Simulizi: Mzimu uliorejea

Simulizi: Mzimu uliorejea

MZIMU ULIOREJEA

Sehemu -27-

Ilipoishia...
"haaaa! haaaaaa! haaaaa."
likaachia cheko,meno yalooza yakaonekana
Mkononi alishika bisu
akawa anamsogelea yule dada!
"mamaaaa!"
dada yule akaachia kilio
"Grooooh!"
jitu likaachia mlio kama wa simba.

Endelea...
mikono ilikuwa imekishikilia kisu,na kukishusha katika shingo ya binti yule bila huruma, jitu lilidhamiria kuua.
mwili wa binti yule mery ulokuwa ukiangalia kwa jeuri na nyodo dakika kadhaa zilizopita! ulitapa tapa na kutulia tuli!
ukitoa macho ya mshangao.
jitu likaachia cheko lingine na kutoweka!
Naima mfanyakazi wa ndani katika nyumba aloishi Martin na mke wake,
baada ya kuambiwa na bosi wake mery atoke pale sebleni akiwa katika chumba chake,
kalala kitandani,
ghafla akashtuliwa na yowe!,
yowe kama la simba,
ndiyo!,
yowe la jitu.
wakati hakiwa katika mshangao ule ghafla akaskia yowe lingine,
yowe la maumivu!
hakutaka kusubiri tena akajinyanyua kitandani pale na kutoka mbiyo,
mara akateleza chini!
maumivu yaka ambaa katika mwili wake kwa wakati ule akuyasikia.
akajinyanyua na kuufata mlango!
akaufungua na kukutana na korido pana!, korido ilounganisha vyumba na sebule, akupunguza mwendo ila alikuja kupiga breki sebuleni pale!
macho yake yalishindwa kustahimili kuitazama sura ya dada yake!
ilotazama kwa uchungu mkubwa!,
yowe likamtoka Naima huku akiendelea kukitazama kisu kikiwa shingoni kwa bosi wake kimelitawanya koromeo.
nguvu zilimuisha nuru katika macho yake ikatoweka,giza likatawala!, akadondoka chini na fahamu zikamtoka!

*************************************

MARTIN alishuka kwenye gari yake, moyoni alikuwa na furaha sana!, alijua siku hiyo ndo mwisho wa maisha ya afisa upelelezi yule, mwenye kibri!, jeuri na anayejifanya anajua!
'tumepoteza wangapi bwana sembuse huyu mmoja?!' martin akaendelea kuwaza huku akiushika mlango na Kuufungua!....
ghafla mshtuko ukamvaa macho yakamtoka!, ni baada ya kuuona mwili wa mfanyakazi wake Naima!,
alipoufikia ule mwili akapatwa na mshtuko mwingine baada ya kuuona mwili wa mke wake!
tena ukiwa na kisu katika shingo yake, kisu kile kile,
kama wao walichokitumia,
ujasiri ukamuisha woga ukamtawala!, machozi yalimdondoka kama mvua!
huku akiwa kachanganyikiwa akatoa simu yake na kumpigia kamishna, na kumueleza kuwa nyumbani kwake kuna matatizo!
mkewe kachomwa kisu,
kamishna alichanganyikiwa!, japo akuambiwa kuwa mwanaye kafariki, lakini hakuwa na shaka juu ya hilo!, bila shaka kisasi sasa kilimgusa hadi yeye!,
akampigia simu MAIMUNA na kumuagiza awaite jb na Nurdini!
ni wazi habari ile ilimchanganya!
dakika kadhaa vijana wale walikuwa mbele yake!,
Kamishna akuongea kitu zaidi ya kulia,
Jb na Nurdin walibaki wakimtazama kwa mshangao
"mauaji yanaendelea! na roho inaniuma sana, badala nyinyi visobwengo mumtafute muuaji mnataka mpeleleze kesi za nyuma huku muuaji akiendelea kutamba mtahani!, sasa ameingilia mpaka familia yangu!, mwanangu MERY hayupo tena duniani"
kamishna aliongea kwa uchungu!,
vijana wale wakashtuka,
ila uso wa jb ukawa wa kawaida,
tena wenye dharau ndani yake!
"kafa katika mazingira gani mheshimiwa?"
Nurdin akaoji!
"vile vile kwa kuchomwa kwa kisu?!,"
"mwanao si ndo kaolewa na martin?!"
jb akaoji! kamishna akamkata jicho la ukali ila nurdin akatingisha kichwa kuafiki!
jb akaendelea "ndo mahana mimi nilipendekeza martin aojiwe na file lake lifunguliwe nikapuuzwa kumbe mlikuwa mnajuana? sasa yamegeuka na bado"
"unasema nin wewe?"
kamishna akaoji kwa ukali hakiwa tayari kumvaa tena jb!
jb akaachia cheko lake la dharau!
"umesahau nlchokufanya etiee nkwambie tu ukwel utajulikana.,"
"Ukweli gani?!"
"Utakapojulikana ndo utautambua"
"Acheni mabishano wakuu twendeni eneo la tukio
Dakika chache baadaye walikuwa eneo lile,wakiwa Mbele ya mwili wa mwanamke yule
Nurdin akiuangalia kwa huruma
" kweli kuna haja ya martin kulazimishwa kumtaja muhusika lazima atakuwa anamjua tu"
Nurdin alinong'ona,maskin laiti kama angejua MARTIN aelewi chochote
Ni kweli hakumtambua muuaji!
Ingawa alielewa ni lazima atakuwa kibaraka,au ndugu wa jb
Ni yupi sasa ambaye kaingilia mpaka familia yake?!
Alikosa jibu,jibu lilikuwa kwa naima aliyekuwa bado kapoteza fahamu
Ndiyo ambaye alitegemewa kuwafungua macho maaskari wale
Je nini kitaendelea
Naima atazinduka?!,

ITAENDELEA...
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu-28-

Ilipoishia...
"kweli kuna haja ya Martin kulazimishwa kumtaja muhusika lazima atakuwa anamjua tu"
Nurdin alinong'ona,maskini laiti kama angejua Martin aelewi chochote
ni kweli hakumtambua muuaji!
ingawa alielewa ni lazima atakuwa kibaraka,au ndugu wa jb
Ni yupi sasa ambaye kaingilia mpaka familia yake?!
Mwenye uwezo wa kuingia katika jumba lake lenye ulinzi mkali pasina walinzi kuhisi chochote?!
alikosa jibu,jibu lilikuwa kwa Naima
aliyekuwa bado kapoteza fahamu!
ndiye ambaye alitegemewa kuwafumbua macho maaskar wale...
Habari zile za kifo cha Mery,zilisambaa kama kuungua kwa makuti,au nyumba ya nyasi
'Mtoto wa kamishna naye atembelewa na bisu la koromeo'
Ni moja wapo ya gazeti la ukweli na uwazi ambalo mmiliki wa gazeti hilo bi sharfia aliandaa makala ilistaajabisha...
Mmiliki huyo ambaye akubainisha jina lake alianzia mbali!
Ni kama aliwafumbua watu macho!

MIAKA MICHACHE NYUMA

SHARFIA miaka ya nyuma alikuwa ni mfanyakazi katika kampuni ilomilikiwa na jb pamoja na martin alikuwa kama katibu muhtasari katika ofisi ile
Mbali na kazi hiyo pia alikuwa ni mwandishi mpelelezi wa kujitegemea alotafuta habari na kuzisambaza katika magazeti mbalimbali na kulipwa kwa habari ile chini akijiandika kwa jina la muhariri xy
Ni jina lililotambuliwa nchi nzima pasina kutambuliwa mmiliki wake!
Alifichua maovu mbalimbali!
Ndo yeye alotegesha kamera katika ofisi za bosi wake wale kuchunguza kila ambacho kinaendelea
Na habari ambayo aliona inafaa kuwa habari aliivujisha.
Mpaka jb alipokuja kufa na Martin kubadilisha wafanyakazi wake
Sharfia alipochukua hela yake ndipo alipofungua gazeti lile ambalo kutokana na habari zake hasa za mauaji Yale tata lilijipatia umaharufu mkubwa sana
Leo hii aliandaa makala akiilaumu serikali kwa kutokufuata kwa umakini mauaji Yale
Alianzia mbali miaka mitatu nyuma alipokufa tajiri mkubwa,mmiliki wa mahoteli na kampuni kubwa ya madini jb,mwili wake ulikutwa ukiwa umetelekezwa huku ukiwa umechomwa kisu cha koromeo
Kesi ile aikujulikana iliishia wapi!!!
Miaka ikasonga mpaka baadaye walipokufa walinzi wawili kwa style ile ile ya kuchomwa visu vya aina ile ile
Bado serikali na jeshi lake LA polisi limekaa kimya
Mauaji hayakuishia hapo mwanasheria wa kampuni ile ya madini naye alikufa kwa kifo hicho hicho!
Na Leo mke wa mmiliki wa kampuni hiyo na mtoto wa kamishna mkuu wa jeshi la polisi naye hatupo naye
Aina ya kifo ni kile lile!!!....
Je serikali imeshindwa kumtambua muuaji?!
Mwisho muandishi alimaliza kwa swali!
Pia aliambatanisha kwa picha,picha ambazo alizipata kwa shida akipambana na insp Nurdin
(Rejea matoleo ya awali)
***
Gazeti lile lilikuwa katika mkono wake!,kichwa kilimuuma insp yule
Aliyarudia Mara kadhaa makala Yale,pembeni katika ofisi ile aliketi jb,mkononi akiwa na gazeti kama lile lile
"Wananchi watatuelewaje sisi?!,sasa mpaka mwandishi anaweza kuchambua tukio hili kwa kina namna hii sisi tupo tu igp akituuliza tutamjibu nini?!,nilisema na ntazidi kusema wahusika wa mambo haya ni Martin na mwenzake kamishna kubali ukatae kwa nini kamishna ataki tumuweke nguvuni huyo mkwe wake!?"
"Jibu unalo jb kamishna alikuwa hataki kwa kuwa kamuozesha binti yake kwake so tungemuweka nguvuni lazima mwanaye angeteseka"
"Swadakta kitendo cha kuficha maovu mtoto wake atunaye tena je ataendelea kukataa tumtie nguvuni martin?!"
"Akatae Mara ngapi?!,kamishna kasema haiwezekani jb ausike na mauaji ya mwanaye tumsake muuaji na si kumbughudhi mfiwa"
"Mh makubwa mna maajabu binadamu nyinyi"
Jb akaongea kwa sauti ndogo, sauti ya kunong'ona
***********
Baada ya mazishi kukamilika,mazishi yaloudhuriwa na mamia ya watu
Kikawekwa kikao
Ni kikao cha watu watatu
Kikao cha siri sana...
Alikwepo komandoo chake!,huyu ni komandoo alotoka katika nchi ya KINTE nadhani mna ifahamu kazi yake katika riwaya ya mfungwa,mtetezi kutoka kinte na ntakuua kwa mkono wangu chaka
Pembeni ya komandoo huyo aliketi kamishna na pembeni ya kamishna aliketi Martin
Nyuso zao zilitawala majonzi na uzuni ilokithiri
Martin akafungua kikao
"Siku mbili zilizopita tumemzika mke wangu kipenzi na mtoto wa huyu aliyoko pembeni yangu kamishna,kifo chake tata,tulikuwa tukimtegemea mfanyakazi wangu naima aloshugudia muuaji kwa bahati mbaya alidondoka na kudondokea kisogo ubongo ukatingishika na kupelekea kupoteza fahamu,fahamu ziliporejea hakuwa na kumbukumbu tena.
Muuaji mpaka sasa ajatambulika hata kumhisi mtu tu ingawa anaacha visu na amna shaka anatumia gloves kwa kuwa katika visu vyote hakuna alama za vidole
Namba moja lazima umtie huyu nguvuni.
Kazi namba mbili,kuna huyu mwandishi wa habari lazima afe!,anatupeleleza sana na kutuwekea kashfa kwa wananchi anaitwa xy saivi anafanyia kazi katika gazeti la ukweli
Na uwazi mchunguze umjue ni nani
Na kazi ya mwisho kuna huyu kisobwengo kutoka makao makuu kaja kwa kazi hii ya kumtambua muuaji sasa badala amsake muuaji anatqka Mimi niojiwe kuhusu muuaji huyo eti ni namjua na ukweli mi simjui"
"Heee kivipi?!"
Ikabidi martin amwelezee komandoo chaka mwanzo mpaka mwisho toka urafiki wake na jb alipokuja kushauriwa na mpz wake amwangamize jb Mali zote ziwe chini yake akatwii na kumuua jb,jinsi nurdin alivyofatilia kesi ile na kumtambua muuaji kamishna akalifunga faili lile miaka mitatu Mbele mauaji Yale yakarejea mpaka pale walipo"
Komandoo chaka akashusha pumzi
"Ni haki yao kukuhisi kuwa unamjua muuaji kwa kuwa wanaokufa wapo chini yako!,na pengine huyo jamaa anajua labda wewe ndo muuaji!"
Chaka kwa sauti ya upole akazungumza
"Na ndo mahana twaitaji afe ili asifikishe habari makao makuu"
Kamishna akachangia
"Wazo zuri ilo limepita Mimi na jeshi langu tutaifanya kazi,hizo kazi mbili ya huyo mwandishi na huyo mpelelezi wenu ni rahisi ntazifanya ila sasa kazi ngumu ni hii ya Tatu ya huyu anayeua kwa kuwacha kisu katika makoromeo,nnaswali kwako martin una uhakika jb alikufa?!"
"Na uhakika?! Na alomuuwa ni kijana wangu kwa kumchoma kisu cha koromeo"
Komandoo chaka akaachia kicheko hafifu
"Unasema ajawahi kuwa na ndugu wala marafiki kukuzidi wewe ambaye pengine unahisi ndo mlipizi?!"
"Kwa kweli ni mewaza sana juu ya ilo ila Mimi ndo nlikuwa rafiki yake mkubwa hakuwa na ndugu, marafiki aliwapata baada ya kutajirika ila rafiki yake mkubwa alikuwa ni Mimi"
"Jb ajafa"
Chaka akaongea kwa kujiamini , wote wakatoa macho kwa mshangao
"Nini?!!!" Wakaoji kwa pamoja
"Nasema jb ajafa yupo mzima na ili muakikishe hili naitaji tukalifukue kaburi lake tupime vinasaba je yule alozikwa ni jb kweli?!...
Pili nahisi kuna mchezo katikati pengine huo ni MZIMU ULOREJEA kuja kulipiza na kama ndo hivyo pindi tukifukua lile kaburi lazima kuna maajabu yatatokea na ikiwa ndo hivyo mko hatarini tena sana ndugu zanguni"
Kwa Mara ya kwanza watu wale wakafunuliwa vichwa vyao,miili ikapata joto
Meno yakagongana mtaalamu chaka akaendelea
"Usiku wa Leo tutaenda makaburini na ili msi dhurike ikiwa tunapambana na mzimu kuna dawa ntawapa mtaiweka mfukoni,msijali kazi imeisha!!!!

MAMBO HAYOOOOOO
KOMANDOO CHAKA KAZINI
AANZA KWA MAFANIKIO MAKUBWA
SASA JE ATAWEZA PAMBANA NA JB KUWANUSURU MARTIN NA KAMISHNA
MWANDISHI WA HABARI SHARFIA JE
JB MPELELEZI JE?!
ITAENDELEA
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu-29&30-

Ilipoishia
Usiku wa leo tutaenda makaburini na ili msidhurike ikiwa tunapambana na mzimu kuna dawa ntawapa mtaiweka mfukoni msijal kazi imeisha!!!!

Endelea...
Martin na Kamishna wakatoa macho kwa mshangao
"Duu!,kwa hiyo komandoo Chaka kwenye mambo yetu ya asili umepitia pitia?!"
Komandoo akacheka kidogo,
"Hamna ndugu zanguni! Ni dawa nloipata nikiwa mafunzoni"
Chaka akajitetea....

*************************************

Giza lilitawala na kuchukua Nuru yote,Nuru iliyoachwa ni nyota chache zilizopendezesha anga lile Na kuonesha utukufu wa MUNGU,hali ya umanyunyu manyunyu iliongeza kasi ya baridi na kuwalazimu wakazi kujistiri kwa makoti na masweta!
Wengi walotembea mtaani katika usiku ule mkononi walishika miamvuli kujikinga na vimanyunyu manyunyu vile...
Katika nyumba moja ya kifahari!,ndani waliketi watu wa Tatu
Ni nyumba alokabidhiwa komandoo chaka,baada ya kutoka nchini kwake KINTE na kuja Tanzania kwa kazi maalumu
"Ule muda wa kuutambua ukweli umewadia,ukweli ambao utaniwezesha Mimi kufanya kazi kwa ufanisi"
Baada ya kuongea maneno Yale Chaka akajinyanyua na kulifata kabati lake akalifungua na kutoka na vimifupa vitatu
Kamfupa kamoja akakiweka ndani ya mfuko wa suruali yake
"Huu ni mfupa wa ngurue nadhani hakuna mtu asiyemjua huyu mnyama,mifupa yake aipatani na viumbe wote wabaya majini,mashetan
i,mizimu,wachawi,mapepo na viuchafu uchafu vyote kila mmoja aweke katika mfuko wake ndo kinga yake"
Wote walistaajabu!,walijua juu ya uhodari wa mifupa ile ila hakuna alohisi kama ndo Chaka aliimahanisha pindi aliposema kuna kinga atawapa
Kila mmoja akachukua mfupa wake na kuuweka ndani ya mfuko wake wa suruali
Wakatoka,na kuingia ndani ya gari,kabla Chaka ajaliondoa gari lile akakumbuka kitu na kurudi ndani.
Alipotoka alikuwa na sururu moja na chepe akaviingiza ndani ya buti la gari
"Tulitaka kusahau vitendea kazi sijui tungefukua na kucha?!"
"Kwa wewe komandoo kwani depot ukufundishwa kuchimba shimo kwa kucha?!"
Chaka akaachia kicheko hafifu!
"No!,Mimi nilikuwa mwanafunz mtiifu!,hizo ni adhabu kaka!,ila kwa kutumia vijiti tumechimba sana tena mashimo makubwa makubwa msinikumbushe jamaniii!"
Waliendelea na maongezi huku mvua sasa ikiwa inanyesha na radi likipiga
Ilo awakujali!!
Ilikuwa lazima wakafukue kaburi lile,na kuchukua sample ya mabaki ya mwili ule kwa ajili ya upelelezi....

***********************************

Mvua ile ilimnyeshea kijana mdogo,usingizi ulimpaa,alikubali kunyeshewa angejistiri wapi na apakuwa na pakujistiri?!
Hapakuwa na nyumba!,eneo lile la makaburini alikubali kunyeshewa na mvua!
Ndo msukumo wa ajira yake!
Kipele ndo jina lake
Mlinzi wa makaburi Yale ya njoro!
Akiwa amejikunyata kwa mateso ya kunyeshewa na mvua pamoja na baridi Kali ndani ya uzio wa makaburini Yale katika usiku ule
Ghafla akashtuliwa na mngurumo wa gari, akatamani kwenda kuchungulia nje ila uvivu na woga ukamlisha pale pale
Nywele zilimsosimka,mapigo ya moyo yalimwenda mbio
Ghafla honi za gari zikasikika nje ya lango la uzio wa makaburi Yale
Kipele hakuwaza Mara mbili akakurupuka kwelekea nje ya lango lile
Akalisogelea lile gari,huku manyunyu ya mvua yakilipiga koti lake
"Sisi ni maafisa wa jeshi la polisi huyu kwa jina anaitwa kamishna Haruna,anayefuata anaitwa Martin na Mimi ni komandoo Chaka!"
Mlinzi kipele akashtuka,wote aliwafahamu kupitia katika vyombo vya habari,walikuwa ni watu maharufu kitaifa
Taifa lilimtambua Chaka na dunia kwa pamoja,pia kamishna wa mkoa hakuna ambaye akujua uchapaji kazi wake na wa mwisho ni tajiri Martin
Kwa mkoa wa Kilimanjaro ndo alioongoza kwa utajiri na kwa taifa akukosekana katika tatu bora
Kwahiyo wote walikuwa ni watu wa zito,ni lazima kipele angeshangaa
Na kweli alibaki kuduwaa pasina kuamini akionacho
Kichwani aliwaza mengi , yalomstaajabisha hasa ujio wa watu wale wazito
Ghafla akatabasamu!,
mawazo yakampeleka tayari ni miongoni mwa matajiri wakubwa anamiliki nyumba za ghorofa na magari ya kutembelea
Wengi wa mabosi waloenda pale makaburini usiku walimlipa kiasi cha hela naye aliwaruhus
e yao ktk makaburi Yale
Leo watu wale alijua ni dili ambalo angeingiza ela ya maana
"Miaka kama mitatu nyuma rafiki yake kipenzi na huyu maharufu kama jb alikufa na tukaja kumzikia huku,kifo chake kilikuwa ni cha utata,na upelelezi wake unaendelea hadi Leo hii! Jana tulipata taharifa kuwa jb yupo hai nchini marekani anakula bata,kwa ufupi kijana huyo jb alikuwa ni fisadi anaeuza madini nje ya nchi na huo mwaka juzi aliibia taifa bilioni 500 akatoroka,ila tukaja kupata taharifa kuwa kauwawa na majambazi tulipopata habari tukaona tuje muda huu kufukua kaburi lake na kuchukua sample kupeleka mahabara ili kujua ni yeye au sie?!"
Ilikuwa ni uongo mkamilifu,kipele akawa hana jinsi zaidi ya kuwakubalia huku wazo lake la utajiri likiyeyuka taratibu
Watu wale wakashuka,wakafungua buti na kutoka na sururu na machepe
Wakaelekea mpaka katikati ya makaburi Yale
Mbele yao kulikuwa na kaburi ambalo juu kulikuwa na kibao kilichoandikwa Jacob Boniphase,tarehe alozaliwa na siku alikufa
"Lete Mimi niwafungulie"
Kamishna akasema akatupiwa sururu ile akapaka mkono mate kidogo na kuinyanyua juu akaishusha katika ukuta ulojengewa kaburi lile
Akatoka na mapande ya mawe akaendelea hivyo hivyo
Ghafla radi kubwa likapiga lililopelekea wote walale chini
Ghafla jb akatokea hatua chache kutoka pale walipo
Macho yake yaling'aa kama ya paka,alikuwa kavaa sanda ilooza na kutembelewa na mafinyofinyo,mwili wake ikiwemo uso ulimomonyoka na kumuongezea taswira ya kutisha
Kichwani hakuwa na nywele hata moja,mkononi alishika fimbo mkia wa tai
Aliwaangalia kwa dharau!
'Mmejileta wenyewe'
Jitu lile likawaza na kupotea
Likatokea pembeni zaidi ya walipo!
Akainyanyua ile fimbo juu lengo aishushe kichwani kwa kamishna alokuwa akilivunja kaburi lake
Ghafla....
Ghafla nini?!!!
Nini kiliendelea?!
Je watafanikiwa kulivunja kaburi lile?!

#Tuendelee_na_sehemu_ya_30

#No_30
Ilipoishia...
Jitu lile likainyanyua ile fimbo juu lengo aishushe kichwani kwa kamishna alokuwa akilivunja kaburi lake
yalokuwa makazi yake
ghafla,...
endelea
Nywele zikamsisimka,mapigo ya moyo yakaongeza kasi ya upigaji
Alishatambua ni nini kiliendelea
Kupitia kipawa na uwezo alokuwa nao,akahairisha zoezi lile
Akatoweka na kutokea pale pa awali
Bado nywele ziliendelea kusisimka vile vile,akaunyanyua mkono wake na kupiga shoti kaburi lile!
Baada ya kitendo kile akaachia kicheko
Kicheko ambacho hakikusikiwa na yoyote kati ya vijana wale

************************************

Kamishna aliendelea na uvunjaji wa kaburi lile pasina kuhisi uwepo wa kiumbe cha ajabu nyuma yake
Alipochoka komandoo Chaka alimpokea na kuendelea
Wote hawakuuhisi ujio wa jb mpaka alipotoweka
Wakafanikiwa kulivunja vunja na kulitoa jeneza lililooza na kuliwa na mchwa
Wakalifungua ndani walikuta mifupa ikiwemo fuvu la kichwa
Wakachukua sample walizokuwa wanaitaji na kulifukia
"Mpaka sasa hatupambani na mzimu laiti kama ingekuwa hivyo angeshatutokea,pili hii fuvu na hii mifupa,mifupa tusingeikuta"
Akaongea Chaka kwa sauti ndogo
"Ngoja tukapime hizi sample ndo tutajua je ni kweli yeye ndo alizikwa?!,na kama siye lazima kuna mtu wake wa karibu anayefanya haya!"
"Ndo nisimjue?!"
Martin akauliza kwa mshangao
"Inategemea!,pengine miaka yote yeye hakuwa nchini na pengine aliposikia ndugu/rafiki yake kafa kwa kuuwawa na kesi yake kutopata suluhu ndo akarejea uwez jua"
Martin akashusha pumzi ndefu!!!
Alichoka kimawazo mpaka kimwili

************************************

Usiku ule ule
Sharfia alitoka bafuni kuoga,akajifuta maji taratibu na kujisogeza katika dressing table yake
Akavua nguo na kubaki kama alivyozaliwa,umbo lake zuri likionekana wazi bila kificho chochote
Akajipaka mafuta kidogo mkononi na kujipaka katika mwili wake laini!
Akainama tena kidogo kuchukua mafuta na kuengelea kujipaka katika mwili wake
Ghafla akaskia upepo ukivuma eneo lile
Upepo kama wa feni
Wakati akiendelea kustaajabu hali ile ghafla akahisi nyuma yake kuna mtu
Kwa haraka akatupa jicho lake katika kipo chake lile
Macho yakamtoka Pima
Akataka kuachia yowe sauti ikakataa kutoka
Akageuka nyuma ghafla
Patupu!!!
Huku akiwa anahema akaenda kukaa kitandani!
Tayari jb alikuwa eneo lile
Na nje ya nyumba ile watu 3 wenye silaha za kivita zilizofungwa viwambo vya kuzuia sauti walikuwa wakiingia kupitia katika ukuta mkubwa wa nyumba ile...
Ni vijana walopewa kazi na chaka,kumchakaza mwandishi yule wa habari
Wakati sharfia akiendelea kutetemeks kitandani pale,ghafla akahisi vishindo nje ya nyumba yake
Kutokana na mauza uza yaliyomtokea sekunde kadhaa mule ndani,halihisi pengine vishindo vile vilikuwa ni mojawapo ya uchawi akakomaa kuomba dua.
Dua iliyomuweka mbali mzimu yule
Ghafla wazo likamjia baada ya kuskia hatua kama za watu
Wazo la kwenda kuchungulia nje kupitia dirisha lile
Akajinyanyua na kulisogelea dirisha akalifunua kidogo na kuchungulia
Almanusura azirahi,wazo lililopenya katika kichwa chake haraka haraka ni kuchukua simu yake na kutafuta namba za insp NURDIN
Ins ambaye kwa muda huo walikuwa na uhasama kutokana na binti yule kuendelea kuripoti habari zile...
'Nimevamiwa na majambazi ins plz njoo niokoe block b,mtaa wa sirin nyumba namba 5'
Muda ule insp Nurdin alikuwa kituoni baada ya kuambiwa vile huku akiwa amechanganyikiwa akampigia simu insp jb ambaye kwa muda ule mzimu ule wenye uwezo wa kutumia nafsi tofauti tofauti kwenye mazingira usiku alikuwa nyumbani kwa binti mrembo Maimuna ( secretary,) wa kamishna
Wakati akiwa pembeni ya binti yule baada ya kumaliza kumshughulikia ghafla akashtuliwa na mvurumisho wa simu yake ya mkono
Akaichukua na kuipeleka skioni
'Block b mtaa wa sirin nyumba namba 5'
Simu ile ikakatwa
"Vaa nguo tuondoke"
jb akamuamrusha binti yule
"Kuna nini tena mpz"
"Nimekwambia vaa!"
Wakati jb aliongea vile tayari alikuwa kashavaa akiweka kola ya shati lake vizuri,akaweka tintedy juu kidogo ya macho yake
"Tunaenda au?!"
"Aku! Mi umeshanchosha hata kushika hiyo silaha siwezi"
Akaongea binti yule kwa sauti ilojaa wingi wa mahaba
Jb akamvamia na kumpiga nusu
Huku akiwa na haraka akatoka baada ya sek kadhaa muungurumo wa gari ukasikika ukitoka eneo lile
Ilikuwa saa nne usiku

************************************

Wakati akiendelea kutetemeka,ghafla akasikia tena upepo ule wa kimaajabu!
Ghafla akahisi tena kama kuna mtu nyuma yake
Ile anageuka akapigwa Kofi lililomfanya apepesuke na kutaka kudondoka
Ila akastaajabu zaidi baada ya kuzuiwa na kitu asichokiona!
Jb alimzuia kwa nyuma na ghafla akatoweka na kumvaa binti yule
Ghafla Sharfia akajihisi kujiamini kupitia kiasi,akiwa na hasira ghadhabu na chuki
"Vaa nguo zako"
Akanong'onezwa na sauti aliyoitambua fika
Sauti ya bosi wake wa zamani jb,akabaki ameduwaaa
"Vaaaa nguo zakooooooo"
Sauti ile ikamkemea,ghafla sharfia akazivamia nguo zake na kuanza kuzivaa haraka haraka,moyo ukiwa mgumu wenye hasira na kujiamini kila dakika ilopotea
"Kaa pembeni ya mlango!"
akaitiii sauti ile,na kuusogelea mlango ule
Moyoni alijishangaa kutokuwa na uwoga ata!!!
Majambazi wale wakaufungua mlango kwa kutumia funguo Malaya walizo kuwa nazo
Wakwanza kuingia akaanza kukimwagia kitanda risasi,alishtushwa akipaishwa kwa teke na binti yule risasi ikamtoka mkononi
Wale wawili walobakia wakamuelekezea binti yule bastola zao
"Nyoosha mikono juu"
Wakatoa amri!
Sharfia akatoa kicheko
Kicheko cha kejeli
"Nyinyi mmeambiwa na bosi wenu CHAKA mnichakaze na si kuniweka chini ya ulinzi"
"Haaaa!!!"
Watu wale wakaduwaaa
Kosa!!!
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu -31 & 32

Ilipoishia...
Nyiny mmeambiwa na bosi wenu CHAKA mnichakaze na si kuniweka chini ya ulinzi
"haaaa!!!"
watu wale wakaduwaa
kosa!!!

Endelea...
SHARFIA alijirusha mzima mzima kwa mateke aina ya tik tak,risasi zile zikiwaponyoka,majambazi wale
Huku wakiwa bado wamepigwa na butwaa kwa kutotegemea Yale yalotokea,
baadhi wakiachia matusi ya nguoni na kujaribu kuziangalia silaha zao zilipodondokea
Sharfia akautumia mwanya huo kuwarukia mateke mawili ya 'double'
Yakawapeleka vijana wale wawili chini,
Wakawa wana gaa gaa kwa maumivu makali,sharfia akakaa kimapigano akimwangalia yule jamaa alobakia
Jamaa Yule akawa amenata kwa sekunde kadhaa na kumfata binti yule kwa spidi,
lakin sharfia alishamwona,jamaa Yule alipomfikia akaruka teke,sharfia akabonyea kidogo chini teke lile likapiga hewa,kijana yule akakosa mhimili kwa ghafla sharfia akampiga mtama,kijana yule akasambaratika chini...
Vijana wote wa Tatu wakawa chini wakigaagaa chini kwa maumivu makali
"Pindi mpewapo kazi ni lazima mjue mnakuja kupambana na mtu wa namna gani,siyo kwa kuwa mmesikia ela mnakubali kiraisi rahisi....
Wakati binti yule akiendelea kuongea ghafla simu ya mmoja wa majambazi wale ikaita ile yule jamaa anataka kuipokea sharfia akaruka hatua moja na kumfikia akamkanyaga mguu
Maumivu aloyapata kijana yule,akaachia yowe,sharfia akamsachi na kuitoa simu ile
'Bosi'
Ndo jina lililosomeka kwenye 'screen' ya simu ile
Binti yule akabonyeza OK sambamba na kuweka loud spika
"nipe ripoti mmefikia wapi?!"
Upande wa pili ukaoji
Sharfia akaachia kicheko hafifu,kicheko cha kejeli...
"Vijakazi wako wapo chini ya ulinzi wangu, ndo nawaza niwauwe au niwasamehe,tatizo awapo katika list yangu,hata nawe chaka achana na Mimi kusalimisha uhai wako ukiendelea?!!!! Tusilaumiane mi si laval zenu nyinyi mfyuuuuuuu"
Akasunya na kukata simu,vijana wale miili yao ilitetemeka,walihisi kuvuliwa nguo na kuachwa uchi,walikuwa ni majambazi walokomaa waloliasi jeshi Leo mtoto wa kike atape Mbele ya macho yao!
Hapana
Awakukubali,na kama wote waliambiana wakajinyanyua na kumzunguka tena Dada yule
"Wote mpo chini ya ulinzi nyoosheni mikono juu"
Wakashtuliwa na sauti kavu,sauti yenye amri walipogeuka wakakutana na midomo miwili ya mitutu ya bunduki...
Naam alikuwa ni insp Nurdin hakiwa ndani ya sare zake za jeshi pembeni yake alikwepo jb akiwa na tshart yake ya jeshi na suruali ya jeans...
"Mkijaribu kufanya ujanja wowote sitosita kuwamiminia risasi"
Jb akawapiga mkwara
Wakati binti yule aliye wekwa kati Sharfia ghafla alijihisi kichwa kikimzunguka!,ghafla ule upepo kama wa feni ukawa ukimpuliza
Na ghafla nafsi ya jb ikatoka katika mwili ule kwa njia ya upepo,sharfia akajishangaa kuwa mchovu mchovu,akapeleka mkono wake katika paji la uso wake jasho lilitapakaa
'Ni nini kinachoendelea hapa?!'
Akajiwazia pasina kupata majibu
Akajaribu kuvuta kumbukumbu,kumbukumbu zake za mwisho ni pale alipokuwa akihisi kuna mtu nyuma yake ila alipogeuka akuona kitu
Pia akakumbuka vishindo alovyovisikia na sauti ile ilomtesa katika maskio yake
Sauti kama ya bosi wake
Akakumbuka alipiga simu polisi pale watu wale walipogonga mlango wake kwa nguvu alafu?!!!
Alafu!....
akukumbuka tena
Akukumbuka kipigo alichowapa watu wale kwani ni wazi hakuwa yeye Bali ni ule MZIMU ULOREJEA
Mzimu wa jb!,ambaye sasa kwa nafsi nyingine alikuwa Mbele yao kama afisa wa polisi mwenye waledi na kazi yake
Majamaa wale awakuwa na ujanja tena zaidi ya kusalimu amri!...
Insp Nurdin akawapiga pingu wote akiwemo na sharfia aliyekuwa akimsaka kwa kukiuka kwake maagizo ya kuripoti taharifa zile...

***********************************

Wakati wakiwa ndani ya gari,furaha imewatawala baada ya kufanikiwa kuichukua ile mifupa bila matatizo yoyote ghafla komandoo chaka akapata wazo
Wazo la kujua kazi alowapa watu wake imefikia wapi?!
Akapeleka macho yake katika saa yake ya mkononi ilikuwa ni saa tano kasoro usiku
Akachukua simu yake na kubonyeza tarakimu kadhaa akaweka maskion mwake simu ikaita baada ya dakika chache ikapokelewa Chaka akaoji kwa kujiamini...
"Nipe ripoti mmefikia wapi?!"
Tofauti na mategemeo yake akapokelewa na sauti nyororo ya kike,sauti iloongea kwa tambo....
"Vijakazi wako wapo chini ya ulinzi wangu...
Chaka akaduwaa,binti akaendelea
Ndo nawaza hapa niwauwe au niwasamehe?!,tatizo hawapo katika list yangu,ata nawe Chaka achana na Mimi....
Chaka akashtuka kwa kuitwa jina lake,kanijuaje jina?!, au ao vijana washatoboa siri?! ,hapana si kwa vijana hawa,vijana alowaamini...
Akaendelea kusikiliza tambo zile
....Achana na Mimi kusalimisha uhai wako ukiendelea?!! tusilaumiane Mimi si leval zenu nyinyi mfyuuui"
Simu ikakatwa
Chaka alichoka!
"Ninini mh!" Kamishna akamuoji akiwa na hamu ya kujua kulikoni
"We acha tu!"
Akajibu Chaka akionesha kuchoka na kukata tamaa.

#No_32
Kamishna akabaki anamwangalia Chaka kwa mshangao
Chaka alionekana kushangaa
"Vijana wangu wameshindwa na mwanamke wako!"
"What?!" Kamishna akaoji kwa mshangao
"Ndiyo nimepiga simu ya jamaa yangu matokeo yake kapokea binti na kusema vijana wale wapo chini ya ulinzi wake na anawaza kuwaua au awaache kwa kuwa hawapo katika list yake,nami niache kumfatilia kama natamani kuendelea kuishi"
"Sharfia ndo kasema maneno hayo?!"
Martin akazidi kuoji huku naye akishangaa
"Ndo ivyo embu nambie Martin huyu binti alishapitiaga jeshi,au kombi yoyote ya mapigano mpaka kuweza kuwaweka chini ya ulinzi wanajeshi watatu tena wenye silaha?!"
"Hapana aiwezekani watakuwa wamekosea njia! Si kwa sharfia nimjuaye Mimi yule hata Mimi naweza kumuua"
Martin akaongea kwa dharau ghafla simu ya kamishna ikaita akatoa kwa kuipokea...
"Alooh mheshimiwa nimefanikiwa kumkamata yule binti ambaye ni mwandishi wa habari baada ya kunipigia simu na kunambia amevamiwa na majambazi na tulipofikia kwake tukamkuta kweli amewekwa kati na vijana watatu ambalo nao tupo nao"
Kamishna akazidi kushtuka
"Mmemkuta binti ndo kawaweka chini ya ulinzi au yeye kawekwa chini ya ulinzi?!"
Kamishna akaoji
"Mh tumemkuta binti kawekwa chini ya ulinzi"
"Akaaa"
Wote wakashtuka
"Sasa aliyepiga simu ni nani? Ikiwa binti ndo aliwekwa chini ya ulinzi?!"
"Ndo swali la kujiuliza ilo bosi"
"But! Akijaaribika kitu huyo binti bado yupo kwenye mikono yetu lazima atangulie! Na vipi kuhusu yule mtu jb maana kwa sasa ndo kikwazo kwangu"
Kamishna aliongea akimwangalia chaka usoni,chaka akujibu kitu akatoa simu yake na kubonyeza tarakimu kadhaa simu ikaita na kupokelewa
"OK nipe ripoti kamanda mmefikia wapi?!"
"Tumefanikiwa kuingia kwenye uzio wa nyumba yake atujamkuta nyumba nzima aina mtu"
"Mlifika saa ngapi hapo!?"
"Toka saa kumi tumeweka patrol eneo lote"
"Gud! Vizuri msiondoke hapo mpaka niwajulishe"
"OK sawa"
Chaka akakata simu!
"Ndo kama mlivyosikia jamaa ajarudi nyumbani leo"
"Embu subiri!..."
Kamishna akaongea na kuitoa radio call yake akabonyeza tarakimu kadhaa na kusikiliza baada ya sekunde chache ikapokelewa
"Aloo upo hapo na huyo jb" kamishna akamuoji
"Ndiyo ovar"
"Ok wapelekeni hao watuhumiwa selo nyinyi mkapumzike kesho saa moja mripoti"
"Yes mkuu" Nurdin akajibu na kukata redio call yake ile
"Safi sana!"
"Kumbe alikuwa na huyo mpuuzi"
"Na sasa ana madakika kadhaa ya kuiona dunia" chaka akamalizia na safari yao ikaendelea
Ilikuwa ni sa saba za usiku....

*************************************

Mida ile ya saa saba za usiku gari ile ya polisi ilichanja mbuga,mpaka kituoni!,
wakashushwa watuhumiwa wale na kuswekwa rumande na yule dada akiwekwa sehemu yake,
baada ya tukio lile! Jb na Nurdin wakaingia ndani ya gari lao kwa safar ya kuelekea nyumbani kupumzika.
"nishushie hapa!" jb akaomba,Nurdin akashtuka,
"wapi tena kamanda ucku huu?!"
"nimesema nishushie hapa! mbona uniskii?"
Jb akaongea kwa ukali akiwa tayari kaishika lock ya mlango wa gari ile. Ikamlazimu Nurdin asimamishe gari na Jb akashuka.
Wasiwasi ukamtawala kachero yule,ulka zake za upelelezi zikamsukuma kumchunguza mtu yule.
Ni mara nyingi tangu kuwasili kwake pale kituoni alishazitilia shaka nyendo zake. Baada ya kuliondoa gari kwa hatua kadhaa na kupotea machoni mwa Jb akalisimamisha gari lile na kushuka kwa mwendo wa haraka na umakini wa hali ya juu akaanza kurudi kule alipomwacha jb!.
Naye jb tangu akiwa ndani ya gari ile alishaitambua hatari ilokuwa nyumbani uwepo wa majambazi walomsubiri aliutambua.
moyoni alicheka kwa dharau.
akiwasikitikia binadamu wale.
Alijua angeenda lazima angezua utata pale ambapo angeificha sura yake ikaonekana tu kwa Nurdin alijua lazima Nurdin angelazimishwa ataje mahali alipo!,
ingekuwa mshangao kwake kwa kuwa si alikuwa naye?
lazma alama ya ulizo ingemtawala!. ndipo alipoamua kushukia njiani. na wakati akiwaza kutoweka ujio wa kurejea kwa nurdin ukambadilisha mawazo yake.
akaamua kutumia hali ya ubinadamu akimpoteza Nurdin maboya!,
Nurdini akiwa na uhakika kuwa ajashtukiwa,akawa akimfatilia jb,jb naye akawa akielekea uelekeo wa nyumbani kwa mpz wake maimuna.
Nurdin alikuwa haujui uhusiano ulokwepo kati ya maimuna na jb,
alishangazwa kumuona jb anaelekea huko. Jb akauparamia ukuta na kuingia ndani, akutaka kupitia getini kukwepa walinzi, vivyo hvyo na nurdin naye akajirusha kwa uangalifu.
jb akachomeka ufunguo katika mlango ule na kufungua akaingia na kuufunga kwa ndani!
Vivyo hvyo Nurdin naye akachomeka ufunguo wake na kuingia.
kwa bahati nzuri jb alimkuta mpz wake bado ajalala,akamkaribisha kwa kumkumbatia.
"vp mpz mmefanikiwa katika operesheni yenu?!"
"yas mpz tumewatia nguvuni hao majambaz na sasa wapo kituoni! tumepewa muda tupumzike asbuh kazini!"
"dah mpz kwa hyo mmeondoka pamoja na nurdin? na umemuagaje? asije akakutilia shaka my hubby!"
"haaah! atajua mwenyewe tuendeleena yetu!"
Ghafla milio tofauti tofauti ikaanza kuskika katika chumba kile...
Nurdin akacheka na kuondoka zake!
'dah yani mtu kaja juzi tu kajiapulia mtoto nami nazidi kubung'aa bung'aa."
akawaza nurdin akiuruka ukuta ule...
Akaliendea gari lake na kuingia
dakika kumi na tano alikuwa mbele ya lango la jumba lake akipiga honi. tayari majambazi walokuwa eneo lile wa nje wakawapa ishara wa ndani.
Lango likafunguliwa na walinzi nurdin akaingiza gari lake ndani akaelekea mpaka parking akashuka na kuingiza funguo akafungua na kuingia ndani,
Akafungua mlango wa chumbani na kuzama ndani kabla ajashtukizwa na teke lililo mpeleka chini! kabla ajanyanyuka akatazamana na mitutu si chini ya saba,watu weusiii tiii!!!
Wenye sura za kutisha, walojazia vifua vyao walikuwa Mbele ya macho yake!
Sura zile azikuwa za Tanzania...
"jb yupo wapi?!"
Akashtuliwa na sauti Kali,sauti ya amri toka kwa mmoja wa mabedui wale na
kabla ajajibu kitako cha bunduki kikatua kichwani kwake,
maumivu makali yakasambaa kwenye mwili wote, kichwa kikapasuka, na damu zikaanza kutiririka!,
maswali yakazaliwa katika kichwa chake!
'wale ni kina nani?!'
'wameingiaje?!, na wameingia vipi? kwa nini wanamuitaji Jb?! na walijuaje kuwa naishi naye?!'
maswali yale yalotiririka katika kichwa chake ayakupata majibu zaidi ya kumfanya awe na butwaa, butwaa lililokatishwa na kipigo kingine, ngumi ilojaa, yenye ujazo ikatua katika paji lake la uso!
Nurdin alihisi ni chuma kapigwa nacho japo macho yaliona ni mkono lakini akili ilikataa kuwa si mkono ule!
"jb yuko wapi?!"
swali lile likarudiwa ila insp yule hakuwa tayari kusema! akawa mkaidi,
mvua ya kipigo ikamshukia! nurdin alilia kama mtoto mdogo!
"wakati tunarudi yeye alishukia njiani sijui alielekea wapi?"
Nurdin akajitetea!
"unaish naye hapa au uish naye hapa?"
"naish naye hapa!"
"iweje ashuke na asikwambie anapoelekea. tutakukata kiungo kimoja baada ya kingine mpaka useme!"
jamaa yule aloonekana ndiyo kiongozi wao akakishusha kisu chake katika kidole cha mwisho, kidole cha mguu kikadondoka chini! nurdini akaachia yowe! jamaa yule akachukua chumvi na kunyunyuzia! Pale penye jeraha palipo toka kidole kile
akachukua sprit na kunyunyuzia!
Nurdin akaachia yowe!
"ntasema jamani! na ntawapeleka,"
Nurdini aliongea huku machozi yakimtiririka kama bomba la mvua
"Sisi ni makatili! na tuna roho mbaya!"
akajigamba jamaa mwingne ikitafuna kile kidole nurdin alichokikata akikichovya kwenye chumvi, damu mbichi zikichuruzika kwenye mdomo wake!

Je nini kiliendelea?!
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu-33 &34

ilipoishia...
"Sisi ni makatili! na tuna roho mbaya!"
Akajigamba jamaa mwingine akikitafuna kile kidole cha Nurdin alichokikata akikichovya kwenye chumvi,damu mbichi zikichuruzika kwenye mdomo wake...

Sasa endelea.....
Si chini ya miaka ishirini sasa yupo jeshini!, alishakutana na watu makatili,wajeuri!,na wenye roho mbaya kupindukia ila hawa walioko mbele yake walikuwa funga kazi
hakuwah kuona au kufikiria kukutana na watu wenye roho mbaya kama hawa!
kwanzia sura zao,macho yao,sauti zao na hata vitendo vyao!,'hawa si watanzania ni wauaji wa kukodishwa hawa'
akajiwazia!
kumbukumbu za mauaji ya kutisha,watu wakichomwa visu,ikamjia,'bila shaka wahusika ni hawa! 'akajiakikishia
,'lakini kwa nini wamtake jb?!' swali hilo ndilo lililo muumiza kichwa,akajizoa zoa na kujinyanyua!
"tutaingia garini kwako na tutatokea getini usilete alama yoyote ya ujuaji ukasabisha kupoteza maisha na kula nyama za watu wasio na hatia, plz umakin waitajika!" nurdin akatingisha kichwa kuafiki.
wakaingia ndani ya gari na nurdin akaliondoa gari taratibu!
alipofika getini walinz tayar walishafungua mlango kwani bosi wao kutoka usiku ilikuwa ni kawaida,
kutokana na kufatilia kesi awakushangaa
baada ya kuskia honi walifungua geti nurdin akapita na kuelekea uelekeo wa nyumbani kwa MAIMUNA, alimuhurumia kijana yule lakini hakuwa na jinsi. ili kuokoa maisha yake kwa makatili wale ni kufanya vile. ilikuwa tayari ni saa tisa za usiku.

**********************************

NDANI YA UCKU ULE ULE WA MANANE

Hakika Maimuna alichoka,tangu ameyajua mapenz akuwah kupata penzi tamu kama la kijana yule,penz lile lilimlevya,na kumtupa katika sayari ya mbali!,ndilo lengo la jb!
"pumzika mamaa, wacha niwasubiri hao mashetani watu!, yah hawakuwa katika list yangu ila MUNGU atansamehe sina budi kuwapoteza! eti fbi leteni hata mashetani waloshindikana!"
jb aliwaza, muda huo huo akajinyanyua na kupiga hatua mpaka sebuleni akaketi katika kochi akikunja nje! alikuwa kazima taa
wale majambazi wakafika katika mtaa ule ambao Martin aliwaelekeza kwa kuwaonesha nyumba
"tutaenda wa nne,nyie watatu mta
abaki hapa na huyo solobwingo tukamalize kazi humo ndani! hakuna kuacha mtu kila kiumbe tutakifyeka na kufyonza damu zao!"
akaongea aliyeonekana kiongozi wao.
"lakini bosi kwanin tusiende wote huyu jamaa tukamuaacha peke yake! tukaondoka na ufunguo au tukamuacha na mtu mmoja?"
"common joson sikujua kama ni mpumbavu kiasi hicho na uctake tuifonze damu yako!, sikutegemea kama utanipinga kwa oja zako za kipumbavu! yule ni polisi tu aliyepitia depo ccp miezi sita! na sisi ni makomandoo,tena majasusi fbi watutegemehao! aiwezekani kimbwa kama kile tukakivamie wote saba no! ata mmoja anaeza kwenda kuteketeza nyumba yote ila kwa kuwa sote tunataman kufyonza damu zikiwa bado mbichi mbich wabaki wanne humu na huyu sis watatu twende!"
yule jamaa akakubali kwa shingo upande, wakajichagua na vijana watatu wakashuka kwenye gari wakimwacha Nurdin katika mshangao mkubwa! kusikia wale ni fbi walokodishwa kwa kazi ya kumwangamiza jb kilimshangaza sana!
akupata tabu kugundua kuwa chanzo ni ubishi wa kijana yule...na kulazimisha kufunguliwa kwa file la jb!
" bosi ndo yupo nyuma ya mchezo mzima!" akajiwazia...alijua hata yeye asingepona.

*************************************

Majambazi wale walizunguka nyuma ya nyuma ile kulipokuwa na geti dogo wakaruka juu ya geti lile na kutokea ndani ya jumba lile
wakatambaa kuelekea katika mlango wa kuelekea ndani ya nyumba palipo na vyumba vya nyumba ile...
walinzi wale walisikia vishindo na kwa haraka wakaelekea upande ule vishindo vilipotokea...
katu hawakujua kuwa wanajipeleka katika vifo, katu hawakutambua kuwa ile haikuwa saizi yao. kwa kuwa wenyewe walienda kwa kukimbia majambazi wale hawakupata tabu kusikia vishindo vyao! wakajibanza kwenye kingo au pembe za ukuta ule wakiwasubiria kwa hamu!...
walipotokea tu walipokewa kwa kipigo kikali, visu vikacharanga vichwa vyao, wakawatenganisha vichwa vyao
walinzi wale wawili kichwa na kiwiliwili! hakika wale walikuwa si binadamu
wawili wakakimbilia kichwa kila mmoja chake,wakiinyon
ya damu yao,na wawili wakikimbilia kiwili wili na kunyonya damu sambamba na kutafuna nyama za binadamu wale kwa uchu.
wale walikuwa ni wa kinte !nchi iliyoko mpakani mwa ganyama! wakitokea katika kabila la wabigirisu! kabila lililopenda kula nyama na damu za binadamu kama chakula chao kikuu.
hawa walikuwa ni makomandoo na wafuasi wa komandoo chaka!
komandoo ambayo aliitetea kinte ilotaka kutawaliwa na raisi wa ganyama(ipo katika riwaya ya mtetezi kutoka kinte) ambao kutokana na uhodari wao katika mapigano na upelelezi walisajiliwa na shirika la upelelezi nchini marekani lijulikanalo kama fbi...
baada ya kumaliza mauaji yale ya kikatili,wakaia
cha miili ile pale na kufata lango la kuingia ndani.katu awakujua juu ya uwepo wa kiumbe tofauti na wao sebuleni pale.kiumbe ambacho kilikuwa na uwezo wa kunyonya damu yao,kama wao wafanyavyo!
kiumbe kilichowasubiria kwa hamu
mzimu ulorejea jb au insp jb
miili iliwasisimka kwa uchu na matamanio ya kuua kikatili na kunywa damu,wakaingiza funguo na kufungua mlango ule.ndani wakakutana na sebule kubwa mtu mmoja akamulika kwa tochi yake kucheki mandhari ya eneo lile.tochi ile ikamulika katika kochi! mmulikaji akapigwa na butwaa,si mmulikaji pekee hata wenzake watatu nao hivyo hivyo walistaajabu!!...
naaam walistaajabu ya Musa kabla awajayaona ya firauni!
jb! aliketi katika kochi lile bila khofu yeyote!,kinywaji kikiwa katika meza yake!,tabasamu likipamba uso wake...
"amna aja ya kushangaa mabwana nlikuwa nawasubiri hapa!,na kwa taharifa tu ujio wenu nliujua na ushenzi wenu wote mlofanya huko nje nimeuona,tangu mkija nlikuwa nawaona!,karibuni! katika siti teh teh teh. akamalizia na cheko la dharau."
"shambulia..."
kiongoz wao akatoa amri
"teh teh teh...teh teh teh teh..teh teh teh teh best unanchekesha sana.!!"...
akawacheka kwa jeuri na kupandisha sauti
"nawe pia si umeshka silaha best!? shambulia...acha kuwaforce wenzako nimekwambia shambulia!?
jamaa yule akabonyeza kifyatulia risasi!
emty...
akawatazama wenzake na kuwapa ishara washambulie...
nao wakamtwiii wakashambulia....
emty...
jb akaachia cheko,cheko lake la dharau akatasua mkono wake aloufunga!
risasi zikaonekana, risasi za bastola zile.
jamaa wale wakagwaya!!
"sisi niwanaume tupambane kiume!"
jb akaongea akijinyanyua pale kochini!
viumbe wale walinywea, walikuwa wadogo kama kidonge cha priton! ila wakakaa tayari kwa mapambano!
kabla jb ajawafikia mtu mmoja akamfata kwa spidi ila alirudishwa kwa teke akaenda kujigonga ukutani!
akuamka tena.
watatu walobaki wakatazamana na kupeana ishara ghafla wakamzunguka jb! ila mwanaume yule akajirusha na kuwatembezea mateke ya rasharasha yalowapeleka chini.
akawanyooshea mikono yake! shoti zikatoka...na kuondoka na uhai wao.
Jb akacheka sana na kurejea kwenye kochi akiiruka miili ile. akakibeba kinywaji chake na kukigwida!...
Nusu saa ilikatika bila ya wenzao kurudi!, wasiwasi ukawavaa,mawasiliano yaliwakatikia ghafla...
aikuwa hali ya kawaida.
muafaka wao ilikuwa ni kuingia ndani ya nyumba ile kujua kulikoni!
wakaafikiana,na wote wakashuka wakiondoka na funguo wakalock milango na kufunga vioo wakazama ndani kupitia ukutani wakiruka miili ya walinzi mlango wa ndani ulikuwa wazi wakaingia,..
ahmadi wakapokelewa na miili ya wenzao...
wakwanza kushughudia akataka kupiga kelele cha ajabu sauti aikutoka!
ni wazi hali ilikuwa mbaya bila kuambiana wakageuka kwa kukimbia kwa nia ya kurudi walipotoka wakajipange upya,
ghafla lango likajifunga!
"mmekuja wenyewe mwaenda wapi sasa?" wakaskia sauti! walipogeuka kuangalia sauti ilipotokea
emty!
hapakuwa na mtu!
mshangao ukawavaa, "si mnapenda damu na nyama nyinyi?! kuleni hiyo sasa!" sauti ile ikazidi kuwasakama...
ghafla mwanga ukawamulikia
mwanga mwekundu!, si mwanga wa taaa,la asha mwanga wa maajabu, vicheko vya ajabu vikaskika, ghafla vilio vya wenzao wakiomba msaada vikaskika, kitendo kilichosababisha wageuke nyuma kuwatazama wenzao...
waliwakuta wamelala vile vile...
ghafla wakahisi wakizungushwa....
kizunguzungu kikawapeleka chini!!!....
"Nyinyi amkwepo katika ilani yangu ya kuwaua ila itabidi mnisamehe..."
wakaisikia tena sauti ile. Ile kugeuka upande ule sauti ilipotokea
mamaaa jitu la kutisha lilikuwa limesimama mkononi limeshika bisu!...
kavaa sanda nyeupeee ilobadilika rangi na kuwa rangi ya udongo,
ilitembelewa na mafinyofinyo na wadudu wasojulikana, shingoni alikuwa na jeraha lililotoa damu mbichi damu ilozingirwa na mafinyofinyo wale na nzi!
jitu alitoa harufu kali iloharibu eneo lote lile.
mbona kimbembe?!.....
Nini kilijiri?!!!

#ENDELEA_NA_SEHEMU_YA_34

#No_34
ilipoishia....
jitu la kutisha lilikuwa limesimama mkononi limeshika bisu!...
kavaa sanda nyeusi ilobadilika rangi na kuwa rangi ya udongo,sanda hiyo ilitembelewa na mafinyofinyo na wadudu wasiojulikana shingoni alikuwa na jeraha lililoloa damu mbichi,damu ilozingirwa na mafinyofinyo na nzi!
jitu alitoa harufu kali iliyoharibu eneo lote lile.
mbona kimbembe?!...

#songa_sasa...
mioyo yao ikawa mizito, ujasiri wote ukawatoka, wakawa wanatetemeka waziwazi...
Pamoja na woga wote walokuwa nao!,ujasiri wa kumwangalia jitu aliyekuwa akiwafata aukuwaisha...
"Nlitaka niwauwe kwa kisu Changu ila nyinyi amkuwa katika orodha yangu hivyo sitowahuwa kwa kisu ilaaaaa"
"Nitawamaliza kwa silaha zenu wenye we"
jitu lile la kutisha likaenda kuokota silaha moja na kuwanyooshea akaikoki! na sekunde chache akatawanya ubongo wao...
Baada ya tukio hilo akaachia kicheko akiitazama ile miili ikitapatapa kabla ijachukuliwa na umauti!...jitu lile likatoweka.
Ni ndani ya usiku ule ule ikiwa inakimbilia saa kumi kasoro za usiku!, Chaka alikuwa katika nyumba yake alokabidhiwa na serikali mpaka atakapomaliza shughuli yake!...
Japo alikuwa kitandani akijaribu kuusaka usingizi lakini usingizi ulimpaa! alichanganyikiw
a hasa baada ya simu yake kutopokelewa! na vijana wake alowapatia kazi
akujua ni nini kilichotokea!..mwisho akapata wazo, wazo ambalo aliliona ndilo lingempa jibu la maswali yake!
akabonyeza tarakimu nyingine tofauti na zile za mwanzo! lengo ampigie kamishna,ndiyo ambaye angeweza kumpa jibu au hata ushauri!
ili jambo inapaswa nilishughulikie mwenyewe sasa!...akawaza huku akiisikiliza simu ya kamishna ikiita...aikupokelewa mpaka ikakata akaipiga tena....
Baada ya kufikishwa kwake! kamishna akashuka kwenye gari!, na kumkabidhi komandoo chaka,
"mfikishe martin kwake nawe ukapumzike asubuh tuonanen ofisini! tukapeleke ile mifupa maabara!"
baada ya kutoa maagizo hayo kamishna akaanza kulisogelea lango la nyumba yake kwa mwendo wa taratibu!, katu akujua ujio wa mgeni alomtembelea ndani ya usiku ule!
mgeni aloketi katika sebule yake! akiwa kakunja nne!
alipita sebule ya nyumba yake pasina kumuona mgeni yule akapiga hatua zake fupi na kuingia chumbani!
mke wake alikuwa kalala fofofo!...
ghafla yule mgeni pale sebuleni akatoweka!!...
na kuja kutokea ndani ya chumba kile
Akiwa kavaa sanda yake ile chafu mkononi akiwa na kisu kilichotapakaa damu!
"kamishna! kamishna! kamishnaaaa"
akaita kwa sauti kali, sauti yenye mtetemo na sauti ilojirudia marambili yani sauti ya mwangi...
ghafla!!!
kamishna akazinduka na kuamka huku mwili ukiwa bado umelala, kilichoamka ni kivuli! kivuli kile kikawa kikimwangalia jitu kwa uwoga!
"kamishna! sikupenda kukuua ila unanlazimisha nikuue!,tena nakuua kifo cha aibu kubwa sana! ni mara ngapi nimekuonya uachane na mimi ujanskia? naitaji nikuzike ukiwa hai..."
Liliongea jitu lile na kumsogelea kamishna alokuwa akilia na kusaga meno akiomba asamehewe!
jitu akujibu kitu akamnyanyua juu na kutoweka naye.
alikuja kutokea katikati ya makaburi!, ambapo pembeni ya pale walipovunja kaburi lile la jb dk chache zilizopita! palikwepo na kaburi jingine,
kaburi ambalo ndani kulikuwa na nyoka mkubwa sana!, bila kujali uwepo wa nyoka yule alomsubiria kwa hamu mzimu yule akamtupa huko na kuchukua beleshi akaanza kufukia kaburi lile!...
"nisamehe!,nisamehe!,nisamehe!.."
kamishna alizidi kulia kwa huruma lakini wala kiumbe yule akumuonea huruma
"mume wangu!,...mume wangu..."
simu ilokuwa inaita ndiyo iliyomuamsha mke wake na kamishna alipo mwangalia mumewe alimwona akiwa anatapa tapa huku akilia asamehewe! mke wake akazidi kumuamsha mme wangu
"amka mme wang!"
ghafla kamishna akashtuka katika ndoto mbaya ile!...
"ni nin mume wangu?!"
mke wake akamuoji lakini kamishna hakuwa na jibu la moja kwa moja
"ni ndoto tu mke wangu!"
akajibu na kupeleka mkono wake mahala ilipo simu yake akaichukua na kubonyeza batani ya bluu kuiruhusu simu ile iingie.
"mpaka sasa nawapigia simu vijana wangu hawapokei sijui wamepatwa na nin?!! plz nakuomba umpigie simu kijana wako yeyote nurdin au jb ili tupate mwangaza nashndwa kujua hali hii inakuwaje?"
chaka akaongea kwa masikitiko!
kamishna akashusha pumzi ndefu
"poa ntakujulisha!"
baada ya kuongea maneno yale akakata simu na kumpigia simu martin. simu ikaita bila kupokelewa mpaka ikakata. akapiga tena. lakini mambo yalikuwa yaleyale...
kamishna naye akachanganyikiwa!!!

ITAENDELEA
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu - 35 & 36 -

Ilipoishia...
Baada ya kuongea maneno yale akakata simu na kumpigia simu Martin,simu ikaita bila kupokelewa mpaka ikakata,akapiga tena lakini mambo yalikuwa yale yale...kamishna naye akachanganyikiwa!!!

#Endelea...
jb! akabaki akiiangalia ile miili kwa dharau!...
alitaka aipoteze! kwa kuipiga shoti, lakini aliona ilo siyo jibu!,siyo jibu kwa walowatuma! wazo lingine likamjia ni kwenda kuwatupa! ama kuwatelekeza mahali! ilo ndilo lilikuwa jibu,
pia aliutambua uwepo wa Nurdini aliyekuwa katika hali mbaya katika gari!
akapiga hatua akiiruka miili ya walinzi na kulifata gari
akafungua! mlango, bado Nurdin alikuwa akigugumia kwa maumivu! jb akamuwekewa mkono katika jeraha lililopo kichwani! jeraha ambalo lilisababishwa na kupigwa kitako cha bunduki na majambazi wale...
shoti ikatoka katika mkono wake na kuyeyusha jeraha lile,maumivu yote yatokanayo na jeraha lile yakayeyuka!,
akapeleka mkono wake katika paji la uso,uloharibiwa vibaya,majeraha yote yakayeyuka,vivyo hivyo mpaka katika kidole kile akakirudishia!...
Nurdin alihisi yupo ndotoni na muda wowote angezinduka.
aikuwa kweli! akabaki akimshangaa kijana yule...
mimi si binadamu Nurdin! jib akafungua mdomo wake kumwambia ukweli! nurdin akabaki katasua mdomo wazi kwa mshangao!
mshangao wa sintofahamu!, ulochanganyikana na woga!,
mimi ni nafsi ya ilodhulumiwa miaka mingi nyuma!
je unakikumbuka kisa cha paka na panya? nlichokupa kipindi flani?!
Nurdin akatingisha kichwa ishara ya kuafiki!
"ok basi mi ndo paka nlokufa miezi kadhaa! japo nafsi yangu bado ipo hai!"
mimi ni mzimu wa jb,mzimu nlorejea kulipiza kisasi kwa martin na wausika wake!
"ina maana wewe jb ndo muuaji?"
"swadaktaaaa!"
nurdin alihisi kuchanganyikiwa!,
"plz naomba nifate!"
jb akafungua mlango na nurdin akatoka wakaelekea katika lango la kuingilia...
nurdin alishtushwa na mauaji alokutana nayo ya kiwemo ya walinzi wale lakini ilo alikumsababisha jb kufanya kile alichokiitaji
Walipofika sebuleni Nurdin alishtushwa baada ya kuiona ile miili ya watekaji wake tena ikiwa na matundu ya risasi katika mapaji yao ya USO
"Una la kujibu insp"
Nurdin akaongea kwa sauti ndogo!,
"Naitaji tuibebe tukaitupe kabla akujapambazuka"
Badala ya kujibu jb kwa kujiamini akaongea
Nurdin hakuwa Mbishi wakasaidiana kuibeba ile miili kwa ajili ya kwenda kuitupa
Wakiziacha maiti za walinzi nje,wakafika sehemu waliyo ona inafaa na kuimwaga miili ile,
Kwa bahati mbaya jb akadondosha kitambulisho chake cha kazi...
Ukawa mwanzo wa maisha mengine yenye utata kwa viumbe wale...
Baada ya kuitelekeza miili ile wakarejea nyumbani kwa ajili ya kupumzika huku nurdin akiwa na mawazo kibao juu ya kiumbe kile...
Ila mawazo hayo hayakumzuia kupata usingizi!
Ilikuwa tayari ni saa kumi na moja za alfajiri

*************************************

Mvurumisho wa alamu ya simu ambayo nurdin aliitegesha alianza kuisikia kwa mbali akafumbua macho yake yalokuwa magumu kufumbuka
Akachukua simu yake na kuangalia mdaa
Ilikuwa saa mbili za asb, Akashtuka
Macho yake yakaelekea kwa jb
Bado alikuwa akikoroma!
Akatingisha kichwa kwa masikitiko
'Watu wengine bwana!,eti si binadamu mi jini jini gani linalala mpaka saiv?!'
Akawaza na macho yake akayaelekezea dirishani
Akashuka kitandani na kulisogelea dirisha lile
Akachungulia nje!!!
Alichokiona bado kidoga azirahi
Kwa woga akageuka nyuma kitandani kumwangalia mwenzake
Kitanda kilikuwa cheupe!!!
Hapakuwa na mtu
Macho yakamtoka Pima!!!!!!!!!
Pasina kuamini akionacho
Je Nurdin kaona nini?!
Vipi kitambuliaho jb alichokisahau katika maiti zile?!
Maimuna akiamka na kuzikuta maiti za walinzi wake pasina kumuona chaka atachukua maamuzi gani?!!!

#ENDELEA_NA_SEHEMU_YA_36

#NO_36

ILIPOISHIA...
Watu wengine bwana!, eti si binadamu ni jini jini gani linalala mpaka saivi?!
akawaza Nurdin na macho yake akayaelekezea dirishani, akashuka kitandani na kulisogelea dirisha lile!
akachungulia nje!!!
alichokiona bado kidogo azirah kwa woga
akageuka nyuma kitandani kumwangalia mwenzake!
kitanda kilikuwa cheupe!! hapakuwa na mtu
macho yakamtoka pima!!!!

#Endelea...
Ni katika alfajiri ile miili ile iliokotwa na wapita njia waloitaharifu polisi na dakika chache polisi waliwasili eneo lile
Akiwepo komandoo chaka na kamishna!
Mpaka muda huo awakuwa na mawasiliano na Nurdin wala jb jambo lililowatia shaka!
Kitendo cha kukutwa kwa kitambulisho kile kikawahakikishia kuwa jb ndo muuaji!
Naye akawekwa kamatuhumiwa namba moja!

************************************

Macho yake yalikuwa mazito kufunguka,mikono yake ikapapasa eneo alilolala
Palikuwa patupu!
Akafungua macho kwa uchovu na kupiga mwayo mkubwa
"Beby!..." Akaita kwa sauti kubwa
Kimya
Akaamka akiwa kajifunga kaupande cha kanga akaelekea bafuni
Alijua wazi mpz wake atakuwa kaondoka!
Akajiandaa kwa kuelekea kazini
Ile anatoka nje akashtushwa na miili ile ya walinzi wake!
Hakuwa na shaka muhusika mkuu ni mpz wake!!!
Huku akiwa kachanganyikiwq Dada yule akatoa simu yake na kupiga namba ya jb
Aikupatikana!!!
Akukata tamaha akapiga ya Nurdin nako majibu yalikuwa Yale Yale
Kwa haraka akarudi sebuleni

HABARI ZILIZOTUFIKIA HIVI PUNDE

Miili ya watu saba imeokotwa ikiwa imekufa kwa kupigwa Risasi katika mapaji ya uso,usiku wa kuamkia Leo
Pembeni ya miili hiyo kilikutwa kitambulisho kilichoandikwa insp jb naye ndo mshukiwa wa kwanza
Jeshi la polisi linamwomba popote alipo ajisalimishe....
Maimuna akaachia pumzi ndefu!,hakuwa na shaka walinzi wake wale waliuwawa na huyo huyo jb
Ni kwa nini anaua?!
Ndo alichopigiwa simu na Nurdin usiku?!!!
Hapana
Akachukua simu yake na kumpigia kamishna akamjulisha juu ya mauaji Yale....
Alijua alikuwa na cha kujibu
Na aliadhimia kusema ukweli pindi akiojiwa...
kumchoma jb....
Na ndivyo ilivyokuwa

************************************

mawazo yalikishambulia kichwa chake!, yamkini akuamini kile akionacho, alihisi yupo ndani ya ndoto kwa taharuki ile!
mawazo hayo yakamskuma kutamani kujua wasifu wa kijana yule
Kijana aliyejitambulisha kama ins jb kutoka makao makuu ya jeshi!,
kitendo cha jamaa yule kuwauwa kinyama makomandoo tena wenye mbinu za mapigano alikumwingia akilini kabisa,
akachukua simu yake ya mezani na kubonyeza tarakimu kadhaa aliitaji kuongea na igp ambaye alimtajia jina mkuu yule wa majesh akaandika jina lile katika laptop yake na namb za askari yule akasachi,
Lakin cha ajabu aikuleta mtu yeyote!
yani katika idara ile hakukuwa na askari kama yule!,
kivipi?!
akuwa na jibu zaidi ya kumjulisha kijana wake! amri ikatoka jb asakwe na kuwekwa nguvuni
zawadi nono ikitangazwa kwa tuhuma za kusababisha mauaji Na kulidanganya jesh zima la polisi.
Kila kona picha yake ikabandikwa, kila chombo cha habari kilimzungumzia! ,jb akawa maharufu midomoni mwa watu.
wakati hayo yakiendelea!...
martini akiwa katika jumba lake kajipumzisha, kutokana na siku mbili kuangaika usiku na mchana, pasina hata kulala usingizi kwa mbali ulianza kumnyemelea!
Ghafla mzuka akazuka ktk sebule ile, akaunguruma kwa sauti ya ajabu,
sauti ilotisha, martin kwa ghafla akafungua macho yake!

Empty!!!!!

akuona kitu, nywele zilimsisimka, moyo ulimwenda mbio!
ghafla akaskia kishindo ahmadi akayaelekeza macho yake pale kishindo kilipotokea
salaale! macho kwa macho na bonge la nyoka Lililotoa ulimi nje kwa uchu!
martin akageuka kuutazama mlango kusudi akimbia akiachia yowe kama kamweuka
mamaaa,mamaaa ile kuufikia mlango ukajirudi na kumgonga kwa nguvu!
Martin akaelekea chini, kishindo kile ndicho kilichowashtua Mke wake na wanawe! walokuwa nje ya nyumba ile!
walipofika walimkuta baba yao kalala chini huku uso ukiwa umemvimba akigugumia kwa maumivu! huku akilalama njoka! watoto wake wakaangalia kule ndani pasina kumuona kiumbe huyo
Hapakuwa na Nyoka wala nini!
jambo ilo likawa la ajabu kwa martin,familia yake ile ilijua wazi baba yao alikuwa anaota!...
Kwa kuwa hali yake aikuwa mbaya sana zaidi ya kuvimba uso alijiandaa na lengo kwenda kwa kamishna kuzungumzia swala ilo....

*************************************

Baada ya chaka kukabidhiwa gari na kamishna ampeleke Martin nyumbani alimfikisha salama kibopa yule
Naye ilikuwa ni muda sasa wa kwenda kupumzika,kila Mara alijaribu kupiga namba za vijana wake bila mafanikio...
"Lazima kutakuwa na matatizo!,dah sitaki kuamini kama vijana wale wameshindwa" akajiwazia
"Ndo uwamini sasa vijana wako nimewateketeza!"
Sauti kavu ikamshtua kutoka nyuma ake, macho yake akayaelekeza katika saidi mirror
Mshtuko aloupata aukuelezeka
Yule yule jb alopewa kazi ya kumwangamiza alikuwa ndani ya gari ile katika kiti cha nyuma kwa tabasamu pana!
Chaka ghafla akafungua mlango na kuanza kukimbia akiliita jina la mama yake,
Mbio zake zikaishia katika nyumba yake,akaingia na kwenda kuemea sebuleni akakaa katika sofa lake huku akihema
"Ni miaka mingi nyuma nlidhulumiwa haki yangu!....
Akashtushwa na sauti ila mmiliki wa sauti ile akuonekana
Na si Mali tu nilidhulumiwa mpaka uhai wangu!, ila mpaka sasa nafsi yangu bado inaishi kwa kuwa siku zangu za kufa bado....
Mtu nlomsaidia akaja kunigeuka akaniua kisa amiliki Mali zote?!!!.....
" unamaana gani?!"
Chaka akapata ujasiri wa kumuuliza naye sauti ile ikamsimulia kisa chote toka urafiki wake na martin mpaka alipomgeuka
Hakika chaka akuamini
Moyo wa huruma juu ya mzimu yule ukamtawala
"Hata Mimi ningekuwa wewe lazima ningerejea!,nin
gerejea kulipiza..."
Chaka akaongea kwa unyonge
"Mke wako yu mjamzito sikutaka kuipoteza furaha yake,nchi yako yajivunia kuwa na wewe sijataka kupoteza MTU kama wewe nnachokuomba achana na hii kesi"
Sauti ile ikatoweka
Chaka alichoka,usingizi ulimchukua pale pale kochini akiwa bado hana maamuzi...

KULIPOPAMBAZUKA

Asubuhi chaka akiwa ndani ya gari lake,kichwani alishapitisha maamuzi
kwa yaliyomtokea usiku! hakuwa tayari kuendelea na jambo lile!..
Kwanza ni kuhatarisha maisha yake kama si ya familia yake hakuwa tayari kuendelea na kesi ile baada ya kuutambua ukweli wote!,
alizidi kukanyaga mafuta ya gari lake Mpaka ofisini aliposhuka na kuelekea moja kwa moja kwa kamishna!
akafungua mlango na kuingia...
kamishna akampokea kwa tabasamu
"ripoti imetoka! ya ile mifupa na inaeleza wazi kuwa mifupa ile niya jb mwenyewe sasa swali kama mifupa ile niya jb ni nani anayeua?!,"
"skia nkwambie kamishna kwanzia leo,kwanza sio leo ni kwanzia sasa nimejitoa ktk kesi hii!"
" what?!"
kamishna akapigwa na butwaa!
"najua ujaamin hili ila nayapenda maisha yangu fedha mlizoniingizia ktk akaunti yangu nitazirejesha!"
" unamaana gani chaka?!"
Chaka akanyamaza kidogo,yamkini alikuwa akiwaza azungimze nini!
"kwanza naomba utambue hii vita si ya binadamu kwa binadamu ni binadamu na sijui mzimu sijui mashetani! nami siwez pambana navyo! jaribuni waganga,na vyombo vya dini lakini kwangu hapana..."
baada ya kumaliza maneno yale akatoka na kuubamiza mlango!....
wakati komandoo chaka anaingia kwenye gari yake! katu akuiona gari ya kifahari!,ilokuwa pembeni yake!
mlango ukiwa wazi na ndani alikwepo kijana mtanashati alokuwa akimwangalia kwa tabasamu pana
yah pengine ni kutokana na mawazo yalomkabili katika kichwa chake,ndo mahana akuliona hilo baada ya kuliondosha gari lake,jamaa yule mtanashat insp jb akashuka katika gari yake na kuelekea katika ngazi!
njiani akipishana na watu ambao awakuwa na taimu na yeye!
si kwamba akuonekana la hasha!
alielekea katika ofisi ya kamishna na alipofika kwa secretary wala akuongea naye dizaini kwamba secretary akumuona!
akagonga mlango, mara moja na kushika kitasa! akakizungusha mlango ukamtwii akaingia ndani!
kamishna alipatwa na mshtuko baada ya kumuona jb! bado kidogo moyo ungechomoka kwenye kifua!..,
Je nini kitaendelea?!

ITAENDELEA
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu - 37 & 38

Ilipoishia...
Akagonga mlango,mara moja na kushika kitasa! akakizungusha mlango ukamtwii,akaufungua na kuchomoza ndani!
kamishna akapatwa na mshtuko, baada ya kumuona jb! bado kidogo moyo ungechomoka kwenye kifua!...

#Endelea
Kwa sekunde kadhaa wakabaki wakitazamana pasina kuongea neno lolote kati yao,
Ila jb akaukata ukimwa
"naskia kamishna mnanisaka mimi kama lulu au dhahabu, likitengwa donge nono kwa atakaye fanikikisha kunikamata, mnanifrahisha sana binadamu!, ila si kiloncho nleta icho!, Najua taifa linakutegemea!,
mchapakazi nisingependa kuendelea kumwaga damu ya wasohusika!
japo kwa namna moja ama nyingine ulistahili kufa!, ila kwa moyo wako wa upendo kwa mchumba angu maimuna!
japo kulitokea mauaji katika nyumba yake!, ulimlinda, na mpaka sasa yupo kazini, sina budi kukushkuru kwa ilo!,
malipo yangu kwako nimetengua kifo kwako, ila onyo usiendelee kujishughulisha na kesi hii, chaka kawa mwelewa kaniskiliza nawe plz kama wapenda kuendelea kuish nskilize kwa ilo!,"
kamishna akaachia kicheko hafifu!
"Sikiliza nikwambie we pepo! kazi yangu nikulinda amani na mali za raia, ni wajibu wangu kumlinda Martin kama raia wa nchi yangu!, ivyo uwezi nitisha kwa maneno! lazima siku moja ntakukamata lazima!"
ghafla kamishna akanyamazishwa na kicheko!
"kama shida yako ni kunikamata nkamate?! npo hapa nkamate wasubiria nin!? mfyuuu"
akaachia msunyo na kugeuka na kuufata mlango akaufungua kabla ajatoka akamgeukia tena kamishna!
"Sitosita kukuangamiza ikiwa utaendelea kufatilia juu ya ili!"
akaubamiza mlango na kutoka, huku nyuma kamishna akajinyanyua na wenge akibwatuka! na kuufata mlango!
"untishi wewe! wewe ni pepo mchafu tu ntapambana na wew mpak.(akaufungua mlango huku akiendelea kubwatuka) kieleweke mshenzi huy..."
ghafla akanyamaza
Akanyamaza baada ya nje kutomuona mtu! baadhi ya maaskari wakimtazama kwa hali ya sintoelewa!
akabaki na butwaa, hata ivyo akaelekea ilipo meza ya secretary wake , kuanza kumuoji!...
"Huyu jb kapitia wapi?"
" jb?! jb gani?!"
maimuna akauliza kwa mshangao!
"kwani ins jb huyu tunayemsaka ajapita hapa kuja ofisini kwangu?!"
heee watu wote wakapigwa na butwaa!!!!!!....
"Bosi hakuna mtu aliyeingia..."
hapo hapo ndipo alipopata picha kuwa wanapambana na mtu wa namna gani!
Kumbukumbu za chaka zikamjia!!!!
Alijua wazi alitembelewa na huyu bwana
mwanzo wakati anamtusi hakuwa na uhakika na mawazo yake! taratibu kama kareruhiwa akajirudisha kwenye ofisi yake!
huku nyuma akimuacha Maimuna katika mawazo makali!
penzi kwa kijana yule lilimtesa!
ila taharifa hizi za kuwa jb si binadamu akuafikiana nazo!
ghafla akarudisha mawazo nyuma!
siku ya kwanza alipomuuliza jb kaingiaje mule ofisini kwa kuwa siku hiyo akumwona wakati anaingia ila alishtuka kamishna na jb wakitoka tu ofisini na kamishna kumtambulisha kwake kama askar kutoka makao makuu,
maimuna akakumbuka pale alipomuhoji jb kuwa alipitia wapi alijibu kuwa yeye ni mpelelezi wa kimataifa na anaweza kuingia bila wao kujua!,
akakumbuka pia jinsi alivyompenda ghafla, maimuna hakuwa wa ivyo! ila kwa jb cku ya kwanza kumuona alimpenda na siku hiyo hiyo wakaingia katika mahusiano!
'hapana kuna kitu ina maana, inamahana..nimelala na mzimu?!
mzimu ulorejea toka makaburin?, mtu alokufa miaka mingi nyuma?! lah!'
Ghafla kichefchefu kikali kikamshika akanyanyuka na kukimbilia bafuni!
kilichofatia ni kutapika! kizunguzungu kikali kikamshika! picha ya jb wakati wakifanya mapenz ikizunguka katika fikra zake! ghafla akaporomoka chini na kupoteza fahamu!...
kishindo kikali cha kuanguka kwa Maimuna kiliwashtua baadhi ya maaskari walokuwepo jirani na vyoo vile!
haraka wakaelekea kishindo kile kilipotokea!
lahaulaa! walishtuka baada ya kumkuta binti yule haraka wakambeba na kumuwaisha hostalini...
baadaye alipozinduka ndipo alipopewa habari ambayo ilimchanganya zaidi!..akuamin kile alichoambiwa na daktari kuwa yu mja mzito
'ana mimba? mimba ya jini? pepo? au mzimu?,au shetani no!'
hakukubali jambo ilo azae na kiumbe kisichoeleweka?!!!
Hapana! alilia! ila mwisho akagundua machozi si jibu la hilo tatizo lake!
baada ya kuwaza sana akapata jibu!
jibu ambalo aliliona ni sahii, kukitoa kiumbe kile...ndio! ulikuwa ndo uamuzi sahii kwa wakati huo
kuonana na dokta haikuwa tabu!
akamweleza shida yake! na kwa kuwa mimba ilikuwa bado changa dokta akaafiki baada ya kuahidiwa donge nono!....
Je dokta atafanikiwa kuitoa embu endelea na sehemu inayofatia hapa chini upate jibu ya swali hili

Nb: USISAHAU KULIKE NA KUSHARE..

BASI ENDELEA HAPO CHINI!

#No_38
Moyo wake ulimuuma sana,japo alijaribu kuuvuta usingizi,ila usingizi ulimgomea
Akazidi kukosa raha!
Alitamani kulia,ila hata machozi yalikuwa mbali nae...
Alishalia sana
"Beby wangu!" Aliita maimuna huku akikipapasa kifua cha jb kilichopanuka na kustawishwa na garden love
"Nambie mpz" akaitika jb huku naye akipapasa matiti madogo ya binti yule...
"Natamani nikuzalie mtoto beby"
"Waoooh kweli honey!"
"Ndiyo mpz na nakwaidi kwa ilo!"
"Ntashkur mpz"
Ghafla akaachia kilio cha kwikwi,
Nikweli alitamani kuitwa mama!,ila sio azae na kiumbe kile...
Kiumbe kisichoeleweka kama ni binadamu, pepo au shetani
"Lazima niitoe,lazima"
Akazidi kuweka nadhiri....

************************************
Alilala katika kitandani kile,akisubiria dokta afanikishe jambo lile
Daktari alivaa gloves na kumsogelea Maimuna...
Ghafla daktari yule akabadilika na kuwa jb
"Kwa nini wataka kuitoa mimba yangu?!"
Woga ukamtawala akawa akirudi nyuma ya kitanda kile...
"Je kina makosa gani mpaka ukihukumu?!"
" aliye kipachika kiumbe hicho tumboni mwako ni MUNGU je alifanya makosa kukuwekea wewe,nakuomba usikitoe na zaa kama utoweza kukilea mi ntarudi kukichukua"
Ghafla palepale jb akatoweka...
Na kurudia sura ya mtu yule,ambaye katu akujua kilichokuwa kiliendelea kwa binti yule,alishtukia ghafla mteja wake kanyanyuka
"Vipi Dada!?"
Akauliza kwa mshangao
"Nimeghairi nitazaa na sitoi mimba tena"
Kitendo cha kumalizia maneno Yale tayari alishaufikia mlango akaufungua na kutoka
alimwacha daktari katika hali ya mshangao,sintoelewa na woga katika moyo wake

*************************************

SURA YA NNE
Ilikuwa ni asubuhi tulivu,hali ya hewa ilikuwa imetulia...
Martin aliegesha gari lake makao makuu ya jeshi la polisi na kushuka,kimuonekano alikuwa kavaa suti ilomkaa vizuri,
Katu usingeweza kutanabahi kama ni mtu mwenye matatizo
Aliingia mpaka mapokezi alipopokelewa na manukato mazuri ya Maimuna...
Mai akampigia simu bosi wake akamruhusu aingiye...
"Habari za tangia Jana ni mbaya kamishna!, mauza uza nyumbani,nyoka wa ajabu kuchapwa na mijeledi si unaona?!"
Alitamka Martin huku akitoa koti la suti yake na shati lake akamuonesha kamishna jinsi alivyovimba
"Pole sana rafiki hali ni mbaya na inazidi kuwa mbaya!,mauza uza hata kwangu yameanza,chaka kajitoa katika kesi hii na karudi kwak!"
"What?!"
"Ndiyo na Nurdin anashughulikia kesi nyingine kajitoa katika kesi hii baada ya kugundua sisi ndiyo tuliokodisha watu wakatake kumuua jb na kumteka yeye,na kumtesa vibaya!"
"Kwa kifupi kaka pamoja na kwamba ripoti ya Hospitalini inaeleza kuwa mifupa ile ni ya jb ila tunapambana na mzimu sijui jini na insp jb hakuwa binadamu yule alicheza tu na akili zetu ndo kahusika wa kila kitu!"
Martin alichoka,ila kamishna akaendelea
"Tunapambana na marehemu jb,rafiki yako wa kitambo,pengine ni mzimu wake,jinamizi lake au chochote kinachofanana na icho,ndiyo aliye muua mtoto wangu kipenzi sasa nakuhaidi tutapambana naye mpaka mwisho...kuna hizi namba hapa za huyu bibi nwa....
Kabla ajamalizia sentensi yake
Ghafla upepo ule wa feni ukasikika mule ndani ghafla kamishna akatoa macho kwa mshangao
" inatosha...umekiuka maagizo yangu sina budi kukutanguliza
"Untishi wewe...kamishna akaropoka akamtazama kwa macho yake makali ya kipolisi
Muda wote Martin alikuwa akishangaa kwani yeye akuuona mzimu ule
Ni kwanini?!
Kamishna alizidi kuutazama mwili ule utishao wa jitu,ulovikwa sanda
" siku zako zinahesabika pepo wewe...
Ghafla kibao kikali kikatua katika shavu lake,kibao ambacho hata martin alikisikia mlio wake,kamishna akamnyooshea simu martin akaipokea
"Bibi nwalau nwalau"
Akatamka jina ilo kwa shida martin akaichek ile simu na kuzikuta namba zile
Kabla ajafanya kitu akamshughudia rafiki yake yule akikohoa
Wazo la kuitaj msaada nje likamjia akatoka aliporejea alikuwa na maaskari
Hali ya kamishna ilikuwa mbaya
"Tangulia mwanaharamu wewe na huyu mwenzako atakufuata niwe na amani ya moyo"
mzimu ule ukamwambia ukizidi kumnyonga
Ghafla akakata roho
Kilikuwa ni kifo cha ghafla,tena cha kushangaza,muda mchache tu alikuwa ni mzima na sasa ni marehemu!
Martin ndiyo aliyechoka zaidi,alijijua ni yeye aliyebakia,na uwezekano wa kupona haukwepo zaidi ya kwenda katika kaburi lile kuomba msamaa pengine angesamehewa
Hakika alijuta kwa alichokifanya
Laiti kama angejua yangetokea haya katu asingemsaliti rafiki yake yule!!!
Majuto ni mjukuu!!!
Hata pale alipokuwa ofisini kwake akilia na kujuta kwa Yale aloyatenda
MZIMU ule ghafla ulitokea...
Martin akuuona,alizidi kulia
Mzimu ule ulimwangalia kwa hasira,hasira iloporomoka nao ukaanza kulia,machozi ya damu
Akatoweka!!!
Ukiwa umeghairi kumwangamiza hasimu wake wa mwisho
Ghafla martin akakumbuka kitu...
Ndani ya makaburi Yale mzimu ule akashtuka...pindi martin alipokumbuka kitu kile...
Martin akatabasamu na kutoa simu yake
Wakati martin anatabasamu mzimu ule ulitetemeka kwa hasira na kutoka nje ya makaburi Yale
Martin akabonyeza simu yake tarakimu kadhaa na kuiweka maskioni ikasarch ghafla ikaita
Mzimu ule pale ulipotokea nje ya makaburi ukaangalia pande NNE zile za dunia lakini ghafla viumbe vingine vilivyovaa kaniki nyeusi na shanga nyekundu kichwani vikatokea...
Mzimu wa jb ukaviangalia kwa hasira viumbe vile
"Nyie vilembwembwe rudini mlipotoka kabla sijafyonza damu yenu"
Jb akaviongelesha kwa ukali,vikacheka kwa kiburi
"Endelea kuwatisha binadamu ila si sisi huu ndo mwisho wako"
Jb akacheka na kuvinyooshea mkono akaachia kombora ambalo viumbe vile viliungana na kulirudisha kombora lile

Ghafla yowe likasikika
Jitu la kutisha jb,lilikuwa chini likiugulia maumivu...
Viumbe vile vitatu vya ajabu vikapotea na kutoka pembeni ya alipo lala jb,vikawa vimemuweka kati

Jb alijaribu nguvu zake,ila zikakataa ni wazi vilembwembwe walizizibiti
Jb akawa angalia kwa hasira...
"Tulia ewe mzimu ulorejea tu naweza kukufanya chochote...
Ghafla bila kutegemea jb akatoweka!,viumbe vile vikajaribu nguvu zao kujua alipokimbilia

Empty
Jb,alijificha!,
Je vile ni viumbe gani?!,na vina ugomvi gani na jb?! Ni swali ambalo Mimi na wewe tunahamu ya kulijua jibu lake
Ila kwa sasa tuachane nalo

Baada ya martin kuweka simu ile skion akapiga namba zile alizoachiwa na kamishna!,akapewa maelezo mahali muhusika anapopatikana
Jb akaaingia katika gari lake kuelekea sehemu ile
Ni kwa mganga bi nwalau nwalau...

Je martin atafika salama?!
Jb kakimbilia wapi?!,vilembwembwe ni viumbe gani na wana ugomvi gani?

Atafanikiwa kummaliza martin
ITAENDELEA
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu -39 & 40

Ilipoishia................................
............
Baada ya Martin kuweka simu ile sikioni,akapiga namba zile alizoachiwa na kamishna!,
akapewa maelezo mahali muhusika anapopatikana...
Jb akaingia katika gari lake,kuelekea sehemu ile...
ni kwa mganga bi nwalau nwalau...

#Endelea......
Kilikuwa ni kijumba kidogo!,ambacho ndani ndo aliishi bibi nwalau nwalau....
Bibi huyo akiwa katika kilinge chake alikuwa akicheza,upepo ulivuma kidogo katika kijumba chake kile...
Tayari alishahisi juu ya ujio wa wageni,au mgeni aliyekuwa akija...
Mganga Nwalau nwalau akazidi kucheza!
,hata Martin alipofika,katika kijumba kile kilichozungushi
wa vitambaa vyekundu alinyooshewa ishara tu aketi uku mbibi yule akiendelea kupiga manyanga sambamba na kucheza!.
"hahahaha!,karibu baba hapa ndo kwa bi nwalau nwalau sema tawile! kama niongeacho ni sahii na kama si sahihi kataa"
martin akatingisha kichwa ishara ya kukubali! bibi mganga nwalau nwalau ambaye pia alishiriki katika story ya nakupenda nasra aliyemuumba nasra jini mvaa gauni jekundu(soma riwaya hiyo) nadhani wengi mtakuwa mnamfahamu!.
ghafla akanyamaza kimya na kuketi akakunja miguu! akachukua mbegu flan nyekundu na kuzitingisha akazibwaga chini! mbegu zile zikatawanyika! akaachia kicheko
"umefika!, maisha yako yapo hatarini!,na tangu ulipotoka kwenu kuja huku mizimu ya babu yang iitwayo kilembwembwe imekulinda usingefika salama
unasumbuliwa na mzimu!, pepo chafu lililotoka makaburini na linakutesa sana!
wakati ulipopata wazo la kuja tu alitaka kukuteketeza ila alitokewa na kilembwembwe wangu akamzuia
Martin akashtuka kuskia vile,akauamini uwezo wa bibi yule...japo maelezo Yale akuyaelewa elewa
"tawile bibi!" Ikabidi aitikie...
Bibi akaendelea...
"mzimu ule ni wa jb aliyekuwa rafiki yako!,kipenz kwa nini ulimuua?"
"nitamaha tu babu nsaidie nimekoma!"
bibi nwalau nwalau akaachia kicheko na kuimba kidogo!,
"wewe ndo umeutenda vibaya u mzimu unajua kwa nini umekuacha mpaka saivi ukiwa hai?! hali ya kuwa wewe ndo muhusika mkuu?"
Martin akatingisha kichwa ishara ya kukataa!
",kuna siri kubwa na lazima tuijue."
"mimi nnachotaka tu unsaidie tusisumbuliwe na ikiwezekana ukiangamize."
bibi yule akacheka tena! na kupiga manyanga,
"mizimu kilembwembwe inataka sadaka! ,tena sadaka ya damu,
damu ya mama yako!
uinywe na nyingine ndo itolewe kama kafara! mzimu ule sasa umejificha na ukifanya hivyo utashikwa na hasira utatoka ukitoka tu mizimu yangu inammaliza."
martin akuamin amuue mama yake?! kwa mara ya kwanza akapakumbuka nyumbani tangu ameondoka hakuwah kurudi...
kumbukumb zake zikarudi nyuma miaka mingi ilopita.

MIAKA 35 NYUMA!

"mdogo wangu usilie! haya yote ni maisha yatapita tu!,kijana mmoja alo onekana mkubwa,mwenye miaka 12 alimbembeleza mdogo wake! ambaye alikuwa na miaka 7 walikuwa katikati ya pori wakikata kuni!"
"yani kama tukitoka hapa tukafue sisi tupike sisi!, shambani sisi mama anaridhika au siyo mama yetu yule?
"hapana mdogo wangu Martin yule ni mama yetu anatupenda sana ila tatizo ni kwa baba yetu ndo anatupa kazi hizi mama awezi ingilia kwa sababu atapigwa! au wewe upo tayari mama apigwe?!"
kijana yule akamuuliza mdogo wake,ambaye alitingisha kichwa kukataa mama yake kupigwa!
"bas kama haupo tazar tuvumilie tu mdogo wangu!"
akamalizia kijana yule aitwaye BRAYSON akamtwisha mdogo wake mzigo mdogo wa kuni wakaondoka!,kue
lekea nyumbani
hayo ndo yalikuwa maisha yao,waliyolazimika kuyazoea
Bryson na Martin walikuwa ni watoto wa bi veriana, bi veriana alikuwa na watoto wa tano wawili baba yao alishakufa, na hao wa tatu mmoja alikuwa mtoto wake alomzaa na huyo mwanaume wawili wakiwa wa huyo baba alozaa na wanawake wa nje!
akawaleta nyumbani
wote walikuwa wa kiume
mzee yule aliwapenda wanae hao wa tatu ila hao wawil wa mkewe aliwachukia
kazi zote wenyewe ndo walifanya ,ila walivumilia mwisho uvumilivu ukawashinda!
siku hiyo ilikuwa hivi!....
Bryson alikuwa shambani akilima ,mdogo wake martin alimwacha nyumbani akicheza na watoto wenzake,
watoto wale wakawa wanacheza mchezo wa mawe, kwa kudhamiria mtoto mmoja akaokota jiwe na kumtandika nalo martin jiwe la mgongoni,
akampasua na damu zikaanza kuchurizika kama bomba la maji!,
bryson kuja akukubali akamvamia yule mtoto alompiga mdogo wake na kuanza kumshambulia, mpaka akamzimisha
bray akajua lazima ameua!
akaamua akimbie kijiji kile!, akiazimia kutokurudi tena huku akimwacha mdogo wake katika mateso makali.
ila hakuwa na budi kupasahau nyumbani! na kweli akapasahau,
akavuka mito,mabonde milima,toka SINGIDA akaja kuishia ARUSHA! mgodin..
Akiwa na miaka ile ile 14,akaanza kufanya kazi za nguvu, Kusaga mawe,
kupeta mchanga, mpaka kuchimba madini na kupasua miamba alipofika kule ili kuogopa kujulikana akabadilisha jina kutoka BRYSON mpaka JACOB au jb!...
na upande wa pili! Martin baada ya kaka yake bray kukimbia, baba yake wa kambo alipokuja! na kuambiwa mwanaye kapigwa mpaka kufikia kuzimia kisa martin hasira zikampanda akampiga martin,na akazidi kumtesa!,
martin akaona sotusheni atoroke akamsake kaka ake bry!, maskin laiti angejua?!!
sijui nini kiliendelea je martin atafanikiwa kumpata kaka yake bry(jb) kumbuka hii ni kumbukumbu anayekumbuka martin akiwa kwa mganga.na kumbuka martin ajui kama jb ni kaka yake

#No_40

Ilipoishia........................
..........
Martin baada ya kaka yake Bray kukimbia, baba yake wa kambo alipokuja! Na kuambiwa mwanaye kapigwa mpaka kufikia kuzimia kisa Martin hasira zikampanda akampiga Martin sambamba na kumzidishia mateso makali...
Martin akaona solution atoroke akamsake kaka yake BRY (JB)!,maskin laiti angejua?!!!......
Songa nayo.....
Njia nzima Nurdin alijawa na wasiwasi,hasa kwa kuwa akujua sehemu anapoelekea,ila aliona afadhali ateseke mtahani,kuliko mateso ya kule nyumbani!,japo akuwa hata na senti tano lakin aliadhimia kusafiri!
Siku ya siku iliwadia,akafanikiwa kutoroka nyumbani,akiwa amependeza,akakaa kwenye siti na safari ikaanza!,pembeni yake aliketi mmama wa makamo ambaye alikuwa amembeba mtoto,baada ya mwendo kidogo wakiwa katikati ya pori kondakta akaanza kupitia tiketi!,kwa kuwa nurdin akuwa nayo alikiegemeza kichwa chake katika magoti yake,ni wazi alikuwa mbali kimawazo!...
kondakta yule alimfikia na kumshtua akiitaji tiketi! martin akamwambia wazi kuwa ana!,kondakta yule akasimamisha gari kwa lengo la kumshusha palepale!
"wew kaka kuwa na huruma sasa ukimshushia hapa porini ataendea wapi? au unataka aliwe na wanyama wa kali?"
dada yule alokuwa kambeba mtoto aliongea,akimwa
ngalia kondakta yule!
"hapana sistar hawa ndo wanaenda jijini kuwa majambazi!,jua hii ni kazi mbaya zaidi kakalia siti!...oya dogo shuka bhana kabla sijakupa kelbu!"
"ngoja! kwanza!..." yule dada akamzuia Nurdin kushuka akafungua pochi yake na kutoa hela akamkabidhi kondakta
"mambo sindo hayo bhana!" konda akajibu tabasamu likiupendezesha uso wake,akaruka siti ile na kuelekea siti za nyuma!
"asante sana dada yangu!,MUNGU atakulipa kwa wema wako sina cha kukulipa mimi!" aliongea Martin huku akilia! dada yule alimuonea huruma akaanza kumbembeleza...
"usilie mdogo wangu!,yameisha we dar unaenda kwa nani?!"
"Naenda kumtafuta kaka yangu!..."
"unajua mahali alipo!"
Nurdin akatingisha kichwa ishara ya kukataa dada yule alimsikitikia sana
"Basi utaenda kukaa kwangu kipindi ambacho unamtafuta kaka yako! kwani tofauti na ivyo utakuwa mtoto wa mtahani!"
Martin alifurahi kuskia vile!,uzuni yote ikatoweka,furaha ikatawala!,aliuona mwangaza wa maisha yake mapya

************************************
Hatimaye mida ya mchana wakaingia katika jiji lile!,jiji lenye shamrashamra,na pilika pilika za hapa na pale!
kama kawaida ya mgeni pindi afikapo eneo ambalo ni geni kwake kushangaa shangaa,hata kwa Nurdin ilikuwa ivyo hivyo!
alilishangaa jiji lile,wakaingia katika basi la tmk na safari nyingine ikaanza!
mara kadhaa wakikutana na "jam" barabarani zilizowachelewesha!
Hatimaye safari yao ikafika mwisho,katika maeneo ya uswazi!...
"we malaya! naona umeamua kwenda kunletea mtoto wako huko shambani kwenu!"
ndivyo walivyopokelewa na baba mwenye nyumba ile!
"siyo hivyo mume wangu,baada ya kunkaribisha na kuniuliza habari za safari unaanza manen...."
"kimya wew mwanamke! sina haja ya kujua hayo naondoka nkirudi nisikikute icho kimdoli chako."
Baada ya jamaa yule kumaliza maneno yale,akafungua mlango na kutoka!
"usijali mwanangu! utayazoea maisha haya,we kaoge ntakuonesha mahali upumzike!"
"ahsante mama!" wote wawili wakanyanyuka na dada yule akaenda kumuonesha Nurdin bafuni,Akaoga na alipotoka akaoneshwa chumba chake akajilaza,kutokana na uchovu kijana yule akukawia kupitiwa na usingizi!
alikuja kuzinduka,njaa ilikuwa ikilishambulia tumbo lake!
akajinyanyua na kukaa! ghafla akaskia kicheko,mara vicheko na sauti ya mama yake yule alomsaidia akiongea!,
akapiga mwayo mrefu na kujinyanyua!,akaelekea sebuleni alipomkuta mama yule na wasichana wengine wawili walofanana kila kitu rika lake wakiwa wanaangalia tv!
Akupata tabu kung'amua kuwa wale ni mapacha
"umeamka mwanangu?!"
dada yule akamshtua kwa sauti
"ndiyo mama!"
"ok njoo nkutambulishe dada zako!,unakumbuka nlikwambia mimi nawatoto wawili mapacha? basi ndo hawa hapa huyu mkubwa kurwa anaitwa Janeth na huyu mdogo ake anaitwa Jenipha wapo kidato cha tatu"
"nashkuru kuwafahamu mama!"
akaitika martin akicheka!
Alistaajabishwa na jinsi walivyofanana
"janeth na jenipha huyu ni kaka yenu anaitwa Nurdin atakuwa hapa nyumbani mkisaidiana kazi mpeni ushirikiano"
"Sawa mama ndo house boy?" janeth akauliza akimwangalia kwa dharau!
"si house boy ni kaka yenu!"
"mbona ukutuambia kama una mtoto mama?" Jenipha naye akadakia!
"muulizeni mama yenu labda nyie atawaskia! nilimwambia si mtaki huyo mtoto! hapa"
Wote wakashtuka na kuangalia sauti ilipotokea
Ndiyo alikuwa Yule yule mume wake,kijana aliye jaa jazba,hasira na wivu teke
"Huyu mtoto hawezi kwenda popote!"
Mama Janeth akaongea kwa hasira
"Kama Mimi ni mume wako lazima aondoke"
"Utanipiga utaniua lakini huyu mtoto aondoki hapaa"
mama janeth akazidi kuweka Ngumu akikimbilia chumbani,mume wake akamfata kwa hasira baada ya dakika chache kilio cha mama janeth kikasikika akiomba msaada,mume wake alikuwa akimpiga...
"Watu wengine bwana mpaka mnasababisha matatizo katika nyumba za watu utakiwi bado unang'ang'ania si uondoke?!"
Janeth akazidi kumsakama,Nurdin
Kijana yule akupenda kusakamwa,alipenda familia ile iishi kwa amani ghafla wazo la kuondoka likamjia akajinyanyua na kukimbilia ndani akaanza kukusanya kila kilicho chake
Ila ghafla,....
Nini tena?! Nini kiliendelea

Itaendelea...
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu -41 & 42

Ilipoishia.........................
...............
Kijana yule akupenda kusakamwa, alipenda familia ile iishe kwa amani ghafla wazo la kuondoka likamjia akajinyanyua na kukimbilia ndani akaanza kukusanya kila kilicho chake ila ghafla....

Songa nayo sasa....

Akashtukia mlango wake ukifunguliwa...
"We uondoki tu!..."
Sauti nyororo ya mtoto wa kike ilimuuliza lakini ghafla ikanyamaza ikimtumbulia macho kwa mshangao...
Alikuwa ni janeth
Alibaki kumshangaa Martin,aliyekuwa akivaa,alikuwa na boxa huku akiwa kifua wazi anajipaka mafuta...
Kutokana na ufanyaji wa kazi ngumu kijijini zikiwemo za kupasua kuni,kokoto ziliugawanya mwili wake na kuitengeneza "sex body"
Ndo maana binti yule alibaki kuduwaa akimtazama kwa macho ya matamanio
"Sa..samahani... Kaka"
Janeth akaomba radhi na kutoka kwa haraka ndani kule akakimbilia chumbani kwake
Penzi la Martin lilimtesa,kijana yule alimteka ghafla
"Ntakupata Martin kwa gharama yoyote ile"
Binti yule akajiwazia akiwa katika kitandani chake...
Kwa upande wa Martin baada ya kumaliza kujipaka mafuta naye akakaa kwenye kitanda chake machozi yakimchuruzika
"Kaka kwa nini uliondoka ukaniacha kaka?!,mdogo wako nateseka uko wapi kaka Brayson ukunambia unaenda wapi ila najua upo hapa hapa jijini ntakusaka kaka yangu wewe ndo ndugu yangu ulobakia"
Kwa uchungu Martin alilalamika,akajinyanyua na kuvaa,tayari alishapata nguvu ya kutamani kumsaka kaka yake,baada ya kumaliza kuvaa akatoka ile amefika sebuleni akakutana na mama Janeth
"Unaenda wapi Martin uwezi kwenda popote utateseka sana hapa jijini lazima nkusaidie usijali kuhusu mume wangu"
Dada yule akaongea kwa unyonge,Jenipha alimwangalia kwa dharau kaka yake yule wa hiyari
"Nashkuru sana kwa wema wako Dada yangu wacha Mimi niende amani ipate kutawala katika nyumba hii"
"Hapana uwezi kwenda popote mwanangu Jenipha rudisha begi ndani"
"Lakini mama mtu si ataki kukaa na baba amtaki si umuache aondoke!"
Jenipha akaongea kwa dharau...
"No mamy Martin lazima akae hapa tumsaidie"
Janeth aliongea akitoka katika chumba chake,akaenda kulichukua begi la martin na kulirudisha ndani
"Sijui kwa nini wewe mtoto una roho mbaya,kuwa na roho kama ya Dada yako!,huyu ni binadamu lazima tumsaidie"
"Mfyuuuuuu!!!....."
Jenipha akasunya na kukimbilia ndani ya chumba chake.......
Baada ya Martin,kubembelezwa sana mwisho akakubali kuendelea kuishi,japo mateso kwa baba mwenye nyumba ile yalizidi kadri siku zilivyokuwa zinaenda
Alizivumilia,mwisho akazizoea na kuona ni kawaida...

*************************************

Ulikuwa ni usiku mnene,ghafla akashtuka,alihisi kuitaji kitu katika usiku ule...
Mwili wake ulichemka,aliitaji upoozwe,akapeleka mkono wake kumgusa mumewe
Na kuanza kumpapasa taratibu,sambamba na kutoa miguno ile,ni wazi alizidiwa....
Mume wake akaushika ule mkono na kwa nguvu akauweka kando
"Siitaji usumbufu naitaji kulala"
"Lakini Mume wangu..."
"Hakuna cha lakini naomba niache"
"Nimezidiwa baba janeth"
"Mfate mume wako huko kijijini alokuzalishia dume atakuridhisha"
"Jamani mume Wang....
Hakika binti yule alikuwa kazidiwa akatoka lengo aende chooni...akiwa kajifunga kamtandio chepesi
Martin naye alishtuka,alikuwa katika maumivu makali,martin wa kiume akulala,aliitaji kumlaza kwa lazima akashuka kwenye kitanda akiwa kavaa bukta ilotuna kidogo kwa mbele akaelekea chooni...
Wote wawili wakakutana katika eneo lile La kuelekea chooni wenye hisia za kufanana
Macho ya tamaa na mshangao ya mama janeth yakabaki kuikodolea macho bukta nyepesi ya martin ilikuwa ikipanda na kushuka kama gorong'ondo atingishapo kichwa
Bila kujielewa akawa akimsogelea Martin
Naye kijana yule macho yake yalokosa pazia yaliuangalia mtandio ule kwa tamaha na kijana yule wa ndani akawa akinesa nesa
Akawa akimsubiria Dada yule kwa hamu,ufahamu uliwatoka wote!...
Mapenzi ni ugonjwa!,mapenzi ni shetani nao walimwacha awaongoze
Wakakumbatiana na kuanza kuoneshana ufundi
Kwa kuwa ile ilikuwa ni sehemu ya wazi wakajisogeza mpaka bafuni
Milio ya kimaaba ikatawala!!!....
Kila mtu akipania kukata kiu yake.....
Wakawa wameufungua ukurasa mpya wa mapenzi
Ukurasa wa laana iloizunguka familia ile
Kwa nini nasema ni laana?!!!!
Basi wakati wakiwa katika tendo lile Janeth akatoka kuelekea chooni,kabla ajaingia akasikia manung'uniko yale ya raha,akatamani kuchungulia
Lahaullah!....alichokiona?!!!!!!!!

#No_42

Ilipoishia........................
.............
Milio ya kimaaba ikatawala!!!...
kila mtu akipania kukata kiu yake....
wakawa wameufungua ukurasa mpya wa mapenzi
Ukurasa wa laana iloizunguka familia ile
kwa nini nasema ni laana?!!!...
Basi wakati wakiwa katika tendo lile janeth akatoka kuelekea chooni,kabla ajaingia akasikia manung'uniko yale ya raha,akatamani kuchungulia
Lahaullah!...alichokiona?!!!
Songa nayo sasa......
Mapigo ya moyo yalianza kubadilisha mfumo wake wa upigaji,mwili wote ulimtetemeka,kadri alivyosikia mama yake akilalamika ndivyo naye alivyojikunja kunja....
Ghafla mama yake akamaliza,akavunja dafu kitendo kilicho onesha muda wowote angetoka
Kwa haraka Janeth akaacha kuchungulia na kurudi ndani kwake,mkojo ulikata,mwili ulimchemka
Kila alipojaribu kulala avikulalika,mwili uliitaji tiba ,kwa Mara ya kwanza moyo wake ukashambuliwa na ugonjwa mbaya sana wa mapenzi
Akajikuta akizitamani sana raha zile,alizozipata mama yake azipate na yeye...akaweka kiapo cha kumnasa Martin kwa gharama yoyote ile
Bila kujali kashatembea na mama yake au la!...

************************************

Brayson kaka yake Martin baada ya kufika jijini Arusha kuogopa kukamatwa baada ya kujua fika kabisa kuwa kijijini ameua wazo la kubadilisha jina likamjia
"Naitwa Jacob lakini wengi upenda kuniita jb"
Ndivyo alivyojitambulisha,akayaanza maisha mapya,akisulubika mgodini kule
Siku zikasonga maisha akayazoea taratibu Pesa ndogo ndogo akaanza kuzishika,hapo ndipo mawazo juu ya mdogo wake yalipoanza kumtesa...
Alijua lazima anateseka!,pindi mgodi ulipotema wakaponda starehe yeye kwake azikuwa na maana
Akuona maana ya kufuja Pesa wakati mdogo wake anateseka kijijini
Damu ni nzito kuliko maji,japo alijua ameua msukumo wa damu ya mdogo wake ikamsukuma kurudi kijijini kumchukua mdogo wake Martin
'Ntateseka naye huku huku ntampangishia chumba atasoma sitaki ateseke kama Mimi ninavyoteseka!,na staki aendelee kubaki kijijini"
Akawaaga rafiki zake na kuanza safari ya kurudi kijijini...

*************************************

Siku ile ile ambayo Martin katoroka asubuhi simba walivamia kijiji kile na kuanza kuua watu
Kwa kuwararua na kuiaribu miili yao vibaya,mpaka wanakuja kuuwawa waliua watu wengi sana!
Mwili uloharibika vibaya ulokutwa nyuma ya nyumba ile, mawazo ya wazazi wale wakajua fika ni mwili wa Martin
Na kwa kuwa Martin pia akuonekana,wakazidi kulipa nguvu wazo ilo
Wakauzika mwili ule....
Baada ya safari ndefu jb akutaka kufika moja kwa moja nyumbani akafikia jirani kwao,ambapo alishtuka baada ya kuambiwa dick akufa!,ni alizimia tu
Pia alishtuka baada ya kuambiwa mdogo wake alikufa kwa kuliwa na simba baada ya simba kuvamia kijiji kile
Alilia!...
Alimlilia mdogo wake
Nguvu za kwenda nyumbani kumwangalia mama yake zikamjia,japo mama yake mzazi alimtesa sana akisaidiana na baba yake wa kambo alijua fika yule ni mama yake mzazi
Kwa hatua fupi fupi akaelekea nyumbani tofauti na mategemeo yake akupokelewa kwa furaha hata!
Mama yake alimkuta amekonda,hata alipomsalimia akuitika,alipoongea akuongea
Akaenda katika kaburi la mdogo wake akalia...aliporudi nyumbani akakuta mlango umefungwa akajaribu kugonga
Kimya
Ikabidi aende kwa rafiki yake kulala huko,akujua kitu gani kilimpata mama yake mpaka kuwa katika hali ile...
Akawachukua wazee wa makamo wakamwombee msamaha lakini hali ilikuwa ile ile awakutaka kumwona Bray pale kijijini....
Bray au jb akaamua kuondoka zake na kurudi Arusha
Miaka miwili alirudi tena akitegemea mabadiliko lakini hali ilikuwa ile ile
Akaapa kutokurudi tena katika kijiji kile...akayatoa mawazo kwa ndugu zake wale,ndugu pekee alikuwa ni martin ambaye kwa sasa alijua ni maiti,
katu akujua kuwa baba yake yule wa kambo alikuwa ni mchawi aliye mloga mama yake na kuutoa upendo wa kwao kwa mama yake yule...

*************************************

"Martin kuna kitu nataka kukwambia"
Aliongea janeth huku akimrembulia macho kijana yule
Walikuwa jikoni,martin akipika
"Nambie tu"
"Niaidi utochukia"
"Nakwaidi sitochukia"
Janeth akaung'ata mdomo kwa pozi la kike
"Martin una mchumba!?"
Kauli ile ilipita moja kwa moja mpaka katika sikio la jenipha alokuwa akipita kuelekea sebuleni akitokea chumbani ilikuwa lazima apite katika korido ile
Akashtuka!...
Akitegemea Dada yake kumpenda kijana yule,alitokea kumdharau sana martin
"Mh!!!...."
Akaguna akiusogelea mlango ule akachungulia kidogo akatega sikio
"Kwa nini umeniuliza hivyo Dada?!"
"Nataka kujua Martin plz nijibu una mpz"
"Mh mi sina"
"Waoooh!,nafrah kuskia hivyo kuna kitu nataka kukwambia martin ila samahani kama nitakukwaza!"
"Sema tu Dada yangu"
"kwanza staki unite Dada pili una jua ni vigumu kwa mwanamke kueleza hisia zake tafadhali nakuomba usije ukaniona Mimi Malaya kwa ichi ntakacho kwambia"
Akanyamaza kidogo kisha akaendelea...
"Wewe ni mwanaume shaibu,mtanashati,handsome boy nimevutiwa na wewe"
"Kivipi jane"
"Nakupenda Martin naitaji use mpz wangu"
"What?!" Martin akaoji kwa mshtuko!,na kile nje jenipha akashika mdomo kwa mshangao
Janeth akujibu kitu akamvamia martin na kumpa mdomo wake
Martin alijaribu kujizuia ila akashindwa akamuachia
Wakazama katika raha ya midomo, binti yule akaanza kutoa mguno
Mguno ulopenya mpaka katika maskio ya jenipha,uvumili
vu ukamshinda binti yule anayefanana kwa kila kitu na Dada yake akakimbilia ndani mpaka kitandani akajitupa na kuangua kilio...
Heee Jenipha nini tena mwenzio ndo kashapenda walia nini?!

Nini kitaendelea?
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu 43 & 44

Ilipoishia.........................
.........
Mguno ulopenya mpaka katika maskio ya Jenipha, uvumilivu ukamshinda binti yule anayefanana kwa kila kitu na dada yake akakimbilia ndani mpaka kitandani akajitupa na kuangua kilio...

Songa nayo sasa...
kila alipojaribu kutafakari alishindwa kupata jibu!,iweje dada yake ampende fukara yule,kila alipofikiria vile akazidi kulia!,kwa vyovyote vile aliamini dada yake kapotea!...
Kwa upande wa Martin bado alikuwa katika hali ya sintofahamu,kiukweli moyoni mwake alijikuta akimpenda janeth lakini mama yake alikuwa chanzo! ni vipi jamii ingemchukuliaje?,
pindi ikigundua amekula kuku na mayai yake akawaza pasina kupata majibu,mpaka anapitiwa na usingizi alikuwa ajapata soln ya jambo lile!
Ulka au tabia ya kutofunga mlango ilimuwia urahisi janeth kuingia ndani ya chumba kile usiku wa manane,
Baada ya kuufunga mlango kwa ndani akapanda kitandani na kuanza kukipapasa kifua kipana cha martini...
Mpapaso huo Martin aliusikia kwa mbali,aliisi pengine ni ndoto!,hisia kali za mapenzi ndizo zilizomuamsha,
akashtuka baada ya kumuona janeth kama alivyozaliwa!,alitaka kumsukuma lakini alishindwa,tayari mwanaume alikuwa hoi bin taabani,wakajikuta wamezama katika mapenzi
pamoja na udogo wote alokuwa nao Martin alijaliwa utundu,wa kuwapagawisha dada zetu hawa.
Janeth alikiri tangu ayajue mapenzi akuwai kufanyiwa kama alivyofanyiwa...moyoni mwake akazidi kumpenda martin mara kadhaa,akaapa kumnyang'anya mama yake na kummiliki yeye!
"beby penzi langu si tamu?!"
"tamu sana!"
"Unanipenda beby!"
"nakupenda sana!"
"naomba ubaki na mimi!"
"usijali mpz! upo peke yako moyoni mwangu"
"Wewe mtamu beby naona wivu ukiwapa utamu wako wanawake wengine! usije kunfanyia hivyo ntakupa wakati wowote utakapoitaji ili mradi uwe na mimi tu Martin unioe!"
"usijali kwa ilo mpz"
"nataka umuache mpaka mama!"
"what?!"
Martin alishtuka katu akujua kama watoto wale wanajua juu ya uhusiano wake na mama mwenye nyumba ile,si Martin pekee aloshtuka juu ya ilo! hata mwanamke mwingine aliyekuwa akiwapiga chabo alishtuka baada ya kuskia maneno yale....
Jenipha!alishtuka, toka usingizini na kushangaa kutokumuona dada yake!,mwanzo alidhani pengine dada yake atakuwa ameenda chooni,dakika zikakatika bila kurejea!...
Tabia yake ya ukimbelembele na hamu ya kujua kila akifanyacho dada yake ikaanza kumshambulia!,machale yakamcheza! kumbukumbu zake zikarudi mchana wakati aliposkia dada yake akimlalamikia Martin juu ya upendo wake kwake!,akahisi kitu!,akutaka kusubiri tena akashuka na kuelekea chumba cha Martin
Mawazo yake yalikuwa kweli akapokewa na miguno ya kimahaba!
moyo wake ukapenda kuchungulia,taratibu mapigo ya moyo wake yakaanza kubadilika!
'dada anafaidi nini kwa huyu fukara?! ambaye siyo leval yake?'
wazo ilo likapita katika kichwa chake!
"Wewe mtamu beby naona wivu ukiwapa utamu wako wanawake wengine! usije kunfanyia hvyo ntakupa wakati wowote utakapoitaji! ili usinsaliti mpz!,martin unioe..."
"usijali kwa ilo mpz"
kauli ile ikamshtua Jenipha!,akatamani kuufahamu utamu huo...taratibu chuki zile,dharau zikayeyuka,hamu ya kutaka kuujua utamu huo ikamvaa.
chembe chembe za wivu zikamtawala,hasa pale alipomwona dada yake akigaa gb katika dimbwi lile la mahaba! ghafla akashtuka
"nataka umuache mpaka mama!"
yah maneno hayo ndiyo yaliyomshtua! akazidi kutega sikio vizuri akistaajabu habari ile ilokuwa ngeni kabisa katika masikio yake!
'ina maana mama anatembea na...no hapana!' akawaza akiondoka eneo lile! hisia zote zikimyeyuka! akarudi chumbani...
Si kwake tu!,hata kwa Nurdin habari ile aikuwa nzuri kwake! hamu yote ya kufanya mapenzi ikayeyuka akabaki katika butwaa!...
Janeth naye pia mshangao ulimvaa, hakuwa na tabia ya kuropoka, majuto ni mjukuu alijuta kwa kuitoa siri ile!,maji yakishamwagika ayazoleki akazidi kukomaa katika msimamo wake ule
"au nimekosea mpz wangu! au nimeongea uongo?!"
Martin hakuwa na cha kujitetea!
akamwachia mwanya Janeth wa kuzidi kuongea
"Tambua yule tayari ni mke wa mtu!, mumewe akijua je?! Baki na mimi mpz"
"Mpsss!,ok beby nimekuelewa vizuri sana kapumzike ntalfanyia kazi"
Janeth akampiga busu na kutoka chumbani kule akiwa mwepesiii...
Alipofika chumbani kwake akamtupia macho mdogo wake
Jenipha alijidai kalala,ila kila mtu kwa wakati ule alikuwa katika mawazo mazito!
Martin aliwaza Janeth kajuaje ishu ile ya yeye kutembea na mama!,akupata jibu ni wazi maisha yake sasa yalikuwa hatarini...
Kwa upande wa Janeth yeye alifarijika sana kumnasa Martin,kijana aliyempenda,alijiisi ni shujaa....
Ila kwa upande wa Jenipha moyo wake ulikosa utulivu!,
'hivi kijana yule ana utamu gani wa kupendwa hadi na mama?!, mama yangu atembee na kikaragosi kama kile?!,hakuna!!!, hapana!!!....
Na Dada kajuaje?! Na mbona alipomuuliza Martin alishtuka?!,itakuwa kweli
Ghafla akakumbuka wakati Dada yake alivyokuwa akijinyonga nyonga kwa mapigo ya kaka martin
Akatabasamu kwa mbali
'Lakini anaonekana anaweza mambo lazima nami anionjeshe utamu wake ntamtisha kumshtaki kwa baba ikiwa atonipa yaaaah'
Akaachia tabasamu....

#No_44
Ilipoishia..............
Baada ya dakika chache hatimaye usingizi ukamchukua
Lakini anaonekana anaweza mambo, lazima nami anionjeshe utamu wake ntamtisha kumshtaki kwa baba ikiwa atonipa
yaaah akaachia tabasamu.....
Songa nayo sasa.......
Akajikuta akijilamba mdomo kwa matamanio makubwa...
Baada ya dakika chache akapitiwa na usingizi...
Kesho yake asubuhi,siku ilianza kukiwa na rasharasha,Martin aliamka raha ikiwa imetoweka katika uso wake...
Alimkumbuka kaka yake
Alimkumbuka mama yake!
'Pengine kaka Bray atakuwa alirudi nyumbani?!'
Wazo ilo likamsukuma kutamani kurudi nyumbani...
"Mama nimepakumbuka sana nyumbani nataka kwenda kusalimia..."
"Beby lakini si ulisema walikufukuza?!"
"Ndiyo lakini nahisi kaka yangu alirudi na nimemkumbuka mama yangu"
Baada ya kubembeleza sana akapewa ruhusa,janeth aliuzunika sana na si janeth tu hata jenipha kwa kutofanikisha lengo lake lakini kwa kuwa aliapa kurudi mapema awakuwa na jinsi...
Siku ya siku ikawadia Martin akapanda garini tayari kwa safari
Baada ya mwendo mrefu hatimaye aliingia katika kijiji chao
Hakika kilikuwa kimebadilika,akachukua boda boda ya kuelekea nyumbani kwao
Kwa kuwa stendi na nyumbani pana umbali...
Kama ilivyokuwa kwa kaka yake naye akupenda kuanzia nyumbani...
Akaelekea mpaka kwa majirani zake
Alimkuta mama peter mama wa rafiki yake kipenzi akiwa anatwanga twanga maindi...
Ghafla mama Yule baada ya kumuona akaduwaa na alipozinduka akatoka nduki akipiga kelele mzimuuuu! mzimuuuuu! Mzimuuuu umerejea mzimuuuuu!
Akaufunga mlango kwa ndani Martin akashtuka!
'Mzimu umerejea?!'
Akajaribu kuwaza jambo ilo bila kulipatia muafaka
'Ina maana mi ni mzimu?!,embu ngoja!"
Akaelekea katika mlango ule na kuanza kuugonga kwa nguvu akiomba afunguliwe ila ikawa tofauti na matarajio yake
Mwisho akaamua kuondoka na kuelekea kwao!...
Alipotokezea nyuma ya nyumba yao akalakiwa na kaburi,macho yake yakatua katika kibao kilichokuwa katika kaburi lile
Martin Ndo jina lililoandikwa alifariki zaidi ya miaka mitatu nyuma tena ile tarehe alotoroka
'Hapana aiwezekani'
Akajiwazia hapo ndipo alipoijua sababu ya mama piter kumkimbia
Alibaki kwa dakika kadhaa
akiwaza,ghafla akapata wazo!,roho ya kijasiri ikamvaa akazunguka Mbele ya nyumba yao...
palikuwa kimya na mlango ulikuwa umefungwa
'Bila shaka watakuwa wameenda shambani'
Akawaza
Akakumbuka sehemu walipokuwa wanaifadhigi ufunguo akaenda kuangalia kweli akaukuta akauchukua na kufungua!
Alijua ni nini alichotakiwa kufanya
Akaelekea katika chumba chao
Baada ya dakika kadhaa alitoka akiwa na beleshi na sururu
Aliitaji kulifukua lile kaburi kusudi ajue ndani walizika nini
Kwa Mara ya kwanza roho ya kikatili na ya kijasiri ikamvaa kijana yule.
Akaanza kuchimbua kaburi lile mpaka akalifikia jeneza akadumbukia chini na kulifungua japo lilikuwa limeliwa na mchwa akalifungua
Akakuta mifupa na fuvu la mtu,akatingisha kichwa
'Ina maana walizika mtu?'
Akajiwazia,akaamua kuruka juu,ghafla kile kitendo cha kuruka akapokelewa na mayowe
Ndugu zake ndo walokuwa wamerudi kutoka shambani
Mama yake,baba yake wa kambo mdogo wake wa kambo na watoto wadogo wadogo wawili bila shaka ni wadogo zake
Kwa mawazo yao walijua martin amefufuka wakakimbilia kwa jirani!
Martin alikuwa kachanganyikiwa
Akujua afanye nini,alijua kwa vyovyote asingeeleweka
Wote wangemwona mzimu
Wazo la kurudi mjini siku hiyo hiyo likamrudia akiapa kutokurudi tena katika kijiji kile
Alisha haribu hali ya hewa
Akaelekea katika kituo cha bodaboda akapanda boda boda ilompeleka mpaka stendi,akapanda basi tayari kwa kurudi alipofadhiliwa jijini Dar
Baada ya safari ndefu alifika salama,japo alikuwa amechoka wote walifurahi kumuona
Si baba mwenye nyumba,mama Janeth na watoto wake wawili
Martin akaanza kuwasimulia kila kitu japo akuwaeleza kama alifukua lile kaburi,wote walistaajabu kwa stori ile
"Itabidi tufunge safari Mimi na wewe na mama yako kwenda kijijini..."
ITAENDELEA
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu - 45 & 46 -

Ilipoishia........................
...........
Martin akaanza kuwasimulia kila kitu,japo akuwaeleza kama alifukua lile kaburi,wote walistaajabishwa kwa habari ile
"Itabidi tufunge safari Mimi na wewe na mama yako kwenda kijijini..."
Martin akashtuka....

Songa nayo sasa........
Akuitegemea habari ile,hasa kutokana na kiapo alichokula
"Sitoweza kurudi nyumbani tena!"
Kwa sauti ndogo ilojaa uchungu Martin akatamka,usoni alimaanisha kile akisemacho...
"No Martin usiseme hivyo kule ni nyumbani kwenu na wale ni ndugu zako tukiwaeleza watatuelewa tu"
"Mh! Sijui..."
Baada ya kubembelezwa sana Martin akakubali kwenda kijijini na walezi wake wale,siku ilofatia baada ya maandalizi wakaingia ndani ya gari tayari kwa kuanza safari.
Moyo wa Martin ilikuwa mzito hasa kwa kitendo chake cha kulifukua kaburi,ndicho kilichomtia wasiwasi
'Ule mda nliokuwa natoka ndani ya kaburi si ndiyo watajua nilifufuka jamani?! ndo maana wakakimbia? Na kukataa kunifungulia mlango?!,ila nlikuwa na haki ya kujua walizika nini?!,kule chini sijui kwa nini sikuwaeleza hili baba na mama'
Martin aliwaza aliwaangalia wazazi wake wale,bila shaka alitamani sana kuwa ambia ila moyo ulikuwa mzito...
Mawazo Yale yakazidi kumnyong'onyesha Martin,furaha yote ilitoweka
Toka kijijini mlandizi mpaka jijini dar kwa miaka hiyo apakuwa mbali ila kutokana na barabara kuwa mbaya walichukua masaa mengi kufika
Walikuwa wamechoka hoi bin taaban ila kutokana na maelekezo ya kijana yule ndogo walifanikiwa kufika salama...
"Sasa itabidi wewe ubaki kwenye gari sisi tutangulie tukaweke mambo sawa,tutakuita sawa?!"
Baba janeth akatoa wazo lililoungwa mkono na wote,mtu na mke wake wakashuka na kuelekea katika nyumba ile!
Bado Martin wasiwasi ulimtawala, hatua ilimvamia hasa alipouona upendo wa baba Janeth
Je ikitokea siku akaugundua uhusiano alokuwa nao baina yake na mkewe, baina yake na mtoto wake?!
'Wamenipenda wenyewe wacha niwatafune!'
Akayatupilia mbali mawazo yake Yale na kumkaribisha zaidi shetani ghafla meseji ikaingia kwenye simu yake
"Vipi mpz umefika salama honey?!"
Ilitoka kwa Janeth akatabasamu na kuanza kuijibu....
Wageni wale walikaribishwa vizuri,huku mioyoni mwa wakazi wale wakistaajabishwa na ugeni ule!...
"Sisi tumetokea jijini Dar es salaam na tumekuja hapa kwa tatizo moja ni juu ya mtoto wenu Martin?!"
"Martin?!..."
Wote walioji kwa mshangao, wakikumbuka pindi alipotoka katika kaburi lile
Ni wazi kwa fikra zao walidhani mzimu ule ulishaleta madhara katika jiji lile
"Kafanyeje huyo Martin?!"
Mama yake Martin akaoji huku alionekana kuchukia ( kukereka) waziwazi
"Swali zuri sana!,miaka mitatu nyuma Martin alikuja jijini Dar akitokea huku kijijini lengo la kuja dar ni kutafuta maisha aliletwa nyumbani na mke wangu huyu hapa"
Wote wakashtuka kwa kusikia habari ile geni kabisa katika maskio yao
"Martin huyu huyu alokufa miaka kadhaa nyuma na kufufuka juzi?!"
Mama Martin akaoji kwa mshangao
"Mimi mwenyewe ndo nashangaa!"
Mumewe naye akajibu kwa mshangao
"Kwanza nachoomba mtambue Martin ajafa,Martin yupo hai!"
Akaweka tuo akiwaangalia wenyeji wake wale,bila shaka alitaka kujua wataipokeaje habari ile na wataipokea kwa uzito gani
"Hapana! Hapana Martin mtoto wetu alikufa na mwili wake tukauzika ila Jana ndo alifufuka na tulishughudia kwa macho yetu wakati akitoka katika kaburi!"
"Martin alikufa na kufufuka?!"
wote waliuliza alama za mshangao zikisomeka katika nyuso zao!
"aswaaa! miaka mitatu nyuma simba walivamia kijiji chetu! na kusababisha mauaji ya kutisha na mmoja wapo wa watu walokutwa wamekufa ni Martin alikutwa nyuma ya nyumba,tulimzika na kaburi lake lipo hapo nyuma!"
"mbona sielewi!,ni martin huyu huyu tuliyenaye sisi?! hapana si kweli!"
mama Janeth alipinga,mume wake akaingilia...
"mke wangu usihamaki mambo yatakuwa sawa tu,wacha tuwasikilize nasi tutatoa maelezo yetu! eeh endeleeni!"
mama Martin akaendelea!
"juzi wakati tulipokuwa tunatoka shambani ghafla tukamuona Martin akitoka katika kaburi lake!"
"whaat?!" wote wakaoji kwa pamoja,ilikuwa ni habari mpya ilowashangaza,ilokuwa ngeni hata kwao kwani Martin akuwasimulia juu ya ilo.
"nahisi kama sijaelewa hapo! martin alitokaje katika kaburi?!" baba Janeth akaoji!
"ni vigumu kunielewa tafadhali naombeni tuzungukeni huko nyuma mkalione kaburi la Martin!"
Bila ubishi wote wakajinyanyua na kuzunguka mpaka nyuma ya nyumba ile,palipokuwa na kaburi...
"bila shaka nadhani mwaliona ili kaburi ni jipya ni baada ya sisi kulifukia baada ya Martin kutoka"
watu wale wakabaki wamelikodolea lile kaburi macho hasa kile kibao kilichoandikwa pale siku alokufa Martin ndo siku mama Janeth alipokutana naye! katika gari kuna nini kinachoendelea hapo kati?! hapakuwa na mwenye jibu la swali ilo
"Ok tumewaelewa ndugu zetu na sisi wenyewe tumeshangazwa na jambo ili! ningependa mfahamu kitu kimoja! mke wangu embu waelezee kila kitu kwa urefu!?"
"sawa mume wangu!,kwa jina mimi naitwa mama janeth au mama jenipha,naishi dar ila wazazi wangu wapo kijiji cha jirani! cha mwavulana,sasa miaka kadhaa nyuma nlitoka kijijini na kuja kupandia gari katika kijiji hiki kwa bahati nzur ktk siti nlopangiwa nlipangiwa na kijana mmoja alokuwa kajinamia muda wote!,na alikuwa akilia,hamu ya kutamani kumjua ni nani ikanvaa Na kwa nin analia?! ndipo nlipoamua kumuuliza kwa sauti ya upole akanambia anaitwa Martin!"
"Martin?! haiwezekani ilikuwa ni tarehe ngapi?"
"hiyo hiyo mloandika amekufa!"
"hapana aiwezekani!..." wazaz wale wakakana
"tafadhali tunaomba mtusikilize na sisi!,ok mke wangu endelea"
"basi nkamuuliza kwa nini analia na anaenda wapi?!,akanijibu analia kwa kuwa ametoroka kwao baada ya kuteswa yeye na kaka yake kwa muda mrefu na kaka yake alitoroka siku chache zilizopita hivyo naye ndo anaenda mjini kumtafuta!"
"Brayson?!" wazazi wale wakatamka kwa pamoja jina lile wakati huo wakitamka Jb Alikuwa amenyanyua nyundo juu na kuishusha katika mwamba ghafla akajigonga kidole kikasagika sagika akaachia yowe!...
katu akujua kuwa kuumia kule kulitokana na kutajwa na wazazi wake kule kijijini...
pamoja na maumivu yote aloyapata akajinyanyua na kushika nyundo kuendelea na kazi!...
muda wote wa kikao kile Martin alikuwa ndani ya gari lile akichart na janeth! wote wakionekana kuzama katika hisia....
Mambo yanazidi kuwa mambo Martin bado anakumbuka yalotokea nyuma kisa cha kupotezana na kaka yake jb (mzimu)
je baada ya kumbukumb zile nin itakuwa mwisho wa vita ile?!
usichoke kufatilia kisa hichi.

#Twende_ep_ya_46

#NO_46

Walezi wale wa Martin walistushwa na habari ile
Martin alionekana akitoka kaburini?!
Kivipi?!
Martin alikufa na waliuzika mwili wake?!
Hapana!!!
Aikuwaingia akilini,wakajaribu kwa kila namna kuwaelewesha wazazi wale ambao awaku taka kuelewa jambo lile
Mwisho wakaamua kuachana nao na kuaga wakiamua kumlea Martin kama mwanao wakarudi katika gari lao
"Vipi baba mmefikia wapi?!"
Wakapokewa na swali kutoka kwa Martin,
Mama Janeth aliishia kutingisha kichwa kwa masikitiko
"Ulikuwa una haki ya kukataa kuja huku mwanangu sijapata kuona watu wabishi kama wale wazazi wako daaah!"
Martin akaachia kicheko hafifu
"Una maana gani baba kusema hivyo?!"
"Wamekana katakata!, wamekiri ile siku ulotoroka ukaja mjini ndo siku ambayo chui walivamia kijiji kile na mwili wako ulikutwa nyuma ya nyumba umeharibika vibaya wakauzika na Jana walishughudia ukitoka nje ya kaburi lile
Mimi na mama yako tumejaribu kwa kila namna kuwaelewesha wamekataa, ivyo tukaamua tuachane nao na kukuchukua na kuendelea kukulea kama mtoto Wetu ivyo usijali
Ila Martin kuna kitu naitaji kukijua kutoka kwako!"
Martin akashtuka!,akatoa macho ya mshangao pasina kujua ni jambo gani ilo akatega sikio vizuri...
"Kuna kitu ambacho nimekiskia kwa wazazi wako na sijakielewa kabisa na mwenye jibu sahii ni wewe!"
Baba Janeth akaoji huku usoni akionekana kuwa na wasiwasi wa waziwazi
"Kitu gani hicho baba?!"
Martin akaoji akiwa na shahuku la kutaka kufahamu
Baba Janeth akaingiza gia na kukanyaga mafuta kidogo!
Alikuwa akiendesha gari kurudi jijini Dar kwa mwendo wa taratibu
"Wazazi wako walisema walikushughudia kwa macho yao Jana ukifufuka ukitoka nje ya lile kaburi
na wanasema siku ile ulipokuja mjini ndo siku ambayo mwili wako ulikutwa umeraruliwa na chui sijui simba na wakatupeleka mpaka katika kaburi lako lilikuwa bado jipya yamkini lilifukiwa Jana,Jana baada ya wewe kufufuka na wanasema walilifukia wao baada ya wewe kutoka na kuondoka mi sijaelewa hapo kabisa
Hasa icho kipengele cha kukuona ukitoka katika kaburi"
Baba Janeth akaeleza wasiwasi wake
"Mpaka wewe baba una mashaka na mimi?!"
Martin akaoji akiwa kakunja sura,in wazi akupenda swali lile...
"Hapana mwanangu ila nataka tu kujua"
"Ok wazazi wangu kwanza niwatake radhi sikuwaeleza haya awali ila niliogopa ila sina budi kuwaeleza sasa ni kweli mimi ndo nilitoka ndani ya kaburi lile..."
"What?!!!"
Wote wakaoji kwa mshangao wakiyatumbua macho yao kumshangaa Martin
"Jana baada ya kuwaaga kuwa naenda kijijini sikufika moja kwa moja nyumbani niliishia kwa jirani ambapo aliishi rafiki yangu wote walinikimbia wakiniita mzimu nlorejea,kiukweli sikuelewa maana ya kauli hiyo
Nikaachana nao na kuamua kuelekea nyumbani nlipopokelewa na kaburi lenye jina langu ukweli nilishtuka...
Hamu ya kutaka kujua alofukiwa ndani ikanishika,na kwa bahati nzuri apakuwa na mtu pale ndani nilikuwa najua mahali funguo ilipo ndo tulipo kuwa tukiuifadhi toka nikiwa nyumbani nilipoenda kuucheki kwa bahati nzuri nikaukuta nkafungua na kwenda kuchukua sururu na chepe na kuanza kufukua kaburi lile!"
Akaweka tuo na kuwa angalia wasikilizaji wake kujua waliipokeaje habari ile
Muda wote wakati anasimulia mama Janeth alikuwa kaushika mdomo kwa mshangao...
Martin akaendelea
"Nililifukua mpaka chini nilipolikuta sanduku nikalifungua na kuingia ndani yake nikakuta fuvu la mtu na baadhi ya mifupa, nikabaki na swali je ni nani alozikwa?!
Baada ya kukosa jibu ndo nikaamua kutoka kwa kuruka kile kitendo cha kutoka tu juu nikawaona wazazi wangu wakitoka shamba waliponiona wakaanza kupiga mayowe mzimu umerejea,mzimu umerejea,mzimu umerejea! Mzimu ulorejea....
Walezi wale wakaangua kicheko,mshangao ile ukiwa bado upo kwenye nyuso zao
Martin akaendelea
...wakakimbia ndani na kujifungia nilibisha hodi awakufungua mwisho nikaona ni bora nrudi zangu mjini"
"Dah pole sana Martin umetuchekesha sana hata ingekuwa ni sisi tusingekuamini ila una makosa kutuficha tangu awali labda tungewaeleza na haya pengine wangetuelewa"
"Kweli mpz!,sasa tutafanyeje?!" Mama Janeth akaoji
"Kilichobakia ni kupima vinasaba! Katika hiyo mifupa...
" ya nini yote haya?!,wameshamkataa mtoto wao hata tufanye nini awatatuelewa tuachane na mambo hayo"
Martin akaongea,wote awakuweza kumkatalia
Wakaamua kuachana na jambo lile
Martin akaapa kutorudi kijijini tena!
Akuiona thamani ya mama yake tena

***********************************

Walifika nyumbani jioni,kwa kuwa walikuwa wamechoka wakaoga na kula baada ya hapo kila mmoja akaenda chumbani kwake kulala
"Leo lazima niupate utamu aupatao Dada na mama"
Jenipha aliwaza,muda huo huo akamwangalia Dada yake alokuwa kafumba macho taratibu akashuka kwenye kitanda kile
"Nitajifanya Mimi ni Janeth ila nitampa penzi tamu zaidi ya la dada mpaka aone tofauti yetu"
Akaendelea kuwaza huku akitoka nje ya chumba kile mpaka chumbani kwa Martin akakiparamia kitanda
Na kuanza kuusambaza ulimi wake ndani ya maskio ya kijana yule
Martin akashtuka na kumpa ushirikiano
"Sshhhh aaaah bebyy yaaaa"
Jenipha akazidi kutoa kilio kitamu pale martin alipozinyonya chuchu zake ndogo
Janeth akashtuka usingizini, akashangaa kutomuona mdogo ake
Macho yake yakadondokea katika mlango
Mlango ulikuwa wazi,akajua mdogo wake atakuwa chooni,dakika zikakatika pasina Jenipha kurejea
Machale yakamcheza
Akashuka kitandani kwa kunyata na kuelekea chumbani kwa martin
"Yaaah oooh shit ingz be by"
Ndo sauti alopokelewa nayo
Moyo ukampasuka paaaaaa
je nini kiliendelea?!

ITAENDELEA
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu - 47 -

Ilipoishia..................
...........
Janeth akashtuka usingizini, akashangaa kutomuona mdogo wake
Macho yake yakadondokea katika mlango,mlango ulikuwa wazi...
Akajua pengine mdogo wake yupo chooni.
Dakika zikakatika pasina Jenipha kurejea,machale yakamcheza akashuka kitandani kwa kunyata kuelekea chumbani kwa Martin
"Ya..aa..h oo..oh shit...ing..za b..e..by"
Ndo sauti alopokelewa nayo
Moyo ukampasuka paaaa

Songa nayo.........
Akuamini kile akisikiacho,mdogo wake kamsaliti?!,mar
tin kamsaliti?!,katembea na familia yake yote kuanzia mama,yeye na mdogo wake bila aibu?!!!
Ni wazi alimchukulia kijana yule ni kicheche wa kutupwa aliyeivamia familia yao...
Chuki ikaanza kujitengeneza katika moyo wake aliegemea ukuta akilia
"Mh janeth mpz penzi lako la Leo ni tofauti na la siku nyingine zote tangu nimekufahamu!"
Janeth akashtuka ni wazi alitambua Martin alijua ana fanya mapenz na yeye akamlaani mdogo wake kwa kuingilia penzi lake
'Ina maana Jenipha alijua juu ya mapenzi yangu na Martin iweje sasa anigeuke Dada yake?!'
Akawaza
"Kwani tofauti yake iko wapi mpz"
"Laleo ni tamu kuliko la siku zote"
"Kweli mpz?"
"Kweli"
Kadri Janeth alivyoendelea kusikiliza maongezi Yale ndivyo yalivyozidi kumchoma moyo wake
Akakimbilia kurudi chumbani kwake,alipojifunika na shuka akaangua kilio,alilia kwa maumivu makali ya moyo
Ndiyo!!!
Alikuwa na haki ya kulia,
"Mimi si Janeth Mimi ni Jenipha"
kule ndani Jenipha akajitambulisha akipapasa kifua cha Martin
Martin akashtuka,akuamini maneno Yale!,alijua fika Jenipha alikuwa ampendi,ni Mara nyingi alimnyanyasa sana pale nyumbani
Yeye alimpenda Janeth
Akamwangalia Jenipha kwa hasira
"Umefanya nini Jenipha?!"
Akamuuliza binti yule
"Umekiri Mimi ni mtamu zaidi ya Dada Janeth,pia najua Mimi ni mtamu zaidi ya mama kwanini usiwe na kitu kitamu?!"
Aliongea Jenipha Akijigeuza geuza kitandani pale
Martin akashtuka,katu akujua kama binti yule angejua juu ya uhusiano wake na mama yao
Akazidi kukosa raha
"Naomba utoke Jenipha"
"Unanifukuza siyo baada ya kuntumia?! Natoka ila nakuomba uachane na hao vikaragosi wako ubaki na Mimi lasivyo?!"
"Utafanyeje?!"
Martin akamuuliza kwa kebehi
"Naomba utoke na usirudie upuuzi huu"
"Usintukane Martin naenda ila sitokubali kukuacha lasivyo basi tukose wote mama,Dada na Mimi"
"Sijakuelewa!"
"Ukiniacha ndo utanielewa kwa heri"
Baada ya kumaliza maneno Yale Jenipha akatoka zake akimwacha Martin katika mawazo mazito
Moyoni akipanga kufanya siri Janeth asijue,maskini akujua janeth alishajua kila kitu
'Ila yule mtoto ni mtamu kwa nini nisiwe naye'
Mawazo ya upotoshaji yakakivamia kichwa chake akikumbuka makeke alopewa pale kitandani
Ghafla mtarimbo ukasimama!
Akaachia tabasamu
'Ntawala wote wa Tatu kila mmoja kwa wakati wake na wakwanza kushika mimba ndo ntakaye mpenda zaidi na ndo ntakayeishi naye na kumpa kipa umbele'
'Na wakishika wote?!'
Sauti nyingine ikamuoji
'Ntajua cha kufanya'
akaipa jibu na kuvuta shuka kujifunika vizuri akiutafuta usingizi
Kutokana na uchovu akukawia akawa katika sayari nyingine...

**********************************

Janeth alizidi kulia akikabiliana na maumivu makali ya moyo,baada ya nusu saa mlango ukafunguliwa Jenipha akaingia
Akapigwa na butwaa kumuona Dada yake akilia,aibu ikamvaa
Damu ni nzito kuliko maji,mapacha wale walifanana kwa kila kitu
Simanzi ile alikuwa nayo Janeth akamuambukiza na mdogo wake Naye akaanza kulia akamfata Janeth na kumpigia magoti akijihisi mkosaji
"Nsamehe Dada Yangu,nsamehe my love"
Wakati wale wakiombana msamaha baba Janeth alikuwa katoka akielekea chooni alipofika katika chumba kile akapokelewa na kwikwi akasogea karibu akatega sikio kusikiliza
"Nsamehe Dada yangu,nsamehe my love"
Akamsikia mwanaye akiomba msamaha huku akilia
'Paaaaaaaaaaaaa'
Kilikua ni kibao kilichotua katika shavu la Jenipha
Binti yule akaachia yowe
Baba Janeth ikamlazimu kuingia
"Ni nini kinachoendelea hapa?!"
Jenipha na Janeth wakaangaliana kwa mshangao,wakiwaza wajibu nini wakashtuliwa na swali lingine....
"Nawauliza mnachogombana usiku huu ni nini?!"

JE WATOTO WALE WATAJIBU NINI?!
NINI KITAENDELEA
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu - 48 -

Ilipoishia.............
......
Jenipha na Janeth wakaangaliana kwa mshangao,wakiwaza wajibu nini?!,...
Wakashtuliwa na swali jingine...
"Nawauliza mnachogombania usiku huu ni nini?!"

Songa nayo sasa.....

"Ni huyu jenipha...analala vibaya usiku kucha ni kunikanyaga kanyaga nimechoka baba..."
Janeth aliongopa sambamba na machozi kuendelea kumtiririka,naye mdogo wake akazidi kuomba msamaa...
"Lakini mwanangu Janeth mdogo wako si kashakuomba msamaa msamehe na wewe jenipha umeshakuwa sasa ujifunze kulala vizuri"
Baada ya mjadala ule kuendelea kwa dakika kadhaa hatimaye Janeth akageukia upande wa Pili wa kitanda kile ishara ya kwamba aliitaji kulala zake,akiyakabili maumivu makali ya moyo
Na baba yao akatoka na kurejea chumbani kwake,akijua ameacha amani chumbani kwa wanaye
"Aaah...Martin...oooh...Tara..tibu...baba"
Baba Janeth akashtushwa na sauti ya mke wake alokuwa akiota...
Alikuwa akimuota Martin
Machale yakamcheza....
"Hapa kuna kitu na lazima nikijue aiwezekani na nilazima nijue juu ya hili na ikiwa hivyo sijui ntamuadhibu adhabu gani huyu kijana"
Akawaza baba Janeth akimwangalia mkewe kwa jicho la mshangao Lililo Changanyikana na simanzi tele ndani yake...
Aliazimia kwanzia siku hiyo aanze uchunguzi wa chini kwa chini...
Taratibu akajilaza kitandani hakiruhusu msururu wa mawazo kujaa kwenye kichwa chake...
Baada ya mawazo mengi kugongana kwenye kichwa chake hatimaye naye akabebwa na usingizi....

***********************************

"Hivi Martin una akili gani lakini ina maana Mimi sikutoshelezi mpaka utembee na wanangu wote wawili?!"
Mama Janeth aliongea kwa hisia,ni baada ya kuugundua uhusiano uliokuwepo kati ya wanawe na kijana yule waloamua kumsaidia
"Hapana mama Mimi siwezi kufanya kitu kama icho,..."
"Ina maana mi naongea uongo?!"
"Hapana mama ila ukweli sina mahusiano yoyote na mabinti zako"
"Sawa si unanificha?!,endelea kunificha hivyo hivyo ila ipo siku moja ukweli utabainika"
"Hakuna ukweli wowote niufichao mama"
"Sawa!,ila Martin kuwa makini na kingine naitaji hapa nyumbani uondoke"
"What?!,ntaenda wapi mama!"
"Umekurupuka kujibu Martin sina maana kwamba Nakufukuza la hasha Bali jua tufanyacho ni hatari kwetu na kinga ni bora kuliko tiba tujihadhari naitaji upange chumba Mimi ntakuwa nakulipia kodi"
"Kazi si itakuwa basi mama?!"
"Hapana!,ntakupa mtaji utafungua hata duka..."
Katu awakujua maongezi Yale yakisikiwa na baba Janeth alojibanza nje ya chumba kile
'Ina maana huyu kijana anadhihirisha ukidume wake katika familia yangu'
Akawaza baba Janeth na kuingia kule ndani kwa ghafla...
Pamoja na maongezi yao aliyoyasikia yalodhihirisha ni wapenzi baba Janeth alishtushwa na mkao alowakuta wamekaa
Kilikuwa ni chumba cha Martin
Akuweza kustahimili kuyatoa macho yake kwa mshangao
Hasira zilimpanda,hakujua ni sangapi aliichomoa bastola yake,
mikono ikimtetemeka akaielekeza kwa Martin
Alikuwa tayari kuua

UNAJUA NI NINI KITAENDELEA
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu - 49 -

Ilipoishia....

Hasira zilimpanda,hakujua ni sangapi aliichomoa bastola yake,
mikono ikimtetemeka akaielekeza kwa Martin
Alikuwa tayari kuua...

Songa nayo sasa.......

Tayari kidole chake kilishaigusa kifyatulia risasi,mdomo wake ulitema maneno kwa hisia akuamin kile akionacho
"Ni wema kiasi gani nlokutendea inamaana ujauona?,au haya ndo malipo stahili ulopaswa kunlipa shetani wewe!..."
"Nisamehe baba...
" siwezi kukusamehe shetani mkubwa wewe umenitia fedheha,una thamani ya kuishi inapaswa utangulie tu"
Ni wakati alipofumba macho aikujulikana Janeth aliingia vipi kule ndani akampush baba yake kwa kikumbo hiyo ikawa salama ya Martin
Kwani alijua alipaswa afanye mini
Akatoka nduki...
Akukumbuka kuchukua kitu chochote
Alikuwa kaponea chupuchupu au kwenye tundu la sindano kama wengine wasemavyo
Baba Janeth baada ya kuanguka chini,huku akiwa mwingi wa jazba machozi yakitiririka akaamka na kuanza kutoa dozi kwa mtoto wake yule sambamba na mke wake nusura ya kuua
Martin baada ya kufanikiwa kutoka nje ya nyumba ile salama,mawazo ya kutokuendelea kubaki jijini dar yakakivamia kichwa chake
Kwa vyovyote vile alijua lazima baba Janeth angemsaka kwa nia moja tu ya kumwangamiza
'Lazima niende nje kabisa ya mji mahali ambapo atanipata kamwe yah mirerani jijini Moshi tena kule naskia wanajificha wauaji,majambazi ndio lazima nami nikachimbe madini"
Kwa kuwa alikuwa na Pesa kidogo akapanda magari ya Arusha na kuianza safari
Katu hakujua kaka yale Brayson alikimbilia huko huko Arusha miaka 20 nyuma,na kimuonekano alibadilika na hata jina alibadilisha...
Alifanikiwa kuingia jijini Arusha mida ya jioni kwa kuwa bado alikuwa na hela akatafuta gesti na kulala...

Asubuh akapanda magari ya mirerani
Na kuelekea mpaka katika machimbo Yale....
Ilikuwa ni vigumu kupata mwenyeji ila akukata tamaha aliishia nje ya machimbo akishangaa mchana alienda kwa mama ntilie kula
Alipotoka aliendelea kushangaa mpaka jioni aliporudi best
Pia akuacha kuchukua Malaya na kulala nao ndani ya wiki moja Pesa yote iliyeyuka maskani yake yakawa kwa mama ntilie yule
Akimsaidia kazi na kumpa wali kama malipo
"Natamani sana nami niingie machimboni kuchimba madini"
Siku moja alimwambia mama ntilie yule,aliye Angua kicheko...
"Mh kwa jinsi ulivyo sharo utaweza kweli?!"
"Mimi ni mwanaume mama kazi yoyite napiga nimetoka dar kuja huku kwa kazi hiyo kivipi nishindwe?!"
"Sawaa tutaona kuna mteja angu mmoja atakuja ntaongea naye akuchukue mkachimbe naye usijali"
"Ntashkuru mama"

*************************************

TUREJEE SURA YA PILI:
"Mama clare chochea kuni ok chochea kuni mama clare chochea kuni yaah chochea kuni watoto wa bibi almando ndo sisi....
Kijana mmoja aliingia huku akiwa anaimba akaenda kuketi kwenye benchi ambapo kulikuwa na jagi limejaa maji akalinyanyua alipoliweka chini lilikuwa litupu
" mama clare naomba ugali mkubwa nikapige kazi..."
Kijana yule alikuwa mcheshi akaagiza chakula,mwili wake ulijengeka kimazoezi
"Bora hata umekuja baba nikukabidhi huyu kijana mwenzako alokuja kutafuta maisha huku mirerani"
Aliongea mama ntilie yule
"Ooh mamaa umenichafua mmen!...sharobaro huyu ataweza kushika nyundo,atajua kupiga baruti?!"
"Ntaweza kaka!"
Martin akajibu kwa unyonge
Jb akamkata jicho kali Martin na kumzawadia tabasamu kijana yule wa kuja akalijibu
"Kwa jina naitwa Jacob au jb kwa kisasa zaidi sijui wewe mlugaluga unaitwa nani?!"
Jb akajitambulisha...
"Naitwa Martin...
Ghafla Jb akashtuka baada ya kuskia jina lile
Alimkumbuka mdogo ake...sura ile ililandana kwa kila kitu na mdogo wake ambaye kwa sasa alijua ni maiti baada ya kwenda kijijini kwa lengo la kumchukua na kukutana na kaburi akaendelea kumsikiliza
....natokea Dzm nimekuja huku Moshi kutafuta maisha"
Vijana wote waliekuwa pale wakaangua vicheko
Martin akaangalia chini kwa aibu!
"Huku si Moshi,huku ni Arusha na upaswi kusema nimekuja kutafuta maisha sema nimekuja kutajirika fala wewe"
Jb akamsahihisha
Martin alishangazwa na jinsi kijana yule alivyokula maskin akujua kama ni kaka yake alokuwa akitamani kumuona
Baada ya Jb kumaliza kula akajinyanyua na kumwambia Martin amfate,ndugu wale wa damu wasojuana wakaongozana kuelekea ndani ya machimbo
"Mwanzo utateseka sana mdogo wangu una budi kuvumilia utakaa na sisi hakuna atakayekunyanyasa katika balo letu tupo wawili Mimi na mshkaji wangu Zuberi ndo jina lake wewe utaongezeka watatu kama nyoka kazi yako ni kupsndisha mchanga wenye madini juu mkiwa wawili utazoea tu dogo"
Jb akatoa maelezo ambayo Martin aliyaelewa........

MWISHO WA KUMBUKUMBU

************************************

"hapana mganga ina maana jb ndo kaka yangu Bry noooooooooooooooooooooooo......
Martin alipiga yowe na kudondoka chini akapoteza fahamu
"Nwalau nwalau Mzee wa kazi nwalau nwalau ashindwi na kazi nwalau nwalau....
Bibi mganga yule akazidi kuimba na kucheza ghafla nje ya nyumba yake ile ya kiganga jitu la kutisha lililovaa sanda likaibuka

Ni MZIMU ULOREJEA

Kuibuka kwa jitu,ndani ya kibanda kile mganga Nwalau Nwalau nywele zikaanza kumsisimka woga ukamtawala,ila aliiyamini mizimu yake vilembwembwe.
Akazidi kuimba...
Mzimu yule baada ya kuibuka kule nje alitoweka na kuja kutoka ndani ya kibanda kile akawa akimwangalia mganga yule kwa uchungu,ni wazi bib kikongwe yule akuliona jitu lile
Mganga akawa anamtibia Martin alolala pale chini!,lengo lake amrejeshe katika fahamu
Akafanikiwa kuzirejesha fahamu zake,baada ya Martin kukumbuka kilichotokea alishindwa kuvumilia kulia kwa uchungu ni wazi alimpenda sana kaka yake...
"Sema upo tayari tukiangamize hichi kiumbe?!"
Martin akanyamaza,mawazo yalikuwa mbali akikumbuka jinsi kaka yake alivyokuwa akimpenda kipindi lile kijijini,machozi yakazidi kumtiririka
"Kwa sasa kiumbe kile si binadamu tena ni adui yako je tukiangamize usipokiuwa kitakuua chenyewe"
Bibi yule akazidi kusisitiza
Martin akamkata jicho la hasira

Itaendelea...
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu - 50 -

Ilipoishia...
"Kwa sasa kiumbe kile si binadamu tena ni adui yako je tukiangamize usipokiuwa kitakuua chenyewe"
Bibi yule akazidi kusisitiza
Martin akamkata jicho la hasira
:

Songa nayo sasa....
"Sina thamani tena ya kuishi ni bora kiniangamize,ni haki yake kuniua kaka Bray kwa nini lakin kaka yangu ukunambia kama ni wewe bry nooo kaka lazima nikufate....."
Ni wazi martin alikuwa amechanganyikiwa akanyanyuka kwa speed na kuingia ndani ya gari lake alishapitisha maamuzi ya kujiangamiza akuona umuhimu wa kuishi.
Baada ya Martin kutoka katika kibanda kile mzimu ule kwa Mara ya kwanza ulitoa machozi
Machozi ya damu!!!....
Nao ukatoweka,ukaja kuibuka ndani ya chumba cha Martin alipikuwa kajifungia huku akiwa kashika bastola yake tayari kwa kujiua
"Noooo mdogo wangu Martin acha nakuomba usifanye hivyo NIMESHAKUSAMEHE"

Martin akuamini akauangalia mzimu ule,wala akuogopa akaukimbilia kwa lengo la kuikumbatia
Patupu
"Mimi ni roho Martin sina mwili utoweza kunishika mdogo wangu"
"Nisamehe kaka ni shetani kaka yangu..."
"Martin mdogo wangu nimekusamehe ila kwa masharti,"
"Masharti?!"
"Ndiyo unapaswa Mali zote tulizochuma wote ukatoe sadaka kusudi nami niishi kwa amani katika nyumba yangu ya milele"
Bila kujali ataishi wapi Martin akakubali...
Mzimu yule akatoweka!

************************************

Martin baada ya kupewa sharti lile kutokana na upendo.alokuwa nao kwa kaka yake akatoka sebuleni na kuita familia yake!
Martin alikuwa na mke na watoto wawili wa kike walokuwa medium lakini wakati huo walikuwa likizo
"Mke wangu kuna kitu naitaji kukwambia,hizi Mali si zangu mke wangu na mwenye we kaziitaji ivyo yapaswa Leo turudi kijijini...
" na nani urudi nae kijijini una hata haya kwa nini usingenambia mapema na kwa taharifa yako hawa si wanao nilikubambikizia tu una uwezo wa kupata warembo kama hawa"
"Mke wanguuu!"
"Ishia hapo hapo nipe talaka yangu"
"Mi ntaishi wapi mama Mery"
"Utajua mwenyewe"
Alimalizia Dada yule na kujinyanyua akafata kabati lake na kulifungua akabeba nguo zake zote na alipomaliza akamfata Martin
"Naitaji talaka yangu"
Martin hakuwa Mbishi akaiandika talaka na kumkabidhi hapo hapo Mbele ya Martin akatoa simu na kupiga namba kadhaa akaweka sauti
"Aloo be by njoo nchukue mpz"
Martin hakuamin mwanamke aliye mpenda akakumbuka kauli ya wahenga 'filisika ujue tabia ya mkeo,'
Ni kweli!!
Mwanamke ambaye ameishi naye zaidi ya miaka 20,ambaye akunukia hata harufu ya usaliti kumbe ni nyoka alomtafuna kwa siri
Akujali!
Dakika chache baadaye gari ya kifahari
Ikaja Martin akashughudia mkewe akipigwa busu na kuingia ndani ya gari,wakaondoka...
Baada ya tukio lile akaelekea kanisani na kuonana na mchungaji akamweleza kila kitu na maamuzi aloyachukua akazikabidhi Mali zote kwa mchungaji
"Umechukua maamuzi ya kiume Martin najua utateseka,ila pambana uchume Mali zako za halali"
"Mchungaji naomba unipatie hata mahali pa kujistiri"
"Martin!,martin!,sitoweza kwa hilo"
"What?!"
Martin akuamin hata mchungaji yule alomkabidhi Mali zake zote mtumishi wa Mungu akuweza kumfadhili?!
Martin akawaza alisahau kuwa hata yule pia ni binadamu mwenye mapungufu...
Baada ya kutoka pale akaridhia kuishi maisha ya mtaani,usiku akienda kulala kwenye kaburi la kaka yake....
Kipele mlinzi wa makaburi Yale alimruhusu akijua fika wawili ni tofauti ya mmoja!
Ndani ya siku mbili aliishi mtaani ila siku ya Tatu usiku wa manane akiwa kalalia kaburi lile ghafla jitu LA kutisha likatoka
Akiwa mwingi wa tabasamu!
"Martin mdogo wangu!"
Martin akashtuka...na kumwangalia kaka yake alotabasamu
Martin naye akatabasamu!!!.....
"mdogo wangu Martin! pole sana kwa mateso uyapatayo, nadhani sasa umejifunza tamaa ni mbaya kwa kiasi gani! na bila shaka utaacha tamaa!,
najua ulinipenda sana na laiti ungejua ni mimi usingefanya ulofanya, hata mimi pia nakupenda sana mdogo wangu ndo maana sipendi uteseke bay tha way bado una nafasi ya kufurahia maisha! kwa kumiliki mali zako za halali! je utazipataje?!
naomba unisikilize kwa makini!....
marehemu baba alikuwa na mali nyingi sana hazina,ya dhahabu aliyoipata enzi za ukoloni!, marehem baba yetu alikuwa ni askari wa kijadi! wa ukoloni ivyo mali zile zipo mafichoni mpaka sasa na wewe ndo unapaswa ukazipiganie! nami ntakuwa nyuma yako!
tambua baba yetu wa kufikia anajua juu ya hazina hii na yeye ndio aliyemuua baba yetu akaishi na mama

Itaendelea...
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu - 51 -

Ilipoishia...
Naomba unisikilize kwa makini!....
marehemu baba alikuwa na mali nyingi sana hazina,ya dhahabu aliyoipata enzi za ukoloni!, marehem baba yetu alikuwa ni askari wa kijadi! wa ukoloni ivyo mali zile zipo mafichoni mpaka sasa na wewe ndo unapaswa ukazipiganie! nami ntakuwa nyuma yako!
tambua baba yetu wa kufikia anajua juu ya hazina hii na yeye ndio aliyemuua baba yetu akaishi na mama

Songa nayo sasa....

Akijua fika mama anajua mahala ilipo hazina ile! maskin kumbe mama ajuh ili wala lile, ndo mpaka saivi ana imani ipo siku mke wake ataitoa hazina ile na kutajirika yeye na wanawe.

Ndo maana walikuwa wakitupiga vita na baba yetu yule wa kufikia alimloga mama yetu ndo maana akutujali,
alitudharau! ila sasa hayo yote yameisha! sitokupa nauli ila akikisha unaenda kijijini ntakupa mwongozo!
kwa sasa naenda kummalizia huyo baba kwa kuwa ndiyo chanzo cha yote na kurudi katika nyumba yangu ya milele!,kwa heri mdogo wangu na hatutoonana tena

Baada ya kumaliza maneno yale mzimu ule ukatoweka!,ukimwacha Martin katika hali ya sintofahamu!,akuelewa kitu alichoambiwa!
akupenda kurudi katika kijiji kile, kijiji alichoapa kutorudi baada ya wazazi wake kumkana kwa kujua kuwa amekufa!
ila kutokana na maelezo alopewa ilikuwa ni lazima aende, akaipiganie azina ile!, ila idadi ya maswali yalikizonga kichwa chake!,
ni vipi ataipata hazina ile hali ya kuwa akujua ilipopatikana?!,pili atafika vipi kijijini hali ya kuwa akuwa hata na senti tano jambo hilo lilimuumiza sana kichwa!...

Na aliumia zaidi pale alipokumbuka kauli ya kaka yake kwamba atorudi tena duniani japo atamsaidia je atamsaidije?!
hali ya kuwa atorudi tena? kwa unyonge akapiga hatua zake fupi kutoka eneo lile la makaburini mawazo yakizidi kukizunguka kichwa chake! alihisi dunia imemuelemea!,..

**********************************

Ndani ya kijiji walichoishi wazazi wa Martin!,mzee wa makamo ambaye miaka yake ilikuwa si chini ya 50, lakin alionekana bado kijana mdogo kutokana na kazi za sulubu na mafunzo ya kijeshi aloyapitia
mawazo yalikishambulia kichwa chake pamoja na umri wote ule alokuwa nao bado alikuwa na fikra tele katika kichwa chake,
alikuwa na siri nzito!,
"huyu mwanamke sikumpenda kabisa!,kuna kitu nlikipenda kutoka kwake nasikitika mpaka sasa sijakipata! staki kuamini kama marehemu John akumueleza mkewe juu ya hazina ile!, ila kama angemweleza mpaka sasa lazima angenieleza lakini anaonekana kutokujua juu ya hili sijui ntafanyeje nakufa maskin mie!..."

Ghafla radi likapiga!
hali ya kuwa hakukuwa hata na dalili ya mvua,Upepo mkali ukavuma na kuleta gharika eneo lile...
lilikuwa ni jambo la ghafla...
machale yakaanza kumcheza mzee yule nywele zikamsisimka,kwa haraka akanuia maneno kadhaa na kutoweka eneo lile!
sekunde chache baada ya mzee yule mwenye nguvu za kichawi kutoweka mzimu ulorejea wenye kutisha ulitokea,
Mzimu wa Jb, kwa mara ya kwanza Jb akayatoa macho kwa mshangao, ghafla akaskia cheko katika maskio yake alafu likageuka na kuwa sauti za kuogofya,
sauti zilizoleta kero katika maskio yake!
"nilijua utakuja Jb,na nakushangaa sana! mdogo wako alikuuwa kikatili ukamuacha hai unafkria kuniua mim sahau hiyo wee pepo rudi makaburini kabla sijakuweka katika mateso ya milele mpaka kiama chako!"
Sauti ile ikakoma,ikisindikizwa na cheko la dharau kwa mara ya kwanza tangia JB arudi duniani alipata kikwazo ambacho akukitarajia!.tena akiwa Ndo anaimalizia kazi yake!

ndiyo,...
Alijua fika yule mzee ni mchawi, tena mwenye nguvu, ila akujua kama nguvu zake zile zingekuja kukinzana au kuzizidi nguvu zake!
hapana akukubali ilo!
akaunguruma kwa sauti kali sauti kama ya mnyama mkali tena alopandwa na ghadhabu!
vicheko mfululizo,vingi tena vyenye kukera na kumzidishia hasira vikayashambulia maskio yake!,
ghafla viumbe vyeusi tii vyenye mapembe katika vichwa vyao vilivyojifunga kaniki nyeusi vikatokea na kumzunguka jb!
jb akajizungusha na kupiga Mateke ya dable bila kutegemea akakumbana na hewa,ni wazi viumbe vile vili kuwa ni kama vivuli viumbe vile vikaachia vicheko kwa kitumia sauti ya mapaka ndani kabisa ya ngoma ya maskio ya jb,kijana yule akazidi kuchanganyikiwa!...

Umakini ukaongezeka akajua viumbe apambanavyo vinaweza kumuua kwa Mara ya Pili...
Naye hakuwa tayari kwa ilo
Ghafla akaufunua mdomo wake na kutoa moto viumbe vile vikaachia mayowe

Bado hali ya hewa nje aikuwa nzuri,mvua ilizidi kupiga,radi nalo likichukua nafasi yake....
ilikuwa ni gharika...
Jb baada ya kuona shambulio lake limefanikiwa akataka kuupanua tena mdomo atoe pigo lingine
Mdomo ukagoma kufunguka
Ilikuwa kama kuna mtu kauzuia,mawazo yake yalikuwa sahihi

Baada ya shingo yake kuipeleka katika pembe ya chumba kile,akamuona adui yake,baba yake wa kambo akiwa kaikunja mikono yake ishara kwamba kauzuia mdomo wake kutoa shambulio
Jb akazidi kufedheheka,ghafla akaupiga mguu chini kwa nguvu,mchawi yule akaacha kuikunja mikono Kama alivyokuwa anafanya
Akampa wasaa jb kuufungua mdomo wake na kuachia shambulio lingine kumwendea yeye
Mzee yule akaachia yowe
Yowe lililomuamsha mke wake,na kubaki kumtumbulia macho mumewe alokuwa akitapatapa pale kitandani
Katu akuona vita ilikuwa ikiendelea katika chumba chake kile....
Akaanza kumuamsha mumewe ambaye sasa alikuwa akitapatapa...kombora lile alilopigwa na jb lilimpeleka chini sasa jb akawa na kazi ya kumnyonga,vile viumbe vingine baada ya kuona mambo yamewawiya magumu vikatoweka

Jb alimnyonga mpaka alipoakikisha katulia na kunyoosha miguu yake ndo akaacha kufanya kitendo kile...
Tayari alishaifanikisha adhma yake,akaachia cheko ambalo kwa mama yake lilipokelewa kama radi nje ya nyumba ile...

Mama yule akazidi kumuamsha mumewe,na ghafla akaachia yowe baada ya kugundua kafariki!,alilia kwa uchungu kilio kilichowafikia mpaka watoto wake wote wakajumuika kuomboleza...
Akuna alotamani kulala tena....

************************************
ITAENDELEA
 
MZIMU ULIOREJEA

SEHEMU - 52 -

Bado mawazo yalimsonga ni kwa namna gani angeweza kupata nauli ya kwenda kijijini kutafuta hiyo hazina aliyoambiwa na kaka yake...
Lakini wazo lingine likagonga katika fikra zake!,
Hata kama angeenda ni vipi angeitambua njia ya kupata hazina ile!...
Akaamua itakavyokuwa na iwe ila lazima arudi kijijini,alifurahi zaidi baada ya kukumbuka kuwa kaka yake alimuhaidi kuwa naye bega kwa bega!
Kumbukumbu hizo zikampa nguvu na hari ya kutafuta nauli kwa juhudi!
Akutaka kupoteza muda siku hiyo hiyo akazunguka mtaani kutafuta kazi!,akapata katika car wash ya kuosha magari...
Siku moja ilikuja gari la kifahari,Martin akaisogelea tayari kwa kuiosha!,kioo kikafunguliwa na kuruhusu harufu Kali ya manukato kusikika katika pua za Martin,macho yake yakatua Mbele ya mtoto mzuri,
Akukumbuka kama alishawahi kukutana na binti Mrembo kama yule au kumzidi tangu amezaliwa,macho yake akabaki ameyagandisha kwa binti yule!
Ghafla nywele zikamsisimka!,mwili ukaanza kumtetemeka,
"Kwa jina naitwa Zena bin Kureysh!"
Sauti laini mfano wa kinanda,lafudhi ya kipwani ikatoka kinywani kwa binti yule!

"Zena Kureysh?!...."

Martin akauliza kwa mshangao,wasiwasi ukiongezeka katika fikra zake
Binti yule akaachia tabasamu jembamba,tabasamu ambalo lilimuongezea uzuri Mara dufu...
"Ndiyo naitwa Zena Kureysh! Kaka vipi kwani au unanifahamu mbona umeshtuka?!"
"No..ha...pa.na..sikufa..hamu" Martin akaongea kwa kigugumizi
Dada yule mwenye asili ya kiarabu akaachia tabasamu tena,bila shaka alitambua udhaifu wa Martin kwake
Ni uzuri wake
Akaachana na jambo lile,akaeleza kilichompeleka
"Ok unaoshaga gari kwa shilingi ngapi?!"

"Elfu tano tu!"

Akatamka Martin kwa haraka
"Ok naomba unioshee naja kulichukua baada ya nusu saa"
Akatamka Dada yule akifungua mlango wa gari lake akashtuka
Macho ya watu wote yakageuka kumtazama Dada yule,alivaa nguo za thamani,Vito vya thamani vilivyoendana na uzuri wake
Dada yule akaenda umbali mrefu alipokuwa mbali na macho ya watu ghafla akatoweka...
Lilikuwa ni jini lililoagizwa....
Liliagizwa nini duniani?!.....
Tuendelee kuwa pamoja

*************************************

ARDHI YA KUZIMU

Ilikuwa ni sherehe kubwa,katika ulimwengu mwingine wa dunia hii
Chini kabisa ya ardhi waloishi wafu walodhulumiwa roho zao
Mizimu,walokuwa na utawala kama wa hapa hapa duniani ila wenyewe waliongozwa na mfalme pamoja na malkia....

Miaka mingi nyuma kipindi cha ukoloni Chrispher akiwa askari wa kikabila aliwahi kuiona hazina ilofichwa na wakoloni wa kiingreza
Kwa kutumia nguvu alojaliwa akaiba kiasi kikubwa cha hazina ile na kuificha katika pori panda
Akaweka ulinzi imara wa kiutamaduni...
Mpaka wakoloni wanaondoka hawakufanikiwa kuiona hazina ile,Chris alifanya siri hata mke wake alijua...

Baada ya wakoloni kuondoka wakasajiliwa katika jeshi la wananchi kipindi icho Chriss alikuwa na watoto wawili Brayson akiwa na miaka 7 na mdogo wake Martin akiwa na miaka 4

Bado aliifanya siri akiogopa kutaifishwa pindi akizitoa Mali zile
Rafiki yake wa pekee John alikuja kufanikiwa kuiona 'diary' iliyoeleza juu ya hazina ile,japo aikueleza mahali ilipo kwa vyovyote alijua mke wake Christopha lazima atajua mahali ilipo

Akaanza kupanga njama za kumwangamiza rafiki yake yule...
Na njama hizo alikuja kuzifanikisha baada ya kupangwa pamoja kwenda Uganda kupigana vita baada ya serikali ya huko kumega kipande cha Tanzania kagera wakisema ipo upande wao
Wakati vita vikiendelea John alimtwanga Chriss bastola ya kichwani
Na kuondoka na uhai wake,jambo ilo liligunduliwa na jeshi na John akafukuzwa jeshini bila mafao yoyote

Tukio lile alilofanya likabaki siri ya jeshi,John akarudi kijijini kwa kuwa alikuwa na dhamira ya kuisaka hazina ile baada ya miaka kadhaa akamuoa mke yule wa rafiki yake alijua anajua mahali alipoifadhi hazina ile!
Miaka ikasonga akiwanyanyasa watoto wale,mpaka Brayson ( jb) akaamua kutoroka baada ya kumpiga mtoto wa Piter mpaka akazimia
Baadaye Martin naye akaja kutoroka akakimbilia dar.

Usikose SEHEMU ya 53.
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu - 53 -

Ilipoishia....

Miaka ikasonga akiwanyanyasa watoto wale,mpaka Brayson ( jb) akaamua kutoroka baada ya kumpiga mtoto wa Piter mpaka akazimia
Baadaye Martin naye akaja kutoroka akakimbilia dar

Songa nayo sasa...

NDIVYO ILIVYOKUWA....

katika sherehe ile katika kiti cha mfalme aliketi jb akiwa mwingi wa tabasamu, pembeni alipepewa na wanamwali warembo walonukia...
Kulia kwake alikwepo kijana mmoja shupavu mwili ulijengeka kimazoezi mkononi alishika mkuki na upinde na kushoto kwake aliketi kijana wa dizaini ile ile
Mbele yake aliketi baba yake Mzee Chriss,naye pia alilindwa kama mwanae...

Walikuwa wakitazama ngoma zilizojipiga huku wadada warembo wakikatika

Ghafla mshereshaji akanyanyua mkono juu na ngoma zile zikagoma
Wadada wale wakainama chini kidogo ishara ya kutoa heshima
Ghafla vilio vya watu wakilia vikasikika!,watu wote wakashtuka kwa jambo lile wakawa tayari kwa kuusubiri ujio huo
Vilio hivyo vikazidi na kuwaumiza masikio na ghafla....

Hali ya hewa ikaanza kubadilika,radi likapiga likitoa mpasuko,upepo mkali ukawa ukivuma na kuepua mapaa

Gharika likatanda katika ulimwengu wa kibinadamu,ndani ya makaburi ya njoro makaburi yalikuwa yakigawanyika na kuacha ufa
Ndani baadhi ya makaburi Yale,vilio vile vilivyosikika kuzimu katika ulimwengu wa wafu
Vilisikika ndani ya makaburi Yale kwa baadhi ya viumbe wenye uwezo wa kuskia

Hata kumomonyoka na kudidimia kwa baadhi ya makaburi Yale laiti kama binadamu na viumbe vyote vingekwepo si wote wangekuwa na uwezo wa kuona matukio Yale
Mpaka uwe na jicho la zaidi,au uwe na uwezo wa ziada...

Makaburi Yale yaliendelea kudidimia ARDHI ikiwabana wafu wale walokuwa ndani yake na kuendelea kuwashusha chini...

Na ghafla wakatokea kule katika ulimwengu wa kuzimu, ulimwengu wa wafu walodhulumiwa roho zao
Ulimwengu waloishi wafu hao mpaka kipindi ambacho MUNGU muumba angeamua kuchukua roho zao na kuzipeleka mbinguni...

Kikawaida mtu akifa kwa kuuwawa au kujiua ni wazi aliidhulumu au kudhulumiwa nafsi yake,
ivyo roho yake uishi kuzimu mpaka pale siku halali alopangiwa na MUNGU ikifika
ndipo usafirishwa kuelekea katika mbingu ya saba na kuweka sahii kabla aijarudi tena duniani na kuwa karibu na maiti au mwili wa marehemu ambapo uifadhiwa katika makaburi na kusubiri parapanda au siku ya mwisho (ya umul kiama) kama matendo yako yalikuwa mabaya mateso utaanza kuyapata huko huko kaburini na kama matendo yako yalikuwa mazuri pepo ( paradiso) utaanza kuipata huko huko

Hivyo basi wale wanaotegemea kuwa makaburini ni mahali pa kupumzika si kweli ndugu zanguni,
Makaburi ni nusu ya pepo na pia kaburi ni nusu ya moto....

Watu wale walopiga mayowe ndani ya makaburi walikuja kutokea katikati ya mkusanyiko wa watu kule kuzimu katika miili yao wakiwa wamefungwa minyororo kama watumwa

Miili yao ilijaa funza na kumomonyoka kama udongo usingeweza kuamini kama watu wale miaka kadhaa nyuma walokuwa watanashati na warembo katika ulimwengu wa dunia
Mfalme mteule jb akaachia kicheko kilichotoka kwa mfumo wa radi na kuacha mwangwi nyuma yake
Ghafla kimya kikatawala,hata MIZIMU ile ilorejea nayo ikanyamaza kulia
Mshereshaji akampa nafasi Jb aongee mawili matatu
"Na shkuru kwa nafasi niliopewa kwanza namshukuru baba yangu Mzee Chriss kwa moyo wake na msaada wake kwangu,mpaka kufanikiwa kuwaangamiza wabaya wangu hawa...
Akawanyooshea kidole viumbe vile vilivyo lala pale chini
...Pili nawashkuru wana kuzimu kwa kuwa na Subira wakati wote nlokuwa duniani kwa kazi maalumu na sasa nimeimaliza na nipo tayari kuwa mfalme wenu na kuwa tumikia kwa kila khali...
Ghafla miguno ikasikika...
Alijua ni miguno ya nini!,akatabasamu na kuendelea...
" ndiyo najua mnachoguna ni juu ya sheria ya himaya hii ya KUZIMU kwamba mfalme lazima awe na mtoto au mke yani malkia atakayerithi ufalme huu ikiwa ntakufa mapema...
"Ndiyoooo"
Mizimu ile ikaitikia...
"Niwatoe shaka kwa ilo na napenda kuwajulisha Mimi sasa ni baba kijacho...."
"Haaaaaaa!"
Mizimu ile ikaguna,wengi walimtambua jb hakuwai kuwa na mpenzi hata rafiki wa kike kule kuzimu sasa anawaambia yeye ni baba kijacho kivipi?!
Jb akawajibu fikra zao...
"Nadhani nyote mnajua Mimi niliuwawa kwa tamaa za Mali na hawa ndiyo chimbuko la yote haya huyu binti ambaye kakondeana...
Jb aliongea kwa uchungu akimnyooshea kidole binti mmoja
" huyu alikuwa mpenzi wangu ila tamaa ya gari na nyumba alohaidiwa na mdogo wangu vikamfanya anisaliti,
Pili huyu Dada mwenzake naye alikuwa mpenzi wa mdogo wangu huyu ndiyo chimbuko la matatizo yote
Alimshauri mpz wake aniangamize ili Mali zote zibaki chini yao,huyu ndiye aliyetoa wazo la kumtumia mpz wangu kuiba nyaraka na hati zote...
Hawa vijana wa nne wanajiita eti 4 killers ndio waloniteka na kuniua kwa kunichoma kisu nami niliwaua hivyo hivyo na huyu babu Jana ndo nimemuua huyu ni rika na rafiki yake baba mchawi mkubwa alomuua baba yangu akatutesa duniani.
Pia nadhani wengi mnajiuliza mbona kuna watu wengine ambao hawapo hapa akiwemo kamishna,Chaka na hata mratibu wa mauaji yote bwana Martin

"Ndiyoooooo"

"Na pia mnataka kujua juu ya mtoto au malkia wangu si ndiyo?..."

Usikose sehemu ya 54...
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu - 54 -

Ilipoishia...

Pia nadhani wengi mnajiuliza mbona kuna watu wengine ambao hawapo hapa akiwemo kamishna,Chaka na hata mratibu wa mauaji yote bwana Martin
"Ndiyoooooo"

#Endelea
"Na pia mnataka kujua juu ya mtoto au malkia wangu si ndiyo?..."

"Ndiyoooooo"
"OK ningependa nianze na swala LA Martin kwanza naomba mtambue Martin ni mdogo wangu wa damu"
Mizimu yote ikaguna,minong'ono ikaanza
"Amemuacha kisa mdogo wake hafai kutuongoza ana upendeleo atukuitaji...

Kelele zikatawala....

Hali ya utulivu ikakosekana ni wazi jb angetakiwa haukumu wote bila upendeleo
Kuwa mfalme ingemaanisha hata katika kiti chake angeongoza kiupendelea

Ni lazima Martin afe kwa kuwa naye aliua tena akiwa mshirika mkuu
Jb akakosa raha....
khofu ikaanza kumtanda,akujua angewajibu nini wananchi wake!...
Macho yake akayagandisha kwa baba yake,baba yake alikuwa kimya,akionekana kuwa katika tafakari kuu...

mshereshaji akaunyanyua mkono wake juu,kelele,minong'ono ile ikakoma,akamwangalia Jb ni wazi alikuwa akitaka atamke neno!,
atoe majibu ya maswali ya wananchi wake wale!

Jb akasafisha koo! na kuendelea...
"ndiyo! najua mwajiuliza kwa nini sikuwa angamiza Chaka,kamishna na mdogo wangu Martin!"
"ndiyooo!"
"kwa sheria zetu za uku kuzimu upaswi kuangamiza asimu ya damu yako! nadhani wote amuijui sheria hiyo itokayo katika familia za kifalme..."
akaweka tuo na kushika kalmati akang'ata na kushika glasi ya sharubati akanywa kidogo na kuendelea...
"ila nimemfilisi kwa kumwambia atoe sadaka mali zangu zote kanisani ametii na sasa ni muosha magari,hiyo nisa babu ilonifanya nimwache hai pili,ni kuhusu baba..."
akaweka tuo tena. na watu wote wakageuza vichwa kumwangalia mfalme wao anayemaliza muda wake...
"nilikuwa na nia thabiti ya kumuua Martin tena kifo kibaya sana,ila baba alizuia hiyo...
ni baada ya kuona kama ningemuua mdogo wangu hazina yake isingepata mtu wa kuitumia mkumbuke mama kashazeeka na mwangalizi mkuu ni Martin japo bado ajafika kijijini,ivyo nilimuachia kazi arudi kijijini akaisake hazina hiyo na kuitumia na mama..."
Mizimu yote ikaridhika kwa jambo lile,Martin kweli alikuwa na haki ya kuishi akimwangalia malkia wao kwa ukaribu zaidi...
Je vipi kuhusu Chaka na kamishna?!
ndiyo lilibaki swali la utata! naye Jb akalijibu kwa ufasaha akianza na komandoo Chaka!
"mkumbuke Chaka alikuwa katika wajibu wake wa kazi!,alotumwa na taifa lake! na nilimwacha kwa kuwa nilimpa onyo akalifatilia na kuacha kunifatilia,mkumbuke Chaka akuhusika na mauaji yangu ila alikuwa akinizuia Mimi kuua na nilipojitoa kwake na kumkanya alinitii je ilo ni kosa wana kuzimu wenzangu
" hapanaaaaaa"
Mizimu yote ikaitika kwa pamoja
"Tuna taka kujua kuhusu kamishna kwa nini umuache hai wakati ndiyo aloshirikiana na Martin kwa ukaribu na yeye ndiyo aliye mwonesha martin kwa mganga Nwalau Nwalau"

Jb akaachia tabasamu pana likifatiliwa na kicheko chembamba sambamba na kuokota kalmati lingine na kumezea na Sharubati akasafisha koo kidogo na kuendelea...
"Nadhani mnakumbuka kauli yangu ya awali kuhusu sheria za huku kwetu kuzimu katika familia za kifalme uwezi kuua nasaba ya familia yako damu moja!"
"Ina maana pia Kamishna ni ndugu yako?!"
"La asha kamishna si ndugu yangu ila nadhani mwakumbuka niliwaambia kuwa kwa sasa Mimi ni baba kijacho,mtoto wake Maimuna ndo kambeba malkia wenu mtarajiwa hivyo kamishna ni baba mkwe wangu sikupaswa pia kumuua"
Mizimu ile ikapiga vigelegele,kufurahia jambo lile
Jb aliwatoa kwenye utata ulogubika vichwa vyao,
Sherehe ya kumsimika ufalme ikaendelea kama kawaida japo kuna kitu kilimuumiza kichwa
Ni juu ya malkia wake Maimuna!
Alitamani sana aishi na mwanamke yule,lakini akujua angeishi naye vipi hali ya kuwa Binti yule alikuwa bado yu hai
Na kuzimu waliitajika wafu tu
Wazo la kumuua likamjia kichwani,akulipinga akaita vibaraka wake wawili na kuwatuma duniani waakikishe wakirudi kwenye ardhi ya kuzimu warejee na malkia yule
Viumbe vile vikatoweka,kuelekea duniani...

***********************************

DUNIANI

KATIKA ULIMWENGU WA BINADAMU

Pale pale binti Yule wa kijini alipotoweka Mara ya mwisho ndo hapo hapo alipotokea
Wapita njia awakuweza kumuona
Alitembea kwa mwendo wa madaa,hakika alikuwa amependeza na uzuri wake uliongezeka Mara dufu ya awali...
Alipofika katika kona ya kuelekea katika 'car wash' ile akajiruhusu aonekane,...
Watu walimshangaa kwa uzuri alokuwa nao....
Kwa upande wa Martin baada ya kumaliza kuosha lile gari akaenda kuketi katika kiti akisubiria gari lingine
Ghafla mawazo juu ya yule binti Mrembo yakamjia akatamani angekuwa naye kimapenzi,lakini tabasamu lake likafifia baada ya kukumbuka hali ya umaskin alokuwa nayo
Laiti kama ingekuwa kipindi chake,kipindi kile akimiliki ma kampuni angeweza kutumia nguvu ya hela kumiliki chombo kile
Kwanza akaguna
Alijua fika chombo kizuri kama kile lazima kitakuwa kimeolewa wazo kwamba kiumbe kile ni jini alikuwepo kabisa
Martin alinasa akanasika
Kwa Mara ya kwanza akauchukia umaskini...
Hamu ya kuinasa hazina ile ikamjia lakini wiki nzima alofanya kazi pale nauli aikumtosheleza kabisa
Hali ilikuwa ngumu,mwisho akayatupia mbali mawazo Yale aloyaona ayatotimia zaidi ya kumfukuzia mteja
Ghafla akamuona binti yule kwa mbali akija
Mwendo wake wa kimadaa,akanata akiwa anamwangalia mpaka alipomfikia Martin akajikuta karopoka
"Zena Kureysh?!"
"Rabeyka"
Akaitika binti yule akimkabidhi noti ya elfu kumi Martin naye akamkabidhi ufunguo
"Ngoja nikupe chenchi"
"Hapana iyo baki nayo"
Martin akashkuru na kuitumbukiza mfukoni
Dada yule akaingia ndani ya gari lake na kumpungia Martin mkono wa kumuaga akaondoka zake
Alipofika kwenye kona AKATOWEKA!!!

Martin kila Mara aliinusa ile ela alopewa akiyanusa marashi mazuri ya binti Yule
Ghafla pikipiki ikaja akashika tenda ya kuiosha ikabidi ile 10000 aiweke mfukoni akaiosha fasta ile pikipiki na baada ya hapo ikaondoka
Bado kumbukumbu juu ya binti yule zilimtesa akatamani kunusa manukato yake
Akaingiza mkono wake mfukoni
Akatoka na bahasha
Mshangao ukamshika
10000 aikwepo akatafuta mifuko yote akuiona
Akazidi kuchanganyikiwa
Na vipi kuhusu ile bahasha akaiangalia vizuri iliandikwa jina lake kwa mwandiko mzuri kupindukia
Akukumbuka kama alipokea bahasha ile kwa MTU
'Sasa imefikaje katika mfuko wake?!'
Akajiuliza swali pasina jibu sahii
Ikamlazimu aifungue
Ghafla akatoa macho Pima,mdomo akauachama wazi,butwaa likambumbukia,mikono ikaanza kumtetemeka,nywele kumsisimka....

Kwak Martin!

Bila shaka u mzima,nafrah kwa ilo!...
Najua unashangaa juu ya barua hii ya kimaajabu ajabu usishangae kwa ili!
Dhumuni la barua hii ni kikueleza juu ya upatikanaji wa hazina ya marehemu baba yako

Usikose - 55 -
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom