Simulizi: Mimi na Boss Wangu

Simulizi: Mimi na Boss Wangu

SEHEMU INAYOFUATA..........

Jambo ambalo lilikwamisha mpango wa Mimi na ESTA kuhusu biashara ya saloon,ni baada ya madam kusafiri kwa muda wa wiki nzima huku akiniahidi akirudi mipango itakuwa kama kawaida.

Matukio ya kununiana bila sababu ndani ya nyumba, mashtaka mbalimbali yalijitokeza ila ilikuwa ni kama kawaida tu kwakuwa wanawake ndivyo walivyo,

Kuna siku nikiwa ofisini nilipokea taarifa ya watu kuumizana Kati ya Dada yangu wa tumbo moja na ESTA , wakipigana kwa sababu zisizoelezeka huku mke wangu akiwa upande wa ndugu yangu.

Nilifikiria kuhusu ESTA, nikagundua wamepanga kumuhamisha kwa nguvu, lakini madam si atarudi siku si nyingi? nilijiuliza

Nikarudi nyumbani,nakumbuka dada yangu na mke wangu walichachamaa huku wote wakidai,Bora wote
Wote tuondoke mkoani ili wewe ukae na ESTA

Mtu gani Kila tukimwambia hatumtaki anang'ang'ania tu , mtoe nakwambia muondoe huyo malaya wako, alizungumza mke wangu,
Huku nikimtazama nikikumbuka urafiki wao wa siku ya kwanza namna walivyokuwa wanakaribishana.

Wakati hayo yakiendelea ESTA alikuwa kashika mkoba mdogo wa kike mkononi huku akiwa na begi dogo la mgongoni,

Leta begi hilo, la kwako ? Yaani mchana kweupe unaniibia,
Ni maneno toka kwa dada yangu wa tumbo moja ambaye alishindwa kuwa na hekima ni kwasababu tu yalifanana, ESTA akarudisha like begi ndani akachukua la kwake,

Muda huu anaenda wapi huyu ,lazima nisimame kama mwanaume huku nikihakikisha , Kila mmoja namdhibiti , sikuwa na maneno na dada yangu, jicho nililomwangalia lilitosha kumfanya akimbilie chumbani kwake , huku nikitoa ukali na msimamo wenye kutaka Kila mmoja aingie ndani si ESTA Wala na nani , niliingia chumbani huku mke wangu akiwa Hana hata neno la kuniambia ikabidi atoke aingie kwenye chumba Chake anacholala na mtoto kwa kipindi hicho.

Nakumbuka nililala bila kula, saa kumi alfajiri niliamka nikajiandaa fresh, Kisha nikawaamsha wote,
Nikasema yafuatayo,

Hii nyumba kiongozi ni nani? Niliuliza

Wote wakajibu ni wewe.

Sasa kuanzia Leo naomba ESTA tafuta pa kwenda sitaki migogoro na malumbano yasiyo ya lazima ndani kwangu, lakini pia wewe mke wangu na dada yangu naomba mniandalie majibu mazuri ni kwanini mmekosa heshima na adabu kwa Sasa, au kwakuwa mama kaondoka ?

Nawapa kutwa nzima Kila mmoja awe na majibu, niliongea huku nikionesha sura ambayo hakuna aliyenijibu,

Sasa shemeji namimi nikupe jibu gani maana Mimi sijui chochote, aliongeza dada wa kazi akijitetea

Wewe haupo naongea na Hawa, nikainuka kuwahi kazini kwangu, kama kawaida shughuli ziliendelea huku uzoefu ukiongezeka, kiasi Cha baadhi ya wafanyakazi kuwa wanajiuliza vitu vingi kwangu ilinipa heshima kubwa kwenye kampuni.

Kama kawaida Kuna mdada ana kiherehere sana pale ofisini, aliingia huku akiwa na taarifa mpya, ambayo kwangu ilinistua,

Mr Daniel, Kuna tetesi nazisikia kuwa yule mke mdogo wa boss atakuja kampuni hii, na hapa tunapoongea yupo South Africa kwa mumewe . Ambako yametokea mabadiliko kwamba mtoto wa boss hatahusika Tena hapa Bali atashughulikia habari zake za ufuatiliaji wa mizigo toka nchi za nje na kuiingiza humu,

Ni kazi ambayo alikuwa nayo zamani kabla hajapandishwa cheo, Sasa sijui yule mwanamke akija hapa itakuwaje maana ni ana majungu sijapata kuona Tena ni mchawi sana yule yaani huwa simpendi basi tu.
Japokuwa haijawekwa wazi kuwa hapa atakuwa nani,
Alimalizia yule dada.

Haina shida Mimi naona Mimi na wewe haituhusu kwasababu atakuja kukaa kwenye nafasi yake na sisi tutampa heshima anayostahili,
Nilijibu kwa kujikaza.

Niliwaza sana kama yule atakuja pale ofisini kwetu maana kiukweli ni mtu mzuri mkiwasiliana mkiwa mbalimbali lakini hayuko poa mkiwa sehemu moja.

Anyway hayanihusu haya nitaongeza tu umakini.

Kuja kushtuka kumbe simu kutoka kwa ESTA iliita sana , ikabidi nimpigie ESTA mtu ambaye hajui kususa maana Mimi nilidhanj pengine hatonitafuta Tena huyu mwanamama.

Samahani shemu Mimi nipo sehemu tu kwa mjumbe wa mtaa huu hapa kwako, lengo la kukupigia simu ni kuulizia ule mpango vipi, maana hata eneo na frem nimeshapata siku nyingi sana kwahiyo nakusikiliza.
Alimalizia.

Subiri nitakuja hapohapo ulipo baadae usitoke.
Nikakata simu,

Nikakumbuka ninavyotoka asubuhi nyumbani nilichimba mkwara ambao lengo nikuwatuliza tu wale ili wasinipande kichwani, nikampigia simu mke wangu ambaye alikuwa mpole sana mithili ya kuniogopa, ila nikamtuliza tu.

Nikapanga lazima niende kwa ESTA kwasababu ya ule mpango wangu, isingekuwa huu mpango pengine ningemuacha apambane na hali yake.Japokuwa huu mpango ni kama hauna uhakika sana kwasababu nilizokuwa naziona ila bado nilikuwa na IMANI, nilitoka kazini nikitembea maeneo ya city centre huku nikiangalia maduka mazuri yanayouzwa nguo za kike,

Nikanunua nguo fulani za mke wangu( jina kapuni)
Bangili na urembo urembo nikaweka kwenye pocket huyooo kutafuta daladala zinazoelekea nje ya jiji.

Nikashuka kwenye daladala huku nikielekea kwa mama mmoja mjane ambaye ndiye mjumbe wetu aliyempokea ESTA.
Nilifika tukasalimiana maongezi yakawaanza

Kwanza baba nikushukuru kwa ukarimu wako wa kumpokea huyu ukakaa naye sikuzote hizo, japo ulifanya kosa kutokuziona mamlaka ili wajue kuwa unahifadhi mgeni,
Huyu ni binadamu angekufa ungefanyaje,?

Nikakiri kosa hasa ukizingatia hata mama yangu mzazi alishasema kipindi fulani nikapuuzia.

Akaendelea yule mjumbe..

Sasa naweza kuwaacha mkaongea wenyewe maana kaniambia wewe ndiye anakutegemea kwa vitu vingi kwa sasa.

Akatupisha,

Nilizungumza mengi na ESTA alishauri angepanga chumba, nilifikiria kidogo nikaona ni wazo zuri Bora apange, lengo awe kwenye himaya yangu mpaka nitakapopiga hela kwa madam, nikashauri atafute chumba kesho yake.
Huku nikimuita yule mama mjumbe.

Kwanza mama Mimi nikushukuru kwa kumpokea huyu ndugu yangu ni kwamba si Mimi niliyemfukuza Bali kalazimika kutoka, nilijitetea

Wewe mwananguu (akiongea kwa sauti ya chini ESTA asisikie)
Mwanamke mzuri Kama huyu unampotezaje? Yaani ningekuwa na mtoto wa kiume ningemwambia amuoe kabisa mtoto kaumbika mtoto mashallah, hebu mpangie chumba basi na wewe hutaki kuwa na wanawake wawili?

Maana kutwa nzima nilimuhoji ananiambia hujawahi hata kutembea naye mwanangu,? Acha uzembe bwanaaa, unaniangusha.aliongea bila breki yule mama mjumbe mswahili kupitiliza mwenye kabila fulani maarufu mwambao wa bahari ya hindi

Sikumjibu neno zaidi ya kucheka tu, nikiwaza jinsi watu tulivyokuwa nyuma kwenye mambo mengi,

Kweli Elimu ni muhimu, yaani kusoma si lazima upate kazi kwanza unaongeza ufahamu, hebu fikiria mtu anafahamiana na mwanamke kwa Mara ya kwanza tayari anawaza angekuwa na mtoto wa kiume amuoe. Hawazi kuhusu magonjwa ya zinaa na ukimwi. Yaani waswahili tunarahisisha sana mambo.

Na ndiko magonjwa mengi ya ngono yaliko,niliwaza sana.

Sasa baba yanguuu nisikufiche niwe mkweli Sina kitu humu ñdani, unaniachaje?

Aliongea yule mama ambaye huenda kwenye ujana wake alikuwa shangingi na sijui, ujumbe aliupataje
Ikabidi nimpe Msimbazi mmoja.
Huku nikiwaza kweli wanaume tumeumbwa mateso,

Yaani muda wote lazima uwe na hela japo do lazima kutoa, lakini Kuna ile kujiepusha na lawama ndogo ndogo.
Tukaagana huku nikisisitiza ESTA atafute chumba. Najua ule mpango wa Mimi na madam Sina uhakika ila ESTA simwachi lazima nibeti hebu fikiria unaipata milioni tano kwa pamoja bila kutumia nguvu nyingi.
Weeee ESTA ninaye , nilijisemea

Nikafika nyumbani kila huku Kila akiwa mtu mnyonge mnyonge, nikamuita mke wangu nikambembeleza plus uongo mwingi huyoo kalainika, niwanawake tu Hawa wametoka kwenye mbavu zetu. Kama huwezi kubembeleza mwanamke basi utapata tabu sana kwenye ndoa yako, watu wengi wameshindwa kukaa na wake au wapenzi kwa kujitia misimamo ambayo baadaye iligeuka Majuto.

Lazima muda mwingine umpe ushindi hata asiostahili kwa ustawi wa penzi au NDOA.
Tuliendelea kutaniana na mke wangu Huku nikiwa namsoma vitu Fulani Mara tukaitwa na dada wa kazi, natoka nje nakutana na mke wa Shedy akiwa kama kakasirika hivi,.

MADAM nasikia tetesi kuwa huenda tukawa sehemu moja, Haina shida je mpango wangu kwa ESTA utafanikiwa? Na ESTA simuachi

Mke wa Shedy anatafuta Nini huyu maan anajua wazi Hawa hatuna uhusiano nao mzuri.

Sehemu ijayo Ina majibu.usichoke

Inaendeleaa.......
Hakuna kuchoka humu
 
na kulia Kisha wakanyamaza huku wakikumbatiana Mara kadhaa hasa madam na ESTA, hata baada ya dereva wa madam kusogea pale alikataliwa akiambiwa Kuna amani tu, akaja kwangu huku akijichekesha chekesha , akitaka kujua kwani Nini kimetokea pale lakini nilimwambia Mimi mwenyewe sijui,

Hata baadhi ya wateja na wafanyakazi wa mgahawa ule walianza kutawanyika huku walikosa majibu, huku kila mmoja aliniangalia Mimi pengine walitamani kuniuliza lakini nilikuwa bize na simu yangu.

Wote wanne walipiga stori pale Kisha wakaniita,

Ahsante sana tolu, lakini pole kwa baadhi ya mitihani iliyokukuta yote kwa yote tumshukuru MUNGU kwa kulimaliza hili jambo salama , dada yangu (akimaanisha mke wangu) hongera sana umepata mume. Nawaombea muishi maisha marefu ikiwezekana mzeeke pamoja. Aliongea madam na kufanya watu wacheke.

Hata Mimi nashukuru hata hivyo najiona nimefunguliwa nimekuwa huru ,nakushukuru sana shemeji yangu. Alisema ESTA.

Sasa tolu hapa hakuna la ziada nadhani ni muda wa kwenda mkapeane hizo hela maana kilichokuwa kinakwamisha kimeshapatiwa ufumbuzi, aliongea madam.

Hapana madam si wapi Wala wapi hizi hela zilishakuwa mzigo kwangu hivyo nilikuja nazo kama kupewa apewe tu mzigo wake, nilishauri.

Sawa, ni kheri zaidi japo muende kule nilikopark gari ndiko kwenye usalama zaidi naomba niletewe PC(personal computer) maana Nina kazi ya kufanya humo, aliongea Madam akimuelekeza dereva atupeleke kwenye gari.

Ndani ya gari, tukiwa watu wanne Mimi, mke wangu, ESTA na yule mama yake wa hiari, nikatoa zile PESA na kumkabidhi ESTA, ambaye alikuwa anatabasamu huku akishindwa Cha kufanya akawa kaziweka hela mapajani mwake.

Sasa shemu, umefanya kazi kubwa sana nadhani hizi hela tunastahili kugawana , alivunja ukimya ESTA.

Hapana shemu we kwanza hesabu mzigo umetimia? Mengine yatafuata, akabaki kaduwaa tu huku akiziangalia mke wangu na mama mchungaji wakaanza kuzihesabu kwa zamu zile pesa nyingi kwao, maana walitumia muda mwingi .

Ni sawa zipo milioni kumi taslimu,walisema kwa pamoja mke wangu na mama mchungaji.

Sawa,Hilo halina shida nilijua shem hawezi kuleta ubabaishaji na ningekuwa Mimi pekee yangu hata nisinge hesabu, je shem tunagawanaje?alizungumza ESTA.

Shemu Mimi nipo na wewe siku nyingi tangu nilivyotambulishwa na mke wangu huyu, hata hivyo ulieleza masahibu yako, pamoja na kumuweka wazi huyo mtu aliyekufanyia ubaya, lakini jinsi MUNGU alivyo mwema hata yeye alikiri makosa yake, kama mlivyoona mwenyewe akiongea muda mfupi ulopita (wote wakatikisa vichwa kukubaliana na Mimi)

Kwahiyo kwanza shida siyo pesa, hatujapatana hapa kwa lengo la kutaka PESA, hata yeye hajatoa pesa kwa lengo la kusamehewa hapana, maana itaonekana kama kanunua msamaha.

Mmesameheana ili kuipa amani mioyo yenu, ukimkosea mtu una kuwa na deni nafsini mwako ambalo linaweza kukutesa kisaikolojia hasa kama hujazoea kumkwaza mtu
Lakini pia kwa aliyefanyiwa kosa anapaswa kusamehe ili kuondoa deni, laana na mikosi ambayo siyo ya lazima, hivyo ukisamehe kwa moyo wa dhati kabisa unakuwa huru kiroho na kimwili.

Kuhusu vijizawadi vya pesa kama hivi unaweza sema havina ulazima, lakini ni kwamba, kwanza aliyetoa hii takrima kwa hiari yake, kaamua kuomba msamaha wa dhati.

Lakini pili atakayepokea ambaye kwa Sasa ni wewe shem tunaamini umesamehe kidhati. Hivyo hizo pesa ni zako shemu. Nilikataa

Umeongea mengi sana baba, lakini kwa mtazamo wangu naona Bora ungepokea hata kiasi kidogo, maana masumbuko uliyopata Mara utake kupelekwa kituo Cha polisi, na mengine mengi hivyo Mimi kwa mtazamo wangu naona unasitahili kuwa sehemu ya huu mgao. Aliongea mama mchungaji.

Lakini nilikataa katakata .

Halafu mume wangu sijui upoje, hujaomba, Bali watu ambao umewasaidia wanakwambia wakupe hela bado unakataa?

Siyo bure jamani khaaah, ukute eti unaona aibu, utakuja kufa masikini wewe.

Aliongea kwa jazba mke wangu akihoji kwanini nakataa hela, alikuwa sahihi kwa sababu hajui mapatano yetu na MADAM aliyenituma hii kazi ambayo nishaifanikisha tayari

Licha ya wale wanawake kumshawishi mke wangu kuwa kama Mimi nimegoma basi achukue yeye bado nilikataa.

Nilikataa kwasababu muda si mrefu mke wangu nitamuonesha kiasi kama kile tukiwa nyumbani sikutaka ajue tukiwa pale, pia kama madam akisikia Kuna chochote kitu nilichukua kwa ESTA ataniona Sina maana, kubwa zaidi madam aliniahidi makubwa kama nitafanikisha zoezi lile, Sasa haraka ya Nini?

ESTA akazisunda hela zote kwenye mkoba wake wa kike, Kisha wote tukatoka kuelekea alipo madam.

Watu walikumbatiana huku wakibadilishana namba za simu, mtu pekee aliyekuwa kakosa amani ni mke wangu, maana muda wote alikuwa ananiangalia jicho baya akiniona kama mzembe Fulani hivi.

Madam aliniita tuongee pembeni tukiwa wawilibtu

Sasa tulo Mimi naona wewe tutaongea zaidi maana Leo nimekuja tu kwakuwa ulinilazimisha ukihofia usalama wako,.

Ujue madam Kuna siku ungesikia nipo ndani maana tayari nilishaonekana kama Nina njama za kutaka kumuua,

Kisa nini umuue, aliuliza madam.

Ni kwasababu nilimpa hela nyingi kiasi Cha kumtisha huyo dada yako sijui mdogo wako,

Achana naye mshamba tu huyo angekuwa mtu mwingine si angekula zile hela, Tena nikwambie tolu huu mpango wa kutaka kupatanishwa na ESTA nilianza siku nyingi tu, nilimtuma mtu nikampa pesa amshawishi huyu ESTA ili tupatane lakini Cha ajabu yule yule mtu aliishia kumtongoza tu ESTA akatembea naye, na Akala hela zangu.
Alisema madam kwa masikitiko .

Nikawaza kumbe Kuna majamaa hawana woga na kitu Cha mtu.
Tuliagana huku madam akiondoka na ESTA na yule mama yake, na Mimi na mke wangu tukatafuta kituo Cha Dala dala. Wakati tukatembea taratibu huku mke wangu akionesha kutokuwa namimi hata kistori tu.

Dah hii adha ya daladala hii, ya ipo siku tu lazima tununue gari yetu mke wangu maana hebu ona watu wanavyogombania mlangoni, Sasa wewe unawezaje Ukiwa na mtoto mdogo, Bora tuite Taxi tu.

Nani wa kununua gari, wewe mume wangu Huyu huyu, ambaye unafanya kazi kuuubwa isiyokuwa na malipo, mbaya zaidi wanakubembeleza chukua basi hata kidogo hutaki wakataka kunipa Mimi umekataa,

Yaani unajifanya mtume mwaminifu kwamba unapatanisha watu bure bila malipo, kwanza ngoja tufike nyumbani utanieleza vizuri we ni mtu wa aina gani ambaye unafanya mambo makubwa bila kunishirikisha na hadi Sasa nashindwa kuelewa uliwezaje kujitesa mwanaume mzima kujaa unafiki wa kupatanisha watu bila maslahi,

Sasa pale hata kama ungesema wakupe milioni moja , kwa kazi uliyofanya nani angeguna unafikiri Cha ajabu eti hutaki hela, pole sana mume wangu nadhani kwako Kuna kitu hakipo sawa,. Aliweka kituo baada ya dereva taxi kuwa amefika tukaingia ndani.

Malalamiko ya mke wangu niliyavumilia baada ya kukuta ni mropokaji asiyekuwa na subira hata hivyo siyo kosa lake maana sikumwelewesha mapema lakini nitamfanyia surprise tukifika nyumbani.

Tulifika nyumbani huku mke wangu akiwa bado kakasirika sana, akawa mkali mkali fulani, Kabla sijamuonesha ule mpango mzima nilipokea simu toka kwa meneja wa kazini kwangu,

Huyu naye anataka Nini kwenye hii wikiendi , nikaweka simu sikioni.

Daniel, nimekuona na mke wa boss mida fulani hapo vipi man kikao gani?
Aliuliza bila hata salamu.

Sasa meneja pale ni mgahawani, Mimi nilienda kivyangu na yeye alikuwa kivyake Sasa kwakuwa ananifahamu ikabidi tujumuike kwenye meza moja vipi Kuna tatizo?

Tatizo lipo, Tena unatafuta kufukuzwa kazi. Akakata simu

Itaendelea..............
 
na kulia Kisha wakanyamaza huku wakikumbatiana Mara kadhaa hasa madam na ESTA, hata baada ya dereva wa madam kusogea pale alikataliwa akiambiwa Kuna amani tu, akaja kwangu huku akijichekesha chekesha , akitaka kujua kwani Nini kimetokea pale lakini nilimwambia Mimi mwenyewe sijui,

Hata baadhi ya wateja na wafanyakazi wa mgahawa ule walianza kutawanyika huku walikosa majibu, huku kila mmoja aliniangalia Mimi pengine walitamani kuniuliza lakini nilikuwa bize na simu yangu.

Wote wanne walipiga stori pale Kisha wakaniita,

Ahsante sana tolu, lakini pole kwa baadhi ya mitihani iliyokukuta yote kwa yote tumshukuru MUNGU kwa kulimaliza hili jambo salama , dada yangu (akimaanisha mke wangu) hongera sana umepata mume. Nawaombea muishi maisha marefu ikiwezekana mzeeke pamoja. Aliongea madam na kufanya watu wacheke.

Hata Mimi nashukuru hata hivyo najiona nimefunguliwa nimekuwa huru ,nakushukuru sana shemeji yangu. Alisema ESTA.

Sasa tolu hapa hakuna la ziada nadhani ni muda wa kwenda mkapeane hizo hela maana kilichokuwa kinakwamisha kimeshapatiwa ufumbuzi, aliongea madam.

Hapana madam si wapi Wala wapi hizi hela zilishakuwa mzigo kwangu hivyo nilikuja nazo kama kupewa apewe tu mzigo wake, nilishauri.

Sawa, ni kheri zaidi japo muende kule nilikopark gari ndiko kwenye usalama zaidi naomba niletewe PC(personal computer) maana Nina kazi ya kufanya humo, aliongea Madam akimuelekeza dereva atupeleke kwenye gari.

Ndani ya gari, tukiwa watu wanne Mimi, mke wangu, ESTA na yule mama yake wa hiari, nikatoa zile PESA na kumkabidhi ESTA, ambaye alikuwa anatabasamu huku akishindwa Cha kufanya akawa kaziweka hela mapajani mwake.

Sasa shemu, umefanya kazi kubwa sana nadhani hizi hela tunastahili kugawana , alivunja ukimya ESTA.

Hapana shemu we kwanza hesabu mzigo umetimia? Mengine yatafuata, akabaki kaduwaa tu huku akiziangalia mke wangu na mama mchungaji wakaanza kuzihesabu kwa zamu zile pesa nyingi kwao, maana walitumia muda mwingi .

Ni sawa zipo milioni kumi taslimu,walisema kwa pamoja mke wangu na mama mchungaji.

Sawa,Hilo halina shida nilijua shem hawezi kuleta ubabaishaji na ningekuwa Mimi pekee yangu hata nisinge hesabu, je shem tunagawanaje?alizungumza ESTA.

Shemu Mimi nipo na wewe siku nyingi tangu nilivyotambulishwa na mke wangu huyu, hata hivyo ulieleza masahibu yako, pamoja na kumuweka wazi huyo mtu aliyekufanyia ubaya, lakini jinsi MUNGU alivyo mwema hata yeye alikiri makosa yake, kama mlivyoona mwenyewe akiongea muda mfupi ulopita (wote wakatikisa vichwa kukubaliana na Mimi)

Kwahiyo kwanza shida siyo pesa, hatujapatana hapa kwa lengo la kutaka PESA, hata yeye hajatoa pesa kwa lengo la kusamehewa hapana, maana itaonekana kama kanunua msamaha.

Mmesameheana ili kuipa amani mioyo yenu, ukimkosea mtu una kuwa na deni nafsini mwako ambalo linaweza kukutesa kisaikolojia hasa kama hujazoea kumkwaza mtu
Lakini pia kwa aliyefanyiwa kosa anapaswa kusamehe ili kuondoa deni, laana na mikosi ambayo siyo ya lazima, hivyo ukisamehe kwa moyo wa dhati kabisa unakuwa huru kiroho na kimwili.

Kuhusu vijizawadi vya pesa kama hivi unaweza sema havina ulazima, lakini ni kwamba, kwanza aliyetoa hii takrima kwa hiari yake, kaamua kuomba msamaha wa dhati.

Lakini pili atakayepokea ambaye kwa Sasa ni wewe shem tunaamini umesamehe kidhati. Hivyo hizo pesa ni zako shemu. Nilikataa

Umeongea mengi sana baba, lakini kwa mtazamo wangu naona Bora ungepokea hata kiasi kidogo, maana masumbuko uliyopata Mara utake kupelekwa kituo Cha polisi, na mengine mengi hivyo Mimi kwa mtazamo wangu naona unasitahili kuwa sehemu ya huu mgao. Aliongea mama mchungaji.

Lakini nilikataa katakata .

Halafu mume wangu sijui upoje, hujaomba, Bali watu ambao umewasaidia wanakwambia wakupe hela bado unakataa?

Siyo bure jamani khaaah, ukute eti unaona aibu, utakuja kufa masikini wewe.

Aliongea kwa jazba mke wangu akihoji kwanini nakataa hela, alikuwa sahihi kwa sababu hajui mapatano yetu na MADAM aliyenituma hii kazi ambayo nishaifanikisha tayari

Licha ya wale wanawake kumshawishi mke wangu kuwa kama Mimi nimegoma basi achukue yeye bado nilikataa.

Nilikataa kwasababu muda si mrefu mke wangu nitamuonesha kiasi kama kile tukiwa nyumbani sikutaka ajue tukiwa pale, pia kama madam akisikia Kuna chochote kitu nilichukua kwa ESTA ataniona Sina maana, kubwa zaidi madam aliniahidi makubwa kama nitafanikisha zoezi lile, Sasa haraka ya Nini?

ESTA akazisunda hela zote kwenye mkoba wake wa kike, Kisha wote tukatoka kuelekea alipo madam.

Watu walikumbatiana huku wakibadilishana namba za simu, mtu pekee aliyekuwa kakosa amani ni mke wangu, maana muda wote alikuwa ananiangalia jicho baya akiniona kama mzembe Fulani hivi.

Madam aliniita tuongee pembeni tukiwa wawilibtu

Sasa tulo Mimi naona wewe tutaongea zaidi maana Leo nimekuja tu kwakuwa ulinilazimisha ukihofia usalama wako,.

Ujue madam Kuna siku ungesikia nipo ndani maana tayari nilishaonekana kama Nina njama za kutaka kumuua,

Kisa nini umuue, aliuliza madam.

Ni kwasababu nilimpa hela nyingi kiasi Cha kumtisha huyo dada yako sijui mdogo wako,

Achana naye mshamba tu huyo angekuwa mtu mwingine si angekula zile hela, Tena nikwambie tolu huu mpango wa kutaka kupatanishwa na ESTA nilianza siku nyingi tu, nilimtuma mtu nikampa pesa amshawishi huyu ESTA ili tupatane lakini Cha ajabu yule yule mtu aliishia kumtongoza tu ESTA akatembea naye, na Akala hela zangu.
Alisema madam kwa masikitiko .

Nikawaza kumbe Kuna majamaa hawana woga na kitu Cha mtu.
Tuliagana huku madam akiondoka na ESTA na yule mama yake, na Mimi na mke wangu tukatafuta kituo Cha Dala dala. Wakati tukatembea taratibu huku mke wangu akionesha kutokuwa namimi hata kistori tu.

Dah hii adha ya daladala hii, ya ipo siku tu lazima tununue gari yetu mke wangu maana hebu ona watu wanavyogombania mlangoni, Sasa wewe unawezaje Ukiwa na mtoto mdogo, Bora tuite Taxi tu.

Nani wa kununua gari, wewe mume wangu Huyu huyu, ambaye unafanya kazi kuuubwa isiyokuwa na malipo, mbaya zaidi wanakubembeleza chukua basi hata kidogo hutaki wakataka kunipa Mimi umekataa,

Yaani unajifanya mtume mwaminifu kwamba unapatanisha watu bure bila malipo, kwanza ngoja tufike nyumbani utanieleza vizuri we ni mtu wa aina gani ambaye unafanya mambo makubwa bila kunishirikisha na hadi Sasa nashindwa kuelewa uliwezaje kujitesa mwanaume mzima kujaa unafiki wa kupatanisha watu bila maslahi,

Sasa pale hata kama ungesema wakupe milioni moja , kwa kazi uliyofanya nani angeguna unafikiri Cha ajabu eti hutaki hela, pole sana mume wangu nadhani kwako Kuna kitu hakipo sawa,. Aliweka kituo baada ya dereva taxi kuwa amefika tukaingia ndani.

Malalamiko ya mke wangu niliyavumilia baada ya kukuta ni mropokaji asiyekuwa na subira hata hivyo siyo kosa lake maana sikumwelewesha mapema lakini nitamfanyia surprise tukifika nyumbani.

Tulifika nyumbani huku mke wangu akiwa bado kakasirika sana, akawa mkali mkali fulani, Kabla sijamuonesha ule mpango mzima nilipokea simu toka kwa meneja wa kazini kwangu,

Huyu naye anataka Nini kwenye hii wikiendi , nikaweka simu sikioni.

Daniel, nimekuona na mke wa boss mida fulani hapo vipi man kikao gani?
Aliuliza bila hata salamu.

Sasa meneja pale ni mgahawani, Mimi nilienda kivyangu na yeye alikuwa kivyake Sasa kwakuwa ananifahamu ikabidi tujumuike kwenye meza moja vipi Kuna tatizo?

Tatizo lipo, Tena unatafuta kufukuzwa kazi. Akakata simu

Itaendelea..............
Patamu kma Asali
 
na kulia Kisha wakanyamaza huku wakikumbatiana Mara kadhaa hasa madam na ESTA, hata baada ya dereva wa madam kusogea pale alikataliwa akiambiwa Kuna amani tu, akaja kwangu huku akijichekesha chekesha , akitaka kujua kwani Nini kimetokea pale lakini nilimwambia Mimi mwenyewe sijui,

Hata baadhi ya wateja na wafanyakazi wa mgahawa ule walianza kutawanyika huku walikosa majibu, huku kila mmoja aliniangalia Mimi pengine walitamani kuniuliza lakini nilikuwa bize na simu yangu.

Wote wanne walipiga stori pale Kisha wakaniita,

Ahsante sana tolu, lakini pole kwa baadhi ya mitihani iliyokukuta yote kwa yote tumshukuru MUNGU kwa kulimaliza hili jambo salama , dada yangu (akimaanisha mke wangu) hongera sana umepata mume. Nawaombea muishi maisha marefu ikiwezekana mzeeke pamoja. Aliongea madam na kufanya watu wacheke.

Hata Mimi nashukuru hata hivyo najiona nimefunguliwa nimekuwa huru ,nakushukuru sana shemeji yangu. Alisema ESTA.

Sasa tolu hapa hakuna la ziada nadhani ni muda wa kwenda mkapeane hizo hela maana kilichokuwa kinakwamisha kimeshapatiwa ufumbuzi, aliongea madam.

Hapana madam si wapi Wala wapi hizi hela zilishakuwa mzigo kwangu hivyo nilikuja nazo kama kupewa apewe tu mzigo wake, nilishauri.

Sawa, ni kheri zaidi japo muende kule nilikopark gari ndiko kwenye usalama zaidi naomba niletewe PC(personal computer) maana Nina kazi ya kufanya humo, aliongea Madam akimuelekeza dereva atupeleke kwenye gari.

Ndani ya gari, tukiwa watu wanne Mimi, mke wangu, ESTA na yule mama yake wa hiari, nikatoa zile PESA na kumkabidhi ESTA, ambaye alikuwa anatabasamu huku akishindwa Cha kufanya akawa kaziweka hela mapajani mwake.

Sasa shemu, umefanya kazi kubwa sana nadhani hizi hela tunastahili kugawana , alivunja ukimya ESTA.

Hapana shemu we kwanza hesabu mzigo umetimia? Mengine yatafuata, akabaki kaduwaa tu huku akiziangalia mke wangu na mama mchungaji wakaanza kuzihesabu kwa zamu zile pesa nyingi kwao, maana walitumia muda mwingi .

Ni sawa zipo milioni kumi taslimu,walisema kwa pamoja mke wangu na mama mchungaji.

Sawa,Hilo halina shida nilijua shem hawezi kuleta ubabaishaji na ningekuwa Mimi pekee yangu hata nisinge hesabu, je shem tunagawanaje?alizungumza ESTA.

Shemu Mimi nipo na wewe siku nyingi tangu nilivyotambulishwa na mke wangu huyu, hata hivyo ulieleza masahibu yako, pamoja na kumuweka wazi huyo mtu aliyekufanyia ubaya, lakini jinsi MUNGU alivyo mwema hata yeye alikiri makosa yake, kama mlivyoona mwenyewe akiongea muda mfupi ulopita (wote wakatikisa vichwa kukubaliana na Mimi)

Kwahiyo kwanza shida siyo pesa, hatujapatana hapa kwa lengo la kutaka PESA, hata yeye hajatoa pesa kwa lengo la kusamehewa hapana, maana itaonekana kama kanunua msamaha.

Mmesameheana ili kuipa amani mioyo yenu, ukimkosea mtu una kuwa na deni nafsini mwako ambalo linaweza kukutesa kisaikolojia hasa kama hujazoea kumkwaza mtu
Lakini pia kwa aliyefanyiwa kosa anapaswa kusamehe ili kuondoa deni, laana na mikosi ambayo siyo ya lazima, hivyo ukisamehe kwa moyo wa dhati kabisa unakuwa huru kiroho na kimwili.

Kuhusu vijizawadi vya pesa kama hivi unaweza sema havina ulazima, lakini ni kwamba, kwanza aliyetoa hii takrima kwa hiari yake, kaamua kuomba msamaha wa dhati.

Lakini pili atakayepokea ambaye kwa Sasa ni wewe shem tunaamini umesamehe kidhati. Hivyo hizo pesa ni zako shemu. Nilikataa

Umeongea mengi sana baba, lakini kwa mtazamo wangu naona Bora ungepokea hata kiasi kidogo, maana masumbuko uliyopata Mara utake kupelekwa kituo Cha polisi, na mengine mengi hivyo Mimi kwa mtazamo wangu naona unasitahili kuwa sehemu ya huu mgao. Aliongea mama mchungaji.

Lakini nilikataa katakata .

Halafu mume wangu sijui upoje, hujaomba, Bali watu ambao umewasaidia wanakwambia wakupe hela bado unakataa?

Siyo bure jamani khaaah, ukute eti unaona aibu, utakuja kufa masikini wewe.

Aliongea kwa jazba mke wangu akihoji kwanini nakataa hela, alikuwa sahihi kwa sababu hajui mapatano yetu na MADAM aliyenituma hii kazi ambayo nishaifanikisha tayari

Licha ya wale wanawake kumshawishi mke wangu kuwa kama Mimi nimegoma basi achukue yeye bado nilikataa.

Nilikataa kwasababu muda si mrefu mke wangu nitamuonesha kiasi kama kile tukiwa nyumbani sikutaka ajue tukiwa pale, pia kama madam akisikia Kuna chochote kitu nilichukua kwa ESTA ataniona Sina maana, kubwa zaidi madam aliniahidi makubwa kama nitafanikisha zoezi lile, Sasa haraka ya Nini?

ESTA akazisunda hela zote kwenye mkoba wake wa kike, Kisha wote tukatoka kuelekea alipo madam.

Watu walikumbatiana huku wakibadilishana namba za simu, mtu pekee aliyekuwa kakosa amani ni mke wangu, maana muda wote alikuwa ananiangalia jicho baya akiniona kama mzembe Fulani hivi.

Madam aliniita tuongee pembeni tukiwa wawilibtu

Sasa tulo Mimi naona wewe tutaongea zaidi maana Leo nimekuja tu kwakuwa ulinilazimisha ukihofia usalama wako,.

Ujue madam Kuna siku ungesikia nipo ndani maana tayari nilishaonekana kama Nina njama za kutaka kumuua,

Kisa nini umuue, aliuliza madam.

Ni kwasababu nilimpa hela nyingi kiasi Cha kumtisha huyo dada yako sijui mdogo wako,

Achana naye mshamba tu huyo angekuwa mtu mwingine si angekula zile hela, Tena nikwambie tolu huu mpango wa kutaka kupatanishwa na ESTA nilianza siku nyingi tu, nilimtuma mtu nikampa pesa amshawishi huyu ESTA ili tupatane lakini Cha ajabu yule yule mtu aliishia kumtongoza tu ESTA akatembea naye, na Akala hela zangu.
Alisema madam kwa masikitiko .

Nikawaza kumbe Kuna majamaa hawana woga na kitu Cha mtu.
Tuliagana huku madam akiondoka na ESTA na yule mama yake, na Mimi na mke wangu tukatafuta kituo Cha Dala dala. Wakati tukatembea taratibu huku mke wangu akionesha kutokuwa namimi hata kistori tu.

Dah hii adha ya daladala hii, ya ipo siku tu lazima tununue gari yetu mke wangu maana hebu ona watu wanavyogombania mlangoni, Sasa wewe unawezaje Ukiwa na mtoto mdogo, Bora tuite Taxi tu.

Nani wa kununua gari, wewe mume wangu Huyu huyu, ambaye unafanya kazi kuuubwa isiyokuwa na malipo, mbaya zaidi wanakubembeleza chukua basi hata kidogo hutaki wakataka kunipa Mimi umekataa,

Yaani unajifanya mtume mwaminifu kwamba unapatanisha watu bure bila malipo, kwanza ngoja tufike nyumbani utanieleza vizuri we ni mtu wa aina gani ambaye unafanya mambo makubwa bila kunishirikisha na hadi Sasa nashindwa kuelewa uliwezaje kujitesa mwanaume mzima kujaa unafiki wa kupatanisha watu bila maslahi,

Sasa pale hata kama ungesema wakupe milioni moja , kwa kazi uliyofanya nani angeguna unafikiri Cha ajabu eti hutaki hela, pole sana mume wangu nadhani kwako Kuna kitu hakipo sawa,. Aliweka kituo baada ya dereva taxi kuwa amefika tukaingia ndani.

Malalamiko ya mke wangu niliyavumilia baada ya kukuta ni mropokaji asiyekuwa na subira hata hivyo siyo kosa lake maana sikumwelewesha mapema lakini nitamfanyia surprise tukifika nyumbani.

Tulifika nyumbani huku mke wangu akiwa bado kakasirika sana, akawa mkali mkali fulani, Kabla sijamuonesha ule mpango mzima nilipokea simu toka kwa meneja wa kazini kwangu,

Huyu naye anataka Nini kwenye hii wikiendi , nikaweka simu sikioni.

Daniel, nimekuona na mke wa boss mida fulani hapo vipi man kikao gani?
Aliuliza bila hata salamu.

Sasa meneja pale ni mgahawani, Mimi nilienda kivyangu na yeye alikuwa kivyake Sasa kwakuwa ananifahamu ikabidi tujumuike kwenye meza moja vipi Kuna tatizo?

Tatizo lipo, Tena unatafuta kufukuzwa kazi. Akakata simu

Itaendelea..............
Balaa lingne
 
SEHEMU INAYOFUATA....

Usiku wa siku hiyo, nilikuwa na mawazo kiasi,

Huyu Madam, anataka nini kwangu, ana watu maarufu wakubwa wakubwa anafahamiana nao, amekosa wasiri wake kuwaeleza juu ya shida yake.

Kwanini Mimi,
Anadhani Mimi mtoto wakiume nitamsaidia Nini.
Halafu kumbe namheshimu bure tu hata Elimu hana ya kutosha yaani ndumba na uchawi vilimbeba,

Ila huyu stori zake zinatisha, yaani kile mwanaume anaye mpata rafiki yake alimpora, na kumroga kabisa, dah mdada ana roho mbaya sana huyu, Tena Sasa hivi sipaswi kujenga naye mazoea kuonekana naye kwa jinsi alivyo anaweza kukuchoma na kukuachisha kazi.

Ila anaonekana kakitembeza sana, maana Kuna Mwajuma wa uwanja wa fisi huwa wanamsifu kuwa aliitendea haki kazi yake ya kujiuza kiasi Cha kupata kibanda Cha vyumba vinne, lakini huyu Madam kiboko, kutoka huko mkoani Hadi kuwateka mtu na baba yake mbaya zaidi bado akapata utajiri wa kutosha. Kweli uchawi upo, na kama anatoka kweli huo mkoa alionitajia, Sina pingamizi kuhusu uchawi,niliwaza sana.

Mke wangu,
Akaitika.

Hivi yule kijana mnaye sali naye ambaye ni fundi ujenzi ana jicho chongo hivi bado yupo? Niliuliza

Ndiyo yupo, huwa anapiga kinanda kanisani? Alijibu

Sawa nataka namba zake au kesho ukimuona mwambie aje hapa nyumbani, nataka aje anipe ramani fulani jinsi fence yangu itakavyokaa,

Heeee mume wangu hivi naye yule ni fundi, mbona kama ni kilema?

Hapana, ni bonge moja la architecture kama hujui, nikamtajia baadhi ya majengo aliyosimamia na yakawa poa,
Na hata lile jicho aliumia kazini hajazaliwa nalo vile. Niliongeza

Haya, naona safari hii hutaki masihara baba, aliongea huku alitoa kicheko flani Cha sanifu.

Mke wangu , hata Kama huku ni uswahilini lakini, lazima nyumba yangu iheshimike hebu fikiria kesho unasema Kuna wageni watakuja naamini tutalazimika kukaa hapo nje kwenye mti huku wapita njia wakiona kila kinachoendelea. Yaani siyo sawa.

Ila nikweli, alijibu.

Halafu mke wangu, hivi umeniambia na ESTA anakuja hapa,?

Ndiyo atakuja, kwanini umeuliza hivyo mume wangu.

Ni kwasababu yeye ana sali kwenye makanisa mengine, kumbuka wanaokuja hapa ni sehemu ya jumuiya yetu.

Nilimjibu hivyo kwa kumpoteza ila nilitaka kuhakikisha ujio wake kwakuwa nilitamani kujua historia fulani ya maisha yake.

Ujue Nini mume wangu, yule ESTA anapenda sana kuwa karibu na Mimi na pia namfariji kwa namna moja au nyingine, unakumbuka siku ambayo ulitoka mkoani Kisha nikakwambia nitampeleka sehemu?

Ndiyo nakumbuka,
Nilimjibu

Basi kibao kilibadilika, baada ya Mimi kumpeleka, akanipeleka Mimi, kama unavyojua nilikuwa nimeishiwa nguvu kwahiyo akataka kunisaidia, Cha kushangaza baada ya kugundua kuwa ofisini kwako ni pale , nilimuona akinyongea sana yule shoga yangu,

Hata baada ya kutoka eneo lile bado hakuwa na amani kama mwanzo alivyokuwa akinifariji kuwa wewe utatoka tu, badala yake akawa yeye ndiyo mwenye mawazo zaidi, huku akiwa anaongea peke yake, siku zingatia mambo yake kwa kuwa nilikuwa nakuwaza wewe. Aliweka kituo

Nilimwelewa sana mke wangu Tena sana kwakuwa tayari nilijua kitu,.

Halafu mume wangu nasikia kumbe ESTA alikuwa malaya balaa, na kachezea maisha sana.

Wewe umemsikia nani? Niliuliza

Dunia Ina Siri baba, eheeeeh kila kitu kipo wazi mbona, wamechezea maisha huko halafu wanakuja kuishi maisha mabaya kiasi hiki, yaani ana maisha magumu yule dada wewe acha , Tena mzuri masikini, kweli uzuri siyo ndiyo kila kitu, Tena pale alipo Hana hata mtoto, sijui atapata lini maskini, wameharibu mimba weeeee Sasa hivi wanahaha,
Aliongea kwa kulaumu

Dunia Ina mapito mengi mke wangu huwezi jua, niliongea kwa utulivu huku huruma ikiniingia kulingana na nikichosikia mchana wa siku ile .
Sikutaka kumsimulia mke wangu, maana nawajua wanawake zetu hawa.

Lakini nikafikiria kama ESTA atakuja nitatumia nafasi hiyo kuongea naye mambo fulani ili nipate kuwianisha vitu, japo sikutaka kumwambia Yale aliyonituma Madam,

Kwanza ningeanzaje, mwanaume nakuwaje hivyo, niliwaza kumsaidia ESTA

Mume wangu ni saa sita hii tayari jumapili ishaingia tulale bwana tupunguze usingizi naona unawaza, unamuwaza huyo ESTA au,

Weweeee Mimi Nina mawazo yangu mke wangu kama tumeishiwa stori tulale, nilimjibu.

Asubuhi ilifika maandalizi ya kanisani yalipamba moto, Mama mzazi akanifuata,

Dani mwanangu Leo unaenda kanisani, kumbuka tangu nifike hapa sijawahi kuona ukijishughulisha na mambo ya kanisani vipi, na kesho kutwa jumanne nasafiri sitaki niondoke bila kuona ukienda kanisani, Sasa Leo lazima utaenda.

Nikaona ishakuwa kesi hii nikajiandaa nikaenda na Mimi ,
Huku nikijifichaficha baada ya Misa kuisha nikawa wa kwanza kutoka na kurudi nyumbani huku nikiwaza sana

MUNGU atusamehe sana , hivi Leo kifuani Nina chale,Tena mbichi kabisa Leo nimeenda kanisani, Yesu mwenye alikataa mtu kuwa wa vuguvugu , leo hii sijulikani wamoto au wa baridi, MUNGU nahitaji huruma yako, nafika nyumbani nilimkuta ESTA kajaa tele anatusubiri,

Shemu huyoooo, alinikaribisha ESTA
Najua kama nimewahi sana ila kwakuwa Sina simu nikaona ni vyema kuwahi, aliongea.

Ina maana huna simu ya mkononi . Niliuliza kwa mshangao.

Ndiyo Nini Cha ajabu nimeamua kuiuza kwakuwa maisha ni magumu Tena na maisha magumu we Daniel acha tu, sijui kwanini MUNGU hanichukui nikapumzike Mimi.
Aliongea kwa uchungu sana.

Hayo siyo maneno Dada yangu,kikubwa ni kuendelea kumuomba MUNGU mbona kila kitu kitakuwa sawa tu,nilimfariji.

Hapana Dani siyo kwangu,Sina makazi maalum Sina familia,kama nyie wenzangu ama kweli ujanja mwingi mbele kiza,naishije mjini Daniel, aliongeza.

Dah,kwani kwa Sasa una kazi gani ya kujiongezea kipato? Nikiuliza

Niwe na kazi gani mwenzangu,Mimi naishi kama omba omba tu.

Nikaingia ndani nikawaza sana
Yule madam anaonekana anajuta kwa kile alichomfanyia mwenzake miaka hiyo na yupo tayari kumsaidia kama kumlipa kwa mabaya aliyomfanyia.

Mmmmh hili ni balaa,na Mimi sitaki kujiingiza kwenye huu upumbavu,kwanini asitafute wanawake wenzie wawaunganishe ,halafu hivi anashindwa kabisa kumsaka huyu akamface mwenyewe,

Natamanj nimwambie kuwa Kuna mtu Ana shida na wewe lakini siwezi,au nimuunganishe yule madam na mke wangu ili ujumbe umfikie ESTA?
Haaaa siwezi kwanza nitamtesa mke wangu na tumbo lake siwezi.

Japo kuwa lazima nitakaa na ESTA ili anipe background ya maisha yake ili lazima nitakaa naye.

Nikachukua kiasi fulani Cha pesa nikampatia huku nikimuahidi kumsaidia na pia nikisisitiza ananunue simu,

Alifurahi na kunishukuru sana.

ESTA mwanamke wa mjini kipindi hicho niliwahigi kumfuatilia sana lakini alinifungia vioo,sikuwa saizi yake

Lakini siku si nyingi nilimtongoza huyu, Kabla hatujakutana tayari nikapata taarifa juu ya shida yake.

Ni mzuri,mrefu kaenda hewani mweupe umbo ni kama madamu yaani wanafanana vitu vingi tofauti yao ni kwamba Madam ana weusi kidogo,wanaita chocolate colour.

Ila madam ana ngozi ya hela, huyu ESTA ukute anaogea mpaka sabuni ya magadi,wakati nafikiria haya nilisikia sauti za watu wengi wakija nyumbani kwangu.

Huku wakiwa wameongoza na mke wangu,

Mke wangu naye yaani kawatoa watu kanisani anawaleta huku wamekula kweli Hawa,haya si mambo ya kuharibu bajeti haya.niliwaza

Mume wangu wakati ibada fupi ikiendelea hapa itabidi ,itabidi tuandae Chakula kwaajili ya ugeni,

Haaaa uandae saizi kwanini usingewahi? niliuliza

Sikujua kuwa tukitoka tu kanisani watakuja moja kwa moja na huu siyo muda wa kubishana, najua ulitoa hela ya vinywaji,ila Leo bajeti zimeongezeka, aliongeza

sikuwa na jinsi ikabidi nifanye nilichoambiwa si wanasema wageni ni BARAKA,

Halafu njoo huku nje haiwezekani watu wanakuja wewe upo ndani tabia yako sijapenda mtu naangaza macho kule kanisani kumbe wewe umetangulia huku

Itaendelea............
Niko apa,nasogea kwa kasi sana,kaz nzur mwandishi keep it going
 
I
dont-kill-my-vibe-hand-260nw-1946948455.jpg
dont-kill-my-vibe-hand-260nw-1946948455.jpg
 
Hongera tolu kwa upatanisho ulioufanikisha. Above all ni kwasababu kulikuwa na maslahi, je ingekuwa bila maslahi binafsi ungejitosa hata kufikia kuhatarisha ndoa yako?
 
SEHEMU INAYOFUATA.................

Kauli aliyoitoa meneja wangu, ilinishtua kiasi, ila niliiipuuza huku nikiwa tayari nimepanga kuwa jumatatu nitampa makavu yake.

Mke wangu nakuomba uje huku chumbani kwanza , nilimuita.
Lengo lilikuwa nikumtoa zile dharau anazonionesha. Nikasogea kwenye droo nikatoa mzigo kama ule aliouona kule ambao huu wa kwangu bado ulikuwa na nembo ya benki husika.

Una lawama sana mke wangu unapenda kulaumu bila hata kuuliza, nakumbuka niliwahi kukwambia kuhusu Nia ya yule boss uliyemuona lakini, ulinikatalia. Sikutaka kukwazana na wewe kwakuwa niliona maslahi mbele yangu.

Niwe mkweli sijawahi kutamani kutembea na ESTA, hata siku moja kwanza nakuheshimu wewe mke wangu pili Dunia imejaa maradhi hii yanini nije kuitesa familia yangu
Hivyo nisiongee mengi ila Yale malipo ya nilichokifanya ni haya(nikichukua ule mzigo na kumtupia kwenye Kochi)

Mmmmh mume wangu, kwanza nashukuru kwa kunitoa hofu maana wivu nao ulichukua nafasi yake, lakini pia nikupe hongera kwa kufanya kazi yenye malipo ambayo unadhani ni mazuri, lakini kwangu hii si kazi nzuri ni kazi ya hatari sana, utakuja kufa kwa kuwekewa mitego, maana Leo hii tayari washakujua unapenda hela za dezo hivyo mtu akitaka kukufanyia jambo baya ni rahisi na mapema tu unakuwa matatizoni,

Duniani hakuna mtu asiyependa pesa, hata Mimi nazipenda sana (huku akigeuzageuza kile kibunda)
Lakini suala kubwa ni zimepatikana kwa njia gani? Aliuliza

Naomba niwe mkweli namna zilivyopatikana hizi hela naogopa hazina tofauti na pesa zilizoporwa, chunga sana wewe ni mume wangu ni baba wa wanangu, nisinge penda ujiingize matatizoni.

Una kazi nzuri, pia una elimu nzuri bado una nafasi kubwa ya kuja kupata kazi zaidi ya hiyo nikwambie hivyo hakuna haja ya kujipatia hizi hela zilizokaa kikamari, si nusura upelekwe polisi?aliuliza

Lakini mke wangu Kuna baadhi ya watu kama wangetegemea mishahara yao wasinge kuwa na mafanikio, hapa ni mjini my wife Kila fursa itakayojitokeza ni vyema nikacheza nayo. Niliweka kituo

Hata kama Kuna fursa kibao na nakuombea lakini siyo kama hizi, yote kwa yote tuachane nayo hayo,
Vipi una mpango gani na hizi pesa , maana hata school fees ya Jack nilikuwa naiwazia, aliongea kwa mbwembwe huku tukitaniana.

Hivi mume wangu kama akija mtu akasema uchague kimoja Kati ya Mimi na hizi pesa utachagua kipi?
Aliuliza kimtego

Wewe mke wangu una thamani isiyolinganishwa na chochote kile hata ningeletewa kilo mawe Mia ya almasi siwezi kukuacha , ni kifo kitatutenganisha au uanze kuniacha wewe. Nilijibu

(Alicheka sanaaaaa) kweli mwanaume atabaki kuwa mwanaume kwa uongo siwawezi hivi unasahau ulinioa kwa mahari ya shilingi ngapi , huoni ile mahari ndiyo thamani yangu halisi , yaani hata ningerudi kwenye usichana ule mbichi Leo bado mahari yangu inaweza isifike milioni mbili.aliongea akicheka.

Mke wangu mahari siyo thamani ya mke , mahari ni uhalali wa mtu kuwa mke wa fulani, Kuna vigezo na masharti Leo hii naweza Kodi ndege ambayo Sina uwezo wa kuinunua, ila kipindi nitachokodi itakuwa kwenye himaya yangu japo Sina haki nayo.
Nilijibu

Au mume wangu ni sawa na kulipia siti kwenye basi unaweza kulala kukaa utakavyo ila huwezi chukua kisu ukate ule mkanda kwakuwa siyo Mali yako, siyo. Alihoji

Enheee ni sawa Leo hii we ukinikosea nikakupiga na kukuumiza hatua za kisheria zitafuata, licha ya kuwa wewe nilikuoa kwa zaidi ya bilioni miatano, yote kwa yote hakuna mfano utakaoendana na thamani ya binadamu,. Nilisisitiza mke wangu akaniunga mkono

Siku hiyo nilifurahi sana na mke wangu japo hakuacha kutokukubaliana na namna pesa ilivyo patikana.
Nikapiga simu kwa fundi wangu nikimtaarifu kuwa bajeti aliyonipigia kuhusu ujenzi wa fence yangu tayari imekamilika hivyo inabidi Kesho yake ambayo ilikuwa ni jumapili, aje anipe picha ya fence mbalimbali japo siyo zile za kishua sana.

Kama kawaida siku inayofuata nilikuwa na fundi ambaye tulimalizana Kila kitu maana namuamini sana, lakini pia ilikuwa ni nafasi ya kwenda mjini nikajipoze kidogo kwani sifa ya pesa ni matumizi kwahiyo nilikuwa naenda kutimiza azma hiyo.

Nilikumbuka sehemu tulipokaa Jana kwenye kikao chetu na madam, nikaona ni sehemu nzuri ambayo Kuna watoto wakali sana, ambapo kwa Sasa wanaitwa ........

Nilifika kwenye mgahawa ule nikiwa nadhifu, siyo kuvaa misuti ika nilitupia jeans Kali na na t shirt na raba zangu safi mithili ya mwanahiphop au mnyamwezi fulani, siyo pigo zangu hizo lakini siku hiyo nikalazimika kufanya hivyo.

Nilitafuta meza moja matata nikakaa zangu huku nikiwa sijali kabisa gharama za Chakula nazoziona kwenye menu, nilipewa huduma safi huku muda ukizidi kwenda, ndani ya mgahawa ule kulikuwa na Kila aina ya mtu hususani warembo wakali lakini Kila mtu alikuwa bize na mambo yake, nikatoa simu huku nikisearch vitu kujikeep bize.

Nilistuliwa na sauti ya madam,

Heeee baba kumbe nawee huwa unakuja hapa, alisema madam akionesha mshituko maana ule mgahawa ni wa watu maarufu na wenye ukwasi.

Hapana MADAM wakati Jana tukiwa hapa Kuna jamaa tuliongea ishu fulani hivyo akataka tuonane hapa.
nilidanganya.

Sawa, basi mimi ndiyo sehemu yangu , hasa kwakuwa mmiliki ni swahiba wangu akimtaja MD fulani wa kituo kikubwa Cha TV na redio.

Nimekuja na ESTA , sema hujamuona kwakuwa kupitiliza, huko juu ghorofani Kuna kitu kaenda kununua,. Aliongeza

Nikawaza, kupatana toka Jana tu tayari wanaongozana.mara ESTA akaja akiwa na mfuko fulani ile maalumu kwenye masuper market , licha ya kuniona hakunichangamkia sana , yaani si ESTA yule ambaye alikuwa akiniona anaanza kutabasamu akiwa mbali,

Leo hii alikuwa kanuna Tena haswa , hawakuagiza chochote, wakawa wanaongea mambo fulani ambapo inaonekana walikuwa wanatoka mahali, licha ya stori za hapa na pale lakini ikifika muda wa Mimi kuchangia point fulani basi ESTA anaichukulia negative, baada ya kugundua ile hali nikaona hapa Bora niondoke.

Sasa madam Mimi mtu niliyeagana naye kukutana hapa naona hatokei , kwahiyo nawaacha,

ESTA akajibu "Haina shida" tena kimikato kama vile alikuwa anasubiri tu niwaage,

Sasa tulo si ukaekae tupige stori mbona mapema hata kama huyo mtu wako haji basi endelea tuongee bwanaaaa tena leo umependeza na nywele zako umekata kama mwanamziki Madilu System, Kaa bwana au unaniogopa, aliongeza Madam.

Hapana dada mwache aende huyu si ana mke , wacha akambembeleze mama watoto, eti si kweli Daniel? aliongea ESTA huku akionesha dharau fulani, hata madam alishagundua kinachoendelea, akaniruhusu niende.

Nikafikiria kitambo kidogo nikaona sipaswi kutumia kilevi hasa ukizingatia ni jumapili siyo poa, nikashika njia kuelekea nyumbani huku nikimuwaza ESTA , kwanini aoneshe dharau kwangu, kagundua Nini?

Yule ESTA Mpole wa juzikati aliyekuwa kapigika naanza kumpoteza, huyu wa Sasa mi ESTA wa zamani enzi za usichana wake alikuwa na nyodo sana.

Lakini mbona kachelewa? Maana umri nao umemtupa mkono, anadhani nani atamtaka? Labda walugaluga na washambabwa mjini siyo mimi,.

Kubwa zaidi nashindwa kujua ESTA kwa Nini kanichukia ghafla na mapema hivi, lakini pia Kuna meneja wangu alinitisha eti kwanini kaniona na madam mgahawani,
Huyu naye anawezaje kuwapangia watu na maisha yao?

Nini kitajiri, usikose sehemu inayofuata, burudika

Itaendelea............
.
.
 
SEHEMU INAYOFUATA......

Siku ya jumatatu asubuhi nilidamkia kazini huku nikipanga kwenda kumuuliza yule meneja alikuwa na maana gani kunipangia habari zangu.

Kufika ofisini , nikatulia huku nikipangilia vitu vyangu vizuri, nikaletewa taarifa kuwa nahitajika ofisini kwa meneja. nilishituka , kumbe bado anayo tu, huyu hakuna lingine analoniitia ni yake tu Sasa Leo atanijua Mimi ni nani.

Nilibisha hodi ofisini kwake nikakuta wapo watatu yeye na msaidizi wake wa kike anaye mtumaga vitu lakini pia kulikuwa na fundi wa mashine ya photocopy akiwa kaifungua yote, niliwasalimia wote wakajibu kasoro yeye tu, hasira zikanipanda.

Hebu weee Kaa hapo unaangalia Nini hapo kwani ni hicho nilichokuitia? Alisema huku akiwa bize na yule fundi.

Sasa Mimi nitajuaje uliloniitia Ukiwa hujaniambia wee vipi bwana. Nilimjibu kijeuri.

Oyaaa wewe huwezi kunijibu hivyo, Mimi nimekuita kama ndugu yangu ili nikushauri , nadhani Haina haja ya watu kusikia, ni kwamba yule uliyekaa naye pale sisi tunamuheshimu sana kama boss wetu na mke wa tajiri hivyo nimekuita ili nikuonye. Waweza kwenda, akaniruhusu.

Kwanza nilimwangalia kwa dharau Kisha nikamwambia..

Wewe nimegundua unatumia cheo chako kunyanyasa watu, kwanza una uhakika gani kama nilikuwa namtongoza madam, na pili unawezaje kuona picha tu ukaanza kuitolea maelezo bila hata upembuzi, maana pale kulikuwa na wanawake wanne akiwemo mke wangu wa ndoa , Sasa huyo mke wa boss wako nilimtongoza saa ngapi una ushahidi?

Kweli wanaokuita chogo hawakosei, nadhani unapaswa kujitafakari namna unavyomuonea wivu mwanamke akiwa na Mimi.
Kabla sijamalizia alishanivaa akitaka tupigane,akanirushia kiti na kunigonga kichwani nadhani kauli ya kusema alimuonea wivu madam ilimuudhi, pia ni mtu mwenye kichogo hivyo wakati nahamia pale nilikuta wafanyakazi wakimwita hivyo kwa Siri ili asijue maana huwa anamaindi sana.

Alitaka kunipiga lakini niliishia kumkunja motherfucker robber hakuweza kufurukuta.nilifanya vile kwasababu alikuwa anataka kunitafutia kesi,hawezi kupigana na Mimi akiwa kavaa miwani,maana ukiona mtu anaanzisha ugomvi akiwa kavaa miwani usuthubutu kupigana naye Sheria zake zitakubana sana

Yule fundi akatuamulia huku Mimi nikikimbilia ofisini kwangu.

Hasira zikiwa zimenijaa, wasiwasi na hofu ya kufukuzwa kazi navyo havikuwa mbali kwenye ubongo wangu.

Huyu chizi Mimi nikifukuzwa kazi nitamtafuta hata mtaani mjinga huyu hawezi kufuatilia mambo yangu, yaani nikipokea barua ya kusimamishwa kazi tu ajue naenda jela mpumbavu huyu. Nilisema kwa sauti huku nikigundua vishikizo viwili vya shati vimetoka kwenye Lile purukushani.

Mr Daniel, aliita Binti wa kike ambaye nipo naye ofisi moja kama anavyopenda kuniita, ni Binti mdogo nilimuona Kama mchunguzi fulani kumbe sivyo ni mambo ya utoto tu nilimgundua hasa baada ya kuwa tupo ofisi moja.

Naona unavuja damu kichwani, ona pia shati sijui limechanika kwani Nini kimetokea si umetoka hapa kwenda kwa meneja,nani kakuumiza.aliuliza

Ni meneja kaniumiza mdogo wangu, vipi nimeumia sana?
(Huku nikijipapasa sehemu panapovuja damu)

Umeumia Mr, hebu fanya mpango uende hospital, akiitaja hospital iliyo jirani na ofisi zetu huku nikimwambua ilivyo na foleni nitatibiwa mapema kweli? Sikuumia kiasi Cha kwenda hospital ila kwakuwa naamini kampuni itagharamia si kesi.

Nakupa namba za dada yangu ni daktari pale mpigie mwambie unatoka kampuni fulani atakusaidia ni dada yangu wa tumbo moja, unajua Nini wewe umepigana na meneja hivyo process za wewe kwenda hospital zitachukua muda Bora uende anakofanyia my sister utasaidiwa kirahisi.

Nilitoka nje ya ofisi nakuta taarifa zinaenea kama moto wa petrol kapigana na meneja kapigana na meneja , wengine wakiongeza kazi Hana, kazi Hana. Taarifa hazikunitisha sana.

Nikaingia kwenye gari la yule Binti baada ya kunikabidhi niwahi nalo hospital, huku nikiwa na hofu maana sikuwa na leseni japo Mara nyingi huwa natembea nayo.nikaisereresha ile Nadia mpaka hospital anakofanyia huyo dada yake, kufika pale nikapiga simu zaidi ya Mara kumi haikupokelewa ila nikiwa nimeegamia gari pale nje alikuja dada mmoja mzuri, mzuri, narudia tena ni mzuri yule dada jamani.

Alikuwa na madaktari wenzie wakishangaa ile gari.....

Jamani hili gari ni la mdogo wangu sijui kafata Nini hapa au anaumwa?
Nikagundua huyu ndiyo mwenyewe maana walikuwa wanafanana japo dada mtu ni mzuri zaidi hasa ile mianya.

Hapana doctor, nimekuja nalo Mimi kanipa mdogo wako, pia nimepiga simu Mara kadhaa hujapokea,. Nikaweka kituo.

Wale madaktari waliangaliana wakacheka huku yule dada akishindwa kuamini maneno yangu, nilionesha kidonda changu kuwa nahitaji tiba waliharakisha nikajikuta napelekwa kwa daktari bingwa kabisa nadhani wajihi wangu uliwatisha alinifunga bonge la bandeji nikaifurahia sana namna ilivyowekwa nilitaka iwe hivyo ili kila mmoja ajue nimeumia kwa kiwango Cha lami.

Baada ya Kila hatua kukamilika nikalipa kiasi fulani Cha pesa Kisha nikarejea kwenye gari huku yule daktari akija usawa wangu.

Jamani bado nipo njiapanda ningependa kukufahamu wewe ni nani. Aliuliza.

Naitwa Daniel (nikitaja full name)
Nafanyakazi kampuni ya******
anapofanyia mdogo wako na tupo ofisi moja kwahiyo baada ya Mimi kuumia akaamua kuniazima gari niwahi nalo kupata tiba.

Mmmmh haya naona tutambuana vizuri baadaye ila Mimi naitwa Dr. Rosemary ukiita Rose inatosha naona tutawasiliana. Nilimsindikiza kwa macho yule Dr.,Kisha nikawasha gari kurudi ofisini huku nikiwa natega sikio Nini nitakuta kimejadiliwa, Kuna majuto fulani yalikuwa yananijia lakini nilijikaza , kila nikiwaza jinsi nitakavyopokea barua ya kusimamishwa kazi tumbo liliunguruma huku haja kubwa isiyo ya lazima ikitaka kutoka.

Nikaliingiza gari, nikapark nikarejea huku waniko na wambea hawakuwa nyuma pole nyingi za kinafiki, nikapitiliza hadi ofisini kwangu nikamkuta yule Binti ambaye tulikuwa kama ndugu hasa baada ya kuwa nilikuwa kama mwalimu wake kwa vitu vingi na kunifanya aniheshimu sana.

Vipi Nini kimejiri hujasikia lolote, hapa niliuliza kwa shauku.
Hapana ila meneja alikuja kukuulizia nikamwambia umewahi hospital kasema ukirudi nimwite aje hapa, alisema yule dada.

Kamwite kama anataka kunimalizia nijue kabisa maana anaitaka roho yangu.

Hapana Wala Hana hizo huwezi amini kaja akiwa Mpole kweli. Aliongeza

Sikia usimwite mimi naendelea na kazi yangu, tukaendelea na kazi huku Binti akishauri ni Bora ukapumzike maana unaweza kukosa umakini. Lakini niligoma

Kuna muda nilipewa taarifa kuwa General manager anatuita kule juu ghorofani, hapa tumbo la kuharisha lilinishika , nilipandisha ngazi nikamkuta meneja niliyepigana naye, na general meneja wakiwa wanakagua vitu kwenye computer.

Nikaingia huku nikikosa kujiamini,
Nikakaribishwa

Wewe nasikia umekuwa bondia unataka haribu taswira ya kampuni vipi, unadhani nani taleta tenda kwenye kampuni iliyokosa displine, kama umechoka kufanya kazi waweza kuacha tu,. Aliongea yule msomali mwenye kiswahili kibovu huku macho yakiwa kwenye computer.

Hapana boss, niliongea Kila kitu tangu meneja chogo alivyonipigia simu hadi, alivyoniita ofisini kwake kunikanya jambo ambalo Hana uhakika nalo. Mambo yale yalimwingia sana yule msomali akaacha hata shughuli alizozifanya na kuwa bize kunisikiliza.

Sasa mbona Mimi mesikia tofauti huku akimugeukia yule meneja, wewe unasema huyu afukuzwe kazi kwa lipi labda,?

Sasa wewe nenda kaendelee na kazi maana hili jambo limemgusa mke ya boss sawa sawa ila nitakuita utakapohitajika. Akaniruhusu nikaondoka

Meneja anataka kunifukuza kazi kwasababu gani, nashukuru general kasema niendelee na kazi. Nilimwambia yule dada ambaye niko naye ofisini muombe MUNGU kaka Mimi Wala sijaona kosa lako alisema yule Binti akionesha kunihurumia

Nilifungasha vibegi vyangu nikaondoka nikiwa nimenyong'onyea kwa mawazo

Nilifika nyumbani huku kila mmoja akinishangaa kulikoni bandeji Tena,

Yaani mume wangu mwaka huu ni wako likitoka hili linaingia hili , baba, umuombe MUNGU mwenzangu utakuja kufa. Nilinyamaza , saa tatu usiku nikiwa kwenye lindi la mawazo simu ya MADAM iliingia, kwanza nilishangaa si kawaida yake kupiga simu usiku ule, nikaipokea nikaweka sikioni, tukasalimiana.

Pole sana tolu sihitaji maelezo toka kwako nimesikia Kila kitu kuhusu wewe na yule kinyamkera, yaani kunitongoza anitongoze yeye halafu akufukuzishe kazi,

Mimi yule alivyonitongoza , nilitaka kumpiga chini lakini niliwaza kuwa naye ni mwanaume aliziwasilisha hisia zake, japo alinikosea adabu unadhani mzee angesikia ingekuwaje, niliyazimazima ili tu kulinda kazi yake Sasa nasema atajuta. Ameyaamsha mwenyewe.

Wewe usijali hakuna atakaye kufukuza kazi hapo labda nikifa.vipi umeumia sana tolu nasikia nusura akuue, kabla sijajibu
Akakata simu.

Nilishusha pumzi taratibu huku nikitabasamu nikawaza Nini kilinifunga nikashindwa kumpigia simu fasta huyu boss wangu.

Mambo ni moto, ESTA kaninunia sijui kwanini, lakini Kuna Binti mrembo ambaye anaitwa Rose, huyu nitamuachaje.

Usichoke kufuatilia hii simulizi

Itaendelea....................
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom