SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,430
- 23,748
- Thread starter
- #201
*ROHO YAKE INADAI --- 43*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Mbali na hivyo, watu kadhaa, haswa majirani, walikuwa wametoka nje ya makazi yao wakitazama eneo la tukio kwa macho ya maulizo na nyuso za mashaka. Kulikuwa na zogo fulani midomoni mwao.
Muda si mrefu gari ya wagonjwa ikawasili eneoni na kujitengenezea vema. Kutoka ndani ya nyumba, ikatolewa miili mitatu ambayo imefunikwa gubigubi, ikatiwa ndani ya gari la wagonjwa na kisha gari hilo kutimka.
ENDELEA
Baadae ikaja kuwekwa bayana ya kuwa afisa Randall alikuwa amefariki, pia mke na mtoto wake mdogo aitwae Bestie. Na kama haitoshi, baadae taarifa zaidi zikaja juu ya kifo cha afisa Williamson. Alikutwa amekakamaa ndani ya chumba chake mwili wake ukiwa mweusi kabisa kana kwamba mtu aliyekitwa na shoti kubwa ya umeme.
Vifo vikawekwa bayana kwenye vyombo vya habari na karibia Boston nzima ikajuzwa. Misiba miwili iliyotokea ndani ya usiku mmoja. Na yote ikiwa imefanana mtindo, yaani muuaji hakuwa anajulikana.
Ila hakuwa anajulikana kweli?
“Padri Alfonso atakuwa ameshamuua,” alisema Brian aliyekuwa ameketi nyuma ya gari hili liendalo. Kwa mbele alikuwa ameketi Wisconsin na Mama ambaye alikuwa ameshikilia usukani.
Katika majira haya ya asubuhi, walikuwa wanaelekea msibani. Msiba wa Brewster. Siku hiyo ndiyo ilikuwa siku ya mazishi yake kwa mujibu wa taarifa. Jana yake hawakupata muda wa kwenda msibani kutokana na kutingwa na shughuli zile za hapa na pale polisi.
“Mbaya zaidi amewaua wote,” akasema Mama. “Ameona awamalize kabisa kufuta ushahidi.”
Kidogo Wisconsin akasema, “ebu twendee kule kwenye kituo cha habari!” Mama akamtazama na kisha akarejesha uso wake haraka barabarani akiuliza, “kufanya nini huko?”
“Nahisi yule dada atakuwa mashakani,” Wisconsin akaeleza. “Kama wale polisi wameuawa wote, basi huenda pia akamuwinda na yule mwanamke ammalize!”
Basi Mama akaongeza mwendokasi akielekezea chombo kule alipoambiwa, muda mchache, kama dakika kumi na tatu, wakawa wamewasili. Wakashuka na kwenda ndani ya ofisi. Pale kwenye ofisi ya mapokezi wakamkuta mwanamke mwingine mwembamba sana mwenye nywele nyingi nyeusi.
Wakamsalimu na kumweleza shida yao, “Tumemkuta Karen?” Mama Brian akauliza pasipo kuonyesha shaka usoni. Yule mwanamapokezi akawatazama kidogo alafu akatabasamu na kutikisa kichwa. “Hapana, hayupo!”
“Atakuja leo?”
“Yah! Atakuja. Ninyi ni wakina nani?”
“Wageni wake tu, tulikuwa na shida naye. Unaweza kuwasiliana naye kumwambia twamngoja?”
“Nishajaribu hilo, nimeongea naye mara moja, lakini baada ya muda sikumpata,” akasema yule dada na kuongezea, “Nimeshampigia mara tano, hajapokea. Mara ya mwisho simu yake haikupatikana kabisa!”
“Unajua unapokaa?” akauliza Mama Brian sasa akiwa ametoa macho.
**
Gari lilipiga breki kali na kisha kukata kona kwa fujo. Mama Brian alikuwa amechanganyikiwa? Aliendesha gari upesi sana na hata wale abiria aliowabeba hawakumkataza wala kumwonya.
Aliyavuka magari mengine kwa haraka, akiwa anabadilisha gia na kukanyagia pedeli ya mafuta, akaadhibu barabara kwa ustadi. Akatembea mithili ya kishada. Uso wake ulikuwa umetambaliwa na mashaka na mikono yake ilikuwa imeshikilia usukani kwanguvu.
Kitu kimoja walichokiamini ni kuwa mwanamke huyo anaweza kuwa mzima, au basi kama sivyo, atakuwa yupo hatarini kwa muda huo, kwani kwa makadirio ya muda ambao aliongea na mwenzake, ilikuwa ni asubuhi hii hii, muda mchache nyuma.
Lakini kwanini hakuuawa usiku? Sababu wauaji walikuwa wakiwamaliza maafisa wa polisi kama ilivyoonyesha wa mwisho kuuawa, afisa Williamson, kwa mujibu wa makadirio ya maelezo ya daktari, alikata moto majira ya alfajiri.
Punde gari lilipokamta breki, likiwa limetumia dakika nane tu kufika hapo, Wisconsin na Brian wakawa wa kwanza kushuka, nyuma wakifuatiwa na Mama yao. Wakagonga mlango, ulipokawia kufunguliwa, Wisconsin akausukuma kwanguvu akitumia bega lake pana. Mlango ukafunguka wakazama ndani.
Kutazama sebuleni hakukuwa na mtu, ila punde kidogo, Karen akatokea akiwa amefungia taulo lake jeupe kifuani. Mwili wake ulikuwa umejawa na maji na macho yake yakiwa yamebebeba mashaka.
Mama Brian akatahamaki kumwona, akaita, “Karen!” na kisha akamkimbilia na kumjulia hali. Karen akasema yu sawa, hakukumbana na tatizo lolote. Ndipo Mama Brian na wenziwe wakaketi na kumweleza kwanini walikuwa wanahofia mpaka kukimbia kuja hapo.
“Kuwa makini sana,” Wisconsin akamhusia. “Huenda muuaji akakufuata na wewe pia.”
Karen, akiwa aliyejawa na woga na mkanganyiko, akatikisa kichwa chake kupokea taarifa hiyo. Akaenda ndani na kujivesha nguo kisha akawaomba wageni wake hao wa dharura wampeleke kazini kwani hana usafiri.
**
“Madam, tunaomba uegeshe upande wako wa kulia, huko kuna nafasi zaidi!” alisema mwanaume aliyevalia sare ya suti nyeusi na mikononi mwake akiwa amevalia glovu nyeupe. Alikuwa hapa maalum kwa ajili ya kazi ya kuwalekeza wageni, aidha wenye vyombo vya usafiri ama lah, waliofika hapa kwenye mazishi.
“Nashukuru.” Mama Brian akakunja kona kufuata maelekezo. Alipoegesha gari na kulizima, wakashuka na kuelekea kwenye viti kadhaa ambavyo viliwekwa kwenye uwanja wa makaburi. Wakaketi na kuchambua eneo.
Hapo kulikuwa na watu takribani thelathini na tatu na magari kumi. Jeneza la Brewster lilikuwa limeshawekwa karibu kabisa na shimo lake na mbele kabisa, kwenye mpangilio wa viti, walikuwa wameketi watu wa karibu wa Brewster, haswa wafanyakazi wenziwe kwani hakuwa na marafiki.
Miongoni mwao, Padri Alfonso na watumishi wawili wa kike waliovalia sare zao kama ilivyo ada wakati wowote.
“Brian,” Wisconsin akaita kwa kunong’oneza. “Hakikisha macho yako yanamtazama Padri Alfonso muda wote, sawa?” Kabla Brian hajajibu, Padri Alfonso akageuka na kuwatazama kwa kuwakazia macho, na kisha akarejesha uso wake mbele.
Brian akauliza, “Atakuwa amesikia?” Kabla Wisconsin hajajibu, wakamwona Padri Alfonso akitikisa kichwa. Wakashtuka na kutazamana kisha hawakuongea tena.
Basi tangu hapo, Brian akawa anamtazama Padri Alfonso kwa woga. Kweli hakubandua macho yake. Hata alipoyafumba, akayafumbua upesi na kuendelea kukodoa.
Muda kidogo Wisconsin akampatia kikaratasi kidogo chenye ujumbe. Akaikichukua na kukisoma.
“Tutawasiliana kwa maandishi,” ujumbe ulisomeka vivyo. Akamtazama Wisconsin na kumtikisia kichwa kama ishara. Wisconsin akamwandikia pia Mama ujumbe kuwa watakuwa wanasiliana kwa maandishi, naye Mama akaelewa.
Muda ukasonga zaidi. Ilipopita lisaa limoja, shughuli za mazishi zikaanza rasmi baada ya ujio wa mwakilishi mkubwa wa serikali. Jeneza likafunguliwa, na watu wakaanza zoezi la kumuaga Brewster kwa mara ya mwisho kabla hajamezwa na udongo.
‘Utaenda kuaga?’ Wisconsin akaandika ujumbe wake kwa peni na kumpatia Brian.
‘Hapana, sitaenda,’ Brian akajibu na kurejesha karatasi.
‘Kwanini?’
‘Naogopa.’
‘Umekuwa ukimtazama Padri Alfonso?’
Kabla Brian hajaandika kujibu, akarusha tena macho yake kumtafuta Padri Alfonso. Hakumwona. Akaangaza kushoto na kulia, hakumwona. Akastaajabu atakuwa ameenda wapi, mara yake ya mwisho kumwona alikuwa amesimama kandokando na jeneza.
Alipomkosa, akarejesha macho yake kwenye karatasi apate kumwandikia Wisconsin ujumbe. Ajabu alipotazama karatasi hiyo, akaikuta tayari ina maandishi. Haukuwa mwandiko wa Wisconsin!
‘Unanitafuta?’ Maandishi yalisomeka hivyo. Brian akahofia sana. Akarusha tena macho yake kuangaza, hakuona kitu. Aliporejesha tena macho yake kwenye karatasi akaukuta ujumbe mwingine, ‘Nipo nyumbani kwenu.’
Hapa sasa ndiyo akatamani kupiga kelele. Haraka akamrejeshea Wisconsin kile kikaratasi kisha akamshtua Mama yake kumtaka waende nyumbani haraka iwezekanavyo!
“Yupo nyumbani!” Brian alisema akiwa amekunja ndita, macho yamejawa na woga. Nyumbani alikuwa amebakia Olivia pekee.
Basi wakatoka upesi na kwenda kwenye gari. Mama akatia ufunguo na kuwasha chombo, ila kabla hawajaondoka, akamwona Padri Alfonso kwa mbali akiwa amesimama na watu watatu wanateta!
Akauliza akistaajabu, “si yule?” wote wakatazama. Kweli alikuwa ndiye. Wakiwa kwenye buwazo hilo, Padri Alfonso akawapatia mkono watu wawili aliokuwa amesimama nao, kisha akaanza kutembea kulifuata gari walilopo wakina Brian.
“Mama, twende!” Brian akasema akimpigapiga mama yake begani, lakini Wisconsin akasema, “Hapana.” wote wakamtazama kwa nyuso za kushangaa.
“Ngoja tuone atafanya nini mbele za watu!”
Basi punde Padri Alfonso akawafikia na kutabasamu. Akawasalimu na kuwakaribisha kwa ukarimu.
“Kuna tatizo lolote?” akauliza.
Mama Brian akawahi kutikisa kichwa na kusema, “Hamna!”
“Una uhakika?” Padri Alfonso akauliza.
“Ndio, hamna!” Mama akasihi. “Nashukuru, padri.”
Padri akamtazama na kumuuliza kwa mara nyingine, “Una uhakika?” sasa hivi macho yake alikuwa ameyakodoa. Mama Brian akasihi baridi na moyo wake waenda mbio.
Ghafla Padri akatabasamu na kusema, “Msijali.” kisha akaenda zake.
**
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Mbali na hivyo, watu kadhaa, haswa majirani, walikuwa wametoka nje ya makazi yao wakitazama eneo la tukio kwa macho ya maulizo na nyuso za mashaka. Kulikuwa na zogo fulani midomoni mwao.
Muda si mrefu gari ya wagonjwa ikawasili eneoni na kujitengenezea vema. Kutoka ndani ya nyumba, ikatolewa miili mitatu ambayo imefunikwa gubigubi, ikatiwa ndani ya gari la wagonjwa na kisha gari hilo kutimka.
ENDELEA
Baadae ikaja kuwekwa bayana ya kuwa afisa Randall alikuwa amefariki, pia mke na mtoto wake mdogo aitwae Bestie. Na kama haitoshi, baadae taarifa zaidi zikaja juu ya kifo cha afisa Williamson. Alikutwa amekakamaa ndani ya chumba chake mwili wake ukiwa mweusi kabisa kana kwamba mtu aliyekitwa na shoti kubwa ya umeme.
Vifo vikawekwa bayana kwenye vyombo vya habari na karibia Boston nzima ikajuzwa. Misiba miwili iliyotokea ndani ya usiku mmoja. Na yote ikiwa imefanana mtindo, yaani muuaji hakuwa anajulikana.
Ila hakuwa anajulikana kweli?
“Padri Alfonso atakuwa ameshamuua,” alisema Brian aliyekuwa ameketi nyuma ya gari hili liendalo. Kwa mbele alikuwa ameketi Wisconsin na Mama ambaye alikuwa ameshikilia usukani.
Katika majira haya ya asubuhi, walikuwa wanaelekea msibani. Msiba wa Brewster. Siku hiyo ndiyo ilikuwa siku ya mazishi yake kwa mujibu wa taarifa. Jana yake hawakupata muda wa kwenda msibani kutokana na kutingwa na shughuli zile za hapa na pale polisi.
“Mbaya zaidi amewaua wote,” akasema Mama. “Ameona awamalize kabisa kufuta ushahidi.”
Kidogo Wisconsin akasema, “ebu twendee kule kwenye kituo cha habari!” Mama akamtazama na kisha akarejesha uso wake haraka barabarani akiuliza, “kufanya nini huko?”
“Nahisi yule dada atakuwa mashakani,” Wisconsin akaeleza. “Kama wale polisi wameuawa wote, basi huenda pia akamuwinda na yule mwanamke ammalize!”
Basi Mama akaongeza mwendokasi akielekezea chombo kule alipoambiwa, muda mchache, kama dakika kumi na tatu, wakawa wamewasili. Wakashuka na kwenda ndani ya ofisi. Pale kwenye ofisi ya mapokezi wakamkuta mwanamke mwingine mwembamba sana mwenye nywele nyingi nyeusi.
Wakamsalimu na kumweleza shida yao, “Tumemkuta Karen?” Mama Brian akauliza pasipo kuonyesha shaka usoni. Yule mwanamapokezi akawatazama kidogo alafu akatabasamu na kutikisa kichwa. “Hapana, hayupo!”
“Atakuja leo?”
“Yah! Atakuja. Ninyi ni wakina nani?”
“Wageni wake tu, tulikuwa na shida naye. Unaweza kuwasiliana naye kumwambia twamngoja?”
“Nishajaribu hilo, nimeongea naye mara moja, lakini baada ya muda sikumpata,” akasema yule dada na kuongezea, “Nimeshampigia mara tano, hajapokea. Mara ya mwisho simu yake haikupatikana kabisa!”
“Unajua unapokaa?” akauliza Mama Brian sasa akiwa ametoa macho.
**
Gari lilipiga breki kali na kisha kukata kona kwa fujo. Mama Brian alikuwa amechanganyikiwa? Aliendesha gari upesi sana na hata wale abiria aliowabeba hawakumkataza wala kumwonya.
Aliyavuka magari mengine kwa haraka, akiwa anabadilisha gia na kukanyagia pedeli ya mafuta, akaadhibu barabara kwa ustadi. Akatembea mithili ya kishada. Uso wake ulikuwa umetambaliwa na mashaka na mikono yake ilikuwa imeshikilia usukani kwanguvu.
Kitu kimoja walichokiamini ni kuwa mwanamke huyo anaweza kuwa mzima, au basi kama sivyo, atakuwa yupo hatarini kwa muda huo, kwani kwa makadirio ya muda ambao aliongea na mwenzake, ilikuwa ni asubuhi hii hii, muda mchache nyuma.
Lakini kwanini hakuuawa usiku? Sababu wauaji walikuwa wakiwamaliza maafisa wa polisi kama ilivyoonyesha wa mwisho kuuawa, afisa Williamson, kwa mujibu wa makadirio ya maelezo ya daktari, alikata moto majira ya alfajiri.
Punde gari lilipokamta breki, likiwa limetumia dakika nane tu kufika hapo, Wisconsin na Brian wakawa wa kwanza kushuka, nyuma wakifuatiwa na Mama yao. Wakagonga mlango, ulipokawia kufunguliwa, Wisconsin akausukuma kwanguvu akitumia bega lake pana. Mlango ukafunguka wakazama ndani.
Kutazama sebuleni hakukuwa na mtu, ila punde kidogo, Karen akatokea akiwa amefungia taulo lake jeupe kifuani. Mwili wake ulikuwa umejawa na maji na macho yake yakiwa yamebebeba mashaka.
Mama Brian akatahamaki kumwona, akaita, “Karen!” na kisha akamkimbilia na kumjulia hali. Karen akasema yu sawa, hakukumbana na tatizo lolote. Ndipo Mama Brian na wenziwe wakaketi na kumweleza kwanini walikuwa wanahofia mpaka kukimbia kuja hapo.
“Kuwa makini sana,” Wisconsin akamhusia. “Huenda muuaji akakufuata na wewe pia.”
Karen, akiwa aliyejawa na woga na mkanganyiko, akatikisa kichwa chake kupokea taarifa hiyo. Akaenda ndani na kujivesha nguo kisha akawaomba wageni wake hao wa dharura wampeleke kazini kwani hana usafiri.
**
“Madam, tunaomba uegeshe upande wako wa kulia, huko kuna nafasi zaidi!” alisema mwanaume aliyevalia sare ya suti nyeusi na mikononi mwake akiwa amevalia glovu nyeupe. Alikuwa hapa maalum kwa ajili ya kazi ya kuwalekeza wageni, aidha wenye vyombo vya usafiri ama lah, waliofika hapa kwenye mazishi.
“Nashukuru.” Mama Brian akakunja kona kufuata maelekezo. Alipoegesha gari na kulizima, wakashuka na kuelekea kwenye viti kadhaa ambavyo viliwekwa kwenye uwanja wa makaburi. Wakaketi na kuchambua eneo.
Hapo kulikuwa na watu takribani thelathini na tatu na magari kumi. Jeneza la Brewster lilikuwa limeshawekwa karibu kabisa na shimo lake na mbele kabisa, kwenye mpangilio wa viti, walikuwa wameketi watu wa karibu wa Brewster, haswa wafanyakazi wenziwe kwani hakuwa na marafiki.
Miongoni mwao, Padri Alfonso na watumishi wawili wa kike waliovalia sare zao kama ilivyo ada wakati wowote.
“Brian,” Wisconsin akaita kwa kunong’oneza. “Hakikisha macho yako yanamtazama Padri Alfonso muda wote, sawa?” Kabla Brian hajajibu, Padri Alfonso akageuka na kuwatazama kwa kuwakazia macho, na kisha akarejesha uso wake mbele.
Brian akauliza, “Atakuwa amesikia?” Kabla Wisconsin hajajibu, wakamwona Padri Alfonso akitikisa kichwa. Wakashtuka na kutazamana kisha hawakuongea tena.
Basi tangu hapo, Brian akawa anamtazama Padri Alfonso kwa woga. Kweli hakubandua macho yake. Hata alipoyafumba, akayafumbua upesi na kuendelea kukodoa.
Muda kidogo Wisconsin akampatia kikaratasi kidogo chenye ujumbe. Akaikichukua na kukisoma.
“Tutawasiliana kwa maandishi,” ujumbe ulisomeka vivyo. Akamtazama Wisconsin na kumtikisia kichwa kama ishara. Wisconsin akamwandikia pia Mama ujumbe kuwa watakuwa wanasiliana kwa maandishi, naye Mama akaelewa.
Muda ukasonga zaidi. Ilipopita lisaa limoja, shughuli za mazishi zikaanza rasmi baada ya ujio wa mwakilishi mkubwa wa serikali. Jeneza likafunguliwa, na watu wakaanza zoezi la kumuaga Brewster kwa mara ya mwisho kabla hajamezwa na udongo.
‘Utaenda kuaga?’ Wisconsin akaandika ujumbe wake kwa peni na kumpatia Brian.
‘Hapana, sitaenda,’ Brian akajibu na kurejesha karatasi.
‘Kwanini?’
‘Naogopa.’
‘Umekuwa ukimtazama Padri Alfonso?’
Kabla Brian hajaandika kujibu, akarusha tena macho yake kumtafuta Padri Alfonso. Hakumwona. Akaangaza kushoto na kulia, hakumwona. Akastaajabu atakuwa ameenda wapi, mara yake ya mwisho kumwona alikuwa amesimama kandokando na jeneza.
Alipomkosa, akarejesha macho yake kwenye karatasi apate kumwandikia Wisconsin ujumbe. Ajabu alipotazama karatasi hiyo, akaikuta tayari ina maandishi. Haukuwa mwandiko wa Wisconsin!
‘Unanitafuta?’ Maandishi yalisomeka hivyo. Brian akahofia sana. Akarusha tena macho yake kuangaza, hakuona kitu. Aliporejesha tena macho yake kwenye karatasi akaukuta ujumbe mwingine, ‘Nipo nyumbani kwenu.’
Hapa sasa ndiyo akatamani kupiga kelele. Haraka akamrejeshea Wisconsin kile kikaratasi kisha akamshtua Mama yake kumtaka waende nyumbani haraka iwezekanavyo!
“Yupo nyumbani!” Brian alisema akiwa amekunja ndita, macho yamejawa na woga. Nyumbani alikuwa amebakia Olivia pekee.
Basi wakatoka upesi na kwenda kwenye gari. Mama akatia ufunguo na kuwasha chombo, ila kabla hawajaondoka, akamwona Padri Alfonso kwa mbali akiwa amesimama na watu watatu wanateta!
Akauliza akistaajabu, “si yule?” wote wakatazama. Kweli alikuwa ndiye. Wakiwa kwenye buwazo hilo, Padri Alfonso akawapatia mkono watu wawili aliokuwa amesimama nao, kisha akaanza kutembea kulifuata gari walilopo wakina Brian.
“Mama, twende!” Brian akasema akimpigapiga mama yake begani, lakini Wisconsin akasema, “Hapana.” wote wakamtazama kwa nyuso za kushangaa.
“Ngoja tuone atafanya nini mbele za watu!”
Basi punde Padri Alfonso akawafikia na kutabasamu. Akawasalimu na kuwakaribisha kwa ukarimu.
“Kuna tatizo lolote?” akauliza.
Mama Brian akawahi kutikisa kichwa na kusema, “Hamna!”
“Una uhakika?” Padri Alfonso akauliza.
“Ndio, hamna!” Mama akasihi. “Nashukuru, padri.”
Padri akamtazama na kumuuliza kwa mara nyingine, “Una uhakika?” sasa hivi macho yake alikuwa ameyakodoa. Mama Brian akasihi baridi na moyo wake waenda mbio.
Ghafla Padri akatabasamu na kusema, “Msijali.” kisha akaenda zake.
**