Mara Ukute huyo Rose nae aliwai kuwa na bifu na Estar
Rose haponi labda sio tolu ninae mjua mimiSEHEMU INAYOFUATA......
Siku ya jumatatu asubuhi nilidamkia kazini huku nikipanga kwenda kumuuliza yule meneja alikuwa na maana gani kunipangia habari zangu.
Kufika ofisini , nikatulia huku nikipangilia vitu vyangu vizuri, nikaletewa taarifa kuwa nahitajika ofisini kwa meneja. nilishituka , kumbe bado anayo tu, huyu hakuna lingine analoniitia ni yake tu Sasa Leo atanijua Mimi ni nani.
Nilibisha hodi ofisini kwake nikakuta wapo watatu yeye na msaidizi wake wa kike anaye mtumaga vitu lakini pia kulikuwa na fundi wa mashine ya photocopy akiwa kaifungua yote, niliwasalimia wote wakajibu kasoro yeye tu, hasira zikanipanda.
Hebu weee Kaa hapo unaangalia Nini hapo kwani ni hicho nilichokuitia? Alisema huku akiwa bize na yule fundi.
Sasa Mimi nitajuaje uliloniitia Ukiwa hujaniambia wee vipi bwana. Nilimjibu kijeuri.
Oyaaa wewe huwezi kunijibu hivyo, Mimi nimekuita kama ndugu yangu ili nikushauri , nadhani Haina haja ya watu kusikia, ni kwamba yule uliyekaa naye pale sisi tunamuheshimu sana kama boss wetu na mke wa tajiri hivyo nimekuita ili nikuonye. Waweza kwenda, akaniruhusu.
Kwanza nilimwangalia kwa dharau Kisha nikamwambia..
Wewe nimegundua unatumia cheo chako kunyanyasa watu, kwanza una uhakika gani kama nilikuwa namtongoza madam, na pili unawezaje kuona picha tu ukaanza kuitolea maelezo bila hata upembuzi, maana pale kulikuwa na wanawake wanne akiwemo mke wangu wa ndoa , Sasa huyo mke wa boss wako nilimtongoza saa ngapi una ushahidi?
Kweli wanaokuita chogo hawakosei, nadhani unapaswa kujitafakari namna unavyomuonea wivu mwanamke akiwa na Mimi.
Kabla sijamalizia alishanivaa akitaka tupigane,akanirushia kiti na kunigonga kichwani nadhani kauli ya kusema alimuonea wivu madam ilimuudhi, pia ni mtu mwenye kichogo hivyo wakati nahamia pale nilikuta wafanyakazi wakimwita hivyo kwa Siri ili asijue maana huwa anamaindi sana.
Alitaka kunipiga lakini niliishia kumkunja motherfucker robber hakuweza kufurukuta.nilifanya vile kwasababu alikuwa anataka kunitafutia kesi,hawezi kupigana na Mimi akiwa kavaa miwani,maana ukiona mtu anaanzisha ugomvi akiwa kavaa miwani usuthubutu kupigana naye Sheria zake zitakubana sana
Yule fundi akatuamulia huku Mimi nikikimbilia ofisini kwangu.
Hasira zikiwa zimenijaa, wasiwasi na hofu ya kufukuzwa kazi navyo havikuwa mbali kwenye ubongo wangu.
Huyu chizi Mimi nikifukuzwa kazi nitamtafuta hata mtaani mjinga huyu hawezi kufuatilia mambo yangu, yaani nikipokea barua ya kusimamishwa kazi tu ajue naenda jela mpumbavu huyu. Nilisema kwa sauti huku nikigundua vishikizo viwili vya shati vimetoka kwenye Lile purukushani.
Mr Daniel, aliita Binti wa kike ambaye nipo naye ofisi moja kama anavyopenda kuniita, ni Binti mdogo nilimuona Kama mchunguzi fulani kumbe sivyo ni mambo ya utoto tu nilimgundua hasa baada ya kuwa tupo ofisi moja.
Naona unavuja damu kichwani, ona pia shati sijui limechanika kwani Nini kimetokea si umetoka hapa kwenda kwa meneja,nani kakuumiza.aliuliza
Ni meneja kaniumiza mdogo wangu, vipi nimeumia sana?
(Huku nikijipapasa sehemu panapovuja damu)
Umeumia Mr, hebu fanya mpango uende hospital, akiitaja hospital iliyo jirani na ofisi zetu huku nikimwambua ilivyo na foleni nitatibiwa mapema kweli? Sikuumia kiasi Cha kwenda hospital ila kwakuwa naamini kampuni itagharamia si kesi.
Nakupa namba za dada yangu ni daktari pale mpigie mwambie unatoka kampuni fulani atakusaidia ni dada yangu wa tumbo moja, unajua Nini wewe umepigana na meneja hivyo process za wewe kwenda hospital zitachukua muda Bora uende anakofanyia my sister utasaidiwa kirahisi.
Nilitoka nje ya ofisi nakuta taarifa zinaenea kama moto wa petrol kapigana na meneja kapigana na meneja , wengine wakiongeza kazi Hana, kazi Hana. Taarifa hazikunitisha sana.
Nikaingia kwenye gari la yule Binti baada ya kunikabidhi niwahi nalo hospital, huku nikiwa na hofu maana sikuwa na leseni japo Mara nyingi huwa natembea nayo.nikaisereresha ile Nadia mpaka hospital anakofanyia huyo dada yake, kufika pale nikapiga simu zaidi ya Mara kumi haikupokelewa ila nikiwa nimeegamia gari pale nje alikuja dada mmoja mzuri, mzuri, narudia tena ni mzuri yule dada jamani.
Alikuwa na madaktari wenzie wakishangaa ile gari.....
Jamani hili gari ni la mdogo wangu sijui kafata Nini hapa au anaumwa?
Nikagundua huyu ndiyo mwenyewe maana walikuwa wanafanana japo dada mtu ni mzuri zaidi hasa ile mianya.
Hapana doctor, nimekuja nalo Mimi kanipa mdogo wako, pia nimepiga simu Mara kadhaa hujapokea,. Nikaweka kituo.
Wale madaktari waliangaliana wakacheka huku yule dada akishindwa kuamini maneno yangu, nilionesha kidonda changu kuwa nahitaji tiba waliharakisha nikajikuta napelekwa kwa daktari bingwa kabisa nadhani wajihi wangu uliwatisha alinifunga bonge la bandeji nikaifurahia sana namna ilivyowekwa nilitaka iwe hivyo ili kila mmoja ajue nimeumia kwa kiwango Cha lami.
Baada ya Kila hatua kukamilika nikalipa kiasi fulani Cha pesa Kisha nikarejea kwenye gari huku yule daktari akija usawa wangu.
Jamani bado nipo njiapanda ningependa kukufahamu wewe ni nani. Aliuliza.
Naitwa Daniel (nikitaja full name)
Nafanyakazi kampuni ya******
anapofanyia mdogo wako na tupo ofisi moja kwahiyo baada ya Mimi kuumia akaamua kuniazima gari niwahi nalo kupata tiba.
Mmmmh haya naona tutambuana vizuri baadaye ila Mimi naitwa Dr. Rosemary ukiita Rose inatosha naona tutawasiliana. Nilimsindikiza kwa macho yule Dr.,Kisha nikawasha gari kurudi ofisini huku nikiwa natega sikio Nini nitakuta kimejadiliwa, Kuna majuto fulani yalikuwa yananijia lakini nilijikaza , kila nikiwaza jinsi nitakavyopokea barua ya kusimamishwa kazi tumbo liliunguruma huku haja kubwa isiyo ya lazima ikitaka kutoka.
Nikaliingiza gari, nikapark nikarejea huku waniko na wambea hawakuwa nyuma pole nyingi za kinafiki, nikapitiliza hadi ofisini kwangu nikamkuta yule Binti ambaye tulikuwa kama ndugu hasa baada ya kuwa nilikuwa kama mwalimu wake kwa vitu vingi na kunifanya aniheshimu sana.
Vipi Nini kimejiri hujasikia lolote, hapa niliuliza kwa shauku.
Hapana ila meneja alikuja kukuulizia nikamwambia umewahi hospital kasema ukirudi nimwite aje hapa, alisema yule dada.
Kamwite kama anataka kunimalizia nijue kabisa maana anaitaka roho yangu.
Hapana Wala Hana hizo huwezi amini kaja akiwa Mpole kweli. Aliongeza
Sikia usimwite mimi naendelea na kazi yangu, tukaendelea na kazi huku Binti akishauri ni Bora ukapumzike maana unaweza kukosa umakini. Lakini niligoma
Kuna muda nilipewa taarifa kuwa General manager anatuita kule juu ghorofani, hapa tumbo la kuharisha lilinishika , nilipandisha ngazi nikamkuta meneja niliyepigana naye, na general meneja wakiwa wanakagua vitu kwenye computer.
Nikaingia huku nikikosa kujiamini,
Nikakaribishwa
Wewe nasikia umekuwa bondia unataka haribu taswira ya kampuni vipi, unadhani nani taleta tenda kwenye kampuni iliyokosa displine, kama umechoka kufanya kazi waweza kuacha tu,. Aliongea yule msomali mwenye kiswahili kibovu huku macho yakiwa kwenye computer.
Hapana boss, niliongea Kila kitu tangu meneja chogo alivyonipigia simu hadi, alivyoniita ofisini kwake kunikanya jambo ambalo Hana uhakika nalo. Mambo yale yalimwingia sana yule msomali akaacha hata shughuli alizozifanya na kuwa bize kunisikiliza.
Sasa mbona Mimi mesikia tofauti huku akimugeukia yule meneja, wewe unasema huyu afukuzwe kazi kwa lipi labda,?
Sasa wewe nenda kaendelee na kazi maana hili jambo limemgusa mke ya boss sawa sawa ila nitakuita utakapohitajika. Akaniruhusu nikaondoka
Meneja anataka kunifukuza kazi kwasababu gani, nashukuru general kasema niendelee na kazi. Nilimwambia yule dada ambaye niko naye ofisini muombe MUNGU kaka Mimi Wala sijaona kosa lako alisema yule Binti akionesha kunihurumia
Nilifungasha vibegi vyangu nikaondoka nikiwa nimenyong'onyea kwa mawazo
Nilifika nyumbani huku kila mmoja akinishangaa kulikoni bandeji Tena,
Yaani mume wangu mwaka huu ni wako likitoka hili linaingia hili , baba, umuombe MUNGU mwenzangu utakuja kufa. Nilinyamaza , saa tatu usiku nikiwa kwenye lindi la mawazo simu ya MADAM iliingia, kwanza nilishangaa si kawaida yake kupiga simu usiku ule, nikaipokea nikaweka sikioni, tukasalimiana.
Pole sana tolu sihitaji maelezo toka kwako nimesikia Kila kitu kuhusu wewe na yule kinyamkera, yaani kunitongoza anitongoze yeye halafu akufukuzishe kazi,
Mimi yule alivyonitongoza , nilitaka kumpiga chini lakini niliwaza kuwa naye ni mwanaume aliziwasilisha hisia zake, japo alinikosea adabu unadhani mzee angesikia ingekuwaje, niliyazimazima ili tu kulinda kazi yake Sasa nasema atajuta. Ameyaamsha mwenyewe.
Wewe usijali hakuna atakaye kufukuza kazi hapo labda nikifa.vipi umeumia sana tolu nasikia nusura akuue, kabla sijajibu
Akakata simu.
Nilishusha pumzi taratibu huku nikitabasamu nikawaza Nini kilinifunga nikashindwa kumpigia simu fasta huyu boss wangu.
Mambo ni moto, ESTA kaninunia sijui kwanini, lakini Kuna Binti mrembo ambaye anaitwa Rose, huyu nitamuachaje.
Usichoke kufuatilia hii simulizi
Itaendelea....................




Bado hujagundua tuu Tolu ni mzembe kabisaa?? Sema kwenye kuzisaka yuko vizurRose haponi labda sio tolu ninae mjua mimi![]()
Mtoto rose na uwa watamu haoSEHEMU INAYOFUATA......
Siku ya jumatatu asubuhi nilidamkia kazini huku nikipanga kwenda kumuuliza yule meneja alikuwa na maana gani kunipangia habari zangu.
Kufika ofisini , nikatulia huku nikipangilia vitu vyangu vizuri, nikaletewa taarifa kuwa nahitajika ofisini kwa meneja. nilishituka , kumbe bado anayo tu, huyu hakuna lingine analoniitia ni yake tu Sasa Leo atanijua Mimi ni nani.
Nilibisha hodi ofisini kwake nikakuta wapo watatu yeye na msaidizi wake wa kike anaye mtumaga vitu lakini pia kulikuwa na fundi wa mashine ya photocopy akiwa kaifungua yote, niliwasalimia wote wakajibu kasoro yeye tu, hasira zikanipanda.
Hebu weee Kaa hapo unaangalia Nini hapo kwani ni hicho nilichokuitia? Alisema huku akiwa bize na yule fundi.
Sasa Mimi nitajuaje uliloniitia Ukiwa hujaniambia wee vipi bwana. Nilimjibu kijeuri.
Oyaaa wewe huwezi kunijibu hivyo, Mimi nimekuita kama ndugu yangu ili nikushauri , nadhani Haina haja ya watu kusikia, ni kwamba yule uliyekaa naye pale sisi tunamuheshimu sana kama boss wetu na mke wa tajiri hivyo nimekuita ili nikuonye. Waweza kwenda, akaniruhusu.
Kwanza nilimwangalia kwa dharau Kisha nikamwambia..
Wewe nimegundua unatumia cheo chako kunyanyasa watu, kwanza una uhakika gani kama nilikuwa namtongoza madam, na pili unawezaje kuona picha tu ukaanza kuitolea maelezo bila hata upembuzi, maana pale kulikuwa na wanawake wanne akiwemo mke wangu wa ndoa , Sasa huyo mke wa boss wako nilimtongoza saa ngapi una ushahidi?
Kweli wanaokuita chogo hawakosei, nadhani unapaswa kujitafakari namna unavyomuonea wivu mwanamke akiwa na Mimi.
Kabla sijamalizia alishanivaa akitaka tupigane,akanirushia kiti na kunigonga kichwani nadhani kauli ya kusema alimuonea wivu madam ilimuudhi, pia ni mtu mwenye kichogo hivyo wakati nahamia pale nilikuta wafanyakazi wakimwita hivyo kwa Siri ili asijue maana huwa anamaindi sana.
Alitaka kunipiga lakini niliishia kumkunja motherfucker robber hakuweza kufurukuta.nilifanya vile kwasababu alikuwa anataka kunitafutia kesi,hawezi kupigana na Mimi akiwa kavaa miwani,maana ukiona mtu anaanzisha ugomvi akiwa kavaa miwani usuthubutu kupigana naye Sheria zake zitakubana sana
Yule fundi akatuamulia huku Mimi nikikimbilia ofisini kwangu.
Hasira zikiwa zimenijaa, wasiwasi na hofu ya kufukuzwa kazi navyo havikuwa mbali kwenye ubongo wangu.
Huyu chizi Mimi nikifukuzwa kazi nitamtafuta hata mtaani mjinga huyu hawezi kufuatilia mambo yangu, yaani nikipokea barua ya kusimamishwa kazi tu ajue naenda jela mpumbavu huyu. Nilisema kwa sauti huku nikigundua vishikizo viwili vya shati vimetoka kwenye Lile purukushani.
Mr Daniel, aliita Binti wa kike ambaye nipo naye ofisi moja kama anavyopenda kuniita, ni Binti mdogo nilimuona Kama mchunguzi fulani kumbe sivyo ni mambo ya utoto tu nilimgundua hasa baada ya kuwa tupo ofisi moja.
Naona unavuja damu kichwani, ona pia shati sijui limechanika kwani Nini kimetokea si umetoka hapa kwenda kwa meneja,nani kakuumiza.aliuliza
Ni meneja kaniumiza mdogo wangu, vipi nimeumia sana?
(Huku nikijipapasa sehemu panapovuja damu)
Umeumia Mr, hebu fanya mpango uende hospital, akiitaja hospital iliyo jirani na ofisi zetu huku nikimwambua ilivyo na foleni nitatibiwa mapema kweli? Sikuumia kiasi Cha kwenda hospital ila kwakuwa naamini kampuni itagharamia si kesi.
Nakupa namba za dada yangu ni daktari pale mpigie mwambie unatoka kampuni fulani atakusaidia ni dada yangu wa tumbo moja, unajua Nini wewe umepigana na meneja hivyo process za wewe kwenda hospital zitachukua muda Bora uende anakofanyia my sister utasaidiwa kirahisi.
Nilitoka nje ya ofisi nakuta taarifa zinaenea kama moto wa petrol kapigana na meneja kapigana na meneja , wengine wakiongeza kazi Hana, kazi Hana. Taarifa hazikunitisha sana.
Nikaingia kwenye gari la yule Binti baada ya kunikabidhi niwahi nalo hospital, huku nikiwa na hofu maana sikuwa na leseni japo Mara nyingi huwa natembea nayo.nikaisereresha ile Nadia mpaka hospital anakofanyia huyo dada yake, kufika pale nikapiga simu zaidi ya Mara kumi haikupokelewa ila nikiwa nimeegamia gari pale nje alikuja dada mmoja mzuri, mzuri, narudia tena ni mzuri yule dada jamani.
Alikuwa na madaktari wenzie wakishangaa ile gari.....
Jamani hili gari ni la mdogo wangu sijui kafata Nini hapa au anaumwa?
Nikagundua huyu ndiyo mwenyewe maana walikuwa wanafanana japo dada mtu ni mzuri zaidi hasa ile mianya.
Hapana doctor, nimekuja nalo Mimi kanipa mdogo wako, pia nimepiga simu Mara kadhaa hujapokea,. Nikaweka kituo.
Wale madaktari waliangaliana wakacheka huku yule dada akishindwa kuamini maneno yangu, nilionesha kidonda changu kuwa nahitaji tiba waliharakisha nikajikuta napelekwa kwa daktari bingwa kabisa nadhani wajihi wangu uliwatisha alinifunga bonge la bandeji nikaifurahia sana namna ilivyowekwa nilitaka iwe hivyo ili kila mmoja ajue nimeumia kwa kiwango Cha lami.
Baada ya Kila hatua kukamilika nikalipa kiasi fulani Cha pesa Kisha nikarejea kwenye gari huku yule daktari akija usawa wangu.
Jamani bado nipo njiapanda ningependa kukufahamu wewe ni nani. Aliuliza.
Naitwa Daniel (nikitaja full name)
Nafanyakazi kampuni ya******
anapofanyia mdogo wako na tupo ofisi moja kwahiyo baada ya Mimi kuumia akaamua kuniazima gari niwahi nalo kupata tiba.
Mmmmh haya naona tutambuana vizuri baadaye ila Mimi naitwa Dr. Rosemary ukiita Rose inatosha naona tutawasiliana. Nilimsindikiza kwa macho yule Dr.,Kisha nikawasha gari kurudi ofisini huku nikiwa natega sikio Nini nitakuta kimejadiliwa, Kuna majuto fulani yalikuwa yananijia lakini nilijikaza , kila nikiwaza jinsi nitakavyopokea barua ya kusimamishwa kazi tumbo liliunguruma huku haja kubwa isiyo ya lazima ikitaka kutoka.
Nikaliingiza gari, nikapark nikarejea huku waniko na wambea hawakuwa nyuma pole nyingi za kinafiki, nikapitiliza hadi ofisini kwangu nikamkuta yule Binti ambaye tulikuwa kama ndugu hasa baada ya kuwa nilikuwa kama mwalimu wake kwa vitu vingi na kunifanya aniheshimu sana.
Vipi Nini kimejiri hujasikia lolote, hapa niliuliza kwa shauku.
Hapana ila meneja alikuja kukuulizia nikamwambia umewahi hospital kasema ukirudi nimwite aje hapa, alisema yule dada.
Kamwite kama anataka kunimalizia nijue kabisa maana anaitaka roho yangu.
Hapana Wala Hana hizo huwezi amini kaja akiwa Mpole kweli. Aliongeza
Sikia usimwite mimi naendelea na kazi yangu, tukaendelea na kazi huku Binti akishauri ni Bora ukapumzike maana unaweza kukosa umakini. Lakini niligoma
Kuna muda nilipewa taarifa kuwa General manager anatuita kule juu ghorofani, hapa tumbo la kuharisha lilinishika , nilipandisha ngazi nikamkuta meneja niliyepigana naye, na general meneja wakiwa wanakagua vitu kwenye computer.
Nikaingia huku nikikosa kujiamini,
Nikakaribishwa
Wewe nasikia umekuwa bondia unataka haribu taswira ya kampuni vipi, unadhani nani taleta tenda kwenye kampuni iliyokosa displine, kama umechoka kufanya kazi waweza kuacha tu,. Aliongea yule msomali mwenye kiswahili kibovu huku macho yakiwa kwenye computer.
Hapana boss, niliongea Kila kitu tangu meneja chogo alivyonipigia simu hadi, alivyoniita ofisini kwake kunikanya jambo ambalo Hana uhakika nalo. Mambo yale yalimwingia sana yule msomali akaacha hata shughuli alizozifanya na kuwa bize kunisikiliza.
Sasa mbona Mimi mesikia tofauti huku akimugeukia yule meneja, wewe unasema huyu afukuzwe kazi kwa lipi labda,?
Sasa wewe nenda kaendelee na kazi maana hili jambo limemgusa mke ya boss sawa sawa ila nitakuita utakapohitajika. Akaniruhusu nikaondoka
Meneja anataka kunifukuza kazi kwasababu gani, nashukuru general kasema niendelee na kazi. Nilimwambia yule dada ambaye niko naye ofisini muombe MUNGU kaka Mimi Wala sijaona kosa lako alisema yule Binti akionesha kunihurumia
Nilifungasha vibegi vyangu nikaondoka nikiwa nimenyong'onyea kwa mawazo
Nilifika nyumbani huku kila mmoja akinishangaa kulikoni bandeji Tena,
Yaani mume wangu mwaka huu ni wako likitoka hili linaingia hili , baba, umuombe MUNGU mwenzangu utakuja kufa. Nilinyamaza , saa tatu usiku nikiwa kwenye lindi la mawazo simu ya MADAM iliingia, kwanza nilishangaa si kawaida yake kupiga simu usiku ule, nikaipokea nikaweka sikioni, tukasalimiana.
Pole sana tolu sihitaji maelezo toka kwako nimesikia Kila kitu kuhusu wewe na yule kinyamkera, yaani kunitongoza anitongoze yeye halafu akufukuzishe kazi,
Mimi yule alivyonitongoza , nilitaka kumpiga chini lakini niliwaza kuwa naye ni mwanaume aliziwasilisha hisia zake, japo alinikosea adabu unadhani mzee angesikia ingekuwaje, niliyazimazima ili tu kulinda kazi yake Sasa nasema atajuta. Ameyaamsha mwenyewe.
Wewe usijali hakuna atakaye kufukuza kazi hapo labda nikifa.vipi umeumia sana tolu nasikia nusura akuue, kabla sijajibu
Akakata simu.
Nilishusha pumzi taratibu huku nikitabasamu nikawaza Nini kilinifunga nikashindwa kumpigia simu fasta huyu boss wangu.
Mambo ni moto, ESTA kaninunia sijui kwanini, lakini Kuna Binti mrembo ambaye anaitwa Rose, huyu nitamuachaje.
Usichoke kufuatilia hii simulizi
Itaendelea....................
Hahaaaaaa. Na mdogo wake akijua ataanza shobo kwa Bwana DanielRose kwisha habari yake