Basi Nenda
JF-Expert Member
- Jul 29, 2017
- 20,142
- 45,808
tupo.Abeeh
Jamani..naona unanitafutia kosa uniache ...nishagunduaHahaha tatizo ww kila mtu unampenda
Sehemu ya 61.
Inawezekana huyu Scaila alikuwa akielekea kulekule ila nilimuokoa. Huyu Scaila sikukutana naye kanisani au sehemu ya maana sana, nilikutana naye njiani, sehemu ya hovyo, kwenye ajali mbaya lakini ndiyo hivyo nikaja kumuoa na kuwa mke mwema kwangu.
Kuna watu wanahisi kukutana na mtu kanisani ndiyo ndoa huwa bora! Hapana! Kuna watu wanakutana huko lakini ndoa yao kila siku huwa ni ugomvi kana kwamba hawajui chochote kuhusu Mungu.
Kitu cha kwanza kitakachoifanya ndoa kuwa bora, katika kipindi cha uhusiano wenu, unachotakiwa kufanya ni kumtengeneza mwenzako awe bora, mwanaume amtengeneze mwanamke na hivyohivyo mwanamke amtengeneze mwanaume.
Unapomuona amevaa nguo, msifie, mwambie jinsi unavyojivunia kuwa mke ama mchumba wake. Hakuna mtu asiyependa sifa, msifie mara kwa mara, sifia mapishi yake, sifia jitihada zake, mavazi yake, sifia kila kitu kwani usiposifia, huko nje akisifiwa kidogo tu, ndugu yangu hesabia maumivu.
Na cha kuongezea, kwenye uhusiano huo, hakikisha kuna unyenyekevu, utakapokosea, jutia kosa lako, omba msamaha wa dhati na si kujifanya wewe mwanaume hutakiwi kumuomba msamaha mke ama mchumba wako.
MWISHO
Natumaini wote mmejifunza mengi katika simulizi hii, kwa yale ambayo ni mafunzo kwenu, yachukueni lakini yale ambayo yataonekana kuwa mabaya kwenu, yaacheni humuhumu.
Ninashukuru kwa kunifuatilia mwanzo mpaka mwisho wa simulizi hii fupi. Ninachopenda kusema ni kuwashukuru kwa kuniunga mkono kwenye kazi hii kubwa.
Kumbuka Kitabu changu cha Shambulio la Damu kipo mitaani na kinapatikana kwa shilingi 10,000 tu kwa namba zifuatazo.
Dar es Salaam........0718069269.
Posta.....................0713454152
Kona ya Riwaya, Kinondoni....0655228085.
Mwanza.................0762337673
Dodoma.................0719422001
Mbeya....................0625726640
Kagera/Bukoba.......0692936800
Zanzibar.................0674294643
SEHEMU YA 34
Kwa wale wasiojua ni kwamba hii ni system ambayo wenyewe waliiweka kuhamisha mawasiliano yako ya WhatsApp kwenye simu na kuwa kwenye kompyuta, yaani kile kitu ambacho ungeweza kukifanya kwenye simu yako, ulikuwa na uwezo wa kukifanya kwenye kompyuta yako kupitia hiyo WhatsApp Web.
“Bebi naomba tukaoge!” aliniambia Scaila huku akiniangalia.
“Kuna kazi nafanya mamiii, nenda tu halafu nitaoga baadaye,” nilimwambia kwa mahaba yote.
“Nataka kwenda kuoga na wewe mpenzi!” aliniambia kwa sauti ya kudeka.
“Nenda tu! Mimi nitakwenda mpenzi,” nilimwambia, sikuishia hapo, nikambusu mdomoni na kujifanya kuwa bize mno.
Akajifanya kama kuchukia hivi, akachukua simu yake, sijui alikuwa akifanya vitu gani lakini akili yangu iliniambia alikuwa akifuta mawasiliano fulani hivi.
Baada ya kumaliza, akavua nguo zake, akavaa taulo na kuelekea bafuni. Hiyo ndiyo ilikuwa nafasi yangu, niliposikia ameanza kujimwagia maji, nikachukua simu yake, haraka sana nikafungua WhatsApp na kisha kwenye kompyuta yangu kufungua WhatsApp Web na kuanza kuscan barcode nilizokuwa nimepewa.
Ni ndani ya sekunde tano, kitu kikajipa, ile WhatsApp yake ikaanza kuonekana kwenye kompyuta yangu, hivho ndicho nilichokuwa ninakitaka, nikafunga kwenye simu yake na kuirudisha ilipokuwa.
Nilihitaji kumfuatilia bila kufahamu lolote lile. Nilitulia chumbani kimya huku nikijifanya kuwa bize. Baada ya kumaliza, akatoka, akavaa nguo ya kulalia na kuja pembeni yangu kuona nilivyokuwa nikifanya mambo yangu.
Alikaa na kuangalia kompyuta kwa dakika kadhaa, akachoka na hivyo kuchukua simu yake, akageukia upande wa pili na kuanza kuchati na watu wake.
Haraka sana nikafungua WhatsApp yake kupitia kompyuta yangu na kuanza kufuatilia, yaani nilitaka kujua kama alikuwa akichati WhatsApp au sehemu nyingine. Ghafla nikaona meseji imetumwa kwenda kwa mtu aliyeseviwa kama Alfred.
Scaila: Baby!
Alfred: Leo nimeshikwa na wivu mkali sana.
Scaila: Kwa sababu gani?
Alfred: Yule jamaa aliyekuja, unayemuita mpenzi wako!
Scaila: Hahaha! Asikuogopeshe bwana! Lile buzi langu tu, ameleta shobo na mimi naruka naye!