SIMULIZI RIWAYA
JF-Expert Member
- Feb 19, 2022
- 415
- 1,275
- Thread starter
- #21
SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya..........08
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
ILIPOISHIA...
Wakati gari waliyopanda David na Tesha ikizidi kwenda kwa kasi, upande wa pili Sasha akiwa juu ya farasi alionekana akiendelea kwenda mbele kwa kasi akipita katikati ya msitu ule mnene asijue huku nyuma alikotoka barabara ilikuwa ikijifunga.
Je nini kitafuata?
SASA ENDELEA....
Femi na Zucc wanawake waliotumwa na Handan kuhakikisha wanamuua David walionekana wakiwa wamesimama pembeni ya barabara. Tayari walikuwa wameshapanga ni namna gani watatekeleza mauaji ya kijana huyo ambaye amejikuta anaingia matatani tangu pale alipolishika boksi la Sasha kwa mikono yake.
"Wanakuja" Alisema Femi.
Zucc akiwa anatazama pembeni aligeuka kutazama upande wa pili wa barabara kwa mbali akaliona lile gari la Tesha ambalo kwa sasa David pia alikuwa ndani yake linakuja kwa kasi sana.
Femi na Zucc walikuwa wamepanga kusababisha ajali ambayo baadae itapelekea kifo cha David ili lengo lao litimie.
"Jitahidi kuwa makini Femi, ni NAFSI ya David pekee ndio tunaihitaji, hatakiwi kufa mtu mwingine tofauti na David"
"Usijali Zucc, ndani ya gari kuna watu wawili na watatu ni David, ni rahisi kuwalinda wengine na kumuua mmoja" Alisema Femi huku akisogea na kusimama katikati ya barabara.
Gari la Tesha likiwa limekaribia kufika pale walipo, Femi aliinua mkono wake wa kushoto akasogeza kiganja chake karibu na mdomo wake. Mara kuna moshi mweupe ukajitokeza juu ya kiganja cha mkono wake. Femi akavuta pumzi ndefu akiwa tayari kuupuliza ule moshi ambao ungekwenda moja kwa moja kwa dereva wa Tesha kisha kumchanganya na mwisho kusababisha ajali. Ajabu ni kwamba dereva wa Tesha hakuwa akimuona Femi pale katikati ya barabara.
David naye ambaye pengine angeweza kumuona hakuwa akitazama mbele, yeye alikuwa amejiinamia huku habari za mama yake kulazwa hospitali zikionekana kumchanganya sana.
"Femi achaaaa....!!" Mara Zucc alipiga kelele kumzuia mwezake.
Kwa kasi ya ajabu Femi aliruka na kusogea pembeni ya barabara tayari alishajua ni kwa nini mwenzake kamzuia asisababishe ajali ile waliyokusudia.
Kulikuwa na basi la abiria linakuja kutoka upande wa pili nyuma ya Femi, na endapo kama angelisababishia ajali gari la Tesha basi kulikuwa na hatari ya kutengeneza ajali nyingine ya basi hilo lililokuwa karibu kabisa.
Mwisho basi lile pamoja na gari la Tesha vilipishana salama salmini bila shida yoyote. Hii ikawa ni mara ya pili David ananusurika kuuawa.
"Huyu mtu inaonekana ana bahati ya pekee" Alisema Femi huku akionekana kukasilika mara baada ya kuipoteza nafasi ile.
"Tumfuate, safari hii tunamuondoa" Alijibu Zucc kisha wakashikana mikono wakapaa umbali wa mita kadhaa kisha wakapotea ghafula.
Upande wa pili katikati ya ule msitu mnene Sasha aliendelea kwenda kwa kasi akiwa juu ya farasi wake. Tayari alikuwa ameshaingia ndani sana ya msitu huo baada ya kwenda kwa zaidi ya dakika kumi.
Akiwa katika mwendo mara ghafula farasi akasimama. Ilikuwa ni hali iliyomshangaza Sasha kiasi, akajaribu kumpiga farasi wake asonge mbele lakini farasi akagoma kusogea, akajaribu tena na tena hali ikawa ni ile ile.
"Ooh! nini shida kipenzi changu" Alisema Sasha huku akimpapasa farasi wake lakini ghafula farasi alimrusha na kumtupa pembeni. Sasha alianguka chini akaumia mgongo, kabla hajafanya lolote farasi wake alikimbia huku akilia kwa sauti akatokomea kwenye msitu mnene.
Sasha akiwa pale chini ndipo aliposhtuka baada ya kugundua kuwa ile barabara aliyokuwa akiifuata imepotea ghafula, sasa alikuwa mwenyewe katikati ya msitu mnene.
Alijikongoja na kusimama kisha akawa anaangaza macho yake huko na kule. Hakuwa akiogopa hata kidogo mazingira kama hayo kwake yalikuwa ni ya kawaida, hayakumtisha.
Sasha alikuwa amedhamiria kwa dhati kuonana na Bi Noha kwa ghalama yoyote ile, alikuwa na shauku kubwa ya kuonana na mtu huyo.
Mara taratibu upepo ulianza kuvuma, upepo ambao ulikuwa ukiongezeka kadri muda unavyozidi kwenda. Sasha aliendelea kusimama imara huku akiangalia pande zote kwa ajili ya usalama wake. Hatimae upepo ukawa ni mkali sana kiasi cha kusababisha kimbuka kikubwa eneo lile.
Sasha alikimbia na kwenda kujificha nyuma ya mti mmoja mkubwa lakini hii haikutoshosha kimbunga kilikuwa ni kikali kiasi cha kuanza kung'oa miti iliyopa juu kama vipande vya karatasi, hali ilitisha mno. Sasha aliendelea kuushikilia ule mti lakini mwisho nao uling'oka na kupaa juu. Ajabu ni kwamba Sasha yeye hakubebwa na kile kimbunga, alibaki amejikunyata pale chini kwa zaidi ya dakika 5 mwisho hali ilianza kutulia na baadae kukawa na ukimya wa ajabu.
Sasha aliinua uso wake taratibu kutazama, alishangaa kuona mazingira ya eneo hilo yamebadilika kabisa. Lilikuwa ni eneo jeupe sana kila mahali kulikuwa kweupe, sakafu juu na pembeni kote kulikuwa kweupe. Mbele yake aliona mlango wa mbao ukifunguka akatoka mwanamke mmoja aliyevaa gauni refu lenye rangi ya machungwa. Alimtazama Sasha kisha akaachia tabasamu pana.
"Haujachelewa Sasha" Alisema yule mwanamke huku akimuonyesha Sasha ishara kuwa asimame na kumfuata. Bila woga Sasha alifanya hivyo, akapiga hatua na kuingia ndani kupitia ule mlango, baada ya kuingia yule mwanamke akaufunga.
Upande wa pili tayari David na Tesha walifika hospitali mahali alipolazwa mama yake David kama alivyoelezwa kwenye simu.
David alishuka kwenye gari upesi akawa anaelekea ndani ya hospitali hiyo. Tesha naye alishuka sekunde chache baadae, akawa anaongea na simu huku akipiga hatua taratibu sana kuingia hospitali.
David akiwa mwenye haraka tayari alishapata maelekezo chumba alicholazwa mama yake akawa anapiga hatua ndefu ndefu kuelekea huko.
Ilikuwa ni wodi ya wagonjwa wa kike chumba namba saba. David alifika akasimama mlangoni, akavuta pumzi ndefu kisha akaitoa taratibu. Alinyonga kitasa cha mlango akafungua taratibu na kuingia.
Uso kwa uso David akagonganisha macho yake na macho ya mdogo wake wa kike, aitwae Tatu. Wakati huo akawaona madaktari zaidi ya watatu wakiwa wamesimama kukizunguuka kitanda alicholazwa mama yake.
Upande wa pili nako mara baada ya Sasha kuingia ndani kupitia ule mlango wa mbao, sasa alikuwa ndani ya chumba kimoja kipana sana, mbele yake aliona wanawake watatu wakiwa wamesimama kukizunguuka kitanda ambacho juu yake alilala bibi kizee moja aliyeonekana kuzeeka sana.
Mara baada ya Sasha kuingia wale watu waliosimama waligeuka kwa pamoja kumtazama. Mmoja kati yao alikimbia nakwenda kumkumbatia Sasha kwa nguvu.
Tatu mdogo wake David alipomuona kaka yake ameingia alikimbia na kwenda kumkumbatia kwa nguvu huku akilia machozi.
Yule mwanamke aliyemkumbatia Sasha naye alikuwa akilia machozi.
"Kaka" Tatu aliita
Wakati huo daktari mmoja akasogea pale walipo
"Wewe ndio David?"
"Ndio mimi Daktari"
"Mama yako alikuwa akikusuburi sana tunakuacha ufanye naye mazungumzo kisha uje ofisini" Alisema daktari
Upande wa pili...
"Sasha" Yule mwanamke aliyemkumbatia Sasha aliita.
"Abeee"
"Bi Noha, amekusuburi kwa zaidi ya miaka 10, aliamini lazima ipo siku utakuja kabla ya kifo chake, hatimaye leo umekuja, haujachelewa Sasha. Tunakuacha ufanye naye mazungumzo muhimu" Alisema yule mwanamke.
Je, nini kitafuata?
Ni nini kinaendelea kati ya matukio haya mawili ya sehemu mbili tofauti lakini yenye kufanana?
Nini maana yake?
Hii ni SASHA MLINZI WA NAFSI sehemu ya 8 tukutane sehemu ya 9.
RIWAYA HII YA KUSISIMUA INAPATIKANA YOTE KWA TSH 1000 TU NJOO WHATSAPP NAMBA
0756862047.
Sehemu ya..........08
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
ILIPOISHIA...
Wakati gari waliyopanda David na Tesha ikizidi kwenda kwa kasi, upande wa pili Sasha akiwa juu ya farasi alionekana akiendelea kwenda mbele kwa kasi akipita katikati ya msitu ule mnene asijue huku nyuma alikotoka barabara ilikuwa ikijifunga.
Je nini kitafuata?
SASA ENDELEA....
Femi na Zucc wanawake waliotumwa na Handan kuhakikisha wanamuua David walionekana wakiwa wamesimama pembeni ya barabara. Tayari walikuwa wameshapanga ni namna gani watatekeleza mauaji ya kijana huyo ambaye amejikuta anaingia matatani tangu pale alipolishika boksi la Sasha kwa mikono yake.
"Wanakuja" Alisema Femi.
Zucc akiwa anatazama pembeni aligeuka kutazama upande wa pili wa barabara kwa mbali akaliona lile gari la Tesha ambalo kwa sasa David pia alikuwa ndani yake linakuja kwa kasi sana.
Femi na Zucc walikuwa wamepanga kusababisha ajali ambayo baadae itapelekea kifo cha David ili lengo lao litimie.
"Jitahidi kuwa makini Femi, ni NAFSI ya David pekee ndio tunaihitaji, hatakiwi kufa mtu mwingine tofauti na David"
"Usijali Zucc, ndani ya gari kuna watu wawili na watatu ni David, ni rahisi kuwalinda wengine na kumuua mmoja" Alisema Femi huku akisogea na kusimama katikati ya barabara.
Gari la Tesha likiwa limekaribia kufika pale walipo, Femi aliinua mkono wake wa kushoto akasogeza kiganja chake karibu na mdomo wake. Mara kuna moshi mweupe ukajitokeza juu ya kiganja cha mkono wake. Femi akavuta pumzi ndefu akiwa tayari kuupuliza ule moshi ambao ungekwenda moja kwa moja kwa dereva wa Tesha kisha kumchanganya na mwisho kusababisha ajali. Ajabu ni kwamba dereva wa Tesha hakuwa akimuona Femi pale katikati ya barabara.
David naye ambaye pengine angeweza kumuona hakuwa akitazama mbele, yeye alikuwa amejiinamia huku habari za mama yake kulazwa hospitali zikionekana kumchanganya sana.
"Femi achaaaa....!!" Mara Zucc alipiga kelele kumzuia mwezake.
Kwa kasi ya ajabu Femi aliruka na kusogea pembeni ya barabara tayari alishajua ni kwa nini mwenzake kamzuia asisababishe ajali ile waliyokusudia.
Kulikuwa na basi la abiria linakuja kutoka upande wa pili nyuma ya Femi, na endapo kama angelisababishia ajali gari la Tesha basi kulikuwa na hatari ya kutengeneza ajali nyingine ya basi hilo lililokuwa karibu kabisa.
Mwisho basi lile pamoja na gari la Tesha vilipishana salama salmini bila shida yoyote. Hii ikawa ni mara ya pili David ananusurika kuuawa.
"Huyu mtu inaonekana ana bahati ya pekee" Alisema Femi huku akionekana kukasilika mara baada ya kuipoteza nafasi ile.
"Tumfuate, safari hii tunamuondoa" Alijibu Zucc kisha wakashikana mikono wakapaa umbali wa mita kadhaa kisha wakapotea ghafula.
Upande wa pili katikati ya ule msitu mnene Sasha aliendelea kwenda kwa kasi akiwa juu ya farasi wake. Tayari alikuwa ameshaingia ndani sana ya msitu huo baada ya kwenda kwa zaidi ya dakika kumi.
Akiwa katika mwendo mara ghafula farasi akasimama. Ilikuwa ni hali iliyomshangaza Sasha kiasi, akajaribu kumpiga farasi wake asonge mbele lakini farasi akagoma kusogea, akajaribu tena na tena hali ikawa ni ile ile.
"Ooh! nini shida kipenzi changu" Alisema Sasha huku akimpapasa farasi wake lakini ghafula farasi alimrusha na kumtupa pembeni. Sasha alianguka chini akaumia mgongo, kabla hajafanya lolote farasi wake alikimbia huku akilia kwa sauti akatokomea kwenye msitu mnene.
Sasha akiwa pale chini ndipo aliposhtuka baada ya kugundua kuwa ile barabara aliyokuwa akiifuata imepotea ghafula, sasa alikuwa mwenyewe katikati ya msitu mnene.
Alijikongoja na kusimama kisha akawa anaangaza macho yake huko na kule. Hakuwa akiogopa hata kidogo mazingira kama hayo kwake yalikuwa ni ya kawaida, hayakumtisha.
Sasha alikuwa amedhamiria kwa dhati kuonana na Bi Noha kwa ghalama yoyote ile, alikuwa na shauku kubwa ya kuonana na mtu huyo.
Mara taratibu upepo ulianza kuvuma, upepo ambao ulikuwa ukiongezeka kadri muda unavyozidi kwenda. Sasha aliendelea kusimama imara huku akiangalia pande zote kwa ajili ya usalama wake. Hatimae upepo ukawa ni mkali sana kiasi cha kusababisha kimbuka kikubwa eneo lile.
Sasha alikimbia na kwenda kujificha nyuma ya mti mmoja mkubwa lakini hii haikutoshosha kimbunga kilikuwa ni kikali kiasi cha kuanza kung'oa miti iliyopa juu kama vipande vya karatasi, hali ilitisha mno. Sasha aliendelea kuushikilia ule mti lakini mwisho nao uling'oka na kupaa juu. Ajabu ni kwamba Sasha yeye hakubebwa na kile kimbunga, alibaki amejikunyata pale chini kwa zaidi ya dakika 5 mwisho hali ilianza kutulia na baadae kukawa na ukimya wa ajabu.
Sasha aliinua uso wake taratibu kutazama, alishangaa kuona mazingira ya eneo hilo yamebadilika kabisa. Lilikuwa ni eneo jeupe sana kila mahali kulikuwa kweupe, sakafu juu na pembeni kote kulikuwa kweupe. Mbele yake aliona mlango wa mbao ukifunguka akatoka mwanamke mmoja aliyevaa gauni refu lenye rangi ya machungwa. Alimtazama Sasha kisha akaachia tabasamu pana.
"Haujachelewa Sasha" Alisema yule mwanamke huku akimuonyesha Sasha ishara kuwa asimame na kumfuata. Bila woga Sasha alifanya hivyo, akapiga hatua na kuingia ndani kupitia ule mlango, baada ya kuingia yule mwanamke akaufunga.
Upande wa pili tayari David na Tesha walifika hospitali mahali alipolazwa mama yake David kama alivyoelezwa kwenye simu.
David alishuka kwenye gari upesi akawa anaelekea ndani ya hospitali hiyo. Tesha naye alishuka sekunde chache baadae, akawa anaongea na simu huku akipiga hatua taratibu sana kuingia hospitali.
David akiwa mwenye haraka tayari alishapata maelekezo chumba alicholazwa mama yake akawa anapiga hatua ndefu ndefu kuelekea huko.
Ilikuwa ni wodi ya wagonjwa wa kike chumba namba saba. David alifika akasimama mlangoni, akavuta pumzi ndefu kisha akaitoa taratibu. Alinyonga kitasa cha mlango akafungua taratibu na kuingia.
Uso kwa uso David akagonganisha macho yake na macho ya mdogo wake wa kike, aitwae Tatu. Wakati huo akawaona madaktari zaidi ya watatu wakiwa wamesimama kukizunguuka kitanda alicholazwa mama yake.
Upande wa pili nako mara baada ya Sasha kuingia ndani kupitia ule mlango wa mbao, sasa alikuwa ndani ya chumba kimoja kipana sana, mbele yake aliona wanawake watatu wakiwa wamesimama kukizunguuka kitanda ambacho juu yake alilala bibi kizee moja aliyeonekana kuzeeka sana.
Mara baada ya Sasha kuingia wale watu waliosimama waligeuka kwa pamoja kumtazama. Mmoja kati yao alikimbia nakwenda kumkumbatia Sasha kwa nguvu.
Tatu mdogo wake David alipomuona kaka yake ameingia alikimbia na kwenda kumkumbatia kwa nguvu huku akilia machozi.
Yule mwanamke aliyemkumbatia Sasha naye alikuwa akilia machozi.
"Kaka" Tatu aliita
Wakati huo daktari mmoja akasogea pale walipo
"Wewe ndio David?"
"Ndio mimi Daktari"
"Mama yako alikuwa akikusuburi sana tunakuacha ufanye naye mazungumzo kisha uje ofisini" Alisema daktari
Upande wa pili...
"Sasha" Yule mwanamke aliyemkumbatia Sasha aliita.
"Abeee"
"Bi Noha, amekusuburi kwa zaidi ya miaka 10, aliamini lazima ipo siku utakuja kabla ya kifo chake, hatimaye leo umekuja, haujachelewa Sasha. Tunakuacha ufanye naye mazungumzo muhimu" Alisema yule mwanamke.
Je, nini kitafuata?
Ni nini kinaendelea kati ya matukio haya mawili ya sehemu mbili tofauti lakini yenye kufanana?
Nini maana yake?
Hii ni SASHA MLINZI WA NAFSI sehemu ya 8 tukutane sehemu ya 9.
RIWAYA HII YA KUSISIMUA INAPATIKANA YOTE KWA TSH 1000 TU NJOO WHATSAPP NAMBA
0756862047.