bioto
JF-Expert Member
- Oct 1, 2017
- 1,261
- 2,099
- Thread starter
- #41
MZIMU ULIOREJEA
Sehemu - 55 -
Ilipoishia...
Kwak Martin!
Bila shaka u mzima,nafrah kwa ilo!...
Najua unashangaa juu ya barua hii ya kimaajabu ajabu usishangae kwa ili!
Dhumuni la barua hii ni kikueleza juu ya upatikanaji wa hazina ya marehemu baba yako
#Songa_nayo_sasa....
Mara ya mwisho kaka yako alikwambia urudi kijijini ukujua pa kuanzia!
Nenda katika kijiji chenu mtafute mganga Nwalau Nwalau yule yule unayemjua yupo kijijini kwa dhihara mwambie waitaji utajiri
Kuna masharti atakupa yatakayokufikisha katika hazina ile ya baba yako
Kumbuka hazina ile inalindwa na mizimu kuwa makini katika masharti na ukikosea kidogo kifo ni haki yako
Wengi walioenda hawakurudi
Ila kwa kuwa ni haki yako naimani utashinda...
Kila la kheri
Ni mimi
Zena Kureysh
Martin akashusha pumzi ndefu,akairudia kuisoma ile barua Mara mbili iliandikwa vile vile akaiweka mfukoni
Ni wazi alikuwa amechanganyikiwa
Akaingiza mkono mfukoni na kuitoa
Akapigwa na butwaa,barua aikwepo zaidi ya ile 10000
Macho yakamtoka...
Akuona haja ya kumsimulia mtu
Ni yupi angemuelewa achia mbali kumuamini?!
Akaendelea na kazi raha ikiwa imemtoweka,akipania kesho yake kuelekea kijijini...na ndivyo ilivyokuwa
***********************************
Hali ya kijiji kile ilibadilika,ukame ulitawala,kwa kuwa Martin alikuwa na kiakiba kidogo akachukua chumba katika nyumba vya wageni
Akutaka kwenda nyumbani kwao mwanzo alipania mpaka amalizane na kazi ya kuikomboa hazina ile ndo angerudi kwao...
Kwa kuwa alifika kijijini usiku alipumzika na hasubui alianza kuyatafuta makao ya bibi mganga yule
Kijijini kile kilikuwa ni kidogo akupata tabu kumpata...
"Hahahahaha waitaji utajiri?! Utaweza?!"
"Ndio bibi"
"Hahahaha kuna hazina ipo katika mapango ya maajabu uko milimani ni wajibu wako kuifuata wengi wameenda hawakurudi ni hatari ha ha ha ha "
"Nipo tayari bibi"
Mganga yule akamtumbulia macho Martin,macho ya mshangao
"Ok kama upo tayari ntakuelekeza,hayo mapango ntakupa dawa ukifika hapo utajipaka usoni na mapango Yale yatageuka na kuwa nyumba ya kisasa kuna ulinzi mkali wa mizimu tafuta njia yoyote uingie huko
Mizimu ile inahisia sana unaweza ukaendaaa...."
Mganga yule akamalizia na kumruhusu Martin kutoka kwa kinyume nyume
Martin akawa tayari kwenda katika mapango Yale
Aliyajua fika kwani anakumbuka wakati wakiwa watoto walikuwa wakikatazwa kwenda katika mapango hayo waloyaita 'mapango ya mizimu'
Pia ndiyo yalikuwa mapango yalotambikiwa na waganga na wazee kwa mila zao
Pindi ukienda kwa nia ya kutambika au kuangalia hayakuwa na shida yalikuwa kawaida tu
Ila ukienda kwa nia ya Hazina mizimu ile ilijua na kukugeuza kitoweo
Ni vipi Martin angeweza kuikomboa hazina ya baba yake?!
Akazidi kusonga mpaka katika pori lile,akawa anaelekea maeneo ya mapango Yale.....
NDANI YA MAPANGO
Walinzi wa falme hii kuna binadamu anakuja,kwa ajili ya hazina kuweni makinii,ulinzi uimarishwe
Sauti kubwa ilisikika katika masikio ya walinzi wale wakawa tayari kumkabili kiumbe yoyote ajaye...
Martin akujua juu ya hilo,yeye alizidi kusonga moyoni akiwa na amani
Baada ya kufika katika mapango Yale akaitoa dawa ile na kujipaka usoni akinuidhia maneno machache aloambiwa na mganga na ghafla Mbele yake pakatokea jumba La kifahari
Walinzi wakiwa pembeni yake,walinzi waloshika silaha ambazo akuziona kabla
Wazo kwamba ataingiaje likamvaa
Uwezo wa kuingia kule aukwepo kabisa...
Ghafla akaguswa nyuma alipogeuka tuu
Akaachia yowe,yowe lililowashtua mpaka walinzi wale wa Mbele
martin alikuwa hatarini tena katika mikono hatari ya viumbe vyenye uchu....akabaki akitetemeka akisubiria miujiza
"Wewe ni nani na unataka nini?!"
Akaulizwa swali ambalo katu akuweza kulijibu akikumbuka sharti alilopewa juu ya kutofunguwa mdomo wake
"Na kuuliza wewe ni nani?!"
Akapachikwa swali lingine kabla maumivu makali ayajatambaa katika mwili wake
Ni mkia wa taa alochapwa nao....
"Tuna kuuliza tena wewe ni nani na unataka nini?!"
"Mimi ni Martin na nataka Hazina"
Akavunja masharti pasina mwenyewe kujielewa akaropoka
Viumbe vile vilistaajabu vikamnyanyua mzoba mzoba mpaka ndani kabisa ya jengo lile katika jiko palipokuwa na sufuria kubwa ilochemka mafuta wakamtupa
akaachia mayowe huku akiporomoka kushuka chini ya mafuta Yale Yalochemka
Akiacha juu viumbe vile vikishangilia kwa kupata nyama ya kukaanga
CHINI YA ARDHI
HIMAYA YA WAFU
Ilikuwa ni katika hekalu la kifalme,hekalu lililotengenezwa kwa almasi na dhahabu tu!
Hekalu lililolindwa kwa ulinzi mkali
Ndani ya hekalu lile katika sebule nadhifu aliketi Mzee wa makamo kichwa chake kilijaa mvi...
Pembeni yake aliketi mwanaye aliyekuwa kava joho la kifalme na kakaa katika kiti cha mfalme pembeni yake walikwepo walinzi shupavu wenye silaha za jadi,silaha ambazo katika macho ya kibinadamu azikuleta maana kabisa
Walishika magamba ya konokono,na zaidi ya hapo hata viungo vyao vilikuwa ni silaha tosha
"Baba lazima nirudi duniani nikamchukue mpz wangu baba siwez ishi mwenyewe humu baba"
Jb alipeleka ombi lake kwa baba yake...
Basi usikose sehemu ya 56...
Sehemu - 55 -
Ilipoishia...
Kwak Martin!
Bila shaka u mzima,nafrah kwa ilo!...
Najua unashangaa juu ya barua hii ya kimaajabu ajabu usishangae kwa ili!
Dhumuni la barua hii ni kikueleza juu ya upatikanaji wa hazina ya marehemu baba yako
#Songa_nayo_sasa....
Mara ya mwisho kaka yako alikwambia urudi kijijini ukujua pa kuanzia!
Nenda katika kijiji chenu mtafute mganga Nwalau Nwalau yule yule unayemjua yupo kijijini kwa dhihara mwambie waitaji utajiri
Kuna masharti atakupa yatakayokufikisha katika hazina ile ya baba yako
Kumbuka hazina ile inalindwa na mizimu kuwa makini katika masharti na ukikosea kidogo kifo ni haki yako
Wengi walioenda hawakurudi
Ila kwa kuwa ni haki yako naimani utashinda...
Kila la kheri
Ni mimi
Zena Kureysh
Martin akashusha pumzi ndefu,akairudia kuisoma ile barua Mara mbili iliandikwa vile vile akaiweka mfukoni
Ni wazi alikuwa amechanganyikiwa
Akaingiza mkono mfukoni na kuitoa
Akapigwa na butwaa,barua aikwepo zaidi ya ile 10000
Macho yakamtoka...
Akuona haja ya kumsimulia mtu
Ni yupi angemuelewa achia mbali kumuamini?!
Akaendelea na kazi raha ikiwa imemtoweka,akipania kesho yake kuelekea kijijini...na ndivyo ilivyokuwa
***********************************
Hali ya kijiji kile ilibadilika,ukame ulitawala,kwa kuwa Martin alikuwa na kiakiba kidogo akachukua chumba katika nyumba vya wageni
Akutaka kwenda nyumbani kwao mwanzo alipania mpaka amalizane na kazi ya kuikomboa hazina ile ndo angerudi kwao...
Kwa kuwa alifika kijijini usiku alipumzika na hasubui alianza kuyatafuta makao ya bibi mganga yule
Kijijini kile kilikuwa ni kidogo akupata tabu kumpata...
"Hahahahaha waitaji utajiri?! Utaweza?!"
"Ndio bibi"
"Hahahaha kuna hazina ipo katika mapango ya maajabu uko milimani ni wajibu wako kuifuata wengi wameenda hawakurudi ni hatari ha ha ha ha "
"Nipo tayari bibi"
Mganga yule akamtumbulia macho Martin,macho ya mshangao
"Ok kama upo tayari ntakuelekeza,hayo mapango ntakupa dawa ukifika hapo utajipaka usoni na mapango Yale yatageuka na kuwa nyumba ya kisasa kuna ulinzi mkali wa mizimu tafuta njia yoyote uingie huko
Mizimu ile inahisia sana unaweza ukaendaaa...."
Mganga yule akamalizia na kumruhusu Martin kutoka kwa kinyume nyume
Martin akawa tayari kwenda katika mapango Yale
Aliyajua fika kwani anakumbuka wakati wakiwa watoto walikuwa wakikatazwa kwenda katika mapango hayo waloyaita 'mapango ya mizimu'
Pia ndiyo yalikuwa mapango yalotambikiwa na waganga na wazee kwa mila zao
Pindi ukienda kwa nia ya kutambika au kuangalia hayakuwa na shida yalikuwa kawaida tu
Ila ukienda kwa nia ya Hazina mizimu ile ilijua na kukugeuza kitoweo
Ni vipi Martin angeweza kuikomboa hazina ya baba yake?!
Akazidi kusonga mpaka katika pori lile,akawa anaelekea maeneo ya mapango Yale.....
NDANI YA MAPANGO
Walinzi wa falme hii kuna binadamu anakuja,kwa ajili ya hazina kuweni makinii,ulinzi uimarishwe
Sauti kubwa ilisikika katika masikio ya walinzi wale wakawa tayari kumkabili kiumbe yoyote ajaye...
Martin akujua juu ya hilo,yeye alizidi kusonga moyoni akiwa na amani
Baada ya kufika katika mapango Yale akaitoa dawa ile na kujipaka usoni akinuidhia maneno machache aloambiwa na mganga na ghafla Mbele yake pakatokea jumba La kifahari
Walinzi wakiwa pembeni yake,walinzi waloshika silaha ambazo akuziona kabla
Wazo kwamba ataingiaje likamvaa
Uwezo wa kuingia kule aukwepo kabisa...
Ghafla akaguswa nyuma alipogeuka tuu
Akaachia yowe,yowe lililowashtua mpaka walinzi wale wa Mbele
martin alikuwa hatarini tena katika mikono hatari ya viumbe vyenye uchu....akabaki akitetemeka akisubiria miujiza
"Wewe ni nani na unataka nini?!"
Akaulizwa swali ambalo katu akuweza kulijibu akikumbuka sharti alilopewa juu ya kutofunguwa mdomo wake
"Na kuuliza wewe ni nani?!"
Akapachikwa swali lingine kabla maumivu makali ayajatambaa katika mwili wake
Ni mkia wa taa alochapwa nao....
"Tuna kuuliza tena wewe ni nani na unataka nini?!"
"Mimi ni Martin na nataka Hazina"
Akavunja masharti pasina mwenyewe kujielewa akaropoka
Viumbe vile vilistaajabu vikamnyanyua mzoba mzoba mpaka ndani kabisa ya jengo lile katika jiko palipokuwa na sufuria kubwa ilochemka mafuta wakamtupa
akaachia mayowe huku akiporomoka kushuka chini ya mafuta Yale Yalochemka
Akiacha juu viumbe vile vikishangilia kwa kupata nyama ya kukaanga
CHINI YA ARDHI
HIMAYA YA WAFU
Ilikuwa ni katika hekalu la kifalme,hekalu lililotengenezwa kwa almasi na dhahabu tu!
Hekalu lililolindwa kwa ulinzi mkali
Ndani ya hekalu lile katika sebule nadhifu aliketi Mzee wa makamo kichwa chake kilijaa mvi...
Pembeni yake aliketi mwanaye aliyekuwa kava joho la kifalme na kakaa katika kiti cha mfalme pembeni yake walikwepo walinzi shupavu wenye silaha za jadi,silaha ambazo katika macho ya kibinadamu azikuleta maana kabisa
Walishika magamba ya konokono,na zaidi ya hapo hata viungo vyao vilikuwa ni silaha tosha
"Baba lazima nirudi duniani nikamchukue mpz wangu baba siwez ishi mwenyewe humu baba"
Jb alipeleka ombi lake kwa baba yake...
Basi usikose sehemu ya 56...