Simulizi: Mchawi

Simulizi: Mchawi

Hii ipo yote kabla sijaanza kuisoma?? Nisije kubaki na arosto.....
 
SEHEMU YA MWISHOOO.

Kwa vile tulikuwa hatujala toka asubuhi tulishambulia chakula chote. Baada ya chakula tulioneshwa sehemu ya kupumzika kwa vile muda ulikuwa umekwenda sana. Kutokana na uchovu wa safari tulilala mpaka siku ya pili.
****

Siku baada ya kupatiwa kifungua kinywa cha uji wa maziwa na viazi, tuliitwa kilingeni, baada ya kukaribishwa na kukaa kwenye ngozi ya chui mzee Ngugude alichukua ungo na kuuweka mbele yetu ndani ya ungo kulikuwa na ndizi saba.

Mbili zilikuwa zimeoza, mbili zilikuwa zimeiva sana na kuanza kubadilika rangi na kuingia weusi kwa mbali na mbili zilikuwa zimeanza kuiva na moja ilikuwa mbichi kabisa.

“Unaziona ndizi hizi?” aliniuliza huku akinisogezea ungo mbele yangu.
“Ndiyo mzee wangu,” nilijibu huku nikizitumbulia macho.

“Umegundua nini?”
“Sijagundua kitu,” nilisema huku nikitikisa kichwa kusisitiza sijui.
“Basi hii ndiyo familia yako.”
“Familia yangu?” nilishtuka kidogo, japokuwa sikumwelewa.

“Ndiyo.”
“Una maanisha nini kusema hii ndiyo familia yangu?”
“Ulipokwenda kwa mganga alikueleza nini kuhusiana na ndizi?”
“Alisema familia yangu imetegewa uhai wake kwenye ndizi.”

“Basi ndizi zenyewe ndizo hizi, nimefanya kazi kubwa kuzivuta, kwa kweli kazi hii ilikuwa ngumu, ngumu sana. Nimekesha kwa kazi hii lakini nimefanikiwa. Kabla ya kufanya kitu chochote nilitaka uone ili niifanye hii kazi.”

“Kwa hiyo hapa panakuwaje?”
“Kazi iliyopo ni kuitoa sumu katika ndizi ili kuyafanya maisha ya familia yako yaondokane na uchawi uliotegwa kwenye ndizi.”
“Sawa mzee.”
“Unaona ndizi hizi mbili zilizooza?”
“Ndiyo.”

“Basi hizi ndizi, ndiyo baba yako na mwanao waliofariki, na hizi zilizoiva sana?”
“Ndiyo naziona.”
“Hizi ndiyo mkeo na mama yako, si unaona zilikuwa zikiendelea kuiva.”
“Ndiyo.”

“Basi zingeoza lazima ungepoteza watu wawili kwa mpigo japo ingechukua muda kutokana na kinga uliyopewa mwisho, hizi zilizoanza kuiva?”

“Ndiyo naziona.”
“Hizi ndizo wanao waliobakia, nao walikuwa wakiiva taratibu japo wasingedondoka, lakini wangeoza na kufa kwa mpigo.”

“Mungu wangu!” nilishika kichwa.
“Usishike kichwa hapa nakuonesha ubaya wa kisasi, ungeweza kufanikiwa kuongeza idadi ya vifo vya watu, lakini matokeo yake yalikuwa haya, ungeipoteza familia yako na wewe kuwa chizi,”
“Na hii ndizi mbichi?”
“Hii ndiyo wewe, ukweli walikushindwa na kukubali wameshindwa. Unaiona hii ndizi pembeni?”

“Ndiyo.”
“Unaona nini?”
“Kuna mistari mweusi kama chale.”
“Basi haya ni makombora yaliyotumwa kukuozesha. Lakini mwili wako umekuwa imara kinga iliyofanyika chini ya mti mkuu ndiyo iliyokulinda.

Kinga yako ingekuwa ya kawaida ya kuchanjwa tu ungebakia jina.”
“Sasa mzee wangu utanisaidiaje?”
“Kuhamisha sumu toka kwenye miili ya familia yako huku ukiona mwenyewe kwa macho yako.”

Alichukua ndizi mbichi nne na kuziweka kwenye ungo mwingine kisha alichukua dawa ya unga mweupe na kuzimwagia zile ndizi taratibu huku akinuiza maneno anayoyajua mwenyewe. Baada ya muda aliweka ungo wenye ndizi mbichi pembeni ya ungo wenye ndizi alizosema ndiyo familia yangu.

“Unauona ungo huu?”
“Ndiyo.”
“Una nini?”
“Una ndizi mbichi.”
“Ngapi?”
“Nne.”
“Vizuri,” alisema huku akichukua ndizi zilizooza na kuzitupa pembeni na ndizi mbichi akiiweka kwenye kikapu.
“Sasa nataka hizi ndizi ziwe kama hizi na hizi ziwe kama hizi.”

“Sawa mzee wangu.”
Aliuchukua ungo wenye ndizi mbichi na kuuweka pembeni ya ungo wenye ndizi zilizoiva na kutulia.

“Naomba macho yako yasicheze mbali asijesema nimebadili ndizi.”
Nilitumbulia macho ungo wenye ndizi mbichi, kila dakika nilishindwa kuelewa ghafla nilijikuta nikichanganyikiwa baada ya kuona ndizi zimebadilika na kuhamia ungo mwingine.
“Umeona nini?” mzee Ngugude aliniuliza.

“Sielewi.”
“Huelewi nini?”
“Naona kama ndizi zimehamia huku.”
“Hapana hazijahama bali sumu nimeitoa na sasa ndizi zilizokuwa ungo huu zimerudi katika hali ya ubichi.”
“Kwa hiyo.”

“Ubichi huo ni uhai. sasa hivi vifo katika familia yako vitatokea kwa amri ya Mungu na si mkono wa mtu.”
Baada ya kusema vile, alichukua unga mweupe na kunyunyizia. Alipomaliza alinieleza niende kuoga maji yaliyokuwa na dawa ili kuondoa mikosi ili nijiandae na safari.

Nilifanya kama alivyonielekeza baada ya kumaliza zoezi lile, alinipa unga mweupe aliyonieleza nibuye kidogo na mwingine niupulize kama kusafisha njia. Nilifanya kama alivyonielekeza kwa kubuya unga kidogo, unga ulikuwa na ladha kama unga wa ngano. Nilipoliza tulipewa ruksa ya kurudi nyumbani Tanzania.

Tulisafiri salama mpaka Mtwara na kuagana na mkalimani wangu ambaye nilimlipa kiasi tulichokubaliana, kutokana na kazi kubwa aliyofanya nilimuongeza kiasi kingine kama asante.

Kwa vile tulifika jioni sikutaka kulala pale Namoto nilikwenda kulala Mtwara mjini ili siku ya pili niondoke na mabasi ya asubuhi.
Siku ya pili asubuhi nilipanda basi kurudi Dar ili niunganishe mpaka nyumbani siku ileile.

Nikiwa ndani ya basi bado nilikuwa na maswali kuhusiana na maneno ya mzee Ngugude, niliyaona kama yanajichanganya. Kuna wakati aliniambia anaweza kuua na kuna wakati alisema hajawahi kuua kwa kweli maneno yale yalinishtua na kuona kama uwezo wa yule mzee ni mdogo tofauti na sifa zake.

Moyoni niliamini kama ningemkuta bi Nyangunda ningeweza kuwakomesha wabaya wangu. Pamoja na kukubaliana na yule mganga niliamini bado nilitakiwa kwenda ndani zaidi. Nilifika Dar jioni na kunganisha safari na kufika nyumbani saa tano usiku.

Nilipofika nyumbani nyumba ilikuwa kimya kuonesha wamelala. Nilipogonga mlango nilifuatwa na mke wa jirani yetu aliyenieleza kitu cha kushtushwa kwamba watoto wangu wako kwake. Niliulizia mama yao yupo wapi, niliambiwa yupo hospitali pamoja na mama yangu wapo chumba cha wagonjwa mahututi (ICU).

“Mungu wangu tatizo nini?”
“Jana waliugua ghafla, kwa kweli hata hatujui ule ni ugonjwa gani.”
“Wapo kwenye hali gani?” niliuliza macho yamenitoka pima.
“Tumuombe Mungu tu hata sijui niseme nini toka jana hatujafanikiwa kuwaona,” alisema kwa sauti ya huzuni.

Nilibakia nimesimama kwa dakika tano nisijue nifanye nini. Bila kujielewa nilijikuta nimekaa chini bila kupenda huku nikiwa na mawazo mengi kuhusiana hali ile ya kufikia mke na mzazi wangu kurudiwa tena na tatizo.

Wasiwasi wangu mkubwa ulikuwa huenda mabadiliko ya mzee Ngugude ya ndizi ndiyo yaliyosababisha yote yale. Bila kuongeza neno nilinyanyuka mzimamzima ilipokuwa nimekaa na kukimbilia hospitali.

Nilikwenda moja kwa moja hadi hospitali kwenye wadi ya Wagonjwa mahututi na kuelezwa wametolewa na kurudishwa wadini ya kawaida. Nilipotaka kuwaona nilikatazwa na kuelezwa nirudi kesho yake kwa vile muda ulikuwa umekwenda sana hivyo wagonjwa kwa muda ule hawakutakiwa kuamshwa.

Kauli ile sikukubaliana nayo nilijua ni kunifariji lakini mama na mke wangu walikuwa amekufa. Nilijikuta nikiangua kilio mbele ya daktari wa zamu na wauguzi kitu kilichowafanya wanishangae.
“Sasa unalia nini wakati tumekueleza uje kesho?” daktari wa zamu aliniuliza huku akionesha kunishangaa.

“Nije kesho kufanya nini ikiwa mama na mke wangu wameisha kufa?”
“Jamani mbona haya makubwa! Tumekwambia wapo salama ila sasa hivi wamelala. Kutokana na hali waliyokuja nayo ya nusu wafu tumewaacha kuangalia afya zao kwanza, bila hivyo ungewakuta nyumbani.”

“Si kweli, wamekufa ila mnanificha,” niliendelea kulia huku nimekaa chini.
“Kaka hakuna aliyekufa hebu ngoja tukawaamshe uwaone ili uridhike japokuwa si sheria kumuamsha mgonjwa aliyetulia kwa ajili ya mtu kumuona tu.”

Kauli ile ilinifanya ninyamaze kidogo, baada ya muda niliitwa na kuingia wadini. Sikuamini nilikutana na mama na mke wangu wapo kwenye hali nzuri kabisa.
“Umeamini?” daktari aliniuliza.

“Hapa nimeamini, mara nyingi mtu akiingia ICU huwa hatoki salama.”
“Haya baba waache wagonjwa wapumzike njoo kesho.”

Niliagana na wagonjwa wangu na kurudi nyumbani nikiwa na maswali mengi kuhusiana hali iliyowatokea. Nilikumbuka kitu maneno niliyoelezwa na mzee Ngugude kuwa kuna hali itatokea na kuwatisha watu lakini ni ya kawaida ni ya kuyabadili mauti kurudi katika uhai.
Mwanzo sikuelewa kutokana na kuchanganyikiwa, niliamini nilichoelezwa ndicho kilichotokea.

Baada ya siku mbili walitoka hospitali wakiwa wazima wa afya. Kitendo kile kilinifanya nibadili mawazo na kuona hakuna haja ya kuendeleza vita ya kisasi. Niliyakumbuka maneno ya marehemu baba kuwa hakuna mwanadamu mwenye uwezo kama Mungu hivyo tulitakiwa kumuabudu yeye.

Alinieleza kwa dini yake kisasi ni haki lakini kusamehe ni bora zaidi. Niliamini ule ulikuwa wakati wa mimi kujikabidhi kwa muumba ili nizaliwe upya. Niliendelea na shughuli zangu kama kawaida huku nikiwa nimejifunza vitu vingi katika maisha yangu.

Niliamini hakuna vita ndogo pia moto hauzimwi na mafuta. Siku zote tulihusiwa kusamehe ili kurudisha amani, pia unapolipa jema kwa baya, ubaya hukosa nafasi lakini ukilipa baya kwa baya vita yake haina mwisho.

Nilijifunza kitu kimoja kikubwa kuhusu mwanadamu kuingilia kazi ya Mungu, kuua ni kazi ya Mungu kuingilia kazi hiyo ni kujiingiza kwenye dhambi ya kujitakia. Uwezo wa kuumba na kuua ni wake yeye peke yake.

Hata unayemuua ukimwacha lazima atakufa tu kwa nini umuue?
Nina imani wengi mmesoma mkasa wangu tokea mwanzo mpaka leo nilipofikia tamati, napenda kuwaomba wote tusikimbilie kuua au kumroga mtu kwa ajili ya mwanamke kwa vile mke au mume bora hutoka kwa Mungu si kwa mapenzi ya mwanadamu.

Kama mwanamke si muaminifu mkanye kama ukishindwa mwache au mtenge, lakini usiue kwa ajili yake. Japo wengi tunaamini waganga wa asili ni wabaya, lakini kama watatokea waganga kama mzee Ngugude dunia itakuwa salama.
Namalizia kwa waganga wa asili, jina lenu linaweza kuwa baya kwa watu kutokana na kuonekana nyie ndiyo chanzo cha matatizo kati ya mtu na jirani yake hata familia kwa familia.

Mganga siku zote anatibu, anayeua au kumroga mtu huyo ni mchawi ni makosa kumwita mganga. Basi chagueni moja kuwa wachawi au waganga. Namalizia kwa kumuomba Mungu anisamehe kwa yote niliyoyafanya kwa ajili ya mke wangu, kwani niliisha kuwa mchawi kamili nilifikia hatua mbaya ya kuroga na kuua pia nilikuwa radhi hata kula nyama ya mtu kwa ajili ya mke wangu.

Najua hukumu yake kwangu ni kubwa lakini kupitia ukurasa huu najutia kila nilichokifanya. Nakuombeni katika mkasa huu chukueni mazuri na mabaya muyaache kwa vile kusudio la kuutua mzigo mzito uliokaa moyoni mwangu ilikuwa kuhakikisha makosa yangu hayarudiwi na mtu mwingine.

Namalizia kwa kuwashukuru wote mliokuwa nami mwanzo hadi mwisho wa mkasa huu, Mungu awabariki, asanteni.

MWISHO

Hatari sana ila ni fundisho...

Ila kiasi fulani inafundisha ishi na hawa viumbe wakina Shunie kwa akili...

Chapter closed...



Cc: mahondaw
 
😀😀

Mbona alisikika mlevi mmoja akisema wakina nyinyi wote akili zenu zinafanana...

Siyo maneno yangu... Ni maneno ya wale binadamu wa siku hizi ambao ni wabishi sana...



Cc: mahondaw
Hapana bwana wachache tu wanatuharibia tunaonekana wote letu moja
 
Sehemu ya 10

“Mwaija nataka uwe mpenzi wangu, nakuhakikishia kwa jina la Mungu kukufanyia mambo yote niliyokuahidi hata kabla ya kukutana nawe kimwili ili uniamini.”

“Na dada?”
“Mwaija, dada yako hajitambui pia hajui hatima ya maisha yake na kusahau uzuri una mwisho.”

“Lakini kumbuka kufahamiana na wewe ni kupitia kwa dada huyohuyo ambaye amekuwa waluwalu.”

“Mwaija nina malengo mazuri na wewe, ukikubali nitahakikisha nakuachisha hii kazi na kukufungulia mini super market utakayoimiliki mwenyewe.”

“Yote umesema mazuri ambayo kila mwanamke anayatafuta kuyapata kwa mpenzi wake. Lakini tatizo siwezi kushea mwanaume na dada yangu, ni matusi kwetu.”

“Mwaija, dada yako si mke wangu ni mpenzi wangu, hata nikimuacha bado ana wanaume wengine. Naomba usiipoteze nafasi hii.”

“Samahani kwa hili siwezi,” pamoja na ahadi nono sikuwa tayari kujidhalilisha.
“Inawezekana nimekushtua ila nakuomba nenda nyumbani jifikirie taratibu kisha utapata jibu. Ila naomba usinifikirie vibaya kwa vile nimekutafutia kazi ndiyo sababu ya kukutaka.”
“Walaa, ila tu siwezi kushea penzi na dada yangu.”

“Najua utasema hivyo lakini kama utamwambia mtu yeyote nilichokuahidi atakushangaa kama utakataa.”
“Ni kweli atanishangaa, lakini heshima ya mtu haibebwi na mtu mwingine bali yeye mwenyewe.”

“Najua Mwaija, ila naomba nilichokuambia kipe muda akilini mwako ili uweze kunipa jibu ambalo najua litakuwa zuri kwako na kwangu.”

“Sidhani kama nitakuwa na jibu tofauti na nililokueleza.”
“Najua una msimamo, naomba utafute mawazo hata kwa rafiki zako wa karibu nina imani utabadilika.”

“Sawa, lakini siamini kama kuna mabadiliko zaidi ya hili nililokueleza. Japokuwa sikuwa tayari kuufungua moyo wangu kwa sasa lakini kwa ukarimu wako na kuonesha kunijali kama ungekuwa huna uhusiano na dada ningeweza kukupa nafasi ya kukufikiria.”

“Sawa Mwaija, bado nasisitiza sitakuwa na wewe kwa ajili ya kukuumiza. Najua umeumizwa hivyo nitajitahidi kuwa mfariji wako.”

“Halafu kuna kitu kingine ambacho nakiogopa, kama usingekuwa na uhusiano na dada bado suala la kutembea na mume wa mtu linanitisha.”

“Mwaija, mke wangu hana kizazi nami nina pesa leo hii nikifariki nani atakuwa mrithi wangu? Nilitaka kuzaa na dada yako lakini alikataa hawezi kuzaa.

“Hebu fikiria nitabadili wanawake wangapi wakati kipindi hiki hali ni mbaya kama usipokuwa makini?”

“Ni kweli, lakini umenipa mtihani mzito.”
“Wala si mzito, upe muda moyo wako kwa vile kitu nitakachokifanya kina manufaa makubwa sana kwako. Mwaija fedha sina sana ila nina uhakika wa kukufanya uishi maisha ya ndotoni.”

“Mmh! Bado mtihani kwangu.”
“Mwaija kama hilo huwezi naomba unisaidie kitu kimoja.”
“Kitu gani?”
“Basi nizalie mtoto mmoja akiwa wa kiume nitakupa milioni 20 akiwa wa kike milioni 10.”

“Tatizo si kukuzalia bali kushea penzi na dada yangu.”
“Mwaija naomba katika hayo mawili moja lifanyie kazi.”
Wakati huo tulikuwa tumefika nyumbani, kabla ya kuteremka bwana wa dada alinipa bahasha.

“Ya nini?”
“Kaifungulie ndani.”
Sikutaka kuhoji, nilipokea. Kabla ya kuondoka alinishika mkono mmoja kwenye bega na kuniangalia kwa muda mpaka machozi yakamtoka.
“Shemu unalilia nini?” nilimuuliza.
“Basi, naomba tulilozungumza usimwambie mtu.”

“Hata siku moja sina tabia hiyo.”
“Nimefurahi kusikia hivyo, naomba uyafanyie yote kazi niliyokueleza.”
“Sawa.”

Tuliagana na mimi kuteremka kwenye gari na kuelekea ndani. Bwana wa dada naye alipaki gari pembeni na kuingia ndani kuonana na dada. Mimi nilikwenda moja kwa moja kuoga ili nipate muda wa kupumzika.

Baada ya kuoga na kula nilijilaza kitandani na kuifungua bahasha ambayo ilikuwa na fedha mpya, nilipohesabu nilikuta laki saba taslimu.

Niliziweka kwenye kabati langu na kurudi kitandani kujilaza. Nilijikuta nawaza vitu vingi kuhusiana na maneno ya bwana wa dada. Machoni kwake alionesha hafanyi mzaha lakini bado sikutakiwa kumkubalia kwa vile ingeonesha jinsi gani familia yetu isivyojiheshimu.

Nilikuwa na wazo la kulitupilia mbali lakini niliamini mama anaweza kunisaidia hata kuweza kulimaliza bila kumuudhi bwana wa dada pia kutogombanisha na dada yangu japokuwa niliamini kabisa katika tabia yake hata kama yule bwana angeamua kuachana naye hakuna chochote kingemgusa moyoni mwake.
Wazo lile sikutaka kuliacha lipite vilevile japokuwa moyoni nilikuwa na uamuzi wangu ambao niliamini utabakia kama ulivyo.

Wazo la kwenda kumueleza mama nililisitisha kidogo na kupanga kwanza kwenda kumwambia da Suzy ili nijue atanipa mawazo gani. Da Suzy toka nianze kazi pale alikuwa mtu wangu wa karibu ambaye tulifikia hatua kila mtu kumweleza mwenzake mambo ya ndani, japokuwa kuna baadhi ya tabia za familia yangu nilimficha.

Siku ya pili nilipokwenda kazini wakati wa chakula cha mchana nilimweleza da Suzy kuwa nina mazungumzo naye baada ya kazi, naye alinieleza atanisikiliza.
Baada ya muda wa kazi tulikwenda kwenye mgahawa ulilokuwa karibu na kazini kwetu.

Kwa vile nilijua mazungumzo yetu yatachukua muda kidogo, nilimpigia simu bwana wa dada kuwa asije kunichukua nitachelewa kidogo. Lakini mwenzangu alipokea tofauti na kujua ninataka kumkimbia kutokana na kauli yake ya kunitaka kimapenzi.

“Mwaija, usifike huko nililofikisha kwako ni ombi tu si lazima. Ulitakiwa kulifanyia kazi na kuliangalia lina uzito gani kama halina mashiko ungeachana nalo na si kukimbiana.”

“Hapana shemu, kuna kitu kitanichelewesha kwa leo, lakini kesho utanichukua kama kawaida,” nilijaribu kumtoa wasiwasi.

“Mwaija mi nipo tayari kukusubiri kwa muda wowote lakini leo nikurudishe nyumbani kama kawaida.”
Mmh! Shem bado alikuwa king’ang’anizi.
“Hapana shemu leo naomba nisikusumbue.”

“Mwaija najua umekasirika, bado nasisitiza ni ombi wala si lazima. Wewe ni mtu mzima mwenye kujua zuri na baya kama ulishawahi kuolewa hakuna kigeni tena kwako.”

“Shemu umeenda mbali sana, kama kungekuwa na mabadiko yoyote ningekueleza. Unavyonifahamu ndivyo nilivyo.”

“Basi naomba ukubali nikusubiri,” shemu alikuwa king’ng’anizi. Ilibidi nimkubalie anipitie ili niondoe wasiwasi wake.
“Basi hakuna tatizo nikimaliza mambo yangu nitakutaarifu.”

“Hapo sawa,” kauli ya bwana wa dada ilinishtua na kujiuliza nini mwisho wa yote kama sitakubaliana na yeye kitu ambacho kilikuwa kwenye mawazo yangu.
Baada ya kukubaliana na bwana wa dada, nilimgeukia da Suzy ambaye alionekana kunishangaa muda wote niliokuwa nikibishana.

“Vipi Mwaija?” aliniuliza baada ya kukata simu.
“Ndiyo yaliyonifanya niombe ushauri wako.”
“Yepi hayo?”
“Ndiyo maana tupo hapa.”
“Mmh! Haya.”

Vinywaji tulivyoagiza vililetwa, wote tuliagiza juisi ya embe mchanganyiko na parachichi. Kila mtu alichukua glasi yake na kunywa kidogo kisha da Suzy alikaa mkao wa kusikiliza.
Baada ya kutulia kwa muda nilimwita da Suzy.

“Da Suzy.”
“Abee mdogo wangu,” aliniitikia huku akinitazama usoni.
“Kuna jambo moja nimekutana nalo jana limenipa wakati mgumu. Japokuwa nilikuwa na uamuzi wangu lakini sikutaka kuamua peke yangu kwa vile naliona jambo lenyewe zito.”

"Jambo gani mdogo wangu?" Niliamua kumpa historia fupi ya maisha yetu na nilichoelezwa na bwana wa dada jana yake.

Da Suzy alionesha kunishangaa, baada ya kunitazama aliniuliza swali.
“Mwaija unataka kuniambia Mzee Sambi si mpenzi wako?”
“Ni shemeji yangu bwana wa dada yangu.”

“Basi sote tunajua yule ni mtu wako.”
“Walaa, ni shemeji yangu.”
“Basi Emma hajui lolote, ingekuwa wewe si mtu wa mzee Sambi lazima angekutongoza. Yule mwanaume mchafu sana, ameishatembea na robotatu ya wafanyakazi pale.”

“Lakini wewe naona anakuheshimu sana.”
Kauli yangu ilimfanya da Suzy kucheka kitu kilichonifanya nishtuke.

“Dada mbona unacheka?”
“Mwaija we mtu wangu wa karibu siwezi kukuficha kitu. Emma alipokuja kazini mimi ndiye nilikuwa mtu wake wa kwanza.”

Nilijikuta nikishtuka lakini nilificha mshtuko wangu. Da Suzy aliendelea kunipasha nisivyovijua.

“ Kwa kweli nilimpenda toka siku ya kwanza kuanza kazi. Kwa vile nilitaka kumvuta karibu yangu, nilitumia muda mwingi kumfundisha kazi.

“Lakini baada ya muda alipanda cheo kwa vile alikuja na elimu yake. Hapo ndipo aligeuka mchafu sana kwa kutembea ovyo na kila msichana mzuri anayekuja kufanya kazi.

“Si kazini hata huko anapokaa simu yake kila siku nilikuwa nakamata ujumbe wa mapenzi wa wanawake tofauti. Nilijaribu kumshauri na nia yetu ilikuwa tuoane lakini hakuonesha kubadilika, niliona kuchangia mwanaume ni kujidhalilisha. Mwisho wa siku nilibwaga manyaga.” Da Suzy alijikuta akinipa historia ya uhusiano wake na bosi wetu Mr Emma.

“Mmh! Pole sana, sasa kazi mlifanyaje?”
“Kwa vile maisha nayajua nilijielekeza kwenye kazi na kumpa uhuru.”
“Lakini wewe si umeolewa?”
“Ndiyo, tena na rafiki wa karibu wa Emma.”

“Mmh! Ilikuwaje?”
“Huwezi kuamini yule mkaka alikuwa akinipenda muda mrefu lakini nilimtolea nje. Baada ya kutendwa na Emma nilimfungulia milango ili kumkomesha Emma.”

“Mmh! Baada ya kuoana nini kilifuata?”
“Hakuna kitu zaidi ya kuheshimiana tu.”
“Ninavyowajua wanaume lazima kuna siku huwa anataka kukumbushia, inakuwaje akiomba?”

“Huwa namueleza tuheshimane, mwanzo alikuwa mbishi lakini sasa amenielewa.”
“Mmh! Wanaume ukiwachekea wanaweza kukuharibia ndoa bure,”
“Umeona eeh, mdogo wangu.”
“Lakini naona kama umri ulikuwa umemzidi?”

“Ni kweli, Emma nimemzidi miaka mitano, lakini nilimpenda sana huwa sipendi kukumbuka penzi langu lililopeperushwa kama vumbi kwenye upepo makali.”
“Mmh! Pole sana dada.”
“Asante.”

Da Suzy alitulia kwa muda akiwa ameinama kuonesha jinsi gani mapenzi yalivyomuumiza kumpenda mtu asiye muaminifu. Baada ya muda alinyanyua uso wake na kuchukua glasi ya juisi na kunywa kidogo na kunitazama kisha alisema:

“Mdogo wangu una mtihani mzito ambao ni sawa na kuitumia turufu moja iliyokuwa mkononi, ikutoe mrithi au ikutoe kapa.”

“Una maana gani da Suzy?”
“Mpaka mzee anakueleza jambo kama hilo ujue basi kakufuatilia muda mrefu. Malengo yake ni makubwa sana kwako.”
“Lakini kumbuka tayari ameishatembea na dada yangu.”

“Ni kweli, lakini kwa tabia ya dada yako ya kutokuwa na bwana mmoja, hiyo ni nafasi ambayo naamini unaweza usiipate mpaka unakufa.

Mtu akujengee nyumba na akununulie gari kwa ajili ya mapenzi ni wachache katika dunia ya leo ambayo wanaume wengi ni matapeli.

“Kama huwezi kukubali kuwa nyumba ndogo basi mbebee ujauzito ili upate hayo mamilioni. Nina imani Mzee Sambi alivyo na hamu ya mtoto lazima ahadi zote tatu atatimiza ukimzalia mtoto.”

“Mmh! Dada unanipa mtihani.”
“Hakuna mtihani, yupo wapi Beka uliyempenda kuliko kitu chochote chini ya jua. Mdogo wangu Waswahili wanasema bahati haiji mara mbili na mchuzi wa mbwa unywe ungali moto ukipoa haunyweki.”

“Kwa hiyo unanishauri nimkubalie?”
“Mwaija mkubalie, nafasi kama hiyo mdogo wangu wenzako tunaiendea kwa waganga wewe inakujia miguuni unataka kuipiga teke?”

“Lakini naogopa kugombana na dada.”
“Fanyeni hata penzi la siri nina imani litakusaidia katika maisha yako.”
“Mmh! Nitajaribu kwa vile umeivunja ngome ya moyo wangu sina budi kukubaliana na wewe,” nilijikuta nikilegeza msimamo
 
Habari mambo naitwa Mr Equator Nimeandika ujumbe huu kuku omba swala moja tu!
Mimi nimetengeza website ya ku share story ambayo ni EquatorStory
Je umekuwa ukipata tabu kupost story zako hapa?
Hili ndo suluhisho lako.
Mimi nataka nkupe nafasi ya kuwa mmoja wapo wa kwanza kutumia hii website
unda account yako na uweze kupost story yako mpya.
 
Hii hadithi mbona inafanana na ile ya ALLY MBETU inaitwa MKE WANGU ALINIFANYA NIWE MCHAWI.
Iliwahi kuwekwa humu na Mzizi mkavu
 
Baharia gani wewe unayependa kitonga?

Anyway, vipi bado unakaa kwa shemeji yako?
 
Back
Top Bottom