Simulizi:Death Of Innocent

Simulizi:Death Of Innocent

*Sehemu ya 02.*


“Father in the name of Jesus and the mighty power of holly spirit, I thank you for every thing that happened in my life! Father you know how innocent I’m in this case, you know I didn’t kill anybody! But the entire world knows I’m a killer, tomorrow I’m dying leaving my wonderful wife and daughter behind me, protect them Lord, make me meet them in heaven! Father you know how much I Love my wife and how much I love my daughter Alicia too. It haunts me badly inside to learn that this is my last moment with them! I’m dying and leaving my Alicia and Belinda alone, but I know with you they will never be alone.....

(Baba katika jina la Yesu na uwezo wa Roho Mtakatifu ninakushukuru kwa kila kitu kilichotokea katika maisha yangu, baba ninajua ni kiasi gani unaelewa sina hatia katika suala hili, unajua wazi sikuua lakini dunia nzima inanijua mimi ni muuaji.

Kesho ninakufa nakuwaacha mke wangu mzuri na mwanangu nyuma yangu, baba uwalinde, nifanye nikutane nao Mbinguni, baba unajua ni kiasi gani ninampenda mke wangu na ni kiasi gani ninampenda binti yangu Alicia.

Inaniumiza vibaya kujua kuwa huu ni wakati wangu wa mwisho kuwa nao, ninajua ninakufa na kuwaacha Belinda na Alicia peke yao lakini ninafahamu wakiwa na wewe hawatakuwa wapweke milele.....) Alipofika hapo Prosper alishindwa kuendelea na kuanza kulia.

“Daddy what’s going to kill you? But you said you will be home this Christmas!” (Baba nini kitakuua, lakini si ulisema utakuwa nyumbani Christmas hii!”) Alicia aliuliza kwa mshangao ilikuwa ni mara ya kwanza kwake kusikia kuwa baba yake angekufa.

“My daughter Alicia let me reveal the truth to you today, the truth that even you mother never knew about!”(Mwanangu Alicia acha nikuonyesha ukweli wote leo, ukweli ambao hata mama yako hakuwahi kuufahamu!)

Baada ya kusema hayo huku Belinda na Alicia wakiendelea kulia, Prosper alisimulia kila kitu kilichotokea katika maisha yake na nini kilichopelekea awe gerezani, Belinda alionekana kufungua mdomo wake kwa mshangao wakati Prosper akielezea kilichotokea, siku zote alielewa kitu tofauti kabisa.

“Kwa hiyo hukumuua baba yako!”
“I didn’t kill him but my mom did!) (Sikumuua baba ni mama yangu aliyemuua baba)
“Why are you in Prison then? (Sasa kwanini upo gerezani).

“Nilimpenda sana mama yangu, sikutaka kitu kibaya kimtoe maana nikasema ni mimi ndiye niliyemuua baba ili tu mama yangu aachiwe huru na mimi nikawekwa gerezani, sikuwahi kukueleza hili Belinda lakini leo ni lazima nikuambie ukweli, nakufa sababu ya mama yangu ingawa naye hivi sasa ni marehemu, nitaonana naye ahera kesho! Nakupenda sana Belinda na kuomba umtunze sana mtoto wetu ingawa naye ni mgonjwa mara kwa mara lakini mpeleke hospitali ipo siku atapona!”

Hawakuongea kitu tena zaidi ya kuendelea kulia kwa pamoja muda mrefu mpaka askari walipokuja na kumfunga Prosper kwa kitambaa cheusi tena usoni, Belinda na Alicia walimkumbatia na kumbusu usoni kwa mara ya mwisho akaanza kuvutwa kutolewa chumbani.

“I love you Belinda! I love you Alicia! I will love you forever, see you in Heaven! (Nakupenda Belinda! Nakupenda Alicia, nitawapenda milele, tutaonana mbinguni!) alisema Prosper huku akivutwa na maaskari kutolewa chumbani.

Walipotoka chumbani huku wakilia Belinda na mtoto wake walinyoosha moja kwa moja hadi kituo cha basi, habari aliyoisikia siku hiyo kwa Prosper ilimsikitisha sana Belinda, alikuwa ameamua kwenda kufanya kila lililowezekana kumwona Mwanasheria Mkuu wa Serikali na kumsimulia juu ya jambo hilo, alipita ofisini kwa wakili wake na kumweleza na wote walinyoosha hadi ofisini kwa Mwanasheria Mkuu!

*********
“Nasikitika leo hamuwezi kumwona ana kazi nyingi sana!” alisema Katibu Muhtasi wake!”

“Hapana dada ni jambo muhimu sana linalohusu kifo, tusipomuona leo kesho mtu ananyongwa na ana uwezo wa kuzuia!” alijibu Belinda huku akilia machozi.

“Hebu subirini nimuulize?” alisema Katibu huyo na kunyanyua simu iliyokuwa mezani kwake, alisikika akiongea na mtu na alipoweka simu chini alimgeukia Belinda.

“Dada nakuhurumia ila sina jinsi ya kukusaidia, Mwanasheria amesema mje kesho saa nne kamili ataonana nanyi!”
“Mume wangu ananyongwa saa 4.30 tu dada!”

“Siwezi kulazimisha awaone kwa kweli huyo ni bosi wangu!”
Belinda na mwanaye waliondoka pale wakilia machozi na kwenda nyumbani kwao ambako Belinda chakula hakikulika wala usingizi haumwijia alikesha usiku mzima akisali kumwomba Mungu afanye miujiza yake.

******
Siku iliyofuata asubuhi na mapema Prosper alianza kuandaliwa kwa ajili ya kifo! Alipewa muda wa masaa mawili kusali na kusoma Biblia ili kutubu dhambi zake, ilipofika saa nne kamili alitolewa chumbani kwake akiwa amefungwa kitambaa cheusi usoni na kupelekwa katika chumba maalum cha kunyongea, kilichoitwa Death room, ambako alilazwa katika kitanda maalum tayari kwa kifo.

Mtaalam wa kuua aliyeitwa bwana Nyonganyonga ambaye kwake kutoa roho za watu ndio ilikuwa kazi yake, alisimama pembeni mwa kitanda cha kifo akimwangalia Prosper kwa huruma ni kwa mara ya kwanza katika kazi yake aliyoifanya kwa miaka 15 alijisikia kumwonea mtu huruma kiasi hicho!
“Kweli uliua?” Alimuuliza Prosper
“Sikuua?”
“Ila?”

“Ni mama yangu aliyeua mimi nilisema nimeua ili kumwokoa mama asife!”
“Kwa hiyo wewe upo tayari kufa kwa ajili ya mama yako?”
“Ni sawa tu!”

“Mama yako hivi sasa yupo wapi?”
“Alifariki kwa Kifua Kikuu muda mfupi baada ya kutoka gerezani!”
“Kwa hiyo upo tayari kufa?”
“Sawa tu!”

Bwana Nyonganyonga alikuwa tayari na sindano yake ya dawa ya Digoxmait Tayari kwa kumchoma Prosper ikitimia saa 4.30 juu ya alama!, sumu hiyo iliua kwa kuusimamisha moyo kusukuma damu.

Wakati huo tayari ilikuwa ni saa 4.20! Prosper alilala pale akisubiri kifo, zilikuwa zimebaki dakika kumi tu achomwe sindano ya sumu, alijaribu kukifikiria kifo na kushindwa kukielewa.

“Hivi inakuwaje mtu akifa, kweli nitawasahau Belinda na Alicia?” alijiuliza Prosper na picha ya mke na mtoto wake ilimwijia kichwani akasikia huzuni kubwa sana moyoni mwake! Alipotupa macho ukutani tayari ilikuwa saa 4.25 zilikuwa zimebaki dakika tano afe!

“Nichome hiyo sindano, nataka kufa unasubiri nini?” Prosper alisema katika hali ya kukata tamaa.

Je, nini kitaendelea?
Haya shangazi ndio naanza safari yangu hapa Shunie

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mahaba mahabani
*Sehemu ya 04.*


“Baba mwache mama! Kwanini unampiga hivyo si keshakufungulia mlango?”
“Wee unanishika unataka kunichangia na mama yako siyo?”

“Sitaki kukupiga baba lakini naomba usimpige mama kiasi hicho hana kosa!”
Wakati Prosper akiongea maneno hayo tayari Kasanda na Nyamizi walishafika na kumnyanyua mama yao aliyekuwa amelala chini akiwa amepoteza fahamu huku damu nyingi zikimtoka mdomoni, midomo yake ya juu na chini ilikuwa imevimba kwa ngumi aliyopigwa na mume wake, wakambeba na kumpeleka chumbani kwao ambako walimmwagia maji akarejewa na fahamu.
“Mama twende polisi!” Kasanda alimshauri mama yake.

“Hapana watoto wangu tukienda polisi baba yenu atafungwa! isitoshe sisi Wanyamwezi hatutakiwi kabisa kushtaki polisi tunapopigwa na waume zetu”

Watu wote katika kijiji cha Tutuo barabara ya kwenda Sikonge walikoishi Prosper na wazazi wake walitambua ukorofi wa mzee Kabaka na hakuna mtu aliyediriki kumkemea, kila mtu alimuogopa.

Kama ungefanikiwa kukutana na mama Kalunde, sio siri machozi yangekutoka, alikuwa ni mama wa makamo, mrefu mwenye umbile la kitutsi,rangi ya ngozi yake ilikuwa nyeusi lakini iliyojaa makovu mengi, kwa kumwangalia ungegundua kabisa kuwa mama huyo aliwahi kuwa tishio wakati wa ujana wake!

Alikuwa ni mama mwenye mateso, alipigwa karibu kila siku na mume wake,hakuwa na sikio moja tayari lilishakatwa na mumewe! Jicho lake la kulia lilikuwa chongo baada ya kupasuliwa na mume wake wakati wa kupigwa miaka miwili kabla ya siku hiyo! Alikuwa ni mama aliyepata mateso makubwa mno katika maisha yake ya ndoa.

Wakati hayo yote yakitokea Prosper alikuwa na umri wa miaka 17 akimalizia kidato cha nne katika shule ya sekondari ya Sikonge, pamoja na matatizo aliyokuwa nayo alifanikiwa kuchaguliwa kuendelea na kidato cha tano katika shule ya sekondari ya St.Magreth ilikuwa ni shule ya bweni, na ilikuwa ni lazima aende kuishi bwenini akiwaacha dada zake Kasanda na Nyamizi pamoja na wazazi wake.

“Prosper tutaweza kweli kumhimili baba akimpiga mama?”
“Mungu atawasaidia dada zangu sina budi kwenda shule ili niwasaidie baadaye!” Prosper aliwaeleza dada zake wakati wa kuagana, akaondoka kwenda zake Moshi shuleni.

Alipofika shuleni kwa mara ya kwanza alikuwa amechelewa na kilichomchelewesha zaidi ilikuwa ni ada, mama yake Kalunde alilazimika kufanya vibarua katika mashamba ya watu ili aweze kupata pesa za kumwezesha Prosper kwenda shule! Baba yake hakujali kabisa.

“Prosper mwanangu usifanye michezo shuleni, si unaona maisha yetu yalivyo na unaona nilivyohangaika? Baba yako hana msaada wowote, yeye ni pombe kila siku na kunipiga mimi tu, familia nzima tunakutegemea wewe uje kuwa mkombozi wetu kajitahidi mwanangu!”
“Sitakuangusha mama nakuahidi! “
“Sawa mwanangu!”

Darasa lao lilikuwa na wafunzi hamsini na mbili kati yao wasichana wakiwa kumi na saba! Ni Prosper peke yake aliyeonekana kuwa na uwezo mdogo kifedha na watu wengi walimdharau, alikuwa na nguo zilizochanika na madaftari yake yalikuwa ni ya kurasa shirini na nne ambayo hayakutumiwa na wanafunzi wengi shuleni hapo! Yalidaiwa kuwa ya watoto wa shule za msingi.

Pamoja na umasikini wake Prosper alijitahidi sana na masomo kama alivyomuahidi mama yake na hiyo ni kwa sababu aliifahamu familia yake, alitaka asome ili apate uwezo wa kuwakomboa ndugu zake, barua zilizokuja kutoka nyumbani kwao zilimweleza juu ya kipigo alichopata mama yake na Prosper alilia.

Wanafunzi wengi walimtenga sababu ya umasikini wake isipokuwa msichana mmoja tu aliyeitwa Belinda!Msichana huyo alimsaidia Prosper kwa vitu vingi shuleni ikiwemo Sabuni, mafuta na hata sukari na wakatokea kuwa marafiki wakubwa.

Katika mtihani wa mwisho wa muhula aliwashangaza wengi pale alipoibuka na kushika namba ya kwanza kati ya wafunzi wote! Ni matokeo hayo ndiyo yalianza kumpa heshima na marafiki wengi shuleni.
******

Shule zilipofungwa kwa sababu Prosper hakuwa na nauli ya kumrudisha hadi nyumbani kwao Tabora, ilibidi abaki shuleni peke yake akijisomea! Alimkumbuka sana mama yake na alitaka kwenda nyumbani lakini kwa sababu hakuwa na nauli alilazimika kubaki peke yake shule nzima.

Shule zilipofunguliwa wanafunzi wote walirejea shuleni na yeye na Belinda msichana aliyeonekana kutoka familia tajiri jijini Dar es Salaam, walisoma na kufanya kila kitu pamoja Belinda alikuwa miongoni mwa wasichana wagumu kuelewa masomo yao, lakini Prosper alitumia muda wake mwingi kumfundisha hatimaye akawa miongoni mwa wasichana waliofanya vizuri katika mitihani yao.

Mwisho wa muhula wa pili Prosper alishika tena namba ya kwanza darasani kwake na Belinda aliibuka katika kumi bora! Kila mtu mpaka walimu wake walishangaa,hilo liliukomaza zaidi uhusiano wao.

“Prosper utakwenda Tabora likizo hii?”
“Mimi? Mimi? Hapana sitakwenda!”
“Kwanini?”

“Sina nauli ya kunipeleka nyumbani nendeni tu mtanikuta!”
“Hapana Prosper this time ni lazima uende!”

“Nitakwenda na nini sina nauli Belinda?”
“Nitakupa nauli ya kukupeleka na kukurudisha!” Alisema Belinda.

Prosper hakuamini aligeuka na kumwangalia Belinda usoni, wote wawili walijikuta wakitabasamu na baadaye kukumbatiana na kuanza kupigana mabusu usoni, Belinda alijaribu kuupenyeza ulimi wake kuuingiza mdomoni kwa Prosper lakini Prosper aliuma meno yake kuonyesha hakupenda kitu hicho kitokee!

“Belinda unataka kufanya nini?”
“Nakupenda Prosper tafadhali tunyonyane ndimi!”

“Nitatapika Belinda sijawahi kufanya kitu kama hicho hata siku moja!”
Belinda alishindwa kuendelea lakini alijua ni kwanini Prosper alisema hivyo, alimwachia na wakaendelea na safari yao kuelekea mabwenini kujipumzisha wakisubiri siku inayofuata.

Asubuhi kitu cha kwanza alichofanya Belinda ni kumkabidhi Prosper kiasi cha shilingi 50,000 kwa ajili ya nauli ya kumpeleka Tabora na kumrudisha shuleni.
“Belinda mbona pesa hizi ni nyingi sana!”
“Zitakazobaki utawanunulia wazazi na ndugu zako zawadi!”

“Ahsante Belinda, sikutegemea!”
“Ahsante wewe kwani bila wewe mimi nisingefanikiwa kimasomo? Isitoshe nakupenda Prosper huwezi kupata taabu wakati mimi nina kitu!”

“Belinda mzazi wako ni nani hasa hapa nchini?” Ilibidi Prosper aulize, sababu alishangazwa na msichana mdogo kama Belinda kuwa na kiasi kile chapesa.

Belinda alimweleza kila kitu kilichokuwepo katika maisha yake, alieleza pia juu ya utajiri wa baba yake na jinsi baba yake alivyompenda sababu alikuwa mtoto pekee wa kike! Hakuacha kumweleza juu ya mama yake wa kambo.

“Nina kila kitu nyumbani isipokuwa upendo wa mama, mama yangu wa kambo ananitesa sana, hanipendi amewafanya hata kaka zangu wa kambo pia wanichukie!”

“Unafikiri ni kwanini?”
“Kwa sababu wanajua baba ananipenda na kuna uwezekano wa kupata sehemu kubwa sana ya mali yake akifa, hiyo nafikiri ndiyo sababu kubwa!”
“Pole!”

“Ahsante, lakini nataka uelewe nakupenda na tukirudi kutoka likizo safari hii nataka kila mtu aelewe jambo hapa shuleni ili wavulana waache kunisumbua!”

“Huogopi kuchekwa Belinda!”
“Kwanini?”
“Sababu mimi ni masikini!”
“Nakupenda kwa jinsi ulivyo Prosper!”
Ni kweli Prosper alikuwa na sura ya kumvutia kila mwanamke kilichomsumbua kilikuwa ni umasikini.

Je, nini kitaendelea?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Savimbi kwa mbaaali anapata jiko[emoji85]
*Sehemu ya 05*


Prosper alikata tiketi ya treni na kusafiri hadi Tabora mjini ambako alipanda mabasi ya kumpeleka hadi nyumbani kwao Tutuo, kiasi cha kilometa sabini hivi kutoka Tabora mjini, njia nzima alimfikiria mama yake alitaka sana kumwona!

Ulikuwa umepita muda mrefu bila kuonane naye! Mawazo juu ya dada zake na baba yake hayakumuumiza kichwa sana, alimuwazia mama yake zaidi, alimpenda sana na hapakuwa na mtu mwingine kama mama maishani kwake!

Aliposhushwa na basi kituoni kitu cha kwanza alichofanya ni kukimbia dukani na kununua vitenge doti tatu kwa ajili ya mama yake na pia alinunua magauni mawili kwa ajili ya dada zake, Nyamizi na Kasanda! Hakusahau kumnunulia baba yake suruali nzuri! Moyo wake ulijaa furaha, alikuwa na hamu kubwa mno ya kuiona familia yake tena.

Baada ya manunuzi hayo alinyoosha moja kwa moja kwenda nyumbani kwao,njiani akiwa amebeba begi lake alishangaa jinsi ambavyo watu walimwangalia na kuonyesha masikitiko.

Alipofika nyumbani kwao hakuna mtu aliyejitokeza kumpokea, mlango wa nyumba ulikuwa wazi, ilibidi aingie hadi ndani akiliita jina la mama yake, lakini hakuitikiwa, mwisho alianza kuita majina la dada zake lakini bado ilikuwa kimya.

Wakati bado akijiuliza maswali kichwani mwake alitokea rafiki yake mkubwa aliyeitwa Kategile na kusimama mbele yake.

“Pole sana Prosper bahati mbaya umechelewa mazishi!”
“Ya nani?” Aliuliza kwa mshangao Prosper.

“Baba yako!”
“Baba?”
“Ndiyo!”
“Baba kafariki lini?”
“Wiki iliyopita!”

Prosper alianza kulia na majirani wengine zaidi walifika na kuanza kumpa pole, walishangaa kuwa hakuwa na taarifa hizo!”
“Sasa mama na ndugu zangu wapo wapi?”

“Wapo kituo cha polisi kati mjini Tabora”
“Wamefanya nini?”
“Ni wao ndio walimpiga baba yako na kumuua!”

Siku iliyofuata asubuhi Prosper alikwenda moja kwa moja kituo cha polisi kati kuwaona ndugu zake pamoja na mama yake, alilia machozi alipomwona mama yake akiwa mahabusu, aliomba kuongea naye akaruhusiwa na wakapewa chumba yeye na mama yake pamoja na dada zake waongee.

“Mama kweli mlimuua baba?”
“Mwanangu nililazimika kufanya hivyo kwani alichukua kisu na kunikata sikio langu la pili…..”Mama yake Prosper alianza kulia.

“Alilitoa?”
“Halipo mwanangu, nimepoteza masikini yangu yote mawili baba yako alikuwa katili mno alistahili kufa na ninakiri nimemuua!”

“Ulimuua na nini?”
“Nilimpiga na mchi kichwani akaanguka na kufa! Huo ndio ukweli mwanangu!”
“Mama ulishindwa kweli kufuata ushauri wangu?”

“Nisamehe mwanangu!”
“Mama hautafia gerezani ni heri nifungwe mimi na kunyongwa lakini wewe uwe huru nakupenda mno mama!” Alisema Prosper huku akilia.

Baada ya maongezi Prosper alirejea mjini ambako alikwenda moja kwa moja kituo cha polisi kati mjini Tabora.

“Naomba kuonana na mkuu wa kituo!”
“Wewe nani na una shida gani?”
“Nina maongezi marefu kidogo siwezi kukueleza wewe!”
Alionyeshwa ofisi ya mkuu wa kituo na kuingia.

“Shikamoo mzee!”
“Marahaba nikusaidie nini kijana!”
“Mzee unakumbuka mzee Kabaka aliyeuawa siku chache zilizopita?”
“Ndiyo si yule aliyeuawa na mke wake?”

“Ndiyo! Yule ni baba yangu na aliyemuua si mama yangu ni mimi! Nilitoroka baada ya kitendo hicho na ninakueleza wazi kuwa nimerudi ili mama yangu aachiwe mimi ndiye niwekwe rumande!”
“Kweli?”

“Huo ndio ukweli ni mimi niliyempiga baba na mchi kichwani akafa!”
“Kwanini?”
“Kwa sababu alikuwa anamtesa mama yetu!”

“Mungu wangu!Afande Charles!”
“Naam Afande!”
“Hebu njoo hapa mara moja!”
Sekunde tano tu tayari askari alisimama mbele ya meza ya mkuu wa kituo.
“Ndiyo afande!”

“Mchukue huyu kijana umpeleke rumande, kumbe ndiye aliyemuua baba yake kule Tutuo na sisi tukawakamata mama yake na dada zake sasa amejileta mwenyewe! Peleka mahabusu haraka na mama yake na dada zake waachiwe mara moja?”
“Sawa afande!”

Askari alimnyanyua Prosper na kumzaba vibao kadhaa usoni, kisha akamchukua na kupelekwa chumba cha mahabusu, muda mfupi baadaye alishuhudia mama yake na dada zake wakitoka mahabusu wakati wanatoka kituoni walisikia sauti ya Prosper ikiita kutoka mahabusu.

“Mama!Mama! Acha mimi nife huku lakini wewe uwe huru baba alikutesa mno na ulikuwa na haki ya ku....!”
“Masikini mwanangu, umefanya nini tena?” Aliuliza mama yake Prosper huku akilia.

Hakuna mtu aliyekuwa tayari kuamini yaliyotokea 
yalikuwa kweli , Prosper alikuwa ameyatoa maisha yake kwa ajili ya mama yake! Ulikuwa ni upendo mkubwa mno kwa binadamu kuonyesha, wengi waliamini ni Yesu peke yake aliyeweza kulifanya hilo, Prosper alikuwa ameudhihirishia ulimwengu kuwa hata binadamu anaweza kuutoa uhai wake kwa ajili ya mwenzake.

“Namhurumia sana Prosper sikupenda ajiingize katika suala hili ni heri ningenyongwa kwa sababu ndiyo niliyemuua baba yenu! Nitafanya nini mimi Ili Prosper atoke mahabusu?” Alihoji mama Angelina huku akilia.

Alilia usiku na mchana kwa siku tatu na hakula chakula kabisa zaidi ya maji katika siku zote hizo, Nyamizi na Kasanda walimbembeleza mama yao lakini hakukubali, alikonda na kupoteza uzito mwingi sana mwilini mwake, sababu ya kumlilia Prosper.
*********************
Mahabusu:

Prosper alikuwa amekaa ndani ya chumba kidogo cha mahabusu mjini Tabora, kilichotoa harufu kali na mbaya ya mikojo! Tangu aingie ndani ya mahabusu hiyo siku mbili kabla alikuwa hajaongea na mtu yeyote kati ya watu wote waliokuwemo.

Alikaa peke yake kwenye moja ya kona za mahabusu hiyo akiwa na mawazo mengi kichwani mwake.
“Acha nife mimi si mama yangu!” Aliongea kwa sauti kubwa Prosper na mzee aliyekuwa karibu yake aligutuka na kumgeukia.

“Kijana mbona unaongea peke yako?”
“Mh! Hapana mzee! Unajua? Mimi!......” Prosper aliongea maneno mengi yaliyochanganyika ambayo hayakutoa jibu la moja kwa moja kwa swali aliloulizwa!

“Niambie kijana ni kitu gani kimekufanya uje hapa mahabusu?”

“Shikamoo mzee!” Prosper aliamkia.
“Marahaba, hebusasa nieleze tatizo lililokufanya uje humu!”
“NIMEUA!”
“Umeua? Watu wangapi?”
“Mtu mmoja tena ni baba yangu!”
“Kha! Hilo ndilo linakufanya ulie? Mbona mimi nimeua watu hamsini na mbili na nimetulia tu!”

“Watu hamsini! Umewanyonga?”
“Hapana, nilizamisha mtumbwi tuliokuwa tukisafiria na watu wote wakafa mimi tu nikaokoka!”
“Kwanini ulifanya hivyo?”

“Nilitaka kuiba pesa zao, wote walikuwa ni wafanyabiashara wakitokea Burundi kuja Kigoma, baada ya mtumbwi kuzama nilichukua mifuko yao ya pesa na kuogelea nayo hadi ufukweni ambako nilikodisha gari likanileta hadi hapa Tabora lakini nilipoingia tu mjini nikakamatwa na ninajua nitahukumiwa kunyongwa lakini bado silii sasa wewe unalia kitu gani na umeua mtu mmoja tu?

Nyamaza bwana usitupigie kelele usikigeuze chumba hiki kliniki, humu wanakaa wanaume bwana!”
“Sawa mzee!”

“Una miaka mingapi kijana?”
“Nina miaka 19!”
“Unaitwa nani?”

“Ninaitwa Prosper! Wewe unaitwa nani?”
“Ninaitwa Savimbi, ulimuuaje baba yako?”
“Nilimpiga na mtwangio kichwani!”
“Kwanini?”

“Sababu alikuwa akimtesa sana mama yangu!”
“Unasoma?”
“Ndiyo!”
“Shule gani?”
“St Magreth huko Moshi nipo kidato cha tano!”

“Sasa hivi shule tena basi! Maisha yako yatakuwa ya gerezani ambako kuna mateso makubwa sana lakini kwa sababu unakwenda na mimi usiwe na wasiwasi nitakusidia, utakula chakula kizuri, utalala mahali pazuri, unavuta sigara?”

“Hapana!”
“Bangi?”
“Hapana!”
“Sawa, lakini kila kitu nitakupatia, utakuwa lakini unalala karibu na mimi sawa?”

“Sawa nitashukuru sana!”
“Umeshaota ndevu?” Jambazi alimuuliza.
“ Zimeanza kuota kidogokidogo!”
“Aisee hebu nione!” Jambazi ali anza kumpapasa Prosper kidevu, ilikuwa kizani hakuna mtu aliyeona kitendo hicho kikiendelea.

“Mzee unafanya kitu gani hicho?”
Ghafla mlango wa mahabusu ulifunguliwa na majina ya watu kadha yakaanza kutajwa, waliosikia majina yao walitoka mmoja baada ya mwingine hadi nje ambako walikuta maaskari wawili wenye bunduki wakiwasubiri na kuwalinda.
“Haya wa mwisho ni Savimbi Mfugambwa,hebu toka nje upesi muuaji mkubwa wee!”

Je, nini kitaendelea?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shunie anti ss twaenda sawa[emoji8]
*Sehemu ya 07*


Jumapili ilikuwa siku sita mbele yao, Belinda hakuwa na njia nyingine kumwona Prosper zaidi ya kusubiri mpaka siku hiyo ifike! Maisha yalikuwa magumu sana kwake kuendelea kusubiri lakini hakuwa na la kufanya aliishi nyumbani kwao Prosper akifanya kazi zote za nyumbani na alitumia pesa alizokuwa nazo kutatua baadhi ya matatizo katika familia hiyo.

Ni yeye alimpeleka mama yake Prosper hospitali ya Kitete mjini Tabora kupimwa, daktari aliamua kumpima makohozi, baada ya kuhisi alikuwa na kifua kikuu na alipigwa X-ray ya kifua na kuonekana mapafu yake yalikuwa yameharibika kabisa.

Makohozi yake yalipopimwa kwa muda wa siku tatu yaligungulika kuwa na wadudu wa kifua kikuu na kuanzishiwa matibabu!Angelina alimshukuru Belinda kupita kiasi.

Siku ya Jumapili ilipofika wote waliondoka kwenda gerezani Isanga, moyo wa Belinda ulikuwa ukidunda kwa nguvu na hakujua nini kingetokea baada ya kukutana na Prosper alishindwa kupata picha halisi ya Prosper kwa wakati huo lakini aliamini bado alikuwa ni kijana mwenye sura nzuri kama alivyokuwa awali.

Walipofika gerezani waliandikisha majini yao na watu waliotaka kuwatembelea, taratibu zote hizo kwa Belinda zilikuwa ni kumchelewesha kumwona Prosper! Baada ya kujiandikisha walionyeshwa chumba maalum cha kumsubiri Prosper aje na kuongea naye!

Dakika kumi baadaye wakiwa wamekaa, Belinda alishuhudia kijana mmoja mwembamba mrefu akiingia chumbani humo, urefu wake ulikuwa sawa na Prosper lakini unene wa mwili na ngozi yake vilikuwa tofauti,alijaa ukurutu mwili mzima! Aliingia chumba akiongozana na mtu mmoja mwenye mwili mkubwa na ndevu nyingi.

Kijana huyo alipotupa macho chumbani akiwaangalia watu waliokuwepo, ghafla aliruka na kukimbia moja kwa moja kuelekea mahali alipokuwa amekaa Belinda! Alipomfikia ndipo Belinda aligundua kijana huyo alikuwa Prosper lakini katika hali mbaya.

“Belinda umefikaje huku?”
“Prosper ni wewe? Umekuwaje hivi mpenzi wangu?”

Waliangushana hadi chini na kuanza kulia, Angelina pamoja na binti zake Nyamizi na Kasanda walishindwa kujizuia na kujikuta wakiangua kilio, mwanaume aliyeambatana na Prosper alikwenda na kumvuta Prosper na kumtoa mikononi mwa Belinda.

“Ha! Hebu achianeni!” Alisema mwanaume huyo ambaye baadaye Belinda alimtambua kwa jina la Savimbi.
“Kwanini?” Prosper aliuliza.
“Kwani huyu msichana ni nani?”
“Huyu ni mpenzi wangu!”
“Nani amekuambia unatakiwa uwe na mpenzi?”

“Savimbi mimi sitakii,niachie bwana niongee na Belinda wangu!”
Sura ya Savimbi ilibadilika na ghafla bila hata kuuliza alimnyanyua Prosper na kuanza kumvuta kumrudisha ndani ya gereza, Belinda alilia na kushindwa kabisa kuelewa kilichokuwepo kati ya Savimbi na Prosper wote walibaki wameangaliana bila kujua la kufanya!

Belinda hakuamini 
alichokiona alishangaa 
ni kwanini mwanaume huyo amchukue Prosper kabla hajamaliza kiu ya maongezi naye, alifikiria sana na kujikuta akilia.

Alishindwa kuelewa ni kitu gani kiliendelea kati ya Prosper na mwanaume aliyemchukua kwa nguvu ukumbini na Prosper alionekana kutokuwa na sauti kabisa mbele ya mwanaume huyo.

Kichwa cha Belinda kilihisi kitu fulani lakini hakuwa na uhakika nacho sana na alishindwa kupitisha moja kwa moja kuwa kulikuwa na uhusiano wa kishoga kati ya Prosper na mwanaume huyo!

“Haiwezekani Prosper ninavyomfahamu hawezi kufanya hivyo!” Aliwaza Belinda!
Hapakuwa na sababu ya wao kuendelea kubaki gerezani siku hiyo, walilazimika kuondoka kwenda hadi stendi ambako walipanda basi na kurudi tena kijijini Tutuo!

Njiani Belinda aliwaza mambo mengi sana juu ya kifo cha baba yake Prosper na alishindwa kuelewa ilikuwaje mpaka Prosper akafikia uamuzi huo wa kikatili, mama yake Prosper ilibidi aeleze kila kitu kuhusu ukatili aliofanyiwa na mumewe na hatua aliyoichukua prosper kumkingia mama yake.
“kwanini hamkwenda mahakamani mama?”

“Mwanamke wa Kinyamwezi hatakiwi kumshtaki mume wake hata kama akipigwa mwanangu!”

“Hivi mama yule mwanaume aliyekuja na Prosper pale gerezani ni nani?”
“Ni rafiki mkubwa wa Prosper anaitwa Savimbi kila mara tukienda gerezani huwa anakuja naye!”

“Mh! Mbona jina lake linatisha?”
“Hivyo ndivyo anavyoitwa!”

Walifika kijijini saa tisa mchana na Belinda aliendelea kuishi kijijini kwa wiki nyingine zaidi akisubiri Jumapili ifike ili aende gerezani kumwona tena Prosper, siku ilipofika walikwenda tena gerezani siku hiyo mama yake Prosper hakwenda kwa sababu hali yake haikuwa nzuri kifua kilimbana sana na alikuwa ameshindwa hata kuhema.

Walikwenda Belinda na dada zake Prosper peke yao na walifanikiwa kuonana na Prosper lakini siku hiyo alikuja peke yake bila Savimbi na kusalimiana nao, dada zake walionekana kushangaa.

“Leo Savimbi yupo wapi?” Nyamizi alimuuliza Prosper.
“Alipigana na Mnyapara jana!”
“Kwanini?”

“Kwa sababu Mnyapara alinipa ugali mkubwa na mboga yenye mafuta!”
“Ndio wakapigana?”
“Ndiyo!”

Belinda alizidi kuyaamini mawazo yake, ilikuwa si rahisi watu wapigane sababu ya Prosper kupewa ugali!Roho ya Belinda iliumia sana na kujikuta akilia alitaka kusema kitu lakini alishindwa sababu dada zake walikuwa pale.

“Wifi zangu mnaweza kunipa nafasi kidogo tu niongee na kaka yenu faragha?”

“hakuna shida wifi!” Walijibu na wote wakatoka nje wakiwaacha prosper na Belinda peke yao chumbani, kilikuwa ni chumba chenye mwanga mdogo.
“Prosper pamoja na matatizo yote yaliyokupata bado nakupenda!”

“Hata mimi nakupenda pia Belinda na sasa ninaamini hunidanganyi penzi lako kwangu ni kweli tupu ingawa nasikitika kuwa nitafia gerezani,bila hivyo tungeoana na kuzaa watoto wetu Belinda!”

“Usiwe na wasiwasi Prosper bado nina uhakika tutaoana!”
“Tutaoanaje wakati mimi tayari nilishahukumiwa kunyongwa?”

“Usijali muujiza wa Mungu utatokea na nikirudi nyumbani nitamshawishi baba yangu anipe pesa ili nikutafutie wakili ajaribu kukutoa gerezani!”
“Baba yako atakubali kweli?”
“Nina uhakika baba atakubali wala usiwe na wasiwasi mpenzi!”

Wote wawili waliangaliana na kujikuta wakitokwa na machozi ya uchungu! Kumbukumbu kubwa sana juu ya maisha yao ilikuja vichwani mwao, mambo mengi waliyoyafanya shuleni na kufurahia maisha yalirejea akilini mwao, Belinda alihisi mapenzi makali sana yakiutwaa tena moyoni mwake!

Kweli alimpenda Prosper kuliko kitu kingine chochote, ni wanaume wengi walishamfuata kumtaka mapenzi lakini hakuwakubali moyo wake ulimpenda Prosper kijana masikini tena aliyekuwa gerezani wakati huo.

Kitu kama sumaku kilijitokeza katikati yao na kujikuta wamekumbatiana na kuanza kupapasana miili yao! Kwa mara ya kwanza katika maisha yao tangu wafahamiane walijikuta wakitamaniana kimwili na mambo yaliyofuata katika muda wa dakika tano ndani ya chumba hicho hayaandikiki wala kuelezeka ila ilikuwa ni raha ambayo wote wawili waliipata kwa mara ya kwanza maishani mwao.

“Proper ahsante! Ninakupenda sana Prosper na sijui nitaishije bila wewe!” Alisema Belinda huku akilia machozi.

“Nakupenda pia Belinda na kama nilivyokueleza bila haya matatizo tungeoana na kuwa mke na mume!”
“Usiwe na wasiwasi Prosper tutaoana tu!” Belinda aliendelea kusisitiza alichokisema awali.

“Hivi sasa unasoma wapi?’
“Mimi?”
“Ndiyo!”
“Baada ya kumaliza kidato cha sita nilijiunga na chuo kikuu cha Dar es Salaam ambako ninasoma Sheria!”

“Kweli?”
“Ndiyo!”
“Unataka kuwa mwanasheria Belinda?”
“Ndiyo!”
“Soma sana uje utusaidie!”

Je, nini kitaendelea?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
*Sehemu ya 08*


Dakika tano baadaye kengele ililia ndani ya gereza na Prosper alinyanyuka na kumkumbatia Belinda walipigana mabusu na kuagana! Mwili wa Prosper ulikuwa mchafu kupita kiasi alihisi Belinda angemwonea kinyaa lakini haikuwa hivyo, Belinda hakujali wala kuonyesha kushangazwa na hali hiyo alizidi kumkumbatia.

“Belinda ni lazima niende sasa muda wa kuongea na wewe umekwisha!”
“Sawa darling lakini jaribu kuwa mwangalifu sana na Savimbi siipendi tabia yake!”

Prosper hakujibu kitu alizidi kuinamisha kichwa chake chini kwa aibu jambo lililomfanya Belinda aendelee kupata uhakika kuwa kulikuwa na jambo kati yao!

Baada ya kuagana Belinda alitoka nje ya gereza na kuungana na wifi zake na safari ya kwenda stendi kupanda basi la kuwarudisha nyumbani ilianza, njia nzima Belinda alikuwa ni mwenye mawazo alifika akiwa amechoka na kujitupa kitandani ambako aliendelea kumlilia Prosper!
***************

Alikaa Tabora kwa wiki tatu bila wazazi wake kufahamu mahali alikokuwa, baba mzazi yake alishamtafuta kila mahali bila kumpata mpaka kukata tamaa! Alitangaza katika vyombo mbalimbali vya habari lakini bado hakufanikiwa kumpata binti yake, wengi walihisi Belinda alikufa lakini baba yake hakuliamini hilo.

Hatimaye mzee Thomson Komba baba yake Belinda aliamua kutangaza zawadi nono ya shilingi milioni kumi kwa mtu yeyote ambaye angefanikisha kupatikana kwa Belinda, wanakijiji wawili wa kijiji cha Tutuo walijitokeza na kwenda kutoa taarifa moja kwa moja kituo cha polisi Belinda akawa amekamatwa.

Siku aliyokamatwa aliiacha familia ya akina Prosper katika majonzi makubwa kwa sababu kwao mkombozi alikuwa ameondoka! Kukaa kwa Belinda katika familia hiyo kulipunguza sana shida zao za maisha, pesa yote aliyokuwa nayo aliitumia katika matumizi ya nyumbani na ni yeye pia aliyenunua dawa za mama yake Prosper.

Alichokifanya Belinda wakati wa kuondoka ni kumtupia Nyamizi dada yake Prosper shilingi elfu hamsini alizokuwa nazo katika mfuko wa suruali ili ziwasaidie.

“Wifi!Pesa hizo zitawasaidia!”
“Ahsante wifi, ahsante kwa kuja tafadhali utukumbuke!”
“Sawa wifi! Muangalieni sana mama sababu hali yake si nzuri!”
*****************

Belinda alichukuliwa kwa nguvu na kupakiwa ndani ya gari lililompeleka hadi Tabora ambako alisafirishwa kwa ndege ya kukodi hadi Dar es Salaam, alipokelewa na kupelekwa moja kwa moja kituo cha polisi ambako aliwekwa rumande na kukaa kwa siku tatu, alipotolewa aliendelea na adhabu nyingine kali nyumbani kwao.

Pamoja na adhabu hizo bado Belinda hakuwa tayari kueleza ukweli juu ya mahali alikokuwa, aliendelea kudanganya kuwa alikwenda kwao na rafiki yake msichana waliyesoma naye darasa moja!
“Bila kuaga?”
“Nisamehe baba!”

Na kweli Belinda alisamehewa na kuendelea na maisha kama kawaida nyumbani kwao lakini mawazo yake yote yalikuwa kwa Prosper aliyekuwa bado yupo gerezani, alimlilia na alishindwa kula kwa sababu yake! Alitamani kuwa na Prosper tena na hakujua kama katika maisha yake angeweza kumpenda mwanaume mwingine kama alivyompenda Prosper.

Belinda alikonda kwa mawazo na baba yake alimshangaa kwa mabadiliko ya afya ya mwili wake, hakuijua sababu ya tatizo hilo, alijitahidi kumpa mtoto wake kila alichotaka kama njia ya kumbembeleza akiamini Belinda alichukizwa na adhabu alizompa.

Chuo kilipofunguliwa wiki mbili baadaye Belinda alirudi tena Mlimani na kuendelea na masomo yake ya Sheria lakini kitabu kikawa kigumu kwake kwani kila alipomfikiria Prosper akili yake ilizidi kuchanganyika na kupoteza pointi.

Kitu kingine kilichomshangaza zaidi ni mabadiliko ya hali yake ya afya, alianza kujisikia mchovu kupita kiasi hasa nyakati za asubuhi, uchovu ulioambatana na kichefuchefu na alitapika sana asubuhi, matiti yake yalianza kuvimba! Mwanzoni alifikiri ni malaria lakini alipokwenda kupimwa damu yake ilikuwa safi.

Hali yake iliendelea kuwa mbaya na alipitiliza mwezi mmoja katika mpangilio wake wa hedhi! Hilo ndilo lilimchanganya zaidi hatimaye akaamua kupimwa kila kitu ndipo alipogundua kumbe alikuwa tayari ni mjamzito wa mwezi mmoja na nusu!

Belinda alichanganyikiwa, alishindwa kuelewa angemwambia nini mzee Thomson! Kila alipoufikiria ukali wa baba yake alizidi kuingiwa na hofu, alijua mzee yule angemuua, asingemwacha hai hata kidogo kwani hayo ndiyo yalikuwa maongezi yake ya kila siku.

“Mtoto wangu akipata mimba ni lazima nimpige risasi!”

Kila alipoikumbuka kauli hiyo ya baba yake alitetemeka mwili na hakujua ni kitu gani angefanya ili kujiepusha na hasira ya mzazi wake, alipoomba ushauri kwa rafiki zake walimwambia afanye kila alichoweza ili aitoe mimba hiyo kabla mambo hayajaharibika na mimba kuwa kubwa zaidi.

Jambo hilo lilimshinda Belinda, alikuwa na uhakika kabisa Prosper angenyongwa na asingemwona tena, alipenda abaki na ukumbusho wa Prosper mwanaume aliyempenda kuliko wanaume wengine wote duniani na ukumbusho pekee ulikuwa ni mtoto na Mungu alikuwa amelikubali hilo.

“Siwezi kuua mtoto wa Prosper lolote litakalokuwa na liwe!” Alisema Belinda.
Alivumilia na mimba yake chuoni mpaka ikafikisha miezi minne akawa haendi tena nyumbani kwao kila mwisho wa wiki, jambo lililowashtua ndugu zake na kuwafanya kaka zake waende shuleni kumuuliza lipi lilikuwa likimsumbua.

Ni hao ndio waliomgundua Belinda na mimba yake na bila hata kusita walizipeleka taarifa moja kwa moja kwa mzee Thomson! Belinda alihisi hilo lingetokea ni asubuhi ya siku iliyofuata tu alipopanda basi kwenda Tabora nyumbani kwao na Prosper kujificha mpaka azae mtoto wake.

******************

Belinda aliingia Tabora jioni ya saa kumi akiwa amechoka hoi bin taaban, hakutaka kupoteza muda hata kidogo mjini alipanda basi la mwisho kumpeleka hadi kijijini Tutuo! Hakuwa na mzigo mwingine zaidi ya begi lililojaa nguo zake mwenyewe, hakuwa na pesa zaidi ya shilingi elfu kumi aliyokuwa amebakiza.

Alijua wazi kuwa alikokuwa anakwenda kulikuwa na taabu kubwa na nzito ikimsubiri, alijua tangu siku hiyo asingepata msaada wowote kutoka kwa baba yake sababu alikuwa amemuudhi kupita kiasi! Isitoshe alijua wazi kuwa mama yake wa kambo na ndugu zake wangemjaza chuki baba yake ili azidi kumchukia.

“Lolote na liwe lakini sipo tayari kumuua mtoto wangu! Ni bora mimi niteseke lakini kiumbe hiki kizaliwe kama ni masomo nitaendelea nayo baadaye ingawa sina uhakika ni nani atanilipia ada!” Aliwaza Belinda wakati akitembea kuelekea nyumbani kwao na Prosper.

Alishangazwa na umati mkubwa wa watu aliouona alipokaribia nyumba yao, wanaume wengi walikuwa wamekaa katika miduara wakiota moto na wengine walionekana kula chakula! Belinda alishindwa kuelewa ni nini kilikuwa kimetokea.

Alipofika kwenye uwanja wa nyumba alishangaa kuwaona wifi zake wakija mbio huku wakilia machozi! Wote walimkumbatia huku wakimtaarifa kuwa mama yao alikuwa amefariki asubuhi ya siku hiyo.

“Mama amefariki leo! Na hapa tulipo hata pesa ya sanda tumekosa!” Nyamizi alimwambia Belinda baada ya kuketi chini huku akilia na kujifuta machozi.
“Ni heri umekufa wifi maana hapa ndani hatuna hata senti, nafikiri utatusaidia pesa kidogo tukanunue sanda na kuchonga jeneza!”

*Je, nini kitaendelea?*
 
Back
Top Bottom