Simulizi: Scaila Michael

Safi sana...

Jamaa nilimuona mjinga ila sasa nimeanza kumuelewa...

Hakuna kitu kibaya kama wenza kupekuana simu zao... ni hatari kuliko hata watu wasiojulikana...



Cc: mahondaw
 
Sehemu ya 56.

Janeth: Inabidi uwe makini sana.
Scaila: Niwe makini ama niache?
Janeth: Kuacha huwezi! Nakujua, cha msingi umakini uongezeke.

Scaila: Nikuulize kitu?
Janeth: Niulize.
Scaila: Hivi tuna malengo gani kwanza?
Janeth: Unamaanisha nini?
Scaila: Yaani kudanga kwetu huku, mwisho wa siku tunataka tuishi vipi hapo baadaye?

Janeth: Mh! Shoga na hayo maswali yako!
Scaila: Tusaidiane kujibiana.
Janeth: Labda kuolewa.
Scaila: Na mwanaume wa aina gani?
Janeth: Atakayenipenda, kunijali na kunisikiliza.

Scaila: Hivi unajua kama Nyemo anayafanya yote hayo kwangu?
Walikuwa wakichati sana lakini baada ya kuuliza swali hilo, kidogo ukimya ukatawala, ni kama Janeth alikuwa akijifikiria ni kitu gani alitakiwa kumjibu rafiki yake huyo kwani meseji nyingine iliyokuwa imeingia, iliingia baada ya dakika tano.

Janeth: Sasa shoga’angu, ndiyo unataka kusema uachane na klabu?
Scaila: Yaani najiuliza, huko klabu kutaisha lini? Umri unakwenda! Kuna kipindi tunatakiwa tuwe na nyumba zetu Jane!

Janeth: Shoga umeniamulia.
Scaila: Hapana! Ninahitaji kukwambia vitu vya muhimu. Namuona Nyemo ni mtu wa tofauti sana, nimewahi kuishi na wanaume watatu lakini huyu wa sasa ni wa tofauti kabisa.

Janeth: Kwani yupo vipi?
Scaila: Ni mpole, mcheshi, ananijali, ananisikiliza, ananipa muda, ninapokosea ananirekebisha, ni mtu wa haraka sana kuomba msamaha kila anaponikosea.
Janeth: Mh!
Scaila: Janeth! Nakwambia ukweli, ungempata mtu kama huyu, ungeachana na sisi.

Janeth: Kwa hiyo unamaanisha nini? Unataka kuachana na sisi?
Scaila: Nilizaliwa peke yangu, nitakufa peke yangu. Nikiolewa na Nyemo, siku akiniacha, hakuna rafiki ambaye atanionea huruma, inawezekana hata wewe ukanicheka na kuniambia nilikosea sana kumtesa kijana wa watu.
Janeth: Unaonekana kubadilika sana kwa maneno haya! Jamaa kakulisha sumu ya maneno ama?

Scaila: Hapana! Ndoa ni maisha! Tunapokosea kuchagua wanaume wa kutuoa, jua tutalia miaka yote mpaka uzeeni na siku tutakapochagua wanaume sahihi, jua tutaishi kwa raha mpaka uzeeni. Janeth! This is right man.
Janeth: Scaila.......
 
Sehemu ya 57.

Scaila: Ni muda wangu wa kubadilika. Nimetembea na wanaume wa kila aina, wafupi, warefu, Waarabu, Waswahili, wanene, wembamba, kote huko sijaona mabadiliko, wanaume wengine walikuwa na manyanyaso ya kila namna, nililia sana lakini cha ajabu, kwa Nyemo imekuwa tofauti.

Janeth: Scaila leo una nini?
Scaila: Nikwambie kitu?
Janeth: Niambie.

Scaila: Nataka niitengeneze nyumba yangu, nikiendekeza starehe, hazitoisha, kila siku zinakuja mpya. Naomba nitafute familia yangu. Ninakwambia ukweli!

Nilikuwa malaya, ila kwa sasa, hapana. Ninataka kuitengeneza nyumba yangu Sitotaka tena kwenda klabu wala kunywa pombe na kuchuna mabuzi.

Janeth: Hebu subiri nikupigie kwanza.
Scaila: Hapana! Nyemo amelala na sitaki kumsumbua. Ila naomba uniache, ukizungumza na mimi, naomba utambue kwamba nimekuwa Scaila mpya. Najua itakuwa vigumu kubadilika haraka, ila ninataka kubadilika kabisa, niwe mtu mwingine.

Janeth: Scaila, hivi unamaanisha ama?
Scaila: Utapata majibu ndani ya siku chache. Kwa heri.

Nikashusha pumzi ndefu, nikwambie ukweli tu meseji alizokuwa amewasiliana na rafiki yake huyo zilinifanya nilengwe na machozi na kuanza kutiririka mashavuni mwangu.

Nilisikia kitu kizito kikiugusa moyo wangu kupita kawaida. Sikutaka kubaki kwa Janeth tu, nikaenda kwa rafiki yake mwingine ambaye naye aliwasiliana naye.

Scaila: Mariam! Nina ujumbe mmoja tu.
Mariam: Hata salamu!
Scaila: Salamu si muhimu sana kama hiki ninachotaka kukwambia.
Mariam: Kipi? Kuhusu Hussein ama Godfrey?

Scaila: Nimebadilika. Ninataka kuolewa.
Mariam: Hahahah!
Scaila: Naomba usiniambie kuhusu klabu wala ishu za mabwana, ninataka kutengeneza nyumba yangu, niwe mke mwema, niolewe na kupata familia yangu.
Mariam: Hahaha! Hivi huyu anayeandika haya ni Scaila ama mwingine?

Scaila: Utapata majibu ya hiki ninachokwambia. Usiku mwema.
Nikaifunga kompyuta ile, nikashusha pumzi ndefu, sikuamini nilichokuwa nimekisoma, nikasimama, nikaufungua mlango na kuelekea jikoni.

Nilimkuta Scaila anaandaa chai kama kawaida yake, hakutaka kabisa Grace aniandalie, siku zote alitamani niwe naonja mapishi yake. Nikasimama mlango na kumwangalia, sikuamini kama alikuwa amemaanisha kubadilika.
 
Sehemu ya 58.

Akageuka na kuniangalia! Aliniona nikiwa tofauti, macho yangu yalikuwa na machozi kwa mbali japokuwa yale yaliyotiririka mashavuni niliyafuta, alishangaa, akanifuata na kusimama mbele yangu.

“Kuna nini? Una nini mpenzi?” aliniuliza huku akiniangalia. Nikamkumbatia.
“Ninakupenda sana! Naahidi kutokukuacha!” nilimwambia kwa sauti ndogo. Alishangaa.

“Kwa nini unalia?”
“Kwa sababu nakupenda!”
“Ndiyo ulie?”
“Ni mambo mengi sana! Ila Scaila, ninakupenda sana! Kama kuumia niliumia sana, nadhani huu ni muda wa kufurahi tena,” nilimwambia..

“Kuna nini lakini?” aliniuliza.
“Mtoto huzaliwa na upendo moyoni mwake, chuki huikuta duniani, ni sawa na mapenzi, kila mtu huzaliwa huku akiwa na mapenzi ya dhati kwa yule ambaye atatokea kumpenda,” nilimwambia.
“Ila?”

“Usaliti hukutana nao humuhumu. Inawezekana marafiki wakasababisha, pombe na vitu vingine,” nilimwambia.
“Unanificha tangu jana! Kuna kitu!” aliniambia.

“Niambie kitu kimoja!”
“Kipi?”
“Unaniahidi kubadilika?” nilimuuliza.
“Kabisa. Kwani umegundua nini?”
“Hutokwenda klabu tena?” nilimuuliza. Akashtuka.

“Kwani mi....”
“Scaila! Usiniambie kwamba huwa huendi klabu. Ninapoamua kusamehe, huwa ninasahau tena. Ninataka ubadilike kama ulivyosema kuwa utabadilika. Achana na akina Janeth! Wale si marafiki, watakupoteza, kuna siku wakipata mwanaume sahihi kama mimi, wataondoka, watakuacha ukiteseka,” nilimwambia.

“Nyemo....”
“Scaila! Jenga maisha yako, na familia yako! Umepata mtu anayekupenda sana, jenga maisha!” nilimwambia huku nikimwangalia.

“Najua!”
“Nikwambie jambo la mwisho?”
“Niambie.”
“Siku zote tamani kuoa ama kuolewa na mtu anayekupenda, siyo na unayempenda,” nilimwambia.

“Unamaanisha nini?”
“Unapompenda mtu, huna uhakika kama naye anakupenda. Ila mtu akikupenda, unakuwa na uhakika kwamba anakupenda. Huyo ndiye mtu wa kujenga naye maisha. Ndoa nyingi zinakuwa na misukosuko kwa sababu watu huoa ama kuolewa na watu wanaowapenda wao ila sio wanaopendwa nao,” nilimwambia.

“Nimekuelewa. Ila hata mimi nakupenda sana na ndiyo maana nimeamua kubadilika!”
“Najua! Nitakupenda maisha yangu yote.”

“Nitakupenda pia.”
“Mara yako ya mwisho kwenda kanisani lini?”
“Mh! Nadhani miaka kumi na tano iliyopita!”
 
Sehemu ya 59.

“Usijali! Tunatakiwa kuwa na hofu ya Mungu, watu wote ila hasa hasa wanawake. Mwanamke ndiye mtu wa kujenga misingi imara ya ndoa na mwanaume hufuata. Wewe ndiye mtu unayetakiwa kuniambia mimi ni kitu gani cha kufanya.

Inawezekana wakati mwingine ninachoka sana na kazi, unatakiwa kunikumbusha kusali, kumtumikia Mungu, ungekuwa Muislamu ningekwambia uwe mtu wa kwanza kuniamsha kwenda msikitini hata kabla ya adhana kuadhiniwa alfajiri,” nilimwambia na kuendelea: “Mwanamke asiyeijenga nyumba yake, huibomoa kwa mikono yake mwenyewe! Misingi imara ya nyumba hujengwa na mwanamke.

Wewe ndiye wa kuwafundisha watoto wetu njia ya Mungu kwa sababu utakuwa nao karibu kila siku kuliko mimi, mimi nitakuwa mkumbushaji tu, ila siku zote wewe ndiye utabaki kuwa mwalimu wetu, utakayeamua familia iende vipi,” nilimwambia.

Alikuwa kimya! Katika maisha yangu nilijifunza mambo mengi sana, moja kubwa ni kuzungumza na mwanamke kuhusu maisha. Wanawake hawapati muda wa kuyajua mambo mengi kwa kuwa wanaume nao hawana muda wa kuwaambia mambo mengi kuhusu maisha.

Mwanaume anapokutana na mpenzi wake, kitu anachokifikiria huwa ni ngono tu, hana hata muda wa kukaa na kumwambia mpenzi wake kwamba leo tuzungumze kuhusu maisha.

Mwanamke akiambiwa njoo nyumbani na mpenzi wake, kama yupo kwenye siku zake, atamwambia mwanaume ‘leo nipo period au siku ya hatari’ anachokijua ni kwamba akienda huko hakuna kingine zaidi ya ngono tu.

Tumewajenga wanawake wetu hivi, inawezekana ukawa na mwanamke ambaye anatamani sana kusikia mipango yako ya kimaisha lakini anapofika nyumbani, huna muda huo, haraka sana unavua nguo na kuanza kufanya mapenzi.
Hatuna mazoea ya kubadilishana mawazo, akili zetu hufikiria sana ngono kuliko mambo mengine.

Duniani hakuna mwanamke anayezaliwa na ubora, ukimuona mwanamke bora, jua kuna mwanaume bora ametumia muda wake kumtengeneza. Ukiona mwanamke sio bora basi jua wewe pia sio bora kwa sababu umeshindwa kumtengeneza.
 
Sehemu ya 60.

Scaila alikuwa na udhaifu mwingi, sasa niliona ni jukumu langu kuanza kumtengeneza na kuwa vile ninavyotaka awe.

Ni jambo kubwa, zito na gumu ambalo wanaume wengi hushindwa lakini kwa kipindi hicho niliamua kuifanya kazi hiyo kwa nguvu zote kwa sababu niliamini huyo mtu nitakwenda kuishi naye kwa miaka mingi inawezekana zaidi ya miaka niliyoishi na wazazi wangu, hivyo ni lazima niishi na mtu bora.

Nikwambie tu, Scaila alibadilika kabisa, hakuwa yule, hata nilipokuwa nikifuatilia mawasiliano yake, hakuwa akiwasiliana na marafiki zake, waliamua kuachana naye kwa kuwa aliwaonyeshea msimamo wa kutaka kubadilika.

Nadhani alimwambia na mama yake kuhusu maamuzi yake, alimwambia kuhusu kubadilika kwake. Niliendelea kuishi naye mpaka nilipokuja kumuoa, akawa mke wangu, mama wa watoto wangu, msaidizi wangu.

Na wiki ambayo tulitimiza miaka mitatu ya ndoa yetu huku tukiwa na mtoto wetu mmoja wa kiume aliyeitwa Jericho, tukapata taarifa za kufariki kwa Janeth, alifariki kwa Ugonjwa UKIMWI.
 
Sehemu ya 61.

Inawezekana huyu Scaila alikuwa akielekea kulekule ila nilimuokoa. Huyu Scaila sikukutana naye kanisani au sehemu ya maana sana, nilikutana naye njiani, sehemu ya hovyo, kwenye ajali mbaya lakini ndiyo hivyo nikaja kumuoa na kuwa mke mwema kwangu.

Kuna watu wanahisi kukutana na mtu kanisani ndiyo ndoa huwa bora! Hapana! Kuna watu wanakutana huko lakini ndoa yao kila siku huwa ni ugomvi kana kwamba hawajui chochote kuhusu Mungu.

Kitu cha kwanza kitakachoifanya ndoa kuwa bora, katika kipindi cha uhusiano wenu, unachotakiwa kufanya ni kumtengeneza mwenzako awe bora, mwanaume amtengeneze mwanamke na hivyohivyo mwanamke amtengeneze mwanaume.

Unapomuona amevaa nguo, msifie, mwambie jinsi unavyojivunia kuwa mke ama mchumba wake. Hakuna mtu asiyependa sifa, msifie mara kwa mara, sifia mapishi yake, sifia jitihada zake, mavazi yake, sifia kila kitu kwani usiposifia, huko nje akisifiwa kidogo tu, ndugu yangu hesabia maumivu.

Na cha kuongezea, kwenye uhusiano huo, hakikisha kuna unyenyekevu, utakapokosea, jutia kosa lako, omba msamaha wa dhati na si kujifanya wewe mwanaume hutakiwi kumuomba msamaha mke ama mchumba wako.

MWISHO
Natumaini wote mmejifunza mengi katika simulizi hii, kwa yale ambayo ni mafunzo kwenu, yachukueni lakini yale ambayo yataonekana kuwa mabaya kwenu, yaacheni humuhumu.

Ninashukuru kwa kunifuatilia mwanzo mpaka mwisho wa simulizi hii fupi. Ninachopenda kusema ni kuwashukuru kwa kuniunga mkono kwenye kazi hii kubwa.

Kumbuka Kitabu changu cha Shambulio la Damu kipo mitaani na kinapatikana kwa shilingi 10,000 tu kwa namba zifuatazo.

Dar es Salaam........0718069269.
Posta.....................0713454152
Kona ya Riwaya, Kinondoni....0655228085.
Mwanza.................0762337673
Dodoma.................0719422001
Mbeya....................0625726640
Kagera/Bukoba.......0692936800
Zanzibar.................0674294643
 
Sehemu ya 61.

Inawezekana huyu Scaila alikuwa akielekea kulekule ila nilimuokoa. Huyu Scaila sikukutana naye kanisani au sehemu ya maana sana, nilikutana naye njiani, sehemu ya hovyo, kwenye ajali mbaya lakini ndiyo hivyo nikaja kumuoa na kuwa mke mwema kwangu.

Kuna watu wanahisi kukutana na mtu kanisani ndiyo ndoa huwa bora! Hapana! Kuna watu wanakutana huko lakini ndoa yao kila siku huwa ni ugomvi kana kwamba hawajui chochote kuhusu Mungu.

Kitu cha kwanza kitakachoifanya ndoa kuwa bora, katika kipindi cha uhusiano wenu, unachotakiwa kufanya ni kumtengeneza mwenzako awe bora, mwanaume amtengeneze mwanamke na hivyohivyo mwanamke amtengeneze mwanaume.

Unapomuona amevaa nguo, msifie, mwambie jinsi unavyojivunia kuwa mke ama mchumba wake. Hakuna mtu asiyependa sifa, msifie mara kwa mara, sifia mapishi yake, sifia jitihada zake, mavazi yake, sifia kila kitu kwani usiposifia, huko nje akisifiwa kidogo tu, ndugu yangu hesabia maumivu.

Na cha kuongezea, kwenye uhusiano huo, hakikisha kuna unyenyekevu, utakapokosea, jutia kosa lako, omba msamaha wa dhati na si kujifanya wewe mwanaume hutakiwi kumuomba msamaha mke ama mchumba wako.

MWISHO
Natumaini wote mmejifunza mengi katika simulizi hii, kwa yale ambayo ni mafunzo kwenu, yachukueni lakini yale ambayo yataonekana kuwa mabaya kwenu, yaacheni humuhumu.

Ninashukuru kwa kunifuatilia mwanzo mpaka mwisho wa simulizi hii fupi. Ninachopenda kusema ni kuwashukuru kwa kuniunga mkono kwenye kazi hii kubwa.

Kumbuka Kitabu changu cha Shambulio la Damu kipo mitaani na kinapatikana kwa shilingi 10,000 tu kwa namba zifuatazo.

Dar es Salaam........0718069269.
Posta.....................0713454152
Kona ya Riwaya, Kinondoni....0655228085.
Mwanza.................0762337673
Dodoma.................0719422001
Mbeya....................0625726640
Kagera/Bukoba.......0692936800
Zanzibar.................0674294643


Safi sana...

Chapter Closed...


Cc: mahondaw
 
Hapa mwisho unawezajikuta unaua mtu
SEHEMU YA 34

Kwa wale wasiojua ni kwamba hii ni system ambayo wenyewe waliiweka kuhamisha mawasiliano yako ya WhatsApp kwenye simu na kuwa kwenye kompyuta, yaani kile kitu ambacho ungeweza kukifanya kwenye simu yako, ulikuwa na uwezo wa kukifanya kwenye kompyuta yako kupitia hiyo WhatsApp Web.

“Bebi naomba tukaoge!” aliniambia Scaila huku akiniangalia.
“Kuna kazi nafanya mamiii, nenda tu halafu nitaoga baadaye,” nilimwambia kwa mahaba yote.

“Nataka kwenda kuoga na wewe mpenzi!” aliniambia kwa sauti ya kudeka.
“Nenda tu! Mimi nitakwenda mpenzi,” nilimwambia, sikuishia hapo, nikambusu mdomoni na kujifanya kuwa bize mno.

Akajifanya kama kuchukia hivi, akachukua simu yake, sijui alikuwa akifanya vitu gani lakini akili yangu iliniambia alikuwa akifuta mawasiliano fulani hivi.

Baada ya kumaliza, akavua nguo zake, akavaa taulo na kuelekea bafuni. Hiyo ndiyo ilikuwa nafasi yangu, niliposikia ameanza kujimwagia maji, nikachukua simu yake, haraka sana nikafungua WhatsApp na kisha kwenye kompyuta yangu kufungua WhatsApp Web na kuanza kuscan barcode nilizokuwa nimepewa.

Ni ndani ya sekunde tano, kitu kikajipa, ile WhatsApp yake ikaanza kuonekana kwenye kompyuta yangu, hivho ndicho nilichokuwa ninakitaka, nikafunga kwenye simu yake na kuirudisha ilipokuwa.

Nilihitaji kumfuatilia bila kufahamu lolote lile. Nilitulia chumbani kimya huku nikijifanya kuwa bize. Baada ya kumaliza, akatoka, akavaa nguo ya kulalia na kuja pembeni yangu kuona nilivyokuwa nikifanya mambo yangu.

Alikaa na kuangalia kompyuta kwa dakika kadhaa, akachoka na hivyo kuchukua simu yake, akageukia upande wa pili na kuanza kuchati na watu wake.

Haraka sana nikafungua WhatsApp yake kupitia kompyuta yangu na kuanza kufuatilia, yaani nilitaka kujua kama alikuwa akichati WhatsApp au sehemu nyingine. Ghafla nikaona meseji imetumwa kwenda kwa mtu aliyeseviwa kama Alfred.

Scaila: Baby!
Alfred: Leo nimeshikwa na wivu mkali sana.

Scaila: Kwa sababu gani?
Alfred: Yule jamaa aliyekuja, unayemuita mpenzi wako!
Scaila: Hahaha! Asikuogopeshe bwana! Lile buzi langu tu, ameleta shobo na mimi naruka naye!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom