Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,165
Mtunzi Juma Hiza 01
ILIKUWA ni siku ya Desemba 23, tena siku mbili tu kabla ya Christmas, dunia nzima ilijawa na shamrashamra za Sikukuu hiyo ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo, maduka mengi jijini Dar yalijaa watu wakinunua nguo na vitu mbalimbali kwa ajili ya sikukuu.
Magari mengi yalisongamana barabarani na kufanya usafiri wa magari kuwa mgumu, sehemu ya kuendesha kwa dakika moja yalikwenda kwa dakika thelathini! Madereva wengi waliyaacha magari yao na kutembea kwa miguu.
“Mary’s boy child Jesus Christ was born on Christmas day, up now here the Angel sing the king was born to day, a man will live forever more because of Christmas day!....” Nyimbo za Chrismas zilitawala kila kona ya jiji la Dar es Salaam.
Siku hiyo Belinda alikuwa ndani ya daladala la kuelekea Segerea akiwa na mtoto wake wa miaka mitano, Alicia! Alikuwa mtoto mzuri mno na mwenye sura ya kumvutia kila aliyemwangalia, wengi walisema alichukua sura ya baba yake! Kila mtu ndani ya basi hilo alitamani kumbeba Alicia lakini Alicia mwenyewe alikataa na kubaki mikononi mwa Belinda mama yake.
Pamoja na uzuri wote huo wa mtoto Alicia alikuwa na kasoro katika mwili wake, hakupitisha hata wiki mbili bila kuugua! Homa na kikohozi hazikumpa nafasi katika maisha yake, Belinda alishatafuta tiba sehemu mbalimbali lakini hakufanikiwa kupata tiba kamili ya mtoto wake.
“Mom what are we going to do for Christmas? Are you going to buy me new clothes? My friends are going shopping with their parents? Mom are you going to take me shopping too? (Mama sisi tutafanya nini Christmas?
Je, utaninunulia nguo mpya? Rafiki zangu wanakwenda madukani kununua nguo mpya na wazazi wao, utanipeleka na mimi kununua nguo?) Alicia alimuuliza mama yake huku akimpigapiga mgongoni.
Belinda alijifanya kutosikia maswali ya mwanae hii ni kwa sababu hakuwa na pesa wala jibu la kumpa mtoto wake ambaye kwa umri wake alikuwa hajaambiwa na mtu yeyote juu ya kilichoendelea katika maisha yao! Kwake kila kitu kilikuwa sawa.
“Mummy! Please answer my question!” (mama tafadhali jibu swali langu!)
“What have you said my dear daughter, I didn’t hear you! (Umesemaje kweli binti yangu mpendwa? Sikukusikia).
“Are you going to buy me new clothes this Christmas?” (utaninunulia nguo mpya Chrismas hii?”) Alicia aliuliza tena lakini bado mama yake aliendelea kukaa kimya, ni kweli hakuwa na jibu la swali hilo, hakuwa na pesa za kumnunulia mtoto wake nguo mpya! Si nguo tu bali hata pesa ya chakula cha siku ya Christmas hakuwa nayo!
Siku hiyo asubuhi walikuwa ndani ya daladala wakielekea kwenye gereza la Segerea kupitia Tabata, ilikuwa ni siku ya mwisho kwenda kuonana na mumewe Prosper aliyekuwa amekaa gerezani kwa muda wa miaka minane baada ya kuhukumiwa kifo kwa kosa la kumuua baba yake mzazi kwa kumpiga na mchi usoni.
Kwa kutumia mawakili Belinda alijitahidi kwa kila alichokuwa nacho kuhakikisha mume wake anatoka gerezani au kufungwa kifungo cha maisha lakini haikuwezekana, Prosper alikaa gerezani muda wote wa miaka minane akisubiri siku ya kunyongwa.
Ni siku iliyofuata ndiyo Prosper alitegemea kufa kwa kupigwa sindano ya sumu aina ya Digoxmait ili kumwondoa kabisa duniani, Prosper hakuwahi kuua kabla lakini kwa kosa hilo moja alihukumiwa kifo!
Ni siku hiyo ya Desemba 23 ndiyo Belinda alitegemea kupewa nafasi ya mwisho kuongea na mumewe kabla ya kifo chake! Ilikuwa ni siku ya huzuni kubwa mno katika maisha yake na kila alipomfikiria mume wake roho ilimuuma sana na kufanya aanze kulia!
Hakuna mtu aliyewahi kumwambia Alicia kuwa baba yake asingerudi tena nyumbani na angenyongwa na kufa! Kila siku walipomtembelea gerezani, ili kumuondolea huzuni Alicia aliyeonekana kumpenda mno baba yake, Prosper alimwambia mwanaye Alicia kuwa angetoka gerezani siku si nyingi, jibu hilo ndilo mtoto aliliweka kichwani, hakuwahi kufahamu kabisa kuwa baba yake tayari alishahukumiwa kifo na alikuwa akisubiri siku yake.
“Mum! Mummy! Dad told me he is going to be with us during Christmas dont you remember? (Mama! Mama! Baba aliniambia atakuja nyumbani Christmas hii? Haukumbuki?) alipaza sauti Alicia mpaka watu ndani ya gari wakageuza shingo zao kumwangalia.
Belinda alishindwa kumjibu kitu chochote badala yake machozi yalianza kumtoka! Maneno ya mwanae yalimuumiza sana moyo alielewa wazi mtoto wake alikuwa haelewi chochote na asingeweza kumwambia ukweli kuwa baba yake alikuwa anakufa siku iliyofuata na walikuwa safarini kwenda gerezani kuagana naye kwa mara ya mwisho! Belinda aliendelea kulia kichinichini.
“Haya Segerea gerezani hapa, wa kushuka sogeeni mlangoni upesi msilete urembo wenu hapa” Alisema kondakta wa daladala na Belinda alisimama na kumshika Alicia mkono wakaanza kusogea mlangoni.
“Shusha hapo gerezani!” kondakta alipiga kelele na dereva akakanyaga breki na Belinda na mtoto wake wakateremka na kuanza kutembea kuelekea gereza la Segerea lililokuwa umbali wa kama mita mia tatu kutoka kituo cha basi.
Walipofika gerezani walionyeshwa chumba maalumu kilichoandaliwa kwa ajili yao kuongea na Prosper, Belinda aliketi chumbani humo akiwa amembeba mtoto wake miguuni, muda wote machozi yaliendelea kumbubujika na kufanya azilowanishe nguo zake.
“Mom stop crying, what are we doing here? Let’s go and see dady!”(Mama acha kulia, tunafanya nini hapa twende tukamwone baba!) Alicia aliendelea kumwambia mama yake.
Kabla Belinda hajatoa neno lolote mara mlango uliokuwa pembeni yao ulifunguliwa akajitokeza askari jela mmoja akiwa na bunduki mkononi mwake na baadaye aliingia mtu akiwa amevaa nguo nyeupe juu hadi chini na akiwa amefungwa kitambaa cheusi usoni, Belinda alipomwangalia mtu huyo alimtambua alikuwa ni mume wake Prosper. Alinyanyuka kitini na kuanza kumfuata.
“We mama hebu kaa chini usubiri utaratibu wa gereza kwanza, usituletee mambo ya uraiani, hapa ni gerezani kuna sheria zake vinginevyo na wewe utajikuta unanyea ndoo!” Askari alimfokea Belinda.
Bila ubishi Belinda alirudi kinyumenyume na kuketi kitini kwake akatulia akisubiri taratibu zote za gereza zimalizike. Prosper alikalishwa chini na kufunguliwa kitambaa usoni, alipowaona mke wake na mwanae alitokwa na machozi, huruma ilimshika kwani alijua kuwa hiyo ndiyo ilikuwa siku yake ya mwisho kuonana na familia yake.
“Mama una saa moja tu na nusu ya kuongea sisi tunaondoka tukirudi tutamchukua mumewe, utumieni vizuri muda mliopewa na mpange mambo vizuri! Hii ni nafasi ya mwisho kuonana na mumeo duniani!” Alisema askari mmoja na baadaye kutoka nje na kufunga mlango nyuma yake.
“Belinda umekuja mama mtoto wangu?”
“Ndiyo Prosper!”
“Hebu kabla ya yote na tupige magoti tumwombe Mungu kwani hii ni siku yetu ya mwisho katika dunia hii kuwa pamoja!” Prosper alimwambia mkewe na wote watatu walipiga magoti chini, Prosper akiwa na pingu zake mikononi na miguuni.
Je, nini kitaendelea?
ILIKUWA ni siku ya Desemba 23, tena siku mbili tu kabla ya Christmas, dunia nzima ilijawa na shamrashamra za Sikukuu hiyo ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo, maduka mengi jijini Dar yalijaa watu wakinunua nguo na vitu mbalimbali kwa ajili ya sikukuu.
Magari mengi yalisongamana barabarani na kufanya usafiri wa magari kuwa mgumu, sehemu ya kuendesha kwa dakika moja yalikwenda kwa dakika thelathini! Madereva wengi waliyaacha magari yao na kutembea kwa miguu.
“Mary’s boy child Jesus Christ was born on Christmas day, up now here the Angel sing the king was born to day, a man will live forever more because of Christmas day!....” Nyimbo za Chrismas zilitawala kila kona ya jiji la Dar es Salaam.
Siku hiyo Belinda alikuwa ndani ya daladala la kuelekea Segerea akiwa na mtoto wake wa miaka mitano, Alicia! Alikuwa mtoto mzuri mno na mwenye sura ya kumvutia kila aliyemwangalia, wengi walisema alichukua sura ya baba yake! Kila mtu ndani ya basi hilo alitamani kumbeba Alicia lakini Alicia mwenyewe alikataa na kubaki mikononi mwa Belinda mama yake.
Pamoja na uzuri wote huo wa mtoto Alicia alikuwa na kasoro katika mwili wake, hakupitisha hata wiki mbili bila kuugua! Homa na kikohozi hazikumpa nafasi katika maisha yake, Belinda alishatafuta tiba sehemu mbalimbali lakini hakufanikiwa kupata tiba kamili ya mtoto wake.
“Mom what are we going to do for Christmas? Are you going to buy me new clothes? My friends are going shopping with their parents? Mom are you going to take me shopping too? (Mama sisi tutafanya nini Christmas?
Je, utaninunulia nguo mpya? Rafiki zangu wanakwenda madukani kununua nguo mpya na wazazi wao, utanipeleka na mimi kununua nguo?) Alicia alimuuliza mama yake huku akimpigapiga mgongoni.
Belinda alijifanya kutosikia maswali ya mwanae hii ni kwa sababu hakuwa na pesa wala jibu la kumpa mtoto wake ambaye kwa umri wake alikuwa hajaambiwa na mtu yeyote juu ya kilichoendelea katika maisha yao! Kwake kila kitu kilikuwa sawa.
“Mummy! Please answer my question!” (mama tafadhali jibu swali langu!)
“What have you said my dear daughter, I didn’t hear you! (Umesemaje kweli binti yangu mpendwa? Sikukusikia).
“Are you going to buy me new clothes this Christmas?” (utaninunulia nguo mpya Chrismas hii?”) Alicia aliuliza tena lakini bado mama yake aliendelea kukaa kimya, ni kweli hakuwa na jibu la swali hilo, hakuwa na pesa za kumnunulia mtoto wake nguo mpya! Si nguo tu bali hata pesa ya chakula cha siku ya Christmas hakuwa nayo!
Siku hiyo asubuhi walikuwa ndani ya daladala wakielekea kwenye gereza la Segerea kupitia Tabata, ilikuwa ni siku ya mwisho kwenda kuonana na mumewe Prosper aliyekuwa amekaa gerezani kwa muda wa miaka minane baada ya kuhukumiwa kifo kwa kosa la kumuua baba yake mzazi kwa kumpiga na mchi usoni.
Kwa kutumia mawakili Belinda alijitahidi kwa kila alichokuwa nacho kuhakikisha mume wake anatoka gerezani au kufungwa kifungo cha maisha lakini haikuwezekana, Prosper alikaa gerezani muda wote wa miaka minane akisubiri siku ya kunyongwa.
Ni siku iliyofuata ndiyo Prosper alitegemea kufa kwa kupigwa sindano ya sumu aina ya Digoxmait ili kumwondoa kabisa duniani, Prosper hakuwahi kuua kabla lakini kwa kosa hilo moja alihukumiwa kifo!
Ni siku hiyo ya Desemba 23 ndiyo Belinda alitegemea kupewa nafasi ya mwisho kuongea na mumewe kabla ya kifo chake! Ilikuwa ni siku ya huzuni kubwa mno katika maisha yake na kila alipomfikiria mume wake roho ilimuuma sana na kufanya aanze kulia!
Hakuna mtu aliyewahi kumwambia Alicia kuwa baba yake asingerudi tena nyumbani na angenyongwa na kufa! Kila siku walipomtembelea gerezani, ili kumuondolea huzuni Alicia aliyeonekana kumpenda mno baba yake, Prosper alimwambia mwanaye Alicia kuwa angetoka gerezani siku si nyingi, jibu hilo ndilo mtoto aliliweka kichwani, hakuwahi kufahamu kabisa kuwa baba yake tayari alishahukumiwa kifo na alikuwa akisubiri siku yake.
“Mum! Mummy! Dad told me he is going to be with us during Christmas dont you remember? (Mama! Mama! Baba aliniambia atakuja nyumbani Christmas hii? Haukumbuki?) alipaza sauti Alicia mpaka watu ndani ya gari wakageuza shingo zao kumwangalia.
Belinda alishindwa kumjibu kitu chochote badala yake machozi yalianza kumtoka! Maneno ya mwanae yalimuumiza sana moyo alielewa wazi mtoto wake alikuwa haelewi chochote na asingeweza kumwambia ukweli kuwa baba yake alikuwa anakufa siku iliyofuata na walikuwa safarini kwenda gerezani kuagana naye kwa mara ya mwisho! Belinda aliendelea kulia kichinichini.
“Haya Segerea gerezani hapa, wa kushuka sogeeni mlangoni upesi msilete urembo wenu hapa” Alisema kondakta wa daladala na Belinda alisimama na kumshika Alicia mkono wakaanza kusogea mlangoni.
“Shusha hapo gerezani!” kondakta alipiga kelele na dereva akakanyaga breki na Belinda na mtoto wake wakateremka na kuanza kutembea kuelekea gereza la Segerea lililokuwa umbali wa kama mita mia tatu kutoka kituo cha basi.
Walipofika gerezani walionyeshwa chumba maalumu kilichoandaliwa kwa ajili yao kuongea na Prosper, Belinda aliketi chumbani humo akiwa amembeba mtoto wake miguuni, muda wote machozi yaliendelea kumbubujika na kufanya azilowanishe nguo zake.
“Mom stop crying, what are we doing here? Let’s go and see dady!”(Mama acha kulia, tunafanya nini hapa twende tukamwone baba!) Alicia aliendelea kumwambia mama yake.
Kabla Belinda hajatoa neno lolote mara mlango uliokuwa pembeni yao ulifunguliwa akajitokeza askari jela mmoja akiwa na bunduki mkononi mwake na baadaye aliingia mtu akiwa amevaa nguo nyeupe juu hadi chini na akiwa amefungwa kitambaa cheusi usoni, Belinda alipomwangalia mtu huyo alimtambua alikuwa ni mume wake Prosper. Alinyanyuka kitini na kuanza kumfuata.
“We mama hebu kaa chini usubiri utaratibu wa gereza kwanza, usituletee mambo ya uraiani, hapa ni gerezani kuna sheria zake vinginevyo na wewe utajikuta unanyea ndoo!” Askari alimfokea Belinda.
Bila ubishi Belinda alirudi kinyumenyume na kuketi kitini kwake akatulia akisubiri taratibu zote za gereza zimalizike. Prosper alikalishwa chini na kufunguliwa kitambaa usoni, alipowaona mke wake na mwanae alitokwa na machozi, huruma ilimshika kwani alijua kuwa hiyo ndiyo ilikuwa siku yake ya mwisho kuonana na familia yake.
“Mama una saa moja tu na nusu ya kuongea sisi tunaondoka tukirudi tutamchukua mumewe, utumieni vizuri muda mliopewa na mpange mambo vizuri! Hii ni nafasi ya mwisho kuonana na mumeo duniani!” Alisema askari mmoja na baadaye kutoka nje na kufunga mlango nyuma yake.
“Belinda umekuja mama mtoto wangu?”
“Ndiyo Prosper!”
“Hebu kabla ya yote na tupige magoti tumwombe Mungu kwani hii ni siku yetu ya mwisho katika dunia hii kuwa pamoja!” Prosper alimwambia mkewe na wote watatu walipiga magoti chini, Prosper akiwa na pingu zake mikononi na miguuni.
Je, nini kitaendelea?