Simulizi:Death Of Innocent

Simulizi:Death Of Innocent

*Sehemu ya 21*


“Kijana nakuonea huruma sana lakini inabidi tu nitimize wajibu wangu wa kukuchoma sindano hii ya sumu, nisamehe sana kukuondoka duniani, haya si mapenzi yangu!” Alisema mzee nyonganyonga kabla hajamchoma sindano hiyo.

“Choma tu mzee!” Prosper alisema kwa sauti ya unyonge lakini mawazo yake yalikuwa kwa Belinda na mwanae alijua kifo chao kingekuwa cha mateso kuliko chake!
“Haya moja! Mbili….tat….!”

Prosper alilala juu ya kitanda cha chuma pembeni yake akiwa amesimama mzee Nyonganyonga ambaye kazi yake ilikuwa ni kuondoa uhai wa binadamu wenzake!

Alilipwa mshahara mkubwa kwa kazi hiyo, prosper alishangaa kuona mzee huyo hamchomi sindano ingawa alikuwa nayo mkononi mwake na muda wa yeye kuchomwa ulishafika alishindwa kuelewa ni kwanini mzee huyo alishindwa kutelekeza wajibu wake.

Prosper alitamani kufa hakutaka kuishi zaidi aliogopa sana kupambana na tatizo la ugojwa wa Ukimwi uliokuwa mbele yake, aliamini hakuwa na uwezo wa kuyastahimili matatizo yanayoambatana na ugonjwa huo!Alijilaumu kwa uamuzi wake wa kukubali kushiriki maisha ya kishoga na mfungwa mwenzake Savimbi ambaye ndiye aliyemwambukiza ugonjwa huo.

“Natamani nisife! Napenda niishi na familia yangu lakini sipo tayari kushuhudia nikikonda taratibu hadi kifo changu!”

Aliwaza prosper na aliponyanyua uso wake kumwangalia mzee nyonganyonga alishangaa kukuta sindano ikiwa imezama tumboni kwake mwenyewe.
“Nime…cho….shwa na ….kazi ya ku…..ua ….bina…damu wenza…..ngu!

Nita…..mwe..leza nini Mu….ngu ni heri nife sitaki kuitoa roho yako wa sababu huna hatia!” alisema mzee nyonganyonga akiangakua chini na mwili wake kukakamaa na ulimi kutoka nje.
“Mzee nyonganyonga umefanyua nini sasa? Kwanini umejiua wewe wakati ni mimi ninayestahili kufa?”

Aliuliza prosper huku akipiga kelele alishindwa kufanya lolote kwa sababu alibanwa na mashine mikononi na miguuni, alianza kupiga kelele kuomba msaada na muda mfupi baadaye waliingia maaskari wawili mmoja akiwa na barua mkononi.

“Vipi kimetokea nini tena?”
“Hata mimi nashangaa nilikuwa nimefumba macho nikisubiri kuchomwa sindano lakini mzee nyonganyonga hakufanya hivyo na nilipofumbua nilikuta sindano imezama tumboni mwake na akaanguka chini!”

“Kweli?”
“Ndiyo! Sasa mnafikiri ni mimi ndiye nimemchoma?”

“Hapana siyo hivyo ila….!”
“Ila nini?”
”Basi tuyaache hayo kakueleza kitu chochote kabla hajajichoma?”
“Alipaanguka chini alianza kusema maneno ingawa kwa shida!”

“Alisema maneno gani?”
“Alisema amechoshwa na kazi ya kuua binadamu wenzake na hakuwa na jambo la kumjibu Mungu!”
“Mungu wangu! Sasa kwanini asingesema tu akabadilishiwa kazi?”

Prosper alibaki ameduwaa akiwashangaa maaskari walionekana kupigwa na mshangao mkubwa na hawakujua ni nini cha kufanya, mzee nyonganyonga alikuwa amelala chini sakafuni, mikono na miguu yake ikiwa imenyooka kuelekea darini! Macho na ulimi wake yakiwa yametoka nje alitisha na picha hiyo ilimuonyesha prosper ni kifo cha aina gani ambacho angekufa.

Aliogopa kupita kiasi na kujikuta akitetemeka mwili mzima lakini kwa sababu alishaamua kufa ili kukwepa mateso ya gonjwa la Ukimwi prosper aliamua kuipuuzia picha aliyoiona sakafuni na kuwageukia maaskari waliokuwa ndani ya chumba hicho.

“Afande!” Aliita na maaskari wote waliokuwa wameinamisha nyuso zao chini wakiushangaa mwili wa mzee nyonganyonga uliolala sakafuni waligeuka kumwangalia.
“Unasemaje prosper?”Wote waliuliza kwa mpigo.

“Sasa mtafanya nini?”
“Kuhusu?”
”Mimi nataka kufa!”
“Hautakufa tena prosper bado una siku nyingi sana za kuishi!”

”Si uchukue hilo bomba la sindano uvute dawa nyingine unidunge kipi kinachokushinda kama mnaogopa basi nitoeni hapa kwenye mashine nijidunge mwenyewe!”

“Haiwezekani tena prosper serikali imeamua kusitisha hukumu ya kifo uliyopewa tena una bahati nafikiri Mungu alikuwa hajapanga ufe kwa sababu mkeo amefika hapa na barua zikiwa zimebaki sekunde ishirini tu!

Hapakuwa na njia yoyote ya kuwahi kama mzee Nyonganyonga asingejiua mwenyewe!” alisema mmoja wa maaskari.
“Ni nini mnasema nini nyinyi mbona siwaelewi?”

“Barua ni hii hapa imetoka kwa mwanasheria mkuu wa serikali hivyo haiwezekani kukuchoma sindano tena!”
“Hebu niione hiyo barua!”Alisema prosper kwa ukali kiasi kwamba maaskari walishindwa kumwelewa kwa sababu alitakiwa kufurahia kukwepa kifo akiwa juu ya kitanda cha mauti.

Askari aliyekuwa na barua hiyo mikononi alimsogezea prosper na kuifungua, prosper alianza kuipitia taratibu tangu mwanzo hadi mwisho wa barua lakini badala ya kufurahia alianza kupiga kelele.

“NATAKA KUFA!NATAKA KUFA! MIMI NATAKA KUFA SITAKI TENA KUISHI!” aliongea kwa sauti ya juu huku akijaribu kujitoa kwenye mashine iliyoshika mikono na miguu yake.

Maaskari waliamua kumfungua prosper akatoka kitandani na kusimama wima, wakiwa hawa hili wala lile maaskari walishtukia prosper anatimua mbio kulifuata bomba lililokuwa chini lengo lake likiwa ni kujichoma nalo ili afe alilifikia na kulishika lakini kabla hajalinyanyua na kutimiza azma yake mguu wa askari ulisimama juu ya kiganja chake prosper alipiga kelele sababu ya maumivu aliyoyapata.

“Kwanini unataka kufanya hivyo lakini yaani badala ya kufurahia amenusurika kifo kimiujiza unataka kufanya ujinga?”

“Braza mimi ni mtu mzima na akili zangu ukiona nataka kufanya jambo jiulize mara mbili kuna tatizo gani, hakuna mtu anayetaka kufa binadamu wote tunapenda kuishi! Kwa hiyo niache mimi nifanye ninavyotaka!”

“Haiwezekani! Afande hebu mtoe huyu chumbani mpeleke katika chumba cha washauri nasha nafikiri utakuwa na tatizo ambalo ni vyema tukalifahamu!”


Askari magereza alimshika mkono prosper ambaye wakati huo aliendelea kulia mfululizo na kutoka naye hadi nje ya chumba cha kifo mbele kidogo aliingia naye katika chumba kilichoandikwa mlangoni “Ushauri Nasaha!” ambao walimkuta mama wa makamo akiwa amekaa nyuma ya meza kubwa.
“Vipi tena?”

“Hukumu yake ya kifo imesitishwa na serikali baada ya kugundulika dakika chache kabla ya kifo kuwa hakutenda kosa lililopelekea apewe hukumu hiyo!”
“Hongera sana kijana nakushauri ukitoka hapa uwe mwema mbele za Mungu kwani amekupa nafasi nyingine ya kunyoosha njia zako unasikia?”

“Usinipe hongera mama mimi sitaki kuishi na kama kuna uwezekano wa kuniua sasa hivi fanyeni hivyo haraka kwani nitajiua mwenyewe!”

Jipu la prosper lilimshtua mtoa ushauri nasaha, aligundua prosper alikuwa na tatizo kubwa lililohitaji muda mrefu wa kuongea naye!

“Kwanza hebu tufahamiane mimi naitwa mama Mpelumbe wewe mwenzangu unaitwa nani?” Mama huyo alianzaia mbali kidogo.

“Naitwa prosper!”
“Aisee wewe ndiye prosper?”
“Ndiyo mama ni vizuri ukiniita marehemu prosper sababu tayari nimeshakufa! Mimi ni maiti inayotembea!”
”Unamaanisha nini mwanangu?”
“Yaani mama hunielewi ninaposema mimi ni maiti inayotembea!”
‘Sikuelewi hata kidogo!”

“Na si mimi tu hivi sasa vijana wengi ni maiti zinazotembea! Ndiyo maana nataka kufa kwa sababu yaliyoko mbele yangu sitaweza kuyahimili!”
”Unamaanisha nini?”
Badala ya kujibu swali prosper aliyekuwa ametulia alianza kulia machozi.


Belinda alikaa nje ya gereza na mtoto wake mgongoni akiendelea kulia machozi!Alishangaa ni kwanini maaskari walichelewa kiasi hicho kurudi kutoka ndani, alijua kwa vyovyote mume wake alikuwa amekufa! Mawazo hayo yalimzidishia huzuni aliamini asingeweza kupambana na maisha peke yake aliumia juhudi zake zote za kumuokoa prosper zilikuwa zimegonga mwamba.

*Je, nini kitaendelea?*
 
Asante sana @shunie.
*Sehemu ya 21*


“Kijana nakuonea huruma sana lakini inabidi tu nitimize wajibu wangu wa kukuchoma sindano hii ya sumu, nisamehe sana kukuondoka duniani, haya si mapenzi yangu!” Alisema mzee nyonganyonga kabla hajamchoma sindano hiyo.

“Choma tu mzee!” Prosper alisema kwa sauti ya unyonge lakini mawazo yake yalikuwa kwa Belinda na mwanae alijua kifo chao kingekuwa cha mateso kuliko chake!
“Haya moja! Mbili….tat….!”

Prosper alilala juu ya kitanda cha chuma pembeni yake akiwa amesimama mzee Nyonganyonga ambaye kazi yake ilikuwa ni kuondoa uhai wa binadamu wenzake!

Alilipwa mshahara mkubwa kwa kazi hiyo, prosper alishangaa kuona mzee huyo hamchomi sindano ingawa alikuwa nayo mkononi mwake na muda wa yeye kuchomwa ulishafika alishindwa kuelewa ni kwanini mzee huyo alishindwa kutelekeza wajibu wake.

Prosper alitamani kufa hakutaka kuishi zaidi aliogopa sana kupambana na tatizo la ugojwa wa Ukimwi uliokuwa mbele yake, aliamini hakuwa na uwezo wa kuyastahimili matatizo yanayoambatana na ugonjwa huo!Alijilaumu kwa uamuzi wake wa kukubali kushiriki maisha ya kishoga na mfungwa mwenzake Savimbi ambaye ndiye aliyemwambukiza ugonjwa huo.

“Natamani nisife! Napenda niishi na familia yangu lakini sipo tayari kushuhudia nikikonda taratibu hadi kifo changu!”

Aliwaza prosper na aliponyanyua uso wake kumwangalia mzee nyonganyonga alishangaa kukuta sindano ikiwa imezama tumboni kwake mwenyewe.
“Nime…cho….shwa na ….kazi ya ku…..ua ….bina…damu wenza…..ngu!

Nita…..mwe..leza nini Mu….ngu ni heri nife sitaki kuitoa roho yako wa sababu huna hatia!” alisema mzee nyonganyonga akiangakua chini na mwili wake kukakamaa na ulimi kutoka nje.
“Mzee nyonganyonga umefanyua nini sasa? Kwanini umejiua wewe wakati ni mimi ninayestahili kufa?”

Aliuliza prosper huku akipiga kelele alishindwa kufanya lolote kwa sababu alibanwa na mashine mikononi na miguuni, alianza kupiga kelele kuomba msaada na muda mfupi baadaye waliingia maaskari wawili mmoja akiwa na barua mkononi.

“Vipi kimetokea nini tena?”
“Hata mimi nashangaa nilikuwa nimefumba macho nikisubiri kuchomwa sindano lakini mzee nyonganyonga hakufanya hivyo na nilipofumbua nilikuta sindano imezama tumboni mwake na akaanguka chini!”

“Kweli?”
“Ndiyo! Sasa mnafikiri ni mimi ndiye nimemchoma?”

“Hapana siyo hivyo ila….!”
“Ila nini?”
”Basi tuyaache hayo kakueleza kitu chochote kabla hajajichoma?”
“Alipaanguka chini alianza kusema maneno ingawa kwa shida!”

“Alisema maneno gani?”
“Alisema amechoshwa na kazi ya kuua binadamu wenzake na hakuwa na jambo la kumjibu Mungu!”
“Mungu wangu! Sasa kwanini asingesema tu akabadilishiwa kazi?”

Prosper alibaki ameduwaa akiwashangaa maaskari walionekana kupigwa na mshangao mkubwa na hawakujua ni nini cha kufanya, mzee nyonganyonga alikuwa amelala chini sakafuni, mikono na miguu yake ikiwa imenyooka kuelekea darini! Macho na ulimi wake yakiwa yametoka nje alitisha na picha hiyo ilimuonyesha prosper ni kifo cha aina gani ambacho angekufa.

Aliogopa kupita kiasi na kujikuta akitetemeka mwili mzima lakini kwa sababu alishaamua kufa ili kukwepa mateso ya gonjwa la Ukimwi prosper aliamua kuipuuzia picha aliyoiona sakafuni na kuwageukia maaskari waliokuwa ndani ya chumba hicho.

“Afande!” Aliita na maaskari wote waliokuwa wameinamisha nyuso zao chini wakiushangaa mwili wa mzee nyonganyonga uliolala sakafuni waligeuka kumwangalia.
“Unasemaje prosper?”Wote waliuliza kwa mpigo.

“Sasa mtafanya nini?”
“Kuhusu?”
”Mimi nataka kufa!”
“Hautakufa tena prosper bado una siku nyingi sana za kuishi!”

”Si uchukue hilo bomba la sindano uvute dawa nyingine unidunge kipi kinachokushinda kama mnaogopa basi nitoeni hapa kwenye mashine nijidunge mwenyewe!”

“Haiwezekani tena prosper serikali imeamua kusitisha hukumu ya kifo uliyopewa tena una bahati nafikiri Mungu alikuwa hajapanga ufe kwa sababu mkeo amefika hapa na barua zikiwa zimebaki sekunde ishirini tu!

Hapakuwa na njia yoyote ya kuwahi kama mzee Nyonganyonga asingejiua mwenyewe!” alisema mmoja wa maaskari.
“Ni nini mnasema nini nyinyi mbona siwaelewi?”

“Barua ni hii hapa imetoka kwa mwanasheria mkuu wa serikali hivyo haiwezekani kukuchoma sindano tena!”
“Hebu niione hiyo barua!”Alisema prosper kwa ukali kiasi kwamba maaskari walishindwa kumwelewa kwa sababu alitakiwa kufurahia kukwepa kifo akiwa juu ya kitanda cha mauti.

Askari aliyekuwa na barua hiyo mikononi alimsogezea prosper na kuifungua, prosper alianza kuipitia taratibu tangu mwanzo hadi mwisho wa barua lakini badala ya kufurahia alianza kupiga kelele.

“NATAKA KUFA!NATAKA KUFA! MIMI NATAKA KUFA SITAKI TENA KUISHI!” aliongea kwa sauti ya juu huku akijaribu kujitoa kwenye mashine iliyoshika mikono na miguu yake.

Maaskari waliamua kumfungua prosper akatoka kitandani na kusimama wima, wakiwa hawa hili wala lile maaskari walishtukia prosper anatimua mbio kulifuata bomba lililokuwa chini lengo lake likiwa ni kujichoma nalo ili afe alilifikia na kulishika lakini kabla hajalinyanyua na kutimiza azma yake mguu wa askari ulisimama juu ya kiganja chake prosper alipiga kelele sababu ya maumivu aliyoyapata.

“Kwanini unataka kufanya hivyo lakini yaani badala ya kufurahia amenusurika kifo kimiujiza unataka kufanya ujinga?”

“Braza mimi ni mtu mzima na akili zangu ukiona nataka kufanya jambo jiulize mara mbili kuna tatizo gani, hakuna mtu anayetaka kufa binadamu wote tunapenda kuishi! Kwa hiyo niache mimi nifanye ninavyotaka!”

“Haiwezekani! Afande hebu mtoe huyu chumbani mpeleke katika chumba cha washauri nasha nafikiri utakuwa na tatizo ambalo ni vyema tukalifahamu!”


Askari magereza alimshika mkono prosper ambaye wakati huo aliendelea kulia mfululizo na kutoka naye hadi nje ya chumba cha kifo mbele kidogo aliingia naye katika chumba kilichoandikwa mlangoni “Ushauri Nasaha!” ambao walimkuta mama wa makamo akiwa amekaa nyuma ya meza kubwa.
“Vipi tena?”

“Hukumu yake ya kifo imesitishwa na serikali baada ya kugundulika dakika chache kabla ya kifo kuwa hakutenda kosa lililopelekea apewe hukumu hiyo!”
“Hongera sana kijana nakushauri ukitoka hapa uwe mwema mbele za Mungu kwani amekupa nafasi nyingine ya kunyoosha njia zako unasikia?”

“Usinipe hongera mama mimi sitaki kuishi na kama kuna uwezekano wa kuniua sasa hivi fanyeni hivyo haraka kwani nitajiua mwenyewe!”

Jipu la prosper lilimshtua mtoa ushauri nasaha, aligundua prosper alikuwa na tatizo kubwa lililohitaji muda mrefu wa kuongea naye!

“Kwanza hebu tufahamiane mimi naitwa mama Mpelumbe wewe mwenzangu unaitwa nani?” Mama huyo alianzaia mbali kidogo.

“Naitwa prosper!”
“Aisee wewe ndiye prosper?”
“Ndiyo mama ni vizuri ukiniita marehemu prosper sababu tayari nimeshakufa! Mimi ni maiti inayotembea!”
”Unamaanisha nini mwanangu?”
“Yaani mama hunielewi ninaposema mimi ni maiti inayotembea!”
‘Sikuelewi hata kidogo!”

“Na si mimi tu hivi sasa vijana wengi ni maiti zinazotembea! Ndiyo maana nataka kufa kwa sababu yaliyoko mbele yangu sitaweza kuyahimili!”
”Unamaanisha nini?”
Badala ya kujibu swali prosper aliyekuwa ametulia alianza kulia machozi.


Belinda alikaa nje ya gereza na mtoto wake mgongoni akiendelea kulia machozi!Alishangaa ni kwanini maaskari walichelewa kiasi hicho kurudi kutoka ndani, alijua kwa vyovyote mume wake alikuwa amekufa! Mawazo hayo yalimzidishia huzuni aliamini asingeweza kupambana na maisha peke yake aliumia juhudi zake zote za kumuokoa prosper zilikuwa zimegonga mwamba.

*Je, nini kitaendelea?*

Sent using Jamii Forums mobile app
 
*Sehemu ya 22*


Ndani na nje ya moyo wake Belinda hakutaka kabisa prosper anyongwe alitaka aendelee kuishi tena wakiwa pamoja na mtoto wao wakisubiri kifo chao ifike n aikiwezekana wafe siku moja! Hakuwa tayari kubaki peke yake duniani akiteseka kumuuguza mtoto wao Alicia pia hakutaka kufa na kumwacha Alicia peke yake duniani kama yeye ndiye angetangulia.

Kifo ni kifo lakini sitaki Prospar afe ghafla kiasi hicho nataka niwe naye niteseke naye hadi mwisho wa maisha yangu! Prospar hana hatia na hastahili kunyongwa!” aliwaza Belinda .

Mom where is dady? Whay is not coming? I wanna talk to him please mom tell them to call him for us”(mama baba yuko wapi? Kwa nini haji? Nataka kuongea naye waambie basi wamwite!) Alicia aliyekuwa mgongoni kwa mama yake alisema maneno yaliyomuumiza moyo mama yake.

Badala ya kujibu swali lake Belinda aliangua kilio kilichomfanya mtoto wake bila kujua kilichomliza mama yake naye aanze kulia. Alicia alimpenda mno mama yake hakuwa tayari kumwona akilia.

“Mom stop Craying! Remember Christimas is just one day from to day and dady will be home to celeblate with us, that is what he told me the last time we came here! He also peomised to buy me a new dress!”

(Mama acha kulia! Kumbuka krisimasi ni siku moja tu kuanzia leo na baba aliahidi kuja nyumbani kusherekea pamoja nasi! Aliniambia hivyo mara ya mwisho tulipokuja na aliniahidi ataninunulia gauni jipya!) Alicia alisema hayo bila kujua siku hiyo ndio baba yake alikuwa ananyongwa.!

Kufungwa na kuhukumiwa kifo cha prosper ndicho Belinda hakutata kabisa mtoto wake akijue aliamua kulifanya jambo hilo siri kwa sababu hakutaka kumuumiza moyo mtoto wake aliyeonekana kumpenda sana baba yake, siku zote alimwambia baba yake alikuwa gerezani kufanya kazi na alikuwa hapewi likizo sababu ya kazi nyingi.

Ghafla akiwa katika mawazo hayo Belinda alitupa macho yake upande wake wa kulia kupitia katika dirisha lenye nondo nene lililokuwa pembeni yake, alishuhudia mwili wa mtu ukiwa umebebwa na maaskari wasiopungua wanne ukitolewa ndani ya chumba na kupelekwa upande wa pili kulikokuwa na kijumba kidogo, ukutani mwa kijumba hicho kuliandikwa maneno “Mortuary!”

Picha hiyo ilimwonyesha Belinda wazi kuwa tayari mume na baba wa mtoto wake tayari alishaaga dunia, aliiona dunia imekuwa giza mwili wake ukalegea na ghafla alianguka chini akiwa na mtoto wake mgongoni.

“Mom!Mom! Mom! What has happen with you? Have you fallen asleep? Please wake up mom is time to go home and do chrismas preparation remember dad will be here in no time!(Mama! Mama!Mama! nini kimekupata? Umelala usingizi? Amka basi muda wa kwenda nyumban kujiandaa na krismasi umefika na baba atakuja hapa muda si mrefu!)Alicia aliongea huku akimpiga piga mama yake mgongoni lakini Belinda hakushtuka.

Mzee Nyonganyonga 
akawa amekufa tena 
kifo cha kujichoma mwenyewe kwa sindano ya sumu iliyomaanishwa kumuua Prosper kama hukumu ya mauaji aliyoyafanya! Kushuhudia kwa maiti yake ikitolewa katika chumba cha mauaji kulimfanya Belinda aamini kuwa aliyekufa ni mumewe Prosper, alilia na kuanguka chini akawa amepoteza fahamu!

Belinda alibaki katika hali hiyo kwa kipindi kirefu bila kujitingisha mtoto wake Alicia akiwa mgongoni kwake, Maaskari Magereza waliokuwa karibu walimfungua nguo aliyombebea mtoto na kumtoa mgongoni! Belinda aliendelea kulala chini bila kufahamu yoyote, maaskari walianza kufikiri alikuwa amepoteza uhai.

Kila mtu alishtuka na hapakuwa na njia nyingine ya kufanya zaidi ya kumkimbiza hospitali, maaskari wawili wenye nguvu walimbeba Belinda mikononi mwao na kuanza kumpeleka kwenye zahanati ya gereza ingawa hakuwa mfungwa.

“Kawaje huyu?” Daktari aliuliza baada tu ya Belinda kuingizwa hospitali.
“Ameanguka ghafla na kupoteza fahamu baada ya kumwona mume wake akitolewa chumba cha mauaji baada ya kunyongwa!”

“Mume wake kanyongwa?”
“Ndiyo!”
“Ni yupi huyo?”
“Ni mfungwa mmoja aliletwa hapa kutoka Tabora!”
“Aliitwa nani?”
“Prosper!”
“He! Yule kijana mpole mrefu?”

“Ndiyo!”
“Kanyongwa yule?”
“Kweli kabisa! Na huyu ndiye mke wake alipouona tu mwili wa mume wake ukitolewa chumba cha mauaji akapoteza fahamu!”

Daktari alisikitishwa sana na habari hizo lakini wakati maongezi hayo bado aliendelea kumpa Belinda matibabu! Dripu za maji ziliwekwa katika mishipa yake na kitanda kilinyanyuliwa miguuni ili damu nyingi zaidi itiririke kwenda kwenye ubongo, hatua ambazo daktari aliamini zingemrejeshea Belinda fahamu zake.

Dakika kama kumi hivi baadaye daktari akiwa bado katika masikitiko juu ya habari aliyopewa, mlango wa wodi ulifunguliwa na kijana mmoja mrefu akaingia akiongozana na maaskari magereza wawili, daktari alipomwona kijana huyo aliguna na kumwangalia askari magereza waliyekuwa naye.

“Mh! Si ulisema kijana huyu ndiye amekufa?” Daktari aliuliza na askari magereza aliyekuwa ameinama alinyanyua uso wake kuangalia mlangoni, hakuamini macho yake yalipokutana na sura ya Prosper.

“Hata mimi nashangaa sasa ni nani aliyekufa maana nilishuhudia mwili wa mtu ukitolea chumba cha mauaji na mtu aliyetakiwa kufa leo ni huyu au kimetokea nini maafande wenzangu?”

Aliuliza askari huyo akiwaangalia maaskari wenzake waliosimama pembeni mwa kitanda alicholala Belinda.

“Ni habari ya kusikitisha sana!”
“Habari gani hiyo?”
“Mzee Nyonganyonga ndiye kafa!”
“Kafa? Kafa vipi?”
“Yeye ndiye kajichoma na sindano ya sumu badala ya kumchoma huyu kijana!”

“Mungu wangu kwanini?”
“Eti amechoka kuua watu wasio na hatia!”
“Nyie nani kawaeleza?”
“Katueleza huyuhuyu kijana!”
“Kwahiyo?”

“Maiti yake iko chumba cha maiti!”
“Na huyu Prosper itakuwaje sasa?”
“Ana bahati sana kwani kuna barua kutoka kwa Mwanasheria mkuu wa serikali adhabu yake imesitishwa mpaka uchunguzi wa kina ufanyike, kuna habari kuwa hakuyafanya mauaji!”

“Mkuu wa gereza ana taarifa hizo?”
“Ndiyo na tumetoka ofisini kwake sasa hivi tumemwacha anashughulikia barua ya kumwachia huru kijana huyu!”

Wakati maongezi hayo yakiendelea Prosper akiwa amembeba mtoto wake Alicia mikononi alikaa pembeni mwa kitanda alicholala Belinda akimwangalia kwa macho ya huruma hasa aliposikia habari kuwa alianguka na kupoteza fahamu baada ya kuona maiti aliyodhani ni yake ikitolewa chumba cha mauaji.

“Daktari mke wangu atapona kweli?”
“Atapona tu wala usiwe na wasiwasi!”
Baadaye daktari ambaye pia alikuwa askari magereza pamoja na maaskari wengine waliondoka na kumwacha Prosper peke yake pamoja na mtoto wake Alicia aliyeonekana kuwa na furaha kupita kiasi kuwa na baba yake.

“Dady wake mom up! We have to go home for Christimas, why has she slept all that time?”(Baba mwamshe mama, twende nyumbani kusherehekea Krisimasi kwanini amelala muda wote huo?) Alicia aliuliza akiwa amemkumbatia baba yake.

Prosper alielewa ni kiasi gani mtoto wake hakuuelewa ukweli juu ya mambo yaliyokuwa yakitokea, hakutaka kumweleza ukweli aliendelea kumbembeleza atulie mpaka mama yake akiamka ndio waondoke kwenda nyumbani.

*Itaendelea.*
 
*Sehemu ya 23*


Kama dakika arobaini na tano hivi baada ya daktari kuondoka, Belinda alijitingisha na kugeukia upande wa pili kisha akayafungua macho yake na kuanza kuangaza huku na kule chumbani, macho yake yalitua moja kwa moja usoni kwa Prosper!Hakuamini kama alichokuwa akikiona kilikuwa ni kweli, ilikuwa ni kama ndoto.

“Prosper!Prosper ni wewe au ni mzimu wako?”
“Ni mimi darling!”
“Lakini umekufa?”
“Sijafa bado niko hai!”
“Aliyekufa ni nani?”
“Ni aliyetaka kuniua badala ya kuniua mimi alijiua yeye!”

“Kweli au naota ndoto?”
“Huoti ndoto ni kweli kabisa Belinda bado niko hai ingawa natamani kufa!”

“Kwanini unasema hivyo Prosper?”
“Nakiogopa kifo kilichoko mbele yangu! Kifo cha Ukimwi ni kifo cha mateso mno ni heri ningechomwa sindano ya sumu nikafa!”

“Prosper kwanini unasema maneno mabaya kiasi hicho? Wala hunifikiri mimi na mwanao wakati hata sisi tutakufa kifo cha aina hiyohiyo? Kwanini sasa tusiishi pamoja mpaka Mungu atakapochukua maisha yetu ikiwezekana siku moja?”

“Sawa Belinda lakini....!”
“Lakini nini Prosper hutupendi mimi na mtoto wako?”
“Nawapenda Belinda na sitatamani kufa tena nimebadilisha msimamo wangu nashukuru kwa kuokoa maisha yangu Belinda!”

Dripu aliyokuwa nayo mkononi ilishachomoka, maji yote yalikuwa yakimwagika chini! Haikuwa rahisi kwa Belinda kuamini alikuwa pamoja na Prosper na wangeendelea kuishi maisha yao yote wakisubiri kifo!

Yeye pia alikiogopa kifo cha Ukimwi lakini kufa pamoja na Prosper haikuwa huzuni kubwa, alijua wazi ni yeye na mchezo wake wa kishoga ndiye aliuleta ugonjwa huo katika familia yao lakini alishamsamehe na hakutaka kukumbuka tena.
*******************

Saa kumi ya jioni siku hiyohiyo waliruhusiwa kuondoka gerezani na kwenda nyumbani kwa Belinda, Prosper hakuamini alipoiona nyumba ambayo Belinda aliishi, ilipambwa na ilikuwa na kila kitu ndani! Maisha ya mke wake yalionekana kuwa mazuri.
“Belinda nyumba yako ni nzuri sana!”

“Sio yangu!”
“Ni ya nani sasa?”
“Sema nyumba yetu sio nyumba yangu!”
“Ok! Nyumba yetu!”

“Tutaishi hapa sote watatu mpaka mwisho wa uhai wetu, baba alinipa nyumba mbili lakini moja ilibidi niiuze ili kupata pesa za kumlipa huyu wakili wetu!” Belinda alisema akimuonyesha wakili wao aliyekuwa amesimama pembeni.

“Ahsante mke wangu kweli penzi lako ni la dhati ni hakika nimechangia sana kuyaharibu maisha yako nafikiri utanisamehe!”
“Usijali Prosper Mungu alipanga tuwe wawili maishani mwetu!”

Wakili wao hakukaa sana kitu kama masaa mawili baada ya chakula cha usiku aliondoka akiahidi kuonana nao kama wangemhitaji ni usiku wa siku hiyo ndiyo Prosper alilala usingizi mororo katika miaka karibu kumi iliyopita kabla.

“Prosper ni miaka mingi imepita nakumbuka mara ya mwisho ni wakati mtoto huyu anapatikana! Ninakuhitaji mume wangu!” Alisema Belinda kwa sauti ya mahaba.

“Hapana Belinda haiwezekani hata kidogo siwezi kuua mtoto mwingine asiye na hatia! Makosa makubwa niliyafanya kwa Alicia na sasa atakufa bila hatia kwa makosa yangu mimi”

“Lakini tunaweza kutumia kinga!”
“Kama ni hivyo sawa lakini sipo tayari upate mimba na kuzaa mtoto mwingine tutakuwa tunaua damu isiyo na hatia!”
“Sawa!”

Baada ya kukubaliana walifurahi kama mke na mume baada ya miaka mingi ya kuishi mbali na kila mmoja wao, ulikuwa ni usiku wa raha mno kwa Belinda pamoja na Prosper kujaa upele na ukurutu mwili mzima bado Belinda alifaidi kila alichofanyiwa.

Siku iliyofuata Belinda alimpeleka Prosper hospitali na kuishughulikia afya yake, katika muda wa miezi miwili tayari afya yake ilisharejea na Prosper alipendeza na kuvutia, uzuri wa sura yake ulianza kurudi.

Kwa pesa kidogo iliyobaki Belinda aliendelea na biashara ya kwenda Zanzibar kununua bidhaa na kuzikopesha maofisini, pesa iliyopatikana kama faida iliwasaidia kuendesha maisha na kutunza akiba kidogo.
****************

Miaka mitatu baadaye:
“Acha mimi niende Zanzibar wewe baki na mtoto si unamwona hali yake ilivyo?” Prosper alimwambia mkewe.

“Kwa kweli inabidi nibaki maana hali yake inazidi kuwa mbaya siku hadi siku, haya majipu ndiyo yanayomsumbua zaidi!”
“Itabidi kesho umpeleke tena kwa daktari ili wambadilishie dawa anazotumia!”

“Sawa mume wangu! Ila nunua mikoba ya kutosha maana mahitaji ni mengi hasa kwenye duka la Kariakoo”
Biashara yao ilishakuwa na maisha yao yalikuwa bora, walipata kila walichokitaka!Kasoro pekee waliyokuwa nayo ni afya ya mtoto wao Alicia, mtoto huyo aliugua karibu kila siku na alibadilisha magonjwa kama nguo.

Prosper alijisikia wajibu kwa ugonjwa wa mtoto wake, alijua bila yeye kujihusisha na ushoga gerezani na Savimbi, Alicia asingekuwa mgonjwa!

Jambo hilo lilimuumiza sana moyo wake hasa alipoona jinsi mtoto wake alivyozidi kukonda.
Kila siku alipokwenda shule alirudishwa nyumbani akiwa hoi, ilikuwa akisoma wiki moja wiki ya pili anakuwa hoi kitandani!

Belinda na mume wake walijua kilichokuwa kikimsumbua mtoto wao lakini hata siku moja hawakudiriki kumwambia ukweli ingawa mara kwa mara Alicia aliuliza juu ya ugonjwa uliokuwa ukimsumbua.

“Mama mimi naumwa nini mbona siponi? Kila siku naumwa! Mbona mimi siko kama watoto wenzangu?”
“Utapona tu mwanangu!”
“Ona haya majipu kila siku yanaota na kupona mpaka lini itakuwa hivi?”

Maswali ya Alicia kwa mama yake yalikuwa mengi kupita kiasi na yalimuumiza sana moyo Belinda!Alishindwa amjibu nini mtoto wake kwa maswali aliyoulizwa ingawa alijua siku moja ni lazima wamwambie ukweli na hakujua siku hiyo ingekuwa lini.

*Je, nini kitaendelea?*
 
Back
Top Bottom