Simulizi: Scaila Michael

SEHEMU YA 31

Maisha baina yangu na Scaila yalikuwa matamu sana, tulipendana kwa dhati na muda mwingi tulikuwa pamoja.

Sikuyaona madhaifu yake kwa wakati huo, kila nilipokuwa nikirudi nyumbani nilipokelewa kwa mbwembwe nyingi na mahaba tele.

Kiukweli hapo ndipo niligundua unapokuwa kwenye mapenzi mazito una nguvu ya kufanya kitu chochote kile.

Scaila aliuteka moyo wangu, alilifahamu hilo na alihakikisha kila siku ninakuwa mtu wa furaha katika maisha yangu yote.

Kwa kweli sikutaka kumfuatilia kabisa hasa kwenye simu yake, nilihitaji awe huru, afanye lolote analolitaka lakini aniheshimu na kujua kwamba mimi ni mume wake mtarajiwa.

Mambo yalikuwa mazuri mpaka pale ambapo niliona anakuwa bize sana na simu. Kama ni kuchati, basi kwa Scaila ilikuwa si mchezo, kila wakati aliishikilia simu yake na kuandika meseji kwenda kwa watu wengine.

Kwa sababu nilimpenda, sikutaka kabisa kumfuatilia, sikutaka kuona akikasirika kwani yeye ndiye alikuwa furaha yangu katika maisha yangu kipindi hicho.

Nilianza kuingiwa na shaka kuhusu simu yake, ila wakati mwingine nilijiambia sikutakiwa kuwa hivyo kwa sababu nilipenda, na mtu ukimpenda, jambo la kwanza kabisa unatakiwa kumwamini.

Hivyo ilikuwa ni hivyo, hata alipokuwa akiiacha simu yake hapo, iwe inaita au ujumbe wa maneno kuingia wala sikujishughulisha nao hata kidogo.

Nakumbuka kuna siku nilirudi nyumbani majira ya saa kumi, siku hiyo niliwahi kwa sababu nilimaliza biashara zangu mapema sana hasa kwenye kukusanya mahesabu na hivyo nilihitaji muda mwingi wa kupumzika.

Nilipofika nyumbani, nilimkuta Grace lakini Scaila hakuwepo nyumbani. Sikutaka kuwa na wasiwasi naye kwa sababu nilimwamini sana.

Nilikaa sebuleni huku nikiendelea kufanya mambo yangu kwenye kompyuta yangu ya mapajani.

Muda ulikwenda lakini hakurudi nyumbani, nilianza kuingiwa na wasiwasi, ikanibidi nifanye maamuzi ya kumpigia simu na kumuuliza alipokuwa. Kabla ya kufanya hivyo, kitu cha kwanza nikaona lingekuwa jambo jema nijue mahali alipokuwa, nikamuita Grace na kumuuliza.

“Wifi yako yupo wapi?” nilimuuliza.
“Alikwenda kwa mama!” alinijibu.
31
 
Sehemu ya 61.

Inawezekana huyu Scaila alikuwa akielekea kulekule ila nilimuokoa. Huyu Scaila sikukutana naye kanisani au sehemu ya maana sana, nilikutana naye njiani, sehemu ya hovyo, kwenye ajali mbaya lakini ndiyo hivyo nikaja kumuoa na kuwa mke mwema kwangu.

Kuna watu wanahisi kukutana na mtu kanisani ndiyo ndoa huwa bora! Hapana! Kuna watu wanakutana huko lakini ndoa yao kila siku huwa ni ugomvi kana kwamba hawajui chochote kuhusu Mungu.

Kitu cha kwanza kitakachoifanya ndoa kuwa bora, katika kipindi cha uhusiano wenu, unachotakiwa kufanya ni kumtengeneza mwenzako awe bora, mwanaume amtengeneze mwanamke na hivyohivyo mwanamke amtengeneze mwanaume.

Unapomuona amevaa nguo, msifie, mwambie jinsi unavyojivunia kuwa mke ama mchumba wake. Hakuna mtu asiyependa sifa, msifie mara kwa mara, sifia mapishi yake, sifia jitihada zake, mavazi yake, sifia kila kitu kwani usiposifia, huko nje akisifiwa kidogo tu, ndugu yangu hesabia maumivu.

Na cha kuongezea, kwenye uhusiano huo, hakikisha kuna unyenyekevu, utakapokosea, jutia kosa lako, omba msamaha wa dhati na si kujifanya wewe mwanaume hutakiwi kumuomba msamaha mke ama mchumba wako.

MWISHO
Natumaini wote mmejifunza mengi katika simulizi hii, kwa yale ambayo ni mafunzo kwenu, yachukueni lakini yale ambayo yataonekana kuwa mabaya kwenu, yaacheni humuhumu.

Ninashukuru kwa kunifuatilia mwanzo mpaka mwisho wa simulizi hii fupi. Ninachopenda kusema ni kuwashukuru kwa kuniunga mkono kwenye kazi hii kubwa.

Kumbuka Kitabu changu cha Shambulio la Damu kipo mitaani na kinapatikana kwa shilingi 10,000 tu kwa namba zifuatazo.

Dar es Salaam........0718069269.
Posta.....................0713454152
Kona ya Riwaya, Kinondoni....0655228085.
Mwanza.................0762337673
Dodoma.................0719422001
Mbeya....................0625726640
Kagera/Bukoba.......0692936800
Zanzibar.................0674294643
Duuh..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom