Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,166
- Thread starter
- #161
*Sehemu ya 15*
“Prosper!”
“Naam Belinda!”
“Sitakusamahe maishani mwangu na hata kama nitakusamahe basi sitasahau siku zote!” Alisema Belinda na kuanza kutembea kwa haraka kutoka chumbani kwenda nje ya gereza.
“Belinda! Belinda! Belinda usiondoke!” Prosper aliita wakati Belinda akitoka chumbani lakini hakugeuka kuangalia nyuma alizidi kutembea kwa haraka huku akilia.
*****************
Alitoka hadi nje ambako alitembea hadi kituo cha mabasi madogo na muda mfupi baadaye daladala moja lilikuja na kusimama pembeni yake, alimbeba vizuri mtoto wake na kuingia ndani na kuchukua kiti cha nyuma kabisa, alikuwa bado na hofu ya kusababisha harufu lakini alipokumbuka kuwa alishafanyiwa operesheni na kuwa mkavu hofu hiyo ilitoweka mara moja.
Belinda aliendelea kububujiwa na machozi hadi wakati anafika mjini, watu wote ndani ya gari walimshangaa na walipomuuliza ni kwanini alilia machozi kiasi kile hakueleza chochote.
Alipomwangalia mtoto wake mzuri Alicia, aliyekuwa ameketi mikononi mwake roho yake ilimuuma zaidi, alikuwa mtoto mzuri mno kufa kwa Ukimwi!
Ilimuuma sana Belinda kujua kuwa hata mtoto wake hakuwa na maisha marefu mbele yake, lakini Alicia hakuwa na taarifa na kilichokuwa kikiendelea aliendelea kutabasamu huku akimpigapiga mama yake usoni.
Alipofika mjini Tabora aliteremka ndani ya basi, alihisi kukata tamaa ya kila kitu! Hakuona sababu ya kurudi tena Tutuo, kijijini kwao Prosper alichofikiria wakati huo ni kurudi tena Dar es Salaam kwa baba yake na kujaribu kumwomba msamaha! Lakini alipokumbuka jinsi baba yake alivyomfukuza kama mbwa roho iliingiwa wasiwasi na kujikuta akisita kuchukua hatua hiyo.
“Kwa kweli baba asingekuwa na matatizo ningerudi Dar , acha tu nirudi Tutuo!”
Baada ya kuwaza sana hatimaye mawazo yake yalimfikisha katika hatua hiyo lakini alipokumbuka kuwa nyumba aliyofikia ingekuwa tayari imekwishabomolewa na mwarabu aliyeinunua ili ajenge mashine, Belinda alikosa mahali pa kuelekea kwa sababu hakuona mahali pengine popote pa kufikia kijijini Tutuo.
“ Lakini acha tu niende, Wanyamwezi ni watu wakarimu sana, nitaomba kukaa kwa mtu yeyote au nitarudi tena kuomba kazi nyumbani kwa Mwarabu Mzee Mohamed nafikiri safari hii atakubali kwa sababu sina mimba na sinuki kama ilivyokuwa zamani!”
Belinda aliamua kurudi kijijini na alichofanya ni kwenda stendi ya basi ambako alipanda basi la kumpeleka kijijini Tutuo, njia nzima aliendelea kulia alijua maisha yake yalikuwa yamefika mwisho! Alihisi hakuwa na maisha tena mbele yake, binafsi hakujionea huruma sana aliyemtia simanzi zaidi alikuwa ni mtoto wake Alicia.
“Masikini Alicia anakufa kwa kosa lisilo lake akini kwanini hasa mtu amuue mtoto asiye na hatia? Prosper alishindwa kuvumilia shida? Nasema sitaki kumwona tena maishani mwangu!” Alisema kwa uchungu Belinda, hakujua alikuwa akiongea kwa sauti kiasi kwamba watu wote ndani ya basi waligeuka kumwangalia.
*******************
Gerezani:
Baada ya kuachwa chumbani Prosper alinyanyuka kwa unyonge na kutembea hadi chumba cha mahabusu na kwa muda mrefu aliendelea kulia na hakuona tena sababu ya kuendelea kuishi, alitamani kufa kukwepa aibu ya kuwaua mke na mtoto wake kwa Ukimwi lakini alishindwa kuelewa ni kwa njia ngani angeweza kujitoa uhai akiwa ndani ya gereza.
Alilia usiku mzima hadi asubuhi, alijuta kwa yote aliyoyafanya na alitamani sana kuonana tena na Belinda ili apate kuongea naye na kumwomba msamaha! Alijua hilo lisingewezekana hata kidogo kwani alikuwa na uhakika Belinda asingerudi tena.
“Laiti ningejua nisingejiingiza katika mchezo huo mbaya, shida za gerezani zingeniua mbona watu wengine wanaishi?”
Aliwaza Prosper huku akilia.
Prosper alikuwa na watu wengi sana wa kuwalaumu kuhusiana na suala hilo lakini watu waliopaswa kuzibeba lawama zote hizo walikuwa ni mama na dada zake kwa kitendo chao cha kumuua baba yake, bila wao kufanya hivyo Prosper aliamini asingeingia gerezani katika maisha yake!
“Ni wao ndio walilaumiwa niliingia gerezani kumwokoa mama na dada zangu, mama mwenyewe amekwishakufa na hata hao dada zangu hakuna hata mmoja anayefika hapa gerezani kunitembelea na bado nyumba na kiwanja alichoacha baba wameuza na kupotea, huu ni ukatili wa hali ya juu sana!” Aliendela kuwaza Prosper.
Baada ya siku hiyo Prosper hakuwaona tena Belinda na mtoto wake Alicia, kesi yake iliendelea katika mahakama kuu kanda ya Tabora na miezi mitatu baada ya Belinda kuondoka kesi hiyo ilifikia hukumu yake, alionekana kuwa na hatia mbele ya sheria baada ya yeye mwenyewe kukiri mauaji hayo ya baba yake mzazi mbele ya jaji Mohamed Simbila na kuhukumiwa kifo kwa kuchomwa sindano ya sumu
Mahakama nzima ilipigwa na butwaa baada ya hukumu hiyo, Prosper hakuonyesha huzuni wala kulia badala yake alitabasamu kwa furaha baada ya hukumu hiyo kutolewa.
“Una namna yoyote ya kujitetea?”
“Sitaki kujitetea Mhesimiwa Jaji, hukumu yako ni sahihi na hii ndiyo niliyoisubiri ili iniepushe na kifo cha mateso kilichopo mbele yangu!Nakushukuru sana mheshimiwa jaji na ninakupongeza sana kwa hukumu hiyo nzuri!” Alisema Prosper huku akicheka.
Bila kuchelewa maaskari walimpiga pingu mkononi na kumwondoa mahakamani, jaji aliyemkuhumu alibaki na maswali mengi sana kichwani mwake, alishafanya kazi ya kuhukumu watu kwa miaka karibu ishirini na alishahukumu watu wengi kifo lakini hakuwahi hata siku moja kumhukumu mtu kifo akicheka! Wengi walilia na kuomba kupunguziwa kifungo!
Siku iliyofuata Prosper ilitolewa amri Prosper ahamishiwe gereza la Keko jijini Dar es Salaam ambako angepambana na kifo chake! Alipakiwa ndani ya treni la abiria kutoka Mwanza kwa safari ya kwenda Dar es Salaam.
Prosper alilia lakini hakulia sababu ya hukumu ya kifo aliyopewa ila alilia kwa sababu alikuwa anapelekwa kufa bila kuonana na mke na mtoto wake kwa mara ya mwisho, alikuwa anakwenda kufa bila Belinda kufahamu ukweli juu yake! Pia alilia sababu yeye alikuwa anakwenda kufa na kuwaacha mkewe na mwanae wakiteseka kwa ugonjwa wa Ukimwi aliowaambukiza yeye.
*****************
Alicia, kijijini Tutuo:
Tayari alishazoea maisha ya nyumbani kwa mzee Mohamed, alifanya kazi kwa nguvu zake zote ili aweze kumridhisha mama mwenye nyumba, alipewa chumba kidogo ambacho alilala na mtoto wake kwa kutandika jamvi chini kila siku!
Ilikuwa ni kawaida yake siku zote kudamka mapema na kufanya kazi zote za ndani na ilipotimu sawa nne aliacha kazi hizo na kuanza kupasua kuni, baada ya kupasua kuni alianza kupika chakula cha mchana na baadaye alianza shughuli za ufuaji wa nguo za kila mtu nyumbani.
Zilikuwa ni kazi ngumu lakini Belinda alizifanya ili aweze kuishi na mtoto wake, katika miezi yote aliyokaa nyumbani kwa mwarabu Mzee Mohamed hakuwahi kumkumbuka Prosper lakini asubuhi ya siku hiyo akipasua kuni kumbukumbu za Prosper zilimsumbua kichwani, alitamani sana kumwona na aliona uamuzi aliouchukua haukuwa wa busara kwa sababu usingeweza kuubadilisha kitu chochote katika maisha yake kama ni virusi alishavipata na ni lazima yeye na mtoto wake wangekufa.
*Je, nini kitaendelea?*
“Prosper!”
“Naam Belinda!”
“Sitakusamahe maishani mwangu na hata kama nitakusamahe basi sitasahau siku zote!” Alisema Belinda na kuanza kutembea kwa haraka kutoka chumbani kwenda nje ya gereza.
“Belinda! Belinda! Belinda usiondoke!” Prosper aliita wakati Belinda akitoka chumbani lakini hakugeuka kuangalia nyuma alizidi kutembea kwa haraka huku akilia.
*****************
Alitoka hadi nje ambako alitembea hadi kituo cha mabasi madogo na muda mfupi baadaye daladala moja lilikuja na kusimama pembeni yake, alimbeba vizuri mtoto wake na kuingia ndani na kuchukua kiti cha nyuma kabisa, alikuwa bado na hofu ya kusababisha harufu lakini alipokumbuka kuwa alishafanyiwa operesheni na kuwa mkavu hofu hiyo ilitoweka mara moja.
Belinda aliendelea kububujiwa na machozi hadi wakati anafika mjini, watu wote ndani ya gari walimshangaa na walipomuuliza ni kwanini alilia machozi kiasi kile hakueleza chochote.
Alipomwangalia mtoto wake mzuri Alicia, aliyekuwa ameketi mikononi mwake roho yake ilimuuma zaidi, alikuwa mtoto mzuri mno kufa kwa Ukimwi!
Ilimuuma sana Belinda kujua kuwa hata mtoto wake hakuwa na maisha marefu mbele yake, lakini Alicia hakuwa na taarifa na kilichokuwa kikiendelea aliendelea kutabasamu huku akimpigapiga mama yake usoni.
Alipofika mjini Tabora aliteremka ndani ya basi, alihisi kukata tamaa ya kila kitu! Hakuona sababu ya kurudi tena Tutuo, kijijini kwao Prosper alichofikiria wakati huo ni kurudi tena Dar es Salaam kwa baba yake na kujaribu kumwomba msamaha! Lakini alipokumbuka jinsi baba yake alivyomfukuza kama mbwa roho iliingiwa wasiwasi na kujikuta akisita kuchukua hatua hiyo.
“Kwa kweli baba asingekuwa na matatizo ningerudi Dar , acha tu nirudi Tutuo!”
Baada ya kuwaza sana hatimaye mawazo yake yalimfikisha katika hatua hiyo lakini alipokumbuka kuwa nyumba aliyofikia ingekuwa tayari imekwishabomolewa na mwarabu aliyeinunua ili ajenge mashine, Belinda alikosa mahali pa kuelekea kwa sababu hakuona mahali pengine popote pa kufikia kijijini Tutuo.
“ Lakini acha tu niende, Wanyamwezi ni watu wakarimu sana, nitaomba kukaa kwa mtu yeyote au nitarudi tena kuomba kazi nyumbani kwa Mwarabu Mzee Mohamed nafikiri safari hii atakubali kwa sababu sina mimba na sinuki kama ilivyokuwa zamani!”
Belinda aliamua kurudi kijijini na alichofanya ni kwenda stendi ya basi ambako alipanda basi la kumpeleka kijijini Tutuo, njia nzima aliendelea kulia alijua maisha yake yalikuwa yamefika mwisho! Alihisi hakuwa na maisha tena mbele yake, binafsi hakujionea huruma sana aliyemtia simanzi zaidi alikuwa ni mtoto wake Alicia.
“Masikini Alicia anakufa kwa kosa lisilo lake akini kwanini hasa mtu amuue mtoto asiye na hatia? Prosper alishindwa kuvumilia shida? Nasema sitaki kumwona tena maishani mwangu!” Alisema kwa uchungu Belinda, hakujua alikuwa akiongea kwa sauti kiasi kwamba watu wote ndani ya basi waligeuka kumwangalia.
*******************
Gerezani:
Baada ya kuachwa chumbani Prosper alinyanyuka kwa unyonge na kutembea hadi chumba cha mahabusu na kwa muda mrefu aliendelea kulia na hakuona tena sababu ya kuendelea kuishi, alitamani kufa kukwepa aibu ya kuwaua mke na mtoto wake kwa Ukimwi lakini alishindwa kuelewa ni kwa njia ngani angeweza kujitoa uhai akiwa ndani ya gereza.
Alilia usiku mzima hadi asubuhi, alijuta kwa yote aliyoyafanya na alitamani sana kuonana tena na Belinda ili apate kuongea naye na kumwomba msamaha! Alijua hilo lisingewezekana hata kidogo kwani alikuwa na uhakika Belinda asingerudi tena.
“Laiti ningejua nisingejiingiza katika mchezo huo mbaya, shida za gerezani zingeniua mbona watu wengine wanaishi?”
Aliwaza Prosper huku akilia.
Prosper alikuwa na watu wengi sana wa kuwalaumu kuhusiana na suala hilo lakini watu waliopaswa kuzibeba lawama zote hizo walikuwa ni mama na dada zake kwa kitendo chao cha kumuua baba yake, bila wao kufanya hivyo Prosper aliamini asingeingia gerezani katika maisha yake!
“Ni wao ndio walilaumiwa niliingia gerezani kumwokoa mama na dada zangu, mama mwenyewe amekwishakufa na hata hao dada zangu hakuna hata mmoja anayefika hapa gerezani kunitembelea na bado nyumba na kiwanja alichoacha baba wameuza na kupotea, huu ni ukatili wa hali ya juu sana!” Aliendela kuwaza Prosper.
Baada ya siku hiyo Prosper hakuwaona tena Belinda na mtoto wake Alicia, kesi yake iliendelea katika mahakama kuu kanda ya Tabora na miezi mitatu baada ya Belinda kuondoka kesi hiyo ilifikia hukumu yake, alionekana kuwa na hatia mbele ya sheria baada ya yeye mwenyewe kukiri mauaji hayo ya baba yake mzazi mbele ya jaji Mohamed Simbila na kuhukumiwa kifo kwa kuchomwa sindano ya sumu
Mahakama nzima ilipigwa na butwaa baada ya hukumu hiyo, Prosper hakuonyesha huzuni wala kulia badala yake alitabasamu kwa furaha baada ya hukumu hiyo kutolewa.
“Una namna yoyote ya kujitetea?”
“Sitaki kujitetea Mhesimiwa Jaji, hukumu yako ni sahihi na hii ndiyo niliyoisubiri ili iniepushe na kifo cha mateso kilichopo mbele yangu!Nakushukuru sana mheshimiwa jaji na ninakupongeza sana kwa hukumu hiyo nzuri!” Alisema Prosper huku akicheka.
Bila kuchelewa maaskari walimpiga pingu mkononi na kumwondoa mahakamani, jaji aliyemkuhumu alibaki na maswali mengi sana kichwani mwake, alishafanya kazi ya kuhukumu watu kwa miaka karibu ishirini na alishahukumu watu wengi kifo lakini hakuwahi hata siku moja kumhukumu mtu kifo akicheka! Wengi walilia na kuomba kupunguziwa kifungo!
Siku iliyofuata Prosper ilitolewa amri Prosper ahamishiwe gereza la Keko jijini Dar es Salaam ambako angepambana na kifo chake! Alipakiwa ndani ya treni la abiria kutoka Mwanza kwa safari ya kwenda Dar es Salaam.
Prosper alilia lakini hakulia sababu ya hukumu ya kifo aliyopewa ila alilia kwa sababu alikuwa anapelekwa kufa bila kuonana na mke na mtoto wake kwa mara ya mwisho, alikuwa anakwenda kufa bila Belinda kufahamu ukweli juu yake! Pia alilia sababu yeye alikuwa anakwenda kufa na kuwaacha mkewe na mwanae wakiteseka kwa ugonjwa wa Ukimwi aliowaambukiza yeye.
*****************
Alicia, kijijini Tutuo:
Tayari alishazoea maisha ya nyumbani kwa mzee Mohamed, alifanya kazi kwa nguvu zake zote ili aweze kumridhisha mama mwenye nyumba, alipewa chumba kidogo ambacho alilala na mtoto wake kwa kutandika jamvi chini kila siku!
Ilikuwa ni kawaida yake siku zote kudamka mapema na kufanya kazi zote za ndani na ilipotimu sawa nne aliacha kazi hizo na kuanza kupasua kuni, baada ya kupasua kuni alianza kupika chakula cha mchana na baadaye alianza shughuli za ufuaji wa nguo za kila mtu nyumbani.
Zilikuwa ni kazi ngumu lakini Belinda alizifanya ili aweze kuishi na mtoto wake, katika miezi yote aliyokaa nyumbani kwa mwarabu Mzee Mohamed hakuwahi kumkumbuka Prosper lakini asubuhi ya siku hiyo akipasua kuni kumbukumbu za Prosper zilimsumbua kichwani, alitamani sana kumwona na aliona uamuzi aliouchukua haukuwa wa busara kwa sababu usingeweza kuubadilisha kitu chochote katika maisha yake kama ni virusi alishavipata na ni lazima yeye na mtoto wake wangekufa.
*Je, nini kitaendelea?*