Simulizi ya Dorcas 01 Mtunzi Juma Hiza

Simulizi ya Dorcas 01 Mtunzi Juma Hiza

Shunie

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2016
Posts
157,400
Reaction score
465,166
*SIMULIZI YA DORCAS-01*


Mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 25 ambaye ni yatima niliyezaliwa peke yangu kwa wazazi wangu ambao sikubahatika kuwaona, kwa sasa naishi jijini Dar es Salaam.

Kutokana na mikasa niliyopitia maishani mwangu, sitapenda kuliweka wazi jina langu halisi ila nitambue kwa jina la Dorcas.

Kwa mujibu wa mama niliyejikuta nipo mikononi mwake kimalezi, mama yangu yangu alikuwa mtu wa Rukwa na baba yangu alikuwa raia wa Zambia aliyekuwa akifanya biashara za bidhaa tofauti pamoja na samaki kutoka Ziwa Tanganyika eneo la Nkasi na kuwapeleka kwao Zambia.

Nilielezwa kwamba, mama na baba walikutana Kilando Namanyele, Rukwa wakaanzisha uhusiano wa kimapenzi ambao ulisababisha kupata ujauzito ambao mama aliubaini baada ya baba kurudi kwao.

Nilielezwa na mama huyo ambaye alifahamiana na mama mjini Sumbawanga katika biashara zao kwamba, mama alipobaini alikuwa mjamzito alitarajia baba akifika Kilando angemfahamisha kuhusu hali yake.

Jambo la kusikitisha ni kwamba baba hakurudi tena Tanzania ambapo mpaka leo haijulikani kama alikufa au alikumbwa na masaibu gani.

Kwa mujibu wa mama huyo ambaye naye hivi sasa ni marehemu, mama aliyekuwa amepanga chumba eneo la Chanji Sumbawanga aliendelea kuilea ile mimba peke yake.

Mama mlezi aliniambia kwamba, mama alipokaribia kujifungua alikwenda kwao Mpanda ili Mungu atakapomsaidia kujifungua salama awe chini ya uangalizi wa wazazi na ndugu zake.

Rafiki huyo wa mama aliniambia alimfanyia maandalizi ya safari ambapo mama alikwenda Mpanda akajifungua salama na kurejea Sumbawanga mjini kuendelea na maisha.

Aliongeza kunieleza kwamba, waliendelea kushirikiana na mama waliyeitana mtu na mdogo wake kiasi cha watu ambao hawakuwafahamu vizuri kudhani walikuwa ndugu wa damu.

Maisha yaliendelea lakini kutokana na mama kuwa na mtoto mdogo yaani mimi, hakuweza kusafiri kwenda mbali zaidi ya kuwa bize kunilea na kufanya biashara ndogondogo.

Nilielezwa kuwa nilipofikisha miezi sita, mama aliondoka na mimi kwenda mkoani Mbeya kwa rafiki yake waliyesoma pamoja aliyemuomba aende huko wakashirikiane kufanya biashara.

Kufuatia ombi hilo la rafiki yake, mama alikwenda Mbeya na kufikia Isanga ambapo rafiki yake huyo ambaye ni Mnyakyusa wa Masukulu wilayani Rungwe alikuwa amepanga chumba.

Mama huyo alinieleza, mama na rafiki yake huyo walikuwa wakifanya biashara ya kununua marahage, mchele na mahindi na kwenda kuyauza.

Wakati mwingine, siku ya Jumanne na Ijumaa ambayo inakuwa na mdana sehemu inayoitwa Kiwira, walikuwa wakienda kufanya biashara huko.

Aliongeza kunieleza kuwa, kwa vile hawakuwa na mtaji mkubwa walikuwa wanapata fedha kiasi walizoendeshea maisha yao huku mama akinilea.

Baada ya mama kukaa Mbeya kama miezi sita alikutana na mama mmoja wa Sumbawanga ambaye alikuwa akifahamu uhusiano wake na baba akamwambia aliwahi kumuona baba akifanya biashara zake Nkasi.

Kufuatia habari hiyo ambayo kwa mama ilikuwa njema sana, aliamua kurudi Sumbawanga kwa lengo la kwenda Nkasi akiwa na imani kabisa angeweza kukutana na baba.

Lengo lake lilikuwa ni kumuonesha mwanaye (mimi) na kama angekuwa tayari waanze kuishi maisha ya mume na mke.

Yule mama alinieleza, alipomshirikisha rafiki yake wa Mbeya alifurahi sana. Baada ya maandalizi tuliondoka na mama kwenda Sumbawanga na kufikia kwa rafiki wa mama aliyekuwa anaitwa mama James.

Sumbawanga tulikaa wiki moja tukaenda Kirando lengo likiwa ni kumtafuta baba.
Baada ya kuwasili Kirando, tulifikia kwa mama mmoja Mfipa ambaye alitupokea vizuri, mama huyo na mama walikuwa wanafahamiana vizuri.

Kwa mujibu wa mama huyo, siku iliyofuata, tulikwenda Nkasi ambako baba alikuwa akipeleka biashara zake na kuwauliza watu kama walikuwa wakimuona.

Jambo la kusikitisha ni kwamba, tulipofika huko baadhi ya watu walisema waliwahi kumuona na wengine walisema hawakuwahi kumuona muda mrefu.

Mama huyo alisema kwa jinsi mama alivyokuwa akihaha kumtafuta baba, wapo wanaume waliomtania kwamba kama angewakubalia walipokuwa wakimtokea asingepata tabu lakini kwa kuwa ‘alimshobokea’ Mzambia ndiyo ilikuwa faida yake.

Aliongeza kuwa, kauli za watu hao zilimuumiza mama ambaye licha ya kukaa kule mwezi mmoja akiamini siku moja baba angefika na kuonana naye hazikuzaa matunda.

Baada ya mama kukaa muda huo alikata tamaa akarudi Sumbawanga kwa rafiki yake ambapo aliendelea na biashara zake huku akinilea.

Niliambiwa kwamba wakati wa udogo wangu sikuwa nasumbuliwa na maradhi ya mara kwa mara na watu walikuwa wakimpongeza mama kwa kunizaa mtoto mzuri.

Maisha yaliendelea huku mama na rafiki yake wakifanya biashara ndogondogo lakini baada ya mwaka mmoja, Yule rafiki wa mama wa Mbeya alimtumia ujumbe kwamba alimhitaji aende huko.

Tulikwenda Mbeya, ambapo mama aliendelea na maisha. Kwa bahati mbaya sana kwa muda wote huo mama hakuwahi kunipeleka Mpanda ili nikaujue ukoo wake.

Nikiwa na miaka minne tukiwa Mbeya, aliwahi kuja mwanaume mmoja ambaye mama alinitambulisha kwamba alikuwa mjomba wangu.

Mama alinitambulisha kwamba mjomba wangu huyo alikuwa anaitwa Samweli na kwamba alikuwa akiishi Morogoro alikokuwa akifanya kazi katika mashamba ya miwa ya Mtibwa.

Mjomba wangu alifurahi sana kuniona, siku hiyo hiyo alipokula alituaga kwamba anakwenda Tunduma kisha Mpanda kuwasalimia wazazi na ndugu wengine.

Ingawa nilikuwa mdogo nilitamani sana kuongozana naye lakini mama aliniambia tungeenda wote atakapopata muda, nikamwambia sawa na maisha yakaendelea.

Kwa kuwa nilikuwa mtundu sana, nikiwa na miaka mitano nilipelekwa katika shule moja ya chekechea ambayo haikuwa mbali na eneo tulilokuwa tukiishi.

Maisha yaliendelea hadi nilipoanza darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Isanga, kwa kuwa kipindi hicho nilikuwa nina ufahamu nilitamani sana kumuona baba.

Kila nilipokuwa nikimuuliza mama baba yangu alikuwa wapi, alikuwa akiniambia alikuwa nchini Zambia, nilipomwambia lini angenipeleka nikamuone akawa ananidanganya tu siku zikawa zinakwenda.

Kuna wakati nilipokuwa namuuliza alikuwa akikosa raha na kuanza kulia, nilipohoji sababu za kulia alikuwa akinidanganya kwamba alikuwa anaumwa.

Ukweli ni kwamba kitendo cha mimi kutaka kumuona baba yangu ambaye hakujua alikuwa wapi kilimuweka katika wakati mgumu sana.

Nakumbuka siku moja rafiki yake ambaye nilikuwa namuita mama mkubwa, aliniita.
Nilipoitika aliniambia nikakae karibu yake, wakati huo mama alikuwa amekaa kwenye kiti kilichokaribiana naye.

“Dorcas!” mama huyo aliniita tena.
Nilipoitika aliniambia kwamba nilikuwa mtoto mzuri sana na mwenye akili nyingi, nikamshukuru, wakati huo sikujua mama mkubwa alitaka kuniambia nini.

Nilipomwambia ndiyo, akasema baba yangu alikuwepo hivyo nisiwe na wasiwasi ipo siku nitamuona kikubwa kuomba uzima, akaniomba nisiwe namuuliza mama kila wakati habari za baba.

Baada ya mama mkubwa kutoa kauli hiyo, mama alinitazama kwa huruma akaanza kulia, mama mkubwa akaanza kumbembeleza na kumsihi anyamaze kwani haikuwa vizuri.

“Dada naumia sana niache nilie tu!” mama alimwambia mama mkubwa.
Kitendo cha mama kulia, kilinihuzunisha sana nami nikajikuta nalia bila kujua kilichomliza mama, mama mkubwa akawa na kazi ya ziada kutunyamazisha.

Je, nini kiliendelea?
 
*SIMULIZI YA DORCAS-02*


Mama alipoendelea kulia, mama mkubwa aliniambia niende nikacheze na wenzangu, nikatoka ndani huku nikiwa sina amani kwani kitendo cha mama kulia kiliniumiza sana.

Nikiwa nimesimama kibarazani, nikawa natafakari kilichokuwa kikimliza mama nikahisi huenda baba yangu alifariki dunia lakini walinificha kuniambia ukweli.

Baada ya kuwaza sana, niliamini baba alifariki nikaanza kulia kisha nikaingia ndani ambapo mama mkubwa na mama waliniuliza nilikuwa nimepatwa na nini.

Kwa kuamini mawazo yangu, niliwaambia kwa nini walikuwa hawataki kuniambia ukweli kama baba yangu alikuwa amefariki, wote walipata fadhaa.

Mama mkubwa aliniambia nisogee karibu yake ambapo alinipakata na kuniambia niondoe mawazo hayo kabisa kwani baba alikuwa hai ila alikuwa Zambia.

Baada ya kuambiwa hivyo na kubembelezwa nilipata amani ya moyo, nilinyamaza nikatoka mapajani mwa mama mkubwa nikaenda nje nikaanza kuosha vyombo sikujua mama zangu waliendelea kujadili nini.

Mwezi wa nne tangu nilipoanza shule, mama alipata tena habari kwamba baba alikuwa akionekana Nkasi, bila kuchelea aliondoka na kuniacha na mama mkubwa akaenda huko kama mwanzo akiamini angekutananye.

Mama akiwa huko, mara kwa mara mama mkubwa alikuwa akiniambia nisiwe napenda kumuuliza mama kuhusu alipokuwa baba, nilipomuuliza sababu aliniambia ipo siku ningekutana naye.

Binafsi nilikuwa nakosa amani ya moyo nilipokuwa nikiwaona wenzangu ambao walikuwa wakilelewa na baba zao ndiyo maana nilikuwa siwezi kutulia bila ya kumbana mama anieleze alipokuwa baba.

Kama ilivyokuwa awali, baada ya mama kukaa Nkasi majuma mawili alirejea na kutufahamisha kwamba licha ya kuwa kule kwa muda ule hakuweza kumuona baba.

Mama alipotueleza hivyo, alianza kulia na kusababisha mashavu yake kuwa na michirizi ya machozi, mama mkubwa akapata kibarua cha kumbembeleza.

Kwa kuwa tayari nilikuwa nina ufahamu, nilimuuliza mama sababu hasa ya kulia kila nilipomhoji habari za baba ilikuwa nini, akaniambia alikuwa akiumia sana mimi kutomuona baba yangu.

Aliongeza kuwa, kikubwa zaidi kilichokuwa kikimuumiza ni pale nilipokuwa nambana kwa maswali aliko baba yangu ambaye hata yeye hakufahamu.

Wakati huo nilikuwa sielewi kama mama alijutia sana kitendo cha kuanzisha uhusiano wa kimapenzi na mtu ambaye hakumfahamu kiundani wala ndugu zake na kufikia hatua ya kupata ujauzito.

Ingawa kitendo cha kutomuona baba kilinikosesha raha sikuwa na la kufanya zaidi ya kuendelea na maisha, hata hivyo wenzangu walipokuwa wakiletewa zawadi na wazazi wao nilikuwa nikimfuata mama na kumwamba nami baba yangu angekuwepo ningepewa zawadi.

Ili kuniweka sawa, mama aliniambia nikiwaona wenzangu wamenunuliwa au kufanyiwa jambo lolote zuri na baba zao niwe ninamwambia kama ni nguo aninunulie nk.

Kweli tangu siku hiyo kila ilipotokea wenzangu wamenunuliwa nguo, viatu au kufanyiwa jambo lolote na baba zao, waliponiambia nami nilikwenda kumwambia mama.

Licha ya mama kuwa na kipato kidogo alikuwa akifanya juu chini kuhakikisha ananiweka sawa kwa kuninunulia chochote ambacho wenzangu walifanyiwa na baba zao.

Miongoni mwa marafiki zangu waliokuwa wakiniweka katika wakati mgumu na kutamani kuishi na baba yangu alikuwa Atuganile ambaye baba yake alikuwa bosi kazini kwao na mfanyabiashara.

Msichana huyo alikuwa anapendwa sana na baba ambaye kila alipopata nafasi alikuwa akimtoa ‘out’ na kumununulia nguo, viatu na vitu vingine mara kwa mara.

Zaidi ya yote kila alipokuwa akimpeleka sehemu za kucheza watoto walitumia gari, nilitamani sana na kuzungumza moyoni kwamba kama name ningekutana na baba yangu angenifanyia hayo.

Kila nilipowaza hivyo, nilikuwa namfuata mama na kuanza kulia nikimtaka anioneshe baba yangu, mama akaishia kulia kwani hakujua angempata wapi.

Tuliendelea kuishi na mama mkubwa aliyekuwa akinipenda sana hadi nilipofika darasa la nne, kipindi chote hicho mama hakuwahi kunipeleka Rukwa.

Mpaka sasa nashindwa kuelewa sababu iliyomfanya mama ashindwe kunipeleka huko licha ya mara kwa mara tulipofunga shule kumwambia anipeleke nikawafahamu babu, bibi na ndugu wengine.

Siku moja nilimbana anitafutie nauli kisha anielekeze ningefika, lakini alinipiga chenga kwamba kipindi kile cha Juni Rukwa kulikuwa na baridi hivyo ningeweza kupatwa na maradhi ya pumu ambayo yalikuwa ya hatari.

Kwa kuwa aliyeniambia hivyo alikuwa mama yangu, niliamini kauli yake, maisha yakaendelea huku nikizidi kupendwa shuleni na nyumbani kutokana na kumheshimu kila mtu.

Kwa upande wa shuleni, walimu walinipenda sana kwani nilikuwa nina akili, msafi nisiyependa mambo ambayo hayakuwa na maana.

Nilipofika darasa la tano siku moja mama mkubwa aliporejea nyumbani kutoka kwenye biashara zake aliongozana na mama mmoja.

Tukiwa tumeketi ndani, alitutambulisha na mama kwamba yule mama alikuwa rafiki yake waliyekutana kwenye mambo ya baishara na kwamba alikuwa akiishi Shinyanga.

Mama yule aliyeonekana alikuwa na uwezo alifurahi kutufahamu na kwa muda mchache aliokuwa pale nyumbani alitokea kunipenda.

Baada ya maongezi, mgeni huyo ambaye alisema alikuwa safarini kwenda Tunduma alinipatia shilingi elfu tano na kuahidi kupita tena wakati akirudi Shinyanga.

Kabla ya kuondoka aliwapatia mama na mama mkubwa kiasi cha fedha ambacho sikukifahamu, tulimshukuru ndipo aliagana akina mama wakamsindikiza.

Akina mama waliporejea, mama mkubwa alitueleza kwamba alifahamiana na yule mama miaka minne iliyopita baada ya kumsaidia kujumua maharage Mbozi na kumuunganisha na jirani yake aliyekuwa akilima mpunga Usangu.

Tangu wakati huo kila yule mama alipokuwa akienda Tunduma kununua nguo na vitu vingine alikuwa akimtembelea japo hakuwa akilala pale nyumbani.

Mama mkubwa alisema, urafiki wao ulikomaa na kuwa kama ndugu ambapo mama mkubwa alikuwa akimuita yule mama dada.

Kama yule mama alivyoahidi, siku mbili baadaye alirejea kutoka Tunduma na kuja Isanga ambapo kila mmoja wetu alimletea zawadi, akina mama walipewa suti na mimi nilipewa gauni zuri sana.

Baada ya kupiga stori za hapa na pale, alituaga ambapo aliondoka na gari binafsi kuelekea jijini Dar es Salaam alikokuwa anafuata mizigo flani kisha aende Shinyanga.

Usiku wa siku hiyo, baada ya kula mama alimsifia sana yule mama wa Shinyanga kwamba alikuwa mkarimu, mcheshi na mwenye upendo wa dhati.

“Ni kweli kabisa unachosema, mimi amenisaidia sana na aliwahi kuniambia asingekuwa na majukumu makubwa ya kuilea familia baada ya mumewe kufariki angeniongezea mtaji,” mama mkubwa alituambia.
Kufuatia kauli hiyo, mama alisikitika sana na kusema:

“Kumbe yule mama ni mjane? Kweli amepata pigo kubwa sana!”
“Ndiyo hivyo, Mungu akiamua kumchukua mtu wake achagui atangulie nani ndicho kilichotokea kwa mama Evance, mume wake katangulia,” mama mkubwa alituambia.

Je, nini kitaendelea?
 
Naona kitu kipya hiki
*SIMULIZI YA DORCAS-02*


Mama alipoendelea kulia, mama mkubwa aliniambia niende nikacheze na wenzangu, nikatoka ndani huku nikiwa sina amani kwani kitendo cha mama kulia kiliniumiza sana.

Nikiwa nimesimama kibarazani, nikawa natafakari kilichokuwa kikimliza mama nikahisi huenda baba yangu alifariki dunia lakini walinificha kuniambia ukweli.

Baada ya kuwaza sana, niliamini baba alifariki nikaanza kulia kisha nikaingia ndani ambapo mama mkubwa na mama waliniuliza nilikuwa nimepatwa na nini.

Kwa kuamini mawazo yangu, niliwaambia kwa nini walikuwa hawataki kuniambia ukweli kama baba yangu alikuwa amefariki, wote walipata fadhaa.

Mama mkubwa aliniambia nisogee karibu yake ambapo alinipakata na kuniambia niondoe mawazo hayo kabisa kwani baba alikuwa hai ila alikuwa Zambia.

Baada ya kuambiwa hivyo na kubembelezwa nilipata amani ya moyo, nilinyamaza nikatoka mapajani mwa mama mkubwa nikaenda nje nikaanza kuosha vyombo sikujua mama zangu waliendelea kujadili nini.

Mwezi wa nne tangu nilipoanza shule, mama alipata tena habari kwamba baba alikuwa akionekana Nkasi, bila kuchelea aliondoka na kuniacha na mama mkubwa akaenda huko kama mwanzo akiamini angekutananye.

Mama akiwa huko, mara kwa mara mama mkubwa alikuwa akiniambia nisiwe napenda kumuuliza mama kuhusu alipokuwa baba, nilipomuuliza sababu aliniambia ipo siku ningekutana naye.

Binafsi nilikuwa nakosa amani ya moyo nilipokuwa nikiwaona wenzangu ambao walikuwa wakilelewa na baba zao ndiyo maana nilikuwa siwezi kutulia bila ya kumbana mama anieleze alipokuwa baba.

Kama ilivyokuwa awali, baada ya mama kukaa Nkasi majuma mawili alirejea na kutufahamisha kwamba licha ya kuwa kule kwa muda ule hakuweza kumuona baba.

Mama alipotueleza hivyo, alianza kulia na kusababisha mashavu yake kuwa na michirizi ya machozi, mama mkubwa akapata kibarua cha kumbembeleza.

Kwa kuwa tayari nilikuwa nina ufahamu, nilimuuliza mama sababu hasa ya kulia kila nilipomhoji habari za baba ilikuwa nini, akaniambia alikuwa akiumia sana mimi kutomuona baba yangu.

Aliongeza kuwa, kikubwa zaidi kilichokuwa kikimuumiza ni pale nilipokuwa nambana kwa maswali aliko baba yangu ambaye hata yeye hakufahamu.

Wakati huo nilikuwa sielewi kama mama alijutia sana kitendo cha kuanzisha uhusiano wa kimapenzi na mtu ambaye hakumfahamu kiundani wala ndugu zake na kufikia hatua ya kupata ujauzito.

Ingawa kitendo cha kutomuona baba kilinikosesha raha sikuwa na la kufanya zaidi ya kuendelea na maisha, hata hivyo wenzangu walipokuwa wakiletewa zawadi na wazazi wao nilikuwa nikimfuata mama na kumwamba nami baba yangu angekuwepo ningepewa zawadi.

Ili kuniweka sawa, mama aliniambia nikiwaona wenzangu wamenunuliwa au kufanyiwa jambo lolote zuri na baba zao niwe ninamwambia kama ni nguo aninunulie nk.

Kweli tangu siku hiyo kila ilipotokea wenzangu wamenunuliwa nguo, viatu au kufanyiwa jambo lolote na baba zao, waliponiambia nami nilikwenda kumwambia mama.

Licha ya mama kuwa na kipato kidogo alikuwa akifanya juu chini kuhakikisha ananiweka sawa kwa kuninunulia chochote ambacho wenzangu walifanyiwa na baba zao.

Miongoni mwa marafiki zangu waliokuwa wakiniweka katika wakati mgumu na kutamani kuishi na baba yangu alikuwa Atuganile ambaye baba yake alikuwa bosi kazini kwao na mfanyabiashara.

Msichana huyo alikuwa anapendwa sana na baba ambaye kila alipopata nafasi alikuwa akimtoa ‘out’ na kumununulia nguo, viatu na vitu vingine mara kwa mara.

Zaidi ya yote kila alipokuwa akimpeleka sehemu za kucheza watoto walitumia gari, nilitamani sana na kuzungumza moyoni kwamba kama name ningekutana na baba yangu angenifanyia hayo.

Kila nilipowaza hivyo, nilikuwa namfuata mama na kuanza kulia nikimtaka anioneshe baba yangu, mama akaishia kulia kwani hakujua angempata wapi.

Tuliendelea kuishi na mama mkubwa aliyekuwa akinipenda sana hadi nilipofika darasa la nne, kipindi chote hicho mama hakuwahi kunipeleka Rukwa.

Mpaka sasa nashindwa kuelewa sababu iliyomfanya mama ashindwe kunipeleka huko licha ya mara kwa mara tulipofunga shule kumwambia anipeleke nikawafahamu babu, bibi na ndugu wengine.

Siku moja nilimbana anitafutie nauli kisha anielekeze ningefika, lakini alinipiga chenga kwamba kipindi kile cha Juni Rukwa kulikuwa na baridi hivyo ningeweza kupatwa na maradhi ya pumu ambayo yalikuwa ya hatari.

Kwa kuwa aliyeniambia hivyo alikuwa mama yangu, niliamini kauli yake, maisha yakaendelea huku nikizidi kupendwa shuleni na nyumbani kutokana na kumheshimu kila mtu.

Kwa upande wa shuleni, walimu walinipenda sana kwani nilikuwa nina akili, msafi nisiyependa mambo ambayo hayakuwa na maana.

Nilipofika darasa la tano siku moja mama mkubwa aliporejea nyumbani kutoka kwenye biashara zake aliongozana na mama mmoja.

Tukiwa tumeketi ndani, alitutambulisha na mama kwamba yule mama alikuwa rafiki yake waliyekutana kwenye mambo ya baishara na kwamba alikuwa akiishi Shinyanga.

Mama yule aliyeonekana alikuwa na uwezo alifurahi kutufahamu na kwa muda mchache aliokuwa pale nyumbani alitokea kunipenda.

Baada ya maongezi, mgeni huyo ambaye alisema alikuwa safarini kwenda Tunduma alinipatia shilingi elfu tano na kuahidi kupita tena wakati akirudi Shinyanga.

Kabla ya kuondoka aliwapatia mama na mama mkubwa kiasi cha fedha ambacho sikukifahamu, tulimshukuru ndipo aliagana akina mama wakamsindikiza.

Akina mama waliporejea, mama mkubwa alitueleza kwamba alifahamiana na yule mama miaka minne iliyopita baada ya kumsaidia kujumua maharage Mbozi na kumuunganisha na jirani yake aliyekuwa akilima mpunga Usangu.

Tangu wakati huo kila yule mama alipokuwa akienda Tunduma kununua nguo na vitu vingine alikuwa akimtembelea japo hakuwa akilala pale nyumbani.

Mama mkubwa alisema, urafiki wao ulikomaa na kuwa kama ndugu ambapo mama mkubwa alikuwa akimuita yule mama dada.

Kama yule mama alivyoahidi, siku mbili baadaye alirejea kutoka Tunduma na kuja Isanga ambapo kila mmoja wetu alimletea zawadi, akina mama walipewa suti na mimi nilipewa gauni zuri sana.

Baada ya kupiga stori za hapa na pale, alituaga ambapo aliondoka na gari binafsi kuelekea jijini Dar es Salaam alikokuwa anafuata mizigo flani kisha aende Shinyanga.

Usiku wa siku hiyo, baada ya kula mama alimsifia sana yule mama wa Shinyanga kwamba alikuwa mkarimu, mcheshi na mwenye upendo wa dhati.

“Ni kweli kabisa unachosema, mimi amenisaidia sana na aliwahi kuniambia asingekuwa na majukumu makubwa ya kuilea familia baada ya mumewe kufariki angeniongezea mtaji,” mama mkubwa alituambia.
Kufuatia kauli hiyo, mama alisikitika sana na kusema:

“Kumbe yule mama ni mjane? Kweli amepata pigo kubwa sana!”
“Ndiyo hivyo, Mungu akiamua kumchukua mtu wake achagui atangulie nani ndicho kilichotokea kwa mama Evance, mume wake katangulia,” mama mkubwa alituambia.

Je, nini kitaendelea?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwenye story nimeona soko la ""kiwila" nilikuwaga na nunua ndizi sana mitaa iyo ukitoa buku wapewa kapu zima la ndizi cjui mpaka leo ndo ivo maana ni miaka 10sasa.( utamu njoo uwongo kolea tunasubiri kusikiliza kilichomkuta mtoto mzuri dorcus)
 
*SIMULIZI YA DORCAS-03*


Kutokana na ukarimu aliokuwa nao mama huyo, mama alihuzunika sana alipoambiwa kwamba mumewe alikuwa amefariki dunia ndipo alimwuliza mama mkubwa kama alikuwa na watoto.

“Aliniambia kwamba ana watoto watatu, wawili wa kike na wa kiume anaitwa Evance,” mama mkubwa alimfahamisha mama.

Mama na mama mkubwa waliendelea kumzungumzia mama huyo wa Shinyanga jinsi alivyokuwa na upendo kwa watu wengine ndipo niliwaacha na kwenda kulala.

Katikati ya usingizi niliota ndoto tupo sokoni mama ambapo alikuwa akiuza mchele na watu walikuwa wengi sana, wakati mama akiwa bize kuwahudumia wateja mtu nisiyemfahamu alinigusa begani.

Nilipogeuka kumwangalia, alikuwa ni mtu mzima ambaye alitabasamu na kunionesha mwenzake na kuniuliza:

“Unamfahamu huyu hapa?”
Kabla sijamjibu, mama aliyewasikia watu hao alipogeuka kuwaangalia aliruka kwa furaha na kumkumbatia yule bwana niliyeulizwa kama nilikuwa namfahamu.
“Gilbert, hivi ni wewe kweli au naota ndoto ya mchana, siamini macho yangu!” mama alimwambia yule bwana.

Jamaa huyo akiwa amekumbatiana na mama huku akitabasamu, alimjibu kwamba alikuwa yeye ndipo mama aliniita na kunifahamisha kuwa yule alikuwa baba yangu.

Kama alivyofanya mama, nami kwa furaha nilimkumbatia baba yangu na kuanza kulia huku nikimuuliza alikuwa wapi muda wote.

Baba ambaye alikuwa amepigwa butwaa kuambiwa mimi nilikuwa mwanaye, akamuuliza mama nilikuwa mwanaye kivipi, ile mama anataka kumwambia nilishtuka kutoka usingizini.

Ndoto hiyo ilinikosesha raha sana nikajikuta ninalia kwa sauti kitendo kilichosababisha mama mkubwa na mama kuamka na kuingia chumbani kwangu kujua nilipatwa na nini.

“Dorcas mwanangu umepatwa na nini mbona unalia?” mama aliniuliza.

Baada ya kuwaona akina mama nikazidisha kulia bila kuwaambia sababu, mama mkubwa aliketi kwenye mfumbati wa kitanda na kuanza kuniuliza sababu ya kulia.

“Nimemuona baba yangu, lakini kabla sijazungumza naye ameondoka,” nilimwambia mama mkubwa.

Kauli yangu iliwashtua ambapo mama aliniuliza baba yangu nilimuona wapi na kusema mbona niliwaacha njia panda!
Niliwafahamisha kwamba nilimuona kwenye ndoto, akiwa na rafiki yake kisha kwa hamaki nikamwambia mama nilimtaka baba yangu, kauli ambayo ilimuumiza sana akaanza kulia.

Kitendo cha mama kulia, kilinifanya nami niendelee kulia, mama mkubwa akawa na kazi ya ziada ya kutubembeleza kisha aliniita:
“Dorcas!”

Nilipoitika aliniuliza kwa nini nilikuwa namuweka mama katika wakati mgumu na kwa nini sikupenda kumuelewa aliponiambia nivumilie ipo siku ningekuja kumuona baba yangu!

Kufuatia kuniuliza hivyo, nilimwambia kilichoniliza ni kitendo cha baba kunijia kwenye ndoto wakati nilitamani sana kumuona laivu ili nami nifurahi naye kama wenzangu.

Kama ambavyo alikuwa akifanya mara kwa mara nilipokuwa nalia kuhusu kuhitaji kumuona baba, aliniomba nisilie na kunipa moyo kwamba ipo siku ningekutana naye.

“Mwanangu Dorcas, kwa kuwa umeanza kumuota baba yako ni dalili kwamba karibu mtaonana, hivyo kuwa na subira, sawa mama?” Dorcas alimkalili mama mkubwa.

Nilimwambia sawa japo sikufahamu ningeonanaje na baba yangu ambaye katika ndoto niliyoota nilisikia mama akimwita kwa jina la Gilbert.

Baada ya mama mkubwa kuniambia hivyo alinieleza nilale kwa amani kisha wakaniacha na kwenda kulala chumbani kwao, sikujua walichoongea huko.

Japo nilikuwa bado mdogo, nikiwa nimejilaza kitandani, sikuweza kupata usingizi kwa wakati kwani muda mwingi nilikuwa namuwaza baba yangu.

Hata hivyo, baadaye nilipitiwa na usingizi hadi nilipokuja kushtuka saa kumi na moja alfajiri na kujikuta kichwa kikiuma sana.

Kutokana na maumivu niliyopata nikaanza kulia na kumwita mama, wote waliamka na kuja chumbani nilikokuwa nalala wakifikiria sababu iliyoniliza ilihusu baba.

Mama mkubwa aliponiuliza nini kilinisibu niliwaambia kichwa kilikuwa kinauma sana, waliniuliza kilianza muda gani niliwafahamisha kwamba ni baada ya kushtuka kutoka usingizini.

Kwa kuwa ndani kulikuwa na panadol, mama mkubwa alizifuata pamoja na maji nikameza kisha akaniambia nilale kitapoa, cha kusikitisha ni kwamba sikupata nafuu.

Haukupita muda mrefu nikaanza kulia kwa sauti huku nikipiga kelele, mama mkubwa akamwambia mama alihisi malaria ilipanda kichwani.

Kutokana na hali niliyokuwa nayo, baadhi ya majirani zetu waliamka na kuja kujua sababu ya kulia kwangu, wakawaambia walihisi malaria ilipanda kichwani.

Akina mama walijiandaa, wakaniandaa na kunipeleka kwenye zahanati moja iliyopo Isanga, daktari aliyekuwepo zamu baada ya kuona situlii, kwa mujibu wa mama mkubwa, alinichoma dawa ya usingizi, nikalala.

Nililala saa nzima, dawa hiyo ilipoisha nguvu niliamka na kujikuta nimepumzishwa pale hospitali nikawauliza nilipatwa na tatizo gani, mama akaniambia nilikuwa naumwa.

Tukiwa tunazungumza na mama, yule daktari aliingia akaniita jina langu na kusema: “ Unajisikiaje sasa?”

Nilimwambia nilihisi kichwa kuniuma akanipa pole na kuniambia nilikuwa nina malaria, kumbe tayari alinichukua damu na kuipima.

Baada ya daktari huyo kuniandikia dawa alimpa mama maelezo ya namna ya kutumia kisha alinitania kwamba niache uoga wa kuumwa, tukarejea nyumbani huku kila mmoja wetu akiamini nilikuwa naumwa malaria.

Kama mama alivyokuwa amepewa maelezo na daktari, baada ya kula alinipatia dawa kisha nilikwenda kulala, mama mkubwa alikwenda kwenye biashara zake na kumuacha mama aliyekuwa akiniangalia.

Siku hiyo nililala hadi alasiri, nilipoamka nilijisikia nimepata nafuu jambo lililomfarahisha mama. Hata mama mkubwa aliporejea na kunikuta katika hali hiyo alifurahi.

Kufuatia kuumwa, sikwenda shuleni siku tatu hadi nilipopa kabisa. Tangu nilipougua nilimaliza wiki mbili ndipo nilianza kutokewa na vitu vya ajabu nikiwa nimelala.

Siku moja nikiwa nimelala chumbani nilijikuta nikikabwa shingoni na mtu ambaye sikumuona, kila nilipojaribu kuwaita akina mama sikuweza kufanikiwa kwani sauti haikutoka.

Hata hivyo, muda mfupi baadaye mtu huyo alianiachia nilipotazama ukutani niliona kama kimvuli cha mtu kikiishia ndipo nikaanza kuwaita akina mama.

Mama mkubwa na mama walipoingia chumbani kwangu walinikuta nimekaa kitandani huku nikihema, mama aliponiuliza nilipatwa na nini nikawaeleza.
“Huenda ulipolala uliangalia juu, mara nyingi mtu akilala chali huota ndoto za kukabwa,” mama mkubwa aliniambia.

Kwa kuwa sikulala chali niliwaambia, mama mkubwa akasema basi kulikuwa na jinamizi lilikuja kunisumbua, kwa hofu niliyokuwanayo niliwaambia siwezi kulala peke yangu mle chumbani.

Akina mama walikubaliana nami tukaenda chumbani kwao ambako tuliendelea kuongea kuhusu jinamizi hilo.
Mama mkubwa alisema alishangazwa sana na jambo hilo kwani tangu alipohamia pale aliwahi kukabwa mara mbili tena zamani, baada hapo haikuwahi kutokea tena.

Kulipokucha nilijiandaa, kutokana na baridi ya Mbeya nilikunywa chai na kipande cha mkate mweusi ulioandaliwa na mama mkubwa ambaye alikuwa akipenda sana kitafunwa hicho kisha niliwaaga akina mama.

Wakati wa kwenda shuleni ilikuwa lazima nipite kwenye uwanja wa nyumba ya mama mmoja sitapenda kumtaja kwa jina, nikamkuta akifagia, nilipomsalimia hakuitikia.

Awali nilifikirim hakunisikia, nikamwamkia tena akawa bize kufagia, nikaamua kumuacha nikaongeza mwendo kuelekea shuleni lakini nikawa najiuliza nilimkosea nini yule mama mpaka asiitikie salamu yangu.

Hata hivyo, kwa akili za kitoto wala sikumfuatilia. Nilipofika shuleni, tulifanya usafi wa mazingira kisha tuliingia darasani tayari kwa kuanza vipindi.

Nakumbuka siku hiyo mwalimu wa kwaza kuingia darasani alikuwa wa kipindi cha hesabu, alipokuwa akitufundisha ghafla nilihisi kichwa kuniuma.

Mwanzo nilifikiria kingepoa lakini kadiri muda ulivyosonga mbele kikazidi kuniuma, nikainama chini ya dawati.
Mwalimu aliponiona aliniuliza sababu za kuinama chini, nilimwambia kichwa kilikuwa kinauma, jambo la kushangaza nilipomweleza hivyo mwalimu, kichwa kikazidi kuuna nikashindwa kuvumilia nikaanza kulia.

Yule mwalimu kwa kushirikiana na wanafunzi watatu walinibeba na kunipeleka ofisini ambako niliendelea kulia, mwalimu alimuuliza mmoja wa wale wanafunzi kama alikuwa akipahamu nyumbani ili akamwambie mama.

Kwa kuwa yule mwanafunzi alikuwa anapajua nyumbani, alikwenda mbio, kwa bahati mbaya hakumkuta mama wala mama mkubwa kwani walikuwa wamekwenda kwenye biashara zao.

Kwa kuwa kutoka pale shuleni kwenda ilipokuwa zahanati hapakuwa mbali, walimu wawili na mwanafunzi mmoja walinipeleka, nikafanyiwa kipimo cha malaria

Majibu yalipotoka sikuwa nayo, nilipewa dawa ya kutuliza maumivu, hata baada ya kumeza bado kichwa kilikuwa kikiuma sana.

Wakati walimu na daktari wakitafakari, akina mama walipopewa taarifa nwa mwanafunzi mmoja walifika na kuniuliza nini kilikuwa kikinisumbua, kwa shida niliwaambia kichwa.

Je,nini kitaendelea?
 
Dorcas analogwa na jilani
*SIMULIZI YA DORCAS-03*


Kutokana na ukarimu aliokuwa nao mama huyo, mama alihuzunika sana alipoambiwa kwamba mumewe alikuwa amefariki dunia ndipo alimwuliza mama mkubwa kama alikuwa na watoto.

“Aliniambia kwamba ana watoto watatu, wawili wa kike na wa kiume anaitwa Evance,” mama mkubwa alimfahamisha mama.

Mama na mama mkubwa waliendelea kumzungumzia mama huyo wa Shinyanga jinsi alivyokuwa na upendo kwa watu wengine ndipo niliwaacha na kwenda kulala.

Katikati ya usingizi niliota ndoto tupo sokoni mama ambapo alikuwa akiuza mchele na watu walikuwa wengi sana, wakati mama akiwa bize kuwahudumia wateja mtu nisiyemfahamu alinigusa begani.

Nilipogeuka kumwangalia, alikuwa ni mtu mzima ambaye alitabasamu na kunionesha mwenzake na kuniuliza:

“Unamfahamu huyu hapa?”
Kabla sijamjibu, mama aliyewasikia watu hao alipogeuka kuwaangalia aliruka kwa furaha na kumkumbatia yule bwana niliyeulizwa kama nilikuwa namfahamu.
“Gilbert, hivi ni wewe kweli au naota ndoto ya mchana, siamini macho yangu!” mama alimwambia yule bwana.

Jamaa huyo akiwa amekumbatiana na mama huku akitabasamu, alimjibu kwamba alikuwa yeye ndipo mama aliniita na kunifahamisha kuwa yule alikuwa baba yangu.

Kama alivyofanya mama, nami kwa furaha nilimkumbatia baba yangu na kuanza kulia huku nikimuuliza alikuwa wapi muda wote.

Baba ambaye alikuwa amepigwa butwaa kuambiwa mimi nilikuwa mwanaye, akamuuliza mama nilikuwa mwanaye kivipi, ile mama anataka kumwambia nilishtuka kutoka usingizini.

Ndoto hiyo ilinikosesha raha sana nikajikuta ninalia kwa sauti kitendo kilichosababisha mama mkubwa na mama kuamka na kuingia chumbani kwangu kujua nilipatwa na nini.

“Dorcas mwanangu umepatwa na nini mbona unalia?” mama aliniuliza.

Baada ya kuwaona akina mama nikazidisha kulia bila kuwaambia sababu, mama mkubwa aliketi kwenye mfumbati wa kitanda na kuanza kuniuliza sababu ya kulia.

“Nimemuona baba yangu, lakini kabla sijazungumza naye ameondoka,” nilimwambia mama mkubwa.

Kauli yangu iliwashtua ambapo mama aliniuliza baba yangu nilimuona wapi na kusema mbona niliwaacha njia panda!
Niliwafahamisha kwamba nilimuona kwenye ndoto, akiwa na rafiki yake kisha kwa hamaki nikamwambia mama nilimtaka baba yangu, kauli ambayo ilimuumiza sana akaanza kulia.

Kitendo cha mama kulia, kilinifanya nami niendelee kulia, mama mkubwa akawa na kazi ya ziada ya kutubembeleza kisha aliniita:
“Dorcas!”

Nilipoitika aliniuliza kwa nini nilikuwa namuweka mama katika wakati mgumu na kwa nini sikupenda kumuelewa aliponiambia nivumilie ipo siku ningekuja kumuona baba yangu!

Kufuatia kuniuliza hivyo, nilimwambia kilichoniliza ni kitendo cha baba kunijia kwenye ndoto wakati nilitamani sana kumuona laivu ili nami nifurahi naye kama wenzangu.

Kama ambavyo alikuwa akifanya mara kwa mara nilipokuwa nalia kuhusu kuhitaji kumuona baba, aliniomba nisilie na kunipa moyo kwamba ipo siku ningekutana naye.

“Mwanangu Dorcas, kwa kuwa umeanza kumuota baba yako ni dalili kwamba karibu mtaonana, hivyo kuwa na subira, sawa mama?” Dorcas alimkalili mama mkubwa.

Nilimwambia sawa japo sikufahamu ningeonanaje na baba yangu ambaye katika ndoto niliyoota nilisikia mama akimwita kwa jina la Gilbert.

Baada ya mama mkubwa kuniambia hivyo alinieleza nilale kwa amani kisha wakaniacha na kwenda kulala chumbani kwao, sikujua walichoongea huko.

Japo nilikuwa bado mdogo, nikiwa nimejilaza kitandani, sikuweza kupata usingizi kwa wakati kwani muda mwingi nilikuwa namuwaza baba yangu.

Hata hivyo, baadaye nilipitiwa na usingizi hadi nilipokuja kushtuka saa kumi na moja alfajiri na kujikuta kichwa kikiuma sana.

Kutokana na maumivu niliyopata nikaanza kulia na kumwita mama, wote waliamka na kuja chumbani nilikokuwa nalala wakifikiria sababu iliyoniliza ilihusu baba.

Mama mkubwa aliponiuliza nini kilinisibu niliwaambia kichwa kilikuwa kinauma sana, waliniuliza kilianza muda gani niliwafahamisha kwamba ni baada ya kushtuka kutoka usingizini.

Kwa kuwa ndani kulikuwa na panadol, mama mkubwa alizifuata pamoja na maji nikameza kisha akaniambia nilale kitapoa, cha kusikitisha ni kwamba sikupata nafuu.

Haukupita muda mrefu nikaanza kulia kwa sauti huku nikipiga kelele, mama mkubwa akamwambia mama alihisi malaria ilipanda kichwani.

Kutokana na hali niliyokuwa nayo, baadhi ya majirani zetu waliamka na kuja kujua sababu ya kulia kwangu, wakawaambia walihisi malaria ilipanda kichwani.

Akina mama walijiandaa, wakaniandaa na kunipeleka kwenye zahanati moja iliyopo Isanga, daktari aliyekuwepo zamu baada ya kuona situlii, kwa mujibu wa mama mkubwa, alinichoma dawa ya usingizi, nikalala.

Nililala saa nzima, dawa hiyo ilipoisha nguvu niliamka na kujikuta nimepumzishwa pale hospitali nikawauliza nilipatwa na tatizo gani, mama akaniambia nilikuwa naumwa.

Tukiwa tunazungumza na mama, yule daktari aliingia akaniita jina langu na kusema: “ Unajisikiaje sasa?”

Nilimwambia nilihisi kichwa kuniuma akanipa pole na kuniambia nilikuwa nina malaria, kumbe tayari alinichukua damu na kuipima.

Baada ya daktari huyo kuniandikia dawa alimpa mama maelezo ya namna ya kutumia kisha alinitania kwamba niache uoga wa kuumwa, tukarejea nyumbani huku kila mmoja wetu akiamini nilikuwa naumwa malaria.

Kama mama alivyokuwa amepewa maelezo na daktari, baada ya kula alinipatia dawa kisha nilikwenda kulala, mama mkubwa alikwenda kwenye biashara zake na kumuacha mama aliyekuwa akiniangalia.

Siku hiyo nililala hadi alasiri, nilipoamka nilijisikia nimepata nafuu jambo lililomfarahisha mama. Hata mama mkubwa aliporejea na kunikuta katika hali hiyo alifurahi.

Kufuatia kuumwa, sikwenda shuleni siku tatu hadi nilipopa kabisa. Tangu nilipougua nilimaliza wiki mbili ndipo nilianza kutokewa na vitu vya ajabu nikiwa nimelala.

Siku moja nikiwa nimelala chumbani nilijikuta nikikabwa shingoni na mtu ambaye sikumuona, kila nilipojaribu kuwaita akina mama sikuweza kufanikiwa kwani sauti haikutoka.

Hata hivyo, muda mfupi baadaye mtu huyo alianiachia nilipotazama ukutani niliona kama kimvuli cha mtu kikiishia ndipo nikaanza kuwaita akina mama.

Mama mkubwa na mama walipoingia chumbani kwangu walinikuta nimekaa kitandani huku nikihema, mama aliponiuliza nilipatwa na nini nikawaeleza.
“Huenda ulipolala uliangalia juu, mara nyingi mtu akilala chali huota ndoto za kukabwa,” mama mkubwa aliniambia.

Kwa kuwa sikulala chali niliwaambia, mama mkubwa akasema basi kulikuwa na jinamizi lilikuja kunisumbua, kwa hofu niliyokuwanayo niliwaambia siwezi kulala peke yangu mle chumbani.

Akina mama walikubaliana nami tukaenda chumbani kwao ambako tuliendelea kuongea kuhusu jinamizi hilo.
Mama mkubwa alisema alishangazwa sana na jambo hilo kwani tangu alipohamia pale aliwahi kukabwa mara mbili tena zamani, baada hapo haikuwahi kutokea tena.

Kulipokucha nilijiandaa, kutokana na baridi ya Mbeya nilikunywa chai na kipande cha mkate mweusi ulioandaliwa na mama mkubwa ambaye alikuwa akipenda sana kitafunwa hicho kisha niliwaaga akina mama.

Wakati wa kwenda shuleni ilikuwa lazima nipite kwenye uwanja wa nyumba ya mama mmoja sitapenda kumtaja kwa jina, nikamkuta akifagia, nilipomsalimia hakuitikia.

Awali nilifikirim hakunisikia, nikamwamkia tena akawa bize kufagia, nikaamua kumuacha nikaongeza mwendo kuelekea shuleni lakini nikawa najiuliza nilimkosea nini yule mama mpaka asiitikie salamu yangu.

Hata hivyo, kwa akili za kitoto wala sikumfuatilia. Nilipofika shuleni, tulifanya usafi wa mazingira kisha tuliingia darasani tayari kwa kuanza vipindi.

Nakumbuka siku hiyo mwalimu wa kwaza kuingia darasani alikuwa wa kipindi cha hesabu, alipokuwa akitufundisha ghafla nilihisi kichwa kuniuma.

Mwanzo nilifikiria kingepoa lakini kadiri muda ulivyosonga mbele kikazidi kuniuma, nikainama chini ya dawati.
Mwalimu aliponiona aliniuliza sababu za kuinama chini, nilimwambia kichwa kilikuwa kinauma, jambo la kushangaza nilipomweleza hivyo mwalimu, kichwa kikazidi kuuna nikashindwa kuvumilia nikaanza kulia.

Yule mwalimu kwa kushirikiana na wanafunzi watatu walinibeba na kunipeleka ofisini ambako niliendelea kulia, mwalimu alimuuliza mmoja wa wale wanafunzi kama alikuwa akipahamu nyumbani ili akamwambie mama.

Kwa kuwa yule mwanafunzi alikuwa anapajua nyumbani, alikwenda mbio, kwa bahati mbaya hakumkuta mama wala mama mkubwa kwani walikuwa wamekwenda kwenye biashara zao.

Kwa kuwa kutoka pale shuleni kwenda ilipokuwa zahanati hapakuwa mbali, walimu wawili na mwanafunzi mmoja walinipeleka, nikafanyiwa kipimo cha malaria

Majibu yalipotoka sikuwa nayo, nilipewa dawa ya kutuliza maumivu, hata baada ya kumeza bado kichwa kilikuwa kikiuma sana.

Wakati walimu na daktari wakitafakari, akina mama walipopewa taarifa nwa mwanafunzi mmoja walifika na kuniuliza nini kilikuwa kikinisumbua, kwa shida niliwaambia kichwa.

Je,nini kitaendelea?

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom