marybaby
JF-Expert Member
- Apr 11, 2017
- 3,260
- 9,197
Hili zao la belinda lipo kweli.?
Au ndo wa mwisho kuzaliwa,?sio kwa mahaba hayo[emoji36]
Sent using Jamii Forums mobile app
Au ndo wa mwisho kuzaliwa,?sio kwa mahaba hayo[emoji36]
*Sehemu ya 08*
Dakika tano baadaye kengele ililia ndani ya gereza na Prosper alinyanyuka na kumkumbatia Belinda walipigana mabusu na kuagana! Mwili wa Prosper ulikuwa mchafu kupita kiasi alihisi Belinda angemwonea kinyaa lakini haikuwa hivyo, Belinda hakujali wala kuonyesha kushangazwa na hali hiyo alizidi kumkumbatia.
“Belinda ni lazima niende sasa muda wa kuongea na wewe umekwisha!”
“Sawa darling lakini jaribu kuwa mwangalifu sana na Savimbi siipendi tabia yake!”
Prosper hakujibu kitu alizidi kuinamisha kichwa chake chini kwa aibu jambo lililomfanya Belinda aendelee kupata uhakika kuwa kulikuwa na jambo kati yao!
Baada ya kuagana Belinda alitoka nje ya gereza na kuungana na wifi zake na safari ya kwenda stendi kupanda basi la kuwarudisha nyumbani ilianza, njia nzima Belinda alikuwa ni mwenye mawazo alifika akiwa amechoka na kujitupa kitandani ambako aliendelea kumlilia Prosper!
***************
Alikaa Tabora kwa wiki tatu bila wazazi wake kufahamu mahali alikokuwa, baba mzazi yake alishamtafuta kila mahali bila kumpata mpaka kukata tamaa! Alitangaza katika vyombo mbalimbali vya habari lakini bado hakufanikiwa kumpata binti yake, wengi walihisi Belinda alikufa lakini baba yake hakuliamini hilo.
Hatimaye mzee Thomson Komba baba yake Belinda aliamua kutangaza zawadi nono ya shilingi milioni kumi kwa mtu yeyote ambaye angefanikisha kupatikana kwa Belinda, wanakijiji wawili wa kijiji cha Tutuo walijitokeza na kwenda kutoa taarifa moja kwa moja kituo cha polisi Belinda akawa amekamatwa.
Siku aliyokamatwa aliiacha familia ya akina Prosper katika majonzi makubwa kwa sababu kwao mkombozi alikuwa ameondoka! Kukaa kwa Belinda katika familia hiyo kulipunguza sana shida zao za maisha, pesa yote aliyokuwa nayo aliitumia katika matumizi ya nyumbani na ni yeye pia aliyenunua dawa za mama yake Prosper.
Alichokifanya Belinda wakati wa kuondoka ni kumtupia Nyamizi dada yake Prosper shilingi elfu hamsini alizokuwa nazo katika mfuko wa suruali ili ziwasaidie.
“Wifi!Pesa hizo zitawasaidia!”
“Ahsante wifi, ahsante kwa kuja tafadhali utukumbuke!”
“Sawa wifi! Muangalieni sana mama sababu hali yake si nzuri!”
*****************
Belinda alichukuliwa kwa nguvu na kupakiwa ndani ya gari lililompeleka hadi Tabora ambako alisafirishwa kwa ndege ya kukodi hadi Dar es Salaam, alipokelewa na kupelekwa moja kwa moja kituo cha polisi ambako aliwekwa rumande na kukaa kwa siku tatu, alipotolewa aliendelea na adhabu nyingine kali nyumbani kwao.
Pamoja na adhabu hizo bado Belinda hakuwa tayari kueleza ukweli juu ya mahali alikokuwa, aliendelea kudanganya kuwa alikwenda kwao na rafiki yake msichana waliyesoma naye darasa moja!
“Bila kuaga?”
“Nisamehe baba!”
Na kweli Belinda alisamehewa na kuendelea na maisha kama kawaida nyumbani kwao lakini mawazo yake yote yalikuwa kwa Prosper aliyekuwa bado yupo gerezani, alimlilia na alishindwa kula kwa sababu yake! Alitamani kuwa na Prosper tena na hakujua kama katika maisha yake angeweza kumpenda mwanaume mwingine kama alivyompenda Prosper.
Belinda alikonda kwa mawazo na baba yake alimshangaa kwa mabadiliko ya afya ya mwili wake, hakuijua sababu ya tatizo hilo, alijitahidi kumpa mtoto wake kila alichotaka kama njia ya kumbembeleza akiamini Belinda alichukizwa na adhabu alizompa.
Chuo kilipofunguliwa wiki mbili baadaye Belinda alirudi tena Mlimani na kuendelea na masomo yake ya Sheria lakini kitabu kikawa kigumu kwake kwani kila alipomfikiria Prosper akili yake ilizidi kuchanganyika na kupoteza pointi.
Kitu kingine kilichomshangaza zaidi ni mabadiliko ya hali yake ya afya, alianza kujisikia mchovu kupita kiasi hasa nyakati za asubuhi, uchovu ulioambatana na kichefuchefu na alitapika sana asubuhi, matiti yake yalianza kuvimba! Mwanzoni alifikiri ni malaria lakini alipokwenda kupimwa damu yake ilikuwa safi.
Hali yake iliendelea kuwa mbaya na alipitiliza mwezi mmoja katika mpangilio wake wa hedhi! Hilo ndilo lilimchanganya zaidi hatimaye akaamua kupimwa kila kitu ndipo alipogundua kumbe alikuwa tayari ni mjamzito wa mwezi mmoja na nusu!
Belinda alichanganyikiwa, alishindwa kuelewa angemwambia nini mzee Thomson! Kila alipoufikiria ukali wa baba yake alizidi kuingiwa na hofu, alijua mzee yule angemuua, asingemwacha hai hata kidogo kwani hayo ndiyo yalikuwa maongezi yake ya kila siku.
“Mtoto wangu akipata mimba ni lazima nimpige risasi!”
Kila alipoikumbuka kauli hiyo ya baba yake alitetemeka mwili na hakujua ni kitu gani angefanya ili kujiepusha na hasira ya mzazi wake, alipoomba ushauri kwa rafiki zake walimwambia afanye kila alichoweza ili aitoe mimba hiyo kabla mambo hayajaharibika na mimba kuwa kubwa zaidi.
Jambo hilo lilimshinda Belinda, alikuwa na uhakika kabisa Prosper angenyongwa na asingemwona tena, alipenda abaki na ukumbusho wa Prosper mwanaume aliyempenda kuliko wanaume wengine wote duniani na ukumbusho pekee ulikuwa ni mtoto na Mungu alikuwa amelikubali hilo.
“Siwezi kuua mtoto wa Prosper lolote litakalokuwa na liwe!” Alisema Belinda.
Alivumilia na mimba yake chuoni mpaka ikafikisha miezi minne akawa haendi tena nyumbani kwao kila mwisho wa wiki, jambo lililowashtua ndugu zake na kuwafanya kaka zake waende shuleni kumuuliza lipi lilikuwa likimsumbua.
Ni hao ndio waliomgundua Belinda na mimba yake na bila hata kusita walizipeleka taarifa moja kwa moja kwa mzee Thomson! Belinda alihisi hilo lingetokea ni asubuhi ya siku iliyofuata tu alipopanda basi kwenda Tabora nyumbani kwao na Prosper kujificha mpaka azae mtoto wake.
******************
Belinda aliingia Tabora jioni ya saa kumi akiwa amechoka hoi bin taaban, hakutaka kupoteza muda hata kidogo mjini alipanda basi la mwisho kumpeleka hadi kijijini Tutuo! Hakuwa na mzigo mwingine zaidi ya begi lililojaa nguo zake mwenyewe, hakuwa na pesa zaidi ya shilingi elfu kumi aliyokuwa amebakiza.
Alijua wazi kuwa alikokuwa anakwenda kulikuwa na taabu kubwa na nzito ikimsubiri, alijua tangu siku hiyo asingepata msaada wowote kutoka kwa baba yake sababu alikuwa amemuudhi kupita kiasi! Isitoshe alijua wazi kuwa mama yake wa kambo na ndugu zake wangemjaza chuki baba yake ili azidi kumchukia.
“Lolote na liwe lakini sipo tayari kumuua mtoto wangu! Ni bora mimi niteseke lakini kiumbe hiki kizaliwe kama ni masomo nitaendelea nayo baadaye ingawa sina uhakika ni nani atanilipia ada!” Aliwaza Belinda wakati akitembea kuelekea nyumbani kwao na Prosper.
Alishangazwa na umati mkubwa wa watu aliouona alipokaribia nyumba yao, wanaume wengi walikuwa wamekaa katika miduara wakiota moto na wengine walionekana kula chakula! Belinda alishindwa kuelewa ni nini kilikuwa kimetokea.
Alipofika kwenye uwanja wa nyumba alishangaa kuwaona wifi zake wakija mbio huku wakilia machozi! Wote walimkumbatia huku wakimtaarifa kuwa mama yao alikuwa amefariki asubuhi ya siku hiyo.
“Mama amefariki leo! Na hapa tulipo hata pesa ya sanda tumekosa!” Nyamizi alimwambia Belinda baada ya kuketi chini huku akilia na kujifuta machozi.
“Ni heri umekufa wifi maana hapa ndani hatuna hata senti, nafikiri utatusaidia pesa kidogo tukanunue sanda na kuchonga jeneza!”
*Je, nini kitaendelea?*
Sent using Jamii Forums mobile app