Simulizi: Sasha Mlinzi wa Nafsi - 1

Msimu wa kwanza na wa pili wa simulizi hii, unapatika kwa Tsh elfu 1 tu piga simu au njoo WhatsApp namba 0756862047 Saul David
1899407713.jpg
322670602.jpg
 
SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya..........13
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
"Hapana turudi" Alisema Tesha na mara hiyo dereva akageuza gari na kuanza kurudi.
Hakuna aliyejua kuhusu majanga mazito yanayokaribia kumkuta David ambaye yuko njiani kuuliwa na wale wanawake wa ajabu kutoka ISRA Zucc na Femi.
SASA ENDELEA...
David alionekana akitembea mara baada ya kutoka nje ya mgahawa akawa analielekea geti dogo linalounganisha uzio wa kuta mbili zinazouzunguuka mgahawa huo.

Sura ya David ilionekana kuwa na tabasamu angavu, bado alikuwa akikumbuka vile vitu alivyoviona ndani ya pochi ya mwanamitindo maarufu Tesha, akaishia kutabasamu mwenyewe.
Akiwa amebakiza hatua kadhaa kulifikia geti mara ghafula alishtushwa na mlio mkali wa vyuma vikigongana nyuma yake karibu kabisa na shingo yake.
David aligeuka haraka kutazama ndipo hapo anapokutana na tukio la ajabu ambalo hakuwa kulishuhudia tangu kuzaliwa kwake.
Wale wanawake wa ajabu waliokuwa wanamfuatilia tangu awali sasa walikuwa nyuma yake yaani Zucc na Femi. Mikononi mwao kila mmoja alikuwa ameshikilia visu vidogo viwili.
Kisu kimoja cha Zucc kilikuwa karibu kabisa na shingo ya David. Ilionekana wazi Zucc alikusudia kumuua David lakini alizuiliwa na kisu cha Femi ambaye alifika haraka kabla Zucc hajakizamisha kisu chake katika shingo ya David.
Wakiwa katika hali hiyo, Zucc na Femi walitazama kwa macho makali huku kila mmoja akionekana kutofurahishwa kabisa na uamuzi wa mwenzake.
David alibaki amesimama huku akiwa ametoa macho kwa mshangao mkubwa. Mwili wake wote ulikuwa ukitetemeka kwa hofu kubwa aliyokuwa nayo. Haja ndogo ilikuwa karibu kumtoka.

"Unaelewa unachokifanya Femi..?" Zucc aliongea kwa jazba sana.
"Siwezi kukuruhusu uvunje sheria yetu Zucc, ninyi ndio mnasababisha majanga hayaishi kutuandama katika mji wa ISRA kwa sababu ya kuzidharau sheria muhimu kama hizi" Femi aliongea huku naye akiwa ameikunja sura yake.
"Femi potea kwenye macho yangu mara moja kabla sijakuumiza..."
"Siwezi kukuacha umuue huyu mwanadamu Zucc, labda uniue mimi kwanza.."
Femi alijibu kisha akageuka na kumtazama David ambaye tayari alishadondoka chini kutokana na hofu kubwa aliyokuwa nayo.

"David, inuka kimbiaa...." Alisema Femi kauli iliyopenya vizuri kwenye masikio ya David.
David akajizoazoa pale chini kujaribu kusimama lakini akajikuta anaanguka tena kwa mara nyingine, hofu ilikuwa imemjaa kiasi cha kumfanya akose nguvu kabisa.
Kufumba na kufumbua ugomvi mkubwa ulianza kati ya Femi na Zucc. Wanawake hawa wa ajabu walianza kupigana kwa kasi sana huku kila mmoja akionekana yupo vizuri katika matumizi ya visu vile vidogo.
Kasi yao ilikuwa ya ajabu sana, kunawakati waliruka juu umbali wa mita kadhaa kutoka ardhini wakakutana hewani na kuendelea kupigana huku wakishuka chini kwa kasi na kutua tena ardhini.
Wakati hayo yakiendelea yule dada muhudumu wa mgahawa alikuwa akishuhudia kila kitu, kupitia kioo cha dirisha la mgahawa huo. Ajabu ni kwamba yeye alikuwa akimuona David pekee lakini hakuwa akiwaona Zucc na Femi. Aliona wakati David akianguka na kujaribu kusimama huku akionekana mwenye hofu. Yule dada muhudumu aliamua kumpotezea akiamini kuna namna David alikuwa na upungufu wa akili kwani hata alipokuwa mle mgahawani alikuwa akionyesha tabia za ajabu ajabu.
Lakini kadri muda ulivyokwenda yule dada muhudumu akaanza kuhisi kitu cha tofauti wakati anaendelea kumtazamaza David.

"Au unamajini huyu kaka..." Alisema yule dada muhudumu huku akiitazama ile noti ya dollar aliyopewa na David akaogopa na kuiweka pembeni ya meza huku akiendelea kutazama nje.
Hadi dakika tatu zinakwisha katika purukushani nzito ya Femi na Zucc hakuna aliyefanikiwa kumgusa mwenzake zaidi ya kuchaniana yale magauni yao marefu. Vipande vya nguo vilivyodondoka chini vilitoweka kwa namna ya ajabu na kupotea.

Hatimae David alifanikiwa kusimama akakimbia kulielekea lile geti dogo lakini kabla hajafika kufumba na kufumbua Zucc alikuwa amesimama mbele yake huku akihema kwa nguvu.

Kwa mara nyingine tena Zucc aliinua kisu chake tayari kumchoma David ambaye hakuwa na namna yoyote ya kujitetea mbele ya mwanamke huyo wa ajabu.
Femi aliyekuwa ameanguka chini mara baada ya kuzidiwa nguvu na Zucc aliinuka tena na kuiona hatari iliyokuwa karibu kumkuta David.
Kwa ustadi wa hali ya juu Femi alivirusha visu vyake vyote viwili kwa pamoja kumuelekea Zucc huku vikimpita David pasipo kumgusa.
Zucc aliyekuwa tayari kumchoma David alijikuta anasitisha zoezi hilo akainama haraka kuvikwepa vile visu viwili vilivyorushwa na Femi. Alipokuja kuinuka tayari Femi alishafika na kusimama mbele ya David kumlinda.
Zucc aliinua mkono wake wa kushoto wenye kisu akaurusha kwa nguvu kumuelekea Femi ambaye alikizuia kisu kile kwa mkono wake kikamtoboa na kumsababishia jeraha kubwa.
Damu yenye rangi ya kijani ikawa inamtoka mkononi lakini bado aliendelea kusimama kidete, kwa mara nyingine akamzoa Zucc na kuanguka naye chini. Purukushani ya aina yake ikaendelea kwa kasi ile ile kama mwanzo.

David akapata wasaa mwingine wa kukimbia kuyatetea maisha yake akafanikiwa kulifikia geti, lakini ile anakanyaga tu getini mara alisukumwa kwa nguvu na watu waliokuwa wanaingia kupitia geti hilo dogo.
David alirushwa kama karatasi iliyopulizwa na upepo, akaanguka chini na kupigiza kichwa chake, aliumia vibaya mno.
Akiwa na hali ya mawenge mawenge pale chini aliinua uso wake kutazama akaona wanaume wanne wakiwa na rungu mkono wa kulia na mkono wa kushoto kila mmoja alishikilia ngao iliyokuwa na maandishi yaliyosomeka M.A.G.N.U.S
Kichwani walivaa vitu kama helmet zilizokuwa na vioo vyenye rangi nyekundu.
David alimuona mmoja kati ya wanaume hao akiweka ardhini kitu kama spika ya redio, akakiwasha. Mara sauti kama mlio wa gari la wagonjwa (Ambulance) ulianza kusikika.
Wakati hayo yakiendelea yule dada muhudumu wa mgahawa alikuwa akishuhudia. Alishtushwa sana na namna watu hao walivyoingia na kumsukuma David. Kwa namna walivyoonekana akaamini kabisa hawa ni majambazi. Yule dada akawa anahangaika kuitafuta simu yake ili awapigie polisi.
Mwili wake ulikuwa ukitetemeka kwa hofu, mara aliona tukio lingine la ajabu tukio lililomfanya yule dada ashindwe kistahimiri, akaanguka chini kama mzigo na kupoteza fahamu.
Wakati mlio ule wa king'ora ukisikika kutoka kwenye kile kifaa, Zucc na Femi walishtushwa na kuacha kupigana walipogeuka kutazama tayari walikuwa wamechelewa. Ule mlio ulikuwa ni kero kubwa kwao, mlio ambao uliwafanya Femi na Zucc kuanza kukosa nguvu wakaanza kuyumba yumba huku wakijitahidi kuziba masikio yao, bado haikusaidia. Yule jamaa mwenye kile kifaa akawa anaongeza sauti zaidi huku wale wengine watatu wakiwasogelea Zucc na Femi taratibu na kwa tahadhali kubwa ngao zao wakiwa wameziweka mbele.

Mwisho Zucc na Femi walijikuta wanakosa nguvu kabisa wakaanguka chini wote wawili. Mara tu baada ya kuanguka sasa wakawa wanaonekana kwa macho ya kibinadamu na hii ndio sababu iliyomfanya yule dada mhudumu wa mgahawa azimie mara baada ya kuona watu wa ajabu wametokea kusikojulikana.
David alishuhudia yote haya akiwa pale chini ardhini, hakujua wanaume hawa wanne ni watu gani, wametoka wapi, kazi yao ni ipi, ni binadamu au nao ni viumbe wa ajabu kama walivyo Zucc na Femi.
Wakati akiwaza hayo mara ghafula anamuona mwanadada mrembo sana Tesha akiingia akupitia lile geti dogo.
Dada huyu ambaye ni super star' mwanamitindo maarufu nchini alikuwa amerudi kwa mara nyingine kuifuata pochi yake aliyoidondosha. Laiti kama angejua asingethubutu kukanyaga tena mgahawani hapo.


Upande wa pili- ISRA
Msitu wa Bi Noha ulikuwa kwenye majanga makubwa. Kimbunga kilikuwa ni kikali mno huku tetemeko la ardhi nalo likizidi kushika kasi. Miti ilikuwa iking'orewa na kurushwa juu huku mingine ikititia na kuzama ardhi. Msitu wa Bi Noha ukawa unatoweka kwa namna ya ajabu mno. Handan, Dumayo na watu wao walionekana wamesimama umbali wa hatua kadhaa kutoka ulipo msitu huo wakawa wanashuhudia kwa macho mambo yanayoendelea.

"Maskini Sasha! Nini kimetokea huko...? Ooh! Jamani naogopa mimi... Tafadhali toka ukiwa salama we binti" Aliwaza Handan huku akionekana kuwa na wasiwasi mwingi.

Katika hali wasiyotegemea, mara wanamuona Sasha anachomoza kutoka katika ya kimbunga kile cha ajabu. Alikuwa juu ya farasi wake anaekimbia kwa kasi sana. Nyuma yake hali ilikuwa ni tete ardhi ilikuwa ikititia huku kimbunga nacho kikimfuata kwa kasi. Sasha alimkimbiza farasi wake kwa kasi sana, laiti kama ingekua ni gari tungesema yuko spidi ya 180.
Hali ilitisha sana kulikuwa na kila dalili kuwa Sasha hataweza kutoka akiwa salama badala yake atamezwa pamoja na msitu huo.
Je nini kitafuata?
Sasha atasalimika?
Vipi kuhusu David na Tesha?
Watu hawa wenye ngao zenye maandishi yanayosomeka M.A.G.N.U.S ni akina nani hasa?

0756862047

ITAENDELEA....
 
SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya..........14
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
Hali ilitisha sana kulikuwa na kila dalili kuwa Sasha hataweza kutoka akiwa salama badala yake atamezwa pamoja na msitu huo.

SASA ENDELEA...

Sasha alijitahidi kumkimbiza farasi kwa nguvu zake zote lakini bado hali ilikuwa si shwari. Kila farasi alipopiga hatua na kuacha ardhi basi nyuma yake ardhi hio ilititia kwenda chini.
Handan mlinzi mkuu wa Sasha alipiga hesabu za haraka haraka ni jinsi gani ya kumsaidia Sasha, haraka akaruka na kumdandia farasi wake kisha akaanzaa kumuendesha kuelekea kule anakotokea Sasha.

Ulikuwa ni uamzi wa kikakamavu uliomuacha kinywa wazi Dumayo pamoja na watu wake, hakuna aliyetegema kama Handan angekubali kujitosa kuelekea kwenye hatari ile.

Sasa ikawa wakutane katikati, Handan anakuja kwa kasi na farasi wake huku upande wa pili Sasha naye akija kwa kasi akilikimbia balaa lile nyuma yake.
Kwa bahati mbaya farasi wa Handan akasimama ghafula. Handan akajitahidi kuvuta kamba ili farasi asonge mbele lakini wapi farasi akagoma katakata huku akiwa anarudi nyuma kupingana na Handan.

Wakati huo Sasha alikuwa amebakiza kama hatua ishirini hivi kumfikia Handan hatimae kasi ya kimbunga na ule mtitio wa ardhi vikamzidi farasi wake kasi.
Sasha na farasi wake wakajikuta wanamezwa na kimbunga kile huku wakienda chini kuelekea kwenye shimo kubwa lililotengenezwa na ardhi iliyokuwa ikititia, tayari msitu wote ulikuwa umezama kwenye shimo.

"Sashaaaaaaaaaa.......!!" Handan aliita na kuweka mikono yake kichwani akiwa juu ya farasi. Lilikuwa ni tukio la kutisha na kuumiza mno.

Tofauti na ilivyokuwa kwa wengine, Dumayo mjomba wake Sasha yeye akawa anatabasamu.

Lakini bado Handan hakutaka kukubali kirahisi namna ile kumpoteza binti wa Mkuu wa ISRA Gu Gamilo. Katika hali ambayo hakuna aliyetegemea, Handan alichukua kamba moja ndefu mno iliyokuwa kwenye shingo ya farasi wake, haraka akajifunga kiunoni kisha upande mwingine wa kamba ile akamfunga farasi wake mguuni kisha akampiga na kumuacha aende, yule farasi akawa anakimbia kurudi alikotoka wakati Handan naye akawa anakimbia kuelekea kwenye shimo lile kubwa.
Bila kusita Handan alifika na kuruka akajitosa moja kwa moja na kuanza kushuka chini kwa kasi huku ile kamba ikiwa kiunoni kwake.

Kitendo hicho kiliwaacha vinywa wazi Dumayo na watu wake. Hatimae yule farasi wa Handan akiwa amefungwa kamba mguuni alifika pale walipo. Lakini bado kamba iliendelea kufunguka kwa kasi kuelekea shimoni kule aliporukia Handan.
Haraka mwanamke mmoja kati ya wale wawili (walinzi wa Sasha) alipanda juu ya farasi wa Handan mwenye kamba mguuni akaanza kukimbia naye kusonga mbele zaidi. Mara kamba ikakaza ikiwa ni ishara kuwa sasa imefika kikomo kati ya Handan shimoni na farasi juu ya ardhi.
Kilichotakiwa sasa ni farasi kuanza kuvuta kamba ile ili kumtoka Handan.

Yule mwanamke wa pili naye alisogeza farasi wake wakaunganisha ile kamba kwenye miguu ya farasi wote wawili kisha wakaanza kuwapeleka mbele huku ile kamba ikizidi kusogezwa na kumvuta Handan.
Mchezo wote huo ulikuwa ukishuhudiwa na Dumayo pamoja na watu wake.
Dumayo aligeuka na kumtazama mlinzi wake mkuu aliyekuwa mkono wa kulia.

"Unajua ni kwa nini siku zote shemeji Gu Gamilo anatuzidi nguvu!?" Aliuliza Dumayo, yule mlinzi akatikisa kichwa akiashiria hajui.

"Angalia wanachokifanya hawa wanawake, hivi ndivyo walivyo watu wake wote wanaomzunguuka Gu Gamilo. Wako tayari kufa kwa ajili yake. Nataka na ninyi muwe hivyo, mpambane kufa na kupona la sivyo hatuwezi kumdhibiti Gu Gamilo" Alifoka Dumayo mjomba wa Sasha, huku zoezi la kumchomoa Handan likizidi kushika kasi .


Upande wa pili...
Turudi nyuma wakati Tesha akiwa njiani kurudi alikotoka mara baada ya kubaini kuwa aliidondosha pochi yake kule mgahawani.
Njiani Tesha alijikuta akimuwaza sana David. Ni kwa muda mfupi sana alikuwa amekaa na mwanaume huyo lakini alijikuta anamzoea ghafula na taratibu David akaanza kuitawala akili yake.

Alijikuta anatamani kuongozana naye wakati wote. Ali-miss uwepo wake, ongea yake vituko vyake na hata tabasamu lake.
Kila alipoyafumba macho yake aliiona taswira ya David ikiwa imeutawala ufahamu wake.
Tesha alikumbuka kwa mara ya kwanza alipokutana na David

,,,,,,, Ilikuwa ni siku ya mwisho ya juma(weekend) aliingia uwanja wa mpira kuangalia mechi ya mpira wa miguu wa wanawake kati ya simba queen na yanga princess . Alifika uwanjani hapo kama mmoja kati ya wahamasishaji wa kampeni ya kitaifa ya Mwanamke jasiri, lakini pia alikuwa katika harakati za kutangaza mtindo mpya kutoka katika kampuni yake ya mitindo maarufu kama Tesha Fashion. Siku hiyo David naye aliingia kama mfanya biashara ndogo ndogo akiuza vinywaji baridi.

Alipopita karibu na Tesha waliangaliana huku Tesha akionekana kuvutiwa na muonekano wa David. Na hapo ndipo alipopata wazo la kumtumia David kwa ajili ya kumrusha roho mpenzi wake Felix aliyekuwa amemtelekeza na kwenda zake Marekani.
Wazo hilo lilipita kwenye ufahamu wa Tesha akaona linafaa. Alimtegeshea David hadi alipopita mara nyingine akamwita na kununua maji. Kisha kwa siri sana wakati Tesha akilipa pesa aliunganisha na kadi ya mawasiliano.

" Kuna namba za simu hapo utanicheki, nina shida na wewe" Alisema Tesha huku akiwa makini asije akanaswa na kamera.
David aliduwaa kidogo akiwa hajategemea kabisa kitu kama hicho kutoka kwa mwanadada huyo maarufu.

Usiku wa siku hiyo David akiwa na shauku kubwa ya kujua ni jambo gani hasa lilimfanya mlimbwende Tesha akampatia mawasiliano ya simu, alipiga simu mara kadhaa na baadae ilipokelewa akajitambulisha na mwisho wakaweka miadi ya kukutana kesho yake asubuhi .
Asubuhi ya siku iliyofuata David na Tesha walikutana na ndipo Tesha alipoweka wazi nia yake ya kutaka kuigiza uchumba na mwanaume huyo na kuahidi kumlipa pesa nyingi.
Ilikuwa ni ngumu sana kwa David kumuamini Tesha kwani hakuona sababu ya msingi kwa Tesha kufanya hivyo lakini Tesha alimvutia kwa kumpa kiasi kikubwa cha pesa . David alizipokea pesa hizo bila hiyana huku wakikubaliana kukutana kwa wakati mwingine kwa ajili ya maelezo zaidi
Lakini tangu siku hiyo David akawa ni mtu wa kumzunguusha Tesha akiogopa pengine atajiingiza kwenye matatizo makubwa kama atakubali kufanya kama anavyotaka super star' huyo.

Mwisho David akajikuta anaanza kuandamwa na vijana walioagizwa na Tesha kumfuatilia kijana huyo kwani tayari alishakula pesa zake.


Kumbukumbu hizi za Tesha zilikatishwa na breki kali ya gari.
"Tumefika Madam" Alisema Dereva.
Tesha hakujibu kitu akafungua mlango wa gari na kushuka. Pembeni aliona gari nyingine aina ya Noah nyeusi iliyokuwa imesimama pembeni ya barabara huku milango yote ikiwa imefunguliwa na kuachwa wazi.
Tesha alipiga jicho kutazama ndani hakukuwa na mtu. Akaendelea na safari yake huku akiwaza pengine anaweza asimkute David mle mgahawani.

"Kama hayupo basi atakuwa hospitali kwa mama yake" Aliwaza Tesha.
Wakati akikaribia geti dogo la kuingilia ndani ya mgahawa huo alisikia sauti kali ya king'ora mfano wa gari la ambulance, sauti hiyo ilikuwa ikitoka ndani mahali anapokwenda.
Tesha hakujali sana akaamini pembeni kuna shughuli ilikuwa ikiendelea mle ndani.

Mwisho alifika getini tayari kuingia ndani, hapo ndipo Tesha alipojikuta anapatwa na mshtuko wa ajabu mara baada ya kushuhudia mambo yaliyokuwa yakiendelea mle ndani.
Aliona wanaume wanne wakiwa na helmet zenye vioo vyekundu, mkononi wakiwa na ngao na marungu makubwa.
Alipotazama pembeni Tesha akagonganisha macho yake na macho ya David aliyekuwa amelala chini ardhini akiwa hoi taabani.
Tesha alibaki katika hali ya mshangao mkubwa asijue cha kufanya, mwili wake ulikuwa umepigwa na ganzi ya ghafula hakuweza kurudi nyuma wala kusonga mbele, bado wale watu wenye helmet walikuwa hawajamuona.
Mara ghafula pasipo kutegemea Tesha alivutwa nje na mtu mmoja ambaye hakumuona sura yake, mtu huyo alimvuta kwa nguvu na kumbana pembeni ya ukuta huku akiwa ameuziba mdomo wa Tesha kwa kiganja chake cha mkono.

"Shiiiiiiiiiiiiii...." Alisema mtu huyo ikiwa ni ishara kwa Tesha kwamba anyamaze kimya.

Ni shillingi elf 1 tu kusoma simulizi hii 0756862047.

Je ni nani huyo?
Katoka wapi?
Kwanini yuko hapa?
Vipi kuhusu Handan na Sasha?

ITAENDELEA...
 
SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya..........15
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
"Shiiiiiiiiiiiiii...." Alisema mtu huyo ikiwa ni ishara kwa Tesha kwamba anyamaze kimya.

SASA ENDELEA...
"Kaka...!!" Tesha aliita kwa mshangao mara baada ya kuutoa mkono wa mtu huyo mdomoni kwake na kumtazama.
"Tuondoke hapa sasa hivi" Alisema yule mtu, alikuwa ni Godfrey kaka yake Tesha
"Umefikaje hapa?" Tesha aliuliza
"Huu sio wakati wake tuondoke kwanza hapa" Godfrey alisisitiza huku akiushika mkono wa Tesha akaanza kumvuta kuelekea kwenye gari lake, wakafika na kuingia ndani. Wakati huo ile sauti ya king'ora kutoka ndani ya mgahawa iliacha kusikika kukawa kimya.
"Vipi jamani kwema?" Aliuliza Dereva wa Tesha mara baada ya kuona mtu na kaka yake wameingia mkukumkuku ndani ya gari.
"Kaka God nini kinaendelea mbona sielewi, wale watu mle ndani ni akina nani?" Tesha naye akaongeza swali lingine huku akimtazama kaka yake kwa macho ya kuuliza. Ni kweli Tesha hakuwa akielewa chochote hadi dakika hiyo. Mambo aliyoyaona mle mgahawani na baadae kaka yake Godfrey anatokea ghafula kumtoa yalizidi kumshangaza.

"Endesha gari bro, tuondoke hapa haraka"Alisema Godfrey, Dereva akatii na kuwasha gari tayari kuondoka.
"Hebu subiri kwanza, usiondoke" Mara Godfrey alimzuia tena dereva huku akiwa ametoa macho kutazama kwenye 'site mirror'
"Pandisha vioo vya gari haraka" Alisema Godfrey, dereva akafanya kama anavyoagizwa.
Godfrey, Tesha na dereva wake waligeuka kutazama kule mgahawani wakawaona wale wanaume waliovaa helmet wanatoka getini mmoja baada ya mwingine huku wakiwa wamewabeba wale wanawake wa ajabu yaani Zucc na Femi ambao walikuwa wamepoteza fahamu wakati huo.
Mwanaume wa mwisho kutoka naye alikuwa amembeba kijana David begani kwake. David naye hakuwa akijilewa alikuwa amepoteza fahamu vilevile.

"David...!" Tesha aliita kwa sauti ya chini akajaribu kufungua mlango wa gari ili atoke lakini Godfrey akamzuia.
"Unafanya nini Tesha hebu jitulize kwanza!"
"Ni David wamemteka David.."
"Sawa, lakini ni hatari kama utatoka. Unataka na wewe uingie kwenye matatizo au?"
"Basi tupige simu Polisi haraka" Alisema Tesha kisha akachukua mkoba wake akatoa simu na kubinya namba 111.

"Acha usipige..." Alisema Godfrey
"Kwa nini kaka, mbona sikuelewi lakini..."
Alisima Tesha, Godfrey hakujibu kitu, akachukua simu yake akawa anawapiga picha wale wanaume wanne ambao waliingia kwenye gari wakiwa wamewabeba watu watatu yaani Femi, Zucc na David. Wakawasha gari lao na kuondoka kwa kasi eneo hilo.

Godfrey aliacha zoezi lake la kupiga picha, akavuta pumzi ndefu na kuitoa taratibu, alionekana mtu mwenye mawazo na wasiwasi mwingi. Akageuka na kumtazama mdogo wake Tesha.

"Nenda nyumbani Tesha nitakuja then tutaongea vizuri.."
"No tuonge hapa hapa, watu wametekwa mbele ya macho yetu alafu wewe kirahisi tu unanizuia nisipige simu polisi kwa nini ani! Istoshe aliyetekwa ni David mwanaume wangu"
"Mwanaume wako how!?" Aliuliza Godfrey huku akimtazama Tesha usoni, Tesha akatazama pembeni kwa aibu ni kama neno hilo lilimtoka kwa bahati mbaya.

"Yes he's my Man, kwani sikukwambia nina kazi naye? alafu kaka Godfrey hebu kuwa serious basi niambie ni nini kinaendelea..."
"Tesha nenda nyumbani kwanza kwa sasa sina muda wa kukueleza ila nakuahidi baada ya saa moja nitakuwa home tutaongea vizuri na kuhusu usalama wa huyo mwanaume wako niachie mimi" Alieleza Godfrey kisha akapokea simu yake iliyokuwa ikiita.
Tesha alipiga jicho la kuibia kutaza jina la mpigaji akalisoma
'Brandina-usalama'

"Hallo..." Godfrey alianzisha mazungumzo.
"Ndio nimefika hapa mbona sikuoni" Ilisikika sauti ya kike simuni.
"Nipo ndani ya hii gari mbele yako, nimeshakuona nakuja" Alijibu Godfrey kisha akakata simu. Nyuma yao aliliona gari dogo aina ya Toyota IST likifunga breki.
"Tesha nikukute nyumbani, just one hour okay" Alisema Godfrey. Kishingo upande Tesha akatikisa kichwa kukubali. Godfrey alishuka garini akapiga hatua na kuingia kwenye ile Toyota, wakati huo dereva wa Tesha naye aliwasha gari wakaondoka eneo hilo.

"Pole" Brandina mwanamke mmoja mweusi na mrembo aliyekuwa ndani ya gari alianzisha mazungumzo mara tu baada ya Godfrey kuingia na kuketi pembeni yake.
"Asante lakini sijafanikiwa kuwafuatilia"alijibu Godfrey
"Kwa nini?" Aliuliza Brandina huku akivua miwani yake
"Mdogo wangu alikuwa hapa, ikabidi nimtoe kwanza, ndiye aliyenichelewesha"
"Mdogo wako yupi Tesha?"
"Ndiyo"
"Tesha huyu super star'.."
"Yap"
"Sasa alikuwa anafanya nini kwenye huu mgahawa wa hadhi ya chini"
"Nafikiri kuna mtu alikuwa anakutana naye na hakutaka kuonekana, ni kijana mmoja anaitwa David naye kachukuliwa na hao majamaa tunao wafuatilia"
"Wamewachukua watu wangapi leo?"
"Watatu, nimeona wanawake wawili na huyu jamaa David ni watatu"
"Oops! Hawa jamaa wanatuumiza akili sana ni kheri serikali itangaze tu jambo hili na kuliweka wazi kuliko kufanya siri na watu wanaendelea kutoweka kila kukicha"
"Sasa kwa nini haitangazi, unajua siwaelewi kabisa?"
"Hawataki kutengeneza taharuki kwa raia, unajua hawa jamaa ni kama wana nguvu flani ambazo sio za kawaida yani ni kama wanatumia nguvu za giza hivi hata sielewi, huwezi kuamini ni miaka mitatu sasa tunaendelea kuwasaka kimya kimya lakini hakuna kitu tumewahi kupata hadi leo zaidi ya kukumbana na matukio ya ajabu ajabu yenye miujiza kibao"
"Lakini mbona kama hawa wanawake waliowateka leo sio wa kawaida yaani kwa kuwatazama tu wanamuonekano tofauti kabisa"
"Ndio maana nakwambia hili suala sio jepesi Godfrey. Kuna wakati hawa jamaa wenye helmet huwa wanaviteka viumbe vya ajabu kama hivyo unavyosema na kuna wakati huwa wanawateka binadamu wa kawaida kama walivyomteka mpenzi wako Dayana mwaka jana"
"Mmh! Sasa ni akina nani hawa?"
"Hatuelewi kabisa, vipi umepiga picha hata moja"
"Yap! Kuna hizi picha nimefanikiwa kuwapiga"
"Okay Good" Aliesema Brandina huku akiipokea simu ya David
Akawa anatazama picha zile moja baada ya nyingine.
"Si unaona hawa wanawake waliowabeba.. wamevaa magauni ya ajabu alafu yanafanana. Kwa Dunia yetu hii ni nani anaweza kuvaa kama hivi na akatoka mtaani kutembea"
"Ni ajabu sana, angalia hata gari la hawa jamaa halina plete number. Ni ngumu kuwapata" Godfrey aliongezea.
Baada ya hapo walishuka na kuingia mgahawani wakakagua mazingira na baadae walifanikiwa kumuona yule dada muhudumu aliyeanguka na kupoteza fahamu.
Brandina alipiga simu kutoa taarifa na punde gari ya wagonjwa ikafika na kumchukua.
"Huyu binti akiamka asizungumze na mtu yeyote hadi nifike mimi sawa" Brandina alitoa maelezo kwa mmoja kati ya watoa huduma wa afya waliofika mahali hapo.
"Sawa afande"
"God naomba unikutanishe na Tesha anaweza kuwa aliona chochote cha kutusaidia"
"Hapana, mdogo wangu hajaona chochote"
"Usijali sitamuingiza kwenye hii kesi isipokuwa nataka maelezo yake kidogo tu" Brandina alimtoa wasiwasi Godfrey.


ISRA...
Jitihada za kumvuta Handan kutoka shimoni ziliendelea, farasi walizidi kusogea mbele huku kamba ya Handan nayo ikizidi kusogea juu taratibu kutoka shimoni. Wakati huo hali ya hewa ilikuwa shwari kabisa kile kimbunga na tetemeko la ardhi vilitoweka ghafula mara tu baada ya Sasha kuzama shimoni akiwa na farasi wake.
Baada ya jitihada kubwa za wale wanawake walinzi wa Sasha kufanyika mwisho kamba ilifika ukomo, watu hawakuamini macho yao mara baada ya kumuona Handan akichomoza kutoka shimoni huku akiwa amemkumbatia Sasha kifuani mwake.
Handan na Sasha walitoka nje ya shimo, wale wanawake wawili walinzi walikimbia na kwenda kuwapokea kwa furaha.
Miili ya Sasha na Handan ilikuwa imejeruhiwa vibaya mno kutokana na misukosuko waliyokutana nayo shimoni. Damu yenye rangi ya kijani ilikuwa ikiwatoka katika maeneo mbalimbali waliyojeruhiwa.

"Asante Handan..." Alisema Sasha huku akimtazama Handan usoni mlinzi wake namba moja aliyejitoa kuyaokoa maisha yake.
"Usijali, lakini kwa nini ukafanya hivyo Sasha? Uliingia kufanya nini msituni?" Aliuliza Handan wote wakawa makini kusikiliza Sasha atajibu nini. Sasha naye akawa anawaza ni jibu gani sahihi la kuwapa kwani tayari alishaelezwa kuwa kila alichoongea na Bi Noha kilikuwa ni siri kubwa. Hakutakiwa kabisa kuufungua mdomo wake kuzungumza kuhusu jukumu zito alilopewa la kumlinda mwanadamu David.
Akiwa anawaza nini ajibu mara watu zaidi ya kumi na tano walifika na kuwazunguuka huku wakiwa wamenyoosha panga zao mbele. Walikuwa ni wale watu kutoka msafara wa Dumayo mjomba wa Sasha.
"Kuna nini? Mnataka nini?" Aliuliza Sasha huku akiwatazama watu hao kwa macho makali.
"Hawajui kitu hawa, mtu wa kumuuliza ni mjomba wako" Handan aliongea kwa sauti ya chini huku akiwapa ishara wale wanawake wengine walinzi wa Sasha wasijaribu kufanya lolote.
Sekunde chache baada Dumayo mjomba wa Sasha naye akasogea karibu akiwa juu ya farasi wake.

"Tunawakamata kwa kosa la kuingia ndani ya msitu bila ruhusa, mmesababisha majanga makubwa sana ndani ya ISRA, kutoweka kwa msitu wa Bi Noha ni laana kubwa ndani ya ISRA, ni lazima muwajibike kwa hili" Alisema Dumayo.

0756862047 Full kwa tsh ELF 1 TU
Je nini kitafuata?
David kapelekwa wapi?
Ni akina nani wamemchukua?
Kwa nini?

ITAENDELEA...
 
SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya..........16
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
Mmesababisha majanga makubwa sana ndani ya ISRA, kutoweka kwa msitu wa Bi Noha ni laana kubwa ndani ya ISRA, ni lazima muwajibike kwa hili" Alisema Dumayo.

Je nini kitafuata?

SASA ENDELEA...
ISRA ...
Mkuu wa ISRA Gu Gamilo pamoja na askari na baadhi ya wafanyakazi wengine ndani ya Ikulu ya ISRA walionekana pembeni ya shimo kubwa mahali palipokuwepo msitu mkubwa maarufu kama msitu wa Bi Noha.
Walikuwa wakitazama maafa makubwa yaliyotokea kiasi cha kusababisha msitu huo kutoweka wote kwa namna ya ajabu sana. Ilikuwa ni hali iliyomshangaza kila mmoja. Hakuna aliyekuwa na jibu sahihi ni kipi hasa kimepelekea msitu huo kupatwa na majanga na mwisho kuzama wote ardhini.
Gu Gamilo baba yake Sasha alitazama kwa umakini huku uso wake ukionekana kujawa na wasiwasi mwingi.
Gu Gamilo alikuwa ni mzee kiasi sura yake iliyokunjamana wakati wote, ilikuwa ni adimu kuliona tabasamu la mzee huyo. Nywele zake ndefu na nyeupe alizozifunga kwa juu, huku kidevu chake kikiwa kimefunikwa na ndevu zenye rangi nyeupe vilevile vilimfanya mzee huyo kuwa na muonekano wa pekee katika ISRA.

Mpaka dakika hiyo hakuna aliyejua sekeseke lilotokea upande wa pili wa shimo hilo kule walipo Dumayo Sasha na akina Handan.

Tukio la kutoweka kwa msitu huo lilionekana kumtisha sana Gu Gamilo kiasi cha mkumfanya akumbuke kwa mara ya mwisho alivyoingia ndani ya msitu huo akafanikiwa kuonana na Bi Noha ambaye kwa sasa ni marehemu. Gu Gamilo aliyakumbuka vizuri maneno mazito aliyowahi kuelezwa na bibi kizee huyu, alisema...

...... Umefanya kosa kubwa bila kufikiria kwa makini Gu Gamilo, kumfukuza Kaka yako MAGNUS nje ya ISRA bado hujamaliza tatizo, kwa kosa alilofanya alistahili adhabu kubwa zaidi ya hiyo. Ipo siku utayakumbuka maneno yangu Siku ambayo Magnus atarudi tena ISRA na kuitikisa kwa mara nyingine. Haijarishi itachukua miaka mingapi lakini jua kwamba Magnus ni lazima atarudi tena akiwa amejipanga vilivyo. Atakushambulia kutoka pande zote, mashariki magharibi kaskazini na kusini. Itakuwa ni siku ambayo utakosa kwa kukimbilia hata msitu wangu ambao pengine ungeweza kujificha hautokuwepo tena, litakuwepo shimo kubwa lisilo na mwisho Gu Gamilo..........
Haya yalikuwa ni maelezo ya Bi Noha ambaye ni kama alijua siku moja msitu wake utatoweka na kubaki shimo.

........Bi Noha, nifanyaje sasa kuzuia hili lisitokee tafadhali nisaidie, nawezaje kumzuia kaka Magnus...........

........Hakuna mtu yeyote ISRA atakae weza kumzuia Magnus, isipokuwa yupo Mwanadamu mmoja ambaye ataweza kupambana naye na kumzuia Magnus asirudi tena ISRA, mwanadamu huyo anahitaji ulinzi. Kama atakufa basi ISRA itakuwa kwenye wakati mgumu, kama akiwa hai basi ISRA itaendelea kusimama...........

........Ni mwanadamu gani huyo Bi Noha, unaweza kuniambia tafadhali.........

.........Mtafute, na hakikisha unamlinda kabla Magnus hajamtambua........

Hizi zilikuwa ni kumbukumbu za Mkuu wa ISRA Gu Gamilo. Baada ya hapo aliondoka kinyonge yeye na watu wake huku kila mmoja akisubiri kwa hamu Gu Gamilo atasema nini baada ya tukio hilo ambalo wengi waliliona kama ishara mbaya kwa ISRA.
Hatimae Gu Gamilo alilejea Ikulu ya ISRA yeye na msafara wake, wakati anaingia lango kuu la Ikulu alipokelewa kwa shauku na mkewe kipenzi Malkia Hella(Mama yake Sasha). Alikuwa akimsubiri Mumewe kwa hamu ili amueleze ni nini hasa kimetokea maana kila mtu alionekana kuogopa.
Alipoiona Sura ya huzuni kwa mumewe Gu Gamilo ilikuwa ni tafsiri tosha kuwa mambo hayakuwa mazuri kabisa.

"Ni nini kinaendelea huko nje Gu Gamilo..." Aliuliza Malkia Hella
"Umetoweka.." Gu Gamilo alijibu kinyonge
"Nini? Nini kimetoweka!?"
"Msitu wa Bi Noha" Ilikuwa ni kauli iliyo muacha kinywa wazi Malkia Hella.
Akiwa katika hali hiyo ya mshangao mara wakasikia mlio wa farasi langoni. Gu Gamilo na mkewe wakageuka taratibu kutazama.
Uso kwa uso wakamuona Dumayo anaingia taratibu na msafara wake. Gu Gamilo aliikunja sura yake akionyesha wazi ni jinsi gani alikuwa anamchukia shemeji yake huyo. Lakini tofauti na Malkia Hella yeye alitabasamu mara baada ya kumuona kaka yake Dumayo anaingia.

Katika hali ya kushangaza nyuma ya msafara wa Dumayo walionekana wanawake wanne wakiwa wamefungwa kamba mikokoni huku wakivutwa na watu wa Dumayo waliokuwa juu ya farasi. Wanawake hawa walikuwa ni Sasha, Handan pamoja na wale walinzi wengine wawili.
Gu Gamilo alitoa macho kwa mshangao asiamini anachokiona.
"Sasha" Gu Gamilo aliita kwa sauti ya chini.
Wakati huo Dumayo yeye awaka anatabasamu tu kama kawaida yake.


Upande wa pili......
David alifumbua macho yake taratibu fahamu zikiwa zimemrejea. Hali akiwa na maumivu makali ya kichwa, alitazama mahali alipo. Alikuwa ndani ya chumba kimoja kipana huku mikono na miguu yake ikiwa imefungwa na vyuma maalumu vilivyokuwa ukutani. Alikuwa ametanuliwa mikono yake na kusimamishwa kama vile yupo msalabani.
Alipotazama mbele akawaona wale jamaa wenye helmet zenye vioo vyekundu wakimalizia kuwafunga watu wengine watatu ukutani kama vile walivyomfunga yeye baada ya hapo wakafungua mlango wa chumba hicho wakatoka na kuondoka. David alitazama kushoto na kulia kwake ndipo akagundua kuwa karibu kuta zote nne za chumba hicho kulikuwa na watu wamefungwa kama yeye na wengi wao walikuwa wamepoteza fahamu hawajitambui. Kwa Haraka haraka aliwahesabu walifika kumi na mbili. David aliogopa sana, hakuelewa ni wapi yupo na amefikaje. Bado kumbukumbu zake zilikuwa hazijakaa sawasawa.

"Oya nyie, nifungueni, njooni mnifungue....mnajua mimi ni nani!??" David alianza kupiga kelele huku akifoka.
"NYIE JAMAAAAAAA..."
David alizidi kupiga kelele.
"Kelele zako hazito saidia kitu, unamaliza nguvu zako bure..."
Mara sauti hii ya kike ilisikika kutoka pembeni yake upande wa kushoto. Haraka David akageuka kutazama ni nani aliyemuongelesha.
Uso kwa uso akagonganisha macho yake na mmoja kati ya wale wanawake waliokuwa wakimfuatilia tangu awali. Alikuwa ni Femi, naye alikuwa amefungwa vilevile kama yeye.

David aliogopa sana alipomuona lakini alipogundua naye amefungwa kama yeye aliduwaa huku kumbukumbu za matukio kadhaa yaliyotokea tangu alipoanza kuwaona wanawake hao wa ajabu zikijirudia kichwani kwake kama filamu.

"We..we. ni nani?"
"Naitwa Femi..." Alijibu Femi huku akitema mate chini, mate yaliyochanganyikana na damu ya kijani.
David alitazama yale mate pale chini kisha akageuka tena na kumtazama yule mwanamke akiwa katika hali ya mshangao mkubwa.

"Fe..femi wa wapi? Kwa nini mlikuwa mnanifuatilia?"
"Kwa sababu tunataka kukuua" Femi alieleza bila kusita
"Bado unaendeleza ukichaa wako Femi si ndiyo?" Mara sauti ya Zucc kutoka upande wa kulia kwa David ilisikika. David alishtuka na kugeuka kumtazama.
"Na wewe pia ulikuwa ukinifuatilia..!" Alisema David lakini bado alionekana kuogopa.
"Achana naye huyo!" Alisema Femi akimtaka David asiendelee kuzungumza na Zucc, David akageuka tena upande wake wa kushoto alipo Femi.

"Mnataka kuniua nimewakosa nini kwani?"
"Tumeagizwa tukuue..." Alijibu Femi lakini kabla hajaendelea zaidi Zucc akamkatisha kwa sauti kali iliyojaa hasira, hakupendezwa kabisa na anachokifanya mwenzake.
"Femi nimesema acha ujingaaaa ..." Alifoka
"Zucc hakuna tulichobakiza kwani hata nikimwambia ukweli kuna ubaya gani? Unafikiri tutapona na tayari tumeshafanya uzembe wenyewe mwisho tumeingia kwenye mikono ya MAGNUS" Alieleza Femi.
"Ma..ma.. Magnus ndio na..nani kwani?" Aliuliza David akiwa ndio kwa mara yake ya kwanza analisikia jina la mtu huyo MAGNUS , mtu ambaye kwa mujibu wa maelezo ya marehemu Bi Noha anatakiwa kupambana naye siku za usoni.
Kabla David hajajibiwa swali lake mara wakasikia mtikisiko mkubwa na baadae wakahisi kama wanasogea mbele.
Kumbe chumba hicho kilikuwa ni moja kati ya vyumba vingi ndani ya Meli moja kubwa ambayo sasa iling'oa nanga na kuanza kukata mawimbi taratibu kuelekea kusiko julikana.

ITAENDELEA...

0756862047
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom