SEHEMU YA 14.
“Una picha zake?”
“Hapana! Lakini ni mzuri..yaani ni mzuri! Grace, duniani kuna wanawake wazuri sana. Yule Scaila, yaani ni mzuri balaa,” nilimwambia kwa msisitizo, yaani yote hiyo nilitaka aamini kwa asilimia mia moja nilichokuwa nikimwambia.
Grace alibaki akicheka tu. Huyu alikuwa mfanyakazi wangu, nililetewa na dada yangu kutoka mkoani Mwanza, alikuwa Msukuma mzuri, mwenye umbo matata sana ila kipindi alichokuwa amekuja jijini Dar es Salaam, hakuwa na muonekano mzuri.
Nilikubali awe dada wa kazi, kwanza kitu cha kwanza nilichokifanya ni kuanza kumbadilisha. Huyu Grace alitakiwa kuwa na muonekano mzuri, msafi kwa sababu pale nyumbani kwangu kulikuwa na marafiki zangu wengi waliokuwa wakifika kunitembelea.
Kipindi cha kwanza walimchukulia kawaida sana ila baada ya kumbadilisha, kila mtu aliyekuwa akifika nyumbani hapo alichanganyikiwa.
Alipendeza mno, wengi waliniambia niwaunganishe naye ila sikutaka kufanya hivyo kwa sababu nilijua ni kwa namna gani marafiki zangu walivyokuwa wahuni, hawakuwa waoaji, na wale waoaji hawakutaka kutulia kwenye ndoa zao kabisa.
“Hebu cheki wezele ile...dah! Nyemo unafaidi sana! Yaani huyu mtoto ukimuweka kwenye kumi na nane zako, usiku mzima wewe unaimba wimbo wa CCM mbele kwa mbele,” aliniambia rafiki yangu, aliitwa Juma Hiza.
“Acha ujinga wako! Dada yangu huyo,” nilimwambia Juma.
“Sasa inakuwaje?”
“Kuhusu nini?”
“Nimeshachanganyikiwa, yaani siambiwi wala sisikii hapa,” aliniambia.
“Tubadilishane basi. Namuomba Amina!” nilimwambia, huyo alikuwa dada yake.
“Hahah! We mjinga sana, nikupe Amina mimi!” aliniambia.
“Kwani kuna ubaya gani! Si mara moja moja unakuja kula kwa shemeji, ukiniona unanipiga mizinga,” nilimwambia kwa utani.
Juma alikuwa na dada yake aliyeitwa Amina, alimpenda mno, alimchunga sana na wanaume hasa sisi marafiki zake kwa kuwa tulikuwa tunajuana ni watu wa aina gani.
Hakutaka kusikia kitu chochote kuhusu Amina, alijitahidi kumlinda na sisi lakini siku ambayo nilikutana naye maeneo ya Mwenge ndipo nilipochukua namba yake na kuisave kama Fundi Bomba.