Ismail Mboya
Member
- Dec 29, 2019
- 65
- 36
Kiongozi tupo hewan kwa ajili yako boss
Kitaeleweka tuSEHEMU INAYOFUATA.........
Nilirudi nyumbani kuungana na familia huku nikitambua hakuna amani ya moja kwa moja,
Ile furaha ya kupokea kiumbe kipya ilitoweka watu walikuwa kimya sana nilisalimia huku mtu pekee aliyekuwa na furaha japo ya kulazimisha ni ESTA, ambaye tayari nilimchukia kwa kiasi fulani.
Daniel mwanangu kabla ya kufanya chochote Nina mazungumzo na wewe,
ni maneno toka kwa mama yangu mzazi
Kwanza mwanangu pole kwa misukosuko na mengi yanayokukabili, watu wote hapa tumeungana kwenye hii familia si kwa kuja kula Raha Bali ni visa na mikasa vimetuunganisha.
Kila mmoja anatambua Nini kimetutoa mkoani kuja hapa, labda nikukumbushe tu kuwa kwenye maisha Kuna mikosi, na mwanangu mikosi ilikutembelea, ukawekwa mahabusu, naamini ulihitaji dhamana kutoka kwa watu wenye uchungu na wewe , hebu kumbuka una marafiki na maswahiba wangapi hapa mjini,hawakukusaidia
Na je, unawezaje kutofautisha nyakati mwanangu au unaishi tu, mwanangu hii ni Dunia,
Nimekuja kutoka mkoani Mimi na dada yako siyo kwamba tulikuwa na uwezo wa kukutoa mahabusu sisi kwenye hii Dunia ya kisasa iliyojaa rushwa , hapana,.ni upendo tu
Unadhani Mimi au dada yako hata mkeo nani angeweza kukunasua kwenye ule mtego wa matajiri wenye pesa wanaoweza kukufanya chochote kile,
Sisi kazi yetu ilikuwa ni moja tu kukuonesha UPENDO tu, mwanangu unatambua kuwa sisi wazazi wako ni maskini si matajiri, tunakutegemea kwenye mambo mengi, unadhani tungekusaidia Nini kwenye kesi yako.
Naomba utambue nafasi aliyocheza mke wako kipindi una matatizo ni sehemu pekee ya kutambua thamani yake kwako, sisemi kuwa hakukosei, najua anakukwaza kwa mambo mengi lakini Mimi kama mama yenu na mama yako mzazi nakuombea na kukukumbusha kuwa makini.usipende kuweka msimamo Kila sehemu mengine yapuuze
Nachoweza kushukuru ni kwamba mkeo kajifungua salama na maendeleo yake yanaridhisha sana tu kwahiyo hatuna Cha kutuweka hapa kwako ni kwamba tuna masaa machache ya kurudi nyumbani mkoani maana ulituomba tukae kwaajili ya mgonjwa hatimaye MUNGU kajalia na kutia wepesi.
Lakini mwanangu nikuulize swali moja ulikuwa na maana gani kumkoromea mkeo?
Mtu ambaye anahitaji UPENDO wa dhati toka kwa mumewe hasa kipindi kama hiki alichojifungua,? Alimalizia Mama kwa mfumo wa swali.
Nikamjibu,
Kiukweli Mama wewe mwenyewe kwa siku ulizokaa hapa , umegundua ni jinsi gani huyu ESTA anavyokuwa karibu na mke wangu, Sasa iweje ujio wake uwe msala kwangu Mimi, kifupi mke wangu kanikera sana.nilimalizia
Sawa mwanangu, naomba utambue kuwa humu ñdani watu wote ni wanawake, hebu jitofautishe basi Dani, hebu jaribu kudharau baadhi ya vitu visivyokuwa na umuhimu , ni aibu kubwa Mimi nianze kuwasuluhisha nyinyi katika kipindi ambacho mkeo katoka kuponea kwenye tundu la sindano,
Yaani ilikuwa ni wakati wa wewe na mkeo kukaa na kuanza kupendekeza jina la mtoto ataitwa nani na siyo kutengeneza malumbano.
Aliweka kituo.
Nilimwelewa sana mama nikaingia chumba fulani ambacho huwa hakitumiki nikamkuta mke wangu akiwa na furaha tu anachezacheza na mtoto tofauti na nilivyofikiri baada yakuona watu wengine kule nje wamenuna nuna yeye alikuwa poa kabisa tulisalimiana nikampa pole huku tukitaniana baadhi ya vitu.
Oooh hiki kipindi kigumu, Mara ooh umeshikaje ujauzito Mimi Sina kazi, Sasa nimemleta huyo hapo mkatae Sasa, alitania mke wangu.
Weee nimkatae, kwanza hii jinsia nilikuwa naisubiri kwa hamu, yaani nataka siku moja kama nitakuwa hai niende pale airport nimuone akishuka kwenye ile midege ya Emirates huku akiwa nadhifu na Yale mavazi yao,
Halafu kwa makusudi nimwambie mbona simu yako haikuwa hewani,nilitania
Wewe mwanangu sitaki awe rubani , huyu atakuwa daktari bingwa nikwambie, alisema mke wangu Huku tukitaniana mambo mengi, ambapo nilifurahi sana,
Maana timbwili nililokuwa nimepanga kufanya nilijikuta nasutwa tu moyoni mwangu ila nikashukuru kama mambo yamekuwa sawa , najua atakuwa kamshitakia mama,
Na bimkubwa navyomjua atakuwa kaniponda weee ili ampe ushindi huyu , bimkubwa hajawahi niangusha kwenye kumbembeleza mtu
Baada ya kupata ile amani ya moyo sikutaka kuzungumzia habari za ESTA muda huo ili kuepusha Shari.
Nilitoka nje kucheki mazingira nikamuona ESTA akiwa anajituma anafua nguo za mke wangu akisaidiana na dada yangu, nilimuhurumia sana , Kuna wakati baada ya kukwazana na mke wangu kwenye simu nilimuona huyu ndiyo chanzo , nikapanga nije nimtimue lakini maisha acha yaitwe maisha
Kama tu Mimi mwanaume nilipigika Hadi nikawa nauza vitu vyangu kipindi fulani itakuwa kwa huyu mwanamke?
Kumbe atafanyaje, ajiuze, Bora kaja kuomba msaada sishindwi kuishi naye tatizo lipo kwa mke wangu lakini pia si madam karidhia tumfungulie biashara?
Kwanza ngoja, Kila kitu kitakaa sawa.
Kaka vipi mbona unaizunguka nyumba kama unaizindika vipi, alitania dada yangu,
Hapana nilikuwa huko nyuma naangalia mahali pa kumwaga tofali nahitaji kuijenga fence.
Ahaaa safi my brother, tunakuombea kwa MUNGU Kila kitu kiwe poa,naona nyumba itapendeza sana
Alijibu
Wakati tunaongea hayo nilipokea simu namba ngeni,nikaiweka sikioni
Habari kaka,za siku nyingi Mimi ni Shedy,
Kwanza nilibadilika, maana sikupenda mazoea Tena na huyu mshikaji,
Unasemaje, niliuliza
Aisee kaka jaribu kusahau yaliyopita Mimi na wewe ni ndugu kabisa unajua tulipotoka, nina mazungumzo na wewe kaka, aliongea kwa tahadhari.
Ongea nakusikiliza,
Sawa ni hivi ,mwenzio baada ya kukuta biashara inayumba na zile shughuli zangu zimekuwa ngumu nilikopa hela kwenye benki ya(akiitaja hii benki maarufu nchini)
Ni kutokana na shughuli zetu kuwa ngumu yaani udalali kwangu umenikataa kabisa, nikaona nikope hela ili niiboost biashara yangu, lakini mambo yamekuwa tofauti sana
Kwanza Kuna mtu hapa kafungua bar ya kisasa ni Mara tatu ya hii yangu kama ujuavyo kipya kinyemi yaani mwezi wa tatu Sasa wateja wangu maarufu anao yeye.
Hebu fikiria Kuna muda nauza kreti moja tu la bia huku vile vikali huuzi kabisa na wahudumu niliokuwa nao wanaihitaji pesa yao kama kawaida yaani ni hasara juu ya hasara , huku wafanyakazi Mara biashara haiendi jumlisha riba, nitatoka kweli kaka.
Aliongea kwa uchungu wa kujipendekeza.
Sasa hayo ni maisha yako, Mimi nahusika vipi, nilijibu
Hapana kaka, Mimi shida yangu ni moja nataka unisaidie, ni kwamba Kuna mwanamke anaitwa ESTA naamini unamfahamu vyema sana yule Mimi namtafuta sana, ni kwamba yule Kuna kipindi alikuwa mpenzi wangu wa Siri, Sasa wakati wa mapenzi yetu alikuwa na kiasi fulani Cha hela , nikamzuga kwamba aniazime niingize kwenye biashara yangu alikubali, baadaye niwe mkweli baada ya kuwa nishamchoka sihitaji kuendelea naye,
Nilimwambia aangalie ustaarabu mwingine , ndipo alipoamua nimpe hela yake kwanza ndipo tuachane lakini nilimtishia kuwa Hana hela kwangu na nitamshitaki, hakuwa na la kufanya ukizingatia pesa zaidi ya milioni tatu tulipeana bila ushahidi wowote,
Aliweka kituo.
Sikia Shedy unanidharau sana kwamba nikutafutue ESTA hapohapo unanipa mkasa wako wa kimalaya,kumbe ndio tabia yako kutembea na wanawake na kuwadhulumu,kwa mfano ukimpata unataka umfanye Nini,niliuliza safari hii ni kwa ukali,
Ni hivi kaka lengo nimuombe msamaha na naahidi kuwa nitamlipa mbele ya ushahidi kwasababu, kila nikizunguka kwa wataalamu Wananiambia Kuna mtu Ana masikitiko juu yangu,ndiyo maana biashara yangu inayumba.alimalizia
Cha kukwambia ni kuwa Sina mahali ambapo nitampata huyu ESTA kwahiyo wewe fanya mambo yako Mimi Hilo lipo nje ya uwezo wangu,nikakata simu.
Mapya haya kwangu,yaani Shedy mjinga sana,na habari zake za kishirikina,
Eti ananiambia kuwa biashara haiendi kwasababu ya masikitiko ya mtu,wakati anajua wazi Kuna biashara mpya kama yake Tena imekuja kisasa halafu bado unatafuta mchawi,
Ni sawa na bus jipya na la zamani route ile ile na nauli ni moja nani atachagua la zamani,?
Kweli nimeamini ushirikina ukizidi na akili inapungua ,
Lakini huyu ESTA naye kumbe mjinga eeh kweli alirogwa akarogeka na kukorogeka , unawezaje kutoa zaidi ya milioni tatu kumpa mwanaume Tena Ukiwa ni maskini,akijifanya Ana mapenzi ya kizungu huu si ulofa huu
Ndiyo maana Kila nikimuuliza baada ya kuuza kibanda chako mkoani kwenu hela ulifanyia Nini haeleweki huyu , niliwaza sana jinsi binadamu tulivyo tofautiana .
Nikarudi ndani huku nikisearch kampuni fulani ya uuzaji wa magari used wakidai bidhaa zao ni Bora sana licha ya kuwa zimetumika nikawa napoteza muda pale,
Mke wangu akavunja ukimya,
Samahani sana mume wangu, kwa Yale tuliyoongea mchana ila tufanye yamepita,
Hivi mume wangu ukimwangalia ESTA kwa ukaribu unadhani ana akili timamu?
Kwanini umeuliza hivyo, mke wangu,ni kwasababu kaja kukaa hapa?
Hapana,
Nahisi Kuna jambo linamsumbua tujaribu kusaidia.
Mke wangu aligundua Nini kwa ESTA?
Nani kampa huo ufahamu kiasi Cha yeye kuwa Mpole na mwenye huruma ?
Itaendelea.....................
Unatufokea nduguMwanzo mlikua mnamkolomea naona saizi mmetia akili. Upole kama wote hahaha




tupo tunaenda pamoja ivo ivo mdgo mdgoSEHEMU INAYOFUATA..............
Nilifikiria sana kauli ya mke wangu, kwanini ahisi ESTA ana mapungufu fulani, lakini nilikuwa na majibu kuwa sababu inayomfanya aonekane hivi ni kwasababu kapigika
Ukiwa na maisha fulani ya mazuri yaani hela ya kubadilisha mboga haikosekani, unaweza kuapa kutofanya kazi zozote za kijinga, yaani unakuwa mithili ya mhitimu wa chuo ambaye kulingana na alichosomea huwa wanajipangia hata mishahara,
Yaani anachagua kazi na kutaka kulipwa anachotaka anasahau kuwa mitaa haihitaji Elimu ya kwenye makaratasi Bali watu, wanapeana connection na marefa ambao bila kuwa na takrima fulani basi utatembea na bahasha miaka yote huku ukijenga urafiki na kazi ambazo ulikuwa ukizikataa mwanzo.
Hivyo kwa upande wa ESTA ni msongo wa mawazo tu unamsumbua huyu akipewa mtaji afanye biashara mbona atatulia huyu?
Lakini Kuna jambo inabidi asaidiwe huyu, ngoja nitamshirikisha mke wangu, nikainuka kuelekea alipo bimkubwa kwakuwa alikuwa akiniita .
Daniel mwanangu kama nilivyokuambia, mkeo kajifungua bila matatizo yoyote, hivyo ni wakati mzuri wa sisi kurejea nyumbani, alisisitiza Mama.
Haaaaa mamaaaa mbona bado?
Mimi nakutegemeeni nyinyi kwa Kila kitu huyu bado hajawa sawa pili huyu dada wa kazi naamini hawezi kummudu mzazi akiwa peke yake,
Naomba ukae kidogo mama, niliongea kwa kumaanisha maana niliona sitakuwa free kabisa nikiwa kazini,
Hapana mwanangu, tumekaa sana pili Mimi najua mkeo Hana tatizo lolote Kuna mambo ambayo sisi huwa tunaangalia yanayotupa tumaini kwa mgonjwa, Mimi niliwahi fanya kazi ya unesi japo Mimi ni darasa la Saba umesahau miaka ile ?
Hivyo nazifahamu hizi kazi sana tu,
Lakini mwanangu huu ni msimu wa kuandaa Mashamba hata baba yako ameshaanza kulaumu, hivyo niache niende nitamwacha dada yako kwa muda mpaka atapotengamaa mkeo japo hapaswi kuchelewa, aliweka kituo.
Sawa mama Mimi nimekuelewa vizuri sana mama.
Nilimaliza mambo yangu huku nikiwa na furaha fulani siku hiyo hasa nikimwangalia ESTA,nikikumbuka ule mchongo wa madam nikaona safi kabisa lazima nipige hela
Kesho asubuhi nilitoa maagizo fulani kwa mke wangu kuwa kwakuwa mama anahitaji kuondoka ningeomba basi baade mida ya saa tisa tuonane mjini .
Nikakubaliana na mke wangu kuwa ESTA kwakuwa ni mzoefu wa mjini atampeleka mama yangu duka lenye nguo za kike hasa watu wazima halafu Mimi nitawafuata baada ya kutoka kazini,
Nilipiga kazi ofisini mida ya saa nane mchana nikapokea simu ya mama kuwa wapo na ESTA kwenye duka fulani maarufu mjini,
Nikafunga vitu vyangu licha ya kuwa ule muda halisi wa kufunga ilikuwa bado nikamuaga meneja kuwa Nina dharula jambo ambalo hakukuwa na tabu,
Nilifika dukani pale , nikatulia zangu nje ya lile duka huku nikimwambia mama Kila kitu kizuri akikiona achague, kweli ikawa hivyo nikaletewa hesabu nikalipa,
Ni mama yangu mzazi ni lazima nimfanyie Kila chema na chenye kumpa faraja.
Wakati nikiwa pale nje hata sijaondoka lilikuja gari fulani la bei ghali sana , nalikumbuka si geni machoni mwangu , akashuka Madam ambaye alikuwa ni Boss wangu wa mwanzo lakini bado alikuwa ni Boss wangu kwakuwa nafanya kazi kwenye ofisi zao.
Tulisalimiana Kisha akazama dukani , kule ambako ESTA na mama mzazi bado wapo wakiwa wanachagua nguo fulani ya ESTA maana mama alinishauri kuwa hatupaswi kumtenga ni mtu kafanya kazi kubwa sana hivyo lazima naye apate zawadi na si yeye tu watu wote wapate yaani familia nzima hasa ukizingatia nyumbani kwangu karibu wote ni wanawake
Nilihisi bajeti itaongezeka lakini acha akina mama waitwe mama, Kila mtu alipata nguo kwa ushauri wa mama huku bajeti ikiwa hata haikufika niliyokuwa nimejiwekea.
Muda kama dakika kumi alitoka Madam akiwa amefurahi sana,
Jamani tolu kumbe huyu ndiye MAMA yetu jamani, nimefurahi sana kumuona MUNGU amlinde jamani,
Aliongea kwa hisia sana ,
Huku kimoyomoyo nikisema siulisema wasikanyage ofisini kwako kipindi nipo mahabusu licha ya kufika hukutaka kuonana nao,
Waliongea wakicheka na kufurahi sana huku nikiwa pembeni natabasamu nikiwaza unafiki wa wanawake hususani kule kukumbatiana Kati ya madam na ESTA.
Eeenhee naona mmekuja kufanya shopping ya nguvu tolu? Aliuliza madam
Ndiyo, ni bimkubwa anasafiri kuelekea mkoani nikaamua nimlete angalau aangalie vitambaa hapa, nilijibu
Sawa Sasa mwambie mama achague nguo anazotaka, wakaingia dukani kwa Mara ya pili huku ESTA akibaki ,akiwa kama hajapendezwa na ujio wa madam pale, just imagine mtu ambaye alikukosea,halafu ana maisha ambayo pengine yangekuwa ni yako, but kila binadamu ana riziki yake pengine isingekuwa hivyo.
Huku mama alitoka na begi jipya kabisa ambalo kanunuliwa na madam mule ndani huku zile pockets za pale dukani zikiwa kama hazina kazi.
Baada ya sisi tumshukuru yeye madam
Akawa anatushukuru sisi akidai ni kama MUNGU tu kamleta pale, tuliagana nikatafuta usafiri binafsi tukaondoka huku nikitambua mama hajafurahishwa na mambo aliyofanyiwa na madam.
Hivi Dani huyu ndiyo boss wako ambaye alikusumbua mwanangu, yaani nimeshindwa hata kukataa hivi vitu lakini ningefanyaje, pia kanipa hii hela mule ndani dukani ni hii shilling laki moja, nimepokea tu maana huyu Binti namuona kama ana wadhifa mkubwa sana, alimalizia Mama.
Mama yanguuu, Mimi natambua Kila kitu ni jinsi gani mmeumia kitendo walichonifanyia Hawa lakini tambueni kuwa nipo kwenye kampuni zao bado, hivi kama Kila kampuni ambayo itatokea migogoro nikaapa kutokufanya kazi nitazisusia kampuni ngapi?
Kikubwa mama mniombee tu , kazi hazipatikani kirahisi lakini pia, matatizo hutokea na lazima nikabiliane nayo,
Wewe hizo zawadi ulizopewa kuwa nazo na amani yaliyotokea tusahau,
Hebu fikiria mke wangu kajifungua na familia ni kubwa ningekuwa Sina kazi ingekuwaje?
Mama alikubaliana na Mimi kwa shingo upande.
Tena Mimi kanipa namba zake za simu eti nimtafute muda wowote, sitaki mazoea naye na hii namba naifuta, alizungumza ESTA tukiwa tunakaribia kushuka.
Kitendo Cha kuonekana wamepeana na namba kilinishtua sana,
Je, ESTA anafuta namba za madam ni kweli, kama ni hivyo sawa, na je kama madam naye anazo za huyu wakaongea wakabembelezana itakuwa sawa lakini mbona kama mpango wangu utavurugika?
Wakisameheana Hawa nitapata hela kweli si watapeana wenyewe, kwanza najuta hata sana kuwakutanisha,
Itakuwaje sehemu ijayo Ina majibu usikose.
Itaendelea.................
Inafundisha San story yakoSEHEMU INAYOFUATA......
Nilitoka nje nikaungane na wale wageni wetu, huku nikiilazimisha furaha ambayo hata sikuwa nayo.
Tuliendelea na ibada huku wale ambao ni viongozi wakiwa wakitoa vijembe vya chini chini,
Jamani ndugu washirika na waamini wa mahali hapa, hebu tuseme kwa pamoja , hii ni jumuiya gani,?
Wote kwa pamoja wakajibu,
Ni ya mtakatifu DANIEL, huku wakishangilia kwa sauti na nguvu sana,
Nikajisemea hapa nasemwa Mimi, lakini nilikuwa Mpole na mtulivu huku nikijikita zaidi kwa wachambuzi mahiri wa biblia, jinsi ambavyo Tunapaswa kumrejesha kondoo aliyepotea.
Baada ya kumaliza ile ibada fupi, huku nikiwa na furaha kuliko mwanzo, kilifuata kikao Cha kutaka nijieleze ni Nini hasa kunanifanya nisipende kwenda kanisani ni takribani miaka miwili Sasa.
Sikuwa na majibu ya kueleweka dhidi ya blah blah tu, ikabidi ESTA atoe tu ushauri kwamba licha ya kuwa yeye alikuwa kwenye dhehebu tufauti ila amependa jinsi waumini wenzangu walivyokuja kwaajili ya kunikumbusha jambo muhimu na la maana kabisa.
Akashauri nipige magoti niombewe ,
Nikafuata Kila nililoambiwa nifanye, kila Jambo likapita wa kuagana tuliagana huku watu wengi wakiwa wanaelekea makwao, kasoro mtu mmoja ESTA aliyekuwa nusu kuondoka nusu kubaki yaani kama ile ibada tungesema tukeshe pengine angefuraji sana.
Haya maisha hayaaaaaahh, yamejaa UNAFIKI sana, Leo hii Hawa waliokuja kutaka nirudi kanisani nikiwachambua mmoja mmoja hakuna aliye msafi, wote wamejaa uchafu Kila kona.
Huyu ESTA mwenyewe Leo hii naye eti yupo kanisa la kiroho, kwa msimamo gani aliokuwa nao , mbona nilimtongoza huyu akakubali, angekuwa mwema, angewaza kutembea na mume wa mtu, Tena mume wa rafiki yake kabisa.halafu historia yake si nimesikia huko makanisani huwa wanawatega wanaume
Hakuna lolote,*********nilitukana kimoyomoyo.
Lakiniiiii,
Sipaswi kumhukumu mtoto wa watu, Huyu ni mwanamke, mtu ambaye Hana kazi mjini, Hana hata biashara yenye mtaji wa elfu kumi, kwanini nimlaumu kwa maamuzi yake, aliamini kuwa akilala na Mimi atapata pesa walau ya kujikimu,Ikamsukuma siku mbili tatu.
Kwanza biblia yenyewe imeweka wazi juu ya udhaifu wa wanawake, sipaswi kumhukumu kwakuwa hakuna binadamu aliyekamilika Mimi mwenyewe Nina chale mbichi kabisa hapa nilipo, MUNGU anisamehe tu.
Nilijiwazia moyoni.
Sasa shemu mi naona niwaache maana naona umejiinamia hata sijui unawaza Nini, alisema ESTA
Hapana shemu ni kawaida tu mbona.
Nilimjibu.
Hapana mume wangu,wewe Leo neno limekuingia vizuri na jumapili ijayo ukumbuke kwenda kanisani,
Alijibu mke wangu Huku wote tukicheka.
Halafu mume wangu huyu ESTA ana shida na wewe ,maana Mimi ameshanielekeza shida yake lakini nikamwambia siwezi kumpa jibu lolote Hadi niongee na wewe.
Ana shida gani,niliuliza.
Mimi naona ni vyema basi nikawapisha muongee halafu utaniambia,mke wangu alionesha kuniamini sana yaani anaingia ndani ananiacha na mwanamke.
Shemu una shida gani,hebu njoo tukae hapa ,nilivunja ukimya.
Shemu,we acha tu maisha nayoishi Mimi ni Sasa na chokoraa maana nimegeuka mbwa koko, ambaye Hana mmiliki kwahiyo Kila anapopita ni kurushiwa mawe ,
Kitu pekee kinachonipa faraja ni kwenda kanisani sehemu pekee ambapo nahisi nasikilizwa,lakini Nako utajikuta unasikilizwa mkiwa hekaluni au ibadani lakini kwenye maisha ya kawaida ni kama Sina rafiki,nikiomba msaada huu nanyimwa nikimtangazia mtu shida Kuna kuwa na uzito wa kupata huo msaada,miezi michache tu hapa nilimpata mchumba pale kanisani ambaye alikuwa tayari kabisa tuoane,
Lakini nilirushiwa maneno,nikatangaziwa vibaya sana mpaka ikafikia hatua nikaambiwa Nina ukimwi yaani wale naosali nao ndiyo waliomshawishi yule mwanaume kuwa haoni nilivyokonda,haoni kuwa nina dalili zote za ukimwi.
Ikabidi yule mwanaume aachane na mpango wetu huku akiniasa nisiwe na mazoea na yeye.
Anaendelea ESTA..........
Nakumbuka Kuna siku nilikutana na yule mwanaume sehemu tu ambayo tulikuwa wawili ikabidi nimuulize kwanini ana sikiliza maneno ya watu kama Hana Imani na Mimi tukapime afya zetu, lakini alinikatalia katakata na kunionya kuwa hawezi kujiaibisha huko mahospital eti sijui anaenda kupima, alinitukana matusi mazito sana Hadi pale alipokuja kutuamlia mwanamke mmoja ambaye sikuwa namfahamu akaniambia twende nyumbani kwangu huku akinibembeleza nisilie wala nisijali na huyo mwanamke ni huyu mkeo.
Aliweka kituo.
Sawa, wewe ESTA nakujua kitambo sana, baadaye ulikuja kupotea ulikuwa wapi? Niliuliza
Mimi bwana nilikuwa na maisha mazuri sana, yule mfanyabiashara wa mbao ambaye nilizaa naye watoto wawili ambao walikufa wakiwa na miezi miwili tu, baada ya hapo upendo Kati yangu na yule mwanaume ukapungua nikaja kugundua kuwa ana uhusiano na rafiki yangu mmoja, ila hayo tuyaache. Alisema kwa sauti ya chini sana na kwa hofu
Nikanote kitu.
Baada ya hapo, nikatoka kuelekea mkoani kwangu(akiutaja huo mkoa)
Nikaifungua biashara fulani ambapo niliishia kufilisika tu, lakini ikatokea bahati ambapo Kuna wakandarasi wa barabara walikuja kutengeneza barabara mkoani kwetu, kwahiyo kukawa na kijana mmoja ambaye alikuwa na hela nyingi sana , akatokea kunipenda sana kiasi Cha kunisaidia mambo mengi kwa kipindi hicho niliweza hata kujenga kibanda kwa wazazi wangu.
Lakini baada ya kazi yao kumalizika alinichukua nije Dar es salaam tuanze maisha ila chaajabu alinibadilikia akanifukuza kwake nikawa natangatanga tu hapa mjini kabla ya ya yule rafiki yangu ambaye alinichukulia bwana wangu wa mwanzo kusikia eti anaye Tena na huyo, nilifikiria sana kwamba kwanini hili jambo la kuporwa wanaume linajirudia sana, ikabidi nirudi mkoani niuze kibanda changu ili nipate pesa ya kujitengeneza na kusafisha nyota.
Kweli nilizunguka kwa waganga wa kienyeji wa kila aina lakini toka hapo na huu uzuri wangu sikufanikiwa kupata bwana mwenye hela kama wale hata baada ya kumgeukia nimroge yule aliyeniibia watu wangu niliambiwa kwa pale nitagonga mwamba hasa kulingana na asili ya kabila na mkoa anaotoka jinsi wanavyosifika kwa ushirikina.
Aliweka kituo.
Pole sana shemu, je ulishawahi kupima afya yako ili ujijue? Niliuliza
Ndiyo, nilipima, Iko hivi baada ya mkeo kunichukua ile siku, alinishauri kuwa kama nimeambukizwa VVU ni vyema nikapime ili nianze dozi mapema,
Binafsi sikuwa na Imani kama nimeathirika , Cha ajabu mkeo akawa analazimisha kuwa ni lazima nipime akidai ananiona nikiwa na dalili zote, hata siku ile ambayo nilitaka kuja kutafakari neno halafu wewe ukawa bize sana, mke wako alisema kuwa lazima nikapime kwakuwa yeye anaziona dalili zote, sikumbishia kwakuwa wengi wape ujue neno likikolezwa na wengi hata Kama la uongo hugeuka kuwa la ukweli..
Tukapanga Mimi na mkeo anisindikize ili tukapime japo nilimwomba twende sehemu isiyokuwa na watu wengi kuogopa macho ya watu.
Tulipendekeza twende kituo Cha afya ambacho ni maarufu sana japo ilikuwa kupima na hela, Mimi sikuwa na chochote hata kumuomba mkeo hela nikaona aibu ,
Nikawa nategemea mpango wa Mimi na wewe ulionambia upo safarini ukishuka tutakutana lodge kabla ya kuona hupatikani, nikaamua kurudi nyumbani,
Kesho yake ilikuwa ni siku ya Mimi na mkeo kwenda hospital lakini nilimkuta akiwa na majonzi kuwa kapata taarifa kuwa wewe una matatizo. Ikabidi nimsindikize mpaka ofisi ulizokuwa unafanyia kazi, nilishtuka kuona kumbe ulikuwa unafanya kazi sehemu nayo ijua vizuri sana, nilishindwa hata kuingia ndani ya geti naamini hata mkeo alishangaa ila sikuwa na namna wala sikumwambia chochote.
Tulirudi huku nikimuaga mkeo njiani nielekee kwangu, baada ya kuwa nimekutana na mbaya wangu ambaye alipata mafanikio ambayo pengine yalikuwa ni yangu
NAMCHUKIA SANA BOSS WAKO
Aliweka kituo
Mara nikamuona house maid yupo mbele yetu,
Shemu unaitwa, nikiangaza macho nani ananiita , nikamuona mama yangu mzazi, akiniita kwa kuashiria vidole akiwa pembeni kabisa,
Eeenhee vipi mama Kuna tatizo, naona si kawaida kuniita ukiwa huku, niliuliza
Hivi we Daniel una akili kweli, hebu angalia saa ni saangapi, yaani ni tabia gani ya kuongea na mwanamke mwingine, kwenye nyumba ya wewe na mkeo, huoni hata aibu,
Aliongea mama kwa sauti ya chini kiukali.
Hapana Mama, kaniruhusu mwenyewe niongee naye,
Hata Kama mwanangu, anaweza kukuruhusu mwenyewe lakini akaja kukubadilikia , sisi wanawake tunajijua wenyewe hebu mruhusu aondoke na wewe ingia ndani, kama masuala yenyewe ndiyo haya Mimi sitakaa hapa sitaki masuala yasiyo ya kinidhamu aliwaka sana MAMA,
Nijaingia ndani, nikagundua kweli mke wangu kanuna.
Nimesikia ukweli wa madam yaani boss wangu wa kike,
Madam anadai anaomba akutane na ESTA amuombe radhi na amsaidie,
Nasikia Leo ukweli wa ESTA
ESTA hataki kusikia Wala kuonana na madam anadai ni mtu aliyemuharibia maisha yake yaani kwake haiwezekani kabisa,
Itaendelea..........
Inafundisha San unaweza mamb yako yaka kwama kutokana na masikitiko ya watu wanaolalamika kuhusu wewSEHEMU INAYOFUATA.........
Nilirudi nyumbani kuungana na familia huku nikitambua hakuna amani ya moja kwa moja,
Ile furaha ya kupokea kiumbe kipya ilitoweka watu walikuwa kimya sana nilisalimia huku mtu pekee aliyekuwa na furaha japo ya kulazimisha ni ESTA, ambaye tayari nilimchukia kwa kiasi fulani.
Daniel mwanangu kabla ya kufanya chochote Nina mazungumzo na wewe,
ni maneno toka kwa mama yangu mzazi
Kwanza mwanangu pole kwa misukosuko na mengi yanayokukabili, watu wote hapa tumeungana kwenye hii familia si kwa kuja kula Raha Bali ni visa na mikasa vimetuunganisha.
Kila mmoja anatambua Nini kimetutoa mkoani kuja hapa, labda nikukumbushe tu kuwa kwenye maisha Kuna mikosi, na mwanangu mikosi ilikutembelea, ukawekwa mahabusu, naamini ulihitaji dhamana kutoka kwa watu wenye uchungu na wewe , hebu kumbuka una marafiki na maswahiba wangapi hapa mjini,hawakukusaidia
Na je, unawezaje kutofautisha nyakati mwanangu au unaishi tu, mwanangu hii ni Dunia,
Nimekuja kutoka mkoani Mimi na dada yako siyo kwamba tulikuwa na uwezo wa kukutoa mahabusu sisi kwenye hii Dunia ya kisasa iliyojaa rushwa , hapana,.ni upendo tu
Unadhani Mimi au dada yako hata mkeo nani angeweza kukunasua kwenye ule mtego wa matajiri wenye pesa wanaoweza kukufanya chochote kile,
Sisi kazi yetu ilikuwa ni moja tu kukuonesha UPENDO tu, mwanangu unatambua kuwa sisi wazazi wako ni maskini si matajiri, tunakutegemea kwenye mambo mengi, unadhani tungekusaidia Nini kwenye kesi yako.
Naomba utambue nafasi aliyocheza mke wako kipindi una matatizo ni sehemu pekee ya kutambua thamani yake kwako, sisemi kuwa hakukosei, najua anakukwaza kwa mambo mengi lakini Mimi kama mama yenu na mama yako mzazi nakuombea na kukukumbusha kuwa makini.usipende kuweka msimamo Kila sehemu mengine yapuuze
Nachoweza kushukuru ni kwamba mkeo kajifungua salama na maendeleo yake yanaridhisha sana tu kwahiyo hatuna Cha kutuweka hapa kwako ni kwamba tuna masaa machache ya kurudi nyumbani mkoani maana ulituomba tukae kwaajili ya mgonjwa hatimaye MUNGU kajalia na kutia wepesi.
Lakini mwanangu nikuulize swali moja ulikuwa na maana gani kumkoromea mkeo?
Mtu ambaye anahitaji UPENDO wa dhati toka kwa mumewe hasa kipindi kama hiki alichojifungua,? Alimalizia Mama kwa mfumo wa swali.
Nikamjibu,
Kiukweli Mama wewe mwenyewe kwa siku ulizokaa hapa , umegundua ni jinsi gani huyu ESTA anavyokuwa karibu na mke wangu, Sasa iweje ujio wake uwe msala kwangu Mimi, kifupi mke wangu kanikera sana.nilimalizia
Sawa mwanangu, naomba utambue kuwa humu ñdani watu wote ni wanawake, hebu jitofautishe basi Dani, hebu jaribu kudharau baadhi ya vitu visivyokuwa na umuhimu , ni aibu kubwa Mimi nianze kuwasuluhisha nyinyi katika kipindi ambacho mkeo katoka kuponea kwenye tundu la sindano,
Yaani ilikuwa ni wakati wa wewe na mkeo kukaa na kuanza kupendekeza jina la mtoto ataitwa nani na siyo kutengeneza malumbano.
Aliweka kituo.
Nilimwelewa sana mama nikaingia chumba fulani ambacho huwa hakitumiki nikamkuta mke wangu akiwa na furaha tu anachezacheza na mtoto tofauti na nilivyofikiri baada yakuona watu wengine kule nje wamenuna nuna yeye alikuwa poa kabisa tulisalimiana nikampa pole huku tukitaniana baadhi ya vitu.
Oooh hiki kipindi kigumu, Mara ooh umeshikaje ujauzito Mimi Sina kazi, Sasa nimemleta huyo hapo mkatae Sasa, alitania mke wangu.
Weee nimkatae, kwanza hii jinsia nilikuwa naisubiri kwa hamu, yaani nataka siku moja kama nitakuwa hai niende pale airport nimuone akishuka kwenye ile midege ya Emirates huku akiwa nadhifu na Yale mavazi yao,
Halafu kwa makusudi nimwambie mbona simu yako haikuwa hewani,nilitania
Wewe mwanangu sitaki awe rubani , huyu atakuwa daktari bingwa nikwambie, alisema mke wangu Huku tukitaniana mambo mengi, ambapo nilifurahi sana,
Maana timbwili nililokuwa nimepanga kufanya nilijikuta nasutwa tu moyoni mwangu ila nikashukuru kama mambo yamekuwa sawa , najua atakuwa kamshitakia mama,
Na bimkubwa navyomjua atakuwa kaniponda weee ili ampe ushindi huyu , bimkubwa hajawahi niangusha kwenye kumbembeleza mtu
Baada ya kupata ile amani ya moyo sikutaka kuzungumzia habari za ESTA muda huo ili kuepusha Shari.
Nilitoka nje kucheki mazingira nikamuona ESTA akiwa anajituma anafua nguo za mke wangu akisaidiana na dada yangu, nilimuhurumia sana , Kuna wakati baada ya kukwazana na mke wangu kwenye simu nilimuona huyu ndiyo chanzo , nikapanga nije nimtimue lakini maisha acha yaitwe maisha
Kama tu Mimi mwanaume nilipigika Hadi nikawa nauza vitu vyangu kipindi fulani itakuwa kwa huyu mwanamke?
Kumbe atafanyaje, ajiuze, Bora kaja kuomba msaada sishindwi kuishi naye tatizo lipo kwa mke wangu lakini pia si madam karidhia tumfungulie biashara?
Kwanza ngoja, Kila kitu kitakaa sawa.
Kaka vipi mbona unaizunguka nyumba kama unaizindika vipi, alitania dada yangu,
Hapana nilikuwa huko nyuma naangalia mahali pa kumwaga tofali nahitaji kuijenga fence.
Ahaaa safi my brother, tunakuombea kwa MUNGU Kila kitu kiwe poa,naona nyumba itapendeza sana
Alijibu
Wakati tunaongea hayo nilipokea simu namba ngeni,nikaiweka sikioni
Habari kaka,za siku nyingi Mimi ni Shedy,
Kwanza nilibadilika, maana sikupenda mazoea Tena na huyu mshikaji,
Unasemaje, niliuliza
Aisee kaka jaribu kusahau yaliyopita Mimi na wewe ni ndugu kabisa unajua tulipotoka, nina mazungumzo na wewe kaka, aliongea kwa tahadhari.
Ongea nakusikiliza,
Sawa ni hivi ,mwenzio baada ya kukuta biashara inayumba na zile shughuli zangu zimekuwa ngumu nilikopa hela kwenye benki ya(akiitaja hii benki maarufu nchini)
Ni kutokana na shughuli zetu kuwa ngumu yaani udalali kwangu umenikataa kabisa, nikaona nikope hela ili niiboost biashara yangu, lakini mambo yamekuwa tofauti sana
Kwanza Kuna mtu hapa kafungua bar ya kisasa ni Mara tatu ya hii yangu kama ujuavyo kipya kinyemi yaani mwezi wa tatu Sasa wateja wangu maarufu anao yeye.
Hebu fikiria Kuna muda nauza kreti moja tu la bia huku vile vikali huuzi kabisa na wahudumu niliokuwa nao wanaihitaji pesa yao kama kawaida yaani ni hasara juu ya hasara , huku wafanyakazi Mara biashara haiendi jumlisha riba, nitatoka kweli kaka.
Aliongea kwa uchungu wa kujipendekeza.
Sasa hayo ni maisha yako, Mimi nahusika vipi, nilijibu
Hapana kaka, Mimi shida yangu ni moja nataka unisaidie, ni kwamba Kuna mwanamke anaitwa ESTA naamini unamfahamu vyema sana yule Mimi namtafuta sana, ni kwamba yule Kuna kipindi alikuwa mpenzi wangu wa Siri, Sasa wakati wa mapenzi yetu alikuwa na kiasi fulani Cha hela , nikamzuga kwamba aniazime niingize kwenye biashara yangu alikubali, baadaye niwe mkweli baada ya kuwa nishamchoka sihitaji kuendelea naye,
Nilimwambia aangalie ustaarabu mwingine , ndipo alipoamua nimpe hela yake kwanza ndipo tuachane lakini nilimtishia kuwa Hana hela kwangu na nitamshitaki, hakuwa na la kufanya ukizingatia pesa zaidi ya milioni tatu tulipeana bila ushahidi wowote,
Aliweka kituo.
Sikia Shedy unanidharau sana kwamba nikutafutue ESTA hapohapo unanipa mkasa wako wa kimalaya,kumbe ndio tabia yako kutembea na wanawake na kuwadhulumu,kwa mfano ukimpata unataka umfanye Nini,niliuliza safari hii ni kwa ukali,
Ni hivi kaka lengo nimuombe msamaha na naahidi kuwa nitamlipa mbele ya ushahidi kwasababu, kila nikizunguka kwa wataalamu Wananiambia Kuna mtu Ana masikitiko juu yangu,ndiyo maana biashara yangu inayumba.alimalizia
Cha kukwambia ni kuwa Sina mahali ambapo nitampata huyu ESTA kwahiyo wewe fanya mambo yako Mimi Hilo lipo nje ya uwezo wangu,nikakata simu.
Mapya haya kwangu,yaani Shedy mjinga sana,na habari zake za kishirikina,
Eti ananiambia kuwa biashara haiendi kwasababu ya masikitiko ya mtu,wakati anajua wazi Kuna biashara mpya kama yake Tena imekuja kisasa halafu bado unatafuta mchawi,
Ni sawa na bus jipya na la zamani route ile ile na nauli ni moja nani atachagua la zamani,?
Kweli nimeamini ushirikina ukizidi na akili inapungua ,
Lakini huyu ESTA naye kumbe mjinga eeh kweli alirogwa akarogeka na kukorogeka , unawezaje kutoa zaidi ya milioni tatu kumpa mwanaume Tena Ukiwa ni maskini,akijifanya Ana mapenzi ya kizungu huu si ulofa huu
Ndiyo maana Kila nikimuuliza baada ya kuuza kibanda chako mkoani kwenu hela ulifanyia Nini haeleweki huyu , niliwaza sana jinsi binadamu tulivyo tofautiana .
Nikarudi ndani huku nikisearch kampuni fulani ya uuzaji wa magari used wakidai bidhaa zao ni Bora sana licha ya kuwa zimetumika nikawa napoteza muda pale,
Mke wangu akavunja ukimya,
Samahani sana mume wangu, kwa Yale tuliyoongea mchana ila tufanye yamepita,
Hivi mume wangu ukimwangalia ESTA kwa ukaribu unadhani ana akili timamu?
Kwanini umeuliza hivyo, mke wangu,ni kwasababu kaja kukaa hapa?
Hapana,
Nahisi Kuna jambo linamsumbua tujaribu kusaidia.
Mke wangu aligundua Nini kwa ESTA?
Nani kampa huo ufahamu kiasi Cha yeye kuwa Mpole na mwenye huruma ?
Itaendelea.....................
Mwanzo nillikuaa naipuuza hi story kumbe Ni nzur na inauahalisia Kia's na mafundisho sanaINAYOFUATA..........
Tulifika nyumbani, mke wangu akitoka chumbani kuja kutupokea pale sebuleni,
Vipi kamanda wangu anasemaje, niliulizia maendeleo ya mtoto wetu mchanga.
Kalala muda mwingi sana mbona, huku furaha zikizidi pale ukumbini baada ya watu kuwa wanapeana surprise mbalimbali, nikaacha nikaingia chumbani kwangu, na kuelekea bafuni.
Siku iliyofuata saa kumi na mbili asubuhi Mimi na mama ilitukuta ubungo stendi kuu ya mkoa kipindi hicho tukiwa tumeshikilia tiketi huku nikisomasoma zile siti kuhakikisha mama anakaa siti husika asije kusumbuliwa baadaye na watu wengine nilizugazuga pale Hadi pale nilipohakikisha gari imeingia Morogoro road huku tukipungiana mkono na bimkubwa nikimtakia safari njema.
Niliishika barabara ya Mandela road kurudi nyumbani kwakuwa ile siku haikuwa ya kazini basi nilitulia nyumbani huku nikifanya kazi ndogo ndogo ikiwemo kutatua mgogoro fulani wa majirani ambao walikuwa wakinisubiri kwa hamu Mimi nikiwa kama shahidi wa kile kiwanja ,
Huku ikiwa kila baada ya lisaa nampigia mama kujua alipo.
Oyaa Mr Daniel Kuna mwanamke yupo pale kwako ni mrefu hivi mweupe, unamwitaje yule, aliuliza yule jamaa ambaye ametoka kushinda ule mgogoro baada ya Mimi kumsaidia beacon zilipo,
Yule anaitwa ESTA, vivi kaka umemwelewa Nini?
Niliuliza,.
Bado tu hujanijibu Dani, nataka kujua uhusiano wenu, ni dada yako, ni shemeji yako au ni nani tako?
Aliongea jamaa,
Hapana yule Hana undugu kabisa na Mimi Wala mke wangu Bali ni rafiki tu wa mke wangu kaja kumsaidia wife baada ya kuwa kajifungua, nilimjibu
Basi sawa , anavutia sana yule mwanamke kifupi natamani hata ningepata namba zake za simu niwe nawasiliana naye, aliongea jamaa ambaye hakuwa akitania,namjua ana hela sana hivyo inawezekana ESTA akapata bahati kuwa na jamaa.
Lakini kaka we si una mke lakini , nilimtania,
Kwanza Mimi Dini yangu inaruhusu Dani, jua Hilo halafu lingine kama labda ni mbadala wa mkeo kwenye hiki kipindi anacholea niambie Mr,
Aliongea jamaa huku akiingia kwenye gari lake,
Hapana kaka yule Mimi naheshimiana naye sana tu siwezi hata kumtongoza ujue, au nikuitie kabisa maana yule ni mtu mzima mnaweza kuyajenga we vipi bwanaaaa, niliongea tukacheka.
Sawa Mr Daniel, Mimi nawahi Leo Nina wageni ofisini kwangu, aliongea huyu jamaa ambaye aliwahi kumiliki duka la pembejeo za kilimo na mifugo miaka ile na Sasa ana miliki kampuni ya ulinzi mjini. Aliwasha gari akaondoka, kitu pekee nilichofurahi ni kusahau kuchukua namba ya ESTA,
Sikutaka apate namba ya ESTA, kwasababu,
Kama ESTA akipata bwana wanguvu kwasasa ni ngumu Mimi kumshawishi aelewane na madam, atakuwa kapata pa kuegemea ni ngumu sana kumshawishi
Na huyu jamaa ni ana pesa ni rahisi kumbadilisha ESTA kwa muda mfupi sana, ngoja nitaongea na mke wangu jambo
Nikarudi nyumbani nikamkuta mke wangu anazungumza na dada yangu nikamuomba tuongee jambo akaja chumbani,
Yaani mume wangu hata hupumziki yaani hata weekend kama hii wewe ni wa kwenda mitaani tu? Mimi unanikera sana ujue, aliongea kwa kumaanisha
Lakini haikunisumbua ni kawaida yeye kuwa na wivu na Mimi hasa kipindi hiki akiwa mbichi nilimpoza maisha yakaendelea,
Sasa mke wangu nilitaka kuongea na wewe jambo kuhusu ESTA , naamini alikusimulia Kila kitu kuhusu matukio yake ya nyuma Kati ya yeye na aliye kuwa boss wangu,
Ndiyo najua si anadai hataki hata mawasiliano naye si eti? Aliuliza
Eeeh Sasa unafikiri atakaa hapa Hadi muda gani , mke wangu?
Kwahiyo ulitakaje mume wangu maana ndiyo tushapata mgeni mume wangu.
Sasa yule mbaya wake yeye hana neno kabisa Tena kapanga kama ESTA atakubali atampa hata mtaji Tena kima Cha kuanzia ni milioni tano Sasa yeye hataki,
Haaaaa kumbe huyu dada ni mjinga eh unaikataaje milioni tano ikiwa maisha yako ni mabaya namna hii, alidakia mke wangu bila hata kujua mambo yanapangwaje.
Nisikilize mke wangu , ni hivi kwanza ESTA hajajua kuwa atapewa hicho kiasi, pili Mimi Nina mpango fulani wa kuweza kupata hela kwa madam kupitia huyu ESTA, maana ubaya ubaya tu walinitesa sana hawa lazima nijifanye namsaidia ESTA ili tu niweze kujipatia hela ambazo naziona zitakuwa ni za Kila Mara yaani, wewe unaemaje mke wangu.
Mume wangu mi naona Kama si vizuri kujipatia hela kwa njia ya utapeli huyo boss wako akijua , na ESTA akijua kuwa umemgeuza chumio atakuonaje,
Utajishushia heshima mume wangu, kwanza Mimi najivunia kabisa kuwa na mwanaume kama wewe , hivyo kwa ulivyo sijategemea kuwa na mawazo kama haya wewe kama unamsaidia ESTA msaidie tu, muunganishe na huyo madam ili wakipatana utabarikiwa sana maana
Kwenye biblia kumeandikwa,
Heri wale wapatanishi
Sasa ikiwa wewe utapatanisha watu kwa masilahi yako binafsi sioni kama inapendeza kwa kweli mume wangu, alisisitiza mke wangu.
Nilijiona nimetoa pasi mbovu kuwa kwanini nimemshirikisha , huyu yeye ni mtu wa kuletewa tu, Kila kitu kinanihusu Mimi hivi anadhani bila mipango ya pesa kwenye vyanzo vingi hii itakuwaje,
Ukiambiwa mjini akili ndiyo haya nayomweleza, Sasa kwanini anapinga?
Niliwaza huku nikijilaumu kumshirikisha, Sasa ataniona Mimi nani nitahakikisha napiga hela bila yeye kujua Wala ESTA mwenyewe kujua,
Sawa mke wangu Mimi wewe ndiyo katibu wangu kwenye hii nyumba kwahiyo naheshimu mtazamo wako MAMA, niliongea ili nimridhishe tu lakini mpango wangu ulikuwa pale pale , hawezi kunipangia huyu hajui tunavyohenyeka.
Saa kumi na moja nikapokea simu kutoka kwa mama akiwa ananitaarifu kuwa amefika salama salimini, nikafurahi sana, nikaona huu ni muda wa kuongea na ESTA jambo.
Nikamuita nikiwa na dada yangu, sikutaka tuwe wawili tu hapana isije mke wangu akahisi vibaya tena
Tukakaa nje, huku nikivunja ukimya lengo nimuulize maswali fulani nijue ana mipango gani?
Samahani shemeji, kwa kuwakatisha shughuli zenu ambazo mlikuwa mkifanya, lengo langu nataka kujua kuwa una mipango gani , maana Kuna mchongo huko mjini nimeupata ila nilikuwa naogopa kukweleza maana isije kuwa una mawazo yako mengine,
Akadakia, niwe na mpango gani masikini Mimi, we shemu kama Kuna maisha sehemu yanapatukana we usisite kuniambia, natamani niwe hata kwenye kibarua fulani maana haya nayoishi siyo maisha kabisa,
Aliongea kwa sauti ya kukwaruza huku akijizuia kulia nikajisemea hapa nimeshinda,.
Najua jumatatu nitazunguza vipi na madam, nilijisemea moyoni
Mke wangu hawezi nipangia jinsi ya kutafuta hela yeye atulie tu atakachotaka atapewa.
Jumatatu ilifika kama kawaida yangu muda wa kula nilitoka nje lengo nipate na nafasi ya kuongea na simu kwa kirefu maana mule ndani Kila dakika mtu anagonga lakini pia maboss hawapendi sana mfanyakazi kuongea na simu binafsi.
Nikatoka nje ya fence nikampigia MADAM
Eeh tolu nambie nimeona kimya tangu ile majuzi, lakini pia ESTA nilimpa namba yangu anitafute vipi mbona amekuwa mkimya?
Mimi kwa kweli sijui,ila nikirudi nitamuuliza mbona hajakutafuta,nilijibu kiuongo huku nikijua ESTA hataki mawasiliano na madam.
Sikia tolu huyo achana naye twende taratibu mbembeleze ,huku ukijifanya unamtafutia biashara fulani afanye kama tulivyokubaliana, alimalizia.
Nikaona siyo muda nitakuwa mshindi,tulimaliza kuongea na madam nikampigia simu ESTA nikimsisitiza akae pembeni,
Shemu bwana nimefikiria
Jambo fulani kuhusu tuliyoongea nimeona tutafute frem ili ufungue hata ya kuuza urembo tu, labda wewe unapendekeza Nini, niliuliza
Waooh shemu kwanza nakushuru kwa kuendelea kunipigania , Mimi shemu biashara ya haraka haraka hapa kwangu kama Kuna uwezekano ni saloon ya kike, hiyo kwangu naiweza na naijua vyema nimekuwa nikipita kwenye saloon za wenzangu kuomba kazi ya ususi , kwa malipo ya chini sana lakini kama nitapata ofisi yangu nitafurahi sana,
Labda kwakuwa sijajua bajeti yako aliweka kituo
Kwani Nini kinatakiwa kwenye hiyo biashara?niliuliza
Sawa kwanza inatakiwa tupate sehemu yenye mzunguko wa watu wengi, Ila siyo mjini kule mafremu ni gharama, kwahiyo tukipata frem ambalo liko kwenye V au junction itakuwa poa sana shemu,
Kuhusu frem usijali,vipi kuhusu bajeti ya vitendea kazi, niliuliza.
Hapo shemu panakuwa pagumu kwakuwa sijui mfuko wako
Ila ukiondoa hela ya frem hela ya vifaa kwa kukadiria ni kama milion moja na nusu, hapo kila kitu kitakuwa sawa.aliweka kituo
Shemu milioni na nusu mbona ndogo labda Kama unafungua biashara
hiyo kijijini, niliongeza
Kwani shemu ulikuwa na kiasi gani, aliuliza kwa pupa.
Ipo kama kama milion tatu hivi . nilimjibu
Ahsante sana shemu, sikutegemea kabisa kweli MUNGU anaweza acha MUNGU aitwe MUNGU, aliongea kwa hisia sana ,
Yaani hapo kila kitu nitaweka nitahakikisha hata kama ni sehemu ndogo lakini iwe ya kisasa,
Japo ya kiswahili
Inaonekana hiyo biashara unaijua vizuri sana shemu, niliuliza
Naijua vizuri sana, ni kwakuwa kwanza Nina sura ya mauzo kitu ambacho ni point namba moja kwenye biashara.
Nikajiuliza hao anaowasuka watakuwa ni wanawake wenzie sura yake nzuri itahusika vipi ingekuwa ni saloon anahudumia wanaume sawa, ila namwachia mwenyewe,
Tafadhali shemu hakikisha mke wangu hapati hii taarifa maana isije kuwa matatizo baadaye, nilionya kwa tahadhari.
Shemu, najielewa, nakuelewa wewe, pia namuelewa mke wako hivyo kuwa na amani kabisa, labda wewe ndiyo umwambie.
Nikakata simu huku nikiwa nimepanga kumtafuta MADAM kesho yake ili mipango ya hela/pesa ifanyike
Nilirudi nyumbani, nikaikuta familia ikiwa na amani ya kutosha, lakini ESTA alikuwa na furaha kuliko mtu yoyote mle ñdani.
ESTA anafurahi baada ya kuahidiwa kutengenezewa kijiofisi Cha kuzugia,
Mimi namuahidi hela ambayo sijaitia mikononi mwangu, je jambo hili litafanikiwa ?
Vipi kuhusu mke wangu akigundua.?
Usikose kufuatilia mambo mazuri yanakuja.
Itaendelea.....,?!:"":!
Ni nzuri mkuu tena sana.Mwanzo nillikuaa naipuuza hi story kumbe Ni nzur na inauahalisia Kia's na mafundisho sana