzi Juma Hiza

Simulizi ya Dorcas 01 Mtunzi Juma Hiza

*DORCAS-16*


Kulipokucha na majirani kukusanyika, yule bwana aliyekuwa anapenda kuniita mjomba, alishauri mama atumiwe taarifa kuhusiana na msiba wa mwanangu.

Hata hivyo, akina babu wawili walisema ni sawa lakini walishauri mwanangu azikwe siku ileile kwa sababu alikuwa bado mdogo kwa sababu hakukuwa na ulazima wa kumsubiri mama.

Pilikapilika za mazishi ziliendelea na ilipofika saa sita, alikuja mtumishi wa Mungu ikafanyika ibada ya mazishi
Baada ya msiba baadhi ya akina mama waliniuliza historia yangu lakini sikutaka kuwaambia ukweli zaidi ya kuwafahamisha kwamba mama yangu alifariki dunia na kwamba alikuwa rafiki wa mama wa Shinyanga.

Waliponiuliza kuhusu baba wa mtoto wangu, niliwadanganya kwamba kulikuwa na kijana alinirubuni na kunipa ujauzito kisha kutoweka ndipo mama akaamua kunipeleka kule kijiji nikae kwa bibi.

Akina mama hao walihuzunishwa na taarifa niliyowapa ambapo yule mama niliyekuwa napenda kwenda kwake alinipa moyo kwamba kila binadamu hukumbana na mitihani hivyo nisihuzunike sana.

Mama huyo aliongeza kuniambia, kikubwa ni kujifunza baada ya kukosea awali ili nisirudie tena kosa.

Alipotoa kauli hiyo niliumia sana moyoni kwa sababu tangu nilipojitambua nilikuwa makini ila Evance ndiye aliyeniingiza kwenye matatizo baada ya kunibaka.

Hata hivyo, sikuwa na jinsi zaidi kumshukuru Mungu na kupanga kuondoka kule kijijini kwa njia yoyote na kurudi mjini ambapo pia nilipanga nisingekaa ningeenda Mbeya kwa mama mkubwa.

Kila nilipokumbuka maisha ya upendo niliyoishi nilipokuwa na marehemu mama na mama mkubwa wa Mbeya, nilijuta kwa nini nilikubali kwenda kuishi Shinyanga.

“Kama ningekuwa Mbeya kwa mama mkubwa, wala nisingebakwa na kupata mimba na kutelekezwa huku kijijini kama vile sina thamani,” nilijikuta nikiwaza moyoni.

Wiki moja baada ya msiba wa mwenzangu sikuona sababu ya kuendelea kuishi kule kijijini, siku moja usiku nikiwa nimeketi na bibi nilimwambia anipatie nauli ili nirudi mjini.

Bibi aliniambia kwamba nisubiri mpaka mama atakapokuja, kauli yake ilinitibua nikamweleza kwa kitendo cha mama kunitelekeza kule bila msaada wowote sikuwa na sababu ya kumsubiri.

Licha ya umri wangu mdogo, nilimwambia bibi mwanaye alikuwa mtu mbaya sana na kumwuliza kama mjukuu wake Emmy ndiye angekuwa alipewa mimba angefanya kama alivyonifanyia.

Kumtetea mwanaye, bibi aliambia kwa anavyomfahamu mama akufanya vile kwa makusudi isipokuwa alihisi kuna jambo lilimbana hivyo nisimuwazie vibaya.

Nilimweleza hata kama angekuwa kabanwa hakunitendea haki kunipeleka kijijini huku akijua nilikuwa mjamzito afadhali hata kama angemtuma mama mdogo aje kuniangalia lakini wote hawakufanya hivyo.

Baada ya kuzungumza mengi na bibi, nilimwomba anitafutie nauli hata kwa kukopa kwa majira zake ili niende mjini, akaniambia nisubiri kukicha atanipa jibu.

Asubuhi bibi aliniaga kwamba anatoka kidogo ambapo alirejea kwenye saa tatu hivi akanimbia alizungumza na mtu mmoja aliyemuahidi kumpatia fedha jioni ya siku hiyo.

Taarifa hiyo ilinifurahisha, nilimsaidia bibi kazi mbalimbali na jioni ilipofika bibi aliondoka aliporejea aliniambia nijiandae kwa safari ya mjini siku iliyofuata.

Nilimshuru bibi, usiku huo niliweka nguo na vitu vyangu kwenye begi tayari kwa alfajiri kuanza safari, bibi aliponiuliza kama ningeweza kufika mwenyewe nikamwambia ningefika.

Kulipokucha, bibi alinisindikiza hadi sehemu ya kupandia magari tukakuta canter moja ikiwa imejaza watu na mizigo, nami nikapanda ambapo hatukukaa sana safari ikaanza.

Tulisafiri kwa muda mrefu ndipo tuliingia Shinyanga mjini, kwa kuwa nilikuwa mwenyeji niliposhuka kwenye gari nikabeba begi langu na kuanza kuelekea nyumbani.

Njiani watu waliokuwa wakinifahamu walinishangaa na kuniuliza mbona nilibadilika sana, badala ya kuwajibu nilianza kulia.

“Dorcas umepatwa na tatizo gani linalokufanya ulie?” dada aitwaye Jasmini alimwuliza.

“Nyie niacheni tu,” Dorcas aliwaambia.
Licha ya kuwaambia wamuache tu, Jasmini aliyehisi huenda Dorcas alikuwa na tatizo kubwa akazidi kumbana ili amwambie kilichomliza ndipo aliwadanganya kwamba alimkumbuka marehemu mama yake.

“Ooh jamani kumbe umefiwa na mama yako?” Jasmini alimwuliza.
Dorcas aliwajibu ndiyo ndipo wakazidi kumpa pole na kumwambia alikuwa na sababu ya kudhoofu kwani kufiwa na mama lilikuwa tatizo kubwa.

“Ndiyo hivyo, yaani kila ninapomkumbuka mama naumia sana,” Dorcas aliwaambia bila kujua kama kilichomliza ni kitendo cha kikatili alichofanyiwa na Evance pamoja na mama yake aliyemtelekeza kijijini.

Kwa kuwa wakati nazungumza na dada Jasmini na mwenzake ambaye sikumfahamu tulikuwa tumesimama, niliagana nao na kuelekea nyumbani.
Nilipokaribia kufika, rafiki zangu Ester na Kalunde waliponiona walinikimbilia wakanilaki kwa furaha kisha kunipokea begi, tukaongozana kwenda nyumbani.

Marafiki zangu hao, kama alivyofanya dada Jasmini, waliniuliza kama nilikuwa naumwa kwa sababu nilikuwa nimekonda na kubadilika tofauti na nilivyokuwa awali kabla sijaondoka.

Pia walinilaumu kufuatia kuondoka bila kuwaaga, niliwaambia niliondoka ghafla na kwamba hali ya hewa ya nilikokuwa ilinikataa kwani mara kwa mara nilikuwa naugua malaria.

Tulipofika nyumbani, Ester ndiye alibisha hodi na hatukukaa muda mrefu pale mlango Emmy alifungua mlango, aliponiona alinirukia kwa furaha!
Emmy ambaye naye hakufahamu jambo lililoniondoa pale nyumbani alifurahi sana na kunieleza alikuwa kanimisi sana, alibeba begi langu na kulipeleka chumbani.

Tukiwa tumeketi sebuleni nilimuuliza alikokuwa mama akaniambia alikwenda Mwanza kwenye shughuli zake za biashara, nilipomuuliza pia kuhusu mama mdogo akaniambia alikwenda Tabora kwa mzazi mwenzake.

Emmy alinifahamisha kwamba pale nyumbani alibaki na mama yake mkubwa, Edina na dada wa kazi ambaye wakati huo alikuwa ametoka.

Wakati tukizungumza, alikuja mama mmoja ambaye sikumfahamu kutokea kwenye korido ya kwenda vyumbani, mimi na akina Ester tulimwamkia.

“Dada Dorcas huyu hapa ni mama mkubwa anaishia Bariadi, mama mkubwa huyu ni dada Dorcas amefika muda mfupi uliopita,” Emmy alitoa utambulisho.

Mama huyo alinipa pole kwa safari na kunikaribisha lakini kwa nilihisi kama alikuwa anataka kuuliza jambo fulani akasita, baada ya muda akina Ester waliaga.

Kutokana na uchovu wa safari sikuwasindikiza badala yake Emmy alifanya zoezi hilo, tukiwa tumebaki na mama mkubwa aliniuliza mtoto wangu alikuwa wapi!

Kufuatia swali hilo nilijua alikuwa kaelezwa kila kitu na mama, swali lake lilinikumbusha mwanangu na ukatili niliofanyiwa, nikaanza kulia.

Mama mkubwa aliponiuliza sababu za kulia, nilimfahamisha kuwa mwanangu alifariki dunia siku chache zilizopita, taarifa hiyo ilimhuzunisha akanipa pole.
Nilimuuliza kama hawakupata taarifa ya msiba, akaniambia hakufahamu chochote, nikamwambia hivyo ndivyo ilivyotokea, akanipa pole tena.

Wakati tunaendelea kuzungumza na mama huyo, Emmy alifika ndipo tulisitisha maongezi yaliyohusiana na kifo cha mwanangu, Emmy aliyekuwa akinipenda aliniandalia maji ya kuoga nikaenda chumbani nikabadili nguo na kwenda bafuni.

Niliporejea sebuleni, nilikuta Emmy kaniandalia chakula na wakati napata mlo dada wa kazi alirejea tulisabahiana na Emmy akanitambulisha kwake.

Usiku nikiwa chumbani na Emmy, aliniuliza mbona nilirejea nyumbani kabla ya shule kufungwa, nilimdanganya kwamba nilikuwa naumwa hivyo niliomba ruhusa, akanipa pole.

Baada ya kupiga stori za hapa na pale, Emmy alipitiwa na usingizi lakini kwa upande wangu sikupata hata tone la usingizi badala yake nilisongwa na mawazo kuhusiana na kitendo nilichofanyiwa na watu wawili, mama na Evance.

Kutokana na kuwaza kwa muda mrefu nikapatwa na hasira nikaanza kulia, wakati huo Emmy alikuwa akiuchapa usingizi wa pono nikaamua kuchukua uamuzi mzito.

Licha ya kwamba sikuwa na fedha, nilipanga kukicha kuondoka Shinyanga na kwenda Mbeya kwa mama mkubwa ambaye niliamini ndiye aliyechukua nafasi ya marehemu mama.

Usiku huo Emmy akiwa amelala, nilikumbuka mama alikuwa akipenda kumuachia fedha za kutosha kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na dharura zingine, nikaamka na kufungua kabati.

Baada ya kufanya hivyo, niliiona pochi ambayo Emmy alikuwa akihifadhia vitu nikahisi ilikuwa na fedha alizoachiwa na mama, nilipoifungua nikaona ilikuwa na noti za shilingi elfu kumi ambazo sikujua idadi yake.

Je, nini kitaendelea?
 
*DORCAS-17*


Baada ya kufanya hivyo, niliiona pochi ambayo Emmy alikuwa akihifadhia vitu nikahisi ilikuwa na fedha alizoachiwa na mama, nilipoifungua nikaona ilikuwa na noti za shilingi elfu kumi ambazo sikujua idadi yake.

Kwa kuwa lengo langu lilikuwa kuchukua kiasi cha fedha kwa ajili ya nauli ya kwenda Mbeya, nilizihesabu na kubaini ilikuwa shilingi hamsini na nne elfu, nikachukua elfu thelathini.

Kiasi hicho cha fedha niliamini kingenifikisha Mbeya bila matatizo, sikupenda kuchua fedha zote kuhofia ningewapa usumbufu wa kukosa fedha za matumizi wakati sikujua mama angerudi lini.

Baada ya kufanya hivyo, nilizihifadhi kwenye moja ya mifuko ya siketi yangu kisha nilichukua karatasi na kuandika ujumbe ambao hadi leo naukumbuka vizuri.

Ujumbe huo niliandika maneno haya: Emmy mimi Dorcas siyo mwizi na sitakuja kufanya kitendo hicho katika maisha yangu hata kama nitakumbana na wakati mgumu kiasi gani.

Kutokana na sababu ambazo zipo nje ya uwezo wangu nimefungua kabati na kukuta pochi yako ambayo ndani ilikuwa na shilingi hamsini na nne elfu, nimechukua shilingi elfu thelathini.

Najua nitakuwa nimeharibu bajeti yenu wakati huu mama akiwa hayupo lakini naomba mnisamehe kwa sababu sina jinsi nimeamua kuchukua fedha hizo ili nifanye nauli ya kwenda kwa mama mkubwa Mbeya.

Naomba Mungu unisamehe kwa kosa nililofanya kwa sababu sina jinsi, naomba mbaki salama na kwa amani kama Mungu akipenda tuonane tutaonana na asipopenda ipo siku tutaonana mbinguni, nakupenda sana Emmy kuliko mama na Evance.
Niombee nifike salama huko niendako, mimi Dorcas.

Nilipoandika ujumbe huo niliuweka ndani ya pocho niliyochukua zile fedha, nikaweka magauni yangu mawili ndani ya begi nikapanda kitandani kusubiri kuche ili nianze safari ya kwenda Mbeya.

Nikiwa macho, Emmy alijitikisa nikajifanya nakoroma ili asijue kama tangu niliponda kitandani sikupata usingizi, akajigeuza na kuangalia ukutani na kuendelea kuuchapa usingizi.

Alfajiri na mapema wote wakiwa wamelala, niliamka nikaoga kisha nikachukua begi langu, nikafungua mlango wa nyumba kubwa nikatoka kisha nikaufunga kwa funguo na kuziingiza ndani kupitia uwazi wa chini ya mlango.

Nilipofanya hivyo, nikafungua geti la kutokea nje kwa uangalifu bila kushtukiwa na kulifunga nikashika njia ya kwenda stendi, kwa kuwa bado kulikuwa na giza nilikuwa na hofu ya kukutana na vibaka.

Nikiwa natembea nikawa namuomba Mungu anipe ulinzi ili niweze kufika salama kwani sikutka kabisa kuendelea kuishi kwa mama ambaye hakuwa na upendo kwangu.

Wakati nikitembea ghafla nikasikia kengele ya baiskeli ile nageuka ikasimama pembeni yangu, moyo ukapiga pa!

Kijana aliyekuwa akiendesha kwa sauti nzito akanisalimia kwa Kiswahili chenye lafundhi ya Kisukuma; “Wewe msichana hujambo?”

Huku nikumuomba Mungu anilinde nikaitikia salamu yake na kumwamkia, akasema marahaba kisha akashuka kabisa kwenye baiskeli ambayo nyuma alifunga kiroba na kuchomeka panga kwenye mkanda wa kaptura kubwa aliyovaa.

“Unatoka wapi na unakwenda wapi usiku wote huu?” Dorcas anasema yule bwana alimwuliza.

Nilimweleza nilikuwa natoka nyumbani naenda kupanda basi kwani nilikuwa nasafiri kwenda Mbeya, akaniuliza nilikuwa natoka nyumbani wapi, nikamwelekeza mtaa ambao ulipakana na alioishi mama.

Nilipomweleza hivyo akasema sawa na kuniuliza kama nilikuwa nasoma, nikamjibu ndiyo na kumdanganya kwamba nilikuwa naenda Mbeya kwenye msiba.

Nilipomwambia hivyo, alichomoa panga na kunikazia macho.

Alipochomoa panga, akauangalia na kuurudisha kwenye hala kisha akaniuliza nilikuwa naenda kwenye msiba wa nani, kwa hofu niliyokuwanayo awali kwamba jamaa huyo alitaka kunidhuru nilivuta pumzi na kuzishusha kwa nguvu.

Japo mama alifariki dunia muda mrefu nilimwambia msiba wa mama, alisikitika sana akachukua begi langu na kulifunga juu ya kiroba kilichokuwa nyuma ya baiskeli yake.

Alipohakikisha alilifunga vizuri akaniambia nipande kwenye bomba la baiskeli kisha nikashika usukani akaisuma kama mita mbili, akadandia na kuanza kuendesha..

Njiani, alinipa pole tena kwa msiba na kuniuliza mbona nilikuwa nasafari peke yangu nikamdanganya kwamba ndugu zangu wengine walitangulia.

Aliendesha baiskeli kwa kasi hadi sehemu tuliyokuwa tukisubiria magari, kutokana na kunionea huruma, yule bwana hakuondoka mpaka lilipokuja gari aina ya Toyota Land Cruiser ambapo dereva alisema anakwenda Nzega.

Kwa kuwa nilielewa kama ningechelewa kupanda basi huenda Emmy angeamka na kukuta ule ujumbe na kuamua kunifuata, nilipanda gari hilo ambalo ndani kulikuwa na wanawake wawili, mmoja wa makamo, kijana wa miaka 15 hivi, mtoto na dereva.

Nilijua huko mbele ningeunganisha na magari ya kwenda Mbeya, yule bwana aliyenipa lifti ya baiskeli kabla ya kuniaga alinipatia shilingi elfu tatu na kunitakia safari njema ndipo gari likaanza safari.

Gari likiwa limeanza kushika kasi, mama aliyekuwa na mtoto akanisalimia kwa kusema; “ Hujambo binti!”
Nikaitikia salamu yake na kumpa heshima yake akasema marahaba ndipo nikakumbuka kwamba wakati napanda garini hatukusalimaina.

Tukasalimiana wote na kuendelea na safari, hatukutembea umbali mrefu, yule mama akaniuliza nilikuwa nakwenda wapi, nikamwambia akasema wao walikuwa wakienda jijini Dar es Salaam lakini watasimama Nzega kwa siku moja kisha kuendelea na safari.

Nilimwambia nikifika Nzega nitaunganisha safari yangu na magari yanayokwenda Dodoma kisha huko ningepanda la Mbeya, akasema sawa.

Kama unavyojua watu mnaposafiri pamoja huzungumza mambo mbalimbali, yule mama aliniuliza jina langu na Shinyanga nilitoka kwa nani.

Aliponiuliza hivyo, sikumjibu kwa wakati akaniuliza mbona nilionekana sikuwa sawa nikamwambia sikuwa na tatizo, akanibishia na kusema alikuwa mtu mzima hivyo nisingeweza kumdanganya na kusisitiza kwa alivyonioa kuna jambo lilinitatiza.

Alipotoa kauli hiyo, dada aliyekuwemo kwenye lile gari akaniambia kama nilikuwa nina tatizo niwaambie kwa sababu kwa wakati ule nilikuwa kama ndugu yao na hata kama lingetokea tatizo wao ndiyo wangenipatia msaada.

Kama vile waliambiana, dereva naye aliniambia kama nilikuwa na tatizo niwaeleze, awali nilitaka kuwaficha lakini nilisikia sauti ikiniambia niwaeleze kila kitu kilichonitokea.

Niliwafahamisha kwamba kuna mambo yalinitatiza ndiyo yaliyonifanya niwe safarini kwenda Mbeya kwa mama mkubwa, yule mama akaniuliza ni mambo gani, nikawaeleza waelewe tu hivyo nilivyowaambia.

Yule mama na dada walibaini niliwaficha kitu wakanibana kwamba niwaeleze, nilipokumbuka mambo waliyonifanyia mama na Evance nikajikuta natiririkwa na machozi.

Jambo hilo liliwapa wakati mgumu ndipo wakaanza kunibembeleza ninyamaze na kuwasimulia kila kitu, nikaamua kuwaeleza mkasa wangu mwanzo hadi mwisho.

Nilipofika mwisho, yule mama alishindwa kujizuia kulia, yule dada akawa mpole na kuniuliza kama yote niliyowaeleza yalikuwa kweli, nikawaambia yalikuwa kweli, wakasikitika sana.

Yule kijana aliyekuwemo kwenye lile gari alisema mama wa Shinyanga pamoja na Evance walitakiwa kushtakiwa ili sheria ichukue mkondo wake, nikawaambia sikuwa na mpango huo Mungu angenilipia.

Je, nini kitaendelea?
 
*DORCAS-17*


Baada ya kufanya hivyo, niliiona pochi ambayo Emmy alikuwa akihifadhia vitu nikahisi ilikuwa na fedha alizoachiwa na mama, nilipoifungua nikaona ilikuwa na noti za shilingi elfu kumi ambazo sikujua idadi yake.

Kwa kuwa lengo langu lilikuwa kuchukua kiasi cha fedha kwa ajili ya nauli ya kwenda Mbeya, nilizihesabu na kubaini ilikuwa shilingi hamsini na nne elfu, nikachukua elfu thelathini.

Kiasi hicho cha fedha niliamini kingenifikisha Mbeya bila matatizo, sikupenda kuchua fedha zote kuhofia ningewapa usumbufu wa kukosa fedha za matumizi wakati sikujua mama angerudi lini.

Baada ya kufanya hivyo, nilizihifadhi kwenye moja ya mifuko ya siketi yangu kisha nilichukua karatasi na kuandika ujumbe ambao hadi leo naukumbuka vizuri.

Ujumbe huo niliandika maneno haya: Emmy mimi Dorcas siyo mwizi na sitakuja kufanya kitendo hicho katika maisha yangu hata kama nitakumbana na wakati mgumu kiasi gani.

Kutokana na sababu ambazo zipo nje ya uwezo wangu nimefungua kabati na kukuta pochi yako ambayo ndani ilikuwa na shilingi hamsini na nne elfu, nimechukua shilingi elfu thelathini.

Najua nitakuwa nimeharibu bajeti yenu wakati huu mama akiwa hayupo lakini naomba mnisamehe kwa sababu sina jinsi nimeamua kuchukua fedha hizo ili nifanye nauli ya kwenda kwa mama mkubwa Mbeya.

Naomba Mungu unisamehe kwa kosa nililofanya kwa sababu sina jinsi, naomba mbaki salama na kwa amani kama Mungu akipenda tuonane tutaonana na asipopenda ipo siku tutaonana mbinguni, nakupenda sana Emmy kuliko mama na Evance.
Niombee nifike salama huko niendako, mimi Dorcas.

Nilipoandika ujumbe huo niliuweka ndani ya pocho niliyochukua zile fedha, nikaweka magauni yangu mawili ndani ya begi nikapanda kitandani kusubiri kuche ili nianze safari ya kwenda Mbeya.

Nikiwa macho, Emmy alijitikisa nikajifanya nakoroma ili asijue kama tangu niliponda kitandani sikupata usingizi, akajigeuza na kuangalia ukutani na kuendelea kuuchapa usingizi.

Alfajiri na mapema wote wakiwa wamelala, niliamka nikaoga kisha nikachukua begi langu, nikafungua mlango wa nyumba kubwa nikatoka kisha nikaufunga kwa funguo na kuziingiza ndani kupitia uwazi wa chini ya mlango.

Nilipofanya hivyo, nikafungua geti la kutokea nje kwa uangalifu bila kushtukiwa na kulifunga nikashika njia ya kwenda stendi, kwa kuwa bado kulikuwa na giza nilikuwa na hofu ya kukutana na vibaka.

Nikiwa natembea nikawa namuomba Mungu anipe ulinzi ili niweze kufika salama kwani sikutka kabisa kuendelea kuishi kwa mama ambaye hakuwa na upendo kwangu.

Wakati nikitembea ghafla nikasikia kengele ya baiskeli ile nageuka ikasimama pembeni yangu, moyo ukapiga pa!

Kijana aliyekuwa akiendesha kwa sauti nzito akanisalimia kwa Kiswahili chenye lafundhi ya Kisukuma; “Wewe msichana hujambo?”

Huku nikumuomba Mungu anilinde nikaitikia salamu yake na kumwamkia, akasema marahaba kisha akashuka kabisa kwenye baiskeli ambayo nyuma alifunga kiroba na kuchomeka panga kwenye mkanda wa kaptura kubwa aliyovaa.

“Unatoka wapi na unakwenda wapi usiku wote huu?” Dorcas anasema yule bwana alimwuliza.

Nilimweleza nilikuwa natoka nyumbani naenda kupanda basi kwani nilikuwa nasafiri kwenda Mbeya, akaniuliza nilikuwa natoka nyumbani wapi, nikamwelekeza mtaa ambao ulipakana na alioishi mama.

Nilipomweleza hivyo akasema sawa na kuniuliza kama nilikuwa nasoma, nikamjibu ndiyo na kumdanganya kwamba nilikuwa naenda Mbeya kwenye msiba.

Nilipomwambia hivyo, alichomoa panga na kunikazia macho.

Alipochomoa panga, akauangalia na kuurudisha kwenye hala kisha akaniuliza nilikuwa naenda kwenye msiba wa nani, kwa hofu niliyokuwanayo awali kwamba jamaa huyo alitaka kunidhuru nilivuta pumzi na kuzishusha kwa nguvu.

Japo mama alifariki dunia muda mrefu nilimwambia msiba wa mama, alisikitika sana akachukua begi langu na kulifunga juu ya kiroba kilichokuwa nyuma ya baiskeli yake.

Alipohakikisha alilifunga vizuri akaniambia nipande kwenye bomba la baiskeli kisha nikashika usukani akaisuma kama mita mbili, akadandia na kuanza kuendesha..

Njiani, alinipa pole tena kwa msiba na kuniuliza mbona nilikuwa nasafari peke yangu nikamdanganya kwamba ndugu zangu wengine walitangulia.

Aliendesha baiskeli kwa kasi hadi sehemu tuliyokuwa tukisubiria magari, kutokana na kunionea huruma, yule bwana hakuondoka mpaka lilipokuja gari aina ya Toyota Land Cruiser ambapo dereva alisema anakwenda Nzega.

Kwa kuwa nilielewa kama ningechelewa kupanda basi huenda Emmy angeamka na kukuta ule ujumbe na kuamua kunifuata, nilipanda gari hilo ambalo ndani kulikuwa na wanawake wawili, mmoja wa makamo, kijana wa miaka 15 hivi, mtoto na dereva.

Nilijua huko mbele ningeunganisha na magari ya kwenda Mbeya, yule bwana aliyenipa lifti ya baiskeli kabla ya kuniaga alinipatia shilingi elfu tatu na kunitakia safari njema ndipo gari likaanza safari.

Gari likiwa limeanza kushika kasi, mama aliyekuwa na mtoto akanisalimia kwa kusema; “ Hujambo binti!”
Nikaitikia salamu yake na kumpa heshima yake akasema marahaba ndipo nikakumbuka kwamba wakati napanda garini hatukusalimaina.

Tukasalimiana wote na kuendelea na safari, hatukutembea umbali mrefu, yule mama akaniuliza nilikuwa nakwenda wapi, nikamwambia akasema wao walikuwa wakienda jijini Dar es Salaam lakini watasimama Nzega kwa siku moja kisha kuendelea na safari.

Nilimwambia nikifika Nzega nitaunganisha safari yangu na magari yanayokwenda Dodoma kisha huko ningepanda la Mbeya, akasema sawa.

Kama unavyojua watu mnaposafiri pamoja huzungumza mambo mbalimbali, yule mama aliniuliza jina langu na Shinyanga nilitoka kwa nani.

Aliponiuliza hivyo, sikumjibu kwa wakati akaniuliza mbona nilionekana sikuwa sawa nikamwambia sikuwa na tatizo, akanibishia na kusema alikuwa mtu mzima hivyo nisingeweza kumdanganya na kusisitiza kwa alivyonioa kuna jambo lilinitatiza.

Alipotoa kauli hiyo, dada aliyekuwemo kwenye lile gari akaniambia kama nilikuwa nina tatizo niwaambie kwa sababu kwa wakati ule nilikuwa kama ndugu yao na hata kama lingetokea tatizo wao ndiyo wangenipatia msaada.

Kama vile waliambiana, dereva naye aliniambia kama nilikuwa na tatizo niwaeleze, awali nilitaka kuwaficha lakini nilisikia sauti ikiniambia niwaeleze kila kitu kilichonitokea.

Niliwafahamisha kwamba kuna mambo yalinitatiza ndiyo yaliyonifanya niwe safarini kwenda Mbeya kwa mama mkubwa, yule mama akaniuliza ni mambo gani, nikawaeleza waelewe tu hivyo nilivyowaambia.

Yule mama na dada walibaini niliwaficha kitu wakanibana kwamba niwaeleze, nilipokumbuka mambo waliyonifanyia mama na Evance nikajikuta natiririkwa na machozi.

Jambo hilo liliwapa wakati mgumu ndipo wakaanza kunibembeleza ninyamaze na kuwasimulia kila kitu, nikaamua kuwaeleza mkasa wangu mwanzo hadi mwisho.

Nilipofika mwisho, yule mama alishindwa kujizuia kulia, yule dada akawa mpole na kuniuliza kama yote niliyowaeleza yalikuwa kweli, nikawaambia yalikuwa kweli, wakasikitika sana.

Yule kijana aliyekuwemo kwenye lile gari alisema mama wa Shinyanga pamoja na Evance walitakiwa kushtakiwa ili sheria ichukue mkondo wake, nikawaambia sikuwa na mpango huo Mungu angenilipia.

Je, nini kitaendelea?
Dorcas kafanya jambo la msingi kutapika uhozo wa Evance na mama yake....nadhani atakuwa okey now. But also atapata msaada wa hao akina mama.....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dorcas kafanya jambo la msingi kutapika uhozo wa Evance na mama yake....nadhani atakuwa okey now. But also atapata msaada wa hao akina mama.....

Sent using Jamii Forums mobile app
matukio ya ubakaji huwa huchukua mda mrefu hasa kwa watendwa kusahau, huwa inawapelekea hata kwenye hatua ya kuwachukia wanaume wote duniani
 
Wanawake wa liobakwa hata kwenye mahusiano ..wanakuwa watata sana.hasa kama mbakaji hakuchukuliwa hatua yoyote..
wanaishi na maumivu!

Sent using Jamii Forums mobile app
Hata mbakaji akichukuliwa hatua, bado kazi bure, itachukua mda sana mtendwa kusahau tukio, hii ni kama mtoto wa kiume ashikishwe ukuta kwa lazima alafu atolewe marinda unafikiri kovu litakauka mapema ndomana ambao sio wastahimilivu huishia kujiua
 
*DORCAS-18*


Wote walimuunga mkono yule kijana kwamba nikafungue mashtaka dhidi ya mama na Evance, nikawaambia niliwasamehe na sikuwa tayari kuwashtaki,nikaanza kulia.

Kufuatia kulia, wote wakaanza kunisihi ninyamaze nikawaambia ingawa sikupenda kuwafungulia kesi na kumuacha Mungu, kitendo walichonifanyia kiliniumiza sana.

“Hata sisi tumeguswa na unyama uliofanyiwa ndiyo maana tunakushauri ukawashtaki ili sheria ichukue mkondo wake,” dereva aliniambia.

Nilimwambia sawa lakini siku moja Mungu angewahuku kwa sababu yeyote anayewafanyia wengine ubaya, malipo yake yapo hapa hapa duniani.

Walipoona sikukubaliana na ushauri wao,waliniacha tukaendelea na safari huku kila mmoja akiwa ananionea huruma, kabla ya kufika Nzega yule mama aliniita jina langu na kunipa pole kwa yote yaliyotokea na kuwalaani mama na Evance.

Mama huyo ambaye tayari alijua hata Mbeya kwa mama mkubwa nilikokuwa nakwenda hakukuwa kwa ndugu zangu wa damu, aliniomba kama sitajali niongozane naye kwenda nyumbani kwake jijini Dar es Salaam.

“Mwanangu, mkasa wako umenigusa sana, kama hautajali naomba twende tukaishi wote nyumbani kwangu Dar es Salaam, nitakutafutia shule ili uendelee na masomo na utakuwa miongoni mwa watoto wangu,” Dorcas anasema yule mama alimwambia.

Kwa kuwa nilijua hakuna kitu kitakachonikomboa maishani mwangu kama elimu, nilifurahi sana kupata nafasi hiyo adimu ambayo nilikuwa naamini ilipotea, nikamkubalia yule mama.

“Nashukuru sana mwanangu kukubali kwenda kuishi nami, hata mume wangu nikimwambia habari zako atasikitika na kukupokea bila kinyongo,” Dorcas anasema yule mama alimwambia.

Nilimshukuru sana kwa ukarimu wake huo, hata yule dada alimuunga mkono tukaendelea kuzungumza na huku safari ikiendelea na kuwasili Nzega mapema.

Tulipofika tukaenda nyumbani kwa ndugu yao, katika maongezi yao waliambiwa mama aliyekuwa mwenyeji hakuwepo nalikuwa amekwenda Igunga.

Kufuatia taarifa hiyo, tuliondoka Nzega kwenda Igunga kwa ndugu yao mwingine ambako tulimkuta yule mama, baada ya maongezi waliamua kuelekea Dar.

Njiani tulikuwa tukizungumza mambo mengi utafikiri tulifahamiana muda mrefu, yule dada niliyemkuta mle kwenye gari kumbe naye alikuwa abiria.

Katika maongezi alitusimulia mateso aliyowahi kupata kutoka kwa mama yake wa kambo namna alivyokuwa akilala bila kula huku akiwa amefanya kazi kutwa nzima.

Alitueleza kuwa kila alipomweleza marehemu baba yake mambo ambayo alifanyiwa na yule mama, alimgeuzia kibao na kumchapa na kumtuhumu alikuwa muongo.

Mkasa wake ulituhuzunisha sana ambapo aliniambia nisihuzunike sana kwani kila kinachotkea katika maisha yetu kinakuwa na sababu.

Alisisitiza kama nitarudi shuleni nisome kwa bidii kwani ni elimu pekee ndiyo ingeweza kunikomboa na kunifanya nisahau yote yaliyonitokea, akaniambia nimshukuru sana yule mama aliyeamua kunichukua niende kwake Dar kwa ajili ya kusoma.

Nilimshukuru yule dada kwa kunipa moyo, tulipofika Singida alituaga kwani alikuwa amefika, kwa jinsi tulivyozoeana tulihuzunika lakini hatukuwa na la kufanya zaidi ya kutakiana heri.

Baada ya yule dada kuteremka, yule mama ambaye mpaka muda huo sikuelewa kama lile gari lilikuwa lake au la nani alimwambia dereva akipata abiria amchukue ili tupate pesa ya matumizi njiani.

Dereva aliondoa gari hadi maeneo ya stendi kuu ya Singida akawaeleza akina mama f’lani kwamba alikuwa akielekea Dar na kulikuwa na nafasi ya mtu mmoja.

Mama mmoja mwenye asili ya Kiarabu aliyekuwa na pochi alichangamka akaingia kwenye gari, safari ikaanza huku kila mmoja akiwa kimya hadi dereva alipoyumbisha gari wakati akiwakwepa mbuzi waliokatiza barabarani.

Kufuatia kuyumba huko kwa gari, yule mama wa kiarabu alipata mshtuko akaangukia upande wa kulia wa kiti alichokuwa ameketi na kupoteza fahamu.
Je, kilifuatia nini? Usikose wiki ijayo. Maoni nicheki kupitia namba hizo hapo juu.

Kitendo cha yule mama kupoteza fahamu kilitukosesha raha, dereva alisimamisha gari pembeni ya barabara tukaanza kumpepea kwa kutumia gazeti lakini hakuzinduka.

“Huyu atakuwa na tatizo la presha, sasa sijui tufanyeje?” dereva alimwuliza mama.

Kwa kuwa mama alikuwa na uzoefu wa mamboya tiba alishauri tutafute sehemu iliyokuwa na kimvuli tuegeshe gari kisha akipigwa na upepo angezinduka.

Alipotoa ushauri huo, dereva alilipeleka gari chini ya mti wenye kimvuli ambapo palikuwa na hewa ya kutosha akafungua milango yote ya gari.

Mama hakuacha kumpepea ghafla yule mama akafumbua macho na kuanza kuangaza huku na huko,hali iliyotupa matumaini, mama akamwuliza alijisikiaje!
Yule mama wa Kiarabu hakujibu badala yake aliendelea kuangaza tu macho yake,mama akasema tumuache kama dakika kumi au zaidi angezinduka kabisa.

Kwelikama alivyosema, baada ya kupita kama dakika kumi na tano, yule mama aligeuza shingo upande aliokuwa mama na kumuuliza tulikuwa wapi.
“Tupo safari tunaenda Dar es Salaam,” mama alimjibu.

Alipoambiwa hivyo, alishangaa na kuuliza; “Tunakwenda Dar es Salaam kwa nani?”
Kufuatia swalilake tulijikuta tukiangua kicheko ndipo mama alimwambia tulikuwa safarini lakini kwa bahati mbaya tulipata tatizo lililomfanya we katika hali ile.

Mama alimwuliza kama hakukumbuka chochote,yule Mwarabu alitulia kwa muda na kuuliza begi lake lilikuwa wapi, mama akamuonesha, alipoliona alitabasamu.

Baada ya kufanya hivyo, aliinuka kisha kuuliza kwa nini dereva aliegesha gari chini ya mti,mama akamsimulia kilakitu kuhusu tulivyonusurika katika jail.

Alipoambiwa hivyo, alimshukuru Mungu ndipo alituambia alikuwa na tatizo la presha ambalo lilimfanya anaposhtuliwa na jambo f’lani alikuwa akipoteza fahamu.

Mama huyo, alifungua begi lake akatoa vidonge akameza viwili na kushushia na maji, akasema alikuwa sawa hivyo tuendelee na safari.

Maongezi yaliyojiri yalikuwa kumlaani mmiliki wa wale mbuzi kufuatia kitendo chake cha kuwaacha wakirandaranda hovyo barabani bila uangalizi.

Dereva aliendesha gari hilo kwa kasi hadi tulipofika Dodoma, tukaenda kula kisha safari ya Dar ikaendelea.

Mungu jalia tulifika Dar, salama salimini na kupokelewa na watoto wa yule mama, yule kaka aliyekuwa akiendesha gari ambaye mpaka muda huo sikufahamu walikuwa na uhusiano gani alituaga na kuondoka na yule kijana mwingine.

Baada kuweka mizigo na mabegi sehemu husika, yule mama alinikaribisha kwa kuniambia pale palikuwa nyumbani kwake hivyo niwe huru kwa kila jambo.

Aliniambia kwamba mumewe hakuwepo na kwamba angerudi usiku ndipo alinitambulisha kwa binti mmoja ambaye alisema ni dada yaani binti wa kazi, akasema anaitwa Tabu.

Je, nini kitaendelea?
 
*DORCAS-18*


Wote walimuunga mkono yule kijana kwamba nikafungue mashtaka dhidi ya mama na Evance, nikawaambia niliwasamehe na sikuwa tayari kuwashtaki,nikaanza kulia.

Kufuatia kulia, wote wakaanza kunisihi ninyamaze nikawaambia ingawa sikupenda kuwafungulia kesi na kumuacha Mungu, kitendo walichonifanyia kiliniumiza sana.

“Hata sisi tumeguswa na unyama uliofanyiwa ndiyo maana tunakushauri ukawashtaki ili sheria ichukue mkondo wake,” dereva aliniambia.

Nilimwambia sawa lakini siku moja Mungu angewahuku kwa sababu yeyote anayewafanyia wengine ubaya, malipo yake yapo hapa hapa duniani.

Walipoona sikukubaliana na ushauri wao,waliniacha tukaendelea na safari huku kila mmoja akiwa ananionea huruma, kabla ya kufika Nzega yule mama aliniita jina langu na kunipa pole kwa yote yaliyotokea na kuwalaani mama na Evance.

Mama huyo ambaye tayari alijua hata Mbeya kwa mama mkubwa nilikokuwa nakwenda hakukuwa kwa ndugu zangu wa damu, aliniomba kama sitajali niongozane naye kwenda nyumbani kwake jijini Dar es Salaam.

“Mwanangu, mkasa wako umenigusa sana, kama hautajali naomba twende tukaishi wote nyumbani kwangu Dar es Salaam, nitakutafutia shule ili uendelee na masomo na utakuwa miongoni mwa watoto wangu,” Dorcas anasema yule mama alimwambia.

Kwa kuwa nilijua hakuna kitu kitakachonikomboa maishani mwangu kama elimu, nilifurahi sana kupata nafasi hiyo adimu ambayo nilikuwa naamini ilipotea, nikamkubalia yule mama.

“Nashukuru sana mwanangu kukubali kwenda kuishi nami, hata mume wangu nikimwambia habari zako atasikitika na kukupokea bila kinyongo,” Dorcas anasema yule mama alimwambia.

Nilimshukuru sana kwa ukarimu wake huo, hata yule dada alimuunga mkono tukaendelea kuzungumza na huku safari ikiendelea na kuwasili Nzega mapema.

Tulipofika tukaenda nyumbani kwa ndugu yao, katika maongezi yao waliambiwa mama aliyekuwa mwenyeji hakuwepo nalikuwa amekwenda Igunga.

Kufuatia taarifa hiyo, tuliondoka Nzega kwenda Igunga kwa ndugu yao mwingine ambako tulimkuta yule mama, baada ya maongezi waliamua kuelekea Dar.

Njiani tulikuwa tukizungumza mambo mengi utafikiri tulifahamiana muda mrefu, yule dada niliyemkuta mle kwenye gari kumbe naye alikuwa abiria.

Katika maongezi alitusimulia mateso aliyowahi kupata kutoka kwa mama yake wa kambo namna alivyokuwa akilala bila kula huku akiwa amefanya kazi kutwa nzima.

Alitueleza kuwa kila alipomweleza marehemu baba yake mambo ambayo alifanyiwa na yule mama, alimgeuzia kibao na kumchapa na kumtuhumu alikuwa muongo.

Mkasa wake ulituhuzunisha sana ambapo aliniambia nisihuzunike sana kwani kila kinachotkea katika maisha yetu kinakuwa na sababu.

Alisisitiza kama nitarudi shuleni nisome kwa bidii kwani ni elimu pekee ndiyo ingeweza kunikomboa na kunifanya nisahau yote yaliyonitokea, akaniambia nimshukuru sana yule mama aliyeamua kunichukua niende kwake Dar kwa ajili ya kusoma.

Nilimshukuru yule dada kwa kunipa moyo, tulipofika Singida alituaga kwani alikuwa amefika, kwa jinsi tulivyozoeana tulihuzunika lakini hatukuwa na la kufanya zaidi ya kutakiana heri.

Baada ya yule dada kuteremka, yule mama ambaye mpaka muda huo sikuelewa kama lile gari lilikuwa lake au la nani alimwambia dereva akipata abiria amchukue ili tupate pesa ya matumizi njiani.

Dereva aliondoa gari hadi maeneo ya stendi kuu ya Singida akawaeleza akina mama f’lani kwamba alikuwa akielekea Dar na kulikuwa na nafasi ya mtu mmoja.

Mama mmoja mwenye asili ya Kiarabu aliyekuwa na pochi alichangamka akaingia kwenye gari, safari ikaanza huku kila mmoja akiwa kimya hadi dereva alipoyumbisha gari wakati akiwakwepa mbuzi waliokatiza barabarani.

Kufuatia kuyumba huko kwa gari, yule mama wa kiarabu alipata mshtuko akaangukia upande wa kulia wa kiti alichokuwa ameketi na kupoteza fahamu.
Je, kilifuatia nini? Usikose wiki ijayo. Maoni nicheki kupitia namba hizo hapo juu.

Kitendo cha yule mama kupoteza fahamu kilitukosesha raha, dereva alisimamisha gari pembeni ya barabara tukaanza kumpepea kwa kutumia gazeti lakini hakuzinduka.

“Huyu atakuwa na tatizo la presha, sasa sijui tufanyeje?” dereva alimwuliza mama.

Kwa kuwa mama alikuwa na uzoefu wa mamboya tiba alishauri tutafute sehemu iliyokuwa na kimvuli tuegeshe gari kisha akipigwa na upepo angezinduka.

Alipotoa ushauri huo, dereva alilipeleka gari chini ya mti wenye kimvuli ambapo palikuwa na hewa ya kutosha akafungua milango yote ya gari.

Mama hakuacha kumpepea ghafla yule mama akafumbua macho na kuanza kuangaza huku na huko,hali iliyotupa matumaini, mama akamwuliza alijisikiaje!
Yule mama wa Kiarabu hakujibu badala yake aliendelea kuangaza tu macho yake,mama akasema tumuache kama dakika kumi au zaidi angezinduka kabisa.

Kwelikama alivyosema, baada ya kupita kama dakika kumi na tano, yule mama aligeuza shingo upande aliokuwa mama na kumuuliza tulikuwa wapi.
“Tupo safari tunaenda Dar es Salaam,” mama alimjibu.

Alipoambiwa hivyo, alishangaa na kuuliza; “Tunakwenda Dar es Salaam kwa nani?”
Kufuatia swalilake tulijikuta tukiangua kicheko ndipo mama alimwambia tulikuwa safarini lakini kwa bahati mbaya tulipata tatizo lililomfanya we katika hali ile.

Mama alimwuliza kama hakukumbuka chochote,yule Mwarabu alitulia kwa muda na kuuliza begi lake lilikuwa wapi, mama akamuonesha, alipoliona alitabasamu.

Baada ya kufanya hivyo, aliinuka kisha kuuliza kwa nini dereva aliegesha gari chini ya mti,mama akamsimulia kilakitu kuhusu tulivyonusurika katika jail.

Alipoambiwa hivyo, alimshukuru Mungu ndipo alituambia alikuwa na tatizo la presha ambalo lilimfanya anaposhtuliwa na jambo f’lani alikuwa akipoteza fahamu.

Mama huyo, alifungua begi lake akatoa vidonge akameza viwili na kushushia na maji, akasema alikuwa sawa hivyo tuendelee na safari.

Maongezi yaliyojiri yalikuwa kumlaani mmiliki wa wale mbuzi kufuatia kitendo chake cha kuwaacha wakirandaranda hovyo barabani bila uangalizi.

Dereva aliendesha gari hilo kwa kasi hadi tulipofika Dodoma, tukaenda kula kisha safari ya Dar ikaendelea.

Mungu jalia tulifika Dar, salama salimini na kupokelewa na watoto wa yule mama, yule kaka aliyekuwa akiendesha gari ambaye mpaka muda huo sikufahamu walikuwa na uhusiano gani alituaga na kuondoka na yule kijana mwingine.

Baada kuweka mizigo na mabegi sehemu husika, yule mama alinikaribisha kwa kuniambia pale palikuwa nyumbani kwake hivyo niwe huru kwa kila jambo.

Aliniambia kwamba mumewe hakuwepo na kwamba angerudi usiku ndipo alinitambulisha kwa binti mmoja ambaye alisema ni dada yaani binti wa kazi, akasema anaitwa Tabu.

Je, nini kitaendelea?
Asante Shunie nlikua naisubiri kwa hamu

the Legend☆
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom