Simulizi: Mimi na Boss Wangu

Simulizi: Mimi na Boss Wangu

Nilitulia, nikapata chakula fresh huku nikiwa na shauku nini kipo kwenye ile barua

Nikaifungua nikaisoma nikawa nimeelewa, ni moja ya kampuni mpya ambazo nilituma maombi miezi miwili iliyopita, kwahiyo ni barua ya wito ikiwa inanitaka nifike kwenye kampuni zao ili taratibu zingine ziendelee.

Nikapumzika, Kisha nikamwita mke wangu,

Enhee habari za hapa,

Ni nzuri sisi tumeshinda salama kabisa mume wangu ila nina mazungumzo kidogo na wewe maana hapa nilipo hali yangu nishakueleza tangu jana, kwahiyo nafikiri ni muda muafaka wa Mimi kuanza kuhudhuria kliniki mapema.

Lakini mume wangu mbona hii taarifa tangu jana hata leo ,naona upo mbali sana, kwanini?

Nipo mbali kivipi, umeniambia upo hivyo ile Jana nimekubali, umeniambia kuhusu habari za kliniki, Mimi sijakupinga!!!!

Ulitaka nifanyeje labda, ulitaka niruke ruke kama wanandoa waliokaa miaka ishirini bila kupata mtoto.

Kwamba pindi nisikiapo hii kauli nishituke? Sisi siyo wagumba mke wangu tumshukuru MUNGU kwakuwa wazima kwahiyo taarifa hiyo haijanishtua, kifupi nimefurahi sana, mahari yangu naona inalipa haikupotea bure, nilitania wote tukacheka.

Basi sawa mume wangu, mimi nimekuambia ili ujue kuwa humu ñdani una mgonjwa tayari, huku akiinuka kuelekea nje.

Nilikaa kitambo pale ndani nikichezea chezea simu huku sijui hata nabonyeza button kwa malengo gani maana nilishachoka, huku nikijiwazia.

Dunia ya Sasa, inahangaika kutengeneza uzazi wa mpango wa kila namna ikiwa ni njia ya ku decrease population ya watu.

Maana tupo wengi mno lakini kumekuwa na milipuko kadha wa kadha ikiwemo Ebola inayowapukutisha watu huko Afrika magharibi, wajuaji wanasema pengine ni mpango wa wazungu katika kupunguza watu.

Lakini pia Nina marafiki wengi ambao wapo vizuri kimaisha lakini ndoa zao zinayumba sababu zikiwa kutopata watoto, na ni kweli, mbona hata rafiki yangu Shedy haelewani na mkewe japo yeye ndiye mtuhumiwa kwamba mimba zinaharibika, watoto wanakufa Mara tu baada ya kuzaliwa, huku lawama zikikaa kishirikina zaidi kwamba jamaa anaua watoto ili nyota ing'ae na kupush biashara zake.

Walimwengu bwana.

Pengine hata haiko hivyo, nilijisemea

Yote kwa yote acha mke wangu azae hata akizaa watoto kumi nipo tayari. Nikainuka nikatoka nje nikawakuta mke wangu na dada wa kazi wanacheka huku wakionesha wanafuraha sana.

Nikawapita, nikaona ngoja hata niende sehemu nikapige stori, huyoo mpaka kwa fundi TV mmoja hivi ambaye vitu vyangu vingi hurekebisha yeye pindi vikisumbua.

Aaaa karibu kaka, karibu sana, ilibaki kidogo nikupigie yaani ni kama MUNGU kasaidia wewe ufike hapa,

Aliongea yule fundi,

Yule jamaa aliyekuwa anataka TV kubwa ananisumbua bwana maana yule bwana ana Banda la kuonesha mipira, kwahiyo alikuwa anahitaji screen kubwa ili kuleta ushindani, maana wateja wamekuwa wakimtukana kwa kwamba TV zake ni ndogo kama side mirror, kwahiyo inamuwia vigumu sana.

Na hela kaka ipo ana mia tano Cash, halafu kaka ile TV yako kubwa mno, yaani kuuuuuuubwa kama nani za projector ni Bora uuze halafu utafute TV fulani ndogo ndogo na Kuna mama mmoja wa kipemba anayo TV anauza yaani ni nchi 21 ila kizuri balaa anauza laki tatu tu.

Kwahiyo ungeuza yako, bado ungebakiwa na hela nyingi tu ha hahaaa akajichekesha.

Baada ya kimya Cha muda mrefu nikamjibu siuzi.

Aaaaa kaka huuzi vipi wakati ulisema mwenyewe na Mimi tayari Kila kitu kipo sawa na hela kaniachia laki tano hizi hapa, sawaa hata Kama kakuachia hela Mimi siuzi TV, tubadilishe hizo stori.

Mara Kuna pikipiki kubwa likatia timu. Oyaaa fundi vipi bwana hadi saizi TV bado au hiyo laki nane umeenda kumuonesha kwanza mkeo ili ajue una hela teh teh yalicheka majamaa, huku nikiwaza kumbe angepata chajuu laki tatu nzima, siyo mbaya mjini hapa lazima ujiongeze.

Fundi akawa anajiumauma maana hata kuwatajia kwamba, ni huyu hapa mwenye TV asingesema, maana dili litabuma. Wanaweza kuongea na mimi yeye asipate chochote.

Nikamuaga fundi huyo nikaelekea sehemu nyingine bado akawa anapiga simu kunishawishi, isingekuwa hivyo niuze TV yangu mwenye nilivurugwa tu na maisha Hadi nikaropoka kuiuza lakini siyo siwezi kuuza.

TV toka Australia niliyopewa zawadi na wazungu sababu ya kuwasaidia wasipelekwe jela baada ya kujikanyaga kwenye serikali ya JK.

Wakakosa hela ya kunilipa ikabidi waniachie vitu vyao ikiwemo tv, ni kama tuzo, kwenye ushindi wa super star, nani auze tuzo?

Njaa tu hizi kuziendekeza,

Jioni nikarudi nyumbani huku nikiwa na hamu ile tarehe ya wito iwe hata kesho, wakati sijaingia hata ndani wale jamaa waliokuwa wanataka TV nilioonana nao pale kwa fundi japo sikufahamiana nao, wakatia timu wakiwa na yule fundi.

Itaendelea............
Nzuri
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom