Simulizi: Mzimu uliorejea

Simulizi: Mzimu uliorejea

bioto

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2017
Posts
1,261
Reaction score
2,099
MZIMU ULIOREJEA.

Sehemu ya 01.

Sayid Mwenny.

Upepo mkali ulivuma ulioambatana na radi sambamba na mvua kubwa iliyonyesha kwa hasira katikati ya Mji wa Moshi, mkoani Kilimanjaro.
Angani hakukua na nyota iliyong'aa wala mbalamwezi kusawazisha nuru katika ulimwengu ule.
Kila mmoja alijifungia ndani ya nyumba zao akiwa usingizini, lakini wengine usingizi uliwapaa wakasikizia dhoruba iliyokua ikiendelea ndani ya nyumba zao.

Miti ilidondoshwa, dhoruba ilitawala na baadhi ya nyumba bati zao ziling'olewa huku kutwa zikidondoshwa na viumbe waliomo katika nyumba hizo kuwa katika hatari ya kupoteza maisha kabisa.

Kila mmoja alikuwa akijaribu kuokoa uhai wake.

Katikati ya jiji lile lile katika jumba moja la kifahari walioko katika nyumba hio hawakuguswa kabisa na dhoruba ile kutokakana na uimara wa ile nyumba yao.Waliichukulia mvua ile kama mvua nyingine iliyowapa starehe katika usingizi wao.

Hali ya makaburini pale haikua tofauti na hali ile ya katikati ya jiji. Mvua ilioambata na radi ilikua pia ilinyesha katika eneo lile la makaburi.
Mlinzi aliyekua anajulikana kwa jina la Kipele alikua mita kadhaa akitetemeka kwa kupigwa na mvua ile katika geti la kuingilia katika makaburi yale palipopendezeshwa na uzio uliotengenezwa kuzunguka eneo lote la makaburi yale.

Hakukua na sehemu nzuri ya kujibanza kukwepa dhoruba ile. Alishudia baadhi ya miti ikidondoshwa na kumtisha kabisa kuenda kusimama karibu ma miti ile. Akabaki kajikunyata akitetemeka kuikubali hali ile.

Mita kadhaa mbele kutoka geti la mlinzi mpaka katikati ya makaburi, palikua na kaburi moja ambalo lilikua limejengewa kifahari. Juu ya kaburi lile kulikua na kibao kilichoandikwa jina la __JACOB MSAKI__kwa kunakshiwa tarehe yake ya kuzaliwa pamoja na siku aliyokufa.
Juu ya kaburi lile kulikua na msalaba wa dhahabu.
Katika kaburi lile ghafla mtetemeko ulianza.Ulikua n mtetemo mdogo ambao ulikua katika kaburi lile tu. Ulikua n mtetemo uliowacha nyufa na kuanza kumomonyoa kaburi lile. Mara ghafla vumbi kutoka ndani ya kaburi lile likaanza kutoka.
Ilikua ajabu,. Lilikua ni vumba ambalo halikua na hata chembechembe ya tope likapanda kuelekea juu.
Mara ghafla jeneza la kifahari likatoka, pamoja na kwamba lilikua limeoza, pengine kwa kuwa lilifukiwa muda mrefu,lakini uzuri wake ulikuwa bado unaonekana waziwazi.
Baada ya kupanda juu likatua pembeni mwa kaburi lile. Ghafla mlango ukafunguka na mtu wa ajabu aliyekua ndani yake akaonekana. Ni wazi kabisa mfu alikua kafufuka kiajabu.
Kiumbe cha ajabu kilichooza na kutembelewa na mifinyifinyo katika suti iliyovubaa kilikua kinatoka katika kaburi lile.

Kumbe kile kikaingia duniani kwa jicho baya. Jicho lenye mng'ao uliotisha pindi kiumbe hai kingine kama kingepata bahati ya kuliona. Ghafla kikaachia tabasamu pana. Meno yaliyooza na mengine kutoboka yakaonekana na moshi mzito ukatoka katika domo lake.

Bado mvua ilikua inaendelea kunyesha sambamba na radi za hapa na pale lakini jitu lile halikushtushwa kabisa na hali ile ya mvua.
Maji ya mvua yalimlowanisha na kumwongeza nguvu ya furaha ya kuingia katika ulimwengu wa dunia hii waishio viumbe aina ya bin-Adam.
Jitu lile likanyoosha mkono mpana katika jeneza lile na ghafla shoti ikatoka kuliendea jeneza.
Ghafla jeneza likatoweka sambamba na eneo lile kusawazika pakawa kama mwanzo.
Jitu lile likaachia muayo mkubwa ulioambatana na radi ambao ulimfikia mlinzi getini na kuchukulia radi lile kama maradi mengine yaliyokua yanaendelea kupiga eneo lile.
Jitu lile likanyoosha mikono juu na kuachia cheko la dharau na kisha kutoweka katika eneo lile.

Katika nyumba ile ya kifahari ambayo wenyeji wake walikua wamelala fofofo, nje ya jumba lile palizuka jambo. Kilikua n kitu ambacho dakika chache nyuma kilitokea katikakati ya makaburi mjini Moshi. Lilikua ni jitu lile la kutisha. Likaangalia kushoto na kisha kulia likaachia tena cheko kubwa.
Lilikua ni cheko liilochukuliwa kama radi kwa waliobahatika kulisikia katika usiku ule mzito ambao ulikua n usiku wa manane.
Jitu likanyanyua mkono wake wa kulia juu na ghafla shoti za umeme zilizoambatana na radi zikatawala. Ghafla bisu lenye kumeremeta likatoka katika kono lake na kisha jitu lile likaachia cheko jingine na kisha likatoweka.

Ndani ya jumba lile katika chumba kimoja kipana walilala watu watatu. Mtu wa makamo pamoja na mtoto wao mdogo. Na wote walilala fofofo bila kushtushwa na mvua ilikua inanyesha.
Ghafla katika pembe ya kuta za nyumba ile likaibuka jitu. Lilikua ni jitu lilelile. Likamwangalia mwanaume aliyelala pale kwa dharau, likamnyoshea mkono ishara ya kumnyonga na mtu yule akawa anachezeshachezesha miguu ishara ya kutapatapa. Na si kwamba mtu yule aliyekua amelala hakua analiona lile jitu.Hapana.Ndani ya usingizi ule aliliona jitu lile na jinsi lilivyokua likimnyonga. Na ni wazi kabisa siku hiyo ndo ilikua mwisho wa maisha yake. Ni kweli asingeweza kusalimika kabisa.
"NILIAPA KUWAMALIZA KWA HIKI KISU, KWAHIVO SITOKUNYONGA"Jitu lile liliongea likinyanyu kile kisu juu likakishusha kwa nguvu kuelekea tumboni kwa yule bwana. "TUTAONA KUZIMU, MWANAHARAMU WEWE" Jitu lile lilitamka na kukishusha kisu kile katika mwa mbavu za mtu yule. Damu zikaruka na jitu lile likatoweka likiuacha mwili ulioharibika vibaya katika kitanda kile.
Mke na mtoto walilala fofofo na bado ilikua ni katikati ya usiku mnene.

Na huu ndio mwisho wa sehemu hii ya kwanza kabisa wa simulizi hii nzuri ya maisha iitwayo "MZIMU ULIOREJEA"
 
MZIMU ULIOREJEA..

Sehemu ya 02.

Jitu lile baada ya kutoweka pale lilikuja kutokea barabara ya juu iendayo stendi,pembezoni ya barabara ile palikuwa na kituo cha bodaboda,ambapo pembeni palikuwa na mabenchi yalochimbiwa.
Pembeni ya kituo kile cha bodaboda usiku ule jitu lile lilipoibukia eneo lile hapakuwa na mtu kwenye mabenchi yale,kilikuwa ni kijiwe cha kahawa jioni,mchana wasafiri wakikaa kusubiri daladala za kuelekea stendi ,kituo hicho na stendi palikuwa na umbali tu mkubwa
Jitu lile likakaa katika benchi lile,likifikiria jambo hili na lile.
Hisia za machozi yakitawala katika nyuso zake,ghafla akakumbuka kitu,kitu kilichomzidishia hasira akajinyanyua na kwa haraka akaanza kuelekea upande alojua yeye mwenyewe.
Roho ya kikatili ikitawala mawazoni mwake
**************

SHANT TOWN
MOSHI
Lilikuwa ni jumba jingine la kifahari,ukutani kulizungukwa na nyaya maalumu za ulinzi,getini kulikuwa na walinzi wawili kifuani walikuwa na silaha nzito za kivita wakipiga story.
Ghafla nyuma ya nyumba ile kikasikika kishindo bila kujiuliza Mara mbili mlinzi mmoja akiwa kashika silaha yake vizuri akatoka eneo lile kuelekea kule kishindo kiliposkika mlinzi mmoja akibaki katika geti lile akiwa kashika silaha yake tayari kwa chochote.
Ghafla kishindo kingine tena kikasikika sambamba na yowe,yowe lile likamsukuma mlinzi yule aliyebaki pale getini kuelekea kule nyuma alipoenda mwenzake.

Kosa!!!
Hakuamini kile alichokiona,mwenzake alichomwa bisu la koromeo macho kayatoa Pima,mlinzi yule akapepesa macho lakini akuona alosababisha taharuki ile
Mshangao ukamvaa!
Bumbuwazi likambumbukia!
Wasiwasi na uwoga ukamtawala!
Kwa kihoro akamkimbilia mwenzake na kuanza kumwita
"Dully,Abdull, nini kimekupata swaiba,"
Akawa akimtingisha kwa nguvu,ghafla akasikia cheko nyuma yake.
Mlinzi yule akageuka,mshtuko kwa kile alichokiona ukamtawala,macho yakamtoka pima,silaha ile nzito ya kivita ikamponyoka,ika
dondoka,Kwa uwoga akiwa akirudi nyuma
Jitu lile la kutisha lilikuwa Mbele yake likimwangalia kwa macho makali,macho yalomtisha mlinzi yule,bisu lenye mpini mpana,na ncha Kali likiwa katika kono lake lenye vinyweleo vya kutosha.

Liliachia tabasamu meno yake yalooza na kutoboka yakaonekana.

"Mliniua kwa mateso makali sana,ila Mimi sitokwangamiza hivyo nimerejea kwa ajili yenu tutaonana kuzimu mwanaharamu wewe"

Jitu liliongea kwa jeuri huku likipiga hatua kumfata mlinzi yule,wazo lililomjia kijana yule ni kupiga kelele lakini hakupata muda huo kwani akujua ni sangapi jitu lile lilimfikia na kumchoma bisu lile la koromeo kama mwenzake, mlinzi yule akadondoka kama zigo na kutapatapa,akatulia tuli.
Jitu likaivuka miili ya walinzi wale na kutokea Mbele ya lango la jumba lile,likazama ndani.
Alipoufikia mlango mkubwa wa kuingilia ndani ulofungwa akanyooshea kono lake mlango ukatii amri ya kufunguka,jitu likapita na mlango nyuma ukajifunga kama awali.

****************

Bado mvua ilikuwa ikinyesha,ila kidogo ilipunguza makali,jitu likaibuka chumbani katika jumba lile LA kifahari alosababisha mauaji nje ya walinzi wawili,macho yake yakatua kwa kijana alolala akikoroma katika kitanda kile ,kisha kwa mke wa kijana yule alovaa kipande cha kanga katika maungo yake
"Fatuma binti mrembo"
Akaita kwa sauti ndogo ya kunong'oneza,sauti ilopenya mpaka katika maskio ya binti yule ghafla akafumbua macho yake
Ana kwa ana na jitu,bisu mkononi
Binti yule akashtuka.

"Kweli wew ni binti mrembo skatai,nyumba hii ndo ilikufanya unsalitii eeh?!!!...c ungenambia unaitaji nyumba? Siwezi kukuacha mzima tutaonana kuzimu mwanaharamu wewe!"
Wakati wote binti yule alikuwa akipikicha macho yake akihisi pengine yupo ndotoni.
Jitu lile lililotoka makaburini usiku ule mnene wenye mvua na gharika za kutisha
Binti yule akabaki ameganda kama sanamu,akishindwa kupiga kelele wala kufanya chochote.
Hatua moja akapiga na hatua jingine akawa kamfikia binti yule akanyanyua bisu lake akamchoma moja kwa moja tumboni,binti akafa akiwa katoa macho na ulimi kaung'atia.

Jitu likatoweka!!!

Likijua kabisa litaacha taharuki pindi mume wa binti yule akiamka na kukuta maiti ya mke wake.

Kizaazaa!...

ITAENDELEA...
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu_ 03_

SAA 11 ALFAJIRI

Mvumo wa sauti ya simu yake ilimshtua katika usingizi wake.
Akajinyanyua na kuikwapua simu ilikuwa kitandani pale akuangaika kuangalia mpigaji kutokana na kumtambua kutokana na mlio wa simu yake alomsetia.
"Kuna mauaji ya kikatili yametokea usiku huu waitajika ofisini haraka sana dakika tano uwe umefika inspekta"
"Ovar kamanda"
Kijana yule alojulikana kama Inspekta NURDIN aliitika sambamba na kuamka hari ya kufanya kazi ikiwa imemtawala,akajimwagia maji haraka na kutoka katika nyumba ile ya kota,mpaka katika kituo chake kidogo cha kazi ofisini akukuta askari yeyote alowasili,ilo akujali macho yake yakatua katika lango LA mkuu wake,mlango ulikuwa wazi kumjulisha kuwa mkuu wake alikwepo akachepuka kuuendea lango ilo
Akajiingiza ndani kwa tabasamu pana,
"Duh hii serikali ya magufuli inafanya kazi vizuri mkuu unaogopa kutumbuliwa unawahi kazini hivi ama kweli hapa kazi tu"
NURDINI aliongea kwa utani,tabasamu likipendezesha uso wake mdogo,tofauti na matarajio yake bosi wake yule akucheka wala kumwangalia macho yake yalikuwa bize katika kalabrasha (file) alilokuwa akiliandika alipomaliza akanyanyua kichwa chake na kumtazama kijana wake yule ambaye alikuwa kimya mzee yule wa makamo mwenye mvi nyeupe kichwani akakohoa kidogo kusafisha koo
"Kama dakika kumi zilizopita nimepokea simu mbili tofauti mauaji ya aina moja yametokea yani walouwawa wamepigwa visu vya makoromeo...."
"What?!!!...."
"Yah na visu vyote ni vya aina moja kutokana na maelezo ya waloripoti tukio kushangaa aina hiyo ya visu naitaji kutuma madaktati na maaskari kwenda kuichukua hiyo miili kwa ajili ya uchunguzi LA kini kabla sijawatuma naitaji wewe uende kama afisa upelelezi mchunguzi na wewe ndo nakukabidhi file ili ripoti ipitie kwangu sawa?!"
"Yes mkuu alitika inspekta yule akilipokea file lile na kupiga saluti moja kubwa na kugeuka kuondoka akaelekea katika ofisi yake na kufungua droo akaliweka file lile na kutoka na kajikitabu kadogo alikiweka ndani ya kabegi chake na kuingia ndani ya gari lake tayari kwa kuelekea eneo la tukio huku nyuma mkuu yule wa kituo akapiga simu hospitalini,wakatoka baadhi ya madaktari katika ambulance na kuelekea eneo la tukio,mkuu yule pia aka wahitaji baadhi ya maafande waelekee eneo La tukio kuchukua miili ile.akijua fika inspekta NURDIN atakuwa kashawasili eneo la tukio kwa uchunguzi kabla

***********

Mke wa Ragiv Kumar alifumbua macho yake taratibu na kuupeleka mkono wake katika mwili wa mume wake akagusa kitu katika mwili wa mumewe
Akashtuka na kupeleka mkono wake katika godoro alipokelewa na unyevu nyevu,mwanzo alihisi pengine ni mvua ila tangu lini mvua ikaingia chumbani mwao ikambidi apeleke mkono wake katika swichi na kuiwasha taa ya chumbani mule
Kitu alichokiona kikamfanya mama yule wa kihindi aachie yowe moja na kutulia tuli akiwa kanyooka,macho ya mshangao akiwa kayatoa Pima
Kelele alopiga ikamwamsha mtoto aloanza kulia kwa nguvu mpaka vyumba vya jirani vikasikia wakasogelea chumba kile cha wazazi wao na kuanza kukigonga bila kuitikiwa mwisho wakakata shauri kukivunja awakuamini walichokikuta hatua ya kwanza ni kupiga simu polisi alipopokea mkuu wa kituo kile kidogo cha MOSHI mjini na kuahidi kutuma maaskari muda ule mkuu yule wa kituo kile alishapata taharifa ya mauaji mengine ya binti na mengine ya walinzi na bosi wao yote yakiwa ya aina moja,ndipo alipompigia kijana wake NURDIN na kumwelekeza maeneo Yale kabla maaskar wengine hawajawasili.ilikuwa ni bado saa kumi na moja kasoro alfajiri.

KATIKA NYUMBA ILE ILE YA KIFAHARI.

Alionekana kijana mdogo akishuka katika kitara cha polisi,ajabu akuvaa sare za jeshi akiwa na kabegi chake mgongoni akauendea mlango wa nyumba ile ndani kulikuwa na watu wengi,vilio vikiskika ilo akujali akaenda mpaka chumbani walipomaiti alipofika alijitambulisha na kuomba watu wasogee afanye uchunguzi wake,kabla ajafanya kitu akamulikwa na mwanga wa kamera inspekta akashtuka na kumgeukia alopiga akakutana na tabasamu pana LA binti mrembo mkononi akiwa kashika kamera na kabla inspekta yule ajafanya kitu Dada yule kwa wepesi wa ajabu akapiga tena picha mbili
"Ooh shit binti unafanya nini?!"
Akalalamika NURDINI macho yake yakiwa kifuani kwa Dada yule palipokuwa na kitambulisho cha kazi
Mwandishi wa habari,mnoko
Akalalamika NURDIN
"Nakukabidhi kesi hii kwa kuwa nahisi inautata ndani yake,usiruhusu mwandishi yeyote wa habari kuchukua tukio ili kwa kuwa likitoka katika vyombo vya habari litasababisha woga kwa wananchi...nakuamini na sitegemehi kama utaniangusha.....
Kauli hiyo ikajirudia katika kichwa chake,kumbukumbu pindi alipoambiwa na mkuu wake pindi alipokabidhiwa kalabrasha lile,macho yake yakarudi kwa binti yule wakatazamana akaanza kupiga hatua kumsogelea kama binti yule alijua lengo la inspekta yule akachoropoka katikati ya watu na kupotea eneo lile
Kwa kuwa muda uliikuwa umeenda NURDINI akaachana naye na kuendelea kuchunguza maiti zile na eneo lile kiujumla (survey) kabla maaskari wengine awajaja
Akiuliza maswali haya na Yale huku aloyaona yanafaa akiyaandika katika kajikitabu chake
Pamoja na yote alishtushwa na kitu kimoja aina ya kile kisu na uchomwaji wake
Kila alipoviangalia aliguna aliikumbuka sura flani katika tukio flani maeneo flani
Yah! Ni sura ya jitu ilimjia akilini,kivipi?!
Alishindwa kujielewa akabaki na butwaa,ghafla wakaingia maaskari wengine na daktari
" naitwa daktar SAMSON MGHONJA ndiyo daktari nlochaguliwa kuichunguza miili hii"
Daktari yule akajitambulisha
"Naitwa inspekta NURDIN ndiyo mpelelezi mwandamizi wa kesi hii ripoti zote naitaji zifike kwangu"
Akaongea inspekta yule naye dokta akatabasamu kuafikiana naye
NURDIN akaaga akiwaacha polisi wale wakiendelea na upelelezi wao mdogo yeye aliitaji kufika eneo lile LA pili ambalo walinzi waliuwawa ndani mwanadada alikuwa kifo cha kikatili...
Kwa mwendo wa gari yake alifika eneo lile wakati akiwa katika harakati za kuingia ghafla akampiga mtu kikumbo MTU yule akadondosha kitu,kwa haraka akainama kuokota na kumwangalia yule alompiga kikumbo
Wote wawili wakapigwa na butwaa
Alikuwa ni yule mwandishi wa.

JE NINI KITAENDELEA?!,JITU YUPO WAPI KAMALIZA SHUGHULI YAKE HUYO BINTI MWANDISHI WA HABARI JE?!

INSPEKTA NURDIN SURA YA JITU IMEMJIA KIVIPI, JE HATAMTAMBUA??!

Usikose sehemu_04_
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu_04_

Kwa mwendo wa gari yake aina ile ya kitara cha polisi,alifika mapema eneo lile,akapokelewa na umati mkubwa wa watu nje ya nyumba ile wakishangaa maiti zile za walinzi.
Akaenda kwenye watu akazipiga maiti zote picha na kuanza kuchunguza eneo lile kwa umakini akiwa amevaa gloves alikichomoa kisu kile katika mwili ule na kuanza kukichunguza
"Ndiyo chenyewe"
Akajiwazia na taratibu kuondoka eneo lile kuingia ndani akiziacha maiti zile pale pale
Wakati akiwa katika harakati za kuingia pale getini akampiga mtu kikumbo mtu yule akadondosha kitu (kamera) kwa haraka NURDIN akainama kuiokota na kumwangalia yule alompiga kikumbo
Wote wawili wakapigwa na butwaa
Alikuwa ni yule mwandishi wa kike
"Naomba camera yangu"
Yule Dada aliongea kishari zaidi
"Haya matukio hayatakiwi kuripotiwa na vyombo vya habari binti ni usalama wa taifa....
Aliongea NURDIN lakini pasipo kutegemea binti yule alijigeuza kwa wepesi wa ajabu na kurusha konde zito,kabla inspekta ajakaa vizuri akaukamata mkono wake na kuuzungusha kidogo
Inspekta akaiachia kamera ile,Yule Dada akapiga hatua kukimbia,akajichanganya na watu na kutoweka eneo lile
Mshangao aloupata NURDIN aukuelezeka,kwa unyonge akapiga hatua kuingia ndani akiacha taharuki eneo lile.

****************

SAA MBILI KAMILI ASUBUHI.
Gari LA kifahari aina ya RANGE lilipakiwa eneo LA parking akashuka kijana mrefu maji ya kunde.
Alikuwa kavaa suti nyeusi ilomkaa vyema akaanza kupiga hatua kuelekea eneo la ofisi ile
Ilikuwa ni kampuni ya kusafisha,na kusafirisha,pamoja na kupima madini
Bwana MARTIN KYANDO mkurugenzi wa kampuni ile ndiye alikuwa kashuka katika range ile na kuelekea katika ofisi yake
Alikuta vijana wake wakiendelea na kazi kama kawaida alifarijika sana kwa kuona vijana wake wakiwahi kazini mapema.
Akapita mpaka kwa katibu muhtasari wake, wakasalimiana kwa bashasha naye akazama ofisini kwake
Akakaa katika kiti na kuanza kupitia
Magazeti ya siku hiyo
Mngurumo wa simu yake ukamshtua na kuichukua simu yake akaipachika sikioni
Akashtuka kwa habari aloipokea toka upande wa pili,macho yakamtoka Pima
Ni juu ya vifo vile vilivyotokea usiku wa siku hiyo,mauaji ya kikatili kwa watu alowafahamu kabisa,akajinyanyua na kutoka pasina kuelewa
anaelekea wapi
Katu akujua kuwa yupo katika ( target ) ya jitu
Kiumbe hatari alosababisha mauaji Yale na kiumbe alobakia katika orodha yake ni yeye
Alikuwa akielekea hospitalini zilipo hifadhiwa maiti zile
Zilikuwa ni za watu wake wa karibu
NURDIN yabiashara wenzake
"Ni kipi kilichotokea MUNGU wangu"
Alijiwazia akipiga break katika hospitali ile ya mawenzi
Wake na ndugu wa marehemu walikwepo eneo lile walikimbia na kumkumbatia MARTIN
Huku wakiwa wanalia,japo yeye alikuwa ni mwanaume tena mwenye roho ngumu lakini alishindwa kuvumilia kuyazuhia machozi yasimtoke
Waandishi mbalimbali wa habari walikwepo wakiuliza ili na lile
INSPECTA NURDIN pia alikwepo eneo lile,kwa uchunguzi maalumu,kila Mara alitupia macho yake maeneo walikwepo waandishi akitegemea kumuona yule binti bila mafanikio
Yule binti atakuwa ni NANI?!,na kwa nini atumie ubabe kwa askari kuichukua camera na nani alomwambia juu ya tukio hill akawah eneo LA tukio kabla yangu?! Hapana kuna kilichopo nyuma ya pazia kwa binti yule lazima ni msake alafu na kisu kilee!!!....ebu ngoja
Aliwaza NURDIN na kuchepuka kumsogelea JACOB alokuwa bado akiwafariji wafiwa
"Sorry,tunaweza kuzungumza?!"
Alitamka NURDIN na kupelekea kijana yule amwangalie inspekta kwa mshangao,inspekta akamtolea tabasamu kumwondoa wasiwasi
Ila bado JACOB hakuwa na amani wakajisogeza pembeni
"tunaweza kuelekea kituoni na mazungumzo na wewe!"
"Mimi?!!"
"Yah wala hata usijali ni mazungumzo ya kawaida"
Wakaingia ndani ya gari na kuelekea kituoni kwa maojihano
Ilikuwa ni tayari saa nne na madakika asubuhi.

**********

SHARFIA ZUBERI mwandishi wa kujitegemea aliingia hofisini na kwenda moja kwa moja mpaka kwa bosi wake
"Hii habari ya leo sijui mtanlipa shi ngapi kwa maana nimempiga inspekta kwa unyeti wake,na ni lazima ichapishwe Leo leo"
Aliongea binti yule akitabasamu mwariri mkuu wa gazeti lile akaipokea kamera ile na kuanza kuzikagua picha zile
Macho yakamtoka Pima kwa kuto kuamini akionacho
"Ni SAA moja saiv naitaji kwenda hospital ilipoifadhiwa miili kama vipi nipe changu nisepe kabisa"
"Hapana Shary ni hatar wewe kwenda tutamtuma mtu hospitalin kumbuka wewe sasa unasakwa"
"Oooh come on nilishasahau ila poa babake peleka katika machine hizo picha nkalale saivi"
Mwariri yule mkuu akujibu kitu akafungua kabati na kutoa burungutu akamkabidhi
Dada yule akazihesabu zilikuwa ni milioni sita akatabasamu na kuondoka eneo lile
Masaa manne baadaye yani SAA tano habari ile ilikuwa katika gazeti La adhuhuri litokalo siku hiyo hiyo.
Ikawa taharuki katika taifa hili Dogo,TAIFA likazizima kwa habari ile
Mkuu wa kituo kikuu cha MAJENGO akashika simu yake na kumtwangia NURDIN huku akiwa na hasira kwa kuvuja kwa habari ile.

ITAENDELEA
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu_05_

KITUONI

Inspekta NURDIN aliketi kwenye kiti chake,mkono wake ukiwa bize kuandika baadhi ya vitu alivyogundua katika file lake
File alilokabidhiwa na mkuu wake wa kituo,macho yake ya katua kwa kijana alokaa katika kiti cha wageni ofisini kwake
Akaufungua mdomo wake ulotoa sauti yake ndogo ya upole ilobeba maswali ya mtego kwa aulizwaye
"Pole bwana Martin Kwa kuwapoteza rafiki zako wa karibu ila JE una we za ukajua au hata kuhisi tu sababu au muhusika wa vifo vyao?!"
Martin akatingisha kichwa kukataa kujua sababu,ni kweli akuitambua sababu hiyo bado alikuwa katika fumbo ambalo kwake ilikuwa ni vigumu kufumbuka.
NURDIN akafungua droo na kutoka na kisu,ni sample na vile visu vilivyokutwa katika makoromeo ya maiti akamkabidhi kijana yule MARTIN Akakipokea na kukitazama
"Kila ukionapo icho kisu huwa unakumbuka wapi?!"
Martin akakipokea kile kisu na kukitazama kwa makini, huku macho ya inspekta wa jeshi LA polisi yakimwangalia kwa ukali na kwa udadisi wa hali ya juu
Ghafla simu ya NURDIN ikaita,kwa mlio alousert wa mkuu wake akapokea
"Unafanya nini NURDIN nilikwambia nini lakin?!"
"Kwani ni nini mkuu?!,..."
"Akuna cha nini nakuitaji ofisini haraka na gazeti LA hadhuhuri"
"Ovar"
Simu ikakatwa,kukatwa kwa simu ile na kutajiwa gazeti LA hadhuhuri kukamkumbusha juu ya binti yule
Binti mwandishi alomponyoka katika mazingira ya kutatanisha
Macho yake yakatua kwa MARTIN aliye kuwa kakishikilia kile kisu akiwa mbali kimawazo
Alimkumbuka jitu....
"*"***"
SURA YA PILI
MIAKA MITANO NYUMA
MACHIMBONI MKOANI ARUSHA
"Mama klare naomba ugali mkubwa nikapige kazi"
Aliongea kijana mmoja mrefu mwenye mwili ulojengeka kimazoezi,baada ya kuingia katika kibanda kile cha mama ntilie kilichopo eneo lile la machimbo
"Bora hata umekuja babaa!,nikukabidhi huyu kijana mwenzako alokuja kutafuta maisha huku mererani"
Aliongea mama ntilie yule,macho yake yakiwa kwa kijana alokaa pembeni yake,alikuwa ni kijana mtanashati kizazi cha sasa huwaita masharobaro
Kijana yule aloingia akamkatia jicho kijana yule alomkuta akamzawadia tabasamu, na kijana yule wakuja akalijibu
"Kwa jina naitwa JACOB AU JB kwa kisasa zaid cjui wewe mlugaluga unaitwa nani?!"
Kijana yule alokuja kuagiza chakula akajitambulisha
"Naitwa MARTIN natokea DSM nimekuja huku MOSHI kutafuta maisha"
Wote walokuwa wanakula wakaangua vicheko,MARTIN akaangalia chini kwa aibu
"Huku si MOSHI ni ARUSHA,na upaswi kusema umekuja kutafuta maisha sema nimekuja kutajirika fala wewe"
JB akamsahihisha,martin alishangazwa na jinsi kijana yule alivyokula,ugali kilo moja alimaliza mwenyewe.ndo maisha ya mgodini baada ya JB kumaliza kula akajinyanyua na kumwambia MARTIN amfate
"Mwanzo utateseka sana,una budi kuvumilia utakaa na sisi akuna atakaye kunyanyasa katika balo letu tupo wa wili Mimi na mshkaji wangu wewe utaongezeka wa tatu kama nyoka kazi yako ni kupandisha mchanga wenye madini juu mkiwa wawili na tolu au na Mimi wakati mmoja kati yangu Mimi na tolu akiendelea kupasua miamba utazoea tu dogo"
JB alitoa maelezo marefu ambayo MARTIN aliyaelewa
Walipofika kazini MARTINI akavalishwa tochi kichwani akavalishwa na kifaa flani cha oxygen na kufungwa kamba JB naye akavaa hivyo hivyo na wakaanza kushika kuelekea chini,walipofika chini kulipokuwa na giza wakaanza kuelekea lilipo balo lao walipofika walimkuta kijana mmoja alokuwa kifua wazi jasho likimtiririka mkononi akiwa na nyundo kubwa akipasulia miamba alipowaona akasitisha zoezi lile
"Tolu nimemleta nyoka huyu tupige naye kazi"
MARTIN aliongea akimwangalia yule walomkuta
"Kwa jina naitwa ZUBERI karibu"
Kijana yule akajitambulisha, muda ule ule bila kuchelewa akashika nyundo yake na kuendelea na kazi
"Kusanya huu udongo wote pamoja"
"Sawa kak..."
Kabla ajamaliza kauli yake kwa ghafla ZUBER alimgeukia na kumtandika teke LA mbavu,MARTIN Akapepesuka na kudondokea mwamba ulochongoka na kutengeneza ncha Kali
Damu zikaanza kumtoka
Akatulia tuli,bila kujitingisha huku damu ikizidi kutiririka
"ZUBERI umeua"
JB akaongea kwa kubwabwaja macho kayatoa Pima,akiuangalia ule mwili kwa woga.

JE MARTIN KAFA?!,MZIMU KATI YA HAO WA TATU NI YUPI NA KWA NINI ALIGEUKA MZIMU NA KUJA KUUA?!

Usikose ya 06.
 
MZIMU ULIOREJEA

sehemu -06_

ZUBERI alimgeukia Martin na kumtandika teke La mbavu,Martin akapepesuka na kudondokea mwamba ulochongoka na kutengeneza ncha Kali damu zikaanza kumtoka,akatulia tuli bila kujitingisha huku damu zikizidi kutiririka,
"ZUBERI umeua...."
JB huku akiwa na wasiwasi,aliongea huku macho akiwa kayatoa Pima akiuangalia ule mwili pale chini kwa uwoga
Songa sasa
Wakati wote jb alokuwa akiteteneka,Uso wa ZUBERI ulikuwa wa kawaida
JACOB alimfata MARTIN pale chini na kumuinamia alimsikiliza mapigo yake ya moyo yalikuwa yakidunda kwa mbali
"Sasa umefanya nini ZUBERI"
JB akamuuliza ZUBER kwa ukali akiwa kamtolea macho ya hasira
"No swaiba nilikuwa namkaribisha jombaa kilingeni....
ZUBERI akuweza kumalizia kauli yake JB alimvamia na kuanza kumshambulia mangumi,na mateke mpaka watu wa balo lingine ndo walokuja kuamua ugomvi huo
ZUBERI alikuwa kajeruhiwa vibaya sana usoni damu zikimchuruzika
Uongozi wa mgodi ule,ikabidi iwapandishe wote juu wakatibiwe kwanza
Baada ya masaa kadhaa wote wakawa katika hali nzuri,wakarudi chini ya ardhi hayo ndo yalikuwa maisha yao,ubabe,ukatili,ili mradi maisha yasonge
Kule chini ya mgodi ilikuwa ni kama kuzimu,kwani njia ya kuingia Chini ulipo mchanga wenye madini ilikuwa ni ndogo sana,walilazimika kutambaa kama nyoka kwa wakusanyaji,huku kukiwa na hewa isiyotosha
Walipokusanya wakutosha waliupakia katika viroba na kupanda navyo juu kwenda kuumwaga wakipokezana taratibu.
Siku zikasonga,MARTIN akaanza kuzoea hali ya kule,na pesa akaanza kuzikamata,
Walikuwa ni vijana wa tatu walopendana,ilipofika jioni walienda club wote,walitokea kuwa marafiki wakubwa
Kila alipo onekana MARTIN alionekana JB,na kila alipo onekana JB alionekana ZUBERI
Siku hiyo wakiwa bar jioni baada ya kutoka machimboni ZUBERI akatoa wazo lake
" muda wa kuwa matajiri milioneya sasa umewadia...."
Aliongea ZUBER akainyanyua glass yake ya bia na kupiga nguchu moja akaiweka chini
"Kivipi kaka ZUBERI?!"
MARTIN kwa shauku alihoji
"Mimi nipo muda mrefu sana hapa mgodini!,nimekuja huku kabla yako wewe JB,na pia nimekuja kabla yako we MARTIN"
Akanyanyua chupa yake na kumimina bia katika glass yake kisha akaendelea
"Siri nyingi sana za huku nazijua!,ili kama tunataka tutajirike balo liteme hatuna budi kumwaga damu!,damu ya mtu....
Aliongea ZUBER kwa kujiamini!,
Tofauti na mategemeo yake JB akakunja sura
" alafu wewe msen..g...e ndo mawazo yako hayo kuua ndo maana ile siku nia yako ilikuwa ni kumuua MARTIN boya wewe nyie ndo mnaoua hata maalbino,sijui huna roho gani wewe...."
"Siyo hivyo MR Yale yalishaisha mbona?! Tutabaki kuwa wachimbaji siku zinaenda,siku zinarudi mwisho tutakufa na vifua vikuu bila kupata mizigo ya mahana si vibaya kutoa nafsi moja zifaidike nafsi tat....
" ishiya hapo hapo zuu kama una cha kuongea
"Lakini kaka j kwa nini tusijaribu tu kufanya hivyo
MARTIN alichangia
" katu siwezi kushiriki dhambi ya kuua,na kama mna nia hiyo Mimi sipo nanyi bora nijitenge nifungue balo langu...."
"Siyo hivyo MR ni kuelewana tu"
"No!,kuelewana katika kuua?!,hapana siwezi"
Alimaliza JB na kujinyanyua akatoka eneo hilo alishavurugwa na alishachukia
Baada ya JB kuondoka na kuwa acha vijana wale wawili wakaendelea na kikao chao
"Sikia nikwambie MR wewe umekuja peke yako!,Mimi nimekuja peke yangu,na yule fala kaja peke yake exactly tumejuana humu humu,hivyo kama ameamua kututosa nasi tumtose asiyependa maendeleo hiyo ni hadui tumtoe kafara fala yule"
Aliongea ZUBER kwa kujiamini, alitegemea MARTIN angeshangaa tofauti na mategemeo yake kijana yule akushangaa,Bali aliachia tabasamu hafifu
"Sasa tutamwangamizaje?!"
Kwa sauti ya upole MARTIN akaoji,
"Ni rahisi tu, tukiwa baloni wakati nyie mwapandisha mchanga mkipandisha safari mbili,safari ya TATU Mimi nitamtwanga nyundo ya kichwa,nyundo moja atunaye tena"
"Alafu..."
"Swadakta!,damu itakayo mwagika ndiyo utajiri wetu,kuna mahali tutapaka tunuizie alafu huo mwili ntakuonesha njia za panya za kupita kwenda kuutupa....
Wakagongesheana mikono kukubaliana kwa jambo lile,
MARTIN aliutamani sana utajiri na aliazimia siku akirudi kwao harudi na gari la kifahari,akanunue majumba ya kifahari aliona malengo yake yakianza kutimia
Baada ya kumaliza vinywaji wakajinyanyua wakiwa wamelewa na kuelekea ghetoni kwao wakiwa wamelewa
Walimkuta JB tayari kashalala.

Usikose ya 07..
 
MZIMU ULIOREJEA.

sehemu -07-

Ilipoishia
Baada ya kumaliza vinywaji wakajinyanyua wakiwa wamelewa chakari na kuelekea ghetoni kwao
Wakamkuta jb akiwa kashalala.

#Songa...

Wakamwangalia KWA macho ya dharau na kujipandisha kitandani tayari kwa kuipitisha siku hiyo na kuikaribisha siku mpya.
Siku ambayo kwao waliiona ni nzuri kwa kutekeleza matakwa ya mioyo ya.
Hata usingizi ulipowabeba ndoto walizo ota ni za ukwasi,wakiwa wameuaga umaskini.
Usilolijua ni sawa na usiku wa Giza
Asubuhi waliamka wote wakiwa ni wenye furaha,awakuwa na kawaida ya kupika walikula mgahawani.
Siku hiyo mpya ilikuwa ni siku ya majonzi kwa GOD,toka yeye alipoamka moyo ulikuwa ukimuuma pasina sababu.
Ilikuwa ni dalili mbaya kwake na alilitambua hilo,baada ya kumaliza kunywa chai wakashuka mgodini na kuanza kazi.
Safari ya kwanza wakapandisha udongo juu na kumuacha ZUBERI chini akiwa anapasua miamba, lengo lake safari ya tatu ndiyo safari ambayo ingekuwa ya mwisho kwa kijana Yule
Nafsi zao zilibadilika na kutengeneza utando wa ukatili katika mioyo yao
Safari ya pili nayo ikawadia wakawa sasa wanamuesabia dakika
Moyo wake ulizidi kumwenda mbio,na kumnyima raha
Safari hiyo walikuwa wakishuka chini ndiyo ZUBERI angemaliza lengo lake.
Lakini aikuwa hivyo wakati wakimwaga ule mchanga ghafla wakasikia tetemeko la ardhi katika eneo lile.
Watu wakaanza kukimbia huku na kule kwa waliokuwa nje,kila mtu akitaka kunusuru roho yake.
Kwa waliokuwepo ndani ya mgodi tetemeko lile likaanza kuporomosha mapande ya maudongo na mamiamba.
Hakukua na uwezekano wa kuokoka katika kisanga kile.
Lilikuwa ni tendo LA dakika kumi lililopoteza mamia ya watu
ZUBER akiwa mmoja wapo,ilibidi serikali wazuie wachimbaji kuendelea kuchimba eneo lile kupisha kufukuliwa kwa maiti zile
Kwa upande wa MARTIN na JB walijawa na simanzi ilojenga kovu LA kudumu mioyoni mwao.
Huku siri ya MARTIN na ZUBERI juu ya kumtoa JB kafara ikibaki katika moyo wa MARTIN akijihisi na mkosi
Ndo kilichomuumiza zaidi
"Ndugu yangu!,tukiruhusiwa kurudi mgodini,mgodi utatema balaa umaskini baybay"
Aliongea JB akiwa na tabasamu hafifu katika uso wake
Baada ya huzuni ya muda mrefu tabasamu likapendezesha sura yake ile ya upole ila ilojaa ukatili ndani yake akafumbua mdomo wake kwa sauti iloanza kuleta matumaini
"Kivipi kaka j"
"Mgodi si umeua?!,umekunywa damu sasa ni muda wa kutajirika"
Aliongea jb,MARTIN akuamini kile akisikiacho akajinyanyua katika kochi na kumkumbatia swaiba wake yule
Mambo yakawa yamegeuka,wakasubiri kwa hamu siku mgodi ukifunguliwa ni baada ya wiki tatu wakaruhusiwa kuanza kazi tena,baada ya serikali kuridhika na hali ya hewa katika tetemeko LA ardhi
Wakarudi katika balo lao,eneo alilofia ZUBERI
Kama JB alivyosema lilikuwa ni eneo lenye Neema
Madini ya kumwaga,kwa ushirikiano wakafanikiwa kununua mgodi ule ukawa chini yao.
MARTIN hakuwa yule wa miezi michache nyuma
Jb akuwa kijana yule wa machimboni wote waliota vitambi
Wakanunua majumba ya kifahari jijini ARUSHA na magari ya kutembelea
Jb akuacha kumkumbuka rafiki yake ZUBERI kila Mara alienda katika kaburi lake alilolijengea na kukatia majani
Ilikuwa ni tofauti na MARTIN yeye aliangalia maisha yake tu
"Nina habari njema kwako Mr"
Aliongea jb tabasamu likiwa limechanua katika uso wake
"Habari ipi mkuu"
Martin alioji!
Ile tenda ya kupandisha wazungu mlima KILIMANJARO MOSHI si imetudondokea sisi
"Waoooo"
Martin akuamini akamkumbatia jb,ilikuwa ni tenda ya mabilioni
Ikabidi waamie katika mkoa huo wakiwa moja ya mabilionea wakubwa nchini TANZANIA
Wakafungua kampuni ya uuzaji na usafirishaji madini huku wakichukua tenda yote ya kupandisha wazungu mlimani
uzuri mmoja wote hawakuwa na ndugu, ndugu ni wenyewe wawili...

**********************************

SURA YA TATU
"Bosi kuna binti kanipa barua hii kanambia nikupe naye wakaondoka"
Katibu muhtasari wa kampuni ile aliongea huku akimwangalia jb,alokuwa akizunguka na kiti
"Yukoje yukoje huyo binti"
Akauliza JB huku akiipokea barua ile
"Alikuwa kajifunga kininja sikuweza kuiona sura yake"
"What!!?"
"Ndiyo bos!..."
"Sasa wewe ulijuaje ni wa kike JE kama alikuwa ni wa kiume kavaa vile"
"No bosi ni kutokana na sauti yake"
"OK na shukuru kaendelee na kazi"
Akatamka jb,Dada yule akatoka na kumuacha bosi Wake akifungua ile barua
Ghafla macho akayatoa kwa mshangao pasina kuamini kile akionacho katika barua ile....

JE NI NINI KILICHOANDIKWA KATIKA BARUA HOYO?!
HUYO DADA NI NANI!

Usikose 08..
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu-08-

ILIPOISHIA
Jb akaifungua taratibu barua ile
Ghafla macho yakamtoka Pima
Akuamini kile akionacho kilichoandikwa katika barua ile..

#Songa

"Kwako mpenzi"
Tulizo LA moyo wangu,tabibu wa nafsi yangu bila shaka u mzima..
Yah hata mm pia ni mzima
Dhumuni la barua hii ni kukweleza Yale yaliyoko katika moyo wangu
Jb tambua NAKUPENDA wew pekee ndo muhasibu wa moyo wangu,sahau yote yalopita tugange yajayo
Ile ilikuwa ni utoto na sasa tu ni watu wazima,ni muda wa kuganga yajayo namba yangu ni 0652281153 naomba nitafute plz kuna zawadi nataka kukupa sijawah mpa mwanaume yoyote hila ntakupa wewe mpenzi..
NAKUPENDA JB
Ni Mimi,
FATUMA.

Jb akuamini kile alichokisoma akapikicha macho na kurudia kusoma tena maneno Yale ila ayakubadilika
Akajinyanyua kwenye kiti kile na kutoka mpaka alipo karibu muhtasar wake
"Umesema alikuwa kavaa nikabu?!!?"
"Yap Bo's kavaa kininja kaziba sura yake"
"Ok ! ahsante"
Aliongea Jb akielekea katika lift akajiingiza na kushuka kuelekea chini
Jengo lile lilikuwa linaghorofa nne hvyo yeye alikaa juu na baadhi ya wafanyakazi
Na msaidizi wake Martin alikaa ghorofa ya Tatu
Akashuka katika ghorofa hiyo na kuingia ofisini kwa rafiki yake yule kipenz Martin alipofika akakaa kwenye kochi na kumkabidhi rafiki yake barua ile
MARTIN akaisoma
Akuielewa
Akairudia tena
Lakini bado akuielewa
Ndipo ilipobidi JB aanze kumsimulia
***
ZAIDI YA MIAKA KUMI NYUMA
Ilikuwa ni familia ya kifukara,iliyoishi katika nyumba moja ya udongo ilolalia upande mmoja
Ilikuwa ni familia waloishi watu wa nne
Baba mama na watoto wao wawili wa kiume,ambaye ata shule awakuweza kwenda kutokana na kuzidiwa ufukara
Mbali na ufukara walokuwa nao familia ile ilitengwa na kijiji kutokana na imani za kichawi
JB mtoto mkubwa wa familia ile alitokea kumpenda binti mmoja jirani yake na kuzifikisha hisia zake
Binti yule alojulikana kwa jina la Fatuma aliishia kumcheka na kumkejeli kitu kilichomzidishia hasira na upendo wake ukageuka kuwa chuki
Chuki iliyokuwa ikizidi kuutafuna moyo wake kila uchwao siku inayofatia!
Kuna matatizo kibao tu yalitokea kwenye familia ikanilazimu niiache familia ile
Sikurudi katika kijiji kile mpaka Leo hii
Na huyo binti nikwambiaye ndo huyo Fatuma aloleta barua kwa katibu muhtasar wangu
"Mh"
Martin akaguna baada ya kuskia kisa icho
"Amejuaje hapa na amejuaje kama umefanikiwa?!"
"Si ndo hapo best miaka kumi mingi si mchezo"
"Ila ilo si tatizo kaka sasa wewe ni Mtu maharufu mfanyabiashara mkubwa unajulikana!,hvyo hapo akuna la ajabu"
(Jb akacheka)
Martin akaendelea
"Na mtoto kajitunza,kajitunza kwa ajili yako yapaswa uwoe kaka miaka inaenda ujana baybay ongea na mtoto huyo vizuri"
Jb akafikiria kidogo ni kweli maneno Yale yalimwingia ipasavyo
Bila kuaga akajiondoa na kuelekea ofisini kwake
Akakaa akiwaza hili na lile,lile na hili mwisho akaamua kushika simu yake na kuandika namba kadhaa akazipiga
Zikaita
Ghafla zikapokelewa kwa sauti nyororo na nzuri
Alikuwa ni Fatuma
"Alooh nani mwenzangu"
Jb akasita mwili ulimtetemeka mdomo ukawa mzito kufunguka
Angeongea nini?!
Akujua kuwa kuna alokuwa akimfatilia kwa karibu kila akifanyacho
Kwa ajili ya manufaa yake
Pia akuziona camera zilizotegeshwa katika ofisi yake ile kwa sababu maalum
Ndiyo alikuwa ndani ya Giza tororoo.....

ITAENDELEA...
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu -09-

SHARFIA ZUBERI katibu muhtasar wa kampuni ile na mwandishi wa kujitegemea wa gazeti La alasiri kiti kilikuwa cha moto
Tabia yake ya udadisi na kutamani kujua kila kilichoendelea kilimpelekea kutegesha kamera katika ofisi ile.
Kitendo cha kumuona yule Dada na kumpa barua,kubabaika kwa bosi wake alijua kwa vyovyote lazima angetengeneza habari
Matokeo yake ayakuwa tofauti na alivyotegemea
JB akazama katika penzi la binti yule Fatuma
Kila kwenye kumbi za starehe walikuwa wote
binti SHARFIA naye akuacha Ku post habari zao
Kwa kuwa wote walikuwa ni wafanyabiashara wakubwa,ila katu Jb hakujua Sharfia ndiyo aliyevujisha habari zao pia akujua kuwa yule alikuwa ni mwandishi wa kujitegemea katika gazeti la alasiri hilo bado lilikuwa ni ficho lililojiifadhi katikati ya moyo wa binti yule mpole na mcheshi.

***********************************
MIEZI MITATU BAADAYE

Moyo ulimuuma,tamaa ya kumiliki Mali zote ikamtawala
Akaweka nadhiri
Kumwangamiza JB na kampuni yote ibaki chini yake
Kwa uwezo wa pesa alokuwa nao uwezo wa kufanya chochote akitakacho alikuwa nao
Ni vipi asifanye?!
Mwanzo lilianza kama wazo,wazo alilopewa na mtu alomjua yeye likaja kubadilika na kuitaji kulifanyia kazi
Ila kuna watu wawili ilikuwa lazima
Awaweke sawa
Mwanasheria wa kampuni ile pamoja na Fatuma mpz wa rafiki yake
Akamuitaji mwanasheria yule wakapate naye lanchi
Akamweleza wazo lake
Mwanzo mwanasheria yule alikuwa mgumu kuelew lakini Martin alijaliwa maneno
Uwezo Wa kushawishi
Maneno ambayo yalimwingia ipasavyo mwanasheria yule mwisho akakubali
"Mimi ninachokuomba unisaidie ni kufoji hati kuzi ghushi kutoka katika jina lake kuja katika jina langu swala la mauaji niachie Mimi naua ki intetnation hakuna atakayejua wala kuhisi kama twausika"
Aliongea Martin kwa sauti ndogo,tabasamu la kejeli likiwa katika domo lake
Swala hilo kwa mwanasheria yule lilikuwa jambo dogo sana akamuhaidi ndani ya masaa 48 litakuwa limekamilika
Martin akafrah kuskia vile....
Wakafunga kikao chao
Na kurejea kazini....

**********************************
Moyo wake ukapasuka,kwa kutokuamini kile akisikiacho
Lengo LA kuitwa pale alijua pengine ni kutongozwa
Yah aliashajipanga jinsi ya kujibu
Ukweli aliujua ndani ya moyo wake
Fatuma
Binti alojaliwa uzuri wa asili,macho madogo umbo namba nane
Usikatae wito kataa maneno
Kosa alilofanya ni kukubali kukutana na MARTIN
Akamlaghai kwa maneno matamu na kufanikiwa kumtupa kitandani
Akampa penzi tamu na katikati ya tendo akawakilisha ombi lake
Ndipo moyo wa binti yule ulipopasuka
"Na kama ukikubali hii nyumba ni Mali yako pamoja na gari ya kutembelea"
Aliongea MARTIN huku ulimi wake ukitambaa katika mwili laini Wa binti yule....
Akakumbuka jinsi alivyokuwa akimbembeleza JACOB kuhusu kumnunulia nyumba bila mafanikio
Leo anapata nyumba ile ya kifahari pamoja na gari LA kutembelea
Akazidi kupagawa
"Na pia nitakupa walinzi ambao watakulinda bure na mshahara wao watachukua ofisini"
FATUMA akakubali jambo lile kuiba hati zote ambazo zilikuwa ni original kwake lilikuwa ni jambo dogo kulinganishwa na utajiri atakaopewa
Gari na nyumba
Moyoni mwake a kumpenda kabisa JB alimpendea hela
Alikuwa naye kwa ajili ya kumchuna bila moyoni mwake alimpenda sana kijana mmoja shombeshombe
Alimpa kila alichoitaji
Huu ni muda sasa wa kuishi na AMOUR.
Akajiwazia Mpaka anaondoka katika nyumba ile alikuwa kashaamua kumsaliti mpz wake yule.
Kazi kwa MARTIN ikabaki ndogo tu kuonana na wazee wa kazi
Four silent killers.
Wauwaji wa NNE wa kimya wasioacha ushahidi.
Makatili wenye roho mbaya zaidi ya roho ya simba au chui
Alijua jinsi ya kukutana nao.

SAPOTI YAKO ITAFANYA RIWAYA HII IKUJIE MAPEMA SHARE UWEZAVYO!....
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu -10-

ILIPOISHIA
4 silent killer wauwaji wa nne wakimya wasioacha ushahidi
Makatili wenye roho mbaya
wenye kurarua zaid ya chui au simba
MARTIN anapanga kukutana nao,dhumuni lake kubwa ni kuwapa kazi ya kumwangamiza Jacob lengo lake Mali zote walizo share zibaki chini yake!
Unahisi nini kitaendelea?!....

Songa nayo sasa!....

#SHERATON_PUB
Ulikuwa ni ukumbi mdogo mziki ukipigwa kwa mbali ndani ya ukumbi huo
wanaume na wanawake wakicheza kuendana na mziki katikati ya ukumbi huo
Taa zilibadilika badilika rangi, kupendezesha eneo lile na kufanya washiriki wajiachie kufurahia tendo lile
Nje kabisa ya ukumbi ule katika eneo walilokaa wanywaji katika meza moja walikaa watu wa tano wakiwa wamezama katika maongezi
Ni MARTIN na four silent killer
Martin akiwapa dili LA mamilioni
Dili LA kumwangamiza rafiki yake kipenzi JACOB
akawapa kabisa na advance ya kazi ile
Akawapa na ramani ya eneo alilopo kijana yule
Mambo yalipangwa yakapangika
Vijana wa kazi wakaondoka wakihaidi usiku huo huo kufanya kazi ile ya kuichoropoa roho ya JB
*********
Ilikuwa ni bonge LA nyumba iliyozungukwa na ukuta mkubwa wenye nyaya za shoti juu yake!
Ndani pembeni ya geti palikuwa na kajumba kadogo ambacho kilikuwa na walinzi wawili walijiegemeza katika ukuta na kupitiwa na usingizi
Walikoroma
Hawakuisikia gari aina ya tax lililopark nje wakashuka vijana wa nne wakiwa na silaha nzito kifuani
Ilikuwa ni SAA nane usiku
Wakalisogelea geti na kuligonga
Walinzi wale wakakurupuka
Na bila kuchukua tahadhari wakafungua geti
Kitendo tu cha kufungua geti,risasi zilizofungwa kiwambo cha kuzuia sauti zikachimba vifua vyao
Wakaporomoka chini
Wakaisogelea nyumba ile
Fatuma akufunga mlango
Kama alivyoagizwa
Hivyo ikawa rahisi kwa wazee wa kazi kuzama mpaka katika chumba kile
Kama uigizaji binti yule alijuwa kuigiza
Majambazi wale wakaanza kumtesa
JB na mwisho wakamchoma kisu cha koromeo
Baada ya mauaji Yale wakapeana 'signal' na binti yule aliye wapa makaratasi Yale ya hati ili kuaribu ushahidi isigundulike kama anausika wakamtwanga bibie yule risasi ya mguu
Wakaubeba mwili wa jb na kuondoka nao mpaka pembezoni mwa bwawa wakautupa hapo
Usiku huo huo
Purukushani zile ziliwaamsha majirani waliofika eneo LA tukio usiku ule ule
Na kuikuta TeX ndo inaishia
Jambo lililoafikiwa ni kupiga simu polisi kabla awajampeleka binti yule hospitalini
Aliyekuwa patroo usiku huo alikuwa ni inspekta NURDIN
Ndo aliyepokea simu ile akiwa kituoni
Akashtushwa na habari ile
Alimjua fika JB
Tajiri mkubwa ndani ya mji ule mdogo wa moshi
Akaamua kuibeba kesi ile
Akajivika yeye kama yeye akiwa na wenzake wawili wakaingia ndani ya gari ya polisi kuelekea eneo la tukio
Usiku huo huo
Wakakagua maiti zile,wakichukua maganda ya risasi zilizotumika
"Mlisikia milio ya risasi?!"
NURDIN alimuuliza shughuda mmoja ambaye alikana
Akaandika katika kitabu chake
Ni wazi aligundua bastola au silaha ilotumika ilifumbwa kiwambo cha kuzuia sauti
Akazama ndani ambalo alimkuta mke wa jb FATUMA akiwa katika maumivu makali ya risasi huku akilia....
"Wameondoka na mume wangu jamanii"
Kama ni ualisia binti yule aliutendea haki
"Wahusika hao unaweza kuwatambua sura zao?!"
"Hapana walikuwa wamevaa kininja
FATUMA akaongopa wakati ukweli wauaji wale sura zao zilionekana
" je wakati walipokuwa wanampiga mumeo walikuwa wanaitaji nini?!"
"Walikuwa wakitaja mzigo ila mwisho wakataja madawa mume Wang akakubali kwenda kuonesha mahali alipoifadhi ndo wakaondoka naye"
FATUMA akazidi kuongopa,picha negative ikajengeka kwa wanausalama wale
Kuwa jb alikuwa muuza madawa ya kulevya
Wakaaidi asubuhi kumsaka
Wakamuwaisha binti yule hospitalini
Asubuhi mwili wa JB ukakutwa pembezoni mwa bwawa akiwa amechomwa kisu cha shingoni
Kwenye koromeo
Ikawa ndo habari ya mjini
Vyombo vya habari vikatangaza tukio lile tajiri muuza madawa auwawa na wenzake
Kizaazaa.

ITAENDELEA..
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu -11-

Habari ile iliwashtua watu wengi sana,Fatuma alipoteza fahamu Mara kadhaa
Huku rafiki yake wa karibu Martin akilisimamia swala hilo
Mtu wa kwanza kushughudia mwili ule alikuwa ni inspekta NURDIN
Yalikuwa ni mauaji ya kinyama
KWA SEKUNDE KADHAA AKABAKI AKIKITAZAMA KISU KILE
Kilivyoirarua shingo ya jb, Akaweka nadhiri ya kumpata muhusika,japo moyoni mwake alikuwa na uhakika kwamba JB ni muuzaji wa madawa ya kulevya kutokana na maelezo ya mpz wake fatuma
Katika vipimo vya awali hakuna alama yoyote iliyo onekana ambayo ingeweza kumtia hatihani mtuhumiwa
Kisu kile kilipopimwa haikuonekana alama ya vidole
NURDIN akazidi kuchanganyikiwaa
Ni wazi muuaji alivaa gloves
Baada ya siku tatu mwili ule ukakabidhiwa kwa wenyewe
Aliye kuwa mpz wake FATUMA na rafiki yake kipenzi MARTIN kwa mazishi
Martini aliyasimamia mazishi Yale mwili ule ukafukiwa katika makaburi ya njoro
Mali zote zikabaki chini ya MARTIN
Akampa nyumba moja ya kifahari FATUMA
Na ili kupoteza ushahidi akabadilisha wafanyakazi na kuwafukuza wote akaweka wapya
SHARFIA akawa mmoja wapo wa wafanyakazi walotimuliwa
Akajiingiza kwenye uandishi wa habari moja kwa moja

************************************
Ngriiiiiii ngriiiiiiiiii ngriiiiiiiiii ngriiiiiiiii ngriiii......
Simu ya mezani iliita NURDIN akapeleka mkono wake katika mkonga na kuipachika sikioni
"Ni kituo cha kati MAJENGO nikusaidie nini?!"
"Sory naongea na afande NURDIN?!"
"Yah"
"OK afande Mimi ni jirani yake na JB na habari nzuri kwako afande"
NURDIN akashtuka
"Uk..oo wap....sai..v wew..."
Akauliza kwa kigugumizi
"Njoo uwanja wa majengo karibu na MAJENGO sec hapa"
NURDIN akujibu kitu akajinyanyua na kutoka ndani ya kituo kile
Kituoni na hapo shule ilipo apakuwa na umbali
Dakika TANO aliwasili kiwanjani hapo na kutoa simu yake akapiga namba kadhaa simu ikapojelewa
"Njoo hapa zilipo bodaboda utanikuta mi ni bodaboda nipo juu ya boxa nimevaa t shart nyekundu na jeans la bluu"
NURDIN akachepuka kuelekea alipoelekezwa
Alipotokeza tu akamuona kijana huyo akimjia
"Panda twende"
Bodaboda yule akatoa amri
NURDIN akaigusa bastola yake ndogo ilokwepo kiunoni,Aliporidhika na usalama wake bila kuwaza Mara mbili akadandia pikipiki ile na dereva akaiondoa taratibu
"Tunaelekea wapi!"
NURDIN akahoji lakini bodaboda yule alikaa kimya akazidi kukanyaga mafuta
"Nimeuliza tunaelekea wapi?!"
Akaoji kwa ukali
Dereva yule akaisimamisha pikipiki yake
Akamgeukia NURDIN
"Mimi ni raia mwema tu,jirani na anapokaa jb siku ya tukio saa nane usiku nlikuwa natoka kibaruani sasa nikawa naelekea home kulala ile nafika katika nyumba ya marehemu nje nikakuta TeX nyeupe na ghafla nikasikia vishindo kwa haraka nikachukua zile namba za gari na kuelekea kwangu nilipopiga simu polisi na baadaye mlipokuja mlikuta tayari wameshamteka marehemu"
NURDIN alishtuka kupata maelezo Yale
Yalikuwa ni maelezo mazito akakaa kimya kuendelea kuskiliza japo alikuwa na maswali rundo ya kuuliza
" Leo nimefanikiwa kugunduwa inapopaki hiyo tax ndo maana nimekuchukua nikupeleke ukaishughudie"
"Unauhakika ni yenyewe?!"
"Na uhakika afande"
"OK twende"
Bodaboda yule akaiwasha pikipiki yake na kuelekea maeneo ya stendi ya MAJENGO
Awakuchukua muda mrefu kufika maeneo Yale
Yule kijana akamuoneshea ins tax hiyo
"OK nashkur kwa ushirikiano wako nikikuitaji ntakutafuta"
Aliongea NURDIN
"Sawa afande"
Yule kijana akawasha bodaboda yake na kuondoka
NURDIN akaisogelea ile tax ilokuwa na tinted vioo vyote ambapo dereva alikuwa ndani yake....

SAPOTI YAKO ITAFANYA RIWAYA HII IKUJIE MAPEMA SHARE UWEZAVYO!....

ITAENDELEA....
 
MZIMU ULIOREJEA

sehemu 12&13

ilipoishia
Awakuchukua muda mrefu kufika maeneo Yale
Yule kijana akamuonesha ins tax hiyo
"Ok!,nashkur kwa ushirikiano wako nikikuitaji ntakutafuta
Aliongea NURDIN
"Sawa afande"
Aliitika yule yule kijana,akawasha boda boda yake na kuondoka
NURDIN akaisogelea ile tax ilikuwa na tinted pande zote

Songa sasa....
Akujali hilo akaielekezea simu yake upande wa nyuma na kuitwanga picha kadhaa,upande wa kati, kwa siri sana
Akajongea eneo la mlango ulikuwa wazi akachungulia akamuona dereva ndani akiwa amelala akajiingiza ndani
"Nipeleke uwanja wa mashujaa"
Akaongea kwa sauti ya upole,akiwa kayakaza macho kwa jamaa yule
Jamaa akuongea neno akawasha gari na kuondoka eneo lile wakaingia lami
"Mimi ni afisa wa polisi Nurdin ndo jina langu naomba tuelekee kituoni"
Alianza kuongea Nurdin sambamba na kutoa kitambulisho chake Yule dereva akatoa macho
"Kwa kosa gani afande?!"
"Utaenda kujua huko huko"
"Hapana afande mi si muhalifu plz tuyamalize"
Aliongea yule kijana huku dhahiri shahiri akitetemeka,woga ukimtawala,
Nurdin akamkazia macho akimsoma usoni
Hizo hazikuwa sifa za jambazi,jambazi aloshiriki katika mauaji ya kikatili kama Yale
Majambazi ambawo awakuacha hata tone la ushahidi katika mwili wa jb
Huyu mwoga hakuwa mmoja hapo
Ila gari yake si ilikuwa eneo la tukio?!
Yah pengine ni dereva wao
Akajiwazia na kujijibu mwenyewe
Akachomoa kakijitabu chake katika kabegi chake kadogo cha mgongoni
"Waweza Ku park gari tujadili kwanza"
"Sawa afande"
Akajibu kijana yule sambamba na kuipaki gari yake pembeni ya barabara
"Kwa jina unaitwa nani?!"
"Kipele chaupele"
"OK unaishi wapi?!"
"Majengo kwamtei"
"OK huwa unakodishaga gari yako?!"
Dereva yule akashtuka kwa swali lile,mshtuko ulotafsiriwa vibaya na inspekta yule
Akazidi kumkazia macho sambamba na kuikunja sura yake
"Nd...I...i.o"
Akaitika kwa kigugumizi
"Ila kwa watu ninaowafahamu tu afande"
Akaongea huku akitoa tabasamu la bandia akijaribu kutengeneza uchangamfu wa kibandia
"Ok!"
Akajibu NURDIN huku akiandika, tabasamu likisomeka katika uso wake ni wazi alilipenda jibu lile kwa sababu ni wazi lilimrahisishia kazi yake
"Mara ya mwisho ulimkodishiaga nani na kwa kazi gani?!"
"Mara ya mwisho juzi rafiki yangu Musa alikuja kulikodisha ila sijui ni kwa kazi gani!"
MUSA alikuwa ni mmoja wa vijana wa 4 killer aliye shiriki kumwangamiza jb ndugu msomaji ok twendeleee.....
"Lilivyorudi lilikuwa kwenye hali gani?!"
Nurdin akazidi kudadisi Huku akiandika,mfukoni tape recordar yake ikirekodi kila kitu
Lilikuwa ni swali LA mtego,
"Lilikuwa s.s..a.waa"
Dereva yule alibabaika kujibu swali lile,ni wazi jibu lake lilikuwa na walakini
"Ukiwa muwazi kwangu sitokutesa tutaachana hapa hapa ila nikigundua unanificha ntakupeleka rumande na utafungwa hivi unajua gari yako imefanyiwa uhalifu siyo kesi ya wizi ni mauaji sasa wewe jifanye msiri kama utoenda kuisaidia polisi mpaka hayo majambazi yakamatwe"
Jamaa akashtuka
NURDIN akatumia mwanya huo huo kumtingisha Alishajua ni mwoga
" kwanza naona napoteza muda wangu washa gari twelekee kituoni kule ukiteswa kidogo utasema kila kitu nakubembeleza umekuwa ndugu yangu?!"
Insp yule akawa mkali kidogo
"No! Afande tuyamalize tu ntakueleza kila kitu ila usije nitaja wataniua"
Ilibakia robo Nurdin aangue kicheko
Akajikaza!
"Ok usijali kwa ilo nieleze"
"Ni haidi kwanza hatutofika kituoni"
"Of corze kama ntaridhika na maelezo yako
" OK,afande ni kweli juzi gari yangu iliporudishwa katika siti za nyuma ilitapakaa damu japo zilifutwa ila niliweza kuzigundua"
NURDIN akatumbua macho yake makali nyuma ya siti zile akuona cha maana akaachana napo
Akaendelea kuandika
"Je ni nani aloikodisha?"
Ni MUSA Rafiki yangu na tajiri kcmc anamiliki mabucha na baa nyingi"
"Umesema ni tajiri MOSHI hii ina maana hana magari mpaka akodishe lako akafanyie uhalifu?"
"Ana magari ila mi sijui nnachoangalia ni pesa ananipaga pesa nzuri sana''
NURDIN akatingisha kichwa kwa masikitiko
" Ok anakupaga sh ngapi?!"
"Kwa usiku mmoja laki mbili na ananijazia mafuta full tank"
"Duuu!!!"
NURDIN akaguna akionekana wazi kushangazwa na jambo lile
"OK unaweza kunipeleka anapoishi"
"MUNGU wangu!,afande si ndo matatizo haya wataniua Mimi nikuelekeze tu! Uende"
Kwa masikitiko akaongea kijana yule,inspekta NURDIN akamkata jicho
"No! Washa gari twende"
"Sawa afande"
Akajibu dereva yule na kuliingiza gari barabarani kuelekea maeneo ya kcmc yalipo makazi ya MUSA
*
Ulikuwa ni mwendo wa dakika 15 ulowafikisha maeneo hayo ya kcmc
Ilikuwa ni bonge la nyumba ambalo kwa nje lilizungukwa na ukuta mkubwa na geti ambalo apakuwa na shaka lililindwa na aina Fulani ya walinzi
"Pita moja kwa moja usisimame"
Insp akatoa amri dereva yule akatii, shida yake ilikuwa ni kuiona tu nyumba hiyo akatoe maelezo kwa bosi wake kamishna GUDLUCK SILVESTER
Ili apewe kibali cha kuikagua nyumba hiyo na kimtia hatiani jamaa huyo
Ikabidi warudi kituoni yule dereva alitegemea angeachiwa baada ya kutoa ushirikiano wa kutosha lakini haikuwa hivyo
NURDIN alitambua ni wazi maisha ya kijana yule yalikuwa hatarini
ivyo akamsweka rumande kama kumficha,na kumueleza kila kitu bosi wake yule
"OK andaa file fatilia kesi hii mpaka uwatie wahalifu mkononi,kila kitu itabidi unieleze,na ukiitaji msaada wowote usisite kunambia
" yas afande..."
Akaitika NURDIN na kujinyanyua kidogo juu ishara ya heshima kwa bosi wake Yule
Alifurahi kupewa idhini ya kufatilia kesi ile akajiondoa ofisini mule na kuelekea katika ofisi yake kwa ajili ya kuliandaa file LA kesi ile.
Huku nyuma kamishna SILVESTER akaikwapua simu yake na kupiga namba kadhaa akaiweka sikioni
Simu ikaita na kupokelewa na sauti nzito...
"NURDIN ndo anafatilia kesi yenu na kaanza kwa mafanikio kamtambua MUSA muondoeni duniani Leo hii kabla mambo ayajaharibika"
"OK mh ilo litafanyika"
Upande wa pili ukajibu na simu ikakatwa
'Ni nani aliye fichua siri hii'
Akawaza MARTIN akiwa juu ya kifua cha binti mdogo,
Ni binti ambaye angeweza kuwa mtoto wake.
Ilo akujali,baada ya taharifa ile hamu ya tendo lile ikamuisha akajitowa na kumuacha binti yule alokuwa katika hali mbaya kihisia akishangaa
Akajiondosha eneo lile na kuchepuka mpaka sebuleni akaketi na kupiga namba kadhaa katika simu yake
"Dakika tano uwe umeshafika hapa home"
Akaongea sekunde ile ile na kukata simu
Akajinyanyua na kuelekea bafuni
Alipotoka alimkuta alomuhitaji kakaa sebuleni
Alikuwa kavaa koti LA laizar mkononi gloves nyeusi Jean's ya bluu raba nyekundu
Kichwani alikuwa na kofia aina ya bushori akivuta sigara kubwa ambazo ni nadra kuonekana hapa nchini
Alikuwa ni SAID au side kwa kifupi kama wengi walovyopenda kumuita
Mmoja wa wauaji wa 4 killer's
MARTIN akiwa kavaa taulo
akaisogelea friji na kuifunguwa akatoka NA chupa ya whisky akaiweka mezani
Side akatabasamu
Ndiyo
Ni kinywaji akipendacho,naye MARTIN aligusa mahala pake
Akarudi katika friji na kuchukua nyingine na glass yake Akaketi,na kujimiminia kiasi kidogo baada ya kuifungua chupa yake Akapiga funda moja
Akakohoa kidogo kusafisha koo
"Kwa jumla mko wa nne,ila kwa sasa rafiki zenu wawili walistaafu kazi hii ya uhalifu na sasa wanalinda kwa marehemu JB,wakipokea mshahara mnene niwalipawo kama ahadi kwa mjane wa marehemu bi FATUMA baada ya kutusaidia kwa kazi yetu"
"Nakumbuka nawe uliitaji kazi!,kusudi uachane na ujambazi yah kazi imepatikana ikiwa utanifanyia kazi"
Aliongea MARTIN kwa sauti ndogo,sauti ya kusisitiza,side akatabasamu
Tabasamu LA kutokuamini kile akisikiacho,ila MARTIN akaendelea
"Naitaji uwe bodyguard wangu ikiwa utafanikisha kumwangamiza MUSA"
"What?!!!!"
Side alitoa macho ya mshangao,akapaliwa kidogo.
Ni wazi akuamini kile akisikiacho
MARTIN akacheka
Cheko LA dharau kisha akaendelea kutoa ufafanuzi
"Na ikiwa tusipofanya hivi,tutaumbuka sote MUSA ni mzembe sijui nini kimetokea anasakwa na wanausalama so naitaji mpigie simu ujue yupo wapi ukammalze si ombi ni amri
Martin akiwa na USO wa ghadhabu hasira za wazi akaongea na kujinyanyua akapiga hatua moja kuondoka na ghafla akageuka....
" rafiki yangu kamishna kanipigia simu kunijulisha kuwa kesi hii kakabidhiwa insp NURDIN na kampa idhini akamkamate MUSA baada ya kuridhika na ushahidi kuwa anausika katika mauaji akikamatwa akateswa atatutaja hivyo auwawe kabla mambo hayaja haribika akakamatwa akaingia katika vyombo vya dola"
"Bosi kwa nini tusimwangamize huyo inspekta?!"
"Tutazidisha upelelezi kwa makachero,hasira juu yetu itaongezeka bora na huyu tutazidi kumpa ugumu insp huyu kutufatilia dakika TANO kutoka sasa naitaji nipokee simu yako habari mbaya kutoka kwa MUSA kabla ajaingia mkononi kwa huyo insp"
Akamalizia MARTIN na kuondoka eneo lile
Side akajinyanyua alishaamua kumwangamiza rafiki yake
" upo wapi best na shida na wewe "
"Nipo home"
"Poa naja"
Akakata simu na kuidandia pikipiki yake Akatoka kwa speed kuelekea kcmc anapoishi MUSA
Muda huo qruzer yenye maaskari wa kutosha wenye silaha nzito za kivita ilikuwa barabarani ikielekea huko huko kcmc wakiwa chini ya insp NURDIN
JE NANI ATAMUWAHI MUSA HUKO KCMC KATI YA MAASKARI NA SIDE
ATAUWAWA AU ATAKAMATWA
ITAENDELEA.....
 
MZIMU ULIOREJEA

SEHEMU 14&15

Ilipoishia jana

Muda huo Cruiser yenye maaskari wa kutosha,wenye silaha nzito za kivita,ilikuwa barabarani ikielekea huko huko kcmc wakiwa chini ya insp NURDIN.

#Endelea.....
Japokuwa MUSA alikuwa ni tajiri na mwenye miradi ya kutosha hakuwa na mtoto wala mke.
Wengi walichukulia kama Yale ni masharti alopewa na mganga wake lakini hiyo haikuwa kweli.
Bado alihitaji kula ujana
Alibadilisha wasichana Kama nguo leo yupo na huyu kesho Yule ndo ilikuwa 'life style' yake.
Jambazi sugu lililojiamini
Akuitaji ulinzi wa kutosha
Alikuwa na kijana mmoja tu alomfundisha kushika silaha na kumpachika hapo getini akimjengea kijumba chake.

Leo hii akiwa sebuleni kwake akiangalia tv ghafla simu yake inaita anaicheki na kuibandika sikioni
"Aloo! Swahiba"
Akaongea kwa sauti ya upole akiachia tabasamu la mbali
"Upo wapi best na shida na wewe"
Upande wa pili akauliza kwa sauti ya mkwaruzo
"Nipo home"
Musa akajibu
"Poa naja"
Upande wa pili ukamalizia na simu ikakatwa.
Alikuwa akiongea na rafiki yake kipenzi SIDE.
Hakika akujua dhumuni la rafiki yake yule ambaye muda huo alikuwa njiani akija kwa lengo moja tu
Kumuondosha duniani
Ndiyo
Side aliwasili katika jumba lile na kupiga honi Mara moja mlinzi akafungua geti baada ya kumchungulia na kumuona ni yeye
Tofauti na mategemeo yake baada ya SIDE kushuka akamsogelea,mlinzi yule akamsubiri akijua kuna kitu alitaka kumwambia
Kosa!
Kwa wepesi wa ajabu side alimrukia na kumkaba kwa mkono mmoja mkono mwingine akauingiza mfukoni kwake na kutoka na kitambaa kama kianjifu
Akampachika nacho puani
Kwa sekunde kadhaa,akamshusha taratibu chini
Akamvutia ndani ya kajumba chake na kumuacha huko
Akaelekea upande wa nyumba ile na kuingia ndani
Akamkuta MUSA bado yupo sebuleni akiangalia runinga
Akakaribishwa vizuri izraeli huyo
Wakaendelea na story za kawaida
Wakati wakiendelea na stori ghafla side akachomoa bastola yake ndogo yenye kiwambo cha kuzuia sauti akamtandika risasi kadhaa za kifuani
Akumpa muda hata wa kusali sala zake za mwisho
MUSA akuweza kupiga hata kelele palepale kwenye kochi akiwa katoa macho akatulia tuli
Damu zikitapakaa eneo lile
Baada ya side kumaliza kazi ile kwa kupitia mlango wa nyuma akatoweka eneo lile
Akijua ajaacha ushahidi wowote wa kumweka pabaya
Alijidanganya
Robo saa baadaye gari ile ya maaskari ilombeba insp NURDIN iliwasili katika nyumba ya MUSA
Maaskari wale wakashuka kijeshi
Na kuizunguka nyumba ile
Wakapigwa na butwaa baada ya kukuta geti lipo wazi
Walipoingia tu ndani katika kijumba cha mlinzi walipokelewa na maiti
Mlinzi yule damu zilimtoka puani
Umakini ukaongezeka baina yao
Wakajipanga
Kuna waliobaki nje,kuna walioizunguka nyumba ile na kwa kunyata wengine wakasogelea mlango mkubwa wa kuingilia ndani
Walipozama ndani wakapokelewa na maiti ilolala kwenye kochi iloonesha wazi imetandikwa risasi kadhaa kifuani
Awakupata tabu kutambua maiti hiyo ni ya MUSA
Macho ya NURDIN yakaangaza eneo lile kwa sekunde kadhaa akisanifu uzuri wa sebule ile kisha yakatua katika mwili wa kijana pale kwenye kochi
Akamsogelea na Kumwangalia kwa ukaribu
Mapigo yake ya moyo yaliongeza kasi ya upigaji
Alijua ile kesi si rahisi kama alivyoufikiria
Katika kumkagua yule maiti akaibuka na simu mfukoni kwake
Ndo kosa alilolifanya said
Kutokuondoka na simu ile wakati alijua fika yeye ndo aliwasiliana na Saidi kwa Mara ya mwisho
Kosa ambalo lilimgharimu na kutompa muda wa kulitafakari kipi cha kufanya
Martin akapigia simu ambulance dakika chache ikawasili na kuichukua mwili ule kwa uchunguzi zaid
Inspekta NURDIN akutaka kubanduka hospitalini
Alitaka kuifatilia kwa u karibu kesi ile
Ghafla akashtushwa na mvurumisho wa sauti
Akaingiza mkono wake na kuuchomoa simu yake
Akashtuka baada ya kuonana mpigaji ni bosi wake
" umefika wapi katika kesi hiyo afande"
Kamishna SILIVESTAR akaoji
"Musa amefariki bosi?!"
"What?!!!"
"Yah mkuu tumefika katika nyumba yake tumekuta mizoga miwili wake na wa mlinzi wake miili ndo ipo hospitalini kwa uchunguzi"
"Ooh down sheet!,umegundua nini afande"
Mkuu wake yule akahoji akijifanya kushtuka
Kumbe ukweli aliujuwa
"Nimefanikiwa kupata simu ambayo nimeona meseji za mwisho alizo chat na jamaa mmoja aitwaye side na kumjulisha kuwa anakuja nyumbani kwake kwa vyovyote anahusika mkuu na lazima atiwe nguvuni"
Mapigo ya moyo ya mkuu yule wa jeshi la polisi yakaongeza kupiga
Baada ya kukataa simu akamtwangia swaiba wake MARTIN
"SIDEVni mpumbavu kama huyo aliye mwondosha duniani naye inaitajika aa ngamizwe"
Martin akashtuka
"Kosa lake ni kumuachia simu marehemu hali ya kuwa anajua alichat naye muda mfupi,kijana wangu yupo mbioni kumkamata na kabla ajamkamata naitaji ili muwe salama naye apotezwe"
Ikumbukwe ndugu msomaji,kamishna yule kila hatowapo habari akaunti yake inatuna
Baada ya kukataa simu,akaachia tabasamu akimsikitikia insp NURDIN
Upande wa pili MARTIN muda ule ule akapiga namba kadhaa na kuibandika simu yake kimapenzi
"Vipi beby nakuomba muda huu ofisini"
"Poa mpz naja"
Simu ikakatwa
Na nusu saa mwanamke mrembo mwenye umbo namba nane aliwasili katika kampuni ile baada ya kuonana na katibu muhtasari wake akaruhusiwa aingie
Akaenda kuketi akimwangalia Martin kwa jicho La tamaa
Jicho lililolegea kama kala kungu manga
Mdomo akaung'atia kidogo
Ni wazi alikuwa akiitaji kitu
MARTIN alilitambua hilo.
Akamsogelea pale alipokaa,akampa mkono binti akaushika na kunyanyuka MARTIN akamvuta
Binti yule akadondokea kifuani kwake
Martin akapeleka ulimi wake katika sikio LA binti yule
Binti akatoa mguno hafifu wa kimapenzi
Akaanza kuhema kwa shida.

#NO_15
Binti yule akadondokea kifuani kwake,
MARTIN akapeleka ulimi wake katika sikio la binti yule
Binti akatoa mlio hafifu wa kimahaba
Akaanza kuhema kwa shida
MARTIN akampa ulimi binti yule akaupokea.
Kwa lugha nyepesi twaweza kusema wakaanza kunyonyana ndimi zao
Wakati wakifanya tendo lile mkono wa MARTIN ulipenya katika tshart alovaa binti yule na kuzipapasa chuchu zake ndogo
Binti akazidi kutoa mguno ule,mguno ambao MARTIN halisi alipousikia alizidi kujiimarisha kwa kutunisha misuli yake na kumuumiza MARTIN katili
Akaitaji kulimega tunda lile,mkono wake ulobakia akauzamisha ndani ya suruali ya jeans alovaa binti yule
Aliishia nje ya ikulu takatifu akaanza kuipapasa taratibu
Sasa ulimi wake alishautoa mdomoni kwa binti yule na kuusambaza katika sikio LA Dada yule
Binti yule akawa huru kutoa milio yote aiwezayo
Dakika kadhaa Mbele kila mtu alikuwa kama alivyozaliwa
MARTIN akiwa kaushika mguu mmoja wa binti yule kwa juu huku akipampu juu chini ,juu chini.
Dada alishindwa kuvumilia kupiga kelele
Akajiachia
Hata muungurumo wa simu yake akuusikia kwani alikuwa katikati ya kisima cha mahaba
'Kisiwa cha malavy Davy"
Ndiyo alikiri moyoni mwake hakukuwa na mwanaume alomshughulikia kama MARTIN
Ndiyo
Martin alikuwa Fundi katika medali hii ya kimapenzi
"Nakupenda JASMIN na natamani nikumiliki,ila kikwazo ni SAID"
"Mp naweza kumuacha kwani ameniowa mpaka asiachwe kwanza yeye muislam Mimi mkristo naye hataki kubadili Dini..."
"No mpz side ni rafiki yangu sana ni aibu Ku kuchukua wewe angali yeye ni mzima..."
Binti yule ambaye Martin alimtambua Kama JASMIN alishtuka kwa kauli ile
"Unamaanisha nini mpz wangu?!"
"Yah naitaji Side afe Leo hii hi"
"Haaa!!! Kivipi mpz?!"
"Si kazi ngumu na ntakulipa milioni 50 gari ya kutembelea na ntakuvisha Pete ya u chumba"
"Waooo! Ila beby ntamuaje sasa nimuwekee sumu kwenye kinywaji yule mwanaume simpendi"
"No beby! Kuna dawa ntakupa unajipaka kidogo mkononi unamgusa wewe unaenda kunawa kuokoa maisha yako baada ya lisaa limoja yani dakika 60 ndo inaanza kufanya kazi!"
Aliongea Martin akajinyanyua akaenda katika kabati LA nguo akalifungua akatoka na kajichupa kidogo na kumkabidhi Jasmin
Binti yule akusema kitu akakisweka katikati ya kipima joto chake kilichojaa vipodozi
Pindi alipoishika simu yake akashtuka baada ya kukuta missed calls 5 za side
Akatabasamu!
"Tena wakati tukiwa kwenye raha zetu huyu ndo alikuwa anatusumbua"
"Mpigie usikie anataka nini?!"
Martin alishauri Jasmin akatii akampigia huku akiwa kaweka loud spiker
"Mpz mbona nakupigia simu upokei?!"
Jasmin akaukunja mdomo wake...
"Sorry my hubby nlikuwa bafuni naoga!"
"OK mpz nakuomba uje hapa Samora inn mwenzako nimezidiwa"
"No honey sitoruhusiwa kutoka chuoni mchana huu"
"Plzzzz mpz njoo mwenzako nipo hoi naitaji tiba yako nakuomba roho yangu uje"
Side akazidi kumbembeleza Israel yule aende pasina kujua binti yule alovishwa roho ya kishetwani na bosi wao martin aliitamani sana nafasi ile na muda ule alikuwa kalalia kifua cha mwanaume na hayupo chuoni kama alivyodai
"BAsi kwa kuwa nakupenda nipe nusu saa nitakuwa nimesha kutibu habiby wangu"
Akajibu Jasmin kwa sauti hafifu,sauti ilotokea puani,sauti ambayo. Ina mtoa nyoka pangoni,sauti ambayo hata mwanaume ambaye si rijali akiisikia si baba lazima msoloboko wake utaonesha uwepo wake.
Akamkonyeza martin
Martin akamdaka
Lakini binti yule akafanikiwa kuchomoka
"Ngoja kwanza nikalifyeke gugu lililomea katikati ya bustani nzuri ya mahaba yetu na kisha Mimi ntakuwa wako pasina kizuizi chochote"
Akaaga Jasmin aliogopa hata kumbusu rijali yule kwa kuofia kuingizwa mtegoni tena
"Sawa mpz kazi njema take care my sweet lovly"
"OK mpz mwaaaaa"
Aksmbusu cha mbalimbali na kufungua mlango na kutoka
"Rest in piace swaiba baada ya hapo namalizia huyu binti then nakaa kwa amani sasa"
Akajiwazia Martin.

***********************************

#SAMORA_INN

SIDE aliona muda auendi,macho yake ayakutua usoni mwa mpz wake JASMIN
Alikuwa na kiburi si alikuwa na fedha za kutosha
Katu akujua yalikuwa moyoni mwa mrembo yule
Akutaka kulewa sana akihofia kutomfaidi Jasmin
JASMIN aliomba ruksa ya kwenda toilet akaenda kujipaka dawa kidogo aliporudi alimsogelea side na kuanza kumpapasa akimpaka dawa ile
Side aligugumia kwa utamu
Ghafla Jasmin akajifanya amebanwa tena na kukimbilia chooni
Lengo lake ni kwenda kuosha mikono yake vizuri
Side alihisi pengine mwenzake tumbo lilimsumbua
Tumbo LA kuhara
Dakika chache baadaye hali yake ikaanza kubadilika
Akawa ana hema kwa shida
Mwili ukaanza kubadilika rangi na kuwa mweusi
Jasmin akusubiri akapotea eneo lile
Akamtumia msg MARTIN kuwa tayari,MARTIN akamwelekeza mahali halipo
Jasmin akaelekea moyoni akiwa mwingi wa furaha
Laiti angejua?!
**********
Inspekta NURDIN baada ya kuonana msg za kutilia mashaka kati ya SIDE na MUSA akamtilia mashaka said
Akachukua zile namba za side na kuziingiza katika simu yake akazipiga
Zikaita bila kupokelewa,akukata tamaha kwa kuwa ni MTU alomuitaji aliendelea kusikiliza ghafla zikapokelewa
"Alooh samahani hapa ni SAMORA INN mmiliki wa simu hii ayupo tena duniani,kama wewe ni ndugu yake tafadhali fika Samora inn upesi"
Ghafla simu ikakatika
NURDIN akabaki kanata kama sanamu simu ikiwa bado sikioni
Alipigwa na bumbuwazi.

Itaendelea...
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu 16&17

Ilipoishia....
"alooh samahani hapa ni SAMORA INN mmiliki wa simu hii hayupo tena duniani kama wewe na ndugu yake tafadhali fika hapa samora inn upesi
Ghafla simu ikakatika.

Insp NURDIN akabaki kanata kama sanamu,simu ikiwa bado sikioni...
Alipigwa na bumbuwazi......

#Endelea

Habari ile ilimughadhibisha,iweje kila anapopata mwanga litokea tatizo?!
Tatizo ambalo linakuwa kama kikwazo kwake?!
Akawaza lakini alijua fika kuwaza vile siyo suluhu ya muwafaka katika swala lile
Akajinyanyua na kutoka ndani ya ofisi yake ile ndogo akuitaji kumshtua mtu yoyote yule akaingia ndani ya kipira cha polisi na kuelekea Samora inn,
iliyokuwa maeneo ya kwamtei
Dakika tatu baadaye alikuwa Mbele ya mwili ulobadilika rangi na kuwa mweusi tii.
ulitisha hata kwa kuangalia Kama kawaida yake INS NURDIN akavaa gloves zake za kazi na kuanza kuchunguza mwili wa marehemu yule
Mmoja wa 4 killers,akaskari wote wa kawaida aliowakuta pale wakampisha,
kama kawaida yake akabeba simu na kuwaachia madaktari kazi ya kuuchunguza mwili ule ili ajue ni aina gani ya simu ilotumika kuudhoofisha na kuubadilisha rangi mwili ule
Kazi ile ikazidi kuwa ngumu,
" unasema marehemu alikuja na mwanamke ambaye u nahisi ni mpz wake na baada ya kuigundua maiti hii. Yeye akuonekana?!"
NURDIN alimuhoji muhudumu wa hotel I hiyo alokuwa zamu
"Ndiyo insp"
Dada yule alokuwa nadhifu alijibu.
Nurdin akamwangalia kwa dakika kadhaa
"Baada ya kugundua juu ya mwili huo ni kitu gani cha kwanza ulichofanya?!"
Lilikuwa swali jepesi kwa muhudumu yule
"Nilimwambia meneja,meneja ndo akawajulisha maaskari na ndugu zake"
NURDIN akashtuka
Akatoa macho ya mshangao
"Ndugu zake?!,wako wapi hao"
Askari yule akahoji sambamba na kumwangalia kila mmoja alokuwa eneo lile...
"nop insp wakati tukiwa tunaishangaa maiti hiyo kabla maaskari hawajaja simu yamarehemu ikaita meneja akachukua na kupokea akamweleza wazi kuwa mwenye simu sasa ni marehemu"
Nurdin akayapeleka macho yake kwa meneja yule
"Kimbelembele ndicho kilichokufanya ukapandishwa cheo na kuwa meneja eeh!"
Kijana yule akakaa kimya
"Una miaka mingapi kazini?"
Akamsweka swali lingine
"Miaka 15"
"Ndani ya miaka hiyo ilishawahi kutokea tukio kama hili katika hoteli yenu?!"
"Hapana afande haijawahi kutokea"
NURDIN akaandika maelezo Yale
"Umeharibu utaratibu mzima wa kesi hii kwa kupokea hiyo simu ni kosa la jinai itakuhusu simu zilipigwa ngapi?!"
"Moja tu afande"
Nurdin alitambua ni ile yeye aloipiga ila kisheria haikuwa haki ndugu msomaji
Ilo ni funzo katika matukio kama hayo tusiguse kitu chochote cha maiti hata maiti yenyewe kwani hiyo ni kazi ya wana usalama wenyewe
Ins akamgeukia Yule msichana wa kwanza
"Unasema marehemu alikuja na binti ambaye alionekana kama mpz wake si ndiyo?!"
Binti yule akatingisha kichwa kuafiki
Nurdin akaachia tabasamu
"Na je ukimwona utamtambua?!"
Msichana yule akashtuka
"Ndi..ndi...hapana"
Yule muhudumu alibabaika kidogo,askari yule akabasamu kumuondoa woga.
"Ucjali binti naomba namba zako ntakutafuta"
"Sawa afande ni 0652281153"
"Jina?!"
"Salha"
"OK mi ni ins NURDIN"
Akajibu afande yule sambamba na kuziandika namba zile katika kijitabu chake na kuondoka eneo lile
Akiacha madaktari wa hospitali ya mawenzi wakiubeba mwili ule kuupeleka hospitalini kwa uchunguzi
NURDIN alijiuliza vifo vile vinatokana na nini?!
Ni wazi vilimchanganya sana
Kwa upande wa MARTIN aliona kazi imeisha alibaki tu Jasmin ili awe guru
Kazi ya kumuua msichana yule kwake ilikuwa ni kazi ndogo
Muda wote tabasamu Aliliyeyusha usoni mwake.

**********************************
Ins wa jeshi LA polisi NURDIN alipiga namba zilizoifadhiwa kwa jina LA my love katika simu ya side
Ni namba zilizopigwa Mara ya mwisho kabla ya kifo chake hakuwa na shaka kuwa zilikuwa ni namba za muhusika
Ghafla sauti nyororo ikapokea simu ile
Na kabla yule dada ajauliza kitu nurdin akakata simu ile,akageuka kitengo cha mawasiliano
"Unaweza kunambia hii simu imetoka sehemu gani?!"
"Dakika tano afande"
"Poa"
"Embu piga tena"
Anasema jamaa wa kitendo cha mawasiliano
NURDIN akatii
Akaipiga simu ile na ikaita
"Mimi ni insp NURDIN inaitajika ujisalimishe mwenyewe kituo cha kati"
Jasmin akashtuka
Kipindi hicho alikuwa nyumbani kwake maeneo ya pasua
Nurdin akaelekezwa eneo hilo akaingia ndani ya gari lake kuelekea nyumbani kwa binti huyo katili.

#No_17

JASMIN amani ilitoweka moyoni mwake,alijua kipindi cha kuingia katika mkono wa Sheria kilikuwa kimewadia
'Maaskari wamejuaje?!,Na MARTIN si alihaidi kunilinda?! Embu ngoja ni m call'
Akaamuwa kumpigia MARTIN na kumwambia kuwa anaitajika kituoni,
MARTIN akamwambia swala lile si la kuongelea kwenye simu waonane muda huo huo ili walijadili swala hilo
JASMIN akakubali,maskin laiti angejua kilichopo moyoni mwa mwanaume huyo???!!!
Dakika kadhaa baada ya JASMIN kuondoka gari ya polisi ilombeba NURDIN ndani yake ilipaki mtaa wa nyuma toka katika mtaa aloishi binti yule akashuka insp akiwa kavaa nguo za kiraia akachepuka kuelekea katika nyumba ile ya jasmin.
Ni nyumba ya kupanga,akamuulizia na kuelekezwa chumba chake
Alipigwa na butwaa baada ya kukutana na kofuli
Akutaka kurudi nyuma akaingiza mkono wake wa kuume mfukoni akatoka na 'master key'
Au ufunguo Malaya akaupachika katika kofuli lile kufuli likatii akazama ndani
Kilikuwa ni chumba kipana kizuri
Nurdin akakagua kagua akuona ushahidi wowote wa mahana
Akapiga tena kitengo cha mawasiliano akawaambia anapiga tena zile namba wamjulishe mdada huyo yupo wapi
Akakata na kupiga namba zile
"Namba unayopiga haipatikani tafadhali jaribu tena baadaye"
Akakata ghafla msg ikaingia
Akafungua na kusoma....
'Sauti hiyo imetoka katika jengo LA makao makuu ya vodacom mliman city'
Ins NURDIN akasonya,baada ya kupewa taharifa ile yani kutopatikana kwa simu ripoti ndo hiyo
Akajikalisha katika kochi aina ya sofa alishakata shauri amsubiri hapo hapo
Nusu saa ikakatika yupo p,ale pale akiwa katika mawazo mazito
Juu ya vifo hivi vya utata na kutopata mwanga japo wa kumuhisi tu muuaji
Mawazo Yake yale akayakatisha baada ya simu yake kuita akaipokea
"Aroo afande kopro kipere hapa
naongea nipo kimbiji kuna mauaji mengine yametokea ya mwanamke kama Yale ya yule kaka wa Samora inn arobadirika rangi"
"Naja hapo saiv"
"Ovar"
Simu ikakatwa
NURDIN akatoka ndani ya chumba kile akasahau hata kufungua mlango wa watu
Akachepuka kuelekea nyuma ya mtaa ule na kuingia ndani ya kipira kile akatoka kwa spedi,alikuwa na uhakika vifo vile vinashabihana na vina lengo LA kuficha kitu
Ni kitu gani?!
Hicho ndicho alichopaswa akijue
Nusu saa alifika na kupokelewa na umati wa watu,waliye mzingira mwanamke mmoja aloanza kubadilika rangi na kuwa kama side
'Bila shaka huyo izrael nlomkosa home kwake ndo kaja kutenda haya kwa mwanamke mwenzake kwa nin lakin?!'
Aliwaza NURDIN na kujitoma uzuri mmoja simu ya binti yule aliikuta,ndo kitu alichokuwa akikikosea MARTIN kuacha ushahidi wa simu
"Huyu Dada alikuwa aliongea na kijana mmoja ambaye alitoweka kabla ya kifo chake na alionekana kama mpz wake"
NURDIN akashtuka!!!
Alitegemea muuaji angekuwa wa kike ila kusikia ni jamaa ake! Akakosa raha
"Huu ni mtandao au?!"
Ghafla wazo flani likaanza kumjia,fikra ambazo akuzipenda ziwe chanya
Muhudumu alitoa maelezo kwa ins NURDIN naye akayaandika
'Vifo hivi vitakuwa vinashabihana,iwe isiwe'
Kijana yule aliwaza akakumbuka ripoti aloipata mapenzi juu ya simu Kali iliyomuondoa duniani side
Mawazo juu ya binti alotoka nyumbani kwake yakamjia,akaapa kumsaka na ndiyo atakaye fumbua fumbo ilo
Maskini akujua kama Dada huyo ndo hiyo maiti ilikuwa Mbele yake
Mwili wa JASMIN ukapelekwa hospitalini Kwa uchunguzi
Bado kidogo roho ingemtoka INS NURDIN Kwa mshtuko baada ya kugundua yule msichana alouwawa kimbiji ndiyo yule alousika na mauaji ya side
Uhusiano wa simu mbili kati ya simu ya side na ya JASMIN ambazo zote zilikuwa katika mkono wake ulimtilia shaka
Na alipopiga namba ya simu ya JASMIN iliita ya yule Dada
NURDIN akapiga ngumi meza kwa mfadhaiko,
'Nini KINACHOENDELEA hapa na nani yupo nyuma ya haya matukio?!"
Akajiuliza mwenyewe kwa sauti kubwa akili ikimchanganya kila alipopiga hatua alirudishwa nyuma
'Itabidi huyu mwanaume aliyekuwa na huyu mwanamke hapatikane haraka atakuwa anajua kila kitu labda naye aangamizwe'
NURDIN aliendelea kuwaza
Akatuma namba zile za JASMIN kitengo cha mawasiliano
"Naomba mnitumie maneno ya MTU wa mwisho aliyeongea naye"
"Dakika mbili mkuu usikate simu"
"OK"
BAADA YA DAKIKA MBILI
"Mkuu unaweza kusikiliza sasa tumekutumia kwa njia ya audio"
"Ovar"
Simu ikakatwa
NURDIN akafungua audio ile alotumiwa na kuanza kusikiliza
JASMIN:aloo mpz
Upande w pili: nambie baby
JASMIN: mpz naitajika polisi ile ushu imesanuka ntafanyeje mpz?!
Upande w pili: (akashtuka) beby swala hili si LA kuongea kwenye simu tuonane ili tulijadili swala hili "
JASMIN: "Wap mpz?!"
Upande w pili: kimbiji
JASMIN: ok!!
Mwisho wa audio ile.,NURDIN akatabasamu ni wazi kila kitu kilikuwa wazi muhusika ni huyo kijana
Na ushahidi ulishapatikana
Akapiga tena simu kitengo kile cha mawasiliano na kuomba namba za huyo jamaa,pamoja na usajili wake
NURDIN alishtuka baada ya kumtambua ni MARTIN
tajiri mkubwa mjini MOSHI,hakukuwa na mtu ambaye alikuwa amfahamu MARTIN
Kumbukumb ya kifo cha jb kikamjia,hakuwa na shaka kuwa lengo la hivyo vifo vya watu wa tatu ni kuficha siri
Yeye ndo muuaji wa jb aliitimisha,huku akisikitika
Ripoti ilikamilika
Ushahidi ulikamilika
NURDIN akapeleka ripoti ile kwa bosi wake GOOD LUCK SILVESTER
"Naomba nisikilize kwa makini bwana NURDIN na si ombi ni amri sihitaji maswali hila nakuomba ufunge ilo faili na uachane na hiyo kesi..."
NURDIN alishtuka,akutegemea kuambiwa maneno Yale na mkuu wake
Kwa dakika moja aliya gandisha macho kwa bosi wake pasina kuyapepesa
Wakiangaliana kama ma jogoo ya kuku yalotaka kupigana

NURDIN KAMTAMBUA MUUAJI ILA KAPIGWA STOP
JE NINI KITAENDELEA?!!!
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu -18-

Ilipoishia toleo lililopita.

"Naomba niskilize kwa makini,bwana NURDIN Na si ombi ni amri,toka ngazi za juu,sihitaji maswali ila nakuomba ufunge ilo file na uachane na hiyo kesi,....
NURDIN alishtuka
Akutegemea kuambiwa maneno Yale na mkuu wake....
Kwa dakika moja akayagandisha macho kwa bosi wake pasina kuyapapasa
Wakiangaliana kama majogoo ya kuku walotaka kupiganaa

#Sasa_endelea!!!......
NURDIN akashusha pumzi ndefu,ishara ya kutua mzigo katika moyo wake.
Kijeshi ilikuwa ni amri kufata maagizo kutoka ngazi za juu
Akajinyanyua kikakamavu,na kupiga saluti akamkabidhi bosi wake file lile,bosi wake yule akalisweka katikati ya mafaili mengine
Kesi ile ikafungwa rasmi
Nafsi ya jb ikadhulumiwa
Ikafanyika pati ya uhakika nyumbani kwa MARTIN,kamishna akiwa kama mgeni rasmi
Kwanzia siku hiyo chokochoko zikasaulika mpaka miaka mitatu Mbele katika makaburi ya njoro wakati mvua ya gharika ikinyesha na kuezua mapaa
Katikati ya makaburi lilipokuwepo kaburi la Jb alipozuka jitu LA kutisha
Jitu lililooza na kutoa mafinyofinyo
Jitu hilo lilifanana na jb kwa kila kitu,
Baada ya kuibuka jitu lile lilienda kumwangamiza mwanasheria wa kampuni yake walokula njama na MARTIN wamuuwe akaghushi nyaraka za kampuni yake
Jitu lilibeba bisu
Kisu kama alichochomwa nacho jb nalo likamchoma jamaa yule bisu la koromeo Kama yeye walivyomchoma kwa kisu kile.
Jitu ( jb) akatoweka na kutokea palipokwepo nyumbani kwake alipokuwa akiishi na mke wake ambapo palikuwa na walinzi wawili walobakia katika group hatari la majambazi la 4 killers baada ya wawili side na musa kufa ili kuficha ushahidi
Ghafla nyuma ya nyumba ile kukaskika kishindo, bila kujiuliza Mara mbili mlinzi mmoja akiwa kashika silaha yake vizuri akatoka eneo lile kwenda kule kishindo kiliposikika
Mlinzi mmoja akibaki katika geti lile akiwa kashika silaha yake tayari kwa chochote
Ghafla kishindo kingine tena kikasikika sambamba na yowe
Yowe lile likamsukuma mlinzi yule aliyebaki pale getini kuelekea kule nyuma alipo enda mwenzake
Kosa!!!
Akuamini kile alichokiona,mwenzake alichomwa bisu Ia koromelo,macho kayatoa Pima
Mlinzi yule akapepesa macho eneo lile lakin akumwona aliyesababisha taharuki ile
Mshangao ukamvaa
Bumbuwazi likambumbukia
Wasiwas na woga ukamtawala
Akazunguka nyuma ya nyumba ile alichokiona kilimshtua
Rafiki yake,mlinzi mwenzake alikuwa chini katika dimbwi la damu yake mbichi
Mwili ukamsisimka
Kwa kihoro akakimbilia mwenzake na kuanza kumwita dully!!! Abdully nini kimekupata swaiba?!
Aliongea kwa uchungu huku akimtingisha kwa nguvu kama kufanya vile Kungemrudishia uhai.
Ghafla akasikia cheko nyuma yake
Cheko la dharau!!!
Cheko la kiburiii!!!!
Cheko La kejeli
Kwa wasiwasi kijana yule akazungusha kichwa chake taratibu kuangalia cheko lilipotokea
Alipatwa mshtuko kwa kile alichokiona,woga ukamtawala,
Macho yakatoka Pima
Silaha ile nzito ya kivita ikadondoka,jamaa yule KWA woga akawa akirudi nyuma
Jitu lile la kutisha likawa likimsogelea huku likimwangalia kwa macho makali,macho yalomtisha mlinzi yule
Bisu lenye mpini mpan,na ncha Kali likiwa katika kono lake lenye vinyweleo vya kutosha
Likaachia tabasamu, meno yake yalooza na kutoboka yakaonekana
"Mlikuwa mkijiita 4 killers ,mkaniua kwa mateso makali sana Leo ndo mwisho wenu........

ITAENDELEA
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu 19 & 20

Jitu (jb) liliongea kwa jeuri huku likipiga hatua kumfata mlinzi yule alobakia
Wazo lililomjia kijana yule ni kupiga kelele lakini akupata wasaa huo Kwani akujua ni sa ngapi jitu lilimfikia na kumchoma bisu lake la koromero kama mwenzake
Mlinzi yule akadondoka kama zigo na kutapatapa akatulia tuli
Jitu lile likaachia cheko lingine LA kejeli na kuivuka miili ya walinzi wale na kutokea Mbele ya lango la jumba lile
Likazama ndani
Alipoufikia mlango mkubwa wa kuingilia ndani ulofungwa akaunyooshea kono lake mlango ukatili amri ya kufunguka jitu lile likapita nyuma mlango ukajifunga kama kawaida
Likaibukia chumbani....
Kitandani walilala mtu na mke wake
Jitu likawaangalia kwa dharau
"Fatuma binti mrembo!..."
Jitu lile likaita kwa sauti ndogo ya kunong'oneza
Sauti ilopenya mpaka katika maskio ya binti yule,ghafla binti Yule akafumbua macho yake
Ana kwa ana na jitu
Likiwa limeshikilia bisu mkononi
Binti yule akashtuka kitendo kilichofanya jitu lile likenue mijino yake mibaya ilotoboka yenye rangi ya silva,ilotembelewa na finyofinyo wadogo ionekane
"Wew ni binti mrembo sikatahi,mrembo ulonitesa kwanzia kijijini nlipokupenda ukanitoa nishai,ila baada ya kufanikiwa ukaja kuniibukia mjini na lijibarua lako la kinafki kwamba unanipenda?!"
"Jacob?!!!....."
Binti yule akapata nguvu ya kuita
"Teh!,teh!,teh! Mimi si Jacob,Jacob mlishamuua eti muondoe gugu lililomea katika penzi lenu,"
"Nisamehe Jacob..."
Fatuma aliomba msamaha jitu likaachia cheko lingine la dharau
"Mim si JACOB,Mimi ni mzimu ulorejea,eti nyumba na gari ndo vilikufanya unsaliti eeh,si ungenambia mpz wangu naitaji nyumba?!,ina maana nyumba ilikuwa ina thamani kuliko roho yangu?! No Fatu siwezi kukuacha mzima tutaonana kuzimu mwana haramu wewe"
Binti yule wakati huo alikuwa akipikicha macho yake akijua pengine yupo ndotoni
Jitu lile lililotokea makaburini usiku ule mnene wenye mvua na gharika za kutisha likazidi kumsogelea binti yule
ambaye ghafla aliduwaa,na Kubaki ameganda kama sanamu
Sanamu la michelini
Akishindwa kupiga kelele wala kufanya chochote
Jitu akapiga hatua moja na hatua nyingine akawa amemfikia kabisa binti yule,akanyanyua bisu lake akamchoma moja kwa moja tumboni
Binti akafa akiwa kayatoa macho kwa uchungu,ulimi kaung'atia
'Adhabu ya usaliti ni kifo'
Leo hii msemo huo ulitimia kwa bi fatma.
Jitu likatoweka
Likijua fika litaacha nyuma taharuki pindi mume wa mwanamke yule akiamka na kumkuta maiti ya mke wake na za wale walinzi kule nje mbona kizaazaa?!
************************************

SURA YA NNE
Ni baada ya vifo vile vilivyosababishwa na jitu lile LA kutisha
Mwanga ulianza kumjia inspekta akamkodolea macho MARTIN kusubiri jibu lake juu ya visu vile
MARTIN akatingisha kichwa ishara ya kukana kuvitambua visu vile
NURDIN akamwangalia kwa macho makali,macho ya kumsuta kibosile yule
"Usijali mzee toa khofu wausika au muhusika wa matukio haya tutamtia nguvuni tu."
Akaongea inspekta nurdin ishara ya kumtia faraja mzee yule
MARTIN akatabasamu,tabasamu la matumaini
Martin alijua kwa vyovyote kuna mtu ambaye yupo nyuma ya mchezo huo
Nyuma ya mauaji hayo
Ndo alipizaye kisasi
Pengine ni ndugu au rafiki yake wa karibu na jb,ni yupi sasa wakati jb hakuwa na ndugu tofauti na yeye wala rafiki wa karibu zaid yake yeye?!
Akazidi kukosa raha
Katu akufikiria kuwa muuaji ni lijitu la kufikirika lililoibuka makaburini usiku wa kuamkia siku hiyo na lilikuwa mtaani
baada ya maongezi ya hapa na pale akamuaga inspekta yule na kutoka katika ofisi ile
Akaelekea ofisi ya rafiki yake kamishna Silvester mkuu wake wa kazi NURDIN aliye msitopisha kijana yule kuendelea na kesi baada ya kumtambua muuaji
"Pole sana swaiba kwa majanga yalokutokea,kwa kuwapoteza washirika wako wakuu ila usijali file hili nimemkabidhi kijana wangu NURDIN lazima muhusika atapatikana tu usijali kwa ilo ni kijana mchapakazi...na namwamin pia"
Baada ya maongezi ya hapa na pale MARTIN akaaga na kutoka nje alipo paki gari yake kulikuwa na gari LA kifahari aina ya pigout 42 mkabala na gari yake
Martin akaingia katika gari yake na kufungua vioo,katu akufatilia gari ile pigout 42
Ndani ya gari ile lililoibukia pale pale,ndani ya gari lile lilikwepo lile jitu la kutisha
Ghafla likabadilika,japo sura ni ile ile ila alikuwa ni kijana mtanashati,alivaa suti ilomkaa vyema,kichwani alinyoa mtindo wa vijana wa enzi hizo ( afro)
ndevu zake alizichonga o na kumuongeza umaridadi
Usingeweza kudhani wala kuhisi ndo lile likiumbe ambao usiku wa kuamkia usiku huo lilikuwa na sura mbovu,ya kutisha, meno yalooza na kutoa mafinyofinyo
Likamkata jicho Kali MARTIN alokuwa akiingia ndani ya gari yake
Jicho lake likatoa shoti ,shoti ilo mpa maumivu makali na ya ghafla ya kichwa Martin
Ila maumivu Yale ayakudumu yakatoweka muda ule ule
'Tutaonana baradhuli wewe!'
Mtu yule akanong'ona mwenyewe
Martin akawasha gari na kuondoka kituoni pale na kumpa wasaa mzuri MTU yule wa ajabu kushuka
Akaelekea uelekeo wa ofisi ya NURDIN na alipoifikia pasina kupiga hodi akazama ndani
NURDIN akashtuka!!!

#No_20
Ujio wa mtu yule alozuka kimaajabu ajabu katika ofisi yake ulimshangaza.
mtu yule akampa tabasamu la kumuondoa wasiwasi ins yule machachari,tofauti na mategemeo yake hofu ilimuandama na nywele zilimsisimka
Kwa nini awe na hofu ya namna ile hali ya kuwa yeye ni afande tena inspekta mwenye mbinu 'musharabu' za kupambana na mualifu yoyote ambaye angekwepo Mbele ya macho yake?!
'Machale' ni aina ya msisimko unaomtokea mtu kuhisi kitu cha hatari kinachotarajia kuja Mbele yake kabla akijamfikia
Machale ndiyo yalomkumba kijana yule,akutaka kuipuuza hali ile,akajitaadharisha kuwa makini....
Mtu Yale akaenda kuketi,katika kiti cha wageni akamwangalia inspekta kwa dharau....
"Ni kusaidie nin mzee?!"
NURDIN akajitutumua kumuuliza swali!
Jamaa yule akajikolesha ishara ya kuweka koo sawa
"Kwa jina naitwa JACOB ukiipenda niite Jb"
NURDIN akashtuka kwa kusikia jina lile,jb akatabasamu meno yake meupe yalojipanga vyema kwa mpangilio mzuri katika kinywa chake yakaonekana
NURDIN akataka kusema kitu akashondwa,akujua aseme nini!
"Na kisa kizuri sana nataka kukupa inspekta ni kisa cha kale ambacho pengine kinaweza kuwa akina mushiko katika maskio yako"
Mtu yule aliyejitambulisha kama 'jb' akaweka tuo kisha akakuna kidogo ndevu zake zilizopendezesha kidevu chake kisha akaendelea....
"Hapo zamani zakale palitokea paka na panya walotokea kuwa marafiki wakubwa sana urafiki wao ulianzia katika shamba moja la mkulima mmoja paka ndo aliye mpokea panya katika shamba lile wakawa wanafanya kazi kwa bidii katika shamba lile na kufanikiwa miaka ya badae kulinunua,na kuwa chini yao wakaweka vibarua na wenyewe wakanunua mashamba mengine mengi katika kijiji kile....
" mh!,..."
Nurdin akaguna akijiona 'boya' kusikiliza kisa kile ila kuna kitu kilim lazimisha kuendelea kusikiliza,akiwa kakunja sura yake JB akaendelea....
"Siku zikasonga tamaa bwana uzuka pindi mafanikio yanaposhika hatamu,ndiyo!!,tamaa ikamshika panya na kutamani kumiliki Mali zote,teh!,teh,teh, kumuua paka ndo yalokuwa mawazo yake eti bwana mdogo panya anaweza kumuua paka?!"
Akiwa kakunja sura akatingisha kichwa kukataa kuwa panya awezi kumuua paka, huku akionesha kuchukua waziwazi simulizi ile ya kale.
Ila sasa ambacho akukishangaa na alipaswa ashangae ni kitendo cha kuendelea kumsikiliza jb wakati uwezo wa kumfukuza alikuwa nao,na stori ile aliichukia katika nafsi yake kwani aikuleta maana yoyote kichwani kwake
Stori ya kale!!!...
Ya paka na panya?!
Kwa nini asiwasimulie wajukuu wake aje amsimulie yeye?!
Alihisi ni mwenda wazimu kamtembelea
''Umekosa na pia umepatia..."
Jb akaendelea
"Si kweli kuwa panya hawezi kumuua paka!,mbona panya yule aliweza kumuua paka?! Na Mali zote kubaki chini Yake?!"
Jb alipofikia pale akakunja sura!,tabasamu lile likayeyuka
"What?! Kivipi haiwezekani panya kumuua paka"
Nurdin akajishtukia maneno mfululizo yamemtoka akaachia tabasamu ni wazi alianza kukipenda kisa kile cha kufikirika cha zama za kale...
Cha paka na panya!!!
Jb akaachia bonge la cheko akajinyanyua katika kiti kile na kuanza kuondoka huku akiendelea kuongea
"Gud kijana panya awezi kumuua paka na ndo maana mpaka sasa paka akikutana na panya anamla kama akimkamata tutaonana tena kijana"
Jb (paka) akafungua mlango na kutoka akimuacha insp NURDIN katika taharuki!!! Ya sintofahamu!!!
"Ina maana huyu jamaa katoka uko alikotoka kuja kuniadidhia habari za paka na panya?!"
Martin akajiuliza akataman tena kumuona jamaa Yule haraka akajinyanyua pale na kulisogelea dirisha akapandisha pazia na kuchungulia nje!!!
Palikuwa patupu
Kwa muda alotoka lazima angemwona tena asingekuwa amefika mbali
NURDIN akashtuka,kengele ya hatari ikagonga katika ubongo wake
Akakifikiria tena kile kisa!
Naaaaam kwa uwazi akakipatia maana,maana ambayo wakati msimuliaji anasimulia hakikuwa na maana yoyote!!!
Wakati huo Jb alikuwa katika mlango wa kuingilia ofisi ya kamishna wa kituo kile Silvestar alimpita katibu muhtasar
Ni wazi mwana dada yule akumuona
Jb akazama ndani ya ofisi
Silvestar akayatoa macho kwa mshangao
JE NINI KITAENDELEA?!
NURDIN KAGUNDUA NINI KATIKA KISA KILE?!
JB ANA KWA ANA NA KAMISHNA SILVESTA NINI KILIENDELEA
ITAENDELEA.....
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu -21-

ilipoishia...
Wakati huo Jb alikuwa katika mlango wa kuingulia ofisi ya kamishna wa kituo kile SILVESTER
JB alimpita katibu muhtasari,ni wazi mwanadada yule akumuona kijana yule
Jb akaufungua mlango na kuzama ndani
Silvester akayatoa macho kwa mshangao....

#Endelea...

DAKIKA KADHAA NYUMA
OFISINI KWA KAMISHNA.

Baada ya NURDIN kumaliza mazungumzo na MARTIN na kuondoka, kijana yule akaelekea ofisini
kwa kamishna yule na kuketi kwenye kochi
Akashusha pumzi ishara ya kutua mzigo
Alimkuta kamishna akiwa bize na makalabrasha yalojaa katika meza yake
Akanyanyua uso kumtazama kijana yule
"Pole sana MARTIN swahiba,juu ya kuwapoteza washirika wako wakuu swala ilo ntalifatilia kwa makini mpaka kumtambua muhusika na nahisi ni MTU alipae kisasi Mimi nipo nyuma yako....
Martin akatabasamu,
Tabasamu la faraja
baada ya maongezi ya hapa na pale martin akaaga muda ambao martin aliondoka ndo muda ambao walikutana na jb sehemu ya maegesho ya magari
jb akashtuka na kuelekea ofisini kwa nurdin akampa visa vya panya na paka na baada ya hapo akatoka na kuelekea ofisi ya kamishna,alienda kuketi kwenye kiti bado kamishna alibaki ameduwaa
'Kwanini secretary ajanipigia simu kunijulisha juu ya kuwa kuna mgeni ni ka mruhusu aingie kama wageni wengine,?!'
Akawaza lakin ghafla akashtuliwa na kicheko hafifu cha kejeli cha kijana yule
" Mimi ni tofauti na wageni wengine unaowajua wewe!"
Kamishna akashtuka
Ni baada ya mgeni yule wa ajabu kumjibu mawazo Yake
"Nadhani atufahamiani kamishna kwa jina mimi naitwa JACOB BONIPHAS ( JB) Ni mpelelezi wa ki taifa kutoka makao makuu ya jeshi la polisi
nimekuja kuungana na maaskari wa huku kwenu kufatilia juu ya vifo tata vinavyoendelea hapa wilayani"
Kamishna akatabasamu,tabasamu la faraja,faraja lenye walakini ndani yake...
Jb aliliona hilo akaingiza mkono wake katika begi lake dogo alilovaa mgongoni akatoka na bahasha kubwa...
Akamkabidhi kamishna yule
Ilikuwa ni barua kutoka wizarani!
Makao makuu ya jeshi la polisi
"Nimekuja huku kwa kazi maalum ni juu ya vifo vinavyoendelea hapa wilayani kwa siku mbili tatu za nyuma"
Kamishna yule akatabasamu,akaipitia ile barua baada ya kuridhishwa nayo akamkaribisha kijana Yule pasina kujua kuwa yule si binadamu....
Akanyanyuka kwa lengo la kwenda kumtambulisha
'Secretary' alishtuka baada ya kutoka bosi wake na mgeni yule ambaye akakumbuka kama alimruhusu aingie au kumuona mahala pale
Aliingia saa ngapi?!
Ilikuwa ndo Mara ya kwanza kumuona ilhali mtu yeyote asinge weza kumuona bosi wake pasina kupita kwake
Hali ya sintofahamu ikatanda katika kichwa chake,ndani ya moyo wake alikiri kijana yule alikuwa ni handsome boy,mtanashati mwenye sex body
Akajikuta akiuvamia moyo wake kwa kasi sana na kuomba hifadhi
Binti yule akajikuta akimwangalia jb kwa macho ya matamanio
"Kwa jina anaitwa Jacob ni afisa upelelezi kutoka makao makuu jb huyu ni katibu muhtasi wangu nadhani wakati unaingia hapa ulionana naye anaitwa MAIMUNA"
binti yule akashtuka Jacob akampa mkono ishara ya kumpa salam,MAIMUNA akaupokea Jacob kwa pembe ya jicho lake akamkonyeza sambamba na kuutekenya kidogo ule mkono
Binti yule akaangalia chini kwa aibu,hisia zikiucharaza moyo wake
Wakaachiliana
"Atakuwa pamoja na ins NURDIN kufatilia hivi vifo tata"
Akamwambia Dada yule,huku wakijiandaa kuondoka wakielekea ofisini kwa NURDIN
*
NURDIN bado mawazo yalimsonga kutokana na ujio wa mtu yule wa ajabu!!!
Kisa chake cha paka na panya kilileta maana flani katika kichwa chake
Maana ambayo akuikubali moja kwa moja!
'Huyu mtu ni nani?!' Wazo hilo likakosa jibu stahiki katika mawazo yake
"Kwanini watu wote wanaouwawa wanachomwa na kisu cha koromeo kama cha....na kwa nini ni washirika wa MARTIN?!,Marafiki zake wa karibu? hapana! Kwa nini iwe ivyo?!,na kwa nini nilipomtambua MARTIN ni muuaji wa kipindi kile nisitishwe?! Kufatilia kesi ile,kuna siri hapa ndani yake kuna kisasi ila aina budi kumpata muuaji...na yule msichana mwana habari je?!'
Wakati akiendelea kuwaza vile ghafla mlango ukagongwa Mara moja Mara ya pili ukafunguliwa na akaingia bosi wake kamishna akiongozana na yule mtu wa maajabu kwake
NURDIN akawatumbulia macho ya mshangao
" nimerudi swaiba"
Kamishna akashtuka akamkodolea macho jamaa yule
"Ushaonana na huyu?!"
Kamishna akauliza kwa wasiwasi akimnyooshea kidole NURDINI
Je jb atajibu nini?!

ITAENDELEA SAA TATU USIKU
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu 22&23

Ilipoishia...
Nurdin akawatumbulia macho kwa mshangao,..
"Nimerudi swaiba"
Kamishna SILVESTER akashtuka akamkodolea macho jamaa yule
"Ushaonana na huyu?!"
Kamishna akauliza kwa wasiwasi akimnyooshea kidole NURDIN...

Endelea....
Jb akatoa kicheko hafifu,
kicheko cha dharau!,
"yah of corz swaiba kabla sijaja kwako nilikuja kumtembelea na kupiga nae story!
"hee!"...
ikawa zamu ya Kamishna kushangaa sambamba na kupigwa na butwaa! kisha akaipotezea hali ile,
"ok ningependa nikutambulishe huyu anaitwa ins NURDIN ndo askar mwenye dhamana ya kusimamia kesi hii"
baada ya kuongea vile kamishna akamgeukia NURDIN
"Insp huyu anaitwa jb ni mpelelez kutoka makao makuu amekuja kukuongezea nguvu katika kesi yako naiman sasa muaji atapatikana kwa haraka zaidi na ripoti ije kwangu kama kawaida!
"yes mkuu"
wote wakaitika sambamba na kutoa saluti ishara ya nidhamu.
kamishna akatoa tabasamu
"naiman mtatumia ofisi hii moja"
baada ya kuongea neno lile akatoka na kuwaacha majamaa wale,jb akaenda kuketi kwenye kiti cha pembeni
"Unaweza kunipatia hilo file nikalipitia pitia?!"
NURDIN hakuwa Mbishi akamkabidhi kijana yule
"Duuu?!"
Jb akatoa mguno hafifu
Nurdin akamwangalia kwa kumshangaa
"Mbona kama ni kisasi?!"
"Kwa nini unahisi ni kisasi?!" Nurdin akamrudishia swali
"Juu ya vifo vyenyewe,kuwa vya aina moja lazima tupate chimbuko la hii kitu"
Nurdin akatabasamu
Hapo ndipo alipo pataka
Chimbuko ni MARTIN
Ndo mwenye jibu la kumtambua muuaji
ikabidi aanze kumsimulia kisa kile kilichotokea miezi kadhaa nyuma juu ya mauaji ya kijana JACOB alokuwa tajiri mkubwa jijini pale mwili wake ulikutwa pembezoni mwa bwawa ukiwa umechomwa kisu cha koromeo
Rafiki yake kipenzi na mfanya biashara mwenzake MARTIN akasimamia mazishi Yale n yeye NURDIN akapewa idhini ya kufatilia kesi ile
Ilikuwa ni kesi ya utata na kila alokuwa akumuusisha na mauaji Yale aliuwawa mpaka mwisho alipokuja kumgundua muasisi au alokuwa nyuma ya mauaji Yale ni MARTIN
Na pindi alipogundua vile akastopishwa kufatilia kesi ile na bosi wake
Ni wazi kulikuwa na mianya ya rushwa katika kesi ile
Na hisi kesi hiyo kwa vyovyote ndo kisasi cha jamaa yule ivyo nahisi ni rafiki yake au ndugu yake na jb atakuwa ndo muhusika wa kumlipizia ndugu au rafiki yake,kazi IPO kumtambua mtu huyo ambaye anaua kama jb alivyouwawa kwa kuchomwa kisu cha shingo"
Baada ya maelezo Yale marefu NURDIN akaweka tuo
Macho yake makubwa akamtumbulia mtu yule akitegemea kupokea mawazo.
katu hakujua kuwa huyo ndo muhusika
Akujua kuwa huyo ndo jb alodhulumiwa nafsi yake na kurejea duniani kulipiza kisasi
Hakujua kuwa yule si binadamu kama alivyo onekana kwa nje
Ule ulikuwa ni MZIMU ULOREJEA
Ulirejea kwa kazi moja tu!
Ambaye alishaifanya na sasa alikuwa akiimalizia
Wakati akimsimulia jb alimsikiliza kwa makini NURDIN alipomaliza jb akaingiza mkono mfukoni na kutoka na pakiti akaiweka mezani akachomoa sigara moja na kuipachika kinywani
akafungua droo na kutoa kiberiti akaiwasha sigara ile na kupiga funda moja akaachia moshi ukasambaa hewani
"Samahani"
Akamtaka radhi NURDIN
"Kuna umuhimu wa kumtambua muuaji lakini kabla atuja mtambua lazima kesi hiyo ya jb ifunguliwe na kutatuliwa"
"Heee aitowezekana kinachopaswa ni kuangalia kesi hii kumpata muuaji wa wausika hawa ile ilishapita"
"Ok! Kwa vyovyote vile Martin anamtambua muuaji yeye si ndo alikuwa rafiki kipenzi wa marehemu basi inapaswa atudadavulie ndugu wa huyu jamaa utakuwa mwanzo wa kuujua ukweli hiyo moja pili lazima kesi ya huyo jamaa ifunguliwe mi si nimetoka makao makuu hili lisipofanyika ntalifikisha ngazi za juu kwanza ngoja nkaongee na huyo ndumi la kuwili lazima martin afikishwe Mbele za Sheria"
Baada ya kuongea maneno Yale akajinyanyua na kuusogelea mlango akaufungua na kutoka
Akaelekea ofisini kwa kamishna
"Vipi mrembo na weza kumuona mzee?!"
"Tena,?!"
"Yah of corze"
Akajibu jb akitoa tabasamu na kuruhusu mpangilio wake mzuri wa meno yake kuonekana
Dada yule akamrudishia tabasamu huku akiupeleka mkono wake katika mkono wa simu kabla ajapeleka mkonga ule sikioni akasita na kuurudisha chini!
"Hivi sazile ulipitia wapi mbona si kukuona?!"
Jb akashtuka akulitegemea swali lile!

#23
Macho yake mkubwa yakanata kwa binti yule akabaki amemkodolea macho
Ghafla akaachia tabasamu pana katika mdomo wake
"Kimwana ukimchunguza bata sana utomla! Ila siyo ishu mimi ni mpelelezi wa kitaifa na si kitaifa tu ni kimataifa hivyo chochote naweza Fanya,popote naeza kwenda na kuingia wenyeji wasitambue"
Binti Yule akaachia kicheko hafifu,kicheko ambacho yeye ukitoa kwa watu maalumu,kwa nia flani
Ya kumtega aliyoko Mbele yake...
Macho yakionesha ishara ya kumuitaji kijana yule,...
"Ok mpelelezi wa kimataifa unaweza kuingia"
Binti yule akaruhusu ilhali akisahau kumjulisha bosi wake
Jb akazama ndani na kumkuta kamishna akiwa bize na ma kalabrasha yalojaa katika meza yake
Kamishna akashtuka kumuona JB pale
Kitendo cha kutopigiwa simu na katibu muhtasi wake kilimshangaza
Alikuwa jambo la kawaida
Akakuna kichwa chake kwa tafakari kuu...
"Bosi mbona kama unaonekana una mawazo nin tatizo?!"
Akashtuliwa na sauti ya kijana yule
"amh aaah!,yah no thing best I'm ok"
"Ok!,siyo ishu kuna kilichonleta bosi!"
"Ok na kusikiliza kijana angu"
Kabla JB ajaongea kitu kamishna akashika mkonga wa simu yake na kupiga mapokezi
"MAIMUNA naomba kahawa moja nawe mh utaitaj nin chai , maziwa au kahawa"
"Maziwa mkuu"
"OK na maziwa"
"Sawa mh"
MAIMUNA akajibu Baada ya kuikata simu ile,akapiga mpaka jikoni na kuitaji vitu hivyo
Baada ya dakika tano mpishi mmoja akamletea na binti yule akaingia navyo ndani.....
Baada ya kuviweka kwenye meza akatoka na kuwaacha wakubwa wake wakianza maongezi
"NA kusikiliza kijana wangu"
"Ok bosi nimeona Yale makalabrasha ya kesi hii tata ambayo bila shaka ndani yake ni kesi ya kisasi!,ikabidi niichimbue kwa jicho la tatu,
nikagundua kuwa kuna siri ilojificha,siri ambayo aikutatuliwa!,siri ambayo laiti kama ingetatuliwa hapo awali wala mauaji haya yasingetokea"
"Una maana gani kijana?!"
Kamishna aliuliza kiunyonge,ni wazi alijua ni nini jb alimaanisha ila alitaka tu udhibitisho,na jb akamzibitishia!...
"Kamishna kesi hii walouawa katika historia inaonesha ni marafiki wa karibu au tunaweza kusema watu wa karibu wa bwana MARTIN...
je kisa nini?!
Kwa mpelelezi yoyote lazima atajiuliza hivyo na ili kupata mtu wa kumpa jibu sahii ni huyo huyo MARTIN kwa lazima au hiari"
Jb alipofika hapo kamishna akakunja uso akupenda jambo lile
"Kivipi afande kwani yeye ndo kawa tuma watu wafanye mauaji hayo mpaka alazimishwe kuwataja?! Na kama ndiyo kuna ushahidi gani nyinyi ni maaskari tena wasomi mlopitia adi nje fanyeni kazi kisomi"
Kamishna aliongea kwa hasira
"Sina maana hiyo joh!,chimbuko la kesi hii martin unajua kivipi?! rudi miaka mingi nyuma kuna mtu aliwahi kuuwawa jb ndo jina lake na kesi ikafuatiliwa na dawati la kituo chako....
Vizuri zaidi wewe ukamkabidhi kalabrasha NURDIN ambaye alikuja kumtambua MARTIN kama muuaji ila wewe kamishna mla rushwa ukamzuia kijana kufatilia hiyo kesi..."
" nani mla rushwa?!"
Kwa jazba kamishna akauliza
"Wewe mla rushwa na kama siyo hivyo kwa nini umzuie kijana kumkamata huyo mse..n...g ( tusi) mwenzako"
Ilikuwa ni fedheha kwa kamishna kutukanwa na kijana yule alokuja siku hiyo hiyo
Hasira zikampanda kwa wepesi wa ajabu akajinyanyua na kurusha ngumi
Ila jb aliiona akaukamata ule mkono na sekunde chache ukalia kaaaaaaaa!!!!
Yowe likafatia...
" uwezi nipiga kamishna mi si mtu wa kawaida ntakuua dakika hii hii fedhuli mla rushwa wewe"
Aliongea jb
Maneno Yale sijui kama kamishna aliyasikia kwani mawazo yake ayakuwa pale
Teh! Teh! Teh! Ndiyo ndugu msomaji mawazo ya kamishna yule yalikuwa nchini Cuba miaka 30 nyuma akiwa bado kijana mdogo mafunzoni
Ndiyo alipopata pigo kama lile
Ila anakumbuka alinyanyuka japo alikuwa na maumivu makali na kuikamata meza na kumtupia mpigaji
Ambaye ni mwalimu wake
Meza ile ikatua kisogoni na mwalimu yule akadondoka na kupoteza maisha
Kwa chuo ikawa sifa nzuri Kwake akapata umaharufu....
Ndiyo
Mawazo hayo yakamtuma ajinyanyue na kuikamata meza ilokuwa Mbele yake kompyuta na ma faili yakidondoka chini na kuielekeza katika kisogo cha kijana yule
Kama miaka ile chuoni Cuba alipoielekezea kwa mwalimu wake
Akaidondoshea hapo kisogoni
Kama alivyoidondoshea kwa mwalimu wake
Ila alicho kiona!....duuu!!!!

Je KAMISHNA KAONA NINI?!
UO NDO MWISHO WAKE?!
 
MZIMU ULIOREJEA

sehemu 24&25

Ilipoishia...
Mawazo hayo yakamtuma ajinyanyue na kuikamata meza ilokuwa mbele yake kompyuta na mafaili yakidondoka chini na kuielekeza ktk kisogo cha kijana yule.
kama miaka ile chuoni cuba alipoielekeza kwa mwalimu wake
akaidondoshea hapo kisogoni
kama alivyoidondoshea kwa mwalimu wake
ila alichokiona!....duuu!!!

Endelea...
Ile meza ilipotua kisogoni ni kama ilitua katika chuma,wala jb akutingishika kwa pigo lile
Kamishna akapigwa na butwaa akainyanyua tena meza lle lakini alishachelewa jb alijizungusha na kumtandika teke
Kamishna akasambaratika chini,akiachia yowe
"Kwa taharifa tu! Mafunzo nlopitia Mimi hata robo yake una! Pili usi jidanganye kupiga simu makao makuu na kueleza nlichokufanya ntaanika maovu yako yote na utaona kitakachofatia so unajua huu ni wasaa wa nani eeh hapa kazi tu Mr natoka naitaji umpe Maimuna file la jb anletee ofisini kwangu
Baada ya kumaliza jb akatoka akimuacha kamishna akigaa gaa kwa maumivu hapo chini
Akajitahidi kunyanyuka na kukaa kwenye kiti chake
'Ina mahana uyu binti akusikia ugomvi humu ndani au?!'
Akawaza kamishna akiangalia uharibifu ulotokea
Simu,mafile na kompyuta yake ndogo vyote vilikuwa chini
Ni baada ya yeye kuinyanyua meza ile kwa ghafla vitu vile vikiwa juu yake
'Eti nimpe file la kesi ya jb siku zake zinaesabika huyu nyang'au ngoja sasa'
Akawaza kamishna Yule na kutoa simu yake mfukoni akabinya tarakimu kadhaa na kuipeleka simu maskioni
Simu ikaita....
Maimuna akatoa macho kwa mshangao,ni baada ya kumuona mpigaji wa simu yake
Alikuwa ni bosi wake!
'Kwa nini asitumie simu ya mezani?!"
Akawaza huku akibinya batani ya bluu kuruhusu simu yake
"Nakuitaji ofisini"
Baada ya kukata simu akajinyanyua na kuelekea ofisini kwa bosi wake
Akashtushwa kwa mandhari alokutana nayo
"Natoka weka ofisi vizuri"
"Kimetokea nini bosi?!"
Kamishna akujibu kitu akavaa koti lake la suti na kutembea huku akichechemea
Ni wazi aliona kuwa secretari wake yule alikuwa akimsanifu
Hata Maimuna pia alipigwa na butwaa
Kwa nini asisikie Sauti ya kudondoka kwa vitu vile?!
Na ni ugomvi kisa nini?!!
Akakumbuka jb pindi alipotoka katika ofisi ile
Akuonesha sura yoyote ya ugomvi
Tabasamu lilipendezesha sura yake kama kawaida
Kitendo cha macho yake na ya jb kukutana moyo wake ukapasukaaaa
Alikiri moyoni mwake kweli kumpenda
Akapeleka macho yake pembeni
Na alipoyarudisha kwa kijana yule alishtuka baada ya kumuona yupo karibu yake
Bado hisia zilimbana na kumsumbua
Akujua ni sa ngapi alimpa mdomo kaka yule,naye jb akaupokea
Wakaama katika sayari hii
Jb akaupeleka mkono wake na kuanza kuyapapasa mapaja laini ya binti yule!
Maimuna alilegea ghafla akazinduka baada ya kujigundua yupo ofisini tena eneo la mapokezi
"Sory jb naitaji nkutoe lanchi Leo"
Binti Yule akaongea kwa sauti nyembamba sauti ilozidiwa na hisia za mapenzi
Jb akaachia tabasamu jingine
"OK madamu ni wewe tu"
Maimuna akashusha pumzi ndefu
'Laiti kama wangekuwa na ugomvi kati ya kamishna na jb,kijana yule angetoka na ghadhabu asingeweza kunfanyia kama alivyofanya abadani'
Binti yule akazidi kuchimba kidonda cha mawazo katikati ya ubongo wake.

#SHERATON_HOTEL
Hilikuwa ni hoteli ya kifahari yenye nyota Tatu
Ndani ya chumba kidogo,chenye thamani zote zinazoitajika ndani,kitandani aliketi kamishna akiwa ameghadhibika
Nje ya hoteli ile,maeneo ya parking ilipaki gari ya kifahari akashuka MARTIN na kuelekea katika lift akabonyeza namba tatu lift ikafanya kazi yake vyema
Dakika chache alikuwa Mbele ya mlango mkubwa akabonyeza kengele,kamishna pale alipolala akashika kitu mfano wa rimonti na kuielekezea katika mlango ile
Mlango ukafunguka na martin akajiingiza ndani
"Vipi mkuu mbona unaniita ghafla ghafla kuna tatizo gani?!"
"Kuna kirusi katika mipango yetu kinachotakiwa kifomatiwe kabla akijala ma faili yetu"
"OK nipe jina na anapoishi"
"Ni nusu komando kutoka makao makuu kaja kwa speed hasubuhi hii anaitaji file la jb lifunguliwe..."
"What?!"
"Yah uchukuliwe sheria na mbaya zaidi kanipiga lazima afe kwa namna yoyote ile....

#No_25
Ilipoishia.....
"Kuna kirusi katika mipango yetu kinachotakiwa kifomatiwe kabla akijala ma faili yetu!"
"ok! nipe jina lake na anapoishi!"
"JB ndo jina lake! kama hasimu wako wa miaka kadhaa!"
pindi Kamishna yule akilitaja jina la jb Martin akashtuka,kamishna akaendelea....
"Ni nusu komandoo!,katoka makao makuu kaja kwa spidi kali asubuhi hii anaitaji faili la Jb lifunguliwe!..."
"Whaat?!"
"yah uchukuliwe sheria na mbaya zaidi kanipiga lazima afe kwa namna yoyote ile..."
endelea...
"Kakupiga? kivipi mh?!"
bado Martin alibumbuwazika
"ndo ivyo! kantukana,kandhalilisha,mla rushwa ni mimi na maneno yote ya kejeli!"
"ooops! pole sana mh! ucjal huyo kiumbe hana masaa 24 atakuwa tayar hayupo katika uso wa dunia niachie mim"
"good! anaishi na Nurdin katika nyumba za kota!,"
"Vizuri tuta mtumia kikosi kazi hakuna litakalo haribika"
"Now naenda home kupumzika stegemei kumuona huyo mpuuzi kesho kazini"
Ni baada ya maneno Yale kamishna akanyanyuka na kutoka ndani ya hoteli ile,
Martin akashika simu yake na kubonyeza tarakimu kadhaa
Akaiweka sikioni...
"Sheraton motel ghorofa ya kwanza chumba namba tano"
Akakata simu na kujitupa kitandani
Ilikuwa moja ya hotel yake kubwa mjini pele,hoteli alopenda kufanyia mikutano yake ya siri,ndo maana hata kamishna akuangaika akaenda pale!

*************************************
Robo saa baadaye Martin alikuwa kazungukwa na vijana wa kazi!
Ni wanajeshi walotumiwa kinyume na viapo usiku
Pindi walipotengewa fungu la fedha walikuwa tayari kufanya walichotakiwa hata kama kilikuwa kinyume na sheria
Wakaelekezwa kuhusu jamaa yule
Jinsi ya kumpata
Na siku hiyo hiyo alipaswa aondoshwe katika ulimwengu huu
Watu wale waliijua kazi
Usiku wa manane ndo muda walopanga kutenda jambo hilo
Na kwa bahati nzuri zaidi usiku huo Nurdin asingekuwepo kwa kuwa angekwepo kituoni kwa ni ilikuwa ni wiki yake ya usiku.

*************************************
Ni katika jumba moja la kifahari lenye ulinzi madhubuti,aliibuka kiumbe wa ajabu
Jitu!
Ni lile lile lenye kutisha lakini safari hii akutisha
Lilivaa nguo zilizo chanika,ndevu katika kidevu chake zilisokotana
Kichwani alikuwa na kipilipili
Alitokea katikati ya lango la ndani ya nyumba ile
Akabonyeza kengele na kusubiria kufunguliwa...
Ndani ya nyumba ile mmama wa makamo alikuwa akiangalia runinga na Dada wa kazi
Ghafla wa kashtuliwa na kengele
Dada yule wa kazi akajinyanyua kutaka kwenda nje ila mama yule wa makamo akamkataza na kwenda yeye
akuwa na shaka kuwa mgongaji ni mumewe kwa kulitambua hilo alihitaji kwenda kumpokea yeye kutokana na mafunzo alofundwa kabla ajaolewa miaka kadhaa nyuma
Akaufikia mlango na kukikamata kitasa akakizungusha!
Na mlango ukamtii na kufunguka
Ahmadi!! Alichokutana nacho almanusura adhirahi
Mtu wa ajabu alikuwa Mbele ya macho yake!
Kichaa si kichaa,mtu ambaye hakuwa na shaka kuwa ni maskini wa kutupwa na lengo la kuja pale ni kusaidiwa
Omba omba
Mawazo Yale yakamuondosha woga na kumjenga katika hali ya dharau
kukitazama kiumbe kile kilichokuja masiku kadhaa toka makaburini
MZIMU ULOREJEA
'Ameruhusiwaje kuingia humu ndani?!,na walinzi getini?!'
Swali hilo likateleza katika ubongo wake
Akiwa ameushika mlango macho yakiwa kwa mtu yule,ila mawazo yalikuwa mbali
Ghafla akashtuliwa na sauti kavu ya kiume yenye kitetemeshi!
"Mmmmh! dada,Mrembo hata unikaribishi?!"
Dada yule akajikuta bila idhini yake akimpisha jitu pale mlangoni
Jitu likaingia mpaka sebuleni na kuketi katika sofa
Binti yule mfanyakazi alipigwa na butwaa akabaki akimshangaa mtu
Yule
"Naima tupishe na maongezi na mgeni"
"Sawa mamaa"
Binti yule akaitika na kutoka sebuleni pale akakimbilia ndani
"Kwa jina naitwa JACOB ni rafiki yake na mumeo wa muda mrefu
"Waoooh nafrah kukufahamu hila mbona uko hivyo?!"
"Ni story ndefu Dada yangu hila walimwengu?!"
"Walimwengu?! Mbona skuelewi?!"
"Walimwengu wabaya Dada Mimi skuwa hivi nilikuwa tajiri mkubwaa nlomiliki majumba makubwa makubwa ila walimwengu wakanifilisi ndo saivi nipo hivi"
"Kwa hiyo ndo umekuja kwa Martin ili iweje?!"
"Ansaidie"
Dada yule akatoa cheko,cheko la dharau
Huku akimwangalia jb kwa dharau
"Naomba utoke kabla sijawaita walinzi"
"Nsaidie Dada yangu hata mia mbili"
"Tokaaaaaa"
Akasema Dada yule sambamba na kumsukuma mtu yule
mtu yule akadondoka
Kosa!!!
"Binadamu Bwana! Mna vichwa vigumu sana teh teh teh vichwa vya panzi wepesi kusahau! Pamoja na kukukumbusha kote umeshindwa kukumbuka,miaka mitatu nyuma we ukiwa mwanafunzi wa chuo una kumbuka ulimshauri nini mpz wako?!...

JE Dada huyu mke wa MARTIN alimshauri nini MARTIN?

VIPI JB MPELELEZI ATAKUFA?!
mtu mvaa nguo chafu je atamfanyeje Dada yule.

ITAENDELEA...
 
MZIMU ULIOREJEA

Sehemu -26-

ilipoishia
"Binadamu bwana mna vichwa vigumu sana teh teh teh teh vichwa vya panzi wagumu kuelewa wepesi kusahau pamoja na kukukumbusha kote umeshndwa kukumbuka?!, miaka mitatu nyuma we ukiwa mwanafunzi wa chuo una kumbuka ulimshauri nini mpz wako?..

Endelea!
"Miaka mitatu nyuma?! mimi kwan nlimshauri nini?!"
aliuliza mdada yule huku akiwa na khof kuu.ujasiri ukimtenga...
"teh! teh teh ndo maana nkasema binadamu wagumu kuelewa ok unakumbuka ukiwa ktk hotel ya sheraton motel tena siku hiyo kulikuwa na uzinduzi wa filam ya upendo ya mr z film production mkiwa ktk viti vya peke yenu...
mawazo ya binti yule yakasafiri mpaka siku hiyo miaka mitatu nyuma.

MIAKA MITATU NYUMA

SHERATON HOTEL
"Hivi beby? utanioa kwel au utanchezea na kuniacha?"
binti yule alimuuliza mpz wake walokaa pamoja katika usiku huo
usiku wa matumaini
"hakika ukimaliza chuo,ntakuoa mke wangu!"
aliongea Martin huku akimkanyaga binti yule mguuni na kumfanya binti yule amtazame kwa matamanio.
"usije ukanchezea na kuniacha ndo mlivyo ny..in..yi..."
aliongea yule binti huku akizidi kubadilika na kumuitaji zaidi Martin
"no! beby siwez fanya hivyo kwako coz i love u"
sasa alipitisha mkono wake chini ya meza na kuyapapasa mapaja ya binti yule alokiri kuzidiwa na hisia
"mpz twende tukapumzike! me nimechoka!"
wakiwa wamezidiwa na kilevi wakajinyanyua na kuelekea mapokezi!
"nyie malaya nipeni funguo naitaji kupumzika!"
alishazoea kuwatukana wafanyakaz wake pindi akilewa dada wa mapokezi haraka haraka alimpelekea ufunguo na kumkabidhi
"Alaf bosi mkurugenzi jb! kashachukua mauzo ya wiki nzima hii..."
"amna shida!"
akajibu Martin huku akiwa kamshika kiuno mwanamke yule mpaka chumbani akamdondoshea kitandani...
na kuanza kumpiga mabusu mwili mzima.Binti yule akawa akigugumia kwa raha
"Leo tunalala wote amna kurudi chuo mpaka keshooo"
"Ni wewe tu mpz kila kitu katika mwili wangu ni Mali yako"
"Mwaaaaaaaaa,mwaaaa...."
"Beby nkuulize kitu?!"
"Yas beby niulize"
"Hivi hizi Mali mko share?!"
"Amna kampuni ya madini ni ya kwangu hila hivi vioteli ndo nimeweka share na marafiki zangu"
"Beby naweza nkakushauri Mali zote zikawa chini yako plz nambie ukweli zote ni Mali zako au mko share?!"
Martin akashtuka!!!
Akamkazia macho binti yule
Binti si kwamba alikuwa kalewa alimaanisha alichokisema
"Inawezekana kweli Merry?!"
"Mimi nipo chuo mwaka wa Tatu ni mwana sheria Mali zilizo ziko share zinaweza kuwa za mmoja kukiwa na sababu mbili Tatu zinazoweza pia kutengenezwa"
"Mfano!?..."
Martin akaoji
"Mmoja wa mmiliki wa Mali hizo akipoteza maisha bila kuacha hati ya urithi mali zile ugawanywa nusu kulipa madeni inayobakia upewa ndugu zake"
Mada ile sasa ilianza kumfuraisha Martin
"Na ikiwa hana ndugu?!"
"Ubaki kwa mmiliki aliyebakia ndo maana nikakuoji je mko ushirika?!"
"Ndiyo mpz"
Akaitikia Martin huku akiona aibu
"Good mpz naitaji ukinioa Mali zote ziwe chini yetu"
"Sasa tufanyeje mpz na Jb yupo hai"
"Jb ni nani?!"
"Ndo ambaye tupo naye share"
"Ntakwambia kesho tukiamka mpz now ni usiku wako nifaidi mpz..."
Martin hakuwa na la kuongea akamvamia mwenzake na kumpa alichostaili...
Wakawa katika mchezo huo kwa masaa kadhaa mpaka walipopitiwa na usingizi

*************************************

Mwanzo alihisi kama mikono laini ikimpapasa katika kifua chake.
Ghafla ulimi ukaanza kutambaa katika maskio yake
Martin wa ukwee akasimama!
Kama antena,akiwa imara
Misuli ilimkaza
Binti yule akacheka na kuupeleka mkono wake kumshika Martin mwanaume halis na kumpapasa
Aliyefanyiwa hivyo akafumbua macho
"Weeee mtoto mbona mtundu hivyo?!"
Martin akalalamika
"No beby jana nlilewa sikumfaidi huyu vizuri asubuhi hii ni maalum kwa ajili yake"
"OK beby"
Aliitika Martin akamdondosha binti yule chini Naye kuwa juu yake
Akaupeleka mdomo wake kwenye mdomo wa binti yule wakagandanaa
Wakibadilishana mate
"Mpz unakumbuka Jana nlikwambiaje?!"
Kwa sauti nyembamba,ilotokea puani binti yule akaoji
"Yah mpz usiku nimewaza sana juu ya hilo"
"Unajua kwa nini nlikwambia tutaongea asubuh?!"
"Kwa kuwa ntakuwa sijalewa"
"Swadaktaaaa!,Jana ulilewa sana mpz nikajua asubuh usingekumbuka nlichokwambia kumbe upo imara"
"Wew ndo ulilewa nkajua ulipngea vile kutokana na ulevi kumbe ulimaanisha mpz nambie sasa"
"Kwel mpz wazihitaji hizo Mali ziwe chini yako?!"
"Ndiyo mpz"
"Lazima huyo mwenzako afe!"
"Whaaat!"
Martin alioji kwa mshangao
"Ndiyo lazima afe,na cha kufanya ongea na mwanasheria wa kampuni yenu abadilishe nyaraka zote"
"Itawezekana kweli?! Si ntafungwa Mimi?!,uwezi fungwa baba angu kamishna ntaongea naye"
"Sawa mpz ila mmh yataka moyo"
"Nkuulize kitu mpz"
"Niulize..."
"Mwanasheria wenu mwamlipa sh ngapi kwa mwezi?!"
"Million 2 na nusu!"
"MPE milioni 15 akufanyie hiyo kazi na mwahidi kama ikifanikiwa utakuwa unamlipa million tano hawezi kataa pili huyo jamaa kaoa na ndugu zake wako wangapi?!"
"Ajaoa na hana ndugu hata mmoja hila anaishi na mwanamke"
"Common mbona simple hivyo muonge nyumba huyo demu atakubali kukupa hati za nyumba"
"Sawa ntajaribu"
"Mpz si kujaribu ni kufanya kwani mistake moja itahatarisha maisha yako kwanza una vijana wa kazi?!"
"Vijana wa kazi?! Wapi hao?!"
"Haaa! Unaniangusha namaanisha wazee wa kazi majambarika"
"Hapana sina"
"OK ntakupa namba vijana hawa wanaitwa 4 killers ni vijana wa baba walipitia jeshi ndiyo watakao muondosha duniani huyo...! Nan tena jina lake?!"
"Jacob au jb"
Dada yule alikumbuka!!!
Akamtumbulia macho kichaa yule aliye kuwa akimwangalia kwa dharau jitu akaachia cheko
"Jb ndo Mimi wewe si ndo ulimshauri mumeo martin anigeuke?!"
"Nsamehee"
"Siwezi kukusamehe 4 killars nishawaondoa,mw
anamke wangu mlomuhadaa kwa kijumba na kigari naye nisha mtanguliza,mwanasheria wangu naye ndo nlimuua wa kwanza sasa zamu yako!!!..."
"Nsamehe jb"
"Mumeo na babako watakufata muda si mrefu"
Ghafla jb akatoweka
Dada yule akiwa kachanganyikiwa akajinyanyua na kukimbia
Ghafla mlango ukajifunga
Tobaaaa!!!
Kicheko kikasikika nyuma yake
Ikamlazimu ageuke
LA haulaaa!!!
Jitu LA kutisha lilikuwa nyuma yake
Ni kama lilivyofufuka makaburini
Lilivaa sanda!,sanda ilooza,sanda ilotembelewa na mafinyofinyo!!!
"Haaaaa haaaaa haaa"
Likaachia cheko,meno yalooza yakaonekana
Mkononi alishika bisu
Akawa anamsogelea yule Dada
"Mamaaaaaaa" Dada yule akaachia kilio
"Grooooooh"
Jitu likaachia mlio kama wa simba
Je nini kitaendelea
Binti huyu atakufa?!

ITAENDELEA...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom