Hadi machozi yamenilenga! Asanteh Shunie*DORCAS-15*
Nikiwa nawaza hivyo, bibi alirudi akiwa na karanga zilizokaangwa akanikaribisha ndipo mama mdogo akamuomba bibi wakaongee jambo f’lani, wakatoka nje.
Walipotoka nilijua mama mdogo alitaka kumweleza bibi masaibu yangu na lengo la mimi kwenda kule kijijini, baada ya dakika kama arobaini waliingia.
Bibi alinipa pole kwa yote yaliyotokea na kuniambia nisiwe na kinyongo na Evance kwani alifanya hivyo kwa sababu ya ujana na kwamba niwe na amani moyoni.
Kauli ya bibi iliniumiza sana kwani nilijua alisema vile kwa sababu aliyenibaka alikuwa mjukuu wake ambapo nilijiuliza kama angefanyiwa binti yao Emmy wangethubutu kusema aliyemfanyia hivyo alifanya kwa bahati mbaya.
Kutokana na uchungu nilioupata, kwanza wa kushindwa kuendelea kusoma, kubakwa na kupewa mimba nilijikuta nikitiririkwa na machozi.
Bibi aliyegundua niliumizwa sana na jambo hilo alianza kunibebembeleza ninyamaze na nivumilie na kwamba atanipa uangalizi mzuri mpaka nitakapojifungua kisha nirudi shuleni.
Kwa kuwa sikuwa na la kufanya, nililazimika kuwa mpole na kuendelea kumkumbuka marehemu mama na kujisemea kama angekuwa hai yote yaliyonitokea yasingetokea.
“Dorcas, nakuomba usiwaze sana jambo lililotokea, kwa kuwa upo na bibi naamini hautapungiwa na kitu na msamehe Evance hayo ni mambo ya vijana, naamini ipo siku atakusaidia kwani hata yeye anajutia kosa lake,” Dorcas anasema mama mdogo alimwambia.
Tukiwa tunaongea huku nikiwa sina furaha zaidi ya kusumbuliwa na msongo wa mawazo, alikuja mama mmoja ambaye nilitambulishwa kwamba alikuwa na undugu na mama.
Tuliposalimiana, bibi alimtambulisha kwamba nimetokea mjini nitakuwepo pale kijijini kwa muda mrefu, yule mama akamwuliza nitakuwa nasoma kule?
Kufuatia kuulizwa hivyo, bibi alimwambia hapana nilikwishahitimu darasa la saba hivyo nitakuwepo kule kijijini kwa muda mrefu bila kumwambia kama nilikuwa mjamzito.
Kwa kuwa tangu tulipofika tulikuwa tunapiga stori, yule mama alinikaribisha kule kijijini kisha akaaga na kwenda kwake ndipo bibi alimwambia mama mdogo aandae mboga ya majani, usiku tulipokula ugali nikaoneshwa sehemu ya kulala.
Kutokana na mazingira yale kuwa mapya na jinsi nyumba ilivyokuwa, sikuweza kupata usingizi mapema, lakini baadaye nilipitiwa na usingizi.
Kulipokucha mama mdogo aliondoka nikaanza rasmi kuishi na bibi ambaye awali tulikuwa tukienda naye shambani lakini kadiri siku zilivyosonga mbele nikashindwa na kuwa mtu wa kushinda nyumbani.
Jambo la kumshukuru Mungu ni kwamba ujauzito wangu haukuniletea matatizo ya kuumwa kama inavyowatokea wanawake wengine, isipokuwa nilikuwa sipendi kula.
Kilichonishangaza zaidi ni kitendo cha mama aliyeahidi kunisaidia kwa kila jambo kukata mawasiliano nami, wala hakuja kunijulia hali na nilipomuuliza bibi aliniambia kwamba huenda alibanwa na biashara zake.
Hata mama mdogo aliyeniacha kule kijijini naye alikata mawasiliano kabisa, kwa ujumla kitendo cha mama kutokuja kuniona kilinihuzunisha sana.
Mbaya zaidi sikuwa na fedha za akiba ambazo ningezitumia kama nauli ya kwenda mjini, kufuatia hali hiyo nikawa sina namna ya kufanya.
Maisha ya kule kijijini yaliniweka katika wakati mgumu sana kwani nilimkumbuka marehemu mama na mama mkubwa wa Mbeya ambao walinilea kwa upendo.
Nilikuwa najiuliza kwa nini mimi pekee nilikuwa naandamwa na mikosi, wa kwanza kutomfahamu baba yangu, kusumbuliwa na wachawi nilipokuwa Mbeya, kifo cha mama, kubakwa na kupewa ujauzito, kukatishwa masomo kisha kwenda kutelekezwa kijijini!
Mambo hayo yaliniumiza sana, kuna wakati bibi akiwa hayupo nyumbani nilijikuta nalia peke yangu na kuiona dunia haikuwa rafiki yangu hata kidogo.
Wakati nikiwa kule kijijini nilikuwa nakwenda katika zahanati moja ambapo zilitolewa huduma za kliniki, kila nilipopimwa niliambiwa mtoto alikuwa akiendelea vizuri na kupewa maelekezo mengine yaliyohusiana na masuala ya uzazi.
Hata hivyo, kitendo cha kutelekezwa na mama kule kijijini kilinifanya muda mwingi kuwa katika msongo wa mawazo na kujiuliza ilikuwaje mama aliyenishauri nikakae kule na aliyefahamu hali niliyokuwanayo anifanyie vile?
Kutokana na msongo wa mawazo niliokuwanao, yule mama wa kwanza kufika pale nyumbani kwa bibi alinigundua mara kwa mara nikawa nakwenda kwake kwa ajili ya mazungumzo nk.
Licha ya kufanya hivyo, aliponiuliza kuhusu mwanaume aliyenipatia ujauzito sikuthubutu kumtaja Evance kama mama alivyoniomba nisimtaje kuhofia mwanaye kupata matatizo ya kisheria.
****
Niliishi kule kijijini hadi ujauzito wangu ulipofika miezi tisa bila mama wala mdogo wake kuja kuniona, usiku nilipatwa na uchungu lakini kwa kuwa kituo kikubwa cha afya ambacho kinatoa huduma za uzazi kuwa mbali chupa ya uzazi ilipasuka.
Baada ya tukio hilo sikukaa muda mrefu kwa msaada wa bibi na jirani zake wawili nilijifungua mtoto wa kiume, kama inavyokuwa karibu kwa wanawake wote, licha maumivu kitendo cha kupata mtoto kilinifurahisha sana.
Akina bibi walinihudumia vizuri na kulipokucha tuliondoka pale kijijini kwa usafiri baiskeli mbili nikapelekwa katika kituo cha afya kilichotoa huduma ya uzazi.
Kwa kuwa nilijifungulia nyumbani, nilifanyiwa uchunguzi kama nilipata maambukizo yoyote lakini ilibainika nilikuwa salama mimi na mwanangu.
Hata hivyo, nilikaa pale hospitali kwa muda wa siku tatu ndipo niliruhusiawa kurudi nyumbani, bibi aliyekuwa akifuga kuku alinihudumia vizuri kama mazazi lakini tatizo sikuwa na nguo za kumvalisha mwanangu kwa sababu sikuwa na fedha.
Kutokana na hali hiyo, nilikuwa namfunga kanga zangu na za bibi, ila yule mama niliyekuwa napenda kwenda kwake aliniletea nguo kadhaa za mtoto.
Kwa kuwa nilihitaji sana kumuona mama na kuzungumza naye kuhusu hatima yangu ya masomo, nilimuuliza bibi kama alimtumia ujumbe kwamba nilijifungua, alisema alifanya hivyo na angefika muda wowote.
Hata hivyo, nilikaa majuma matatu, si mama wala mama mdogo aliyetokea nikaendelea kuishi katika mazingira magumu na mwanangu hadi nilipomaliza mwezi.
Kwa kuwa afya ya mwanangu na yangu zilikuwa nzuri, nilizungumza na yule mama jirani wa bibi anikopeshe fedha ili niweze kwenda mjini ambazo angerudishiwa na mama.
Mama huyo aliyekuwa akitegemea kupata fedha kwa kuuza mazao wakati wa minada, akaniambia nisubiri kama angezipata angenipatia tena bila kunikopesha kwa sababu alikuwa ananionea huruma maisha niliyoishi kule kijijini na mwanangu.
Hata kabla ya kunipatia fedha hizo, nilimshukuru kwa ukarimu wake nikamwambia nitamsubiri mpaka atakapozipata, maisha yakaendelea.
Niliendelea kuishi huku nikisubiri kupewa nauli na yule mama na kufikisha mwezi mmoja na nusu, siku moja usiku mwanangu alipatwa na homa kali pamoja na ugonjwa wa Inimonia akawa anashindwa kupumua vizuri.
Kwa kuwa ilikuwa usiku ilituwia vigumu kutoka tukaamua kusubiri kukuche ndipo tumpeleke zahanati lakini ilipofika saa tisa kuelekea saa kumi mwanangu alifariki dunia.
Awali sikufahamu kama mwanangu alifariki hadi bibi alipokwenda kuwaamsha majirani ambapo alikuja babu mmoja na mkewe, bwana mmoja aliyekuwa akipenda kuniita mjomba na Yule mama aliyeniahidi kunipatia nauli ya kwenda mjini.
Baada ya kuzungumza na bibi ndipo Yule mama aliniambia mwanangu alifariki dunia hivyo niwe jasiri kwa sababu ilikuwa bahati mbaya.
Taarifa hiyo ilinihuzunisha nikaanza kulia kwani licha ya changamoto nilizopitia nilimpenda sana mwanangu na sikuhitaji kumpoteza, akina bibi waliendelea kunibembeleza.
Hata hivyo, nilimchikia sana mama pamoja na Evance kwa vitendo walivyonifanyia, mama kunipeleka kijijini na kunitelekeza na kijana wakle kunibaka na kunipa ujauzito.
Pamoja na chuki niliyokuwanayo, sikutaka kumuonesha mtu yeyote hali hiyo zaidi ya kusema ipo siku Mungu angenilipia kwa ukatili niliofanyiwa, nilipomkumbuka mama maumivu yalizidi kuwa makali nikajikuta nalia kwa sauti.
Tangu muda alipofariki mwanangu, hatukulala tena hadi kulipokucha ambapo watu walikusanyika na kujadiliana namna ya kumpumzisha mwanangu.
Je, nini kitaendelea?
*DORCAS-15*
Nikiwa nawaza hivyo, bibi alirudi akiwa na karanga zilizokaangwa akanikaribisha ndipo mama mdogo akamuomba bibi wakaongee jambo f’lani, wakatoka nje.
Walipotoka nilijua mama mdogo alitaka kumweleza bibi masaibu yangu na lengo la mimi kwenda kule kijijini, baada ya dakika kama arobaini waliingia.
Bibi alinipa pole kwa yote yaliyotokea na kuniambia nisiwe na kinyongo na Evance kwani alifanya hivyo kwa sababu ya ujana na kwamba niwe na amani moyoni.
Kauli ya bibi iliniumiza sana kwani nilijua alisema vile kwa sababu aliyenibaka alikuwa mjukuu wake ambapo nilijiuliza kama angefanyiwa binti yao Emmy wangethubutu kusema aliyemfanyia hivyo alifanya kwa bahati mbaya.
Kutokana na uchungu nilioupata, kwanza wa kushindwa kuendelea kusoma, kubakwa na kupewa mimba nilijikuta nikitiririkwa na machozi.
Bibi aliyegundua niliumizwa sana na jambo hilo alianza kunibebembeleza ninyamaze na nivumilie na kwamba atanipa uangalizi mzuri mpaka nitakapojifungua kisha nirudi shuleni.
Kwa kuwa sikuwa na la kufanya, nililazimika kuwa mpole na kuendelea kumkumbuka marehemu mama na kujisemea kama angekuwa hai yote yaliyonitokea yasingetokea.
“Dorcas, nakuomba usiwaze sana jambo lililotokea, kwa kuwa upo na bibi naamini hautapungiwa na kitu na msamehe Evance hayo ni mambo ya vijana, naamini ipo siku atakusaidia kwani hata yeye anajutia kosa lake,” Dorcas anasema mama mdogo alimwambia.
Tukiwa tunaongea huku nikiwa sina furaha zaidi ya kusumbuliwa na msongo wa mawazo, alikuja mama mmoja ambaye nilitambulishwa kwamba alikuwa na undugu na mama.
Tuliposalimiana, bibi alimtambulisha kwamba nimetokea mjini nitakuwepo pale kijijini kwa muda mrefu, yule mama akamwuliza nitakuwa nasoma kule?
Kufuatia kuulizwa hivyo, bibi alimwambia hapana nilikwishahitimu darasa la saba hivyo nitakuwepo kule kijijini kwa muda mrefu bila kumwambia kama nilikuwa mjamzito.
Kwa kuwa tangu tulipofika tulikuwa tunapiga stori, yule mama alinikaribisha kule kijijini kisha akaaga na kwenda kwake ndipo bibi alimwambia mama mdogo aandae mboga ya majani, usiku tulipokula ugali nikaoneshwa sehemu ya kulala.
Kutokana na mazingira yale kuwa mapya na jinsi nyumba ilivyokuwa, sikuweza kupata usingizi mapema, lakini baadaye nilipitiwa na usingizi.
Kulipokucha mama mdogo aliondoka nikaanza rasmi kuishi na bibi ambaye awali tulikuwa tukienda naye shambani lakini kadiri siku zilivyosonga mbele nikashindwa na kuwa mtu wa kushinda nyumbani.
Jambo la kumshukuru Mungu ni kwamba ujauzito wangu haukuniletea matatizo ya kuumwa kama inavyowatokea wanawake wengine, isipokuwa nilikuwa sipendi kula.
Kilichonishangaza zaidi ni kitendo cha mama aliyeahidi kunisaidia kwa kila jambo kukata mawasiliano nami, wala hakuja kunijulia hali na nilipomuuliza bibi aliniambia kwamba huenda alibanwa na biashara zake.
Hata mama mdogo aliyeniacha kule kijijini naye alikata mawasiliano kabisa, kwa ujumla kitendo cha mama kutokuja kuniona kilinihuzunisha sana.
Mbaya zaidi sikuwa na fedha za akiba ambazo ningezitumia kama nauli ya kwenda mjini, kufuatia hali hiyo nikawa sina namna ya kufanya.
Maisha ya kule kijijini yaliniweka katika wakati mgumu sana kwani nilimkumbuka marehemu mama na mama mkubwa wa Mbeya ambao walinilea kwa upendo.
Nilikuwa najiuliza kwa nini mimi pekee nilikuwa naandamwa na mikosi, wa kwanza kutomfahamu baba yangu, kusumbuliwa na wachawi nilipokuwa Mbeya, kifo cha mama, kubakwa na kupewa ujauzito, kukatishwa masomo kisha kwenda kutelekezwa kijijini!
Mambo hayo yaliniumiza sana, kuna wakati bibi akiwa hayupo nyumbani nilijikuta nalia peke yangu na kuiona dunia haikuwa rafiki yangu hata kidogo.
Wakati nikiwa kule kijijini nilikuwa nakwenda katika zahanati moja ambapo zilitolewa huduma za kliniki, kila nilipopimwa niliambiwa mtoto alikuwa akiendelea vizuri na kupewa maelekezo mengine yaliyohusiana na masuala ya uzazi.
Hata hivyo, kitendo cha kutelekezwa na mama kule kijijini kilinifanya muda mwingi kuwa katika msongo wa mawazo na kujiuliza ilikuwaje mama aliyenishauri nikakae kule na aliyefahamu hali niliyokuwanayo anifanyie vile?
Kutokana na msongo wa mawazo niliokuwanao, yule mama wa kwanza kufika pale nyumbani kwa bibi alinigundua mara kwa mara nikawa nakwenda kwake kwa ajili ya mazungumzo nk.
Licha ya kufanya hivyo, aliponiuliza kuhusu mwanaume aliyenipatia ujauzito sikuthubutu kumtaja Evance kama mama alivyoniomba nisimtaje kuhofia mwanaye kupata matatizo ya kisheria.
****
Niliishi kule kijijini hadi ujauzito wangu ulipofika miezi tisa bila mama wala mdogo wake kuja kuniona, usiku nilipatwa na uchungu lakini kwa kuwa kituo kikubwa cha afya ambacho kinatoa huduma za uzazi kuwa mbali chupa ya uzazi ilipasuka.
Baada ya tukio hilo sikukaa muda mrefu kwa msaada wa bibi na jirani zake wawili nilijifungua mtoto wa kiume, kama inavyokuwa karibu kwa wanawake wote, licha maumivu kitendo cha kupata mtoto kilinifurahisha sana.
Akina bibi walinihudumia vizuri na kulipokucha tuliondoka pale kijijini kwa usafiri baiskeli mbili nikapelekwa katika kituo cha afya kilichotoa huduma ya uzazi.
Kwa kuwa nilijifungulia nyumbani, nilifanyiwa uchunguzi kama nilipata maambukizo yoyote lakini ilibainika nilikuwa salama mimi na mwanangu.
Hata hivyo, nilikaa pale hospitali kwa muda wa siku tatu ndipo niliruhusiawa kurudi nyumbani, bibi aliyekuwa akifuga kuku alinihudumia vizuri kama mazazi lakini tatizo sikuwa na nguo za kumvalisha mwanangu kwa sababu sikuwa na fedha.
Kutokana na hali hiyo, nilikuwa namfunga kanga zangu na za bibi, ila yule mama niliyekuwa napenda kwenda kwake aliniletea nguo kadhaa za mtoto.
Kwa kuwa nilihitaji sana kumuona mama na kuzungumza naye kuhusu hatima yangu ya masomo, nilimuuliza bibi kama alimtumia ujumbe kwamba nilijifungua, alisema alifanya hivyo na angefika muda wowote.
Hata hivyo, nilikaa majuma matatu, si mama wala mama mdogo aliyetokea nikaendelea kuishi katika mazingira magumu na mwanangu hadi nilipomaliza mwezi.
Kwa kuwa afya ya mwanangu na yangu zilikuwa nzuri, nilizungumza na yule mama jirani wa bibi anikopeshe fedha ili niweze kwenda mjini ambazo angerudishiwa na mama.
Mama huyo aliyekuwa akitegemea kupata fedha kwa kuuza mazao wakati wa minada, akaniambia nisubiri kama angezipata angenipatia tena bila kunikopesha kwa sababu alikuwa ananionea huruma maisha niliyoishi kule kijijini na mwanangu.
Hata kabla ya kunipatia fedha hizo, nilimshukuru kwa ukarimu wake nikamwambia nitamsubiri mpaka atakapozipata, maisha yakaendelea.
Niliendelea kuishi huku nikisubiri kupewa nauli na yule mama na kufikisha mwezi mmoja na nusu, siku moja usiku mwanangu alipatwa na homa kali pamoja na ugonjwa wa Inimonia akawa anashindwa kupumua vizuri.
Kwa kuwa ilikuwa usiku ilituwia vigumu kutoka tukaamua kusubiri kukuche ndipo tumpeleke zahanati lakini ilipofika saa tisa kuelekea saa kumi mwanangu alifariki dunia.
Awali sikufahamu kama mwanangu alifariki hadi bibi alipokwenda kuwaamsha majirani ambapo alikuja babu mmoja na mkewe, bwana mmoja aliyekuwa akipenda kuniita mjomba na Yule mama aliyeniahidi kunipatia nauli ya kwenda mjini.
Baada ya kuzungumza na bibi ndipo Yule mama aliniambia mwanangu alifariki dunia hivyo niwe jasiri kwa sababu ilikuwa bahati mbaya.
Taarifa hiyo ilinihuzunisha nikaanza kulia kwani licha ya changamoto nilizopitia nilimpenda sana mwanangu na sikuhitaji kumpoteza, akina bibi waliendelea kunibembeleza.
Hata hivyo, nilimchikia sana mama pamoja na Evance kwa vitendo walivyonifanyia, mama kunipeleka kijijini na kunitelekeza na kijana wakle kunibaka na kunipa ujauzito.
Pamoja na chuki niliyokuwanayo, sikutaka kumuonesha mtu yeyote hali hiyo zaidi ya kusema ipo siku Mungu angenilipia kwa ukatili niliofanyiwa, nilipomkumbuka mama maumivu yalizidi kuwa makali nikajikuta nalia kwa sauti.
Tangu muda alipofariki mwanangu, hatukulala tena hadi kulipokucha ambapo watu walikusanyika na kujadiliana namna ya kumpumzisha mwanangu.
Je, nini kitaendelea?