Grahams
JF-Expert Member
- Mar 19, 2016
- 18,836
- 57,467
Vijana wanasema Hii Imeendaa 🤗
Naendelea kuisoma taratibu kwa macho yangu ya Kizee 🤪
Vijana wanasema Hii Imeendaa 🤗
Zimefika Mjukuu, naye anakusalimu sana 🤗Msalimie bibi![]()
Aisee hapa nimepata uchunguSEHEMU YA KUMI:
Yalipita mawiki kadhaa, ilikua asubuhi najiandaa kutoka kwenda kwenye biashara zangu, school bus inayombeba Lameck ilikua imeshaondoka kama nusu saa hivi, dada alikuja mbio akanambia mama baba amenipigia simu anasema pokea simu yako.
Nilikua metoka bafuni kuoga, kwhiyo simu itakua ilipigwa wakati nipo bafuni...
Nikakuta missed calls kama nne za mme wangu, sio kawaida yake, niseme tu nilipatwa na mshtuko ila nikajikaza...mme wangu akapiga tena wakati najiandaa kununua salio nimpigie, nikaipokea kwa kihoro...dommy akaniuliza kama nimeshatoka nyumbani, nikamwambia hapana...nipo najiandaa, akanambia usitoke nakuja...nikamuuliza dommy mbona hivyo kuna nini? Akanambia naomba tu nisikilize mke wangu, usitoke nyumbani...
Nikakaa katika msongo wa mawazo, nikamuita dada na kumuuliza baba alipokupigia alisemaje? Dada akanambia alinambia nikwambie upokee simu...nikasema sawa hamna tatizo, nikaamua kutumia huo mda kumsaidia dada kumuogesha mwanangu wa pili, huku nikimsubiria dommy arudi, baada ya kama lisaa na nusu dommy akafika, nadhani foleni ilimchelewesha, dommy akanambia chukua mkoba na vitenge kuna mahala tunaenda, nikamwambia vitenge? vya nini tena? akanambia nitakueleza wife...hebu fanya nachokwambia .
Nikawaza tugombane kisa vitenge tu jamani, nikaingia ndani nikatoka na vitenge viwili, hao tukaingia kwenye gari na safari ikaanza...dommy hakua yule niliyemzoea , muongeaji na mcheshi, akaendesha gari kwa umakini sana hadi Amana hospitali, nikaona nivunje ukimya ....honey hospitali asubuhi yote hii tunakuja kumuona nani? mbona hunielezi vizuri...mme wangu akainama aliponyanyuka alikua ameloana machozi, akanambia nisamehe grace...nimeshindwa kwa mara nyingine kuwalinda, nikiwa katika sintofahamu nikaona gari ya nyumbani kwetu inaingia pale hospitali, baba na mamangu walishuka wakiwa wameongozana na wadogo zangu wote wawili...
Nikaona kama wananichanganya, nikataka kushuka, kwa Kasi Dominic akaniwahi nisifungue mlango, mama na baba wakaja pale tulipopaki gari, baba akafungua mlango na kuniambia grace ....pole mwanangu kipenzi...mama akanichukua hadi nyuma ya gari, akanifunga vile vitenge style ya kinyakyusa, kitenge kikakazwa tumboni...mama akanambia nisamehe grace...sikusimama vema katika kuombea ndoa yako kabla hujaolewa, nisamehe mwanangu...
Nikamwambia mama, wewe ni mamangu mpenzi, naomba uniambiae nini kimetokea....mama hakujibu kitu akanikumbatia kwa upendo akanambia atakwambia mmeo...dommy akaja akanambia twende tukamuone mtoto...
Nikapatwa na kama mshtuko wa ghafla, mwanangu ameondoka asubuhi na school bus, mwingine memuacha na dada , huyu naekuja kumuona Amana ni yupi? Baba na mama wakazidi kuniambia nijikaze...
Tukaingia ndani hospitali, badala ya kuelekea wodini tukaelekea upande wa mochwari, nikasimama kwanza, nikawaambia ...hata kama mwanangu yupo hapa, ndio awe huku? hebu acheni masikhara jamani..
Nikaanza kuita jina la Lameck kama mtu aliechanganyikiwa, baba na mme wangu wakashauri nirudishwe kwenye gari, nikarudi pamoja na mama, sikua na nguvu nikakaa chini kwanza.
Nikamwambia mama, mnanikosea ....naomba uniambie kilichotokea, mama akanambia niahidi utakua mtulivu grace, nikamwambia naahidi mama...akanambia gari ya shule aliyopanda Lameck imetumbukia mto msimbazi, watoto kumi kati ya 40 waliokuwepo wamefariki hapohapo kwa kunywa maji, watoto wengine wamesombwa na maji...tupo hapa kuweza kutambua mwili wa Lameck...wewe ni mama unamjua vema mwanao katika hali zote, maiti zimevimba sababu ya majeraha na kunywa maji mengi...jikaze uweze kumtambua mwanao....
Huwezi amini sikuweza hata kulia, nilimuangalia mama nikamwambia twende huko kwenye utambuzi , mama akiwa bado hajaamini kama natumia akili yangu ya kawaida au wazimu umenirudia , akashangaa nimeshanyanyuka na kuelekea walipoelekea baba na Dommy.
Mtoto wako uliemuweka miezi tisa tumboni ni wako jamani...ile bond ni ya ajabu sana, nilizipiga hatua kama kichaa, mama alikua anafanya kazi ya kunikimbiza, mamangu ana mwili kiasi, nilimtesa sana ile siku...
Nikafika huko mochuari , mlangoni nakutana na baba na Dommy, wananishangaa nimefikaje pale,.mara wakamuona mama anakuja mbiombio, mama akafikia kukaa kwanza...
Nikamwambia dommy nipeleke nikamuone mwanangu,dommy akanambia hawajamuona labda atakua katika wale waliondoka na maji, nikamwambia mwanangu yupo hapa nipeleke ...baba akamwambia sawa acha aingie na yeye akaangalie...niliingia ndani, masikini vitoto vyote kumi vilikua vimehifadhiwa sakafuni...vimefunikwa na mashuka ya hospitali, wakasema wameshindwa kuwaweka kwa majokofu ili kurahisisha zoezi la utambuzi, nikapiga jicho moja tu, nikagundua alama ya weusi kwa mbali chini ya jicho la Lameck..mwanangu mpenzi alikua amelala pale chini, mwanangu, malaika wangu alikua amelala pale chini bila uhai...oh dear Lord...
daah asante Nana japo umenitoa machoziSEHEMU YA KUMI NA MBILI:
Mathew alikua sasa, taratibu za kumpeleka kwa bibi ake kwa ajili ya birthday zilirudi tena kwa Kasi...nikaona kama birthday ndio gharama ya maisha ya mwanangu acha tu afanyiwe...sikutaka tena ligi, ili mradi amani ilikuwepo basi sikutaka tena maugomvi, swala tu wasiniumize mimi wala mwanangu kihisia wala kimwili.
Mathew alipofikisha miaka mitano alianza kupata ugonjwa wa ajabu, alikua anaangula kila ifikapo tarehe 20 ya kila mwezi....na ndio tarehe aliyofariki marehemu baba yangu mkwe. Mara ya kwanza nilijua ni masikhara lakini mda ulipozidi kwenda nikaona hii Sasa sio kawaida...kila tarehe 20 mtoto anaangula kwa miezi mitatu mfululizo, nikaanza kupambana na hospitali, nilizungumka kwa specialist wote hapa dar bila mafanikio, tukaomba transfer tukaenda aghakhan Nairobi, bado mtoto hakua na nafuu, tena akawa anazidi, akawa anaangula anakaa hata masaa matano badala ya lisaa limoja kama awali.
Mme wangu ikabidi amuangukie mama ake kua naomba unisaidie mwanangu apone, mama mkwe akamwambia mme wangu , sio wewe wa kuja kupiga magoti nataka aje mkeo..Muulize mkeo alichokifanya siku amekuja kwenye kikao miaka kadhaa nyuma, mwambie yale matusi ndio gharama yake hii, rudini tena Lupembe. Dominic alirudi nyumbani akiwa amekasirika isiyo kifani, akanambia napambana kwa ajili yenu na bado unafanya mambo kinyume na makubaliano? Ile siku nilisema sitoweza tena? Kama gharama nayotakiwa ni kwenda kutendewa tena unyama na mamake kama kikao cha kwanza, sitomudu....nilipiga magoti nikamtafuta Mungu kwa bidii...nilitubu kukubali kutumika na miungu kwa miaka yote hiyo, nilisali na kufunga kwa kumaanisha sana. Dominic hakua akirudi nyumbani, nilhamisha makazi pia pamoja na mwanangu ile nyumba nilipangisha.
Nikiri tu maisha hayakua rahisi lakini Mungu ni mwema alinipigania, nilipambana na maombi pamoja na matibabu ya hospitali hadi mwanangu alikaa sawa . Nilikuja kusikia kua Dominic alioa tena mwanamke alietafutiwa na mamake, sikutaka kujihusisha na ile familia tena.Miaka mingi mbele kijana wangu akiwa mkubwa wa kwenda secondary nakuja kuonana na Dominic akiwa amedhoofu mnooo...akaomba radhi na akaomba wasaa wa kuongea nami, nilimruhusu tukatafuta mahala tukaongea, akanambia kua mama alifariki miaka mingi na pia alioa lakini watoto walikua wanafariki kila mwaka...
Akanambia anajutia kwa kushindwa kua baba bora kwa wanangu...na akaomba radhi kwa yote aliyonipitisha, akanambia alipambana lakini amekubali kushindwa, na hapo alipo anapambana na maradhi mbalimbali maana majini yaliyoachwa na mamake yanamshinda kwaio yametafuna watoto wake, wadogo zake wamefariki kwenye ajali mfululizo na yeye yamempa maradhi ya kudumu...ananambia mimi ni kitu bora kuwahi kutokea kwake, na kua hakunistahili...alinambia atakuja wakili kuniletea documents za kusaini kuhusu mali anazomiliki na alivyofanikiwa kuchuma maana hana familia nyingine zaidi yangu, alinipa hongera kwa kua jasiri na kusimamia msimamo wangu katika imani...
Aliomba japo amuone Mathew kwa picha, nikamwambia next Friday ni graduation yake karibu sana....hakuamini kua hatimaye Mathew anamaliza form four...Alikuja kwa graduation na akajitambulisha kwa Mathew maana ni miaka mingi ilikua imepita, tukapata wasaa wa kuishi na Dominic kwa miaka mitano mingine, alikuja kufariki katika ajali mbaya ya gari iliyoondoa na maisha ya watu wengine nane....Mungu ampumzishe mahala pema Dominic wangu, who am I to judge him....nilimpenda sana ila alichagua fungu lingine ....
Mwisho:
Ahsanteni...Nawapenda mnooo..
Just Nana...
Asante Sana
Asante kwa tag Madam🥰
kwahiyo hii ni simulizi ya kweli inayokuhusu wewe au ni hadithi tuuPole mpenzi....
ulivotaja lupembe ni kwetu huko ila mimi nipo mufindi kwenda lupembe napandisha milima nikajua ni tukio la kweli coz uchawi huko lupembe upo kwa sanaaaHadithi tu rafiki...
Nimewahi sikia story kuhusu uchawi na maeneo hayo, nikaona nikiiweka kwa story itanoga, ila naamini ushirikina upo kila sehemu my dear ingawa baadhi ya maeneo ni vinara kama usukumani, Tanga, kigoma na Sumbawanga...it's just a story ,enjoy...nothing personalulivotaja lupembe ni kwetu huko ila mimi nipo mufindi kwenda lupembe napandisha milima nikajua ni tukio la kweli coz uchawi huko lupembe upo kwa sanaaa
ni story nzuri sana mpenziNimewahi sikia story kuhusu uchawi na maeneo hayo, nikaona nikiiweka kwa story itanoga, ila naamini ushirikina upo kila sehemu my dear ingawa baadhi ya maeneo ni vinara kama usukumani, Tanga, kigoma na Sumbawanga...it's just a story ,enjoy...nothing personal